Veriafya

Veriafya Taarifa za afya zilizothibitishwa, rahisi na zinazoeleweka

08/02/2026

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi alizungumza haya Februari 21, 2024, kwenye mjadala wa Utapiamlo na Lishe Bora uliorushwa na kituo cha TBC

08/02/2026

Tatizo la Asidi kujaa Kooni husumbua watu wengi, na baadhi hushindwa kuelewa sababu za kutokea kwake.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za upasuaji kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila, Dkt. Godlove Mfuko, baadhi ya mambo yanayoweza kupelekea kutokea kwa hali hii ni Matumizi ya Chai yenye viungo vingi, Soda, ulaji wa vyakula vyenye mafuta hasa Chips pamoja na Tomato Sauce

Video: ITV Tanzania

06/02/2026

Pamoja na mambo mengine, Uwepo wa Uvimbe kwenye t**i unaweza kuwa ni miongoni mwa Dalili Muhimu za Ugonjwa wa Saratani ya Mat**i.

Ungana na Dkt. Lulu Sakafu, Bingwa Mbobezi wa Radiolojia kutoka MNH- Mloganzila kwa elimu zaidi.

Video: Video: MNH-Mloganzila TV

Ulaji wa Wali Mweupe k**a chakula kikuu kwa muda mrefu unaweza kusababisha Upungufu wa Vitamini B1 unaopelekea kupata Ug...
06/02/2026

Ulaji wa Wali Mweupe k**a chakula kikuu kwa muda mrefu unaweza kusababisha Upungufu wa Vitamini B1 unaopelekea kupata Ugonjwa hatari wa 'Beriberi' unaosababisha Uchovu, Ganzi Miguuni na Mikononi, kutoona vizuri, kuchanganyikiwa na mwisho Moyo hufeli na Misuli hupooza

Inashauriwa kutumia Wali wa Kahawia (Brown Rice) ambao una Ganda la juu linalobeba Vitamini hiyo tofauti na Mweupe ambao Ganda hilo huondolewa wakati wa kuukoboa au kutumia aina za Nafaka kamili ambazo hazijakobolewa mfano Mahindi, Ngano na Shayiri

06/02/2026

Je, unafahamu kuhusu Dalili za Ugonjwa wa Kuvimba kwa Tezi Dume?

Ungana na Dkt. Mgendi Hamis, Daktari Bingwa wa upasuaji mfumo wa Mkojo kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa ufafanuzi zaidi.

Video: MNH-Mloganzila TV

Viazi vitamu ni chanzo kizuri cha vitamini A kwa mfumo wa afya ya Macho. Hii ni kwa sababu vina 'Beta-carotene', ambayo ...
06/02/2026

Viazi vitamu ni chanzo kizuri cha vitamini A kwa mfumo wa afya ya Macho. Hii ni kwa sababu vina 'Beta-carotene', ambayo mwili hubadilisha kuwa Vitamini A muhimu kwa kuona vizuri, hasa Usiku.

Kutumia viazi vitamu mara kwa mara husaidia kulinda Macho na kupunguza hatari ya matatizo ya kuona yanayohusiana na upungufu wa Vitamini A.

Pia, viazi vitamu vina Viondoa Sumu viingine vinavyo saidia kudumisha macho yenye afya na kupunguza kuzeeka kwa seli za Macho, hivyo kupunguza hatari ya Kupoteza Uoni hasa Umri unapokuwa mkubwa

05/02/2026

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi alizungumza haya akisisitiza umuhimu wa kutunza lishe za Watoto, suala linalopaswa kuanza kuzingatiwa tangu Mama akiwa Mjamzito.

Hii itasaidia kuwaepusha Watoto ili wasipatwe na Udumavu unaoweza kuathiri Ukuaji wao

Video: TBC

Mkojo unaweza kutumika kuonesha nguvu ya mfumo Uzazi wa Mwanaume, hususan Afya ya Tezi DumeKitaalamu, dalili mojawapo ya...
05/02/2026

Mkojo unaweza kutumika kuonesha nguvu ya mfumo Uzazi wa Mwanaume, hususan Afya ya Tezi Dume

Kitaalamu, dalili mojawapo ya Kuvimba kwa Tezi Dume ni mwanaume kushindwa kurusha Mkojo umbali mrefu pindi anapojisaidia haja Ndogo, hasa ikiwa Mwanzoni alikuwa na uwezo huo

Kwa wanaume, ukiona hili linatokea, fika Hospitalini mapema kuchunguzwa, na ikiwa una tatizo, uweze kusaidiwa mapema

Kwa mujibu wa Tafiti Mbalimbali za Kimaabara, ulaji wa Stafeli unaweza kusaidia kupunguza hatari ya kupatwa na Saratani ...
05/02/2026

Kwa mujibu wa Tafiti Mbalimbali za Kimaabara, ulaji wa Stafeli unaweza kusaidia kupunguza hatari ya kupatwa na Saratani ya Mat**i, Utumbo, Tumbo na Mapafu.

Hii inatokana na uwepo wa Kamikali za Acetogenins ambazo huharibu usafirishwaji wa Nishati inayotumiwa na Seli za Saratani katika kukua na kusambaa Mwilini.

Pia lina nyuzi lishe nyingi na maji vinavyosaidia mwili kuondoa Sumu na kuboresha Mmeng’enyo wa chakula, hivyo kuimarisha kinga ya Mwili.

04/02/2026

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi alizungumza haya k**a sehemu ya kuwakumbusha Watu umuhimu wa kutunza afya na kuishi Mtindo bora wa Maisha utakaosaidia kujilinda dhidi ya Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza

Video: TBC

Mtama ni chakula chenye virutubisho muhimu kwa watoto. Una Nishati inayowasaidia kukua na kuwa na nguvu kwa shughuli za ...
04/02/2026

Mtama ni chakula chenye virutubisho muhimu kwa watoto. Una Nishati inayowasaidia kukua na kuwa na nguvu kwa shughuli za kila siku, na pia una Protini zinazochangia ukuaji wa mwili.

Una Madini chuma na Magnesiamu yanayosaidia kutengeneza damu na kuimarisha Mifupa. Hii husaidia mtoto kuepuka upungufu wa Damu na kuwa na afya bora.

Zaidi ya hayo, Mtama una nyuzi lishe zinazosaidia mmeng’enyo wa chakula na kuzuia choo kigumu. Ni chakula rahisi, salama na chenye faida kwa watoto.

04/02/2026

Unajua kuwa Mama kuwa Mkali sana ni miongoni mwa sababu zinazotajwa kuwa visababishi vya mtoto kupata 'Chango?'

Fuatana na Dkt. Jackline Urio, Bingwa wa Magonjwa ya Watoto Kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili akifafanua baadhi ya visababishi vinavyoweza kupelekea Mtoto apatwe na hali hii.

Video: Muhimbili TV

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram