Veriafya

Veriafya Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Veriafya, Dar es Salaam.

Una vidonda vya tumbo? Usitumie Gofen (Ibuprofen) na Diclofenac maana huongeza maumivu na kiungulia na wakati mwingine z...
29/04/2026

Una vidonda vya tumbo? Usitumie Gofen (Ibuprofen) na Diclofenac maana huongeza maumivu na kiungulia na wakati mwingine zinaweza kusababisa kuvujia kwa damu tumboni.

Ikiwa una Vidonda vya tumbo na unahitaji dawa ya maumivu ya mwili au hata kutuliza Homa, tumia Paracetamol (Panadol) kwani ni salama.

Epuka kutumia dawa za maumivu bila ushauri wa mtaalamu wa afya ili kulinda afya ya tumbo lako.

Tendo la ndoa linapaswa kuwa salama kwa afya yako. Ikiwa unapata Maumivu makali ya Kifua au Kichwa ghafla, hiyo si ishar...
29/04/2026

Tendo la ndoa linapaswa kuwa salama kwa afya yako. Ikiwa unapata Maumivu makali ya Kifua au Kichwa ghafla, hiyo si ishara njema.

Maumivu ya Kifua yanaweza kuwa dalili ya Mshtuko wa Moyo, hasa kwa wale wenye Magonjwa ya Moyo, wakati maumivu ya kichwa yanaweza kuashiria ongezeko kubwa la Shinikizo la Damu au hata kupasuka kwa Mshipa wa Damu kwenye Ubongo hivyo kusababisha Kiharusi (Stroke).

Usijifanye shujaa. K**a maumivu haya yanatokea wakati wa tendo, acha mara moja. Ikiwa yanatokea baada ya tendo usipuuze, nenda Hospitalini kwa uchunguzi.

Tafiti zinaonesha kuwa kunusa nguo za Mwenza wako kunaweza kusaidia kupunguza Msongo wa Mawazo na hisia za Upweke. Matha...
28/04/2026

Tafiti zinaonesha kuwa kunusa nguo za Mwenza wako kunaweza kusaidia kupunguza Msongo wa Mawazo na hisia za Upweke.

Mathalani, Utafiti mmoja uliochapishwa kwenye Jarida la ‘The Journal of Personality and Social Psychology’ unaonesha kuwa washiriki waliopata fursa ya kunusa nguo zilizovaliwa na wenza wao walipata viwango vya chini vya Cortisol, homoni inayohusiana na Msongo wa Mawazo.

Pia, Utafiti wa Chuo Kikuu cha British Columbia unapendekeza kuwa harufu ya Mwenza inaweza kuboresha Usingizi na kutoa hisia za usalama, sawa na athari za uwepo wake wa kimwili. Hii inatokana na jinsi ubongo unavyohusisha harufu zinazojulikana na hisia za faraja na uhusiano wa kihisia, hivyo kusaidia kudhibiti Msongo wa Mawazo na kuboresha Hisia za mtu.

27/04/2026

Matumizi ya Bidhaa za Tumbaku k**a Sigara, Unywaji wa Pombe kupita kiasi pamoja na Kushiriki tendo la Ndoa kwa njia ya Mdomo ni miongoni mwa Mambo yanayoweza kuchangia hatari ya Kuugua Saratani ya Koo

Sikiliza ufafanuzi Daktari Bingwa wa Magonjwa ya uzazi na Wanawake, Abdul Mkeyenge akifafanua Suala hili kwa Undani.

Video: Mwananchi Digital

Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu huathiri Afya taratibu bila Mhusika kugundua. Viatu hivi hubadili Jinsi unavyotembea n...
27/04/2026

Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu huathiri Afya taratibu bila Mhusika kugundua. Viatu hivi hubadili Jinsi unavyotembea na kusababisha Shinikizo kubwa kwenye Vidole, Kiuno, Magoti na Mgongo. Matokeo yake ni maumivu ya Miguu, Majeraha ya Misuli na hata matatizo ya Mgongo, Magoti na Kisigino yanayoweza kutokea baadaye maishani, hasa baada ya kufikia umri wa Ukomo wa Hedhi

Pia, High Heels zinaweza kufanya miguu ichoke haraka na kupunguza mzunguko wa Damu, jambo linaloweza kusababisha mishipa kuvimba na Miguu kuwa mizito.

Kwa afya bora ya miguu, inashauriwa kuvaa High Heels kwa muda usiozidi Masaa 2-4 kwa siku. Ikiwa unahitaji kuvaa kwa muda mrefu, hakikisha unapata muda wa kupumzisha miguu yako kwa kuvua viatu hivyo mara kwa mara na kufanya mazoezi ya kunyoosha miguu.

Wazee wanapaswa kula vyakula vyenye madini ya Calcium na Vitamin D ili kuimarisha na kuboresha afya ya mifupa ikiwemo ku...
27/04/2026

Wazee wanapaswa kula vyakula vyenye madini ya Calcium na Vitamin D ili kuimarisha na kuboresha afya ya mifupa ikiwemo kuzuia maumivu ya magoti, visigino, kiuno na Maungio ya Mwili pamoja na kuifanya iwe imara ili isivunjike kirahisi.

Dagaa, Maziwa na Yogurt ni vyanzo bora vya calcium. Pia, Dagaa wana Vitamin D inayosaidia mwili kufyonza calcium vizuri. Lakini, ni muhimu kuhakikisha Maziwa na Yogurt havina sukari za Nyongeza ili kuepusha Changamoto ya Kisukari.

Ni muhimu pia kuwahamasisha wazee kupata Mwanga wa Jua la asubuhi na kufanya mazoezi mepesi k**a kutembea ili kusaidia kuimarisha afya ya mifupa yao.

26/04/2026

Vilevi huathiri hadi Mbegu za Kiume na kuzifanya zishindwe kupanda vizuri via vya Uzazi vya Mwanamke hivyo kutoweza kulirutubisha Yai na kutunga Ujauzito

Msikilize Dkt. Ngechu Wambui, Afisa Tabibu kutoka Beta Health Care Clinic akitoa elimu hii kupitia kituo cha Televisheni cha Citizen TV Kenya.

Video: Citizen TV Kenya

Brokoli ni Mboga iliyojazwa na wingi wa 'Sulforaphane' viini ambavyo husaidia Kupambana na Saratani na hivyo Hupunguza h...
26/04/2026

Brokoli ni Mboga iliyojazwa na wingi wa 'Sulforaphane' viini ambavyo husaidia Kupambana na Saratani na hivyo Hupunguza hatari ya kupata Saratani ya Tezi Dume, Matiti au Utumbo Mpana.

Hii hufanikishwa kwa kuzuia Seli Mama zisiendelee Kuzalisha Seli za Saratani na hivyo hukukinga kwa Kuzuia na Kupunguza Kasi ya Saratani inayoendelea Kukua Mwilini lakini si Tiba ya Saratani iliyokwisha Kukua au Kusambaa Mwilini.

25/04/2026

Unakubaliana na Daktari Bingwa Bobezi wa Magonjwa ya Figo, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Garvin Kweka kwa kiwango gani?

Video kwa hisani ya Tanzania Association of Women Certified Accountants (TAWCA)

Mayai ni chakula salama kwa Wajawazito na hayahusiani na madai Potofu kwamba husababisha watoto kuzaliwa bila nywele au ...
25/04/2026

Mayai ni chakula salama kwa Wajawazito na hayahusiani na madai Potofu kwamba husababisha watoto kuzaliwa bila nywele au wenye vichwa vikubwa.

Mayai yana virutubisho muhimu k**a Protini, Choline, Vitamini D, Madini chuma ambayo husaidia katika ukuaji mzuri wa ubongo na mwili wa mtoto tumboni.

Hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kuwa ulaji wa mayai unahusiana na kasoro za kuzaliwa k**a hizo. Badala yake, kula mayai kwa kiasi sahihi huchangia afya bora kwa mama na mtoto, mradi tu yamepikwa vizuri ili kuepuka maambukizi k**a Salmonella yanayoweza kuhatarisha usalama wa Mama na Mtoto

25/04/2026

Je, unajua kuwa Matumizi ya Kope Bandia yanaweza kusababisha Upofu? Sikiliza sehemu ya Mahojiano ya Daktari wa Macho, Johannes Mfwili aliyofanya kwenye kipindi cha Med Counter cha Azam TV

Uking’atwa na Mnyama, hasa Mbwa, Paka au wanyama wa porini, ni muhimu kuchukua hatua za haraka ili kuzuia maambukizi hat...
24/04/2026

Uking’atwa na Mnyama, hasa Mbwa, Paka au wanyama wa porini, ni muhimu kuchukua hatua za haraka ili kuzuia maambukizi hatari ya Kichaa cha Mbwa (Rabies).

Osha jeraha mara moja kwa maji safi na sabuni kwa angalau dakika 15, kisha fika Hospitalini upatiwe Chanjo ya Kichaa cha Mbwa

Usipuuzie hata k**a jeraha ni dogo, kwani virusi vinavyosababisha Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa huweza kusafiri hadi kwenye Ubongo na kusababisha kifo ikiwa havitatibiwa mapema.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share