Veriafya

Veriafya Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Veriafya, Dar es Salaam.

06/04/2026

Ugonjwa wa Presha hujulikana k**a muuaji wa Kimyakimya kwani dalili zake hasa kwenye hatua za awali huwa hazipo wazi hivyo ni muhimu kujijengea utaratibu wa kupima afya mara kwa mara ili kuepuka athari zake.

Dkt. Engerasia Kifai, Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete

Video: Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Tampon inapaswa kuvaliwa kwa Masaa 4 hadi 8 lakini haipaswi kuzidi masaa 8 ili kuepuka hatari ya maambukizi, hasa Toxic ...
06/04/2026

Tampon inapaswa kuvaliwa kwa Masaa 4 hadi 8 lakini haipaswi kuzidi masaa 8 ili kuepuka hatari ya maambukizi, hasa Toxic Shock Syndrome (TSS), maambukizi nadra lakini hatari yanayosababishwa na Bakteria.

Ni muhimu kubadilisha Tampon mara kwa mara kulingana na kiwango cha Hedhi. Ikiwa damu inavuja haraka, inaweza kuwa bora kubadilisha tampon kila masaa 4-6 ili kuepuka uvujaji na maambukizi. Pia, inashauriwa kutumia tampon yenye uwezo wa kufyonza unaolingana na kiwango cha damu ili kupunguza hatari ya matatizo ya kiafya.

Aidha, tampon haipaswi kuvaliwa wakati wa kulala kwa zaidi ya masaa 8. Badala yake, unaweza kutumia Pedi za usiku kwa usalama zaidi.

06/04/2026

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi aliyasema haya Machi 2, 2026 kwenye Busati la Msikiti wa Mtoro

Video: Dua TV

06/04/2026

Watu wenye Presha ya Kupanda na Changamoto za Magonjwa ya Moyo hawashauriwi kutumia kiasi kikubwa cha maji kwani huongeza mzigo wa Moyo katika kusukuma Vimiminika Mwilini, hali inayoweza kuufanya uchoke zaidi na kuongeza Ukubwa wa tatizo

Sikiliza Ufafanuzi wa Maria Samlongo, Afisa Lishe kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete

Video: Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Baadhi ya Wanaume hutumia mchanganyiko wa vinywaji vya kuongeza nishati (Energy Drinks) na vidonge vya kushusha homa na ...
05/04/2026

Baadhi ya Wanaume hutumia mchanganyiko wa vinywaji vya kuongeza nishati (Energy Drinks) na vidonge vya kushusha homa na kutuliza maumivu aina ya Panadol kuongeza nguvu za kiume

Mchanganyiko huu ni hatari kwa afya kwani huongeza msukumo wa damu mwilini, huongeza mapigo ya Moyo Pamoja na kuufanya Moyo ufanye kazi kubwa kuliko kawaida hivyo kusababisha Upanuke pamoja na kuua Figo ambazo huhusika na kuchuja damu Mwilini

Aidha, Panadol ni dawa inayotajwa na tafiti kuwa na uwezo mkubwa wa kuharibu ini pindi inapotumiwa vibaya hivyo ni muhimu kuacha tabia hii inayohatarisha Afya kwa kuchangia Magonjwa yasiyo ya kuambukiza

05/04/2026

Wanawake wenye Ujauzito tayari na walio na Matatizo ya kiafya, hasa kwenye Moyo, Presha kubwa, Kipanda Uso na Magonjwa yanayoathiri Ini hawashauriwi kutumia dawa za P2

Sikiliza ufafanuzi wa Daktari Bingwa wa wanawake, Emmanuel Mafwili kutoka Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Njombe alioutoa kupitia Uplands FM

Video: Uplands FM

04/04/2026

Kitaalamu, haishauriwi kutumia P2 zaidi ya Miezi miwili mfululizo. Aidha, matumizi yake hayapaswi kuzidi mara 3 kwa Mwaka

Sikiliza ufafanuzi wa Daktari Bingwa wa wanawake, Emmanuel Mafwili kutoka Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Njombe alioutoa kupitia Uplands FM

Video: Uplands FM

04/04/2026

Unapokuwa umefunga Chakula, Mwili kupitia Mchakato wake wa asili hujisafisha kwa kula Vimelea vya Magonjwa. Hali hii huimarisha afya

Prof. Mohamed Janabi, Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika

Video: Muhimbili TV

04/04/2026

P2 si njia rasmi ya Uzazi wa Mpango, ni njia ya dharura inayotumika katika mazingira machache kuzuia Ujauzito usio tarajiwa

Sikiliza ufafanuzi wa Daktari Bingwa wa wanawake, Emmanuel Mafwili kutoka Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Njombe alioutoa kupitia Uplands FM

Video: Uplands FM

Ugonjwa wa Homa ya Ini hasa aina B huwa ni hatari sana kwa afya. Shirika la Afya Duniani (WHO) linabainisha kuwa Ugonjwa...
04/04/2026

Ugonjwa wa Homa ya Ini hasa aina B huwa ni hatari sana kwa afya. Shirika la Afya Duniani (WHO) linabainisha kuwa Ugonjwa huu huwa na uwezo mara 100 wa kushambulia na kuambukiza kuzidi VVU na unaweza kusababisha Kufeli kwa Ini na hata kupata Saratani ya Ini na hatimaye Kifo

Njia za Uambukizwaji wake hufanana na jinsi VVU/UKIMWI unavyoambukizwa. Ni muhimu kujikinga kwa kupata Chanjo 3 za Ugonjwa huu pamoja na kuepuka ngono zembe ambazo kwa kiasi kikubwa huwa ni chanzo cha Maambukizi

03/04/2026

Mwanaume usifanye mapenzi kila siku, uwezo wa kutungisha Mimba hupungua

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram