Veriafya

Veriafya Taarifa za afya zilizothibitishwa, rahisi na zinazoeleweka

Wizara ya Afya na Huduma za Kibinadamu ya Somalia imethibitisha uwepo wa mlipuko mpya wa Ugonjwa wa Dondakoo (Diphtheria...
07/12/2025

Wizara ya Afya na Huduma za Kibinadamu ya Somalia imethibitisha uwepo wa mlipuko mpya wa Ugonjwa wa Dondakoo (Diphtheria) ambapo takribani watoto 50 wamefariki huku wengine zaidi ya 1,000 wakiambukizwa.

Katika taarifa yake iliyotolewa Desemba 7, 2025, Wizara imesema watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 15 ndiyo walioathirika zaidi.

Ugonjwa huu hushambulia sehemu za Koo, na huenezwa kwa njia ya hewa, mate au majimaji yanayotoka kwenye sehemu za maambukizi na huambatana na dalili za Kukosa hamu ya kula na kushindwa kula, Vidonda kooni, Kutoa k**asi iliyochanganyika na damu, Utando kwenye koo ambao humzuia mtoto kumeza na hata kupumua, Maumivu makali ya shingo hivyo kumfanya mtoto ashindwe kumeza na kupumua, kupooza sehemu za paji la uso hadi shingoni pamoja na Kifo.

Dondakoo hukingwa kwa Chanjo inayotolewa mara tatu kwa mtoto kwenye umri wa wiki 6, wiki 10 na wiki 14 na kwa Tanzania, hutolewa Bure kwenye Vituo vyote vya Kutolea huduma hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wa umri huu wanapata chanjo ili kuwakinga dhidi ya Ugonjwa huu hatari

Kiss ina nguvu ya kipekee katika kuondoa huzuni, mawazo na hasira. Inapofanyika, mwili huachilia homoni za furaha k**a o...
07/12/2025

Kiss ina nguvu ya kipekee katika kuondoa huzuni, mawazo na hasira. Inapofanyika, mwili huachilia homoni za furaha k**a oxytocin, dopamine na serotonin, ambazo husaidia kupunguza msongo wa mawazo na kuimarisha hisia za upendo na faraja.

Pia, kiss hupunguza kiwango cha cortisol, homoni inayohusiana na msongo wa mawazo na hasira. Ndiyo maana unapombusu mtu unayempenda, unahisi utulivu na furaha, huku akili ikipata nafasi ya kupumzika na kusahau huzuni.

Zaidi ya hayo, kiss huimarisha uhusiano wa kihisia kati ya wapenzi kwa kuongeza uaminifu na ukaribu. Ni kitendo kidogo lakini chenye nguvu kubwa ya kuleta furaha na kuondoa hisia hasi.

Watoto wanapofikia umri wa kuanza kula vyakula tofauti, wazazi hujawa na furaha na matarajio makubwa. Hata hivyo, ni muh...
06/12/2025

Watoto wanapofikia umri wa kuanza kula vyakula tofauti, wazazi hujawa na furaha na matarajio makubwa. Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa baadhi ya vyakula vinaweza kusababisha mzio.

Karanga, samaki, almonds, maziwa na mayai ni miongoni mwa vyakula vinavyosababisha mzio kwa baadhi ya watoto. Mzio unaweza kusababisha vipele, kuvimba Mwili au hata matatizo ya kupumua.

Wazazi wanashauriwa kuanza kwa kumpatia kiasi kidogo cha aina hii ya vyakula ili kuona k**a mwili wa Mtoto utakipokea bila shida kabla ya kumpatia kwa kiasi kikubwa.

Usisafishe Pasi kwa Panadol, ni hatari kwa Afya kwani Panadol inapoyeyuka kwa moto, hutoa gesi zenye sumu k**a Formaldeh...
04/12/2025

Usisafishe Pasi kwa Panadol, ni hatari kwa Afya kwani Panadol inapoyeyuka kwa moto, hutoa gesi zenye sumu k**a Formaldehyde na Nitrates, ambazo zinaweza kusababisha Miwasho kwenye Macho, Koo na Ngozi, Maumivu ya Kichwa, Matatizo ya Kupumua na kwa muda mrefu, huongeza hatari ya Magonjwa Sugu k**a Saratani.

Badala ya kutumia Panadol, tumia njia salama k**a kuchanganya Baking soda na maji kutengeneza pasta laini, kisha ipake kwenye pasi iliyo baridi na uifute kwa kitambaa.

Pia, unaweza kutumia Vinegar na Chumvi kusafisha mabaki ya uchafu kwa ufanisi.

Tampon inapaswa kuvaliwa kwa Masaa 4 hadi 8 lakini haipaswi kuzidi masaa 8 ili kuepuka hatari ya maambukizi, hasa Toxic ...
04/12/2025

Tampon inapaswa kuvaliwa kwa Masaa 4 hadi 8 lakini haipaswi kuzidi masaa 8 ili kuepuka hatari ya maambukizi, hasa Toxic Shock Syndrome (TSS), maambukizi nadra lakini hatari yanayosababishwa na bakteria.

Ni muhimu kubadilisha Tampon mara kwa mara kulingana na kiwango cha Hedhi. Ikiwa damu inavuja haraka, inaweza kuwa bora kubadilisha tampon kila masaa 4-6 ili kuepuka uvujaji na maambukizi. Pia, inashauriwa kutumia tampon yenye uwezo wa kufyonza unaolingana na kiwango cha damu ili kupunguza hatari ya matatizo ya kiafya.

Aidha, tampon haipaswi kuvaliwa wakati wa kulala kwa zaidi ya masaa 8. Badala yake, unaweza kutumia Pedi za usiku kwa usalama zaidi.

Kwa afya bora ya Mtoto, hasa mwenye umri wa chini ya Miaka 5, yai lililochemshwa ndilo chaguo linalofaa zaidi kuliko yai...
02/12/2025

Kwa afya bora ya Mtoto, hasa mwenye umri wa chini ya Miaka 5, yai lililochemshwa ndilo chaguo linalofaa zaidi kuliko yai la kukaanga.

Yai la kuchemsha hupikwa bila mafuta, Jambo linalolifanya kuwa salama na lishe safi kwa mtoto, tofauti na yai la kukaanga ambalo mara nyingi hutumia mafuta mengi ambayo si rafiki kwa afya ya mtoto mdogo. Aidha, huwa rahisi kumeng’enywa na tumbo la mtoto, na husaidia kupunguza uwezekano wa matatizo ya tumbo au mzio. Mbali na hilo huhakikisha halina vimelea hatari k**a Salmonella, hivyo kumkinga mtoto dhidi ya maradhi yanayoweza kusababishwa na mayai ambayo hayajapikwa kikamilifu.

Kwa upande mwingine, yai la kukaanga linaweza kuwa na ladha nzuri lakini si chaguo bora kwa mtoto mdogo, hasa linapotengenezwa kwa mafuta mengi au linaongezewa viungo vikali na chumvi, ambavyo vinaweza kudhuru afya ya Mtoto.

Kwa ujumla, wazazi au walezi wanashauriwa kumpatia mtoto yai lililochemshwa vizuri k**a sehemu ya mlo wake wa kila siku ili apate protini ya kutosha kwa ukuaji wa mwili na ubongo. Ingawa yai la kukaanga linaweza pia kuliwa na watoto, inashauriwa liwe limetengenezwa kwa kiwekewa mafuta mengi, viungo na chumvi.

Karanga, Korosho na Mbegu za maboga ni vyakula vyenye virutubisho muhimu vinavyoweza kusaidia kuboresha ubora wa shahawa...
01/12/2025

Karanga, Korosho na Mbegu za maboga ni vyakula vyenye virutubisho muhimu vinavyoweza kusaidia kuboresha ubora wa shahawa.

Vina madini k**a zinki, Magnesiamu na Selenium ambayo huhusika katika uzalishaji wa mbegu za kiume zenye afya. Pia, vyakula hivi vina mafuta yenye afya na Viondoa Sumu vinavyosaidia kupunguza madhara ya sumu mwilini na kuimarisha uzazi.

Kwa kula kwa wingi vyakula hivi pamoja na lishe bora, Mwanaume anaweza kuongeza nguvu na uimara wa mbegu za kiume, hivyo kuboresha afya ya uzazi kwa ujumla.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu ongezeko la Joto nchini kutokana na kusogea kwa Jua la Utos...
29/11/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu ongezeko la Joto nchini kutokana na kusogea kwa Jua la Utosi pamoja na upungufu wa mvua, hali inayofanya uso wa dunia katika maeneo husika kuwa karibu zaidi na Jua ambapo lipo pia ongezeko la unyevu angani, hasa katika maeneo ya pwani, hali iliyoongeza hisia ya Joto kwa binadamu.

Hali hii inaweza kusababisha uchovu wa mwili, kizunguzungu, kupoteza fahamu, au kupanda kwa joto la mwili kupita kiwango cha kawaida (heat stroke), ambayo ni hatari kwa maisha.

Aidha, watu wengi wanaweza kupatwa na pungufu wa maji mwilini kwa kutoa Jasho kupita kiasi kiasi hivyo kusababisha maumivu ya kichwa, uchovu, mapigo ya moyo kwenda kasi na kushuka kwa shinikizo la damu.

Wanawazito, Watoto, Wazee, Wagonjwa wa shinikizo la damu, kisukari, pumu na magonjwa ya moyo wako katika hatari zaidi kwani joto kali linaongeza kazi kwa mfumo wa moyo na mapafu.

Kwa wakati huu, tunashauriwa Kunywa maji ya kutosha mara kwa mara hata k**a huhisi kiu, kuepuka kukaa juani muda mrefu, Kuaa nguo nyepesi zisizo na rangi nyeusi, na zenye kuruhusu hewa kupita, tumia feni, kiyoyozi, au fungua madirisha kuongeza mzunguko wa hewa, Wazee, watoto, wajawazito na wagonjwa wa magonjwa sugu wazingatie tahadhari zaidi na kuepuka Joto.

Juisi ya miwa ni kinywaji kinachochacha haraka ikiwa kitaachwa muda mrefu bila kuhifadhiwa vizuri baada ya kutengenezwa,...
27/11/2025

Juisi ya miwa ni kinywaji kinachochacha haraka ikiwa kitaachwa muda mrefu bila kuhifadhiwa vizuri baada ya kutengenezwa, hivyo kusababisha madhara kwa afya ikiwemo Maumivu makali ya tumbo, kuhara, kichefuchefu, kiungulia na kutapika pamoja na maumivu ya kichwa na kizunguzungu.

Miongoni mwa viashiria vya Juisi iliyochacha ni uwepo wa Harufu kali au inayofanana na pombe, ladha kali/mbaya isiyo ya kawaida, Povu kuongezeka pamoja na Mabadiliko ya rangi.

Kuzuia hali hii, unashauriwa kunywa mara tu baada ya kukamua (ndani ya dakika 20–30), Kuiweka kwenye friji ikiwa hutaitumia mara moja pamoja na Kutumia vyombo visafi sana inapokamuliwa. Ukiona imeanza kuwa na harufu au ladha ya ajabu, usinywe, tayari imeanza kuchacha.

Kunywa mchanganyiko wa Limao (Ndimu) na Tangawizi kila siku asubuhi kunaweza kuleta faida nyingi kwa afya.Mchanganyiko h...
26/11/2025

Kunywa mchanganyiko wa Limao (Ndimu) na Tangawizi kila siku asubuhi kunaweza kuleta faida nyingi kwa afya.

Mchanganyiko huu husaidia kusafisha mwili kwa kutoa Sumu (Detox), kuboresha mmeng’enyo wa chakula, kuongeza kinga ya mwili kutokana na vitamini C ya limao na viambata vya kupambana na Uvimbe Joto vilivyopo kwenye Tangawizi.

Pia husaidia kupunguza uzito, kuongeza nishati asubuhi na kupunguza maumivu madogo madogo mwilini k**a vile ya tumbo au viungo. Ni kinywaji rahisi lakini chenye nguvu ya kiafya.

25/11/2025

Namna nzuri ya kufuturu baada ya mfungo.

Prof. Mohamed Janabi

Kabla ya kugusa Sehemu zako za Siri, hasa wakati wa Kujisafisha, Kujikuna au wakati wa Faragha, hakikisha unaosha mikono...
24/11/2025

Kabla ya kugusa Sehemu zako za Siri, hasa wakati wa Kujisafisha, Kujikuna au wakati wa Faragha, hakikisha unaosha mikono yako kwa Sabuni na Maji safi.

Mikono michafu inaweza kusababisha maambukizi ya njia ya Mkojo, Fangasi, Muwasho kwenye Uume au Uke, Kutokwa na uchafu usio wa kawaida na Maumivu wakati wa Kukojoa au tendo la Ndoa.

Hili ni jambo rahisi, lakini lina mchango mkubwa sana katika kulinda afya yako ya Uzazi.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram