Veriafya

Veriafya Tunazungumza afya!

13/11/2025

Ni HATARI!, ⚠️

Usimpake mtoto dawa hizi za kuua mbu. Ni hatari kwa watoto.

Ufafanuzi wake wa kitaalamu upo hapa

Watu 613 wakiwemo Wajawazito 155 wamebainika kuwa na Ugonjwa wa Kaswende katika kipindi cha Januari-Oktoba, 2025 ndani y...
12/11/2025

Watu 613 wakiwemo Wajawazito 155 wamebainika kuwa na Ugonjwa wa Kaswende katika kipindi cha Januari-Oktoba, 2025 ndani ya Halmashauri ya Mji wa Njombe, hali inayotajwa kuwa changamoto kubwa kwa afya ya jamii katika eneo hilo.

Takwimu hizo zimetolewa na Mratibu wa Magonjwa ya Zinaa wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Dkt. Shella Myemba wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Njombe ambapo ameeleza kuwa mwenendo wa maambukizi unazidi kuongezeka kutokana na mienendo hatarishi ya ngono.

Dkt. Myemba amesema idadi kubwa ya wagonjwa wa Kaswende inatokana na watu kutozingatia matumizi ya kinga na kutokuwa waaminifu katika uhusiano, jambo linaloongeza hatari ya kusambaza ugonjwa huo kwa kasi.

Kutembea Miguu peku, hasa kwenye Nyasi, Mchanga au Udongo, kuna faida nyingi kwa afya ya mwili na Akili. Inasaidia kuima...
11/11/2025

Kutembea Miguu peku, hasa kwenye Nyasi, Mchanga au Udongo, kuna faida nyingi kwa afya ya mwili na Akili. Inasaidia kuimarisha Misuli ya Miguu, kuboresha Mzunguko wa Damu na kusaidia mwili kusawazisha umeme wa asili, jambo linaloweza kupunguza Uchovu na Maumivu mwilini.

Tabia hii pia hutuliza Akili na kupunguza Msongo wa Mawazo. Miguu inapogusa ardhi moja kwa moja, huchochea mishipa ya fahamu na kusaidia kupunguza viwango vya Homoni ya stress, hivyo kumsaidia mtu kupata utulivu wa kiakili na Usingizi mzuri zaidi usiku.

Hata hivyo, ni muhimu kuhakikisha unatembea kwenye sehemu safi na salama ili kuepuka Maambukizi au Majeraha.

Muuguzi wa huduma ya afya nchini Ujerumani amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya...
10/11/2025

Muuguzi wa huduma ya afya nchini Ujerumani amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya wagonjwa 10 na jaribio la kuwaua wengine 27.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la AFP, Muuguzi huyo wa kiume ambaye jina lake limehifadhiwa aliwadunga wagonjwa dozi kubwa ya dawa za kutuliza Maumivu Makali za Morphine na Midazolam wakati wa zamu zake za usiku ili apate muda wa kulala na kupunguza mzigo wa kazi

Makosa hayo yalitekelezwa kati ya Desemba 2023 na Mei 2024 katika hospitali ya Wuerselen, magharibi mwa Ujerumani na Wachunguzi wanaripotiwa kuchunguza visa vingine vingi vya kutiliwa shaka wakati wa kazi yake.

Kesi hiyo inafanana na ile ya muuguzi Niels Högel, aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka wa 2019 baada ya kupatikana na hatia ya kuua wagonjwa 85 katika hospitali mbili kaskazini mwa Ujerumani ambapo Mahakama iligundua kuwa alitoa dozi zenye sumu za dawa za moyo kwa watu waliokuwa chini ya uangalizi wake kati ya mwaka 1999 na 2005.

Kunywa Juisi ya Matunda, hasa Chungwa na Apple walau dakika 30 kabla ya Kufanya kipimo cha Ultrasound kunaweza kusaidia ...
10/11/2025

Kunywa Juisi ya Matunda, hasa Chungwa na Apple walau dakika 30 kabla ya Kufanya kipimo cha Ultrasound kunaweza kusaidia kumwamsha au kumfanya mtoto tumboni awe 'Active' wakati wa kipimo hicho hivyo kusaidia kupata picha na muonekano mzuri zaidi.

Hii ni kwasababu Juisi hii ina sukari asilia ambayo hutoa nguvu ya haraka, na ikiwa imehifadhiwa kwenye baridi, baridi yake pia huchangia kumfanya mtoto kuwa na msisimko zaidi.

Hata hivyo, ni vizuri kuwasiliana na daktari wako kabla ya kunywa, hasa kama una Kisukari cha Mimba au masharti ya lishe maalum.

Kope bandia na lenzi za macho za urembo zinaweza kuwa chanzo cha matatizo makubwa ya macho kwa wanawake, ikiwemo upofu. ...
28/10/2025

Kope bandia na lenzi za macho za urembo zinaweza kuwa chanzo cha matatizo makubwa ya macho kwa wanawake, ikiwemo upofu. Ingawa hutumika kuongeza mvuto, zinaweza kuharibu macho kama hazitatumika kwa usahihi.

Lenzi bandia zisizo salama au zisizotunzwa vizuri huweza kusababisha maambukizi, kuvimba kwa macho, na hata vidonda vinavyoweza kuleta upofu. Kope bandia pia huambatana na gundi zenye kemikali kali zinazoweza kusababisha kuwasha au uharibifu wa macho.

Ili kujikinga, hakikisha unatumia lenzi bandia zilizoidhinishwa na wataalamu wa macho, usivalie lenzi za marafiki, na usitumie kope bandia mara kwa mara bila ushauri wa daktari. Uzuri wa macho yako ni muhimu, lakini afya ya macho yako ni ya thamani zaidi.

27/10/2025

Ushauri wa Prof. Janabi kwa wazazi kuhusu Maziwa wanayowapa watoto

Video: TBC

Mwanaume kuwa na matiti makubwa kuliko kawaida ni hali inayojulikana kama gynecomastia. Hii hutokea pale ambapo kuna usa...
23/10/2025

Mwanaume kuwa na matiti makubwa kuliko kawaida ni hali inayojulikana kama gynecomastia. Hii hutokea pale ambapo kuna usawa usio wa kawaida wa homoni za kiume (testosterone) na za kike (estrogen), na kusababisha tishu za matiti kukua zaidi ya kawaida.

Sababu zake zinaweza kuwa ni mabadiliko ya homoni wakati wa kubalehe, matumizi ya dawa fulani (kama za pumu, vidonge vya nguvu au steroids), matumizi ya pombe au bangi, magonjwa ya ini, figo au tezi. Wakati mwingine huweza pia kutokea bila sababu maalum.

Matibabu hutegemea chanzo. Ikiwa ni mabadiliko ya homoni ya muda, huweza kuisha yenyewe. Lakini kama hali inaendelea, daktari anaweza kupendekeza dawa za kusawazisha homoni au upasuaji wa kuondoa tishu ya matiti. Ni muhimu kumwona daktari kwa uchunguzi sahihi.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram