Mafundi Bora Wa Magari Tanzania

Mafundi Bora Wa Magari Tanzania Tunajihusisha na matengenezo ya magari,kukagua magari, na kuuza vipuri(spares) vya magari.

Ushauri! ukinunua betri dukani, mwambie muuzaji alipime kwanza... ukikuta umeme uko volt 12 na kuendelea chukua kawashe ...
22/10/2025

Ushauri! ukinunua betri dukani, mwambie muuzaji alipime kwanza... ukikuta umeme uko volt 12 na kuendelea chukua kawashe chombo chako bila kuchaji.. ila ukikuta chini ya volt 10 kurudi chini hilo sio zuri, maana yake toka itengenezwe imeshindwa kutunza umeme, ivo bac haito kua na uwezo wa kudumu kwa muda mrefu.

21/10/2025

19/10/2025
Critical dashboard warning lights
18/10/2025

Critical dashboard warning lights

18/10/2025
Wale madereva wa           hii ni mahususi sana kwenu, muda na wakati wowote tupo pamoja nanyi kuwahudumia vyombo vyenu ...
27/09/2025

Wale madereva wa hii ni mahususi sana kwenu, muda na wakati wowote tupo pamoja nanyi kuwahudumia vyombo vyenu vipatapo shida barabarani.

  ..MNAPOTAKA KUPANDA BODA BODA TUWE NA BODA MAALUM SIO KUPANDA BODA YOYOTE ILE ..ALAFU DEREVA WA BODA AWE NA NIDHAMU NA...
28/08/2025

..MNAPOTAKA KUPANDA BODA BODA TUWE NA BODA MAALUM SIO KUPANDA BODA YOYOTE ILE ..ALAFU DEREVA WA BODA AWE NA NIDHAMU NA MWILI WAKE NA CHOMBO CHAKE MFANO AWE ANAVAA VIATU..AWE ANAVAA VIZURI NGUO..PIKIPIKI YAKE IWE NA VIGEZO VYOTE MFANO HELMENT.SIDE MIRA..DEREVA AWE MTU WA MAKAMO...WENGINE SIO MADEREVA KAMILI...JANA KUNA BODA KABEBA ABILIA ALIPOINGIA BARABARANI WOTE WAKAINGIA CHINI YA FUSO WAKATOKEA NYUMA YA FUSO WAKIWA WAMEKUFA...NILIPOULIZA KWA BODA WANGU AKASEMA YULE NDIO ANAANZA KUENDESHA ABILIA LEO NA KAJIFUNZA PIKIPIKI KWA SIKU TATU TU...HAJUI SHERIA ZA BARABARA..HAJUI KEEP LEFT INATAKA NINI NDIO KILICHOTOKEA...TUNAPOTEZA NGUVU KAZI YA TAIFA

BIMA YA MAGARI YA THIRD PARTY INAFAIDA GANI KWA MIE NINAYEKATA BIMA?Ndugu WasomajiKwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria...
10/03/2025

BIMA YA MAGARI YA THIRD PARTY INAFAIDA GANI KWA MIE NINAYEKATA BIMA?
Ndugu Wasomaji
Kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria ya Bima za Magari Tanzania (Motor Vehicle Insurance Act, Cap.169), kila chombo cha moto lazima kiwe na bima ya utatu (Third party policy). Maana ya neno ni *Third party* ni mtu wa tatu.

*Kwa nini mtu wa tatu?
Ni mtu wa tatu kwa sababu mtu wa kwanza *first party* ni yule mwenye gari. *Second party* ni kampuni ya Bima (Insurer). Hawa ndio wahusika (parties) kwenye mkataba wa bima (contract of insurance). Mtu mwingine yeyote ambaye sio mhusika katika mkataba huo wa bima anaitwa *thirdy party*. Kwa hiyo kwa mfano, *Johnson* ana gari ambalo amekatia bima ya third party kwa kampuni ya *A2Z Insurance Limited*, hapa mkataba wa bima ni kati ya Johnson na A2Z Insurance Ltd. Watu wengine wowote k**a vile dereva, abiria, dereva/mmiliki wa gari jingine au mali iliyopo barabarani ni third party. Hao third party niliowataja hapo ndio walengwa (Wanufaika) wa mkataba wa bima kati ya Johnson na A2Z na sio Johnson mwenyewe wala gari yake. Hivyo, ikitokea gari ya Johnson imepata ajali na kumjeruhi au kumuua mtu yeyote (mfano abiria waliokuwemo ndani ya hiyo gari), hapo abiria ndio watakaolipwa. Au k**a gari ya Johnson iligonga gari ya Jamal na kuiharibu, basi kampuni ya bima ya A2Z italipia gharama za matengenezo ya gari la Jamal na sio la Johnson.

Kampuni ya bima ya A2Z ingeweza tu kulipia gharama za matengenezo ya gari la Johnson (aliyekata bima) na lile la Jamal, iwapo tu Johnson angekuwa amekata bima kubwa (mseto) ambayo huitwa *comprehensive*. Nje ya hapo, Johnson itabidi ajigharamie matengenezo ya gari lake hata k**a gari lake lilikuwa na bima, sababu bima yake ni third party (inamhusu mtu mwingine sio yeye Johnson).

*Sasa basi Kuna faida Gani ya Kulazimishwa Kukata Bima ya Third Party Wakati mimi Mwenyewe Sifaidiki Nayo*?
Huenda na wewe umekuwa ukijiuliza swali hili. Basi jibu ni hili.
1. Bima ya third party imewekwa na serikali kwaajili ya kumlinda mwananchi asiye sehemu ya mkataba wa bima. Ndio maana bima hii ni ya lazima, tofauti na bima ya comprehensive.
2. Kisheria anayesababisha madhara ana wajibu wa kurekesbisha madhara hayo kwa kumlipa fidia yule aliyemsababishia madhara. Hivyo, k**a wewe una gari endapo utagonga mtu au kuharibu mali ya mtu mwingine una wajibika kisheria kulipa gharama ya uharibifu huo uliousababisha.
3. Kwa kutambua kuwa sio kila wakati, mmiliki anakuwa na hela ya kulipia fidia ya hasara serikali ikaweka utaratibu wa bima ili mmiliki anapotakiwa kulipa hiyo bima, kampuni ya bima ndio ilipe.
4. Hivyo, basi bima ya third party inamsaidia mmiliki wa gari lililosababisha ajali kumlipa fidia mtu aliyesababishiwa ajali, badala ya mmiliki kutoa hela mifukoni mwake.
Kwa hiyo, ndio kusema kwamba k**a Johnson alipokuwa akiendesha gari aliligonga gari la Jamal na kusababisha Jamal na abiria wake waumie, na pia gari kuharibika sana. Wajibu wa Johnson ni kumlipa fidia Jamal na abiria wake na kukarabati lile gari. Tuseme kwa mfano gari hasara aliyoipata Jamal ni 5,000,000 na abiria wanatakiwa kulipwa 2,000,000. Basi kiwango hiki cha 7,000,000 kitalipwa na kampuni ya bima badala ya hizo fedha kutoka mifukoni mwa Johnson.
Ni matumaini yangu kwa maelezo haya utakuwa umeongeza uelewa

Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote.

Spark Plug Socket Wrench T-Handle 14mm,16mm& 21mm ,Spark Plug Tool,Spark Plug Removal Tool,Spark Plug Socket Wrench,Car ...
29/07/2024

Spark Plug Socket Wrench T-Handle 14mm,16mm& 21mm ,
Spark Plug Tool,Spark Plug Removal Tool,Spark Plug Socket Wrench,Car
PRICE: 5,000Tsh

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mafundi Bora Wa Magari Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Mafundi Bora Wa Magari Tanzania:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram