Tanzania Paralympic Committee

Tanzania Paralympic Committee Tanzania Paralympic Committee (TPC) is the organization which enhances sports and athletes for Tanza

Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya TANZANIA Paralympic Committee ndugu Ernest Nyabalale alikuwa ni miongoni mwa wachezaji w...
16/10/2023

Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya TANZANIA Paralympic Committee ndugu Ernest Nyabalale alikuwa ni miongoni mwa wachezaji walioiwakilisha timu ya kuogelea ya TPC. TPC imeshiriki ikiwa ni miongoni mwa timu 11 zilizoshiriki Mashindano ya kuogelea ya kwanza ya Taifa kwa watu wenye ulemavu Tanzania 🇹🇿. Ernest ameshika nafasi ya tatu baada ya kutanguliwa na wachezaji wawili wa timu ya ZANZIBAR Talent Swimming CLUB kutoka Zanzibar katika mtindo wa freestyle katika bwawa la GYMKHANA CLUB DAR ES SALAAM.

Mashindano ya kuogelea kwa watu wenye ulemavu yamefanyika kwa mara ya kwanza Tanzania 🇹🇿. Ni furaha iliyoje kuona wachez...
16/10/2023

Mashindano ya kuogelea kwa watu wenye ulemavu yamefanyika kwa mara ya kwanza Tanzania 🇹🇿. Ni furaha iliyoje kuona wachezaji 82, vilabu 11 na makampuni na taasisi zaidi ya 14 zikifanikisha mashindano haya. HONGERA pia kwa Baraza la Michezo la Taifa BMT na pia Baraza la Taifa la michezo ZANZIBAR kwa mchango wenu na ushirikiano mliotoa na kufanikisha Chama cha Kuogelea kwa watu wenye ulemavu Tanzania TPSA wakaweza kufanikisha mashindano haya.

Ni tukio la kihistoria, tarehe 14.10.2023 tunza tarehe hii siku ya Nyerere hapa Dar es Salaam kutakuwa na mashindano ya ...
26/07/2023

Ni tukio la kihistoria, tarehe 14.10.2023 tunza tarehe hii siku ya Nyerere hapa Dar es Salaam kutakuwa na mashindano ya kutafuta vipaji vya kuogelea kwa watu wenye ulemavu.

Hili tukio si la kukosa kabisa, watu wenye ulemavu ni muda wa kujiandaa na mazoezi kuanzia sasa hadi siku ya tukio.
Taarifa zingine MUHIMU zinafuata

*Tanzania Kushiriki Mashindano ya Ulaya - Poland kuelekea Kombe la Dunia 2022.*Timu ya Taifa ya Tanzania kwa mpira wa mg...
11/05/2022

*Tanzania Kushiriki Mashindano ya Ulaya - Poland kuelekea Kombe la Dunia 2022.*

Timu ya Taifa ya Tanzania kwa mpira wa mguu kwa walemavu Tembo Warriors imepata mwaliko rasmi wa kushiriki mashindano ya ulaya nchini Poland. Mashindano hayo yanayojulikana k**a *Amp-Futbal Europe 2022* yanayo tarajia kufanyika mwezi wa sita kati ya tarehe 10 hadi 13 katika mji wa *Warsaw Poland.*

Mashindano haya yanatajia kushirikisha nchi nne, nchi tatu kutoka bara la ulaya (England, Italy na Poland) na nchi moja kutoka Africa. Tanzania ndiyo nchi pekee ya africa iliyopata mwaliko kati ya nchi 18 za Africa na nchi ya pekee kati ya nchi nne za Africa zilizofuzu kwenda kombe la Dunia.

Rais wa Shirikisho TAFF ndg. Peter Sarungi amesema kwamba Tanzania inazidi kung'ara katika mchezo huu na hii inatokana na ushiriki wa Serikali yetu na wadau wengine kusaidia kulea na kuhudumia mchezo huu nchini. Mfano mzuri uliochukuliwa na mataifa mbalimbali ya nje ni utayari na ukubali wa *Rais Samia Suluhu na Serikali yake* kugharamia na kuandaa mashindano ya Africa (CANAF 2021)

Kamati ya Paralimpiki Tanzania na Chama cha Riadha Tanzania kwa watu wenye ulemavu (Tanzania Para Athletic Association-T...
05/05/2022

Kamati ya Paralimpiki Tanzania na Chama cha Riadha Tanzania kwa watu wenye ulemavu (Tanzania Para Athletic Association-TPAA) imeteua makocha wa Timu ya Taifa.
Tunawatakia kila heri na mafanikio makubwa na kuweza kuinua viwango vya wachezaji wetu.
Hongera Kocha Iddi Muhunzi na Kocha Bahati Mgunda.

25/04/2022
"Sports associations for people with disabilities hail President Samia" https://www.ippmedia.com/en/sport/sports-associa...
10/12/2021

"Sports associations for people with disabilities hail President Samia" https://www.ippmedia.com/en/sport/sports-associations-people-disabilities-hail-president-samia%C2%A0

​​​​​​​A day after President Samia Saluhu Hassan hosted Tanzania's amputee football team 'Tembo Warriors' players and officials in a function,which took place in Dar es Salaam early this week, some leaders of sports associations for people with disabilities have hailed the President fo...

18/11/2021

Kwa Mara ya Kwanza Mashindano ya Afrika ya mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu kufanyika Tanzania mwezi huu katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Ni michuano muhimu kuelekea katika kombe la Dunia kwa watu wenye ulemavu.
Hongereni sana Tanzania Amputee Football Federation (TAFF) na wadau wote muhimu wakiwemo serikali ya Jamhur ya Muungano ya Tanzania na Tanzania Football Federation

Asante Mhe *Rais Samia Suluhu Hassan* kwa kusisitiza maandalizi mazuri ya mashindano haya.

Rais wa TPC ndugu Tuma Dandi akiwa picha ya pamoja na Rais wa International Paralympic Committee ndugu Andrew Person (ri...
18/11/2021

Rais wa TPC ndugu Tuma Dandi akiwa picha ya pamoja na Rais wa International Paralympic Committee ndugu Andrew Person (right).
Ni furaha kubwa kukutana na Rais wa IPC kwa ajili ya maendeleo ya michezo ya watu wenye ulemavu nchini Tanzania na duniani kwa ujumla.

04/11/2021

Kwa Mara ya Kwanza Mashindano ya Afrika ya mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu kufanyika Tanzania mwezi huu katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Ni michuano muhimu kuelekea katika kombe la Dunia kwa watu wenye ulemavu.
Hongereni sana Tanzania Amputee Football Federation (TAFF) na wadau wote muhimu wakiwemo serikali ya Jamhur ya Muungano ya Tanzania na Tanzania Football Federation

Asante Mhe *Rais Samia Suluhu Hassan* kwa kusisitiza maandalizi mazuri ya mashindano haya.

Rais wa Tanzania Paralympic  Committee ndugu Tuma Dandi anaiwakilisha Tanzania katika Mkutano Mkuu wa African Paralympic...
31/10/2021

Rais wa Tanzania Paralympic Committee ndugu Tuma Dandi anaiwakilisha Tanzania katika Mkutano Mkuu wa African Paralympic Committee unaofanyika jijini Rabat nchini Morocco.
Tunakutakia Mkutano Mkuu mwema

20/09/2021

Asante sana Simba Sports Club kwa kutupa nafasi amputee football katika Simba day. Hakika event ilifana na mmefanya jambo kubwa kwa watu wenye ulemavu. Tunawaombea Simba Mwenyezi Mungu awatimizie ndoto yenu ya kuchukua ubingwa wa afrika, ubingwa wa Tanzania kwa Mara nyingine Tena na mutetee kombe la Azam.
Tumejisikia wenye furaha na kuthaminiwa sana na jamii yetu. Asante sana Simba Sports. Kwa hakika hatutasahau siku hii ya Simba 19.9.2021.

17/09/2021

Mahojiano ya Kocha Bahati Mgunda na TV3 yanaendelea

17/09/2021

Kocha wa Timu ya Taifa ya Riadha Mr. Bahati Mgunda akiwa studio TV3 kuzungumza masuala mbalimbali ya Michezo ya Paralympic Tokyo Japan

Kikao cha strategic plan ya TPC pamoja na wadau wake. Tunashukuru sana BMT na serikali kwa ujumla kuhudhuria kikao hiki....
15/09/2021

Kikao cha strategic plan ya TPC pamoja na wadau wake. Tunashukuru sana BMT na serikali kwa ujumla kuhudhuria kikao hiki. Aidha wadau wengine wote mliohudhuria mmetoa michango kizuri na TOC tutafanyia kazi.

06/09/2021

Kuna sababu nyingi sana kwa nchi kushiriki katika michezo. Moja ya sababu ni kuitangaza nchi ila sasa tunatakiwa kuitangaza nchi kwa kushinda medali ndio iwe ni ajenda kubwa kwa nchi. Ila tunatakiwa tujiandae zaidi na zaidi kutimiza ndoto yetu hiyo..

06/09/2021

Kufungwa kwa Michezo ya Paralympic ndio mwanzo wa Maandalizi wa Michezo ya 2024 Ufaransa. Tutajipanga ili twende tukiwa imara zaidi kuliko wakati wote tulioshiriki.

Address

Studio, Kinondoni
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Paralympic Committee posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram