28/10/2025
Leo tarehe 28 Oktoba 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, ametoa wito kwa watumishi wote wa taasisi hiyo na Watanzania kwa ujumla kujItokeza kwa wingi kupiga kura kesho tarehe 29 Oktoba 2025, ili kuweza kuendeleza mapinduzi yaliyoanzwa miaka minne iliyopita kwenye sekta ya Afya.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Dkt. Msemo amesisitiza umuhimu wa amani, umoja na uwajibikaji wa kiraia katika kipindi hiki muhimu kwa taifa, ndio nguzo pekee ya kuendeleza maendeleo kwani hakuna maendeleo mahali ambapo hamna amani hivyo nivyema kuitunza amani iliyopo ili kila mmoja wetu ashughulike na kujiletea maendeleo kwake na taifa kwa ujumla.
“Kura yako ni sauti yako. Tujitokeze kwa wingi, kwa amani na kwa upendo kwa nchi yetu ili kuweza kuchagua viongozi wenye kuweza kuleta tija k**a ilivyokuwa kipindi cha miaka minne iliyopita ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,” amesema Dkt. Msemo.
Dkt. Msemo Ameongeza kuwa Dkt. Samia ameonesha dhamira ya dhati ya kukuza sekta ya Afya, hususan katika eneo la matibabu ya Saratani, jambo linaloleta matumaini mapya kwa Watanzania wote.
Kesho tarehe 29/10/2025, ndio siku pekee ambapo watanzania watajitokeza kwaajili ya kufanya maamuzi ya kuwachagua viongozi wanaowaona wanafaa kuanzia ngazi ya madiwani, wabunge mpaka Rais kwa ajili ya kuwaongoza kwa miaka mitano ijayo kuanzia 2025 – 2030.
.mseti_na_cancer