Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Wanawake wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wameungana na wanawake wengine kuadhimisha siku ya wanawake duniani leo Machi...
08/03/2026

Wanawake wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wameungana na wanawake wengine kuadhimisha siku ya wanawake duniani leo Machi 8, 2026 katika viwanja vya Barafu Mburahati jijini Dar es Salaam, wakilenga kuhamasisha haki na usawa kwa wanawake na wasichana.

Maadhimisho haya yaliyoongonzwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Mhe. Arbelt Chalamila yamehudhuriwa na mamia ya wanawake kutoka taasisi mbalimbali za umma na binafsi, vikundi vya kijamii pamoja na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kusherehekea mafanikio ya wanawake na kujadili namna ya kuimarisha usawa wa kijinsia katika jamii.

Akizungumza katikq maadhimisho hayo, mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila amewasisitiza wanawake juu ya umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya taifa huku akiwataka kuendelea kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi na kutumia fursa zilizopo kuboresha maisha yao na ya jamii inayowazunguka.

Maadhimisho haya yamefanyika chini ya kauli mbiu isemayo, "Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050” inayohamasisha wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za uongozi na maendeleo ya kijamii na kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kupaza sauti ya usawa na haki kwa wanawake.

Maadhimisho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wanawake na wadau mbalimbali ili kujadili changamoto zinazowakabili pamoja na kuweka mikakati ya kuimarisha afya, ustawi na maendeleo ya wanawake nchini.

HERI YA SIKUKUU YA WANAWAKE DUNIANI....

Saratani ya Mlango wa kizazi na matiti ndio Saratani zinazowaathori kinamqmq wengi Duniani, katika kuadhimisha siku yenu...
08/03/2026

Saratani ya Mlango wa kizazi na matiti ndio Saratani zinazowaathori kinamqmq wengi Duniani, katika kuadhimisha siku yenu tunawa kumbusha kufanya uchunguzi mara kwa mara kwani Saratani ikigundulika mapema inatibika....

Je wajua?....
08/03/2026

Je wajua?....

Heri ya siku ya wanawake Duniani...
08/03/2026

Heri ya siku ya wanawake Duniani...

Tunawatakia heri ya siku ya wanawake Duniani....
07/03/2026

Tunawatakia heri ya siku ya wanawake Duniani....

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo amefanya mazungumzo na Mhariri wa Uhuru Communi...
06/03/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo amefanya mazungumzo na Mhariri wa Uhuru Communication Bw. Abdallah Mweri, wakati mhariri huyo alipotembelea katika Taasisi hiyo.

Bw. Mweri pia ametembelea maeneo mbalimbali katika Taasisi hiyo ikiwemo sehemu za mashine za LINAC, PET CT-Scan, pamoja na sehemu mbalimbali za Taasisi hiyo ili kujifunza kuhusu mambo mbalimbali yanavyokwenda hapo ORCI.

06/03/2026
06/03/2026

Elimu kuhusu kipimo cha Biopsy..

05/03/2026

Jasmin Said akielezea safari yake kuhusu ufanyaji wa uchunguzi wa Saratani ya Matiti..

05/03/2026

Ukweli kuhusu 'Biopsy'

Usikose kupitia hapa uweze kujifunza juu ya uchunguzi wa Saratani.....
04/03/2026

Usikose kupitia hapa uweze kujifunza juu ya uchunguzi wa Saratani.....

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram