13/03/2026
K**ati ya kudumu ya bunge ya afya na Masuala ya ukimwi wamefanya ziara katika taasisi ya Saratani Ocean Road leo tarehe 13/3/2026 ambapo ametembelea maeneo mbalimbali na kujionea uwekezaji mkubwa wa mashine za kisasa uliofanywa na serikali ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekti wa k**ati hiyo Dkt. Johannes Lukumai amesema kuwa Dkt. Samia amewekeza kiasi cha shilingi Tilioni 6.7 katika Wizara ya afya, akionesha jinsi gani awamu hii ya sita imetoa kipaumbele zaidi katika sekta ya afya.
Aidha Dkt. lukumai amempongeza Dkt. Msemo kwa juhudi kubwa aliyoifanya kuibadilisha ORCI na katika kutambua hilo amewaagiza wizara ya Afya kuhakikisha kuwa wanampatia cheti cha pongezi na kutambua juhudi za mabadiliko makubwa aliyoyafanya katika kipindi chake cha miezi kumi na tatu tu tangu ateuliwe kuwa mkurugenzi katika Taasisi hiyo.
Katika hatua nyingine Dkt. Lukumai ameishauri k**ati yake kuridhia shauri lake la kumualika mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo bungeni ili aweze kutoa elimu juu ya Saratani kwa wabunge.
Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo ameishukuru k**ati kwa kutembelea taasisi hiyo huku akielezea juhudi za kuongeza mashine za kisasa za tiba ya mionzi na kusema kwa sasa ORCI ina jumla ya mashine tano za mionzi, ambapo tatu ni mashine mpya kabisa za kisasa aina ya LINAC mashine moja na Cobalt mashine mbili, zikiwepo zile mashine zilizokuwepo awali ambazo ni LINAC mbili.
Dkt. Msemo amesema kuwa kuongezeka kwa mashine hizo kumeongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa taasisi yake kutoa huduma za tiba ya mionzi kwa wagonjwa wengi zaidi kwa wakati, hivyo kupunguza changamoto ya kusubiri huduma kwa muda mrefu K**a ilivyokuwa awali.
Aidha Dkt. Msemo amesisitiza kuwa uwepo wa mashine hizo utavutia kwa kiasi kikubwa sana suala la tiba utalii kwani kwa sasa wagonjwa watalazimika kusubiri kwa muda mfupi wa wiki mbili ukilinganisha na nchi jirani ambapo huduma hii wagonjwa wanalazimika kusubiri kwa miezi zaidi ya tisa.
Maboresho hayo yanaendelea kuiweka ORCI katika nafasi ya kuwa kituo cha ubora katika uchunguzi na matibabu ya Saratani Afrika