Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Taasisi ya Saratani Ocean road kwa kushirikiana na Taasisi ya Aerospace medical and training centre leo tarehe 31 March ...
31/03/2026

Taasisi ya Saratani Ocean road kwa kushirikiana na Taasisi ya Aerospace medical and training centre leo tarehe 31 March wameweka kambi ya uchunguzi wa Saratani kwa watumishi na wananchi waliofika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Aman Karume uliopo Zanzibar.

Karibu tukufanyie uchunguzi......
26/03/2026

Karibu tukufanyie uchunguzi......

25/03/2026
Ni Radio Uhuru, jumatatu asubuhi, usikose kutufatilia ujue kuhusu Saratani ya Utumbo mpana....
22/03/2026

Ni Radio Uhuru, jumatatu asubuhi, usikose kutufatilia ujue kuhusu Saratani ya Utumbo mpana....

Usikose kufuatilia kipindi hiki tafadhali ili kujifunza kuhusu Saratani ya Utumbo Mpana...
22/03/2026

Usikose kufuatilia kipindi hiki tafadhali ili kujifunza kuhusu Saratani ya Utumbo Mpana...

Tunawatakia heri ya sikukuu ya Eid El-Fitri...
20/03/2026

Tunawatakia heri ya sikukuu ya Eid El-Fitri...

DKT. MSEMO AZINDUA KAMATI YA USHAURI NA USAJILI KUHUSU  SARATANI ( CANCER REGISTRY)  K**ati  ya ushauri na usajili kuhus...
19/03/2026

DKT. MSEMO AZINDUA KAMATI YA USHAURI NA USAJILI KUHUSU SARATANI ( CANCER REGISTRY)

K**ati ya ushauri na usajili kuhusu saratani imefanya uzinduzi wa k**ati hiyo chini ya mwenyekiti wake ambae pia ni mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika majengo ya Taasisi hiyo leo tarehe 19/03/2026.

Dkt. Msemo amesema kuwa k**ati hii itasaidia katika ukusanyaji wa takwimu juu ya wagonjwa wa saratani nchini ambapo inakadiliwa kwa mwaka watu zaidi ya milioni 10 hupoteza maisha.

Dkt Msemo amewataka wanak**ati kuwajibika na kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuongeza ufanisi ili iwe rahisi katika ukusanyaji wa takwimu na kuisaidia serikali katika zoezi hili.

Nae meneja wa ushauri na usajili kuhusu Saratani Dkt Johnson Katanga ameeleza juu ya changamoto watakazo kutana nazo wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za wagonjwa wa saratani, ambapo amesema baadhi ya changomoto hizo ni pamoja upungufu wa vitendea kazi wakati wa ukusanyaji takwimu.

Aidha Dkt. Katanga amewataka wanak**ati kuwakumbusha wauguzi kuwasajili wagonjwa wa saratani ili kuweza kupata takwimu sahihi juu ya wagonjwa hao katika mkoa wa Dar es salaam.

K**ati hii ya ushauri kuhusu saratani inaundwa na hospitali zaidi ya tano kutoka wilaya ya ilala, Dar es salaam. Hospital izo ni pamoja na ORCI, Muhimbili, Amana na Besta.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo, amekabidhi zawadi ya sikukuu ya Eid El-Fitri kw...
19/03/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo, amekabidhi zawadi ya sikukuu ya Eid El-Fitri kwa wafanyakazi wote wa Taasisi hiyo leo tarehe 19/03/2026, huku akiwatakia sikukuu njema ya Eid El-Fitri.

Akipokea zawadi hizo kwa niaba ya watumishi wa Taasisi ndg Mnaro Msuya ambae pia ni Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi tawi la Taasisi ya Saratani Ocean Road amemshukuru mkurugenzi kwa moyo aliouonesha na kusema kuwa ni viongozi wachache sana huwakumbuka watumishi hasa kwenye Taasisi zenye watumishi wengi k**a hii.

Sikukuu ya Eid-El-Fitri husherehekewa na waislamu mara baada ya kumaliza siku 30 za mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo kwa mwaka huu inatazamiwa kuwa tarehe 20/03/2026 au 21/03/2025 kutegemeana na mwandamo wa mwezi.

Kwa maoni na ushauri tafadhali wasiliana nasi kupitia namba zilizopo hapo juu.....
18/03/2026

Kwa maoni na ushauri tafadhali wasiliana nasi kupitia namba zilizopo hapo juu.....

Usikose kufuatilia kipindi hiki....
18/03/2026

Usikose kufuatilia kipindi hiki....

K**ati ya  kudumu ya bunge  ya afya na Masuala ya ukimwi wamefanya ziara katika taasisi ya Saratani Ocean Road leo tareh...
13/03/2026

K**ati ya kudumu ya bunge ya afya na Masuala ya ukimwi wamefanya ziara katika taasisi ya Saratani Ocean Road leo tarehe 13/3/2026 ambapo ametembelea maeneo mbalimbali na kujionea uwekezaji mkubwa wa mashine za kisasa uliofanywa na serikali ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekti wa k**ati hiyo Dkt. Johannes Lukumai amesema kuwa Dkt. Samia amewekeza kiasi cha shilingi Tilioni 6.7 katika Wizara ya afya, akionesha jinsi gani awamu hii ya sita imetoa kipaumbele zaidi katika sekta ya afya.

Aidha Dkt. lukumai amempongeza Dkt. Msemo kwa juhudi kubwa aliyoifanya kuibadilisha ORCI na katika kutambua hilo amewaagiza wizara ya Afya kuhakikisha kuwa wanampatia cheti cha pongezi na kutambua juhudi za mabadiliko makubwa aliyoyafanya katika kipindi chake cha miezi kumi na tatu tu tangu ateuliwe kuwa mkurugenzi katika Taasisi hiyo.

Katika hatua nyingine Dkt. Lukumai ameishauri k**ati yake kuridhia shauri lake la kumualika mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo bungeni ili aweze kutoa elimu juu ya Saratani kwa wabunge.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo ameishukuru k**ati kwa kutembelea taasisi hiyo huku akielezea juhudi za kuongeza mashine za kisasa za tiba ya mionzi na kusema kwa sasa ORCI ina jumla ya mashine tano za mionzi, ambapo tatu ni mashine mpya kabisa za kisasa aina ya LINAC mashine moja na Cobalt mashine mbili, zikiwepo zile mashine zilizokuwepo awali ambazo ni LINAC mbili.

Dkt. Msemo amesema kuwa kuongezeka kwa mashine hizo kumeongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa taasisi yake kutoa huduma za tiba ya mionzi kwa wagonjwa wengi zaidi kwa wakati, hivyo kupunguza changamoto ya kusubiri huduma kwa muda mrefu K**a ilivyokuwa awali.

Aidha Dkt. Msemo amesisitiza kuwa uwepo wa mashine hizo utavutia kwa kiasi kikubwa sana suala la tiba utalii kwani kwa sasa wagonjwa watalazimika kusubiri kwa muda mfupi wa wiki mbili ukilinganisha na nchi jirani ambapo huduma hii wagonjwa wanalazimika kusubiri kwa miezi zaidi ya tisa.

Maboresho hayo yanaendelea kuiweka ORCI katika nafasi ya kuwa kituo cha ubora katika uchunguzi na matibabu ya Saratani Afrika

11/03/2026

Bi Sarah afurahishwa na huduma za ORCI, aishukuru serikali ya awamu ya sita, wizara ya Afya oa.oja na ORCI...

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram