Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Heri ya wiki ya maabara...
24/04/2026

Heri ya wiki ya maabara...

23/04/2026

Mgonjwa wetu anaendelea kuoata huduma kwa msaada wa ustawi wa jamii pekee.

22/04/2026
Usikose kutazama kipindi hiki....
22/04/2026

Usikose kutazama kipindi hiki....

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo mapema jana akiwa pamoja na mwenyeji wake, Ra...
21/04/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo mapema jana akiwa pamoja na mwenyeji wake, Rais wa Zhejiang Cancer Hospital, Prof. Xiangdong Cheng, wametiliana saini makubaliano ya ushirikiano kati ya taasisi hizi mbili.

Dkt. Msemo amesema kuwa makubaliano haya yanalenga kuimarisha huduma za saratani kupitia kubadilishana ujuzi na uzoefu ambapo Wataalam kutoka Zhejiang Cancer Hospital wanatarajiwa kuja Tanzania kuwajengea uwezo wataalam wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, hasa katika matumizi ya teknolojia ya kisasa ya PET-CT pamoja na Cyclotron ikiwa ni huduma muhimu iliyozinduliwa mwaka huu na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Aidha Dkt. Msemo amesisitiza kuwa wataalam kutoka ORCI nao watapata fursa ya kwenda China kwa ajili ya mafunzo ya hali ya juu, hatua itakayoongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wagonjwa wa saratani nchini Tanzania.

Huu ni ushahidi kuwa kwa kushirikiana Taasisi hizi mbili, kuna uwezekano wa kufika mbali zaidi katika kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha.

Dkt. Msemo yupo nchini China kwaajili ya mkutano maalum wa wadau wa Saratani ambapo atatumia fursa hii kushirikiana na Taasisi zinazojihusisha na matibabu huu ya Saratani ili kujenga ufanisi kwenye utoaji wa huduma hiyo nchini.

Hongera sana Dkt. Diwani Msemo....
20/04/2026

Hongera sana Dkt. Diwani Msemo....

Usikose kusikiliza kipindi hiki, ni jumatatu ya tarehe 20/04/2026
18/04/2026

Usikose kusikiliza kipindi hiki, ni jumatatu ya tarehe 20/04/2026

Watumishi wa Taasisi ya saratani ocean road siku ya tarehe 14/4/2026 wamefanya uchaguzi wa kuchagua wafanyakazi bora wa ...
15/04/2026

Watumishi wa Taasisi ya saratani ocean road siku ya tarehe 14/4/2026 wamefanya uchaguzi wa kuchagua wafanyakazi bora wa mwaka katika kila idara ya taasisi hiyo.

Wafanyakazi bora hao kutoka katika idara mbalimbali za Taasisi ya saratani ocean road ni Ferouz Dihile, Mohamed Mbwana, Richard Makala na Nyangazi Ndatima.

Wengine ni Devota Mtei, Elikaanany Mafie, Hamisi Mbazi, Hamisi Malima na Penina Mnandi.

Ushindi wa Mfanyakazi Hodari wa ORCI umekwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Diwani Msemo.

Aidha uchaguzi huo wa wafanyakazi bora umesimamiwa na chama cha wafanyakazi wa serikali na afya tawi la Taasisi ya saratani ocean road (TUGHE- ORCI).

Saratani ya koo....
14/04/2026

Saratani ya koo....

Leo Jumanne tarehe14/4/2026 Taasisi ya JEMA FOUNDATION chini ya Mkurugenzi  Jema Baruani imetoa msaada wa mashine maalum...
14/04/2026

Leo Jumanne tarehe14/4/2026 Taasisi ya JEMA FOUNDATION chini ya Mkurugenzi Jema Baruani imetoa msaada wa mashine maalumu zinazotumika katika tiba kemia zijulikanazo k**a Infusion pump, ambazo zina thamani ya shilingi za kitanzania Milioni 40, Ikiwa ni moja ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa mdau wa JEMA FOUNDATION ambaye anatimiza miaka 40.

Bi Jema Baruani amesema kuwa Taasisi yake imetoa vifaa ivyo ikiwa ni njia mojawapo ya kurudisha shukrani kwa jamii hasa wenye uhitaji wa matibabu ya magonjwa ya saratani.

Nae Bi. Nancy Moshi ambaye ni rafiki wa mdau ambaye anasherekea siku yake ya kuzaliwa, ametoa shukrani za dhati kwa niaba ya mdau uyo kwa kushukuru na kuziomba taasisi nyingine au wadau wengine wakiwa wanasherekea siku zao za kuzaliwa wawe wanasherekea katika kutoa msaada kwa wenye uhitaji.

Kwa upande wake Afisa muuguzi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Bi. Chausiku Chapuchapu kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI Dkt. Diwani Msemo, ametoa shukrani za dhati kwa uongozi wa Taasisi ya JEMA FOUNDATION pamoja na wadau wake kwa kutoa mashine hizo ambazo zitatumika katika tiba kemia.

Aidha Bi. Chapuchapu ametoa wito kwa wadau mbalimbali pamoja na Taasisi nyingine waweze kuiga Mfano wa JEMA FOUNDATION na mdau wake katika kutoa msaada kwa wenye uhitaji na wasiojiweza.

Je unaelewa nini kuhusu Saratani ya koo na Saratani ya maeneo ya kichwa na shingo? K**a unahitaji kujifunza tafadhali en...
12/04/2026

Je unaelewa nini kuhusu Saratani ya koo na Saratani ya maeneo ya kichwa na shingo? K**a unahitaji kujifunza tafadhali endelea kubaki nasi ili kujifunza zaidi ........

Tunawatakia mapumziko mema ya siku ya Karume......
07/04/2026

Tunawatakia mapumziko mema ya siku ya Karume......

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share