Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.....
13/11/2025

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.....

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo leo tarehe 12/11/2025 ametembelea ubalozi wa ...
12/11/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo leo tarehe 12/11/2025 ametembelea ubalozi wa India na kufanya mazungumzo na balozi Bishwadip Dey, kuhusu kuimarisha mahusiano baina ya Taasisi ya Saratani ya Ocean na Taasisi za saratani za India hasa zile zinazomilikiwa na Serikali ikiwemo Tata Memorial Hospital.

Dkt. Msemo amesema kuwa mazungumzo hayo yamelenga katika kuijengea Taasisi ya saratani uwezo wa rasilimali watu katika tiba za saratani pamoja na kunufaika na teknolojia za kisasa ambazo zinapatikana nchini India.
Hii itasaidia kuboresha tiba utalii pamoja na kuokoa fedha za serikali zinazotumiwa kupeleka wagonjwa India na pamoja na nchi zingine.

Aidha Dkt. Msemo amemshukuru Mheshimiwa Balozi kwa kukubali kuwa daraja la mashirikiano kati ya Taasisi ya Saratani Ocean Road na Taasisi za India kwani hili pia litajenga nguzo imara ya kidiplomasia baina ya watanzania na watu kutoka India.

Kwa upande wake Mheshimiwa Balozi Bishwadip ameipongeza Taasisi ya Saratani Ocean Road kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuokoa maisha ya watanzania.

Wakati huo huo Balozi Bishwadip ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuboresha miundombinu ya matibabu ya saratani kwa kununua mashine mpya zenye Teknolojia ya kisasa kwaajili ya kusaidia watanzania katika kipindi hiki cha awamu ya sita ya uongozi wa Dr Samia Suluhu Hassan.

11/11/2025
Rais wa bunge la Comoro ambae pia ndie  kiongozi wa pili na msaidizi wa Rais wa nchi hiyo Bw. Moustadroine Abdou, mapema...
05/11/2025

Rais wa bunge la Comoro ambae pia ndie kiongozi wa pili na msaidizi wa Rais wa nchi hiyo Bw. Moustadroine Abdou, mapema leo amesema kuwa atahakikisha wacomoro wote wenye shida za Saratani wnaletwa nchini Tanzania na kufikishwa katika Taasisi ya Saratani ocean road na kupata tiba stahiki.

Akizungumza katika ziara fupi aliyoifanya mapema leo katika Taasisi hiyo, Bw. Abdou amesema amestaajabishwa sana kuona mashine za kisasa zilizopo hapa ORCI na kusema kuanzia sasa hakuna haja ya wacomoro kupoteza pesa za walipa kodi wao kuoeleka wagonjwa Ulaya na Asia huku akisisitiza kuwa Taasisi ya Saratani ocean road inatosha kuwa mkombozi wa wananchi hao.

Katika hatuaa nyingine Bw. Abdou amesisitiza kuwa ili kupata wateja wengi kutoka nchi mbalimbali barani Afrika na hata nje ya nchi ya Afrika ni vyema watanzania wakadumisha Amani iliyopo na kujiepusha na kila aina ya vurugu ambazo zinaweza kuleta sintofahamu.

Aidha amempongeza Dkt. Samia kwa kuwezesha Taasisi hiyo kuwa na vifaa hivyo na kuahidi nchi yake kushirikiana na Tanzania ili kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kiafya.

Nae Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw. Said Yakubu amesema nchi ya Tanzania siku zote ipo tayari kwa ushirikiano waowote na Comoro hivyo amemtoa hofu Mhe. Abdou kuhusu jambo hilo, huku akisema kuwa uhusiano huu utaimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizo mbili.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo amemshukuru Mhe. Abdou kwa ziara hiyo na kusisitiza kuwa ujio huo pia umekuwa ni wa kukuza ushirikiano zaidi, hivyo ORCI haItaacha fursa yoyote itakayotokana na wananchi wa Comoro.

Hii ni ziara ya siku moja ambapo kiongozi huyo pqmoja na ujumbe wake, wametembelea maeneo mbalimbali ya ORCI na kujionea namna uchunguzi na matibabu yanavyofanyika katika Taasisi hii.

Tunakutakia majukumu mema ya kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania..
05/11/2025

Tunakutakia majukumu mema ya kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania..

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu ya kuiongoza Tanzania...
05/11/2025

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu ya kuiongoza Tanzania...

Mafanikio makubwa sana yaliyopatikana Taasisi ya Saratani ocean road.....
28/10/2025

Mafanikio makubwa sana yaliyopatikana Taasisi ya Saratani ocean road.....

Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw. Said Yakub leo tarehe 28/10/2025 ametembelea katika Taasisi ya Saratani ocean road ...
28/10/2025

Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw. Said Yakub leo tarehe 28/10/2025 ametembelea katika Taasisi ya Saratani ocean road na kujionea namna usimikaji wa mashine mpya ya mionzi unavyoendelea.

Bw. Yakub amemshukuru mno Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka madaktari bingwa kutoka Taasisi ya Saratani ocean road,kwani hiyo imesaidia kupunguza hofu kuu ya ugonjwa wa saratani sababu mbali na matibabu waliyoyapata lakini pia wameweza kupata elimu itakayowasaidia namna ya kujiepusha na maradhi hayo.

Aidha Bw. Yakub, ameisifu ORCI kwa namna ilivyojiandaa kupokea wagonjwa wa saratani kutoka Comoro kwani vifaa vilivyowekezwa ni vya kisasa na hivyo kuashiria kuwa hakuna haja ya wagonjwa kutoka Comoro kwenda nje ya Afrika, bali ni kuja Tanzania na huduma watazipata k**a zile za nchi zilizoendelea.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo amemshukuru Bw. Yakub kwa ujio huo na kumuahidi kila kipindi ambacho madaktari watahitajika kwenda Comoro wapo tayari kufanya hivyo kwani Taasisi ya Saratani ocean road sio ya watanzania pekee bali pia hata waafrika kwa ujumla.

Leo tarehe 28 Oktoba 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, ametoa wito ...
28/10/2025

Leo tarehe 28 Oktoba 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, ametoa wito kwa watumishi wote wa taasisi hiyo na Watanzania kwa ujumla kujItokeza kwa wingi kupiga kura kesho tarehe 29 Oktoba 2025, ili kuweza kuendeleza mapinduzi yaliyoanzwa miaka minne iliyopita kwenye sekta ya Afya.

Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Dkt. Msemo amesisitiza umuhimu wa amani, umoja na uwajibikaji wa kiraia katika kipindi hiki muhimu kwa taifa, ndio nguzo pekee ya kuendeleza maendeleo kwani hakuna maendeleo mahali ambapo hamna amani hivyo nivyema kuitunza amani iliyopo ili kila mmoja wetu ashughulike na kujiletea maendeleo kwake na taifa kwa ujumla.

“Kura yako ni sauti yako. Tujitokeze kwa wingi, kwa amani na kwa upendo kwa nchi yetu ili kuweza kuchagua viongozi wenye kuweza kuleta tija k**a ilivyokuwa kipindi cha miaka minne iliyopita ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,” amesema Dkt. Msemo.

Dkt. Msemo Ameongeza kuwa Dkt. Samia ameonesha dhamira ya dhati ya kukuza sekta ya Afya, hususan katika eneo la matibabu ya Saratani, jambo linaloleta matumaini mapya kwa Watanzania wote.

Kesho tarehe 29/10/2025, ndio siku pekee ambapo watanzania watajitokeza kwaajili ya kufanya maamuzi ya kuwachagua viongozi wanaowaona wanafaa kuanzia ngazi ya madiwani, wabunge mpaka Rais kwa ajili ya kuwaongoza kwa miaka mitano ijayo kuanzia 2025 – 2030.

.mseti_na_cancer

SportPesa Leo wametoa msaada wa mahitaji  mbalimbali ya msingi kwa kwa wagonjwa katika Taasisi ya saratani ocean road.Sp...
24/10/2025

SportPesa Leo wametoa msaada wa mahitaji mbalimbali ya msingi kwa kwa wagonjwa katika Taasisi ya saratani ocean road.

SportPesa imetoa msaada huo katika jitihada za kuunga mkono juhudi za serikali katika kusaidia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kugharamia matibabu.

Leo mapema viongozi wa Taasisi ya saratani ocean road wamepewa mafunzo maalum ya ufuatiliaji na tathimini kutoka ofisi y...
23/10/2025

Leo mapema viongozi wa Taasisi ya saratani ocean road wamepewa mafunzo maalum ya ufuatiliaji na tathimini kutoka ofisi ya waziri Mkuu na wizara ya afya.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo amesema mafunzo hayo yatasaidia hasa kuona namna utekelezaji wa Taasisi unavyofikia malengo yaliyowekwa na serikali.

Aidha Dkt. Diwani ametoa pongezi kwa serikali kwa kuanzishwa rasmi kwa shughuli ya ufuatiliaji na tathmini katika Taasisi za umma.

Pamoja na hayo Dkt. Diwani amesema kila kinacholetwa na serikali kinafanyiwa kazi na k**a Kuna sehemu panaitaji maboresho basi tunatoa maoni.

Kwa upande wake muwezeshaji kutoka Idara ya ufuatiliaji na Tathimini wizarani Bw. Kiwanila Kiiza amesema serikali imeamua kuwekeza na kuelekeza Taasisi zake zote za umma kuanzishwa shughuli za ufuatiliaji na tathimini rasmi kwa kuwa hapo kabla hazikuwepo, hivyo itawalazimu Taasisi kuwa na Idara rasmi za ufuatiliaji na tathmini kwa maeneo yote.

Mafundo hayo ni siku mbili ambapo yamenz leo trehe 23/10/2025 na kutegemewa kumalizika kesho.

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram