Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Leo mapema Taasisi ya Saratani Ocean Road imepokea msaada wa vifaa tiba kutoka BMG Group International Limited.Vifaa hiv...
12/12/2025

Leo mapema Taasisi ya Saratani Ocean Road imepokea msaada wa vifaa tiba kutoka BMG Group International Limited.

Vifaa hivyo vimepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo.

Dkt. Msemo amesema Taasisi imepata faraja kubwa pamoja na wagonjwa watafarijika kwa msaada huo kwa kuwa msaada huo utarahisisha moja kwa moja huduma kwa wagonjwa.

Dkt. Diwani ameongeza kwa kusema kitendo hicho kilichofanywa na BMG Group International ni kitendo kilichotukuka na Taasisi itahakikisha vifaa vyote vitatumika kwa ajili ya wagonjwa husika.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa BMG Group International Bw. Amani Temu amesema msaada huo waliotoa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii na Ili kuifikia jamii kwa ufanisi ni kutoa msaada huo kwa Taasisi ya saratani ocean road.

Bw. Temu amesema msaada huo waliotoa utaongeza zaidi ufanisi wa watumishi wa Taasisi ya saratani ocean road katika kurudisha afya njema kwa wagonjwa wa Saratani.

Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi ORCI, Dkt. Asafu Munema, mapema leo amemkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani...
12/12/2025

Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi ORCI, Dkt. Asafu Munema, mapema leo amemkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, cheti cha ithibati cha huduma za maabara kilichotolewa na SADCAS ambapo hii ni hatua kubwa inayothibitisha kuwa ORCI ndiyo Taasisi inayoongoza kwa ubora kwa kufuata viwango vya kimataifa kwenye matibabu ya Saratani.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Dkt. Msemo amesema, ORCI inaendelea kujipambanua na kwa sasa ipo kwenye mkakati wa kuhakikisha huduma zake zote zinapata ithibati, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuvutia tiba utalii nchini, hususan kwa wagonjwa wa Saratani kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Taasisi ya Saratani Ocean Road imekuwa mwanga wa matumaini kwa wagonjwa wengi, ikiwa na vifaa vya kisasa, wataalamu wenye weledi, na mazingira rafiki kwa tiba na uchunguzi. Ubora huu umeifanya kuwa moja ya Taasisi zinazotegemewa zaidi Afrika Mashariki na Kati kwenye uchunguzi na matibabu ya Saratani.

Cheti hiki kimekuja wakati ambao Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa, ameelekeza Taasisi zote chini ya wizara ya Afya kuhakikisha zinapata ithibati ili kuimarisha huduma za kiafya na kuongeza uwezo wa kutoa tiba kwa kiwango cha kimataifa.

ORCI imeanza kuvutia wageni mbalimbali kutoka barani Afrika kwa ajili ya mafunzo, ushirikiano na hata kupata matibabu. Wageni kutoka Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini, Nigeria, Comoro, na mataifa mengine wameendelea kutembelea taasisi hii ili kujifunza na kushirikiana katika mapambano dhidi ya Saratani ikiwamo kupata matibabu.

Cheti hicho cha ithibati kimetolewa mwaka huu ambapo kitadumu mpaka mwaka 2027 ambapo Taasisi ya SADCASS itakuja tena kufatilia k**a bado Taasisi hii imeendelea kubaki na ubora uleule uliopatikana kwenye uchunguzi wa awali wa mwaka huu.

Heri ya sikukuu ya Uhuru wa Tanzania Bara....
09/12/2025

Heri ya sikukuu ya Uhuru wa Tanzania Bara....

Taasisi ya Saratani ocean road leo wameitikia wito wa waziri wa Afya wa kuwataka kufika Muhimbili kwaajili ya kuhudhuria...
08/12/2025

Taasisi ya Saratani ocean road leo wameitikia wito wa waziri wa Afya wa kuwataka kufika Muhimbili kwaajili ya kuhudhuria kikao kazi maalum kwa watumishi wote wa Afya nchini.

Miongoni mwa mambo ambayo ameyasisitiza ni kuhakikisha kuwa watoa huduma wote wa Afya, wanatoa huduma kwa haki bila upendeleo wowote ule.

Hata hivyo Mhe. Mchengerwa amewataka watumishi hao kuongeza jitihada katika utumishi hao huku wakiepuka maneno yasiyofaa kwa wateja wao.

Katika kikao kazi cha watumishi wa Afya kilichofanyika katika hospitali ya Muhimbili....
08/12/2025

Katika kikao kazi cha watumishi wa Afya kilichofanyika katika hospitali ya Muhimbili....

Kikao kazi cha watumishi wa Afya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
08/12/2025

Kikao kazi cha watumishi wa Afya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili

05/12/2025
Baadhi ya watumishi kutoka Bugando wamefika Taasisi ya Saratani Ocean road lengo likiwa ni kupata elimu kuhusu namna bor...
03/12/2025

Baadhi ya watumishi kutoka Bugando wamefika Taasisi ya Saratani Ocean road lengo likiwa ni kupata elimu kuhusu namna bora ya utoaji waa matibabu ya saratani kwa kuanza na uchunguzi mpaka matibabu yenyewe, piaa wamejifunza namna viongozi wanavyowaongoza watumishi, njia gaani bora za kuwafanya watumishi wawe na Amani kufanya kazi lakini kikubwaa zaidi ni namna mifumo ya manunuzi inavyotumika kukamilisha jambo hili bila kuwa na matatizo.

Watumishi hao kutoka bugaando wameshukuru kupata elimu hiyo na wameahidi kuitumia vyema katika Taasisi yao ili kuifanya iwe inatoa hudum katika mazingira bora ya kiutumishi.

Leo mapema watumishi wa Taasisi ya saratani Ocean Road wameanza kupata mafunzo ya huduma kwa mteja kutoka kwa wakufunzi ...
02/12/2025

Leo mapema watumishi wa Taasisi ya saratani Ocean Road wameanza kupata mafunzo ya huduma kwa mteja kutoka kwa wakufunzi wa "Resourcehub".

Mafunzo hayo yamefunguliwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Tiba na Uhakiki wa ubora wa huduma wa Taasisi ya saratani ocean road Dkt. Sadiki Siu kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya saratani ocean Dkt. Diwani Msemo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika majengo ya Taasisi hiyo.

Dkt. Siu amewataka watumishi wa Taasisi hiyo wanaoshiriki mafunzo hayo, wazingatie kila kinachofundishwa ili nao wawafundishe wengine ambao hawakubahatika kufika katika mafunzo.

Vilevile Dkt. Siu, amewataka watumishi hao kuhakikisha mbinu na maarifa mbalimbali watakazopata katika mafunzo hayo wazitumie katika kuboresha huduma kwa wateja.

Kwa upande wake Mkufunzi kutoka "Resourcehub" Bw. Erick Chrispin amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa watumishi kwa kuwa yanakumbusha majukumu ya mtumishi kwa mteja na kuongeza matokeo bora.

Mafunzo hayo ya huduma kwa mteja yatafanyika kwa muda wa siku mbili yaani leo tarehe 02/12/2025 mpaka kesho tarehe 03/12/2025.

Leo Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) imetembelewa na Mwenyekiti mpya wa Bodi ya udhamini Prof. Ephata Kaaya aliyete...
01/12/2025

Leo Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) imetembelewa na Mwenyekiti mpya wa Bodi ya udhamini Prof. Ephata Kaaya aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwaajili ya kuja kuangalia maendeleo mbalimbali yaliyofanyika katika Taasisi hiyo.

Ziara hii imekuwa fursa muhimu kwa uongozi wa ORCI kuonesha maendeleo ya usimikaji wa mashine mpya kabisa za COBALT na LINAC pamoja na kukagua majengo yanayoendelea kuboreshwa na uongozi huo.

Prof. Kaaya ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Saratani Ocean road kwa kuwa na kasi kubwa katika kuhakikisha Taasisi hiyo inapiga hatua kubwa kufikia maendeleo wanayoyataka kutoka pale ilipokuwa awali.

Aidha Prof. Kaaya amesema ameshangazwa na kuona hospitali inang'ara pamoja na kuwa na mabadiliko mengi makubwa hasa ukizingatia kuwa katika kipindi ambacho ameondoka mpaka sasa ni muda mfupi huku akiamini kuwa Mambo makubwa k**a hayo yasingeweza kufanyika katika kipindi hicho.

Katika hatua nyingine Prof. Kaaya amesema kuwa anajivunia mno kuwa na kiongozi k**a Dkt. Msemo hivyo, amewataka viongozi wengine wote kuhakikisha wanakwenda na kasi hii ya Dkt. Msemo na kuahidi kuwa bodi itak**ata kasi hiyohiyo na kuondoka na viongozi kuelekea kwenye mafanikio yanayotegemewa kufikiwa na Taasisi hiyo.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Diwani Msemo amesema kuwa amefurahishwa sana na ujio huu kwani umewapa nguvu kubwa ya kuelekea kwenye malengo anayoyataka.

Dkt. Msemo amewasisitizia viongozi wenzake kuongeza kasi ili kufikia malengo ya Taasisi kwani hayo ndio maono ya Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hasan ya kuleta furaha kwa watanzania wote kwa kuhakikisha kuwa wanapata tiba ya saratani kwa wakati.

Dkt. Msemo amemwambia Prof. Kaaya kuwa kuongezeka kwa mashine hizo za mionzi sio tu kuwa zitawezesha wananchi kutibiwa kwa wakati bali zitaifanya Taasisi ya Saratani Ocean Road kuwa kinara wa utalii tiba katika ukanda wa Afrika.

Aidha Dkt. msemo amesema kuwa kwa sasa wanapambana kwaajili ya kupata Ithibati za kimataifa ili kuweza kuhudumia watu wa mataifa mbalimbali hasa wale wanaotokea nje ya Bara la Afrika ambapo amesema kuwa hiyo ndiyo ndoto yake.

29/11/2025
Geita mpo tayari...?
29/11/2025

Geita mpo tayari...?

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram