Dr barna

Dr barna Ushauri juu ya �afya yako na tiba sahihi. �call me 0654 605 471

30/01/2023

Pitia hii

30/01/2023

Usizarahu hii..👇

Mungu akiwa na wewe hakuna kizuiziNaomba mungu akusimamie na kujaalia kila hatua unayopiga iwe ya mafanikio kwako na jam...
08/11/2022

Mungu akiwa na wewe hakuna kizuizi

Naomba mungu akusimamie na kujaalia kila hatua unayopiga iwe ya mafanikio kwako na jamii kwa ujumla

Nawatakia jioni njema

K**a unasumbukiwa na UTI sugu na umeshakata tamaa usijali nimekuandalia products safi ambayo ni kiboko kabisa ya UTI yan...
27/09/2022

K**a unasumbukiwa na UTI sugu na umeshakata tamaa usijali nimekuandalia products safi ambayo ni kiboko kabisa ya UTI yani sio huponesha bali hii huondosha na kumaliza kabisa UTI . Wasiliana nami kwa simu namba 0654 605 471 ili upate tiba sahihi

Je maambukizi ya njia ya mkojo ni ugonjwa wa zinaa?Maradhi ya njia ya mkojo (Urinary track Infections-UTIs), ni maambuki...
27/09/2022

Je maambukizi ya njia ya mkojo ni ugonjwa wa zinaa?

Maradhi ya njia ya mkojo (Urinary track Infections-UTIs), ni maambukizi ambayo baadhi ya watu wamekuwa wakiyafananisha na maradhi ya zinaa. Hii ni kutokana na kwamba maambukizi haya hushambulia na kuathiri sehemu zinazokaribiana na za siri au hata sehemu zenyewe za siri za mwanadamu. Lakini je, ukweli ni upi kuhusu maradhi haya na wataalamu wanasemaje?

BBC Idhaa ya Kiswahili imezungumza na muathiriwa wa UTI pamoja na daktari bingwa wa magonjwa ya uzaji pamoja na UTI.

Zainab Nkumbo Kayenga (sio jina lake halisi), ni mama wa watoto watatu mwenye umri wa miaka 32, ambaye alipitia changamoto kubwa wakati alipopata maambukizi ya UTI kwa mara ya kwanza.

''Nilipopata UTI kwa mara ya kwanza nilihisi maumivu makali upande wa chini wa tumbo, na nilipokuwa nikienda haja ndogo nihisi uchungu sana...nilidhani ni maumivu ya tumbo tu ya kawaida, nikahisi ni hali tu ya ujauzito, kwasababu ndio kwanza nilikuwa nimepata ujauzito. Lakini maumivu hayakuisha na baada ya siku chache nilianza kukojoa mkojo wenye damu, nikaanza kutoa harufu sehemu za siri, ikabidi niende hospitalini na kupewa dawa...ndipo nilipoambiwa nilikua ninaumwa UTI'''

Bi Zainab anasema katika kipindi hiki mumewe alimshuku kuwa alimletea ugonjwa wa zinaa:

''Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwani mume wangu alidhani nina ugonjwa wa zinaa na kuamua kunitenga na kunikasirikia na hata kutishia kuwa angeniacha. Hata hivyo daktari alimueleza kuwa alichokua akikidhania sicho'' Zainab aliiambia BBC kwa njia ya simu.

Wataalamu wanasemaje?
Dkt. Iganatius Kibe, daktari bingwa wa magonjwa ya uzazi nchini Kenya, anasema UTI ni ugonjwa ambao huwapata wanawake wengi na mara nyingi wanawake wajawazito wamekuwa wakiupata kutokana na mabadiliko ya homoni za mwili wakati mama anapopata ujauzito.

Hata hivyo anasema maambukizi haya ya njia ya mkojo yameongezeka zaidi nyakati hizi kwasababu wanawake wengi wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za kusafisha sehemu zao za siri:

''Mara nyingi wanawake wanafikiria wanaume ndio wanawaletea ugonjwa huu wa UTI, kwasababu wanatumia vitu mbalimbali kusafisha sehemu zao za siri k**a vile kemikali, avokado, maziwa ya mgando, yote haya yanaharibu tindikali asilia ambayo inasafisha sehemu ile ya siri ya mwanamke...matokeo yake tindikali hii tunaiita PH kwa lugha ya kitaalamu ikiisha pale unapata mwanamke anaanza anapata maambukizi ya kudumu ya UTI, kujikuna na kutoa maji maji ya harufu mbaya'' anasema Dkt. Iganatius Kibe

Dkt Kibe anasema maambukizi ya njia ya mkojo- UTIs, yamekuwa yakiibua mgogoro baina ya wenza au wanandoa huku wakilaumiana kila mmoja kumletea mwenzake ugonjwa wa zinaa.

''Tatizo hili nalishuhudia kila mara, hasa maambukizi haya ya UTI yanapogeuka na kuwa ugonjwa wa zinaa. Unapata UTI ilianza k**a maambukizi ya kawaida yanayosababisha kuungua kwa kibofu cha mkojo na mirija ya mikojo, lakini baadaye hali hii inahamia katika sehemu za siri za mwanamke na kuziunguza hadi kwenye shingo ya uzazi na kusambaa hadi shemu nyingine na eneo zima la nyonga tunaita -Pelvic Inflammatory Disease . Inapofikia hapo mwanamke anaweza kumuambukiza mwanaume bakteria wale na hapo ndio unageuka kuwa ugonjwaa wa zinaa'' anasema Dkt Kibe.

Daktari anawashauri wanaume wenye wenzi waliopatwa na maambukizi ya UTI kuambatana na wake zao na kufanyiwa vipimo vya maabara kubaini iwapo wameambukizwa bakteria aina ya E.colli na aina nyingine za bacteria na hata virusi ili wawe na uhakika na afya zao.

UTI ni nini hasa?

Kulingana na madaktari bingwa wa magonjwa ya uzazi pamoja na, maambukizi ya njia ya mkojo husababishwa na vimelea au bakteria hatari ambao huzidi uwezo wa kinga ya mwili katika mfumo wa mkojo. Maambukizi haya yanaweza kuathiri mafigo, kibofu cha mkojo na mirija inayopita katikakati ya viungo hivyo.

Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa UTI ni mojawapo ya aina za maambikizi yanayowakumba watu wengi zaidi duniani na watu takriban milioni 8.1 hutembelea hospitali au kliniki kila mwaka kuwaona madaktari kutokana na maradhi haya.

Maambukizi ya mkojo yanaweza kugawanywa katika aina mbili ya njia ya juu ya mkojo na ya njia ya chini. Njia ya juu inajumuisha figo na mrija unaopeleka mkojo katika kibofu cha mkojo (ureter), na njia ya chini ya mkojo yenye kibofu cha mkojo na mrija unaoelekea sehemu ya nyonga.

Kwa wengi maambukizi ya njia ya mkojo husababishwa na bakteria aina E. coli , ambayo kwa kawaida hupatikana katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.

Dalili za UTI

Dalili za maambulizi ya UTI zinategemea una umri gani, jinsia na ni sehemu gani imeathiriwa ya njia ya mkojo.

Dkt kibe anashauri ni vyema kwa mtu kufanyiwa vipimo vya maabara vya mkojo na damu kabla ya kupewa dawa za kutibu UTIs ili kubaini ni aina gani ya bakteria wanaosababisha maambukizi uliyonayo.

Dalili za kawaida za UTI ni pamoja na:
Haja ya kwenda haja ndogo kila mara
Kupanda kwa joto la mwili
Kuhisi baridi mwilini
Maumivu ya mgongo
Mkojo mzito wenye harufu kali na damu
Maumivu au muwasho unapokwenda haja ndogo
Kichefuchefu na kutapika
Maumivu ya misuli na tumbo

Hatari zake

Zaidi ya asilimia 50 ya wanawake wote hupata walau wakati mmoja maambukizi ya UTI maishani mwao, huku asilimia 20 na 30 wakipata maambukizi ya mkojo yanayojirudia, zinasema tafiti mbalimbali.

Wanawake wajawazito wanakabiliwa na uwezekano mkubwa wa kupata maambukizi ya UTI kuliko wanawake wengine, lakini maambukizi hayo yanapotokea yana uwezekano mkubwa wa kusambaa hadi katika mafigo, Hii ni kwasababu ya mabadiliko mwilini wakati waujauzito yanayoathiri njia ya mkojo.

Maambukizi ya UTI miongoni mwa wanawake wajawazito yanaweza kusababisha hatari ya afya za wakinamama wajawazito na watoto na hivyo DKT anasharu kuwa wanawake wajawazito wanapaswa kufanyiwa vipimo kubaini uwepo wa bakteria katika mkojo wao, hata k**a hawana dlili na kutibiwa kwa dawa za abitiotics kuzuia usambaaji wa bakteria hao.

Ni nani anayeweza kupata UTI?

Watu wa rika zote na jinsia zote wanaweza kupata maambukizi haya ya njia ya mkojo. Hatahivyo, baadhi ya watu wana hatari ya kupata. Mambo yafuatayo yanaweza kuongeza uwezekano wa kusababisha UTI:

tendo la kujamiiana hususan linapofanyika mara kwa mara na linapojfanywa na wenza zaidi ya mmoja au wapya
kisukari
uchafu wa mwili
kutomaliza mkojo kabisa katika kibofu unapokojoa
utopata kinyesi
kuziba kwa mirija ya mikojo
mawe kwenye figo
matumizi ya baadhi ya tembe za kuzuia mimba
wanawake waliopitisha umri wa kujifungua
watu waliofanyiwa upasuaji wa njia ya mkojo
kinga dhaifu ya mwili
kutotembea kwa muda mrefu
Matumizi ya muda mrefu ya dawa za antibiotics, ambazo zinaweza kuvuruga bakteria asilia wazuri wa mfumo wa haja kubwa na njia ya mkojo.
Athari zake
Mambukizi mengi ya njia ya mkojo huwa sio makali, lakini baadhi yanaweza kusababisha matatizo makubwa, hususan yanaposhambulia sehemu ya juu ya njia ya mkojo.

Ugonjwa wa muda mrefu wa figo au unaorejea rejea unaweza kusababisha uharibifu wa kudumu, na baadhi ya maambukizi ya ghafla ya figo yanaweza kutishia maisha, hususan ni k**a bakteria wataingia kwenye mfumo wa damu hali inayofahamika k**a epticaemia kwa lugha ya kitaalamu.

Pia huongeza hatari ya wanawake kujifungua vijusi au wenye uzito wa chini wanapozaliwa.

Je unaweza kuzuia?
Kuna hatua mbalimbali ambazo zikichukuliwa zinaweza kupunguza hatari ya kupata maambukizi ya UTI. Kulingana na Dkt Ignatius Kibe njia kuu ya kuzuia maambukizi ya njia ya mkojo ni pamoja na kuacha kutumia vipodozi, mafuta, losheni, manukato, kemikali na vitu vingine kusafisha sehemu za siri.

''Sisi madaktari hatutaki mwanamke aweke tindikali sehemu zake za siri, tindikali ya mwili asilia iliyopo kwenye njia za mkojo na uke inatosha...wanawake waache kabisa'', alisisitiza Dkt Kibe na kuongeza kuwa: ''Hiyo sehemu iachwe tusije tukaiharibu kwa kuoshwa na makemikali hatutaki kamwe!. Dawa zinazonunuliwa na kuweka sehemu za siri ziachwe!'', alisema.

Hatua mbali mbali ambazo zikichukuliwa zinaweza kupunguza hatari ya kupata maambukizi ya UTI:

Kunywa maji mengi na uende haja ndogo mara kwa mara ili kusafisha njia ya mkojo
Epuka vinywaji k**a vile pombe na kahawa ambavyo vinaweza kudhuru kibofu.
Nenda haja ndogo mara baada ya kufanya tendo la ngono.
Jipanguse kuanzia mbele kwenda nyuma baada ya kwenda haja ndogo na kubwa.
Hakikisha sehemu zako za siri ni safi kila wakati.
Kuoga kwa maji yanayotiririka( showers) ni bora zaidi na epuka kutumia mafuta.
Pedi (s**o) zinazotumiwa nje ni bora zaidi kuliko zile zinazoingizwa ndani
Epuka kutumia bidhaa za manukato katika sehemu ya siri.
Vaa nguo ya ndani(chupi) iliyotengenezwa kwa pamba na nguo ambazo hazikubani ili kuhakikisha sehemu zako za siri zinakua karibu.
Watu wanashauriwa kuwasiliana na madaktari iwapo watahisi kuwa na dalili za UTI, hususan k**a wana uwezekano wa kupata maambukizi ya figo.

Maambukizi ya UTI kwa wanaume

UTI ni maambukizi ya nadra kwa wanaume. Wanaume wenye chini ya umri wa miaka 50 wanaopata maambukizi haya ni kati ya 5 na 8 katika kila wanaume 10,000 zinasema tafiti. Hatari ya maambukizi haya huongezeka kutokana na umri.

Wanaume wanapopata maambukizi ya njia ya mkojo huathirika maeneo sawa na ya wanawake.

Kwa wanaume, hatahivyo, saratani ya korodani pia husababisha hatari ya maambukizi ya UTI.

Mwanaume aliyetahiriwa ana uwezekano mdogo zaidi wa kupata maambukizi ya njia ya mkojo kuliko mwanaume ambaye hajatahiriwa.

Mchakato wa matibabu utakuwa sawa na ule unaopitiwa wanawake wenye maambukizi ya mkojo

Kwa ushauri na tiba wasiliana nami nikusaidie kwa namba 0654 605 471

JUA UGONJWA WA KISUKARI,CHAZO CHAKE,DALILI NA TIBA YAKEKISUKARI NI NINI HASWA?Sukari mwilini hutokana na vyakula pamoja ...
27/09/2022

JUA UGONJWA WA KISUKARI,CHAZO CHAKE,DALILI NA TIBA YAKE

KISUKARI NI NINI HASWA?

Sukari mwilini hutokana na vyakula pamoja na vinywaji tunavyotumia kila siku na hutumika kuupa mwili nguvu. Glukosi ni aina ya sukari ambayo huzipa chembe za mwili nishati. Hata hivyo ili glukosi iingie ndani ya chembe hizo inahitaji insulini. Insulini ni kemikali (Homoni) ambayo hutokezwa na kongosho (Pancrease).

Kisukari ni ugonjwa unaotokana na mtu kuwa na sukari nyingi kupita kiasi kwenye damu. Ugonjwa huo huvuruga utaratibu wa kuingiza sukari ndani ya chembe kutoka kwenye damu kwa kuwa chembe huhitaji sukari ili kupata nishati.

Ugonjwa wa Kisukari hutokea pale ambapo tezi ya kongosho inaposhindwa kutengeneza kichocheo (Homoni) aina ya insulin au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho na kusababisha kuongezeka kwa sukari (Hyperglycemia) au kushuka kwa kiwango cha sukari (Hypoglycemia). Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababishwa na kuwa na kiwango kidogo cha insulin mwilini, mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili.

TAKWIMU MBALIMBALI ZA UGONJWA WA KISUKARI

Kulingana na ripoti mbalimbali karibu watu milioni 316 ulimwenguni pote wana kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu, ingawa wengi wao hawajui wana kiwango hicho. Kwa mfano, nchini Marekani pekee asilimia 90 ya watu wenye sukari nyingi kwenye damu hawatambui k**a wana tatizo hilo. Ingawa asilimia 8.3 ya watu watu wa Marekani wana Kisukari ambayo ni sawa na watu milioni 25.8 na kufanya Kisukari cha 7 kusababisha vifo vya watu Marekani.

Mamilioni ya watu wana ugonjwa huo lakini hawana habari! Ni ngumu zaidi kutibu ugonjwa wa kisukari kwa kuwa mtu anaweza kuishi nao kwa muda mrefu kabla haujagunduliwa. Hiyo ndiyo sababu watu husema kwamba ugonjwa huo huua kimyakimya.

NINI CHANZO HASA CHA KISUKARI?

Ili kuelewa vyema ugonjwa wa kisukari ni muhimu kwanza kuelewa namna chakula kinavyovunjwa vunjwa na kutumiwa na mwili ili kuzalisha nguvu. Wakati chakula kinapoyeyushwa matukio kadhaa hutokea. Moja ni sukari inayoitwa glucosi ambayo ni chanzo cha nishati/nguvu mwilini huingia katika damu. Tukio la pili ni kiungo kinachoitwa kongosho (Pancrease) kutengeneza kichocheo cha insulini. Kazi ya insulini ni kuondoa glucosi katika damu na kuingiza katika misuli, seli za mafuta na ini, ambako hutumika k**a nishati.

Watu wenye kisukari huwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kuliko inavyotakiwa kwa sababu miili yao haiwezi kupeleka sukari kwenye seli za mafuta, ini na misuli ili ihifadhiwe kwa ajili ya kuzalisha nguvu. Hii ni kutokana na moja ya sababu zifuatazo, huenda kongosho zao haziwezi kutengeneza insulini ya kutosha au seli za mwili wao haziathiriwi na insini k**a inavyotakiwa au sababu zote hizo mbili.

Main Symptoms of Diabetes FikraPevu.com
K**a wewe ni mnene kupita kiasi, hufanyi mazoezi kwa ukawaida au una watu wa ukoo walio na kisukari, huenda tayari una kiwango cha juu cha sukari kwenye damu. Ongezeko la sukari kwenye damu mbali na kuwa kisababishi cha kisukari, hali hiyo inahusianishwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa akili uitwao 'DEMENTIA'.

Kula sukari nyingi sio sababu ya ugonjwa wa kisukari. Lakini lazima tuseme kwamba kula sukari nyingi si nzuri kwa afya yako kwani utaongeza uzito wa kuweza kuathiri uwezo wa mwili wako kujikinga na maradhi tofauti. Ugonjwa wa kisukari umeitwa kwa kufaa "ugonjwa unaoathiri kiini cha nishati ya mwili". Mwili unaposhindwa kutumia glukosi, mifumo mbalimbali ya mwili inaweza kuacha kufanya kazi au hata kusababisha kifo.

Ugonjwa wa Kisukari kitaalamu hujulikana k**a 'DIABETES MELLITUS'. Jina 'Diabetes Mellitus' linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha 'kunyonya' na neno la Kilatini linalomaanisha 'tamu k**a asali'. Maneno hayo yanafafanua vizuri sana ugonjwa huo, kwani maji hupita mwilini mwa mtu aliye na ugonjwa wa kisukari kana kwamba yananyonywa na mdomo na kupitia kwenye njia ya mkojo kisha kutoka nje ya mwili. Isitoshe mkojo huwa na ladha tamu kwa kuwa una sukari. Ndiyo sababu kabla ya kuvumbua njia bora za kupima ugonjwa huo, mbinu moja ya kutambua k**a mtu ana ugonjwa wa kisukari ilikuwa kumwaga mkojo wa mgonjwa karibu na kichuguu cha sisimizi. Ikiwa sisimizi wangevutiwa na mkojo huo basi hilo lilimaanisha kwamba mkojo una sukari

NI NANI ANAWEZA KUWA NA UGONJWA WA KISUKARI?

Watu walio katika makundi yafuatayo wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kisukari:-

– Wenye uzito uliozidi,

– Wenye historia ya kuwa na wagonjwa wa kisukari katika familia zao,

– Wanawake waliozaa watoto wenye kilo 4 au zaidi,

– Watu wasiojishughirisha au wasiofanya mazoezi,

– Wenye shinikizo la damu,

– Wenye msongo wa mawazo na

– Wenye matumizi makubwa ya pombe na sigara.

Watu hawa wanashauriwa kupima sukari yao kila mwaka wakiwa na umri wa miaka 45 na kuendelea.

Kuna hatari kubwa ya kuugua ugonjwa huo ikiwa mtu ana mafuta mengi katika tumbo na kiuno chake kuliko katika mapaja yake. Mafuta katika kongosho na ini huvuruga uwezo wa mwili wa kudhibiti kiasi cha sukari kwenye damu.

Wavutaji wa sigara wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi kwani zoea hilo hudhuru moyo na mfumo wa mzunguko wa damu na kubana mishipa ya damu. Kitabu kimoja kinasema kwamba asilimia 95 ya watu wanaougua kisukari ambao hulazimika kukatwa viungo ni wavutaji wa sigara.

DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI

~ Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati.
~ Kwenda haja ndogo mara kwa mara. Watoto kukojoa kitandani.
~ Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.
~ Kupungua uzito au kukonda licha ya kula vizuri.
~ Kusikia njaa kila wakati na kula sana.
~ Wanawake kuwashwa ukeni.
~ Kutoona vizuri.
~ Kupungua nguvu za kiume au hamu ya kujamiiana kwa wanawake.
~ Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole.
~ Miguu kuoza na hata kupata gangrini.
~ Kukaukwa na ngozi na pia kupata aina ya ngazi katika miguu.
~ Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka.
~ Majipu mwilini.

Wenye dalili hizi wanashauriwa kupima sukari ili kubaini k**a wana kisukari.

Kwaushauri zaidi na tiba wasiliana nasi kwa namba 0654 605 471

Je una tatizo la ugumba? Fahamu sababu tano na tiba yake kwa wanaumeWanaume wengi hunyamaza wakati wanapoanza kuathiriwa...
27/09/2022

Je una tatizo la ugumba? Fahamu sababu tano na tiba yake kwa wanaume

Wanaume wengi hunyamaza wakati wanapoanza kuathiriwa na tatizo la kushindwa kutekeleza wajibu wao katika ndoa ikiwemo tatizo la kushindwa kushiriki tendo la ndoa.

Hivyobasi mara nyingi hulazimika kujiondolea lawama hiyo na badala yake kusema kwamba kizazi cha wake zao ndicho chenye tatizo.

Utafiti umeonesha kwamba wanaume wenye kati ya umri wa miaka 18 hadi 35 ni asilimia 15 ya idadi ya watu.

Kwanini baadhi ya vifo hutokea ghafla wakati wa tendo la ndoa?
‘Walitulazimisha tufanye mapenzi hadi mara 15 kwa siku’
Vilevile wanaume wenye zaidi ya umri wa miaka 40 ni asilimia 40 ya wale wasioweza kuwatosheleza wake zao kindoa kutokana na tatizo linaloathiri sehemu zao za siri. (uume kushindwa).

Hali hiyo humfanya mwanaume kuhisi kukejeliwa na jamii ambayo hubeza hali hiyo.

Mwanaume au mwanamke aliye katika hali hiyo pia anaweza kukejeliwa au kupokea shutuma chungu nzima kutoka kwa jamii iwapo siri yake itajulikana nyumbani ama mahala popote pale.

Kutokana na hilo wanaume ambao hujipata katika hali hiyo ya kiafya hupendelea sana kutoshiriki katika mjadala kuhusu suala hilo kwasababu hujihisi kukatishwa tamaa.
Upungufu wa nguvu za kiume na athari za matumizi ya mitishamba isiyoidhinishwa kisayansi

Kunapotokea hali k**a hiyo , magonjwa mengine pia huanza kumwathiri mwanaume k**a huyo na mara nyingi huogopa kushiriki na wake zao katika tendo la ndoa.

Na iwapo mwanaume anashindwa kutekeleza wajibu wake nyumbani, humfanya mke wake kuanza kumshuku na hivyobasi kusababisha kuzuka kwa ugomvi wa mara kwa mara bila sababu.
Je ina maana gani mwanamume kushindwa kushiriki tendo la ndoa na mke wake?
Hali ya maumbile nyeti kushindwa kuwa tayari, kwa kitaalamu Erectile dysfunction (ED) ni wakati ambapo mwanamume hawezi kushiriki katika tendo la ndoa kwa dakika 15 mfululizo.

Utafiti umeonesha kwamba iwapo mwanaume ana uwezo wa kushiriki katika tendo la ndoa, sehemu yake ya siri huonesha mihemko nyakati za alfajiri anapoamka.

Lakini daktari Abass anasema kwamba iwapo sehemu ya siri ya mwanaume haina mihemko, au iwapo hawezi kushiriki katika tendo la ndoa basi huenda yeye ana tatizo la ugumba.

Kuna sababu kadhaa kwanini hali hii huwakumba waathiriwa.
1.Ukosefu wa homoni za kiume za kutosha mwilini:
Testosterone ni homoni za kiume zinazowafanya wanaume kuhisi kuwa wanaume huku estrogen zikiwa homoni za k**e ambazo humsaidia mwanamke kupata ujauzito .

K**a wanaume, viwango vya homoni za oestrogen katika mwili wa mwanamke hupungua wakati mwanamke anapofikisha umri wa miaka 50.
Wanaume wengi hunyamaza wakati wanapoanza kuathiriwa na tatizo la kushindwa kutekeleza wajibu wao katika ndoa ikiwemo tatizo la kushiriki katika tendo la ndoa.

Kwa upande wa wanaume viwango vya homoni za kiume havipungui , lakini hukabiliwa na changamoto ambazo mara nyingi hupuuzwa.

2.Msongo wa mawazo:
Shinikizo la kiakili ni miongoni mwa sababu kuu zinazosababisha ugumba miongoni kwa wanaume. Msongo wa mawazo unaweza kutokea iwapo mwanaume hana kazi, iwapo mwanaume hana fedha ama iwapo kuna changamoto katika ndoa yake ama kutoka kokote kule.

Dalili hizi ni tofauti na zile za kufanya mazoezi , kwasababu mazoezi husaidia moyo kusukuma damu vyema katika misuli muhimu. Sonona husababishwa na mgando wa damu kila mahali mwilini.

3.Kushiriki mazoezi mbali na tendo la ndoa mara kwa mara:
Hili ni suala linalohitaji msisitizo ili kuzuia ugumba. Mtu anapaswa kujifunza kufanya mazoezi kwa muda mfupi kila siku.

''Je Unajua mazoezi ambayo huwashauri wagonjwa wangu kufanya? Ni kushiriki katika tendo la ndoa mara kwa mara.

Na kuna utafiti unaothibitisha hili, ambao naweza kusema kwamba ni ushahidi ulio sawa'', alisema Dkt Abbas.

4.Unyanyasaji wa kingono:

Dkt. Abass anawashauri wanaume kushiriki katika tendo la ndoa mara 21 kwa mwezi . Inadaiwa kwamba kushiriki katika tendo la ndoa mara kwa mara kunasaidia kuzuia saratani ya tezi dume.

5.Ukosefu wa maji safi

Suala hili linaonekana k**a la kushangaza kwa watu wengi, kulingana na Dkt Abbas.

Hatahivyo , anaelezea kwamba ukosefu wa maji safi , ambayo hayana virutubisho , huathiri afya ya uzazi ya wanaume. Aliongezea kwamba serikali imelazimika kuhakikisha uwepo wa maji safi ya kunywa kwa kuweka dawa k**a vile Fluoride, Calcium na Selenite.

Inahakikisha kwamba maji yana virutubisho vyote ili afya ya wanaume iwe bora.

Pata ushauri wa bute na tiba kwa kutupigia simu namba 0654 605 471 or WhatsApp 0654 605 471

TAFAKALI.. ? 🤔
15/09/2022

TAFAKALI.. ? 🤔

Address

Mbagala
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 21:00 - 15:00
Tuesday 09:00 - 15:00
Wednesday 09:00 - 15:00
Thursday 09:00 - 15:00
Friday 09:00 - 12:00

Telephone

+255654605471

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr barna posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr barna:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category