11/03/2022
DALILI HATARI ZA KISUKARI NA TIBA YAKE.
•Kukojoa mara kwa mara:
Jee, umekuwa na tabia ya kwenda kupata haja ndogo mara kwa mara? K**a jibu ni ndiyo, basi figo zako sasa haziwezi kuirudisha glucose kwenye mfumo wa damu na badala yake zinachukua maji kutoka kwenye damu na kusababisha kibofu kijae mara kwa mara.
•Kiu Isiyoisha:
K**a unakojoa mara kwa mara, utapata kiu isoisha kwa sababu mwili unahitaji kurudisha maji uliyopoteza kwenye mkojo.
• Njaa Kali:
K**a isulin yako haifanyi kazi au k**a huna insulin, mwili wako unakosa glucose ya kuupa nguvu. Katika kutafuta njia nyingine ya kupata nguvu, mwili utakuwa na njaa ili uupatie chakula.
• Kupungua uzito kusiko kawaida:
Hili huwatokea zaidi wagonjwa wa Type 1 Diabetes kwa sababu kwa kukosa insulin na seli kukosa chanzo cha kupata nguvu, mwili huanza kuvunjavunja misuli na kuyeyusha mafuta ya mwili ili upate nguvu hiyo hali inayochangiwa zaidi na tabia ya kisukari cha aina hiyo kujitokeza kwa ghafla.
• Uchovu wa mwili:
Mwili unapokosa glucose ya kuzipa seli nguvu, uchovu hutokea.
• Hasira:
Hasira zinaweza kuwa ni sababu ya mwili kukosa nguvu.
• Kutoona vizuri:
Ugonjwa huu husababisha mtu kushindwa kuviona vitu vizuri. Tatizo hili hutibika lakini mara nyingine hali huweza kuwa mbaya kiasi cha kuwa na tatizo la kudumu au kupata upofu.
• Vidonda kutopona vizuri au haraka:
Unapokuwa na sukari nyingi katika damu, uwezo wa mwili kuponya vidonda hupungua.
• Magonjwa ya ngozi:
Mwili wenye sukari nyingi ndani ya damu huwa na uwezo mdogo sana wa kujiponya kutokana na maambukizi ya wadudu. Wanawake wenye kisukari huwa na maambukizi zaidi na hupata shida kubwa ya kuponya maambukizi ya sehemu nyeti za miili yao.
• Kuwashwa kwa ngozi:
Kuwashwa kwa ngozi mara nyingine ni dalili ya kuwa na kisukari.
• Kuwa na fizi nyekundu au zilizovimba:
Fizi nyekundu na/au zilizovimba huweza kuwa kuwa ni dalili ya kuwa na ugonjwa wa kisukari, mara nyingine meno hulegea.
• Uwezo mdogo wa kushiriki tendo la ndoa:
Hili ni tatizo hasa la wanaume wenye umri unaozidi miaka 50, ambapo mara nyingi watakosa uwezo wa kushiriki tendo
K**a una dalili hizi (Piga 0764777110) tukuhudumie maana madhara yake ni makubwa mno.