01/02/2026
Umri mzuri wa kubeba mimba na kuzaa ni miaka ya 20s. Hapo ndipo mwanamke anakuwa na mayai ya kutosha na chansi ya kushika mimba ni kubwa sana
Iwapo Mwanamke Hana shida katika Mfumo Wake Wa Uzazi,
Kadri umri wa mwanamke unavyosogea, Mayai ya Uzazi huwa yanapungua idadi na Ubora kwa Kasi zaidi
ππ½ Hii inatokea kwa sababu ya utaratibu uliopo wa mayai kupungua na kuzeeka (Oocyte aging) ambao hupelekea kupungua kwa ubora na wingi wa mayai.
Mwanamke mwenye umri mkubwa anaweza akaendelea kupevusha mayai ila akashindwa kupata mimba kutokana na uchovu wa mayai na mayai kukosa ubora π€
Pia upungufu wa baadhi ya homoni muhimu zinazochochea upatikanaji wa Ujauzito
Hivyo Nafasi ya kubeba ujauzito inapunguaa.
Mwanamke huchukua muda mrefu kushika ujauzito!
Pia uwezekano mkubwa wa Mimba kuharibika ni Mkubwa!
Unaweza kupata zaidi changamoto za wakati wa ujauzito, sukari wakati wa ujauzito, shinikizo la damu la juu, na mimba kuharibika
:
NB : Hayo yote pia yatachangiwa na hali binafsi ya kiafya . Sio wote wanaopitia hizo changamoto ila risk ni kubwa zaidi kwa wale ambao wapo over 35.
USHAURI WANGU
K**a huna matatizo ya uzazi ni vyema ukaanza kuzaa mapema!! Walau ukifika miaka 35 uwe umeshazaa hata mara moja!!
Kwako ambaye Bado hujazaa na una matatizo ya uzazi, basi usikate tamaa endelea kutafuta chanzo za tatizo na kujipambania
Mungu ni Wetu Sote, Fanya Sehemu yako, iliyobaki Weka Duah Na Maombi kulingana na Imani yako ππ½π
Ukihitaji msaada wetu tupo tayari kukuhudumia, Wasap +255(0789699225), Dr Sam Makata