Dr Sam Makata

Dr Sam Makata Tunasaidia wanawake na wanaume kurejesha afya ya uzazi kwa tiba lishe asilia, tukilenga chanzo cha tatizo. Ushauri binafsi WhatsApp +255 789 699 225

Umri mzuri wa kubeba mimba na kuzaa ni miaka ya 20s. Hapo ndipo mwanamke anakuwa na mayai ya kutosha na chansi ya kushik...
01/02/2026

Umri mzuri wa kubeba mimba na kuzaa ni miaka ya 20s. Hapo ndipo mwanamke anakuwa na mayai ya kutosha na chansi ya kushika mimba ni kubwa sana

Iwapo Mwanamke Hana shida katika Mfumo Wake Wa Uzazi,

Kadri umri wa mwanamke unavyosogea, Mayai ya Uzazi huwa yanapungua idadi na Ubora kwa Kasi zaidi

πŸ‘‰πŸ½ Hii inatokea kwa sababu ya utaratibu uliopo wa mayai kupungua na kuzeeka (Oocyte aging) ambao hupelekea kupungua kwa ubora na wingi wa mayai.

Mwanamke mwenye umri mkubwa anaweza akaendelea kupevusha mayai ila akashindwa kupata mimba kutokana na uchovu wa mayai na mayai kukosa ubora πŸ€”

Pia upungufu wa baadhi ya homoni muhimu zinazochochea upatikanaji wa Ujauzito

Hivyo Nafasi ya kubeba ujauzito inapunguaa.

Mwanamke huchukua muda mrefu kushika ujauzito!

Pia uwezekano mkubwa wa Mimba kuharibika ni Mkubwa!

Unaweza kupata zaidi changamoto za wakati wa ujauzito, sukari wakati wa ujauzito, shinikizo la damu la juu, na mimba kuharibika
:

NB : Hayo yote pia yatachangiwa na hali binafsi ya kiafya . Sio wote wanaopitia hizo changamoto ila risk ni kubwa zaidi kwa wale ambao wapo over 35.

USHAURI WANGU
K**a huna matatizo ya uzazi ni vyema ukaanza kuzaa mapema!! Walau ukifika miaka 35 uwe umeshazaa hata mara moja!!

Kwako ambaye Bado hujazaa na una matatizo ya uzazi, basi usikate tamaa endelea kutafuta chanzo za tatizo na kujipambania

Mungu ni Wetu Sote, Fanya Sehemu yako, iliyobaki Weka Duah Na Maombi kulingana na Imani yako πŸ™πŸ½πŸ™Œ

Ukihitaji msaada wetu tupo tayari kukuhudumia, Wasap +255(0789699225), Dr Sam Makata

Unajua kugusanisha ngozi yako na ya mtoto wako kunaweza kusaidia ukuaji wa ubongo wake?Wengi tunajua skin-to-skin contac...
31/01/2026

Unajua kugusanisha ngozi yako na ya mtoto wako kunaweza kusaidia ukuaji wa ubongo wake?

Wengi tunajua skin-to-skin contact husaidia maziwa kutoka vizuri, humtuliza mtoto na humuweka kwenye joto sahihi.

Lakini kuna jambo kubwa zaidi ambalo mama wengi hawajui πŸ™‚

Kisayansi, kugusanisha ngozi ya mzazi na mtoto miezi ya mwanzo ya maisha huchochea ukuaji wa ubongo wa mtoto (brain development).

Mguso huu huamsha mfumo wa neva wa mtoto, hujenga hisia ya usalama, na kusaidia ubongo kujifunza kutambua mazingira mapema.

Watoto wanaopata mguso huu mara kwa mara huonesha:
βœ” utulivu zaidi
βœ” usingizi mzuri
βœ” ukuaji mzuri wa kihisia na akili
βœ” uwezo mzuri wa kujifunza wanapokua

Na faida hii si kwa mama tu β€” hata baba au mlezi anaweza kufanya.

Jinsi ya kufanya skin-to-skin kwa usahihi:
πŸ”Ή Mlaze mtoto kifuani kwako ngozi kwa ngozi kusiwe na nguo Kati ya Ngozi Yako na Mtoto

πŸ”Ή Uso wa mtoto uangalie juu karibu na kifua chako

πŸ”Ή Mfunike nguo au blanketi ili asipoteze joto

πŸ”Ή Fanya angalau dakika 30–60 kila siku

Hili ni muhimu hasa kwa watoto wachanga na waliozaliwa kabla ya muda.

Nakufundisha hivi kwa sababu ukuaji wa mtoto na Uwezo Wake wa Akili hauanzi shuleni β€” unaanza siku za mwanzo kabisa za maisha.

Zingatia hili, kumpa Afya Njema Kwa Mtoto Wako Baadae

Na kwako Dada Yangu unayeteseka na Changamoto za Uzazi na Kushindwa Kupata Ujauzito Kwa muda Mrefu

Nina Ujumbe Wako Hapa
, afya yako ya uzazi nayo ina nafasi kubwa kwenye ubora wa mimba na mtoto utakayempata.

Changamoto k**a homoni kuvurugika, maambukizi ya mara kwa mara, PCOS au fibroids huathiri safari ya uzazi.

Programu ya UzaziRestore (30–90 days) husaidia kurejesha afya ya uzazi kwa njia ya asili ili mwili wako uwe tayari kwa ujauzito salama na mtoto mwenye afya.

πŸ“² Wasap +255(0789699225)
Nieleeze changamoto yako nikushauri kitaalamu.

Uzazi bora huanza na maandalizi sahihi ya mwili wa mama.

UMESHAJARIBU KILA NJIA KUBEBA MIMBA β€” LAKINI BADO HAKUNA MAFANIKIO?Leo naomba nikuambie kitu muhimu sana... πŸ™πŸ½Si kila uj...
31/01/2026

UMESHAJARIBU KILA NJIA KUBEBA MIMBA β€” LAKINI BADO HAKUNA MAFANIKIO?

Leo naomba nikuambie kitu muhimu sana... πŸ™πŸ½

Si kila ujauzito huja kwa bahati,
Mengine huhitaji kuandaliwa na akili, mwili na moyo.

K**a umechoka, umehangaika…
Na bado moyo wako haujakata tamaa kabisa…

Basi huu ni ujumbe wa dhahabu kwa ajili yako. ✨

πŸ‘‡πŸΎ
MPANGO SAHIHI KABLA YA UJAUZITO – HUANZA KABLA YA KUUSHIKA

Katika kazi yangu ya kuwasaidia wanawake, nimegundua kuwa:
Wanawake wengi hufikiria matibabu baada ya kushindwa.
Lakini siri ni hii: kujiandaa mapema = nafasi kubwa ya kupata ujauzito.

πŸ“Œ Hatua Muhimu za Kuchukua Kabla ya Mimba:

1️⃣ Fanya uchunguzi wa kitaalamu mapema.
Daktari atakushauri namna ya kuandaa mwili wako kwa ujauzito.

Hii ni pamoja na virutubisho muhimu k**a Folic Acid.

2️⃣ Badili mfumo wa maisha yako miezi 3-6 kabla.
Ulaji sahihi unaweza kurekebisha homoni na kuongeza mayai yenye afya,

3️⃣ Zingatia uzito wa mwili.
Uzito mkubwa ni chanzo cha mvurugiko wa homoni, presha, kisukari, na matatizo ya mayai.
Kuwa na mwili ulio kwenye usawa huongeza nafasi ya kushika mimba kwa haraka.

4️⃣ Epuka msongo wa mawazo.
Stress hupunguza uzazi, hushusha homoni muhimu na kuchelewesha mimba. Tafuta utulivu wa akili πŸ™πŸ½πŸ§˜πŸ½β€β™€οΈ

πŸ“› Acha tabia hizi sasa:
❌ Pombe
❌ Kafeini nyingi
❌ Junk food k**a chipsi, baga, pizza
❌ Sukari na wanga uliopitiliza

🌿 Sasa Sikiliza kwa Makini Mama…
Siyo kila mtu ana muda wa kusubiri zaidi ya mwaka.
Na siyo kila moyo unaweza kuvumilia miaka ya majaribu.

Kwa sababu hiyo, nimeandaa programu maalumu ya tiba:

UZAZIRESTORE β€” Tiba Asili Kukusaidia Kubeba
Ujauzito Ndani ya Siku 30 Mpaka 90 Pekee,

Kwa Kukusaidia:-
πŸ’  Kutibu changamoto sugu za uzazi
πŸ’  Kurudisha hedhi, kupevusha mayai
πŸ’  Kuandaa kizazi kwa ujauzito wenye afya

Program hii Imekuwa Msaada Kwa maelfu ya wanawake waliokata tamaa β€”
Na sasa wanaitwa MAMA kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi ya maumivu. πŸ‘ΆπŸ½πŸ’–
---

πŸ“£ OFA KWA WANAWAKE 60 TU
Kwa sasa, program ipo kwenye PUNGUZO:
πŸ’Έ TZS 260,000/= tu (kutoka 485,000/=)

Ni nafasi ya mwisho kwa wale waliokuwa wakilia kimoyomoyo kwa muda mrefu.

Sio tena majaribio β€” ni tiba yenye ushuhuda hai.

πŸ‘‰πŸ½ Unahitaji msaada? β€œNATAKA” Kwenye Komment/ DM

Hili pia ni swali ambalo wanawake wengi huniuliza β€” na Siku zote ni vizuri kuuliza kuliko kubaki na hofu πŸ™‚Jibu la moja k...
31/01/2026

Hili pia ni swali ambalo wanawake wengi huniuliza β€” na Siku zote ni vizuri kuuliza kuliko kubaki na hofu πŸ™‚

Jibu la moja kwa moja ni: HAPANA.

Ukishapata ujauzito wa kweli, hedhi husimama. Mwili hauwezi kuwa na mimba na wakati huohuo uendelee na Kupata period.

Sasa hapa ndipo mkanganyiko hutokea πŸ‘‡
Wanawake wengine hutokwa na damu mwanzoni mwa ujauzito na kudhani ni hedhi.

Lakini hiyo SI PERIOD β€” ni bleeding ya ujauzito.

Kisayansi, takribani 10–15% ya wajawazito hupata damu kidogo hasa chini ya wiki 16 za mimba.

Damu hii inaweza kuwa ishara ya mambo yafuatayo:
β€’ Mimba kutishia kutoka (threatened miscarriage)
β€’ Kondo la nyuma kujishikiza (implantation bleeding)
β€’ Mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi (ectopic pregnancy)
β€’ Mimba zabibu (molar pregnancy) au Jina lingine Mimba ya Uongo
β€’ Au sababu nyingine zisizojulikana... N.k

Muhimu ujue:
Kutokwa na damu ukiwa mjamzito SI JAMBO LA KUPUUZWA.

Inaweza kuongeza hatari ya:
β€’ Mimba kuharibika
β€’ Kujifungua kabla ya wakati
β€’ Mtoto kuwa na uzito mdogo
β€’ Mama kupungukiwa damu

Lakini pia nikutie moyo
Wanawake wengi wanaopata damu mwanzoni mwa mimba bado hujifungua salama.

Tofauti iko kwenye kuwahi kuchunguza.

Ukiona damu ukiwa mjamzito:
βœ” Usikae kimya
βœ” Nenda hospitali mapema
βœ” Fanya vipimo kujua chanzo

K**a daktari wa uzazi, nakuambia ukweli huu kwa sababu lengo ni mimba yako iwe salama hadi mwisho.

Na k**a unapitia changamoto za uzazi k**a:
β€’ mimba kuharibika mara kwa mara
β€’ homoni kuvurugika
β€’ PCOS, PID, fibroids
β€’ kushika mimba kwa shida

Hizi mara nyingi zina chanzo kwenye afya ya mfumo wa uzazi.

Programu ya UzaziRestore (30–90 days) husaidia kurejesha afya ya uzazi, kusawazisha homoni na kuandaa mwili kwa ujauzito salama.

πŸ“² Nitumie Ujumbe Wasap+255(0789699225)
Nieleeze changamoto yako, nikushauri hatua sahihi.

Afya ya uzazi ni maandalizi β€” na mwili unaweza kurekebishwa, Na Kuitwa Mama TenaπŸ™

Mama, k**a uliwahi kujifungua kwa operation (C-section), najua hili swali limewahi kupita akilini:β€œJe, naweza kujifungua...
31/01/2026

Mama, k**a uliwahi kujifungua kwa operation (C-section), najua hili swali limewahi kupita akilini:

β€œJe, naweza kujifungua kawaida mimba inayofuata?”

Jibu ni: Inawezekana kwa baadhi ya wanawake β€” lakini si kwa wote.
Hapa tunatumia tathmini za kitabibu zaidi, si majaribio.

Kwanini ulifanyiwa operation mara ya kwanza?
Sababu za kawaida ni: mtoto kuwa mkubwa, njia kutofunguka, mtoto kupata shida wakati wa uchungu, au nyonga kuwa finyu (CPD).

Sasa, ili ujaribu kujifungua kawaida (VBAC – vaginal birth after cesarean), kuna mambo muhimu πŸ‘‡

βœ”οΈ Mshono uwe umepona vizuri
Angalau miaka 2–3 ipite kabla ya mimba nyingine. Mimba ya mapema huongeza hatari ya mshono kuchanika wakati wa uchungu.

βœ”οΈ Sababu ya operation ya kwanza isiwe ya kudumu
K**a ilikuwa mtoto mkubwa tu β€” sawa.
Lakini k**a ni nyonga finyu au contracted pelvis β€” mara nyingi operation hurudiwa.

βœ”οΈ Mimba ya sasa iwe salama
Mtoto ageuke vizuri, ashuke vizuri, na njia ifunguke bila tatizo.

Sasa niseme ukweli ambao wengi wanaogopa kusikia:
Hofu kubwa kwa mama mwenye mshono ni kizazi kuchanika (uterine rupture).

Hiki kikitokea:
β€’ Maisha ya mtoto huwa hatarini
β€’ Mama anaweza kupoteza damu nyingi
β€’ Wakati mwingine kizazi huondolewa kuokoa maisha

Ndiyo maana hatufanyi maamuzi kwa kusikia story za watu.
Kila mwili ni tofauti.

Ushauri wangu kwako:

πŸ”Ή Usilazimishe kujifungua kawaida kwa sababu mtu mwingine aliweza

πŸ”Ή Panga mapema na daktari wako mpango wa kujifungua

πŸ”Ή Epuka dawa za kuongeza uchungu kutoka kwa watu wa mitaani

πŸ”Ή Usipate mimba kabla mtoto hajafikisha miaka 2

K**a daktari wa uzazi, lengo langu ni mama salama na mtoto salama, si kuthibitisha ujasiri.

Na k**a una historia ya:
β€’ C-section
β€’ mimba kuharibika
β€’ PCOS, fibroids, PID
β€’ kushindwa kushika mimba

Mfumo wako wa uzazi unaweza kurekebishwa kwanza kabla ya mimba.

Programu ya UzaziRestore (30–90 days) husaidia kurejesha afya ya uzazi, kusawazisha homoni na kuandaa mwili kwa ujauzito salama.

πŸ“² Nitumie Wasap +255(0789699225)
Nikuongoze kulingana na hali yako binafsi.

Afya ya uzazi ni maandalizi β€” si kubahatisha.

Hili ni swali ninaloulizwa sana Inbox kwangu. Uenda nawe Umewahi kujiuliza Swali hili Pia, Majibu yake yapo hapaWengi hu...
31/01/2026

Hili ni swali ninaloulizwa sana Inbox kwangu. Uenda nawe Umewahi kujiuliza Swali hili Pia, Majibu yake yapo hapa

Wengi huamini unaweza kuhisi mimba imeingia siku ileile ya tendo la ndoa au siku chache baadae.

Ila Kisayansi hilo haliwezekani.

Hebu nieleze kwa lugha rahisi πŸ‘‡

Baada ya tendo la ndoa, mbegu ya mwanaume hukutana na yai la mwanamke ndani ya siku kadhaa.
Hapo hutengeneza kijusi (fertilization).

Lakini bado hapo huwezi kuitwa mjamzito wala huwezi kujua chochote.

Kijusi kinahitaji siku 7–10 kujishikiza kwenye mfuko wa uzazi (implantation).

Ni baada ya kujishikiza ndipo mwili huanza kutoa homoni ya hCG β€” homoni ya ujauzito.

πŸ‘‰ Ndiyo maana kipimo cha mimba kwa mkojo huonyesha majibu sahihi kuanzia siku 14 baada ya kutungwa mimba.

Kabla ya hapo, hata k**a ulijisikia Dalili za Wengi za Ujauzito
K**a vile Kuhisi:
β€’ kichefuchefu
β€’ maumivu ya matiti
β€’ uchovu

Hizi mara nyingi ni dalili za Mabadiliko ya homoni zako kawaida pia, sio ishara ya Moja Kwa Moja ya Wewe Kuwa na ujauzito.

Pia hii ndiyo sababu dawa za dharura za kuzuia mimba (emergency contraception) mfano P2, zinaweza kufanya kazi ndani ya siku 1–4 baada ya tendo la ndoa.

Kadri muda unavyopita, ufanisi hupungua.

Natumaini Umejifunza Kitu Leo,

Pia kwako unayetafuta Ujauzito Kwa muda Mrefu Bila mafanikio
Sasa niseme kitu cha muhimu kwako pia,

K**a umekuwa ukitafuta mimba bila mafanikio, tatizo mara nyingi si β€œBAHATI MBAYA” β€” bali shida Ipo katika Moja Kati ya Haya:

β€’ Ovulation kutokuwa sawa
β€’ homoni kuvurugika
β€’ PCOS, cyst, fibroids
β€’ PID au mirija kuziba
β€’ maambukizi ya uke ya mara kwa mara

Haya yote huathiri Kizazi na uwezo wa kushika mimba.

Ndiyo maana naliunda Tiba ya kutibu Toka Ndani,- kwa kurekebisha chanzo, sio kufunika dalili Tena

Programu ya UZAZIRESTORE (30–90 days) imewasaidia wanawake wengi:
βœ” kurekebisha homoni
βœ” kusafisha mfumo wa uzazi
βœ” kuboresha ovulation
βœ” kuongeza nafasi ya kushika mimba kwa njia ya asili

K**a daktari wako, nakwambia kwa uaminifu:
Mwili wako unaweza kurejea kwenye hali ya kawaida na ukabeba mimba.

Kwa HatuaNdogo

πŸ“² Nitumie Wasap 0789699225
Nieleeze changamoto yako, nikushauri hatua sahihi.

Afya ya uzazi ni safari β€” na unaweza kuianza leo

Asante kwa swali Muhimu sana, na Njoo Hapa tujifunze Pamoja.Swali letu Kuu ni hili Hapa...πŸ‘‡πŸ‘‰ Mimba huanza kusomeka kweny...
30/01/2026

Asante kwa swali Muhimu sana, na Njoo Hapa tujifunze Pamoja.
Swali letu Kuu ni hili Hapa...πŸ‘‡
πŸ‘‰ Mimba huanza kusomeka kwenye UPT baada ya muda gani?

labda nijibu Hapa Kwa ufupi Kitaalamu...

Baada ya yai kurutubishwa, huchukua takribani siku 6–7 kujishikiza kwenye mfuko wa mimba (implantation).

Ndipo mwili huanza kuzalisha homoni inayoitwa hCG (human chorionic gonadotropin) β€” ndiyo homoni inayopimwa na kipimo cha mimba.

πŸ”¬ Kwenye damu:

hCG inaweza kuonekana kuanzia siku ya 10–11 tangu mimba itungwe.

🚽 Kwenye mkojo (UPT):

Huonekana vizuri zaidi kuanzia siku 12–14, au baada ya kuchelewa kwa hedhi.

⚠️ Ukipima mapema sana, UPT inaweza kuonyesha negative ilhali mimba ipo bado ndogo.

βœ… Ushauri wangu wa daktari:

Pima baada ya kuchelewa kwa hedhi siku 3–5 kwa majibu sahihi zaidi.

K**a bado una dalili lakini UPT ni negative, rudia baada ya siku 3 Hadi 5 au fanya kipimo cha damu.
Kwa Majibu Sahihi zaidi

Ikiwa Unahisi Dalili za Ujauzito Kila mara na siyo Mjamzito

hiyo ni Dalili hatarishi, Fanya Kumuona Daktari Kwa Vipimo na Msaada Sahihi

Ikiwa una Swali au Unahitaji Msaada Binafsi, nipo hapa Kukusaidia

Tuma Ujumbe Kupitia Wasap+255(0789699225), Dr Sam Makata

Nimeeleza kwenye slides hivi vyakula sahihi vya kuandaa mwili wako kushika mimba naturally, Ukizingatia Haya Ndani ya Si...
30/01/2026

Nimeeleza kwenye slides hivi vyakula sahihi vya kuandaa mwili wako kushika mimba naturally,

Ukizingatia Haya Ndani ya Siku 30 Mpaka 90 Pekee utapata Mabadiliko Makubwa Sana, na ata kufikia lengo Kuitwa Mama Kija Bila Matumizi ya Dawa Kali

πŸ‘‰ Comment neno β€œUZAZI”

πŸ‘‰ Au nitumie DM β€œLISHE”
Nikupe mwelekeo Binafsi sahihi wa kurejesha uzazi wako kutoka kwenye chanzo chake.

Uzazi si bahati. Ni maandalizi sahihi.
β€” Dr Sam Makata

Nakuombea na wewe mwaka huu uniletee ushuhuda k**a huu,Mungu akuguse tumbo lako, Amen!!Nb: Nguvu ya Uzazirestore Package...
29/01/2026

Nakuombea na wewe mwaka huu uniletee ushuhuda k**a huu,Mungu akuguse tumbo lako, Amen!!

Nb: Nguvu ya Uzazirestore Package inaendelea kufanya kazi, k**a unasumbuliwa na matatizo ya uzazi njoo upate ushauri na msaada!

Kwa Msaada Binafsi, Nitumie Ujumbe Kupitia Wasap+255(0789699225), Dr Sam Makata

Vipimo Muhimu vya PID – Siyo Ultrasound PekeeMama, nataka uelewe hili vizuri:πŸ‘‰ PID ni maambukizi, na maambukizi hayaonek...
29/01/2026

Vipimo Muhimu vya PID – Siyo Ultrasound Pekee

Mama, nataka uelewe hili vizuri:
πŸ‘‰ PID ni maambukizi, na maambukizi hayaonekani kwa macho ya ultrasound mara nyingi.

Ndiyo maana Madaktari bingwa hutumia mchanganyiko wa vipimo, si kipimo kimoja.

πŸ§ͺ 1. Swab Test (Cervical / Vaginal Swab) – NDICHO KIPIMO BORA ZAIDI

Hiki ndicho kipimo muhimu kuliko vyote kwa PID.

Swab hufanya nini?

Huchukua sampuli ya uchafu kutoka shingo ya kizazi

Hutuonyesha aina halisi ya bacteria

Hutambua Chlamydia & Gonorrhea (wasababishi wakuu wa PID)

πŸ‘‰ Kwa nini ni bora?
Kwa sababu hutibu chanzo, si kubahatisha dawa.
Bila swab β†’ antibiotics nyingi β†’ PID inarudia β†’ uzazi unaathirika.

🩸 2. Vipimo vya Damu (FBP / CRP)

Hivi hupima:

K**a kuna maambukizi makali mwilini

Kiwango cha inflammation (uvimbe wa ndani)

πŸ‘‰ Havikuambii wapi PID ilipo,
lakini vinathibitisha kuwa mwili unapambana na infection.

🚽 3. Kipimo cha Mkojo

Husaidia:

Kuondoa UTI au magonjwa yanayofanana na PID

Kuhakikisha hakuna mimba (muhimu sana kabla ya tiba)

πŸ‘‰ Ni cha msaada, siyo cha kuthibitisha PID pekee.

πŸ–₯ 4. Ultrasound ya Nyonga (Support Test)

Ultrasound husaidia kuona:

Majimaji kwenye mirija

Kuvimba kwa ovari

Abscess (maambukizi makubwa)

πŸ‘‰ Lakini ukweli ni huu:
Unaweza kuwa na PID kali na ultrasound ikaonyesha HAUNA P.I.D

Ndiyo maana ultrasound haitoshi peke yake.

Vipimo Bora Zaidi vya PID ni:

βœ” Swab Test (Muhimu sana)
βœ” Pelvic examination ya daktari bingwa
βœ” Vipimo vya damu (kuona uzito wa infection)
βœ” Ultrasound (kuangalia madhara)

πŸ‘‰ Ukifanya ultrasound pekee, unaona matokeo – sio chanzo Cha Tatizo.

Na Utaendelea kuishi Kwa kutibu Matokeo Maisha Yako Yote, Bila kudeal na Yule Adui Mkuu

Hivyo ata Ujauzito kwako itaendelea Kuwa Mtihani, na ata Wakati Mwingine Inaweza kupelekea Ndoa kuvunjika kisa Cha Kukosa Mtoto

Ikiwa upo na Changamoto na Unahitaji Msaada Kwa kina, Nitumie Ujumbe Kupitia Wasap+255(0789699225), Dr Sam Makata

Nitakusaidia kulingana na Changamoto Yako

Je Una Uvimbe pembeni ya Uk'e unauma au unarudia mara kwa mara? Usipuuze!Hili linaweza kuwa Bartholin Cyst β€” tatizo amba...
28/01/2026

Je Una Uvimbe pembeni ya Uk'e unauma au unarudia mara kwa mara? Usipuuze!

Hili linaweza kuwa Bartholin Cyst β€” tatizo ambalo wanawake wengi wanalo bila hata kujua.

Kwenye uk'e kuna tezi ndogo zinaitwa Bartholin glands.
Kazi yake ni kutoa ute wa kulainisha uk'e na v***a, hasa wakati wa tendo la ndoa.

Lakini mirija ya tezi hizi ikiziba πŸ‘‰ ute hukwama πŸ‘‰ uvimbe (cyst) unatokea.

⚠️ Wanawake wengi hawana dalili.
Lakini uvimbe ukipata maambukizi hugeuka jipu (Bartholin Abscess)

πŸ‘‰ maumivu makali, homa, kushindwa kutembea, na maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Kitaalamu, daktari anaweza kutambua tatizo hili kwa kuangalia tu.

Lakini fahamu hili muhimu sanaπŸ‘‡πŸ½
❌ Kupasua na kukamua usaha pekee hakumalizi tatizo β€” ndicho chanzo cha kurudia mara kwa mara.

πŸ“Œ Suluhisho la kudumu huhitaji:

Matibabu sahihi ya kitaalam (mf. Marsupialization au catheter maalumu)

Na kurekebisha chanzo halisi cha maambukizi kwenye mfumo wa uzazi

🌿 Ndiyo maana si kila uvimbe unatibiwa kwa njia ile ile.

πŸ‘‰ Usisubiri uvimbe ukuumize zaidi au uharibu afya yako ya uzazi.

K**a Umejifunza Kitu, Basi Usiache KUSAVE na Kushare post hii kwa mwanamke mwingine apate elimu hii muhimu.

πŸ“² Kwa ushauri binafsi na mpango sahihi wa matibabu
Wasiliana nami Dr Sam Makata kupitia Wasap: +255(0789 699 225)

Uzazi si bahati β€” ni maandalizi sahihi kwa wakati sahihi.

Wanawake wengi wanahangaika Wanachukua muda mrefu bila Kupata Ujauzito/ mtoto…ilhali tatizo kubwa siyo ugonjwa β€” ni kuto...
28/01/2026

Wanawake wengi wanahangaika Wanachukua muda mrefu bila Kupata Ujauzito/ mtoto

…ilhali tatizo kubwa siyo ugonjwa β€” ni kutokujua siku sahihi za kubeba mimba.

Na hili Wataalamu Wa Afya Uwa hutulisemi sana, lakini naliona kila siku kliniki kwangu.

K**a hujui siku zako za Hatari, unaweza ukawa unaonana na mwenza wako β€œkihisia” tu, siyo kibaolojia.

Ndiyo maana wengine wanaanza hata kutumia dawa kali za uzazi bila sababu, kumbe mwili wako uko sawa.

Hebu nikuelekeze kwa lugha nyepesi πŸ‘‡

Mwili wako unajieleza, unahitaji tu kuusikiliza.

πŸ”Ή 1. Ute wa utelezi uke'ni
Ukiona ute mweupe au usio na rangi, unaoteleza k**a yai bichi β€” hiyo ni ishara kubwa ya siku za kubeba mimba.

Sio kila mwanamke anauona wazi, lakini ukitokea, ujue mwili wako uko tayari.

πŸ”Ή 2. Joto la mwili kuongezeka
Siku za ovulation joto la mwili hupanda kidogo (kutoka ~36.9 hadi 37.5Β°C au zaidi). Kipimajoto cha kawaida kinatosha kabisa.

πŸ”Ή 3. Kuongezeka hamu ya tendo la ndoa

Ndiyo, hii ni science ya Mwili wa k**e. Mwili unapokaribia kutoa yai, homoni huongezeka na hamu nayo huongezeka.

Ila uwe makiniβ€”ndiyo maana tunachanganya ishara Zaidi ya Moja Kwa Pamoja, sio ishara moja tu.

πŸ”Ή 4. Kufahamu mzunguko wako wa hedhi (HII NI MUHIMU SANA)
Mzunguko siyo siku za kuona damu pekee.

Mzunguko Wa Hedhi Ni kuanzia siku ya kwanza ya hedhi hadi siku ya kwanza ya hedhi inayofuata.

Ukishajua idadi ya siku zako, unapunguza siku 14 toka Mzunguko unaofutaβ€” hapo ndipo siku ya yai kushuka (ovulation day) Kwa lugha Yetu tunaita SIKU ZA HATARI

πŸ‘‰ Mbegu za mwanaume hukaa mwilini siku 2–3

πŸ‘‰ Yai hukaa masaa 24–36
Ndiyo maana siku za kubeba mimba huwa siku chache tu, siyo mwezi mzima.

Hivyo Dada Yangu,
kaa chini leo.

Andika mizunguko yako ya miezi 3 iliyopita. Hapo ndipo safari ya matumaini inaanza.

Na k**a umekuwa ukipambana na:
β€’ PCOS
β€’ Fibroids / cyst
β€’ PID, mirija ya uzazi kuziba
β€’ Maambukizi ya uke yanayojirudia
β€’ Homoni kuvurugika
β€’ Kutopata ujauzito kwa muda mrefu

πŸ‘‰ Uzazi hauhitaji kubahatisha, unahitaji kurekebishwa mzizi wa tatizo

Ili kufikia Lengo Lako la Kuu, la Kubeba Ujauzito na Kuitwa Mama πŸ™

Address

OFISI IPO, Jengo La Makumbusho Complex Floor Ya Pili, Kijitonyama Makumbusho
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Sam Makata posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr Sam Makata:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category