Swaakid

Swaakid My name is Swabira E. Saidi. Welcome to my page, where inspiring videos meet real talk and motivation. Letโ€™s learn, grow, and win together. ๐Ÿ™

03/10/2025

Nasikia baridi! Pumba-fffff ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ

02/09/2025
02/09/2025
Baada ya miaka minne ya ndoa yetu mume wangu alianza kubadirika, akawa mkali sana, hata nikimtania ananifokea na kuniamb...
16/08/2025

Baada ya miaka minne ya ndoa yetu mume wangu alianza kubadirika, akawa mkali sana, hata nikimtania ananifokea na kuniambia niache utoto, mara kadhaa nilimwandalia chakula lakini alikataa kula na kusema ameshiba, kila siku ilikuwa ni kumwaga chakula, tulishakaa vikao na vikao lakini hakubadirika, nikaanza kupoteza tumaini la ile ndoa na nikatokea kuichukia sana ndoa, kwakuwa mimi ni mkristo na tulifunga ndoa kanisani sio rahisi hata kidogo kuvunja ndoa kwahiyo tuliishi hivyo hivyo, ilifika hatua analala huko huko akirudi asubuhi ananiambia alisinzia kwenye daladala akapitiliza, nikiwa mbishi kukubali utetezi wake ananipiga kipigo cha hatari, kwahiyo ikawa mazoea yake.

Sasa kumbe alikuwa na mchepuko ambao ulikuwa x wake kabla hajanioa mimi, yaani alikuwa na mwanamke wakaachana, akanioa mimi halafu wakarudiana, alikuwa akiwa ndani anakuwa busy sana na simu, muda wote anachat nikimuuliza 'mume wangu unafanya nini kwenye hiyo simu muda wote hutaki hata tuongee'? Ananiambia "Usifatilie mambo ya wanaume wewe kazi yako ni kuosha vyombo na kudeki" fanya ukadeki hata chooni k**a umekosa kazi ya kufanya", nilikuwa naumia sana kwa majibu yake, ni kwa kila swali nililokuwa namuuliza majibu yake sio rafiki, hata tukiwa chumbani ananiambia maneno magumu sana ili nisuse kukutana nae, kwa mfano kuna siku aliniambia "Sogeza hilo tumbua lako hapa nikusaidie maana nyege zisije zikakuua nikasingiziwa mimi ndio nimeua" na hata tukikutana zikizidi sana ni dakika 5 amemaliza kila kitu, nikimwambia mimi bado jibu lake litaniliza hata wiki nzima.

Alikuwa na tabia ya kwenda kwa huyo mchepuko akiamua analala huko akiamua anarudi na akirudi anakuwa busy na mchepuko kwenye simu, kuna siku nikaamua kumsimulia mama mkwe na wifi ninayopitia, wakaniambia "Vumilia ndivyo ndoa zilivyo ila tutaongea nae" sometimes wananiambia "Muombee atabadirika", basi ikawa kila nikiwatafuta wananiambia hivyo hivyo, halafu baadae wanamtafuta wanamwambia yote, mume wangu anakataa halafu anaanza kunisingizia makosa mengine hata nikiyasikia naishia kudondosha machozi tu, ilimradi tu ajisafishe kuwa hana kosa lolote na huwa wanamsikiliza yeye anachoongea, mimi hata niende mikono imekatika niwaoneshe watasema sio kweli. Nikaapa sintorudia kushtakia familia yake tena.

Sasa miezi mitatu iliyopita mume wangu alikuja nyumbani na perfume nzuri sana pamoja na maua, akafika anaiweka mezani, kwa hisia zangu nikajua ameninunulia mimi pengine anataka kunipa zawadi na turejeshe upendo wa zamani ndoa yetu iendelee vizuri, akawa ameingia chumbani akatoka na nguo kadhaa, akapakia kwenye begi nikashangaa maua na ile perfume inawekwa kwenye begi, akaniambia "wewe mwanamke mi nasafiri chakula kipo tusisumbuane, bye" nikamuuliza sasa unaenda wapi hatujaagana vizuri na hiyo perfume na maua vipi? Akasema Kinachofanya nikuchukie ni hayo maswali yako ya kunifatilia mambo yangu, kwani maua na perfume yanakuhusu nini wewe, kuna kitu yamekukosea? Mmmh nikaishia kuguna tu, nikajiuliza huyu mwanaume ananichukia hivi kwasababu ya huo mchepuko au ndio asili yake makucha yameanza kujionesha, na je wanaume wote wangekuwa k**a yeye dunia ingekuwaje? Mbona amekuwa rimbukeni wa hovyo kabisa, kumnyanyasa mkeo kiasi chote hicho kisa wanawake wa nje?! Nililia sana kwa uchungu, niliomba dua nyingi mpaka kwa kiruga changu nikaililia mpaka mizimu ya mababu na mabibi wa enzi, nikiwaomba wanioneshe mbinu wao waliishije hapo kabla yetu.
Siku hiyo sikula na siku iliyofata nilifunga kwa maombi, Mungu anioneshe njia lakini pia k**a ni kutoka kwenye hii ndoa nitoke salama nimechoka.

Nilikuwa nikipiga anakata, nikamuacha, hakuwahi kunitafuta mpaka mwezi ulipoisha ndio niliona simu yake mida ya saa 10 jioni, kupokea nikasikia analia mke wangu naomba unisaidie niko hoi sana, kuna ugomvi ulitokea kati yangu mimi na huyu mwenzangu tukawa tumegombana sasa akanisukuma kwa bahati mbaya nikawa nimejigonga kwenye nguzo ya kitanda damu zilivuja sana puani nikazimia, yule mwanamke kuona nimeanguka akajua ameua akaamua kukimbia kwa hofu ya kukwepa kesi ya mauaji, tangu amekimbia hajarudi, naomba ufanye utaratibu uje unichukue unipeleke hospital." Nitakuelekeza mke wangu we kachukue bajaji unipigie.
Aliponiambia hayo sikuamini masikio yangu nilihisi k**a naota, maana hajawahi kuniita mke wangu tangu amebadirika, ni majina ya hovyo hovyo tu, leo kulikukoni?! nikaona hapana huyu atakuwa amekula njama na mchepuko wake wanidanganye niende waniue ili wawe huru, nikamwambia pole ila siwezi kufanya hivyo, wapigie mama yako na wifi waje wakuchukue mimi siwezi.
Akasema siwezi kuwatafuta wao nielewe, aliposema hawezi kuwatafuta wao ndio nikaamini huyu mwanaume anataka kuniua nikazima na simu.

Sikuwasha simu kabisa mpaka wiki ilivyoisha ndio nikawasha simu, nikakutana na meseji kibao zote nilizipuuza, ikabidi niwapigie wazazi wake kuwaeleza michezo ya mtoto wao, mama yake akaniambia, nipeleke huko mwanangu alipo na usiponipeleka nitajua wewe ndio umemteka ili wamuue halafu unajifanya haujui kitu" nikihisi k**a masikio yangu yamepigwa shoti ya umeme kwa maneno hayo ya mama mkwe, nililia sana nikajiona mwanamke mwenye mikosi kuliko wote duniani, nikiona mtu hata mtandaoni ameandika "am single" namuonea wivu sana, nikiona makala zako watu wanatafuta wachumba yaani nawaonea huruma mno japo wanaume hawafanani lakini kwangu kitu kinaitwa ndoa nikifanikiwa kuachika kwa hii ya kwanza, sidhani kabisa k**a naweza kurudia, siwezi na siwezi tena nakwambia kaka Halisi Naturalist.

Sasa hivi hapatikani tukipiga, familia yake wamenipeleka polisi kushtaki, nikahojiwa nikaeleza yote nikaonesha na ushahidi wa meseji alizotuma, kwahiyo familia imenipa mtihani wa kuwapeleka alipo mume wangu la sivyo watanionesha, yaani wananipa vitisho vingi wakidai mimi nimemuua na maneno mengi ya kashfa, najuta sana kuolewa kwenye hii familia ya kishetani, mtoto wao shetani mama shetani na kila mtu, hawana utu hata chembe, roho zao ziko kinyume nyume, hapa nilipo sielewi naanzia wapi, naombeni ushauri wenu waungwana, sijali k**a kuna mwanafamilia atasoma hii makala, someni tu mjue ushetani wenu.๐Ÿ˜“

NB: ๐Ÿค”

K**a wewe ni FIRST BORN yaani MTOTO WA KWANZA tambua kwamba nafasi yako ni ya kipekee sana kwenye familia.Hii si nafasi ...
15/08/2025

K**a wewe ni FIRST BORN yaani MTOTO WA KWANZA tambua kwamba nafasi yako ni ya kipekee sana kwenye familia.
Hii si nafasi ya kawaida k**a unavyofikiria, bali ni nafasi yenye mzigo na uzito mkubwa usiichukulie poa hata kidogo, wewe ni wa kwanza kupita kwenye mlango wa maisha ya familia yenu. Hiyo inakufanya uwe njia ya baraka au laana kwenye familia yenu. Soma hii makala kwa makini utajifunza kitu kikubwa hata k**a wewe si wa kwanza kuzaliwa ila unazaa.

Kiroho katika familia mtoto wa kwanza anachukuliwa k**a kiongozi wa kiroho wa watoto wengine. Hata k**a wazazi bado wapo, na wewe unakuwa k**a mzazi na hata ukitoa laana inaweza kushika, wadogo zako huona mwanga na giza kupitia kwako. Maisha yako ya sala, heshima kwa Mungu, na nidhamu ya maadili huwa dira kwao. Ikiwa wewe utachagua njia sahihi, mara nyingi wadogo zako watafuata. Lakini ukipotea, nao wanaweza kupotea kirahisi kwa sababu "maji hufuata mkondo" na mkondo wenyewe ndio wewe.
Wachawi na mapepo yakitaka kuingia kwenye familia yanapitia kwa mtoto wa kwanza ndio yanasambaa kwa wengine, wachawi wakiroga kwa ajili ya kuharibu familia basi kazi yao inakuwa rahisi sana, rejea katika maandiko pale ilipotolewa amri ya kuua wazaliwa wa kwanza, unadhani hii ilikuwa na maana gani? Kwanini wazaliwa wa kwanza? Tafakari utapata jibu. Wewe ni lango kwahiyo mtoto wa kwanza hurusiwi kuishi upendavyo, huruhusiwi kuishi utakavyo, wewe utaishi kwa kujilinda kwa ajili ya wengine, wewe utaishi kwa kuwalinda wana familia, wewe ndio msaada wao wa kuwasaidia kila kitu, USIJISAHAU.

Wazazi wanapokuwa na changamoto, mara nyingi mtoto wa kwanza ndiye anayebeba jukumu la kusaidia, unaweza kuwa mshauri, mlinzi au hata mzazi wa pili kwa wadogo zako.
Maneno yako kwao yana nguvu kubwa sana unaweza kuwatia moyo wakafanikiwa au kuwavunja moyo wakashindwa.
Hata laana au baraka zako kwao mara nyingi huonekana kuwa na uzito, kwa sababu nafasi yako ni k**a daraja la kifamilia.
Kwahiyo k**a wewe ni mtoto wa kwanza halafu ni kilaza, hujielewi upo upo mpaka unazidiwa akili na wadogo zako badirika kuanzia leo, maana baraka za wadogo zako ziko mikononi mwako, ukinyooka kila kitu kitanyooka kwao, unaweza kuona k**a hadithi lakini ndio ukweli wenyewe.

Mtoto wa kwanza mara nyingi huwa kielelezo cha nidhamu kwa familia, wadogo zako huangalia mavazi yako, marafiki zako, maamuzi yako, hata namna unavyoshughulika na changamoto. Ikiwa unajitahidi, wadogo zako hujifunza kujitahidi. Ikiwa unalegea nao huona hakuna haja ya kusimama imara.
Wewe ndiye mstari wa mbele unaofungua njia, ikiwa njia yako ni safi, ni rahisi kwao kupita, ikiwa ni mbovu wote huchafuka.
Acha kujiweka nyuma nyuma heshima yako ni kubwa sana na mara nyingi wadogo zako wakikudharau huwa lazima dunia iwafunze, hata k**a kwa kuchelewa, ila ukitumia ukubwa wako kuwanyanyasa usitarajie hilo.

Uongozi wa asili uliowekwa ndani yako sio wa kawaida, haijalishi jinsia wewe ni kiongozi, hata k**a hujisikii k**a kiongozi, bado uko hivyo. Nafasi yako haiwezi kufutwa, ni k**a alama ya kuzaliwa iliyowekwa na Mungu, unapaswa kufahamu kwamba maneno yako na mienendo yako huacha alama kubwa kwa wadogo zako, kwa familia na hata kizazi kijacho.

Wewe k**a mtoto wa kwanza ni lango, lango la baraka au lango la laana, ni juu yako kuamua ni aina gani ya lango unalifungua kwa ajili ya ndugu zako.
Chagua kuwa mkondo safi unaoleta mafanikio, upendo, mshik**ano na heshima.
Ukianza kuleta vita na mgawanyiko kwenye familia basi tambua hakuna mtu anaweza kuiunganisha hiyo familia, vita vitaendelea mpaka kiama mpaka pale utakaporekebisha makosa yako wewe mwenyewe na si mwingine.
Jitahidi kusamehe, kuwa mfano wa nidhamu na heshima, kuwa kiongozi wa sala na mshauri wa familia. Nafasi yako ni k**a taa juu ya mnara, kadri inavyongโ€™aa ndivyo familia nzima inavyopata mwanga.

Swabira E Saidi

(You can share this information to others but without editing and putting your name. This information has been copy righted under Halisi Naturalist, any form of plagiarism or data manipulation will be regarded as an offence.)

Leo wakati naenda kazini nilipanda daladala moja hivi kutokea ubungo mawasiliano kuelekea kurasini ninapofanyia kazi, ni...
14/08/2025

Leo wakati naenda kazini nilipanda daladala moja hivi kutokea ubungo mawasiliano kuelekea kurasini ninapofanyia kazi, nikiwa ndani ya daladala nilikaa seat moja na mama mmoja, alikuwa kajiinambia analia, sikutaka kumuuliza chochote safari ikaendelea, baadae akaniambia "samahani kaka k**a una salio naomba unisaidie niongee na mtu" nikaona sio kesi ngoja nimsaidie simu, nikatoa simu mfukoni nikampa, akaweka namba akaanza kuongea.

Alikuwa anaongea na mwanae wa k**e kwa jinsi nilivyosikia mazungumzo, inaonesha mwanae mwingine wa k**e alifukuzwa katika nyumba aliyokuwa anaishi kisa kushindwa kulipa kodi, na alikuwa mgonjwa hajiwezi hivyo mama huyo alikuwa njiani kuelekea kule alipo mwanae aliyefukuzwa.
Baada ya mazungumzo nikamuuliza mama mbona unalia halafu mazungumzo yako yamejaa huzuni nini shida? Akaniambia "mwanangu hii dunia kuna watu tulikuja kuteseka tu, ukizaliwa masikini kwenye ukoo masikini ukazungukwa na masikini basi ujue kuwa wewe dunia hii hauna haki, hauna thamani na upo upo tu kukamilisha ratiba" nikamwambia hapana mama usiongee hivyo,, jaribu kufupisha tatizo ulilonalo ili nielewe.

Akasema mimi nina binti yangu ameolewa na mwanaume ambaye na yeye maisha yake sio mazuri ni mpambanaji, anafanya kazi viwandani na wanalipwa Tsh 150,000 kwa mwezi, k**a hakuna shida zinazojitokeza katikati hiyo pesa huwa inawatosha wakijibana bana vizuri, lakini safari hii imekuwa tofauti kwani mwanangu wa k**e amejifungua kwa operation sasa gharama zilikuwa kubwa hata pesa ya chakula cha mzazi tumekosa anakula ugali tu huu huu, tulichanga changa na mume wake akaongezea gharama kwa ajili ya mke wake kujifungua maana mimba yake nayo ilikuwa na changamoto nyingi sana.
Kwahiyo imepelekea washindwa kulipa kodi, na hapo walipo imezidi miezi miwili hawajalipa sasa mwenye nyumba kachachamaa mwisho kawafukuza, ametupa vitu nje amefunga nyumba yake mwanangu na kichanga chake wako nje wanapigwa na baridi, mwanangu hana hata nauli ya kuja nyumbani lakini pia kidonda cha operation bado hakijapona, ndio maana nimeenda nimlete nyumbani japo sijajua nitamlisha nini.
Huyo niliyempigia ni binti yangu mwingine yupo mwanza anahangaika na yeye huko, akipata ka elfu 5, elfu 10 anafanya kunirushia nipate usaidizi, nimempigia kumueleza anayopitia dada yake k**a anaweza kuwa na msaada wowote.

Nikamuuliza huko mwanza anafanya kazi gani akasema hajui, nikamuuliza tena amekujibuje akasema amenijibu kuwa hana atajitahidi kufikia jioni anitumie elfu 10.
Nikamuuliza mume wako yuko wapi? Akasema yupo lakini na yeye ni dhoofulihali hana chochote kwanza anaumwa miguu muda mrefu nimemuacha nyumbani.
Daah niliumia sana, hali ya maisha ni changamoto sana kwa watu wengi ila kuna kesi ukizisikia mpaka unachanganyikiwa, unaona k**a umependelewa ingawa na wewe una ya kwako.

Nilichokifanya nilimwambia mama usijali Mungu atakusaidia, nilipofika uhasibu nikashuka, ila baada ya kushuka nilianza kubabaika moyoni, niliumia sana nikashindwa kabisa kuvumilia, ikabidi niliwahi lile gari nikapande, nilichukua boda na nilienda kupandia kituo cha mbele, ila yule mama hakuniona maana alikuwa amekaa nyuma, gari ilipofika zakhiem nilimtazama yule mama anasimama ashuke ikabidi nishuke mimi kwanza, na yule mama akashuka nikabana sehemu asinione, nikaanza kumfata nyuma nyuma, akaenda mpaka kituo cha gari za mbagara kuu, alipopanda mimi nikachukua boda nikamwambia aifate ile gari, mpaka kuna sehemu yule mama akashuka nikawa namfata nyuma nyuma, hatimaye nilifika pale alipokuwa anaenda.

Kwakweli alishtuka sana kuniona na k**a sio kwa ujasiri huwenda angezimia, maana aliniona nimeshuka halafu ananiona mbele ya macho yake, hisia zake zilimfanya awaze pengine mimi ni jini, lakini nikajaribu kujieleza mpaka akatulia, hali niliyoikuta pale ilikuwa ni kweli kabisa, mwanae alikuwa nje amkalia ndoo amempakata mwanae na amejifunika kanga mpaka usoni kukinga jua huku vitu vikiwa hapo hapo, niliumia sana, na nikaahidi kumsaidia japo mimi sio tajiri ila nitasaidia tu.
Bank nilikuwa nina k**a 1.3M nilienda bank mbagara pale nikachota 700k nikaenda kuwapa, na nikawaambia mtaamua wenyewe mnafanyaje, k**a kulipa kodi au kuhama, maamuzi mnayo nyie, nikawaambia sihitaji mje mnitafute kunipa shukrani au chochote, msaada wangu ni huo ila sihitaji mahusiano yoyote, nikawaaga pale nikaondoka.

Siku nzima imeisha nawaza hilo tukio ๐Ÿ˜“

NOTE: (You can forward this information to others but without editing and putting your name. This information has been copy righted under Swaakid , any form of plagiarism or data manipulation will be regarded as an offence.)

Habari samahani naombeni ushauri, hapa nilipofikia naona nimefika mwisho kabisa nahitaji akili mpya kuvuka hapa, mimi ni...
13/08/2025

Habari samahani naombeni ushauri, hapa nilipofikia naona nimefika mwisho kabisa nahitaji akili mpya kuvuka hapa, mimi nilioa mwanamke miaka minne iliyopita, alikuwa mwanamke mzuri tu, mpole na mstaarabu, na kwa bahati nzuri nilienda kuoa nyumbani kwetu, tulifunga ndoa halali kabisa na nashukuru nilimkuta na usichana wake, kwa hilo nampongeza sana.
Ninaishi Ukonga Dar es salaam kwa sasa, mwanzo ndoa yetu ilikuwa na amani lakini baada ya miaka miwili mwanamke alianza kubadirika, akawa hanisikilizi tena, ninachomkataza anakuwa mkaidi na mbishi, akawa anatoka sana nyumbani nikijaribu kumzuia anasema mimi ni mnyanyasaji, ikabidi niwe natumia kufosi akikataa namuadhibu kwa viboko au makofi.

Akanishtaki kwao na kwetu kuwa mimi nampiga namuonea na mambo mengi, nilipojaribu kuwaelewesha sababu walinioinga na kusema sipaswi kumpiga no matter what.
Basi kile kitendo kiliniuzi sana na sikufatilia nikamwambia lazima uniheshimu na kunitii kinyume na hapo lazima uchezee kichapo, wao wana ndoa zao na sisi hii ni ndoa yetu, kilq mmoja apambane na ndoa yake,
Nimejaribu kukuonya kwa mdomo lakini hukuwahi kunisikia je ulitaka nifanyeje? Nikuache tu mpaka siku utakapokunya kwenye sahani? Mwanamke akawa anagomba tu, maneno yanamtoka, anaweza kuongea kuanzia asubuhi mpaka jioni bila kuchoka.
Nikawa najiuliza hivi nimeoa sabufa au nimeoa binaadamu?.

Yote tisa ila tabia yake ya kuongea sana ndio ilikuwa no.1 katika tabia zote ambazo nilikuwa sizipendi, yaani anaongea wakati wote mpaka muda wa kulala, ile hali ilininyima amani kwa kiasi kikubwa sana, ikapelekea mpaka ninaporudi kazini nitafute pa kwenda angalau muda usogee sogee ndio nirudi nyumbani, na nilikuwa najitahidi kuondoka kabla hajaamka, nikaona k**a ile ndoa inaniboa, nikaona k**a niko kifungoni ndani ya nyumba yangu mwenyewe!.
Nikaja kugundua kumbe ana marafiki/shoga zake ndio wanamshauri vibaya na kumuharibu akili, ikabidi nikomae na hao shoga zake, nikamzuia katu katu asiwe na uhusiano nao, lakini kwakuwa sishindi nyumbani juhudi hazikuzaa matunda.

Wale shoga zake wakamwambia eti mimi nina mchepuko ndio maana namtesa, yaani walimwambia kuwa ninamtesa kwasababu tu ya kumzuia ukaribu nao, kumzuia tabia za kiburi na mdomo mrefu, kumzuia kutoka nyumbani bila uwepo wangu au ruhusa yangu, wakamwambia mengi, kwamba mimi ni mkoloni n.k
Ilifika time akajifungua mtoto, muda wote nyumba ilikuwa inajaa watu na wengine siwafahamu, kila nikitoka nikirudi nakuta makelele wanawake wanacheka sauti ya juu kisha wanagonga mikono.
Nikawa nakaa kimya tu nisionekane mbaya, kumbe baadhi yao ndio walikuwa wanamtafutia mabwana.
Niligundua hilo siku moja ambapo nilimkuta anaongea na simu na baada ya kusikia anaongea nilijificha, nikasimama mlangoni, sikusikia vizuri alichokuwa anaongea ila kuna maneno kadhaa yalinipa mashaka.
Nikafungua mlango ghafla na kuingia kabla hata ya salamu nikamwambia leta hiyo simu, akagoma kunipa, nilimtandika kibao kimoja mpaka nikasikia mkono unawasha, simu ikaanguka nikaichukua, kufungua hivi nakuta namba haina jina.
Kuchukua ile namba kupiga naambiwa namba hii haipo, nilichoka! Ikabidi nimuite yeye mwenyewe nikamwambia piga namba hii mbona naona hapa kwenye call log mmeongea dakika 3 halafu napiga namba hii hii naambiwa haipo, akajibu yeye hajui.

Kwa hasira nilizokuwa nazo, nilitaka kila kitu kiwe wazi, nikatoa laini nyingine ya tigo ambayo huwa siitumii sana nikaweka kwenye simu nikainunulia salio nikaanza kupiga ile namba lakini niliambiwa 'Namba hii haipo", nilishangaa sana, kivipi haipo na wakati ndio namba inayoonekana kwenye simu ya mke wangu? Ikabidi nichukue simu ya mke wangu nipige mwenyewe, ile namba iliita kwenye simu ya mke wangu na huyo mtu alipokea, nikaa kimya akaanza kuongea Haloo halooo sauti ni ya kiume, nikakata, nikapiga tena kwangu ila naambiwa namba hii haipo.
Nilipanga nitampigia huyo mtu kwa baadae, nikaenda kuoga nikala chakula, nikaenda chumbani kulala kwanza kupumzisha akili.

Simu sikumrudishia mke wangu, ilibidi nimpokonye simu kwa uchunguzi zaidi, ziliingia meseji nyingi za kipuuzi kutoka kwa mashoga zake nikawa nasoma napuuzia tu, nikapitia chatting nyingi, nilipoingia whatsapp nikakuta sms "Mbona unapiga hauongei baby au hiyo ng'ombe yako imesharudi?" Nilihisi ubongo umehama sehemu yake, nilipanic mpaka nikashindwa kulala, nilikataa nawaza kumkata mtu k**a slice za mkate, ila nikajituliza akili.
Niliview profile nikaona namba mbili tofauti, yaani ile unabonyeza profile ya mtu ili uone picha, namba, na bio yake, mimi niliona namba ziko mbili tofauti, ndio nikagundua kwanini ile namba nilipokuwa nikipiga naambiwa namba hii haipo.

Kumbe mke wangu alichukua namba ya bwana wake na wakati wa kui-save sehemu ya kuweka jina la muhusika aliweka namba nyingine ambayo haipatikani yaani badala ya kuandika Juma anaandika 0765*******, kwahiyo ukiona inaita utachukua hii namba inayoonekana k**a jina kumbe ni trick tu ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ, alifanikiwa kunigeuza mjinga.
Ili kufupisha stori ni kwamba nilijiridhisha kuwa anatembea na yule jamaa, nilichofanya nilimwambia jamaa amchukue mke wangu amuoe maana naona wamependana sana, siwezi kuendelea na mwanamke ambaye yuko kwenye upendo na mwanaume mwingine. Mi nikamchunia mazima, mke wangu alivyokuwa mjinga akanisusia mtoto akiwa na miezi 9, akimaanisha kuwa itashindwa kumlea hivyo nitalazimika kumrudisha.

Alipofanya hivyo nikasema huyu mwanamke hanijui kumbe, wiki hiyo hiyo nikahama nilipokuwa nakaa nikahamia pengine japo kodi ilikuwa bado ipo ya miezi k**a minne hivi, sikujali hilo, nikaondoka, nikatafuta housegirl ambaye alikuwa mmama mtu mzima, nikamchukua na mdogo wangu wa k**e nikaishi nao wakinilelea mwanangu, mpaka amekuwa hivi alivyo yule mwanamke alinisumbua sana kuomba msamaha, mameseji masimu, nikaamua kubadirisha namba.
Kuna sehemu nikikuwa najenga nyumba imekamilika mwaka huu mwenzi wa pili na tulishahamia ndio tunaishi hapa kwa sasa, sijui nani alimuomesha, mwezi wa 6 alikuja kunipiga goti nimsamehe kuwa atajirekebisha nikamwambia siwezi tena acha kujipendekeza kwangu sikutaki.
Sasa hivi amekuja na mbinu mpya kwamba anamtaka mwanae, nimpe mwanae la sivyo atanishtaki na nitashindwa kwa mujibu wa sheria.

Hivi huyu mwanamke anaweza kushinda kesi na kumchukua mtoto? Wakati alimtelekeza mwenyewe? Na je nitumie mbinu gani ili akate tamaa na maisha yangu na mwanangu, yaani simpendi hata kumuona tu, nikimuona au kumsikia moyo unaishiwa nguvu hapo hapo, nisaidieni ni ananikera to the maximum.

Mzee alileta ujuaji sasa hivi nimejipata ananitafuta anataka nimsaidie, hii dunia ina mambo mengi ya kustaajabisha, na m...
13/08/2025

Mzee alileta ujuaji sasa hivi nimejipata ananitafuta anataka nimsaidie, hii dunia ina mambo mengi ya kustaajabisha, na mimi k**a mwanaume siwezi kurudia makosa aliyofanya mzee, ni bora nilee mtoto hata k**a sio wangu kuliko kumtelekeza halafu baadae nipeleke pua yangu eti nataka msaada, hell no.
Iko hivi mzee wangu alimuoa mama akiwa binti mdogo (early 20s), baadae akampa ujauzito akatokomea kusiko julikana akidai ameenda kutafuta maisha, siku zilienda na kwenda mimba inazidi kuwa kubwa na hatimaye ukafika muda wa kujifungua, mama yangu hakuwa hata na akiba ya doti moja ya kanga ndani, alidhalilika sana mpaka kufikia kusaidiwa na wasamalia wema vinguo.
Mama alitembea na vilaka mwili mzima si hilo tu alidhoofika sana kiafya maana alijifungua kwa operation na hakupata matunzo ya aina yoyote hata uji tu ๐Ÿ˜ญ.
Ikafika hatua akatoka pale nyumbani na kuhamia ukweni, yaani kwao baba ili angalau tupate msaada hata wa chakula.
Maisha hayakuwa mepesi pale kwa babu, alinyanyaswa kiasi kwamba alijaribu kutaka kujiua mara kadhaa akafeli, kulima ilikuwa yeye, asubuhi mpaka jioni yuko busy na mimi mgongoni, halafu kulikuwa na wanawake wengine (wake wa vijana wa hiyo familia) ambao nao walikimbia wake zao wakaenda kutafuta maisha, kwahiyo ulikuwa ni mji mkubwa na ilionekana k**a kero fulani kwa wao kuishi pale, so mateso yalikuwa makali, kazi za shamba masika na za bustani kiangazi, na hapo hawapewi hata mia ya kujikimu k**a wanawake watu wazima.

K**a baada ya miaka 7 baba yangu alirejea, alirudi na mke mwingine ambaye alikuwa na mtoto mdogo wa k**a miaka 5, akamfikishia kwenye nyumba aliyokuwa akiishi na mama yangu, tangu amefika hakujisumbua kututafuta wala kwenda kwao kusalimia, ilipita k**a miezi mitatu tangu amefika ndio akawa ameenda kwao kusalimia, alifika na baada ya salamu za hapa na pale mama yangu aliitwa, akaambiwa huyu hapa mwenzio amerudi kusanya matambala yako muongozane, baba akamkatisha babu "mzee mimi nimekuja na mke mwingine na nimemfikishia kule kwangu, sijaja nae kwa makusudi maana naandaa mazingira ili nimlete kumtambulisha mumjue" wakamlaumu pale lakini kwa baadae wakaungana nae.
Lakini wakamwambia lazima uondoke na mzigo wako, nilikuwa mdogo lakini nilikuwa naelewa sana situations.

Kishingo upande baba akaondoka na sisi mpaka nyumbani, njia nzima mama alikuwa analalamika na kulia, huwezi amini tulipofika baba alimwambia mama wewe utakuwa unalala sebuleni na mtoto, sisi tutalala chumbani, ukiona umeshindwa kuvumilia njia ni nyeupe unaweza ukaondoka, shida mama kwao ilikuwa ni mbali sana na pia walikuwa masikini mno ๐Ÿ˜“.
Alikondeana sana na alichekwa mno na majirani kwa kuishi nyumba moja na mke mwenza wakati nyumba ni chumba kimoja na sebule, si hilo tu yule mke wa baba aliishi k**a mfalme, kazi zote alifanya mama yangu, na alitambiwa na mke mwenzie kila uchwao, uzalendo ukamshinda akaja kuondokaga pale nyumbani, akaenda kijiji cha tatu kutoka tulipokuwa tunaishi.
Hakuwa na nauli, alitembea kwa mguu na mimi nikichoka ananibeba au ananiweka juu kwenye mabega yake, najikaza natembea mpaka tukafika, lakini hakujua anaenda wapi na kwa nani, aliianza tu safari ya imani.

Alipofika kijijini pale aliamua kukaa sehemu, jirani na mji fulani, mchana akaenda kuniombea chakula akijifanya kuna mtu anamsubiri waendelee na safari, kwa bahati nzuri tulikula wote tukanywa maji tukashukuru Mungu kwa siku hiyo.
Tulikaa pale mpaka usiku, ikabidi mwenyeji aulize mbona huyo mtu hafiki, akasema labda amepata matatizo njiani hata mimi nina wasiwasi, tukapewa sehemu ya kulala, usiku tumelala mama akawa ananiambia kila kinachoendelea na kuniomba ushauri, nilikuwa mtoto mdogo sana lakini alifanya hivyo ili angalau ayatoe ya moyoni kwa kujiona ana mtu wa kuongea nae.
Palivyokucha ikabidi aongee ukweli wake wote kwa wale wenyeji na wakaamua kumsaidia, kuna jiko lilikuwepo, wakampa kiwe chumba chake, tukasafisha vizuri tukapewa mkeka na vikoi viwili ndio tukawa tunalalia.
Tulifurahi sana maana ilikuwa ni amani, hata mimi japo nilikuwa mtoto kuna amani fulani nikaanza kuipata, nikaanza kucheza na watoto wengine wakati tulipokuwa kwa baba sikuwa na mood ya kucheza, nachezaje kila muda naona mama analia, mama anafokewa, mama anagombezwa, nilijikuta nakaa around muda wote.

Kulikuwa na mashine za kukoboa mpunga jirani, yule mama aliyetukaribisha kwake akaja kumpeleka mama yangu kwenye hizo mashine kufanya kazi mbali mbali mfano kuanika na kuanua mpunga, kupepeta pumba, na nyingine nyingi ili apate hata 500 ya sabuni, mama alifanya kazi k**a mwendawazimu na kila akipata 5000 anachukua 2000 anampa yule mama aongezee kwenye pesa ya mahemezi ya chakula, elfu 3 anatunza, alikuwa hakosi kuniletea kitu hata k**a ni p**i ya 100 tu, ilimradi nifurahi nisiwe mnyonge.
Alipiga kazi sana, tulikaa pale miaka miwili, akaenda kupanga chumba kimoja, akakodi na shamba hekari moja.

Mwaka ule ule tulipofika kwenye ile familia nilipelekwa kuanza shule, mpaka nafika miaka 7 nilikuwa sijaanza shule ๐Ÿ˜ญ, so baada ya mama kupanga na kukodi shamba, hakuacha ile kazi mashineni, aliendelea nayo, tulihamia jirani tu na pale tulipokuwa tunaishi na ile familia ilibaki kuwa ndugu wa karibu, mama alivuna gunia 5 tu za mahindi kwa heka lakini bei ilikuwa nzuri, aliuza zote, akaunganisha na pesa aliyotunza akawa na kiasi kizuri tu cha pesa.
Tukaenda kwa wenyeji wetu akawaaga na nakumbuka siku hiyo ulipikwa ubwabwa na soda za kumwaga, aliwaaga tukaenda kwao mama.

Nilipelekwa shule, mama akawa na biashara ya kuuza nafaka na mafuta ya kula, kwakweli ile biashara iliendelea na nimesoma kupitia hiyo hiyo biashara maana nilisoma hizi shule za kata, ila kwa uchungu niliokuwa nao aisee sikufanya mchezo, nilikaza sana nikafaulu kwa marks za juu kote nilipopita. Mpaka nakuja kutoboa kimaisha haikuwa rahisi hata kidogo.
Mama yangu alikuwa mgonjwa mgonjwa nikampeleka hospital kubwa Dar es salaam, akakutwa na tatizo la moyo, kwamba moyo ulitanuka, lakini nashukuru Mungu lile tatizo liliishaga, niliambiwa msongo wa mawazo na sonona ndio ilikuwa sababu.

Sasa baba yangu mzazi ananitafuta anataka nimsaidie, anasema nimkatie kibali nimpe na mtaji afanye biashara ya mbao, kwakweli bora nionekane hayawani ila kumsaidia mzee siwezi kabisa, maana humo katikati kwenye story yapo mengi sijasema ila nilishawahi kumtafuta kipindi nipo form 2 alichonijibu alisema "wewe hapo ulipo umeshakuwa halafu wewe wa kiume usipende kuomba omba pambana". Nikamwambia napambana vipi na mimi ni mwanafunzi, akajibu, aliyekulipia ada usome ndio unatakiwa umpe matatizo yako yote kuhusu shule ayamalize, nikamwambia lakini baba mbona hunitafuti hata kuniulizia tu ujue hali yangu! Akasema sasa nikishajua hali yako wewe utafaidika na nini? Nilisimama nikaenda kupanda gari, sikujibu neno.

Ushauri wangu kwa wanawake ambao mnaolewa, jitahidini kuangalia na ukoo, ukiona kaka mtu, mdogo mtu, dada mtu, wana matukio ya hovyo ya kufanana usijaribu kuingia kwenye hiyo familia utajuta sana maisha yako yote, ukoo wa kina baba naweza sema baba mdogo na baba mkubwa zangu wote wako hivyo japo viwango vinatofautiana wapo wenye nafuu.
Sasa najiuliza huyu mzee ananiomba msaada ina maana amesahau yote au anatafuta lawama tu?!

25/07/2023

Watch, follow, and discover more trending content.

Address

Mbezi Beach Africana
Dar Es Salaam
00000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Swaakid posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Swaakid:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram