Jali Company Limited

Jali Company Limited Jali Company Limited Jali Company Limited is established in accordance to Tanzania National Companies registration Act on 4th December 2009.

The Company Deals with Fumigation service, sell of all types of laboratory equipement, supplies and consumables, hospital equipment, pharmaceticals, drugs and consumables. It also deals with Fumigation services and Cleaning services.

02/05/2023

Chagua, utachukua nusu kuku au robo Ng'ombe?

Namshukuru Mungu kwa ajili yako Gladness.Nakutakia heri katika siku yako ya kuzaliwa.happy birthday daughter.
25/01/2022

Namshukuru Mungu kwa ajili yako Gladness.Nakutakia heri katika siku yako ya kuzaliwa.happy birthday daughter.

09/05/2021

Happy Mother's day.

18/02/2020
26/06/2017

Tunawatakieni Iddi Njema

04/06/2017

Ramadhani Kareem

06/11/2016

Juma hili tunaenda kujadili kuhusu Kunguni(Bedbugs). Je unamjua Kunguni? Madhara yaletwayo na kung'atwa na Kunguni?
Karibu tujadili.

30/10/2016

MENDE
Somo lililopita tuliona japo kwa uchache sana madhara yaletwayo na mdudu msumbufu Mende, nikukaribishe tena kwenye safu hili ya leo kuhusu hatua za maisha ya Mende na jinsi ya kumzuia au kumwondoa ndani kwako bila kutumia sumu kali wala kemikali.
B: HATUA ZA UKUAJI WA MENDE
K**a ilivyo kwa wadudu wengi Mende huanzia hatua ya yai, na hupita hatua tatu hadi kifikia hatua ya mwisho ya ukuaji mende mzima (adult). Hatua hizo ni Yai;
Ni Muhimu ifahamike kuwa kuna jamii nyingi sana za mende zaidi ya 4000 ambao huwa na tofauti ndogondogo za maendeleo ya UKUAJI NA TOFAUTI ZINGINE ila kati ya aina hizi kuna aina tatu wanaoishi majumbani mwa watu. Hapa naenda kuzungumzia zaidi wale mende ambao wamekuwa ni tatizo kubwa kwa Watanzania na kwingineko duniani majumbani.
1. Yai
Mayai ya mende yanakaa ndani ya mfuko wa mayai wa rangi ya kahawia unaobeba wastani ya mayai 35 ujulikanao kitaalamu k**a Ootheca (Fuko la mayai). Ukubwa wa ootheca moja inakaridiwa kuwa mm 7 urefu na mm 2 upana japo hutofautiana sana ukumbwa kati ya jamii moja ya mende na nyingine.
Kwa jamii nyingi za Mende, dume huyarutumbisha viyai ndani ya jike na huendelea kujitengeneza ndani ya ootheca. Jamii zingine za mende hubaki na mayai hayo na hukomaaa hadi kuanguliwa ndani ya mwili na vifaranga huwa k**a wanazaliwa; mfano k**a vile Madagascar hissing cockroach.
Jike hutaga mayai mfululizo anapofikia hatua ya mwisho ya ukuaji na kwa maisha yake yote ya watani wa siku 100 kutegemeana na jamii ya mende. Mende mmoja anauwezo wa kutaga mayai kwa makadirio k**a 4oo hivi. Kwa aina ya mende waliozoeleka na wanaopatikana kwa wingi nchini Tanzania hubeba mayai (ootheca) mwilini mwao hadi linapobakiza siku mbili au siku chache kuanguliwa kisha hulitagia sehemu salama na ngumu kufikika na binadamu. Mara nyingi mende jike mzima(adult) huonekana akiwa na fuko la mayai mwilini mwake kila aendapo.
2. Vifaranga (Nymph)
Vifaranga huanguliwa vikiwa vidogo sana, rangi nyeupe, vilaini na hawana mabawa ambao hukua huku wakibadili rangi hadi kufikia mende mzima. Vifaranga mara nyingi huanguliwa ndani ya siku 24 hadi 38 na idadi ya vifaranga vitakavyoanguliwa hutofautiana kutokana na aina (Spicies) ya mende.
Vifaranga hupitia hatua mbalimbali za kujibadili (molting) mpaka kufikia kuwa mende mzima. Vifaranga (Nymph) na mwisho mende mzima na mara zote vifaranga (Nymph) ni mara tatu ya mende wazima yaani Vifaranga (nymph) 75% na Wakubwa (adult) ni 25% ya mende wote waliopo kwenye makazi ya binadamu.
3. Mende Mzima (Adult)
Japo kuna jamii za mende ambazo hazina mabawa jamii nyingi wana mabawa, jamii hizi ambazo ni wasumbufu sana ndani ya makazi ya watu nchini mwetu Tanzania na Africa mashariki wana mabawa na huweza kuruka japo kwa umbali mfupi na hii huwa saidia sana kusambaa kutoka kwa jirani mmoja hadi kwa mwingine. Mende hujifisha mchana na usiku hula na kutembea.
Japokuwa mende ana uwezo wa kukaa bila kula kwa muda wa miezi mitatu hawezi kuishi bila kunywa maji, Mende huishi kwa kula mabaki ya vyakula, kunywa maji hula pia kwenye njia ya maji machafu na pia chooni na wanaweza kuziba masinki k**a wapo wengi sana kwenye nyumba.
Kwa asilimia kubwa mende husambaa kupitia wasafiri hukaa kwenye mabegi, redio na viafaa vingine vinavyosafirishwa na ukifika unako kwenda huhamia ndani ya nyumba.
Hotel nyingi zinapata mende kupitia wateja wao wanaokuja kulala huleta mende bila kujijua

C) JINSI YA KUWAONDOA NA KUWAZUIA WASIJE NYUMBANI BILA KUTUMIA WATAALAMU WALA
Kuna njia mbali mbali za kupambana na mende nyumbani kwako bila kutumia wataalamu wa kupulizia sumu au chemikali za kununua.
1. Majani ya Bei (Laurus nobilis); mende hawaupendi mmea huu na hivyo ukikatakata na kuweka sehemu sehemu za mende kucheza na kula mende huondoka
2. Sumu ya mende ya kujitengenezea;
Chukua kijiko kimoja cha chakula ya asidi ya boric changanya na vijiko viwili vya unga wa mahindi na kijiko kimoja cha kokoa changanganya vizuri na nyunyiza sehemu ambazo mende hupenda.
NB mchanganyiko huu ni sumu hivyo weka mbali na watoto
3. Mtego wa mende;
Vaselini uliotandazwa vyema kwenye kiboksi hunasa mende na hawataweza kutembea juu ya vaselini. Ni vizuri kuweka chakula cha kuwavutia Mende ili waje kwenye mtego.
4. Mchanganyiko wa sabuni na Maji;
Changanya sabuni ya maji na maji iwe nyepesi kiasi cha kuweza kupuliza kwa kutumia chupa ya kupulizia. Kwa kutumia chupa ya kupulizia ama bomba ya kuogeshea mifugo hakikisha unamdondokea mende, ikimdondokea tumboni ni vizuri zaidi. Matone madogo mawili yakimpata mende tumbuni hufa baada ya muda mfupi
5. Amira (Baking Powder) and sugar;
Changanya kwa uwiyano sawa sukari na amira (Baking Powder) kasha nyunyiza seheme mende wanapenda kukaa sukari itawavutia kula na Amira itawauwa kwa kuwa fanya wavimbiwe.
6. Sprei ya Nywele (Hair Spray);
Wapulizie mende sprei ya nywele watakufa mara moja
7. Wanyime maji na chakula;
Kumbuka mende wanahitaji maji kuliko wanavyohitaji chakula; hapa unashauriwa mabomba yote yafungwe vyema yasiwe yanavuja maji, maji yakimwagika hakikisha unayakausha kwa kudeki na kuacha nyumba yote kavu na sinki zote zifunikwe vyema usiku na mchana pia kwa kutumia kizibo cha sinki; jokofu pia zisivuje.
Jitahidi mabaki ya chakula yasibaki popote jikoni na chumba cha kulia chakula (dinning) pia, vyakula vinavyobakizwa vivunikwe vyema kwenye bakuli mbalimbali na kuwekwa kwenye jokofu au mahali pakuhifadhi chakula, vyombo vioshwe mara tu baada ya kula. Kumbuka kipunje kidogo cha chakula kinawashibisha mende wengi hivyo umakini kwenye hili unatakiwa.
8. Mchanganyiko wa Matango, pilipili na Limao
Koroga mchanganyiko huu kisha weka sehemu ambazo mende hupendelea kikaa/kuishi na mende watakimbia ndani kwako hawatakaa.
Safisha nyumba yako sana;
Anzia jikoni pawe pasafi sana bila mrundikano wa vitu na vyombo visivyosafishwa. Vyakula vilivyobaki vifunikwe vyema na kuwekwa kwenye jokofu.
9. Ficha chakula;
Chakula chochote ambacho mende hula kitunzwe vyema sehemu ambapo mende hafiki kwenye jokofu pia matumda huwapatia chakula na maji pia yatunzwe vyema
10. Safisha Sakafu;
Nasisitiza kuwa Mende anahitaji maji ili kuishi jitahidi kuhakikisha hawapati maji kwa kusafisha na kukausha sakafu; ondoa pia mabaki ya chakula, michirizi ya chakula na matone ya chakula kwenye sakafu na ukutani au popote pale.
11. Ondoa chombo/debe la taka kila siku
Hii itawanyima chakula mende ambao mara ngingi hujilisha ndani ya chombo cha taka pia nashauri chombo taka cha nje kisikae sana karibu na nyumbu ili kuepusha mende wasiende kujilisha huko usiku na kurudi ndani.
12. Maji ya Moto
Hii nimeshudia sehemu/jamii nyingi za nchi yetu, maji huchemshwa na yanabaki yakiendelea kuchemka na huchotwa kwa kutumia chombo na kuyarushia kwenye mikusanyiko wa mende vifaranga na wakubwa haraka kabla ya kupoa. Hii ikifanyiki kila siku mende huisha. Njia hii ni vizuri ikaendana na 9 hadi 12 kwa pamoja hizi zitamaliza tatizo lamende bila kutumia sumu ama kemikali ambazo huitaji mtaalamu ama garama kubwa.

D) KUZUIA MENDE WASIRUDI
i. Ziba Nyufa
Nyufa za kuta za nyumba pamoja na fenicha huwa makazi mazuri ya mende hivyo wanyime makazi hayo kwa kuziba nyufa za fenicha na kuta za nyumba
Ziba nafasi k**a vile zile zilizopo kati ya kabati ya kujengea na ukuta kwa kutumia simenti au gundi maalum ya mbao waweza kumshauri fundi afanye hivyo wakati wa kutengeneza kabati na k**a umepanga ama unaishi kwenye nyumba ya mwajiri basi jitahidi kuhahakiosha hili linafanyika.
ii. Wazuie mende wasiingine ndani
Weka nyavu kwenye madirisha na sehemu za kupitishia hewa kwenye nyumba pia milango iwekewe visuia wadudu kwa chini na zibaki zimefungwa wakati wa usiku. Tundu lolote lisilo (kioo, mbao, Ukuta nk) la lazima lizibwe.
iii. Epuka marundo ya mazao ya miti karibu na nyumba
Marundo ya mbao, kuni, mabanzi, nk huwa ni kivutio cha mende hivyo yakiwa karibu na nyumba hupelekea mende kuhamia ndani, hivyo nashauri zikae mbali na nyumba ya makazi.

12/10/2016

MENDE
MADHARA YA MENDE KWA BINADAMU
1. KERO; mende wanapokuwepo kwenye nyumba ama makazi ya binadumu husababisha kero k**a kupita na kukatiza hovyo, huingia kwenye vyakula na vinywaji na hivyo kusababisha hasara, waweza kumtambaa mtu na hata kumng’ata, hufanya uaharibifu kwa kung’ata na kuweka matundu kwenye nguo, wana harufu Fulani ambayo sio nzuri, anaweza kuchafua nguo ama katarasi nyeupe kwa kunya juu yake.
2. KUCHAFUA CHAKULA; mende hula karibu kila kitu ambacho binadamu anakula na bahati mbaya mdudu huyu hukaa pia chooni na kwenye njia za maji machafu na hivyo huweza kubeba vimelea vya magonjwa mbalimbali kutoka huko na kusababisha magonjwa kwa njia hiyo.
3. KUOTESHA WADUDU WA MAGONJWA; utafiti umeonyesha baadhi ya vimelea vya magonjwa wanaweza kuota kwenye mfumo wa chakula wa mende, na kwa kuwa mende anapopita na kula chakula chako huwa na tabia ya kucheua na kutema mate yake kwenye chakula hicho hivyo kuweka vimelea hivyo vya magonjwa kwa binadamu k**a magonjwa ya tumbo na hata majipu.
4. HUNGATA NA KUUMIZA BINADAMU; hii hutokea mara chache lakini k**a mende ni wengi sana wanaweza kunga’ta watu na hata kusababisha majeraha makubwa kwa kula ngozi za mwili, kucha, vidole hata midomo.
5. KUINGIA KWENYE MATUNDU YA WAZI YA MWILI; Mende wadogo wanaweza kuingia na kusabsabisha matatizo kwenye sehemu za mwili k**a vili masikio, pua, mdomoni, nakadhalika
6. ALLEGIES; mende wanaweza kusababisha aleji kwa binadamu; kinyesi, mate na majimaji ya mende pamoja na mabaki ya miili yao hupelekea aleji kali sana kwa baadhi ya watu, ikiwemo kupiga chavya, kutokwa machozi, mapele, nk.
7. SUMU KWENYE CHAKULA ILETWAYO NA VIMELEA; hii kisayansi haikuelezewa vizuri lakini utafiti umeonyesha kuwa penye mlipuko wa (food poisoning) mende wakiuwana mende (kuondolewa) food poisoning nayo huisha
8. Athma; wagonjwa wa athma wanashambuliwa na athma mara nyingi zaidi kwenye nyumba zenye mende. Na wakati mwingine huhatarisha uhai wa watu hawa. Watu wenye athma wakinusa vileta aleji vya mende hupelekea kushambuliwa na athma.
9. Uharibifu wa vifaa vya dhamani; hungia kwenye vifaa vya dhamani k**a redio, saa computer nk na kuweza kuleta uharibifu mkubwa wenye dhamani ya ma- laki ama mamilioni ya fedha
10. Ongezea ………

10/10/2016

Wapendwa naomba leo tujadili madhara ya Mende; Wewe unavyofahamu Mende ana Madhara gani? (madhara yoyoyte yale)

09/07/2016

THE IMPORTANCE OF MOSQUITOES CONTROL.
"Mosquitoes are the most dangerous organism in the world" it transmits diseases which kills millions of people worldwide annually.
Look at these statistics;
Mosquitoes transmit disease to over 700 millions people per year
The following diseases are transmitted by mosquitoes.
1. Malaria; every year 515 million people gets infected and 1 to 3 Million people mostly children dies!
2. Yellow fever; Annual infections approximated to be 200,000 and 30,000 death
3. Filariasis; there are 120 million people currently infected.
4. Encephalitis this disease is characterized with headache, fever, sensitivity to lights, weakness and seizure.
Deaths are common.
5. Epidemic Poly arthritis
More than 400 people are infected annually.
In developed countries deaths caused by mosquitoes transmitted diseases are very few in some countries no mosquitoes at all! Many of the countries eliminated mosquitoes using fumigation.

Control of mosquitoes;
There are many ways of controlling mosquitoes; but personally I recommend and emphasis on fumigation. Fumigation kills all mosquitoes species hence eliminates those minute deadly bites of mosquitoes.

Reference; www.gatesnotes.com

Please visit our websites; www.jalicoltd.blogspot.com

09/07/2016

Why you must control Mosquitoes?
"Mosquitoes are the most dangerous organism in the world" it transmits diseases which kills millions of people worldwide annually.
Look at these statistics;
Mosquitoes transmit disease to over 700 millions people per year
The following diseases are transmitted by mosquitoes.
1. Malaria; every year 515 million people gets infected and 1 to 3 Million people mostly children dies!
2. Yellow fever; Annual infections approximated to be 200,000 and 30,000 death
3. Filariasis; there are 120 million people currently infected. Affects lower extremities including genitalia. Mostly in Asia, Africa, central America, South America
4. Encephalitis this disease is characterized with headache, fever, sensitivity to lights, weakness and seizure.
Deaths are common.
5. Epidemic Poly arthritis
More than 400 people are infected annually.
in developed countries deaths caused by mosquitoes transmitted diseases are very few in some countries no mosquitoes at all!
Control of mosquitoes;
There are many ways of controlling mosquitoes; but personally I recommend and emphasis on fumigation. Fumigation kills all mosquitoes species hence eliminates the minute deadly bites of mosquitoes. For your fumigation and mosquito control needs please visit our website; www.jalicoltd.blogspot.com like our page Jali Company Limited. Instagram jalicoltd

03/08/2014

Address

P. O. Box 62228, Kinondoni Mkwajuni
Dar Es Salaam
P.O.BOX62228,DARESSALAAM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jali Company Limited posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Jali Company Limited:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram