04/04/2025
🏞ELIMU YA UTAMBUZI 🏔🎠SEHEMU YA PILI
IJUE NGUVU YAKO YA ASILI
Katika ELIMU ya nguvu iliyopo ndani kiasili ,huwa imejificha sana lakini pia huonekana kwa watambuzi,
TAMBUA
Kila kiumbe kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu kina ujuzi wa kipekee na utambuzi wa elimu kabla ya kufundishwa au kujijua zaidi basi anauwezo wa kujua vitu vingi, kusikia mbali, kujua matukio yajayo na ya sasa hata yaliyopita
Mfano halisi upo katika viumbe wote ila nitazungumzia mwanaadamu yaani bin adam (uzao uliotokana na NABII wa kwanza ADAM) ndie muwakilishi wetu
MTOTO
Kabla ya kuzaliwa mtoto ikiwa anajulikana kuwa kuna kiumbe kinakuja(mama akiwa mjamzito) taarifa zitawafikia wengi hata usiposema basi nuru ya uwepo wa mtoto huyo hujulikana kabla ya kusema au kujua
Hapa ndipo utapata kuona wazazi au watu wanaotuzunguka kumjua mtu ni mjamzito kabla hata yeye mwenyewe hajajua
Je, ni kwanini.?
Ni kutokana na nguvu ya kiumbe hicho inajionesha kabla ya ujio wake, hata mnyama au mdudu atajua kuwa kuna kiumbe anakuja na ndio maana, mjamzito hupata ishara mbalimbali za kusikia kitu,kuhisi, kutembelewa na viumbe tofauti watakao onesha ujio wa mtoto k**a chura,nyoka,mjusi,paka,mbwa nakadhalika(n.k)
Pia hata hali ya hewa inaweza kubadilika k**a upepo mkali au tulivu,mvua, radi,jua kali ,joto,baridi n.k,
MZAZI ukiwa makini basi utaitambua nguvu ya mtoto wako mapema sana na kumfanya awe na nguvu kwa makuzi ,maadili, malezi na mienendo mizuri kwa kufuata asili yake pindi utakapo ijua nguvu yake utapata kuijua kinga yake mapema kabla ya kuzaliwa kwake ,WAZAZI wote wanahitajika kuelewa hili ili wapate kuikomboa nguvu ya mtoto kabla ya muongozo wake kudhibitiwa kwani muongozo ndio unao itumia nguvu, na nguvu hiyo ni msaada kwa wengi waliopotea au kupoteza,
Niwaeleweshe kidogo, muongozo uliokuwa nao ndio unaoweza kuitumia nguvu na kukufanya wewe ujijue na uweze kufanya kitu ,na ndio maana nilitoa elimu ya kuwa nyota haichukuliwi wala kuibiwa ila inadhibitiwa na kupotezewa muelekeo kwa maana ya muongozo