20/03/2025
UGONJWA WA RUBELA
Ugonjwa wa rubella unaojulikana pia k**a surua ya ujerumani ‘’German measles’’ ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi. Ugonjwa huu umekua adimu sana siku hizi kwa sababu ya chanjo inayotolewa kukinga ugonjwa huu utotoni. Kwa kawaida husababisha upele mwekundu unaosambaa usoni na kisha kuenea mwili mzima.
Mara nyingi ugonjwa huu hausababishi dalili yoyote. Mtoto anaweza kuanza kupata homa ya kawaida, kuvimba kwa tezi na kutokwa na mak**asi siku 2 – 3 baada ya kuambukizwa. Watu wazima wanaweza kupata maumivu ya kichwa na maumivu ya viungo.
Tatizo kubwa zaidi linaloweza kusababishwa na ugonjwa wa huu ni kwa mama mjamzito. Ugonjwa huu unaweza kuleta athari mbaya kwa mtoto aliye tumboni, hasa akiambukizwa katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito.
JIFUNZE ZAIDI HAPA 👉
https://wikielimu.org/ugonjwa-wa-rubella-surua-ya-ujerumani/