AFYA BILA Mipaka

AFYA BILA Mipaka Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from AFYA BILA Mipaka, Health & Wellness Website, Dar es Salaam.

tunatoka huduma ya kutibu maradhi mbalimbali yanayosumbua jamii yakiweni na maradhi sugu kama kisukari, matatizo ya uzazi, presha, vidonda vya tumbo mifupa na misuli,maradhi ya watoto na mengine mengi.

VIDONDA VYA TUMBO(PEPTIC ULCERS),VIDONDA VYA TUMBOHivi ni vidonda ambavyo vinapatikana kwenye kuta za tumbo (stomach) na...
12/06/2025

VIDONDA VYA TUMBO(PEPTIC ULCERS),

VIDONDA VYA TUMBO
Hivi ni vidonda ambavyo vinapatikana kwenye kuta za tumbo (stomach) na utumbo mwembamba (duodenum).

▪️FAIDA
_Kwenye kuta za tumbo kunazalishwa utando mzito wa k**asi (protective mucous coating) kwaajili ya kulilinda tumbo na utumbo mwembamba. Pia huzalishwa asidi (Hydrochloric acid) kwaajili ya kusaidia kumeng'enywa chakula na kuua vijidudu (bacteria) wanaongia tumboni kupitia chakula, maji au kugusana midomo kati ya m/Maambukizi na mzima mfano kissing ._

SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo husababishwa na sababu kuu mbili.:

1.▶️ Maambukizi ya bacteria (Helicobacter Pylori i.e H.Pylori infections)

H.pylori mara baada ya kuingia tumboni hudhoofisha ute mzito wa k**asi ndani ya tumbo na utumbo mwembamba, hivyo huruhusu asidi kupenya na kuingia ndani zaidi ya kuta za tumbo. Asidi na bacteria husababisha maumivu na kidonda kwenye kuta za tumbo na utumbo mwembamba. Umbile la mnyongoroto la huyu bacteria pia huchangia kuchimba zaidi kuta za tumbo na utumbo mwembamba.
_FAIDA_
Nilisema ndani ya tumbo kunazalishwa asidi kwaajili ya kuua vijidudu (bacteria).
_*Swali*_: Kwanini bacteria huyu hauliwi(hadhuriki) na hiyo asidi?.
_*Jibu*_: H.pylori anaweza kuishi tumboni bila kuuliwa na hiyo asidi kwasababu anajizalishia kemikali (enzymes) iitwayo *UREASE ENZYMES*, ambayo inabadili urea kuwa ammonia (basic compound) ambayo inapambana na asidi (neutralization) na kufanya mazingira yawe ya kawaida kwake.

2.▶️ Matumizi ya muda mrefu madawa ya kuondosha maumivu (Nonsteroidal anti-inflammatory drugs i.e NSAIDS)
Ndani ya tumbo na utumbo mwembamba kunazalishwa kemikali iitwayo *Cyclo -oxygenase (COX-1)* isoenzymes inayobadili asidi iitwayo *arachidonic acid* kuwa kemikali iitwayo *prostaglandins*. Hii prostaglandin huupa ukuta wa tumbo na utumbo mwembamba ulinzi. Madawa haya ya kuondosha maumivu mfano Aspirin,Ibuprofen Diclofenac n.k yanapotumika kwa muda mrefu huleta madhara ya kuzuia kuzalishwa kwa COX-1 ambapo husababisha prostaglandin iwe finyu tumboni mwishowe kuta za tumbo hupata michubuko na vidonda vya tumbo hutokea.

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO⤵️
1.🧷 Kupata maumivu ya tumbo ya kuwaka moto (kuunguza) baada na kabla ya kula
2.🧷 Kupatwa na kiungulia(heartburn) karibu na chembe ya moyo
3.🧷 Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa
4🧷 Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu
5.🧷 Kupata haja kubwa ya rangi ya kahawia au nyeusi cheenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu
6.🧷 Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
7.🧷 Kushindwa kupumua vizuri.
8.🧷Kuharisha hasa unapokula vyakula vinavyochochea vidonda vya TUMBO.
9.🧷Kupata choo kigumu k**a cha mbuzi
10.🧷 Maumivu ya mgongo
11.🧷 Tumbo kuwaka moto.
12.🧷 Kupungukiwa damu na kupelekea kupata kizunguzungu.
13.🧷 Mwili kudhoofika na kupungukiwa kilo
14.🧷 Dhakari(Uume) kulegea/kusinyaa na kushindwa kuhimili tendo la ndoa.
15.🧷Mapigo ya moyo kwenda mbio.
16.🧷 Macho kupunguza nguvu ya

VICHOCHEZI VYA TATIZO
Unaweza kuongeza ukubwa wa tatizo la vidonda vya tumbo au kuchelewa kupona hata K**a unatumia dawa ikiwa utafanya yafuatayo:

1. 🧷Uvutaji sigara (smoking)
2.🧷Unywaji wa pombe (alcohol drinking)
3.🧷 Kuwa na msongo wa mawazo kupitiliza (untreated stress)
4.🧷Kula vyakula vyenye viungo vingi
5.🧷 Kunywa kahawa
6.🧷Kula vyakula vyenye kuleta gesi.
7.🧷Kula vyakula vyenye asidi mfano jamii ya ndimu au nyanya.
8.🧷 Kula kupita kiasi
9.🧷 Kutokua na ratiba maalum ya kula mfano kukaa na njaa kwa muda mrefu n.k
_Itambulike hizi sio visababishi vya vidonda bali huchochea vidonda kutopona na kuchimbika zaidi._

DALILI HATARISHI ZA VIDONDA VYA TUMBO (COMPLICATIONS)

Vidonda vya tumbo vikiiachwa bila kutibiwa kwa muda mrefu au mgonjwa akijiweka kwenye vichochezi, hujiweka kwenye dalili hatarishi k**a zifuatazo:
1.◾ Damu kuvujia ndani ya tumbo (internal bleeding)
2.◾ Kupatikana tundu ndani ya tumbo au utumbo mwembamba(percolation)
3.◾ Kuziba kwa njia ya chakula kitokacho tumboni kwenda kwenye utumbo mwembamba(obstruction).
4.◾ Kupata saratani ya tumbo(gastric cancer)
5.◾ Kupoteza maisha(death)

TIBA ZA VIDONDA VYA TUMBO
Tunatoa tiba sahihi na salama kabisa ya Vidonda vya tumbo ambazo zimeshafanyiwa vipimo na zipo kisheria zimethibitishwa na taasisi kubwa za kiafya duniani pamoja na tanzania.

Muhimu.

⚫ Ni vyema kutambua kuwa dalili hizi pia zinaweza kusababishwa na magonjwa mengine, na kwamba uwepo wa moja au zaidi ya dalili hizi haimaanishi kwamba mtu ana tatizo la vidonda vya tumbo. Ikiwa una wasiwasi kuhusu dalili yoyote, ni muhimu kwenda hospital kwanza kufanya vipimo kujua tatizo ni nini hasaa kabla ya kutumia dawa.

+25564699353
+255745680156

DR MSUYA HERBAL CLINIC
-----------------------------------------------------------

*SABABU KUU ZA MAUMIVU YA MIFUPA, MGONGO, KIUNO, MAGOTI, SHINGO, MIGUU KUVIMBA NA KUWAKA MOTO.*Sababu zipo nyingi lakini...
03/06/2025

*SABABU KUU ZA MAUMIVU YA MIFUPA, MGONGO, KIUNO, MAGOTI, SHINGO, MIGUU KUVIMBA NA KUWAKA MOTO.*

Sababu zipo nyingi lakini hizi ni sababu kuu 👇👇;
*1.Kuwa na infection (mashambulizi ya bakteria na virusi) kwa mfano virusi vya influenza, hepatitis.*

*2. Kuwa na uzito mkubwa kwa sababu ya mafuta mengi mwilini.* Watu wenye uzito mkubwa husababisha kuwa na uvimbe kwenye viungio kitaalamu hutambulika k**a inflamation.

*3.Mfumo wa kinga mwilini (autoimmune diseases) kushambulia maeneo ya viungo na kupelekea inflamation ama kuuwa seli.*
*4.Kukusanyika kwa asidi ya uric kwenye viungo (uric acid) mara nyingi hii huathiri miguu na utahisi k**a miguu inawaka moto.* Kutokunywa maji kwa wingi kunaweza kuwa moja ya sababu ya hambo hili.
*5. Watu wengine walio hatarini ni wenye kunywa pombe, wenye maradhi ya Figo, wenye shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda), marahi ya ini kisukari na shida kwenye tezi ya thyroid.*
6. Ongezeko kubwa la uric acid Mwilini.

*7. Kulainika na kuvunjika kwa mfupa laini (cartilage) kwenye magoti.*

8. Upungufu wa *kilainisho cha maungio (synovial fluid)* maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo.

9. Ugonjwa huu husababishwa na kuharibika kwa gwegwedu. *Kuvimba kwa viungo kunaweza kusababishwa na mfumo wa kinga kushambulia tishu za mwili kimakosa na kuziharibu hasa uti wa mgongo.*
10. Kuwa na majeraha
*11.Kufanya kazi ngumu kwa muda mrefu.*
*12. Kukosa muda WA mazoezi ama kukaa Sana Kwa muda mrefu (siku nyingi).*
13. Kuwa na saratani
*14. Kumung’unyika na kuvunjika kwa mifupa kutokana na ugonjwa unaojulikana k**a osteoporosis.*
15. Udhaifu wa mifupa na matege kwa sababu ya ukosefu wa madini muhimu kwenye mifupa. *Madini k**a vile Zinc, Calcium, Manganese, Magnesium, Phosphorus na Iodine.*

*Kuhusu tiba 👇👇👇;*

0694699353

Kunywa maji asubuhi mara tu baada ya kuamka kuna faida nyingi kwa afya. Hizi ni baadhi ya faida kuu:1. Huamsha mfumo wa ...
24/04/2025

Kunywa maji asubuhi mara tu baada ya kuamka kuna faida nyingi kwa afya. Hizi ni baadhi ya faida kuu:

1. Huamsha mfumo wa mmeng'enyo – Maji huanza kusafisha tumbo na kuamsha mfumo wa mmeng'enyo wa chakula, hivyo kusaidia usagaji bora wa chakula siku nzima.

2. Husaidia kuondoa sumu mwilini – Maji husafisha figo na kusaidia kuondoa sumu zilizokusanyika usiku wakati wa usingizi.

3. Huongeza nishati – Mwili unapoanza siku ukiwa na maji ya kutosha, huongeza nguvu na kuboresha utendaji wa mwili na akili.

4. Huboresha afya ya ngozi – Unywaji wa maji asubuhi huisaidia ngozi kuwa na unyevu na kung'aa, pamoja na kupunguza chunusi au matatizo ya ngozi.

5. Huongeza mfumo wa kinga – Maji safi yanasaidia seli kufanya kazi kwa ufanisi, hivyo kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa.

6. Huzuia kuvimbiwa – Kunywa maji kabla ya kula chochote husaidia kulainisha utumbo na kuzuia matatizo ya choo kigumu.

Unapokunywa maji asubuhi, ni bora kunywa glasi 1-2 za maji ya uvuguvugu kabla ya kula chochote.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 07:00 - 17:00
Tuesday 07:00 - 17:00
Wednesday 07:00 - 17:00
Thursday 07:00 - 17:00
Friday 07:00 - 17:00
Saturday 07:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA BILA Mipaka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram