Dakika Tisini

Dakika Tisini h

K**a ni kweli… basi soka la Africa bado lina maswali mengi kuliko majibu!Leo tumeshuhudia mchezaji wa zamani wa Yanga, J...
03/10/2025

K**a ni kweli… basi soka la Africa bado lina maswali mengi kuliko majibu!

Leo tumeshuhudia mchezaji wa zamani wa Yanga, Jesus Moloko, akiomba jezi na hata kupewa pesa na Fiston Mayele, aliyewahi kung’aa naye pale Jangwani na sasa anakipiga Pyramid.

👉 Swali gumu: Hivi wachezaji wanaoimba na kupigiwa makofi makubwa pale Taifa leo tunawapa thanani kubwa ila baadae wanasahaulika kiasi hiki?

Je, hii ni ishara kwamba:

1. Klabu haziwalipi vizuri wachezaji wake k**a tunavyosikia? 🤔

2. Au ni kwamba wachezaji wenyewe hawana mpango wa maisha baada ya soka?

Kwa macho ya wengi, kitendo cha Mayele kumpa Moloko jezi na pesa kinaonekana cha utu na urafiki… lakini kwa macho ya wachache, ni aibu kubwa kwa klabu kubwa k**a Yanga na mchezaji mwenyewe kufikia hatua ya kuomba msaada hadharani. 😬

⚽ Sasa nauliza nyie mashabiki:

Ni heshima kwa Mayele kumpa msaada mwenzake hadharani tena mbele ya kamera?

Au ni doa linaloonyesha namna mfumo wa soka la Afrika Mashariki ulivyo dhaifu kwa wachezaji wake?

HIVI ADHABU HIZI ZINA MAANA KWELI AU NI MAIGIZO TU?Waamuzi wa mechi za JKT Tanzania vs Azam na Mbeya City vs Yanga wamef...
03/10/2025

HIVI ADHABU HIZI ZINA MAANA KWELI AU NI MAIGIZO TU?

Waamuzi wa mechi za JKT Tanzania vs Azam na Mbeya City vs Yanga wamefungiwa kuchezesha zaidi ya mechi tatu, na mchezaji wa Yanga Ibrahim Bacca naye ameingia kwenye kifungo.

Lakini hebu tujiulize:
- Mechi zikiharibiwa na waamuzi, je adhabu pekee ni kuwapa adhabu ya kuwafungia michezo michache?
-Timu zilizoumizwa na maamuzi mabovu zinapata nini? Haki yao iko wapi?
👉 Na kwanini kila mara kinachoadhibiwa ni mtu mmoja mmoja lakini sio mfumo mzima uliooza unabaki pale pale?

Inaonekana TFF inapenda zaidi kuua mjadala badala ya kushughulikia kiini cha tatizo. Mashabiki tunaachwa tukibishana mitandaoni ilhali uwanjani mambo yale yale yanaendelea.

Sasa swali kwenu mashabiki:
Je, hizi adhabu ni hatua za kweli za kurekebisha soka letu… au ni maigizo tu ya kutuliza hasira za mashabiki?

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dakika Tisini posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram