18/09/2025
*TOFAUTI KATI YA KUONGEA NA KULALAMIKA*
🍃🏓▫️Kuna tofauti nyingi kati ya kuongea na kulalamika, ila naomba nifafanue mbili kubwa ambazo ukizingalia utajua k**a unaongea au unalalamika?
🍃🏓▫️(1) Unalalamika ukiwa na hasira, ukiwa umenuna, ukia umeudhiwa. Mtu anapokufanyia kitu, ukaongea wakati anakufanyia basi unakua unalalamika.
🍃🏓▫️Kwa mfano, mume wako amechelewa kurudi, una hasira umenuna, ukaanza kumuambia kwanini unaruidi saa anane, basi hapo utakua unalalamika.
🍃🏓▫️Lakini kuongea ni toafuti, unasubiri akili imepoa, huna hasira, kitu kilitokea jana au siku mbili nyuma, kichwa kimetulia, umepanga maneno kisha unamuambia kuwa siku hizi unachelewa sana, nini tatizo, anakaumbia wote mkiwa mmetulia, iwe ni uongo au kweli lakini kichwa chako kimetulia na chake kimetulia.
🍃🏓▫️(2) Kulalamika ni kurudia kitu kile kile kila siku.
🍃🏓▫️Inaweza kua hajakosea, lakini mtu anafanya kitu kile kile kila siku, na wewe unaongea kitu kilekile kila siku, hapo unalalamika.
🍃🏓▫️Mwenza wako ni mtu mzima, k**a umemuambia kitu mara moja au mbili basi kuna mawaili, moja ndiyo alivyo huwezi kumbadilisha na pili inawezekana anafanya makusudi ataacha akiamua.
🍃🏓▫️Kumuambia mtu kitu kile kile kila siku haisaidii yeye kukiacha kile kitu zaidi unakua unalalamika.
🍃🏓▫️Sasa kuongea hapa ni kumuambia mtu kitu mara moja, akirudia utamuamba tena na akirudia tena unanyamaza kwani ndivyo alivyo hata utembee uchi au uongee mishipa ya uso ipasuke hataacha au anakufanyia tu makusudi ili kukukomoa.
🍃🏓▫️ Mtu anayekufanyia makusudi ni k**a soda, ya koka, jinsi unavozidi kuitingisha ndivyo inazidi kutoa mapovu, hataacha mpaka nawe uache kuongea, atajiona k**a huudhiki basi ataacha asipoacha basi unapotezea maisha yanaenda.