26/02/2026
Mambo haya Bwana!
Jana usiku nilimdanganya mke wangu nikamwambia naenda kununua vocha. Badala yake nikapitia kwa mama mmoja jirani yangu, ambaye mume wake huwa anachelewa sana kurudi.
Nilipoingia tu, Mwenyeji wangu akanipitilizisha Chumbani ili akanipe nilichofuata, maana tulishakuwa tumeyajenga kwenye SMS. Ile nimeingia Chumbani hata hatujakaa sana, ghafla tukasikia sauti ya pikipiki ya mume wake ikipaki nje ya nyumba. Inaonekana leo karudi mapema. Nikaingiwa na hofu, nikajikuta mwili wote unatetemeka, k**a nataka kukojoa, iliyochanganyika na tumbo la kuhara fulani hivi. Mwenyeji wangu akawaza haraka akanyanyua kitanda, na mimi nikajua kinachofuata ni kutumbukia haraka chini ya kitanda.
Baba mwenyenyumba alivyoingia ndani akamwambia mkewe aende dukani (centre) akachukue chakula cha kuku alichonunua asubuhi, maana alikuwa amesahau. Mkewe akatoka haraka, Lakini Mara tu mke wake alipotoka, nikamsikia mzee akipiga simu mtu fulani, anamwambia aje haraka kabla mkewe hajarudi.
Nikiwa bado nimejificha chini ya kitanda, nikasikia sauti ya mwanamke mwingine akiingia, wanacheka cheka. Yule mke wake alikuwa hajafika mbali sana dukani, Nikamsikia nje akimwita mumewe na kumwambia karudi kufuata hela ya mchezo, ameona arudi aje aichukue ili apitishe kabisa na huo mchango wa kikoba.
Ile kusikia Sauti ya Mke wake Nje, Yule Baba akamshauri yule mwanamke aliyekuwa naye ndani atimbe chini ya uvungu wa kitanda. Alipoingia uvunguni, akanikanyaga nikamuonesha alama ya kidole ya Shii, 😭 Enhee kumuangalia vizuri Enhee ni Mke wangu! Tumejikuta wote uvunguni mwa kitanda kimoja cha mtu mwingine.
Yule mwanaume akaanza kumfokea mkewe kwanini Amerudi si angeenda tu huku akisogeza kanga ya yule mwanamke wa uvunguni kwa mguu wake, maana ilikuwa imebaki nje ya Uvungu.
Ungekuwa wewe ndiyo sisi Ungefanyaje?