Kazini hadi Kustaafu KAZI

Kazini hadi Kustaafu KAZI 0685444006

Wastaafu wanajisifia hapo eti hustle zao hazikurekodiwa na media wala kufuatiliwa na wadaku, mitandao haikuwepo enzi hiz...
26/10/2025

Wastaafu wanajisifia hapo eti hustle zao hazikurekodiwa na media wala kufuatiliwa na wadaku, mitandao haikuwepo enzi hizo🤣
Hebu toa mawazo yako rafiki...💃

KUPENDA NI UPOFU-Part 2Abbi aliendelea kushuka kimaisha. Kwa kila jambo alimpa kipaumbele John akawa mtumwa kwake. Hafan...
22/10/2025

KUPENDA NI UPOFU-Part 2
Abbi aliendelea kushuka kimaisha. Kwa kila jambo alimpa kipaumbele John akawa mtumwa kwake. Hafanyi jambo hadi John amshauri. Ndoa ikaendelea kusubiri kuondolewa vipingamizi hivi na vile kutoka kwa John. Maisha ya sogea tukae yakaendelea kati ya hawa wawili. Hayawi hayawi mwisho huwa. Tetesi zikaanza kusikika John anao mchepuko Maria. Hutumia pesa na mali za Abbi kumhonga huyo mchepuko. Siku isiyo na jina John na Maria walipata ajali ya gari. Walinusurika lakini gari la Abbi lilikuwa hoi....matengenezo yenye gharama yalihitajika. Kufupisha habari ni kuwa, Abbi alikuja kunilalamikia kuwa, John alimtia hasara nyingi kimaisha. Kimwili: Alimuibia vitu vingi sana k**a vitenge, vitambaa nk vilivyokuwa vipya. Abbi alikuwa na tabia ya kununua vitu na kuhifadhi kabatini kwa nyakati zijazo. John aliuza mchanga, kokoto na matofali viĺivyokuwa vikisubiri ujenzi ambao uĺikawia😪gharama ya kutengeneza gari ilikuwa kubwa mno....
Kinafsi na kiroho: Abbi alijeruhika vikubwa...alipata depression,alishuka kiimani hata kutohudhuria nyumba ya ibada kikamilifu, alipoteza marafiki wengi nk. Kumbe John kazi yake ni mission town...hana fani yoyote khaaaa😭
Nilimshauri Abbi aanze upya. John alihamia kwa Maria na kuendeleza narcissism yake...
Mimi huweka pakti ya tissues mezani pangu. Siku hiyo nusura ziishe🤣Abbi alilia na kuomboleza!!!
Alisema kila kitu...inasikitisha.
Wanawake acheni kulialia na mjitafakari. Sogea tukae ni ndoa halisi au mnatafuta balaa?
Niwaulize swali. Ukila mtaji wa biashara, una biashara tena?
Kuishi sogea tukae kutamhamasisha mpenzi akuoe? Ikiwa mtu anapata maziwa ya ng'ombe bure atahitaji kufuga ng'ombe wa nini tena?
Ndoa za dini, za serikali, za kimila ni ndoa zinazotambulika. Sogea tukae ipo kwenye kundi gani?
Mimi ni Mama Mstaafu kukupa nasaha ni wajibu wangu. Tafadhali wanawake JIPENDENI NA KUJITHAMINI. Msikubali kutumiwa.
Mapenzi si kitu kimoja tu....ni mchanganyiko wa mambo mengi. Kwenda picnic, kusoma kitabu pamoja maktaba, kulima bustani pamoja, kuhudhuria midahalo pamoja, kufanya majukumu ya jamii pamoja nk....yote haya ni mapenzi au kuwa pamoja na kufahamiana zaidi. Ati binti anathubutu kusema " Aliniambia nimzalie ili anioe, nilipopata ujauzito tu akaniacha kaoa mwingine. " Mie huchukia maneno yanayofanana na haya...kwa nini uzae ndipo uolewe?
Viongozi wa dini mko wapi watu wanawake wanaangamia huku...njooni upesi tuwasaidie huku.
Taarifa ya mwisho, Abbi alijifungua mtoto. Baba wa mtoto ni John, alikataa kujihusisha na chochote kuhusu mtoto huyo. Watoto ni baraka itokayo kwa Mungu, wasihusishwe na skendo zozote.
Ndoto za Abbi zote zilikufa, ataanza upya pale alipoishia, wakati ukiwadia. Hizo ndio kazi za narcissists. Tena ni wengi mno. Kila la kheri marafiki. Baadae✍️

KUPENDA NI UPOFU....Part 1      Hi. Abigail alikuja kuniona k**a tulivyopatana. Mimi humwita Abbi kifupi. Nilishangaa ku...
15/10/2025

KUPENDA NI UPOFU....Part 1
Hi. Abigail alikuja kuniona k**a tulivyopatana. Mimi humwita Abbi kifupi. Nilishangaa kumuona amechujika usoni tena utanashati wake ulipungua. Hakuwa Abbi yule niliyemzoea.
Alinieleza kisa chake kilichomleta kwangu. Alikuwa na mchumba (au mpenzi), aliyemtesa kihisia na kiroho pia. Kiufupi, huyo John alitengana na mke sogea tukae. Alimlaghai Abbi kuwa angemuoa. Ahadi zilizidi bila kutekelezeka. Mwishowe walianza kuishi pamoja sogea tukae. Kanisa liliingilia kati, kuwa wafunge ndoa. John alitoa story nyiiiingi....mara ohh ex wangu anatishia kunishtaki maana nimeishi nae miaka 15....mara ohh tusubiri kidogo nipate pesa ninazozidai kutoka kampuni fulani milioni 50....visingizio viliongezeka siku hadi siku.
Abbi alikuwa na maisha ya kuridhisha. Alikuwa na kiwanja na msingi wa nyumba aliouanza. Aliishi kwenye apartment na alikopeshwa gari ofisini kwake ili afike mapema kazini. Changamoto za usafiri wa umma hazikumsumbua.
Abbi alianza kushuka kimaisha bila yeye kujijua, baada ya kukutana na John. Siku nyingine alipelekwa kazini asubuhi na kurudishwa jioni na John. Gari ilianza kuchangiwa, leo anayo Abbi kesho John. Hakuna tatizo, mapenzi yakinoga ndio hivyo.
Abbi akaanza kushinda ndani kila wikendi, hata kanisani Jumapili ikawa taabu kuhudhuria. Kiwanjani kwake hakupaendeleza tena, fundi akawa akimfuatilia nyumbani bila kufanikiwa.
Maongezi ya Abbi yakajaa John tu....mara ohh yule dada hajiheshimu, akimuona John anajirahisi.....ohh nikampikie snacks za wiki John nk. Kiufupi, Abbi niliyemfahamu miaka mingi alikuwa tofauti na huyu aliyekuja kuniona siku hiyo....
Kulikoni? Nifuate part 2 ujue visa na mikasa iliyompata dada Abbi. Nimekumbuka habari ya Abbi baada ya Olivia Erastus Andrew kutoa post ya narcissist....John alikuwa narcissist. Abbi alikuwa kipofu wa mapenzi, aliathirika. Wanaokuwa kwenye mahusiano na narcissists huharibikiwa kimaisha....
Tuwe makini. Baadae kidogo.✍️

13/10/2025

Leo Mstaafu sina hamu ya kula wala kunywa na siumwi. Unanishauri nifanyeje mpendwa🤔

10/10/2025

Nilitamani dawa za kisukari hizi zitolewe bure hapa Tz....leo mgombea Urais mmojawapo ameahidi ikiwa atachaguliwa atafanya hivyo, si kwa kisukari tu, bali pia kwa cancer, figo na moyo. Wastaafu shout out hurray...

Habari....mstaafu zingatia haya mambo 7 tafadhali kwa ustawi wako.....nawe ambae bado upo kazini jambo lako nakuletea pu...
10/10/2025

Habari....mstaafu zingatia haya mambo 7 tafadhali kwa ustawi wako.....nawe ambae bado upo kazini jambo lako nakuletea punde tu....💃

MAMBO 7 HATARI KWA MAISHA YA USTAAFU
Habari za leo. Nimekuta hii habari Google nimeona niilete hapa, ili tuisome na kutoa mawazo yetu. Maisha ya ustaafu yapaswa kuwa bora zaidi, kwani unakuwa bosi wako mwenyewe 😂...basi uhondo wa ngoma usikunogee sana ukaharibu stepu za uchezaji🙆‍♀️
1. USIKUMBATIE MAMBO YA ZAMANI.
Ustaafu ni wakati wa kufurahia matunda ya kazi ya myaka iliyopita, wastaafu wengi hawafurahii kwa kukumbuka jana yao. Ni asili ya binadamu kuangalia jana. Jana yenye mafanikio, yenye ukuu, yenye kupendeza au kuchukiza na mengineyo. Iwapo jana hiyo tutaiwaza mara kwa mara, itatunyima kuangalia leo yetu tunayoiishi, ni hatari🤔. Inaweza kusababisha ushindwe kujaribu mambo mapya au kukutana na watu wapya. Acha tabia hii. Kumbatia siku uliyo nayo zaidi na karibisha fursa zote za siku hiyo kujifunza, jana na kesho zitajishughulikia zenyewe.
2. KUPUUZIA AFYA
Ni rahisi kupuuzia afya unapostaafu. Mhemko wa kustaafu, kutaka kila kitu ufanye, kutokuwa na ratiba ya mambo yako kwa masaa 12 ya mchana ni hatari kwa afya. Mwandishi anasema alikuwa anaangalia tv hadi masaa ya alfajiri🙄 akisikia njaa anakula vitafunwa akiwa kwenye tv duh....afya yake ilipozorota alijirudi na kuanza kulala masaa sahihi na kufuata sheria nyingine za afya. Tujiwekee ratiba sahihi ili tusitetereke kiafya.
3. KUJIEPUSHA NA JAMII
Wengi tunafikiri kujiondoa kwenye shughuli za jamii ni kupata muda wa kupumzika. Kujitenga ssna ni kukaribisha upweke. Tuwe na kiasi tuweke uwiano. Watafiti wanasema upweke ni hatari kwa afya, kwamba athari zake ni sawa na mtu aliyevuta sigara 15 kwa siku😯. Upweke unaambatanishwa na magonjwa ya moyo, kiharusi na hata kusababisha vifo vya ghafla. Ustaafu ni wakati unaofaa kufahamiana na wengine, kujiunga na clubs, kuanzisha hobby, kujitolea kwenye jamii, kufanya kazi part time nk...yote hayo yanawezekana kwa kiasi.
4. KUKATAA MABADILIKO
Ustaafu ni mabadiliko makubwa kimsisha, ni sawa kujisikia kukosa uhakika, lakini si sahihi kukataa kubadilika na kujaribu fursa ambazo zipo mbele yako. Kuwa na mawazo chanya na ubadilike kwa mazuri ili ukue upya katika phase hii ya ustaafu.
5.KUTUNZA VINYONGO
Maisha ni milima na mabonde, vikwazo na suluhu, mwisho wa siku kila mmoja wetu kabeba vinyongo.
Kuvikumbatia vinyongo ni hatari kwa mioyo yetu. Anza maisha ya ustaafu kwa kuamua kuvitupilia mbali....usimchukie mtu yeyote, usikumbuke mabaya...fanya ibada zaidi, samehe na sahau kwa ajili yako mwenyewe. Umri wako sasa ni wa kuishi kwa furaha na amani kuliko chochote, jifikirie wewe kwanza.
6.KUDHARAU VIPAUMBELE VYAKO
Hili ni kosa, usiache vipendaroho vyako eti kwa vile umestaafu ni maisha mapya...usiache uchoraji wako, kupiga piano kwako, kucheza ngoma, kuimba nk...furaha yako ni hivyo, viendeleze ukichanganya na vipya...wahenga walisema usiache mbachao kwa msala upitao, vipendaroho vya zamani visiachwe.
7.KUWAZA UCHUMI KUPITILIZA.
Ni kweli umestaafu kipato chako kitapungua. Sasa utaweka pesa zaidi kuliko kuzipokea. Utaogopa na kuingiwa na mashaka. Usiondoe amani yako kwa kuwaza sana utakaribisha magonjwa. Kuwa na kiasi, tumia hekima katika pesa zako matumizi yasizidi kipato unachopata wakati huu. Epuka matumizi yasiyo na tija. Kabla ya kununua kitu jiulize ukikikosa kitakuathiri?
Hisani:geediting.com, Google

Mama mstaafu mchana wa leo nilitoka kihivi kwa chakula. Nilishapunguza mafuta, chumvi na sukari. Napendelea vya kupwaza ...
09/10/2025

Mama mstaafu mchana wa leo nilitoka kihivi kwa chakula. Nilishapunguza mafuta, chumvi na sukari. Napendelea vya kupwaza na chukuchuku. Kupanga ni kuchagua. Karibu😋

MAWASILIANO KIGANJANI... Nimeshasahau tulivyokuwa tukiwasiliana zamani...simu za mezani kunyonga hendeli na mtu posta ku...
20/09/2025

MAWASILIANO KIGANJANI...
Nimeshasahau tulivyokuwa tukiwasiliana zamani...simu za mezani kunyonga hendeli na mtu posta kupokea kwa maneno mawili tu NUMBER PLEASE...
Kisha zikaja simu za mezani zenye namba kuanzia 1 hadi 9 then 0. Wazazi waliweka kufuli maana bill zilikuwa kubwa wakati wa likizo kupeana michapo na mashosti....🙆‍♀️
Hadi leo tumefika kwenye mobile phones....simu za kiganjani....💃
Hapo nilienda kubadili protector imeanza kuchoka sasa...
Shikamoo teknolojia. Napata kila kitu kwenye simu yangu, nyakati za Avalon, Drive inn, Empress, Empire nk ni story tu hivi sasa....
Nikijiita MSTAAFU ni kukubali yaishe mpendwa wangu 🤣🤣🤣

20/09/2025

Tuchague vyakula bora kwa afya za umri wetu...sio bora chakula...🤣
Kwa mfano mimi sitakiwi kula biskuti lakini mjukuu wangu bila biskuti na ice cream hakosi akiingia supermarket....
Hahahaaa....ama kweli wakati ni ukuta nisipigane nao...💃
Nimemaliza event yangu salama ndio nikaingia hapa....feedback ya event baadae.
Nawatakieni nyote wakati mzuri....

Address

Madale
Dar Es Salaam
022

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kazini hadi Kustaafu KAZI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram