15/02/2026
🩺 BAWASIRI NI NINI?
Bawasiri ni uvimbe wa mishipa ya damu inayopatikana ndani au nje ya tundu la haja kubwa .
Hutokea pale mishipa hiyo inapopata shinikizo kubwa kwa muda mrefu, na kujaa damu kupita kiasi.
📌 AINA ZA BAWASIRI
1️⃣ Bawasiri za Ndani (Internal Hemorrhoids)
Zipo ndani
Mara nyingi haziumi sana
Huonekana kwa damu kutoka wakati wa kujisaidia
2️⃣ Bawasiri za Nje (External Hemorrhoids)
Zipo nje
Huleta maumivu, kuwasha na uvimbe unaoshikika
3️⃣ Bawasiri Zilizotoka Nje (Pr*****ed)
Huanzia ndani lakini hutoka nje
Wakati mwingine hurudi ndani zenyewe au hubaki nje
4️⃣ Bawasiri zenye Damu Kuganda (Thrombosed)
Damu huganda ndani ya uvimbe
Husababisha maumivu makali sana