MAMA Anayejali Huwajibika

MAMA Anayejali Huwajibika Watoto ni zawadi anayotupatia Mungu ili tuweze kuitunza na kuifurahia, tuwapende na kuwajali

Katika picha hizi hapa chini Kuna kitu cha kujifunza.Tuongeze uelewa kuhusu Saratani ya Matiti.
12/11/2023

Katika picha hizi hapa chini Kuna kitu cha kujifunza.

Tuongeze uelewa kuhusu Saratani ya Matiti.

Tuongeze uelewa kuhusu magonjwa yasiyoambukiza.Leo tunajifunza kuhusu Saratani ya Matiti.Karibuni sana
11/11/2023

Tuongeze uelewa kuhusu magonjwa yasiyoambukiza.

Leo tunajifunza kuhusu Saratani ya Matiti.

Karibuni sana

Hongera sana kipenzi changu Christina kwa kupokea baraka yako ...Mungu akutunze na kukupa afya njema wewe na mtoto wako....
10/03/2023

Hongera sana kipenzi changu Christina kwa kupokea baraka yako ...Mungu akutunze na kukupa afya njema wewe na mtoto wako.

Nawapenda😘

Hellow wapenzi ,hope mko poa kabisa....Basi bwana ngoja niwape story ,kwenye maisha yetu ya kila siku kuna wakati mtu un...
22/02/2023

Hellow wapenzi ,hope mko poa kabisa....Basi bwana ngoja niwape story ,kwenye maisha yetu ya kila siku kuna wakati mtu unaweza jikuta umefikia hatua ambayo hata wewe mwenyewe ukijitazama unasema eee bwana eee its enough😄

Mwaka jana september nikasema isiwe tabu ,kwann na ukunga wangu huu afu ninenepeane k**a tukunyema weee nitawabebaje wajawazito wangu leba wakilemewa,basi bwana nikarudi darasani kwenye kuishi maisha ya kula mlo kamili

Taratibu uzito ulionilemea ukaanza kuisha na mpaka sasa naanza kujifurahia maana mwili wa awali ulinikera balaaaaa japo ilikuwa mtu akiniambia wewe mnene nambishia kuliko kawaida🤣

Msinicheke ndio maisha lakini...,hebu kwenye commemt na wewe tupe ushuhuda wako unaotamani tuujue

Wewe ni mama uliyejifungua na unapitia changamoto mbalimbali za malezi na hujui pa kuanzia?? Wewe ni mama mwenye mtoto m...
15/02/2023

Wewe ni mama uliyejifungua na unapitia changamoto mbalimbali za malezi na hujui pa kuanzia??

Wewe ni mama mwenye mtoto mdogo na unapitia changamoto za kupata maziwa ya kutosha?

Unaona mtihani kila siku kwenda hospital kuuliza maswali yanayokusumbua kuhusu malezi??

Usipate tabu tenaaa, midwife_anitha anaweza kuwa mkunga wako unayeweza kumtumia kila unapohitaji huduma ya kitaalamu.

Haijalishi uko mkoa gani ,njoo uungane na familia ya midwife_anitha uweze kusimamiwa, kuelekezwa na kusaidiwa katika changamoto zako zote za malezi upate kufurahia safari yako ya kulea mtoto bila shida.

Jinsi ya kuungana na familia yetu ni rahisi njoo wasap kwa namba 0713599154 utapata maelekezo kamili.

Anayejali Huwajibuka

Mjamzito hakikisha katika safari yako ya ujauzito unaye mkunga unayeweza kumuamini na kumshirikisha juu ya afya yako hat...
13/02/2023

Mjamzito hakikisha katika safari yako ya ujauzito unaye mkunga unayeweza kumuamini na kumshirikisha juu ya afya yako hata k**a yuko mbali nawe.... hii itakusaidia sana kuweza kupata msaa wa haraka pale unapouhitaji ikiwemo ushauri na msaada wa kisaikolojia.

Kipindi cha ujauzito ni kipindi ambacho mama anapitia mabadiliko makubwa ya kimwili na kiakili kutokana na mabadiliko ya homoni hivyo ili uweze kujua kipi ni cha mawaida na kipi ni cha hatari ni muhimu ufanye mawasiliano na mkunga wako..

midwife_anitha nipo kwa ajili yako wewe mama mjamzito ,karibu sana nipate kukusimamia katika safari yako hii muhimu ya kuwa mama.

karibu yako



0713599154

Midwife Anitha meet up with mama K wa dodoma...Nimepata uzoefu mzuri sana kukutana na wateja wangu, sisi kwa pamoja tume...
06/02/2023

Midwife Anitha meet up with mama K wa dodoma...

Nimepata uzoefu mzuri sana kukutana na wateja wangu, sisi kwa pamoja tumekuwa na wakati mzuri sana ...pia tumejifunza umuhimu wa kuepukana na hofu wakati wa ujauzito.

Ikiwa uko Dodoma na unatamani kupata nafasi adimu k**a hii ya kumeet up with midwife_anitha ,kaa mkao mzuri ujiunge nasi event inayokuja.

Midwife_anitha nipo kwa ajili yenu kuhakikisha safari ya ujauzito ni nzuri ma salama kwako kila wakati.

Nafasi za kujiunga na group la wajawazito bado zipo karibu sana nikuhudumie 0713599154

Niulize chochote kuhusu masuala ya ujauzito na masuala ya malezi ya watoto nikupe msaada wa kitaalamu kabisaa ,usifanye ...
06/02/2023

Niulize chochote kuhusu masuala ya ujauzito na masuala ya malezi ya watoto nikupe msaada wa kitaalamu kabisaa ,usifanye safari ya ujauzito na malezi peke yako...hakikisha unaye midwife_anitha kwa msaada wa haraka na wa uhakika.

Mkunga anaokoa maisha

DALILI ZA HATARI WAKATI WA UJAUZITO👉🏼Ni muhimu kuwa makini na Afya ya mama kwani wakati wowote wa ujauzito dalili hizi z...
02/02/2023

DALILI ZA HATARI WAKATI WA UJAUZITO

👉🏼Ni muhimu kuwa makini na Afya ya mama kwani wakati wowote wa ujauzito dalili hizi zinaweza kutokea na kuhatarisha Afya ya mama.

1.Kujisikia kuchoka sana, kukosa pumzi na mapigo ya moyo kwenda mbio
2.Kutokwa na damu ukeni
3.Maumivu makali ya kichwa na kutoona vizuri
4.Kupoteza fahamu na kutetemeka
5.Kuvimba mikono ,miguu na uso
6.Kupata uchungu mapema kabla ya miezi 9
7.Kutokwa uchafu wenye harufu au majimaji ukeni
8.Dalili za Malaria k**a vile kusikia Baridi ,homa na kutapika
9.Mtoto kupunguza kucheza au kutocheza kabisa.
10.Kuona Maluweluwe

Uonapo dalili hizi wahi kituo cha kutolea huduma za Afya kwa msaada wa haraka

Karibuni darasa la wajawazito 0713599154

KUBEMENDA NI NINI?? 👉 *Kubemenda* Ni neno la kiswahili naweza kusema ambalo lilianzishwa na wahenga likiwa na maana kwam...
13/01/2023

KUBEMENDA NI NINI??

👉 *Kubemenda* Ni neno la kiswahili naweza kusema ambalo lilianzishwa na wahenga likiwa na maana kwamba mtoto hakui kulingana na hatua za ukuaji wanazopitia watoto wengine wenye Afya nzuri , yeye anadhoofu na kudumaa

👉Sasa wahenga Hawa wakatoa sababu karibu 3 zinazoaminika kwamba zinaweza *kumbemenda mtoto* endapo zitafanywa na wazazi.

👉Sababu hizo Ni
1.Mama Anayenyonyesha kushiriki tendo la ndoa na mwenzi wake(kwamba shahawa zitaenda kuharibu maziwa na mtoto ataumwa)

2.Mama Anayenyonyesha kubeba Ujauzito mwingi huku ananyonyesha(kwamba joto la mama litamdhuru mtoto)

3.Mama Anayenyonyesha au mwenzi wake kushiriki tendo la ndoa na mtu mwingine(kwamba like jasho baada ya shughuli linampa mtoto magonjwa)

Ndivyo utafiti wangu umekutana na Mambo haya

👉Tukija kitaalamu Sasa he Ni kweli Kuna kubemenda mtoto K**a wanavyosema??

👉Jibu Ni *hapana*,hii Ni dhana tu ambayo ipo kwenye jamii na haijathibitishwa kisayansi kwani Hakuna uhusiano wowote wa dhana hizo na mtoto kuharibika.

Sababu zinazopeleka mtoto kushindwa kukua kulingana na hatua za ukuaji za kawaida zipo nyingi K**a vile:-

1.Mtoto kutonyonyeshwa vizuri
2.Mtoto kuwa na matatizo ya kinywa hivyo hawezi kunyonya.
3.Mtoto kuanzishiwa mapema chakula Cha nyongeza kisichokuwa na Virutubishi muhimu kwa ajili ya ukuaji
4.Magonjwa K**a vile homa Kali, pneumonia na maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa mtoto.
👉Ni Ukweli usiopingika mama Anayenyonyesha anapaswa kuendelea kushiriki tendo la ndoa na mwenzi wake kila wanapohitaji kwa ajili ya kuimarisha ndoa Yao

👉Mama aliyebeba Ujauzito anaweza kuendelea kumnyonyesha mtoto aliyenaye Hadi pale atakapohisi ameshindwa kabisa na anaweza kuendelea kumnyonyesha mpaka atakapojifungua na kunyonyesha watoto wote wawili kwa wakati mmoja
👉Baba au mama kuchepuka Hakuna uhusiano wa kuharibu maziwa kwa sababu shahawa hazina uwezo wa kufika kwenye maziwa

Zingatia:Ni muhimu wazazi kuzingatia usafi wa mwili kabla mtoto hajanyonyeshwa ili kutompa jasho anyonyapo *pia* michepuko inaweza kuwa chanzo Cha kupata magonjwa K**a VVU na kusababisha kumuambukiza mtoto hivyo kupelekea mtoto kupata shida ya Afya.

TUJIFUNZE KUHUSU ULAJI WA NANASI WAKATI WA UJAUZITO.👉JE, Ni kweli nanasi Halifai kuliwa wakati wa ujauzito? Ni swali amb...
04/01/2023

TUJIFUNZE KUHUSU ULAJI WA NANASI WAKATI WA UJAUZITO.

👉JE, Ni kweli nanasi Halifai kuliwa wakati wa ujauzito?

Ni swali ambalo Wajawazito na watu wengi hulijadili na kutoa maoni mbalimbali kuhusu tunda hili, karibu ujifunze pamoja nami.

👉Nanasi Ni tunda zuri linalosaidia Kuongeza Kinga ya mwili, kutibu mafua, kupambana na saratani, kuondoka Maumivu pamoja na kulinda moyo.
👉Kwa mujibu wa USDA nanasi huundwa kwa maji, nishati, protini, wanga, nyuzilishe na Aina mbali mbali za Sukari na folate, pia Lina vitamin C pamoja na madini chuma, Calcium , potassium , magnesium pamoja na phosphorus

👉Licha ya Faida hizi zote tunda hili huusishwa na kuharibu Ujauzito mchanga kwa wanawake na Jambo Hili hutokana na uwepo wa vimeng'enya vya bromelain ambavyo kiasili hupatikana kwenye nanasi pekee

👉 Bromelain Ni Nini hasa?? ,Hili Ni kundi kubwa la vimeng'enya vunavyopatikana kwenye tunda la nanasi, na kazi kubwa ya Bromelain Ni kusaidia mmeng'enyo wa vyakula vyenye asili ya protini, Husaidia kutibu changamoto za mfumo wa upumuaji kwa kupambana na maambukizi ya bakteria na virusi, Husaidia kuondoa Maumivu ya mwili hasa Yale yanayotokea kwenye maungio ya mifupa , kuvimba kwa tishu pamoja na baridi yabisi, huzuia kuongezeka kwa shinikizo la juu la damu , kiharusi, shambulio la moyo pamoja na kuzuia kuganda kwa damu kwenye mishipa na hupambana na bakteria wabaya hasa wale wanaosababisha magonjwa ya kunywa , uzazi na mfumo wa chakula nk

👉Matumizi ya Vidonge vya Bromelain wakati wa ujauzito hayashauriwi kwa sababu vinaweza kumfanya apoteze damu nyingi pamoja na kuharibu Ujauzito

👉Lakini Kiasi Cha Bromelain Kinachopatikana kwenye nanasi Ni kidogo Sana kuweza kuleta athari zozote kwa Ujauzito , pia Hakuna tafiti za kisayansi zinazothibitisha madhara ya nanasi kwa binadamu hivyo nanasi linabaki kuwa tunda Bora Sana kwa wanawake Wajawazito.

👉Ili kufikia kiwango Cha kidonge kimoja Cha Bromelain ambacho kina madhara mjamzito anahitajika kutumia mananazi 10 kwa wakati mmoja, lakini Ulaji wa kawaida wa nanasi Ni salama kabisa kwa kipindi chote Cha Ujauzito wako.

Imeandialiwa

mtaalamu

👉Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya kila mmoja aliyeniunga mkono Katika safari yangu ya kutoa Elimu kupitia ukurasa huu wa ...
31/12/2022

👉Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya kila mmoja aliyeniunga mkono Katika safari yangu ya kutoa Elimu kupitia ukurasa huu wa Instagram, hamkuniacha peke yangu mlinisupport kwa kiasi kikubwa Katika mwaka 2022

👉Nilianza na wafuasi elfu moja lakini mpaka tunahitimisha mwaka 2022, familia yetu inatakribani wafuasi 2000++ ,haikuwa rahisi Lakini Mkono wa Bwana umekuwa nasi.

👉Ninawatakia heri ya mwaka mpya 2023 watu wangu wa nguvu, ninawaombea Baraka za Bwana ziambatane nanyi Katika mwaka 2023.

👉Nipende kuwaahidi 2023 nitawapatia Elimu zaidi kuhusu masuala yote yanayohusu Afya ya uzazi , Uzazi salama na Malezi ya watoto ambayo yataboresha Afya zenu kwa ujumla kwa kupata kilicho Bora.


31/12/2023

Address

Bahi
Dodoma

Opening Hours

Monday 09:00 - 18:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255713599154

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAMA Anayejali Huwajibika posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MAMA Anayejali Huwajibika:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram