Afya Yako Point

Afya Yako Point We Care About Your Health

08/03/2026

K**a kongosho halifanyi kazi vizuri, mwili hushindwa kutengeneza au kutumia insulini ipasavyo.

Matokeo yake sukari hubaki nyingi kwenye damu badala ya kuingia kwenye seli za mwili kutoa nguvu,ndiyo maana watu wengi wenye changamoto ya sukari hupata dalili k**a:
• Uchovu wa mara kwa mara bila sababu
• Kiu kali isiyoisha
• Kukojoa mara nyingi
• Mwili kukosa nguvu na uzito kubadilika

Tatizo mara nyingi halianzi kwenye sukari pekee… linaanza kwenye mfumo wa kongosho na insulini kutofanya kazi vizuri.

Ukianza kuona dalili hizi mapema, ni muhimu kuchukua hatua kulinda afya yako kabla hali haijawa kubwa zaidi.

07/03/2026

Kosa ambalo wengi hulifanya kwa kuhisi haliwahusu ambalo na wewe hutakiwi kulifanya

07/03/2026

Kuchoma k**a sindano na ganzi kwenye mikono au miguu ni dalili ambazo zinaweza kuonekana kwa watu wenye Kisukari na pia Shinikizo la Damu (Presha) kwa sababu magonjwa haya yote mawili huathiri mishipa ya damu na mishipa ya fahamu.

Wakati mtu ana kisukari, kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kwa muda mrefu huanza kuharibu mishipa ya fahamu,na ndiyo maana mtu huanza kuhisi kuchoma k**a sindano kwenye miguu au mikono ganzi kwenye vidole,maumivu au kuungua kwenye nyayo hasa usiku.

Kwa upande wa presha, shinikizo kubwa la damu huathiri mzunguko wa damu kwenye mishipa midogo. Hali hii inaweza kufanya damu isifike vizuri kwenye mishipa ya fahamu, na kusababisha kuchomachoma k**a sindano,ganzi kwenye mikono au miguu na wakati mwingine kizunguzungu au maumivu ya kichwa.

Mara nyingi dalili hizi mbili huweza kuonekana pamoja, kwa sababu kisukari na presha vina uhusiano mkubwa na vinaweza kusababisha uharibifu wa mishipa ya damu na mishipa ya fahamu kwa wakati mmoja.

Ndiyo maana mtu akianza kuhisi kuchoma k**a sindano kwenye miguu,ganzi kwenye vidole,miguu kuungua au kufa ganzi ni muhimu kupima sukari ya damu na presha mapema, kwa sababu dalili hizi zinaweza kuwa ishara ya mwanzo ya matatizo haya.

06/03/2026

Leo ninazungumza na wewe ambaye umekuwa ukipitia changamoto za Figo, umehangaika mara nyingi bila kupata majibu sahihi, na labda hata hujui k**a dalili unazozipata zinatoka kwenye Figo zako.

Wewe ambaye kila siku unakojoa mara nyingi sana au mara chache kupita kiasi, na hata ukikojoa unahisi maumivu makali sehemu ya chini ya tumbo au mgongoni.

Unayehisi miguu kuvimba, uso kuvimba asubuhi, mwili kuchoka bila sababu, uchovu wa kupindukia, au shinikizo la damu kupanda mara kwa mara bila kuelewa chanzo.

Au pengine umekuwa ukipata U.T.I zinazojirudia mara nyingi kiasi kwamba zimekutesa kwa muda mrefu na hujui ni kwa nini hata ukimeza dawa, tatizo linakuja tena na tena.

Ninazungumza pia na wewe ambaye una harufu kali kwenye mkojo, mkojo wa rangi ya njano iliyokolea sana, au hata rangi ya kahawia.

Hizi zote ni ishara kwamba Figo zako zinateseka kimya kimya.

K**a umekuwa ukiamka asubuhi kichwa kinauma, miguu imejaa maji, au mwili mzima unahisi mzito basi tambua kuwa mwili wako unakuomba msaada.

MADHARA YA KUPUUZA DALILI ZA FIGO
– Mwili kuvimba siku hadi siku
– Maumivu makali ya mgongo na kiuno
– Kuvimba uso asubuhi
– Shinikizo la damu kupanda mara kwa mara
– Kukosa nguvu za mwili, kutozingatia kazini
– U.T.I sugu ambayo inaumiza kila mara
– Na hatari kubwa zaidi: kushindwa kwa figo
Ukishafikia hatua ya figo kushindwa kufanya kazi, gharama zake ni kubwa na huzuni yake ni kubwa zaidi na yote haya yanaweza kuzuilika leo, mapema.

Usisubiri mpaka figo zikose kabisa uwezo.
Mwili wako umekuonya vya kutosha.
Sasa ni zamu yako kuusikiliza.....suluhisho lipo wasiliana nami kupitia
0746 334 963

05/03/2026

Usije kuingia kwenye gharama kubwa baadaye fanya hivi leo uokoe afya yako na kuepukana na gharama kubwa baadaye

05/03/2026

Sikiliza hii kwa wewe ambaye unapitia changamoto hii ya kisukari au presha lakini pia share na mwingine mwenye changamoto k**a hii

26/02/2026

Chumvi nyingi huumiza figo polepole japo mwili unahitaji chumvi kidogo tu, lakini ikizidi Figo zinaongezewa kazi ya kuchuja sodiamu iliyozidi,hivyo zinachoka taratibu na uwezo wa kuchuja taka unapungua.
Hii inaweza kusababisha uvimbe miguuni, uso kujaa maji na shinikizo kuongezeka.

Chumvi nyingi huongeza shinikizo la damu (presha) kwani Sodiamu ikizidi mwilini huvuta maji mengi kwenye damu hivyo
Damu inakuwa nyingi kuliko kawaida na
Mishipa inalazimika kusukuma damu kwa nguvu.Ndipo presha inapanda bila sababu ya moja kwa moja,Presha inapopanda inaleta shida kwenye figo zaidi, maana mishipa ya damu ndani ya figo inabanwa.

Chumvi nyingi inavuruga mzunguko wa damu na husababisha mishipa kuwa myembamba,na kuta za mishipa kuwa ngumu (atherosclerosis).

Damu kusafiri kwa tabu kwenda kwenye viungo na hii husababisha dalili k**a:
Kizunguzungu
Mikono/miguu kufa ganzi
Moyo kwenda mbio
Uchovu usioeleweka

Mwisho wake figo na moyo hudhurika.
Presha ikikaa juu muda mrefu huharibu mishipa midogo inayosambaza damu kwenye figo.
Hii hupunguza uwezo wa figo kusafisha damu na sumu hivyo hatari ya figo kushindwa kazi huongezeka.

Na kwa moyo unaweza kupata heart failure, mapigo yasiyo sawa, au kiharusi.

JINSI YA KUPUNGUZA HATARI HARAKA
• Punguza chumvi kwenye chakula, epuka kuongeza mezani
• Epuka vyakula vya viwandani (vina chumvi nyingi sana)
• Kunywa maji ya kutosha
• Kula matunda na mboga kila siku
• Angalia presha mara kwa mara

Moja ya madhara ya ugonjwa wa kisukari ni kukatwa baadhi ya viungo,je nini kinapekelekea hali hiyo na je ni nini ni sulu...
19/02/2026

Moja ya madhara ya ugonjwa wa kisukari ni kukatwa baadhi ya viungo,je nini kinapekelekea hali hiyo na je ni nini ni suluhisho??

Hii ni swali muhimu sana,sasa nitoe maelezo kwa urahisi lakini kwa kina ili upone hali yako na hofu yako;

Wagonjwa wa kisukari, hasa wale wenye sukari isiyodhibitiwa, wana hatari kubwa ya matatizo ya miguu na vidole. Hali hii hutokea kwa sababu:

Madhara ya neva (neuropathy)ambayo huathiriwa na uwepo wa sukari nyingi mwilini amabyo huharibu mishipa ya fahamu (nerves).

Hii husababisha kupoteza hisia katika miguu au viganja na vidole vya mikono au miguu. Mgonjwa anaweza kushindwa kuhisi maumivu,k**a vile ya kuumwa na majeraha madogo.

Madhara kwa mishipa ya damu (poor circulation).Kisukari kinaweza kuharibu mishipa midogo ya damu, hasa miguu na vidole.Damu haifiki vizuri sehemu hizi, hivyo majeraha hayaponi haraka.

Kuungua au kuvimba kwa vidonda
Maambukizi (infections) yanapokuwa, mwili hawezi kupambana vizuri kwa sababu kinga ya mwili imeathirika.
Hii inaweza kusababisha vidonda vikubwa vinavyoshindwa kuponywa.

Matokeo ya hali hii ni vidonda visivyopona vinaweza kuharibu tishu.
Mara nyingi, ikiwa majeraha ni makubwa au yameambukizwa vibaya, daktari anaweza kupendekeza kukatwa kidogo au kimoja cha kidole, mguu au sehemu fulani ili kuokoa maisha au kuzuia maambukizi kuenea.

Suluhisho na kinga ni udhibiti wa sukari mwilini kufuatilia sukari ili isizidi kwa kujenga kinga mwilini ,lishe bora, kudumisha uzito wa mwili, na kuzuia shinikizo la juu la damu.

Kwa maneno mengine, kukatwa viungo ni suluhisho la muda mfupi ila sio mwisho inapotokea maambukizi makubwa au tishu kuharibika shida iakuwa kubwa zaidi lakini kinga na udhibiti wa sukari inaweza kuzuia hali hiyo kabisa.

Leo ninazungumza na wewe ambaye umekuwa ukipitia changamoto za Figo, umehangaika mara nyingi bila kupata majibu sahihi, ...
11/02/2026

Leo ninazungumza na wewe ambaye umekuwa ukipitia changamoto za Figo, umehangaika mara nyingi bila kupata majibu sahihi, na labda hata hujui k**a dalili unazozipata zinatoka kwenye Figo zako.

Wewe ambaye kila siku unakojoa mara nyingi sana au mara chache kupita kiasi, na hata ukikojoa unahisi maumivu makali sehemu ya chini ya tumbo au mgongoni.

Unayehisi miguu kuvimba, uso kuvimba asubuhi, mwili kuchoka bila sababu, uchovu wa kupindukia, au shinikizo la damu kupanda mara kwa mara bila kuelewa chanzo.

Au pengine umekuwa ukipata U.T.I zinazojirudia mara nyingi kiasi kwamba zimekutesa kwa muda mrefu na hujui ni kwa nini hata ukimeza dawa, tatizo linakuja tena na tena.

Ninazungumza pia na wewe ambaye una harufu kali kwenye mkojo, mkojo wa rangi ya njano iliyokolea sana, au hata rangi ya kahawia.

Hizi zote ni ishara kwamba Figo zako zinateseka kimya kimya.

K**a umekuwa ukiamka asubuhi kichwa kinauma, miguu imejaa maji, au mwili mzima unahisi mzito basi tambua kuwa mwili wako unakuomba msaada.

Sasa suluhisho sahihi juu ya figo zako limepatikana lakini kabla ya matibabu, ni muhimu zaidi kuelewa chanzo ili tatizo lisiendelee kukurudia tena.

CHANZO CHA MATATIZO YA FIGO

Kutokunywa maji ya kutosha
Hii ndiyo sababu kubwa. Ukiwa na upungufu wa maji, figo zinahangaika kutoa taka mwilini. Ndiyo maana unapata U.T.I, maumivu ya mgongo na uchovu.

Mafuta mengi, vyakula vya chumvi na chemicals nyingi mwilini ni moja ya vitu ambavyo hupelekea
Figo kujaa taka,hivyo zinashindwa kupitisha damu vizuri. Hapa ndipo pressure inapanda na mwili unaanza kuvimba.

Matumizi ya antibiotics bila ushauri
Dawa zisipotumiwa vizuri zinaharibu figo taratibu bila wewe kuona mapema.

Kisukari na presha
Haya ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kuharibu figo kimya kimya kwa miaka mingi.

U.T.I sugu au inayojirudia bila kutibiwa ipasavyo huenda juu mpaka kwenye figo na kuanza kuharibu mfumo wa kuchuja damu.

MADHARA YA KUPUUZA DALILI ZA FIGO
– Mwili kuvimba siku hadi siku
– Maumivu makali ya mgongo na kiuno
– Kuvimba uso asubuhi
– Shinikizo la damu kupanda mara kwa mara
– Kukosa nguvu za mwili, kutozingatia kazini
– U.T.I sugu ambayo inaumiza kila mara
– Na hatari kubwa zaidi: kushindwa kwa figo
Ukishafikia hatua ya figo kushindwa kufanya kazi, gharama zake ni kubwa na huzuni yake ni kubwa zaidi na yote haya yanaweza kuzuilika leo, mapema.

CHUKUA HATUA SASA
Kwa wale wa Dodoma Tunapatikana:
📍 Ipagala – Shule ya Biblia Emmausi (maarufu k**a kanisa la Biblia Emmausi)
Na kwa gharama ndogo ya TSh 5,000 tu, unamuona daktari na kupata mwelekeo sahihi wa afya yako leo.

Usisubiri mpaka figo zikose kabisa uwezo.
Mwili wako umekuonya vya kutosha.
Sasa ni zamu yako kuusikiliza.
Kwa mawasiliano na msaada wa haraka save namba hizi:
📞 0746 334 963
Kwa wale wa mikoani tunafanya delivery mkoa wowote.

Ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini haswa?Uwepo wa Glucose nyingi inayozunguka katika mfumo wako wa damu husababish...
06/02/2026

Ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini haswa?

Uwepo wa Glucose nyingi inayozunguka katika mfumo wako wa damu husababisha ugonjwa wa kisukari, bila kujali aina.

Ingawa, sababu kwa nini viwango vya sukari kwenye damu yako ni vikubwa hutofautiana kulingana na aina ya ugonjwa wa kisukari.

Hizi hapa ni Sababu mbali mbali zinazochangia hali hiyo:

1- Tatizo la Insulin resistance:

Aina ya 2 ya kisukari hutokana hasa na ukinzani wa insulini. Ukinzani huu wa insulini hutokea wakati seli kwenye misuli, mafuta na ini hazitoi matokeo inavyopaswa dhidi ya insulini.

Sababu na baadhi ya hali huchangia viwango tofauti vya ukinzani wa insulini.

Sababu hizo ni pamoja na;

-Uzito mkubwa au kunenepa kupita kiasi,
Kutokufanya Mazoezi ya mwili.

-Mabadiliko ya Vichocheo au homoni mwilini.

-Swala la kimaumbile au Genetics factor
Matumizi ya baadhi ya dawa fulani.n.k

2-Tatizo kwenye Mfumo wa kinga
mwili(Autoimmune disease)

Kisukari aina ya kwanza(Type 1 diabetes) pamoja na Latent autoimmune diabetes in adults (LADA) ambapo nilitaja aina hii hapo awali, hutokea wakati mfumo wako wa kinga unaposhambulia seli zinazozalisha insulini kwenye kongosho lako.

3- Tatizo la Hormonal imbalances:

-Wakati wa Ujauzito, placenta huweza kutoa homoni zinazosababisha ukinzani wa insulini. Unaweza kupata kisukari wakati wa ujauzito ikiwa kongosho yako haiwezi kutoa insulini ya kutosha kushinda ukinzani wa insulini uliojitokeza.

Hali nyingine zinazohusiana na homoni k**a vile tatizo la akromegali pia zinaweza kusababisha kisukari cha Aina ya 2.

4- Uharibifu wa kongosho(Pancreatic damage):

Uharibifu wa kongosho lako kutokana na hali k**a vile ajali, upasuaji au jeraha unaweza kuathiri uwezo wake wa kutengeneza insulini, na kusababisha ugonjwa wa kisukari hasa Aina ya 3 ya kisukari(Type 3 diabetes).

5- Matatizo ya kimaumbile au kigenetic(Genetic mutations):

Mabadiliko fulani ya kijenetic yanaweza kusababisha Ugonjwa wa kisukari hasa kuanzia kwa watoto wachanga,aina hii ya kisukari hufahamika k**a neonatal diabetes.

6- Utumiaji wa muda mrefu wa baadhi ya dawa

Aina za Ugonjwa wa KisukariKuna aina kadhaa za Ugonjwa wa kisukari.1.Kisukari aina ya kwanza(Type 1 Diabetes)2.Kisukari ...
05/02/2026

Aina za Ugonjwa wa Kisukari

Kuna aina kadhaa za Ugonjwa wa kisukari.

1.Kisukari aina ya kwanza(Type 1 Diabetes)

2.Kisukari aina ya Pili(Type 2 diabetes)
Kisukari cha

2.Mimba(Gestational diabetes)

Pamoja na aina nyingine kadhaa ambazo watu wengi hawazizungumzii kabisa ila zipo,mfano kuna
Type 3 Diabetes

Latent Autoimmune Diabetes In Adults (LADA)

Maturity-onset Diabetes

Neonatal diabetes.

Sasa tuangalie aina hizi za kisukari, tukianza na ;

1. Kisukari aina ya Kwanza(Type 1 diabetes)
Aina hii ya Ugonjwa huhusisha kongosho au Pancrease kutokuzalisha na kutoa Insulin kabisa.

Hapa kongosho haitengenezi Insulini kabisa, kwa sababu mfumo wa kinga ya mwili hushambulia seli za kongosho zinazotengeneza insulini.

Aina hii ya 1 ya kisukari kwa Kawaida hugunduliwa kwa watoto na vijana, lakini inaweza kutokea katika umri wowote pia.

2. Kisukari Aina ya Pili(Type 2 diabetes)
Kwa aina hii, mwili wako hautengenezi insulini ya kutosha au seli za mwili wako hazitumii vizuri ipasavyo insulini iliyopo.

Hii ndiyo aina ya Ugonjwa wa kisukari ambao huwapata Watu Wengi Zaidi na Inaathiri zaidi watu wazima, lakini kwa sasa hata vijana na watoto wanakuwa nayo pia kutokana na ulaji na mtindo wa maisha tunayoishi kwa sasa.

Katika aina ya 2 ya kisukari, kongosho hutengeneza insulini kidogo kuliko ilivyokuwa hapo awali, na mwili wako unatengeneza ukinzani dhidi ya insulini ndogo iliyopo yaani Insulin Resistance.

3. Kisukari cha Mimba(Gestational diabetes):
Aina hii ya kisukari inatokea wakati wa ujauzito, na kawaida hupotea baada ya ujauzito au baada ya kujifungua.

Ingawa baadhi ya tafiti zinaonyesha ikiwa una kisukari wakati wa ujauzito, uko katika hatari kubwa ya kupata kisukari cha Aina ya 2 baadaye maishani.

Dalili Za Ugonjwa wa kisukari

Ukali wa dalili unaweza kutofautiana kulingana na aina ya ugonjwa wa kisukari ulionao.

Dalili hizi kawaida huwa kali zaidi katika aina ya 1 ya kisukari kuliko kisukari cha Aina ya 2.

Dalili za kisukari kwa Ujumla ni zipi?

Dalili za ugonjwa wa kisukari ni pamoja na:

1.Kuongezeka kwa kiu na kinywa kuwa kikavu zaidi.
2.Kukojoa mara kwa mara.
3.Kupata sana Uchovu wa mwili
4.Macho kutokuona vizuri au kuona marue rue
5.Kupunguza Uzito kwa kasi bila Sababu inayoeleweka, au
Mtu kukonda
6.Kupata Ganzi au hali ya kuchoma choma katika mikono au miguu yako.
7.Vidonda kupona polepole au kuchelewa zaidi kupona
8.Kuwa kwenye hatari ya kupata Maambukizi ya mara kwa mara ya ngozi,
9.Kupoteza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa wanaume na wanawake na pia kupata maambukizi ya Fangasi ukeni n.k

Katika somo lijalo tutaona ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini?

Address

Moshi,Dar Es Salaam
Dodoma
MOSHI

Telephone

+255746334963

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Yako Point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya Yako Point:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram