Dr Godson Afya Page.

Dr Godson Afya Page. 📍Tunasaidia na kutatua changamoto za Afya, kwa kutumia mimea tiba, vyakula, matunda na Tiba lishe. "OKOA MAISHA, OKOA NGUVU KAZI"🌿

Kwa matokeo mazuri bila madhara kimwili.
📍Kwa ushauri, tiba 🇹🇿+255781918586(WhatsApp/piga).
📍DODOMA, TANZANIA.

12/02/2026

Zingatia hili k**a unahitaji kubeba ujauzito.
#🇰🇪🇹🇿🇺🇬🇶🇦🇷🇼🇳🇦 ゚viralシ

03/02/2026

Jitahidi kuipata Karafuu kwa sababu wengi wamekuja na shuhuda nzuri hata kiafya tafiti zinaonesha wanawake wenye matatizo ya kutopevusha mayai ya uzazi

Chukua unga wa karafuu kijiko kidogo kimoja, au punje za karafuu kijiko kidogo, chemsha kwenye maji nusu lita, ikishapoa chuja na kunywa glass moja Asubuhi na glass nyingine Usiku..

Anza ratiba hiyo ukitoka period hadi siku za ovulation

Naishauri karafuu kwa sababu inasafisha sana mirija ya uzazi pia husaidia kuondoa maumivu makali ya hedhi

Kwa wanaume, Chai ya karafuu na tangawizi ni nzuri kwa afya ya tendo la ndoa

Faida ya zaida kwa mwanamke, Karafuu inasaidia sana kuondoa harufu mbaya ukeni, kuondoa ukavu ukeni, kuongeza hamu ya tendo la ndoa...

Muhimu achana na matumizi ya sukari nyingi katika vyakula na vinywaji vyako

kwa changamoto yoyote ya kiafya kuhusu UZAZI tujuze kupitia namba +255781918586.


01/02/2026

💔 “Kila mwezi unaona hedhi, wakati moyo wako unataka kuona mistari miwili ya ujauzito?”........

“Umejaribu kila kitu, lakini bado mimba haipatikani?”......

👉 K**a hii ni story yako, soma hadi mwisho…

🤰 KWANINI WANAWAKE WENGI HAWAPATI MIMBA?
Wanawake wengi wanahangaika kupata ujauzito si kwa sababu hawawezi, bali kwa sababu ya changamoto zisizoeleweka vizuri, k**a:
✅ Mchanganyiko wa homoni (Hormonal imbalance).
✅ Tatizo la ovulation (yai haliachiliwi kwa wakati sahihi).
✅ Maambukizi ya mfumo wa uzazi (PID, fungus, bacteria n.k.).
✅ Mzunguko wa hedhi usio wa kawaida.
✅ Stress, lishe duni na mtindo wa maisha.
✅ Tatizo la mirija ya uzazi (fallopian tubes)...... Na.

Cha kushangaza ni kwamba, wanawake wengi hawajui chanzo halisi cha tatizo lao.

LAKINI TUMAINI LIPO!
Ukweli ni huu......

Mwanamke anaweza kupata ujauzito ikiwa atapata..... 👇👇
✔️ Taarifa sahihi kuhusu afya ya uzazi.
✔️ Ufuatiliaji sahihi wa mzunguko wa hedhi.
✔️ Ushauri wa kitaalamu unaoendana na hali yake.
✔️ Hatua sahihi za kiafya kwa wakati.

Wanandoa msikate tamaa....Usikate tamaa!
Wengi waliokuwa wamekata tamaa leo ni wazazi wa furaha.

🔥 Program hii tayari imesaidia
👉 Wanawake zaidi ya 50+
walioteseka kutopata ujauzito kwa muda mrefu,
na leo wana furaha ya kuona ndoto zao zikitimia 🤱✨.

📞 Je, na wewe unataka kupata ujauzito?
Usiendelee kubahatisha!...

👉 Wasiliana nasi sasa kupitia WhatsApp au Piga. Tutazungumza nawe kwa lugha ya upole na kitaalamu zaidi kubaini changamoto yako na chanzo halisi na Kukusaidia...
📞+255 781 918 586(WhatsApp/piga)
✍️Imeandaliwa na....
Godson
(Mshauri na mtatuzi wa masuala ya uzazi)
📍Dodoma-Tanzania.

Jifunze kisha chukua hatua💉🩺.

13/01/2026

Mmea huu wenye shina Jekundu na majani Manene (Mchicha-mwitu)— siyo magugu, bali ni Dawa na Virutubisho Adimu! 🩺

—Una kiwango kikubwa cha Omega-3 Haya Ni mafuta muhimu kwa Moyo na Ubongo 🧠 (k**a Yale ya kwenye samaki)!

—Faida Zake za Haraka:👇

↳ Hudhibiti Shinikizo la Damu (BP).

↳ Husaidia Macho 👁️ na huimarisha Mifupa 🦷.

↳Hufanya Detox ya Figo/Ini 🫘.

↳Huzuia Saratani na Anemia 🩸.

—JINSI YA KUTUMIA 👇
Andaa Juisi/Smoothie, Changanya na nanasi au ndizi. 🍹

Saladi: Majani mabichi yana uchachu mtamu! 🥗

Au unaweza Kaanga k**a mchicha wa kawaida.

Acha kuung'oa, anza kuutumia! Mwili wako utakushukuru 💪
Jifunze kisha Chukua hatua 🩺📌
_____________________

Jiunge nasi katika group la Afya na kujipatia Elimu mbali mbali kuhusu Afya. 👇👇

https://chat.whatsapp.com/CHNrXDdOIfO55XJXzDhpYs

12/01/2026

Kichoma-nguo: Gugu la Ajabu Linaloweza Kuokoa Afya Yako!🩺

Umewahi kukereka na gugu hili linalonata kwenye suruali yako? Ndiyo.... tunazungumzia Blackjack (Bidens pilosa), au k**a wengi wanavyoliita, Mchunga au Kichoma-nguo .🪻

Kwa wakulima ni kero, lakini kwa wataalamu wa mitishamba, ni hazina ya dawa.

Usidanganyike na muonekano wake wa gugu la kawaida. Mmea huu mdogo wenye maua meupe na njano unapakia nguvu ya ajabu ya tiba.🌻

Hizi ndio Faida Zinazoibeba Siri ya Mmea Huu:👇

↳ Husaidia sana kudhibiti viwango vya sukari na shinikizo la juu la damu🩺

↳ Husaidia Kudhibiti PID

↳ Tiba ya Magonjwa ya Minyoo

↳ Kupambana na Malaria 🦟

↳ Huponya Majeraha __Majani yake yakiwa yamepondwa na kupakwa, huongeza kasi ya uponyaji wa vidonda na majeraha ya kuungua.

↳ Hutumika kutibu kuhara na magonjwa mengine ya tumbo🤰.

↳ Siri ya Ngozi Nzuri Hasa Katika ulimwengu wa vipodozi vya kisasa, sehemu za mmea huu zinatumiwa k**a mbadala wa asili wa retinol (vitamin A) kupunguza makunyanzi, huku zikiwa rafiki kwa ngozi nyeti na nyororo
.....Mchunga Ni Tiba ya jadi inayoaminika ulimwenguni kote na Ni tiba ya haraka ya asili iliyo karibu nawe.

JINSI YA KUTUMIA KIRAHISI:👇

→ Kausha mizizi na shina, kisha uichemshe na kunywa k**a chai ya mitishamba Glas moja kutwa mala mbili hii Ni njia rahisi ya kupata virutubisho vyake.🍵

Au unaweza kutumia majani yake machanga k**a mboga ya majani.... Ni kitoweo chenye ladha na lishe bora (kina madini mengi k**a chuma na zinki).🥣

NB: Wakati mwingine, shujaa wa afya yako hajifichi kwenye maduka ya kifahari, bali anapatikana kwenye uwanja wako wa nyuma.....

Unapong'oa Kichoma-nguo, Unashughulika na zaidi ya gugu—Anza Leo uone Faida Zake

Jifunze kisha Chukua hatua 🩺📌

12/01/2026

Dalili za ujauzito.
Mfunze na mwenzio.

11/01/2026

Afya ni msingi wa kila tunalolifanya Leo. 💪

Afya ya uzazi na ujauzito ni muhimu ipewe kipaumbele sababu inagusa sehemu nyingi za maendeleo ya mama na mtoto, si tu kwa mama hata baba pia.

Karibu ujiunge na Darasa letu kwaajili ya kutoa Elimu na utatuzi wa changamoto za uzazi kwa akina mama wajawazito na wale wasiopata ujauzito.

Darasa linaanza Leo Rasmi, shiriki nasi kwa kugusa link itakayokupeleka moja kwa moja kwenye group. 👇👇

https://chat.whatsapp.com/GkU7ji78WCAFvRLDnejLSa

Au tutumie ujumbe mfupi WhatsApp ukisema“NIUNGE KWENYE GROUP"
kwenda namba +255781918586.
.

10/01/2026

Wapendeni wake zenu hizo ni roho zenu.

Kupitia wao ndyo idadi yetu inaongezeka😁.

Wakiwa kipindi cha ujauzito tuwafariji pia hata baada ya kuzaa tuwape mahitaji kamili.

Hongera yako wewe Mama ajae 2026.
.

10/01/2026

kwanza jenga mazoea ya kufanya mazoezi ya Kegels walau reps 50+ kila siku ndani ya mwezi lazima utaona changes

Pia jenga mazoea ya kupata vyakula vya kuimarisha misuri na msukumo wa damu, na mara kadhaa nawaandikia, kitunguu saumu, karafuu, tangawizi, karanga, dark chocolates, kahawa, habat soda (rejea somo hadi mwisho)

Msitawaliwe na uoga haya mambo yanatulika

Muhimu wakati mnatafuta kuwa imara tena msitumie msosi ya kutiwa mafuta mengi, pombe, sukari nyingi katika milo au vinywaji acheni au punguza kisha jiamini kwa kuchukua hatua ndogo ndogo kila siku, everything's gonn' be alright

K**a umepiga sana punyeto miaka ya ujanani na umeanza kuona madhara yake au bado hujaanza kuyaona, nakushauri kuwa na ulazima wa kufanya zoezi hili kila siku walau mara 50 au zaidi ili kuimarisha misuri inayoshikilia uume wako kusimama imara na kuzuia / kuruhusu mbegu kutoka

Wengi wa wahanga wa kupiga punyeto ni kumwaga mapema tena ndani ya sekunde kadhaa kwa sababu ya udhaifu wa misuri, hata ujizuie vipi unajikuta umeachia wazungu tu

Jipe siku 30 za kujiimarisha kupitia hili zoezi

K**a unaona hata hamu ya kufanya tendo imepungua au hujiskii kufanya tendo baada ya kumwaga au unaposhiriki bao la pili inakuchukua muda mrefu kumwaga au wazungu hawatoki kabisa, nakushauri kupata mlo wenye madini ya zinc kwa wingi ili kuongeza kiwango cha uzalishwaji wa homoni ya kiume

Katika kutibu changamoto hizi mwanaume jitahidi kuweka hofu pembeni, ili uweze kuwa imara, inafaa sana kuzingatia sana ulaji wako na kuhakikisha jogoo lako linaweza kusimama imara bila kuwa legevu ili kupenyeza katika uke na kurusha manii mbali kwenye kizazi.

Mwanaume | Unahitaji sana Madini Ya Zinki hasa k**a unaona mambo ya chumbani hayaendi vizuri,

Unaweza kuandaa hii lishe k**a una brenda

Mahitaji ni Karanga Mbichi, Almonds, Korosho, Mbegu za maboga na Tende (tupa mbegu ubakize maganda yake)

Nafaka hizi zina madini ya zinc kwa asilimia zaidi ya 70%

Chukua viambata vyote hivyo, saga vyote kwa pamoja kwenye brenda kisha utaweka maziwa fresh.

Usiongeze sukari wala Asali.

Tumia glass moja kila siku jioni baada ya Mazoezi ya Kegels..

2: ZOEZI LA KEGEL
Kati ya mazoezi yenye faida kubwa ni zoezi hili kwani mbali na kutumika kukata kitambi, kuondoa maumivu ya mgongo, kiuno na nyonga, zoezi hili linaimarisha sana msuri unaoshikilia uume pindi unapokuwa umesimama [pelvic floor muscle], na usichokijua ni kwamba linathibiti kwa kiwango kikubwa ukuaji wa ngiri na tezi dume.

~Tenga dakika moja au zaidi kufanya zoezi hili ili uwe shuhuda wa maarifa haya
Cha kufanya:

Lala chali, kunja miguu kuelekea kwenye kiuno kisha binua kiuno kuelekea juu kwa sekunde 15 kisha shuka then binua tena kiuno kwa raundi 15 hivi inatosha. [Mimi hulifanya zoezi hili ninapoamka asubuhi na usiku kabla sijalala], unaweza tazama tutorial yake, video zaidi nimekutumia (chuka hatua)

3: MTINDO WA MAISHA [wengi tumeharibikiwa hapa]
Kuwa makini katika katika kile unachokiingiza mwilini na matendo pia, Epuka ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, achana na junk foods, pombe isipokuwa mvinyo mwekundu [k**a imani yako inaruhusu kunywa kiasi], achana upigaji punyeto k**a bado unafanya hivyo kwa kuuminya au kuusugua u**me husababisha kutanua misuri na kuifanya kuwa legevu zaidi na kunywea kuwa k**a wa mtoto, weka mbali picha za ngono maana ndio sababu kubwa ya kupata hamu ya kujichua.

JINSI YA KUANDAA TIBA LISHE

Kwa kuwa mwanaume Unahitaji sana Madini Ya Zinki, Unaweza kuandaa hii lishe k**a una brenda

Mahitaji ni Karanga Mbichi, Almonds, Korosho, Mbegu za maboga na Tende (tupa mbegu ubakize maganda yake)

Nafaka hizi zina madini ya zinc kwa asilimia zaidi ya 70%

Chukua viambata vyote hivyo, saga vyote kwa pamoja kwenye brenda kisha utaweka maziwa fresh.

Usiongeze sukari wala Asali.

Tumia glass moja kila siku jioni baada ya Mazoezi ya Kegels.

Mabadiliko utayapata baada ya siku 15 Tu.

Muhimu mwanaume punguza matumizi ya sukari nyingi katika milo au vinywaji, wacha matumizi ya pombe, sigara na vyakula vyenye mafuta mengi

Ukihitaji dawa iliyoandaliwa kutoka kwetu ipo [JUISI na Mafuta] Kwa ajili ya kuondoa madhara ya punyeto, pia nayo unaweza kuandaa mwenyewe, ni rahisi sana

Tafuta Asali mbichi ya nyuki wadogo lita moja, Tangawizi kubwa nne au sita [osha, menya kisha katakata vipande], Vitunguu saumu ujazo wa glass moja [menya vizuri kuondoa maganda yake], Unga wa msamitu vijiko nane, Unga wa mdalasini vijiko sita mpaka nane, Unga wa habat sawda [black seed] vijiko vinne mpaka sita.

Chukua Tangawizi na Vitunguu saumu uweke kwenye blenda kisha usage mpaka vyote viwe laini.

Weka Unga wa Msamitu, Mdalasini na Unga wa Habat sawda kwenye blenda kisha taratibu huku ukiwa umewasha blenda mimina taratibu Asali mbichi ya nyuki wadogo mpaka lita nzima iishe kwa muda wa k**a dakika mbili juisi yako itakuwa tayari.

Zima blenda na uweke juisi yako kwenye kifungashio safi ikae kwa masaa 6, itakuwa tayari kwa matumizi

MATUMIZI:
Utakuwa ukilamba/kula vijiko viwili asubuhi unapoamka kabla hujala chochote, na usiku utatumia tena vijiko vitatu kabla ya kulala

Nikukumbushe kwamba hii tiba yako ni kwa ajili ya changamoto zako zote za upungufu wa nguuuvu za kiume

Kuanzia kwenye kuongeza wingi na ubora wa manii, kuondoa athari zilizotokana na upigaji punyeto na kuongeza kiwango cha msisimko ktk tendo la ndoa.

Unaweza kutumia Tiba Asili ambayo tumekuandalia Tayari

Ni ya kunywa, na tutaisafirisha mpaka mkoa wako au nchi jirani.

Dawa yetu Unaitumia kwa siku 25 na kumaliza kabisa tatizo la ngu*vu za kiume

Mafuta ya Kunyoosha Uume Pia ya lo, kwa wale waliojichua saana yaan wanavibamia.

Tunapatikana Dodoma Majengo.

Wasiliana nasi kwa Kupiga Simu / WhatsApp 0781918586.

NAKUSISITIZA SANA KATIKA MILO:

Sio kila mlo ni wa kubugia, vyakula vingine huwa si vizuri haswa vyakula hivi vya kisasa.
K**a mwanaume hakikisha katika milo yako ya siku nzima angalau unapata vyakula vitatu au zaidi katika orodha hii, hata k**a ni mara tatu kwa wiki sio mbaya.

Vyakula k**a chaza, pweza, tende, mbegu za maboga, asali ya nyuki wadogo, bamia, ndizi mbivu, mbegu za tikiti, pilipili, zabibu, mvinyo mwekundu, tangawizi, chai ya iliki na mdalasini, vitunguu saumu, viazi vyekundu, unga wa habat sawda, udishe au msamitu, ni vyakula ambavyo kazi yake katika mwili ni pamoja na kuchochea uzalishwaji wa homoni za kiume kwa wingi na kuleta mzunguko wa damu katika mishipa, hivyo hukuwezesha uume kujaa damu na kudumu kwa muda mrefu katika mishipa ya uume wakati wa tendo

09/01/2026

Miongoni mwa matatizo yanayoweza kuathiri uzazi wa mwanamke hadi kushindwa kupata mimba ni pamoja na haya.

1.Kuziba kwa mirija ya uzazi (Fallopian tubes) – Huzuia yai kukutana na mbegu.

2. Uvurugaji wa homoni (Hormonal imbalance)– Husababisha matatizo ya ovulation (kutokutunga kwa yai).

3. Uvutaji wa sigara, msongo wa mawazo, na uzito kupita kiasi– Hupunguza uwezo wa uzazi.

4. Fibroids (Vimbe kwenye kizazi) – Huzuia upandikizwaji wa mimba kwenye mfuko wa uzazi.

5. PCOS (Polycystic O***y Syndrome)– Husababisha mayai kutokomaa au kutotoka kabisa.

6. PID (Pelvic Inflammatory Disease)– Maambukizi sugu huathiri kizazi na mirija ya uzazi.

Ushauri :Mwanamke mwenye dalili k**a kutopata hedhi vizuri, maumivu ya tumbo ya mara kwa mara, au kushindwa kupata ujauzito kwa muda mrefu bado ana nafasi ya kupona na kubeba ujauzito k**a atafuata miongozo sahihi.

K**a wewe ni mwanamke au ni Mme na mkeo anapitia miongoni mwa changamoto hizo karibu kwa ushauri na utatuzi wa changamoto hizo

08/01/2026

KUMBWA KULIKO: IJUE SIKU YA KUPATA MIMBA au KUMPA MWANAMKE MIMBA...🩺

Nimeamua kuweka wazi kwa urefu, kwa sababu kuna wengi wanahitaji kujua ili kuepuka mimba zisizotarajiwa, na pia kwa wale wanaotafuta ujauzito—ELIMU HII NI KWA WOTE.....👇

Elimu hii inaweza kubadilisha maisha yako au ya mtu wako wa karibu....SOMA MPAKA MWISHO..

Ipo hivi....

Kuna siku maalum (Na ni chache sana) ambapo mwanamke akikutana kimwili na mwanaume, anaweza kushika mimba.....

Kwa lugha ya kitaalamu siku hizo, Hizi hujulikana k**a "Fertile Window"

Unajuaje siku hizo..?

Twende pamoja mpaka mwisho wa elimu hii, Nitakuonesha namna ya kuzitambua — Bila kufuata ramli, Bali sayansi ya mwili wako...

Kabla ya kuendelea na Somo letu la leo— ZINGATIA HILI. ..

↳ Unapojifunza kuhusu mimba, hormones ni kila kitu, Na hormones huchochewa moja kwa moja na lishe bora....

↳ Wanawake, Hakikisha mwili wako unapata virutubisho vya kutosha kila siku katika mlo wako..

↳ Wanaume Kula vyakula vinavyoongeza mbegu zenye nguvu — K**a karanga, korosho, mbegu za maboga, almonds na unywe maji mengi...


Jinsi ya Kutambua Siku ya Kupata Mimba Kwa Njia ya Hesabu...👇

Hatua ya kwanza, Tambua mzunguko wa hedhi....

— Je, ni siku 21, 28, au 32?

↳ Hili ni sehemu ya muhimu, Kwa sababu kila kitu kinahesabiwa kutoka hapo...

Ipo hivi....

↳ Mbegu ya mwanaume huishi ndani ya mwili wa mwanamke kwa siku 3–5...

↳ Yai la mwanamke linaweza kurutubishwa ndani ya masaa 12–48 tu...

Hii ina maana kwamba... Mbegu iliyoingia leo, inaweza kurutubisha yai kesho au hata kesho kutwa...!


Jinsi ya kukokotoa siku za mwanamke kupata mimba....👇

↳ Kwa wanawake wengi, yai hutolewa (ovulation) siku 12–16 kabla ya kuona hedhi.

Hesabu hivi, Chukua mzunguko wako wote, toa siku 12, halafu toa siku 4 tena. ..

MFANO: Mwanamke mwenye Mzunguko wa siku 21..

21 - 12 = 9
8 - 4 = 5

So, Siku ya 5 hadi ya 9 ni siku za hatari Mwanamke huyu mwenye mzunguruko wa siku 21 atapata mimba....

Tuone kwa Mzunguko wa siku (28) wanawake wengi mzunguko wao ni siku 28...

28-12 = 16
16 - 4 = 12

Siku ya 12 hadi ya 16 Mwanamke mwenye mzunguruko wa siku (28) anaweza kutoa yai...

Na ni muda ambao uwezekano wa kupata mimba ni mkubwa zaidi...

08/01/2026

KUMBWA KULIKO: IJUE SIKU YA KUPATA MIMBA au KUMPA MWANAMKE MIMBA...🩺

Nimeamua kuweka wazi kwa urefu, kwa sababu kuna wengi wanahitaji kujua ili kuepuka mimba zisizotarajiwa, na pia kwa wale wanaotafuta ujauzito—ELIMU HII NI KWA WOTE.....👇

Elimu hii inaweza kubadilisha maisha yako au ya mtu wako wa karibu....SOMA MPAKA MWISHO..

Ipo hivi....

Kuna siku maalum (Na ni chache sana) ambapo mwanamke akikutana kimwili na mwanaume, anaweza kushika mimba.....

Kwa lugha ya kitaalamu siku hizo, Hizi hujulikana k**a "Fertile Window"

Unajuaje siku hizo..?

Twende pamoja mpaka mwisho wa elimu hii, Nitakuonesha namna ya kuzitambua — Bila kufuata ramli, Bali sayansi ya mwili wako...

Kabla ya kuendelea na Somo letu la leo— ZINGATIA HILI. ..

↳ Unapojifunza kuhusu mimba, hormones ni kila kitu, Na hormones huchochewa moja kwa moja na lishe bora....

↳ Wanawake, Hakikisha mwili wako unapata virutubisho vya kutosha kila siku katika mlo wako..

↳ Wanaume Kula vyakula vinavyoongeza mbegu zenye nguvu — K**a karanga, korosho, mbegu za maboga, almonds na unywe maji mengi...


Jinsi ya Kutambua Siku ya Kupata Mimba Kwa Njia ya Hesabu...👇

Hatua ya kwanza, Tambua mzunguko wa hedhi....

— Je, ni siku 21, 28, au 32?

↳ Hili ni sehemu ya muhimu, Kwa sababu kila kitu kinahesabiwa kutoka hapo...

Ipo hivi....

↳ Mbegu ya mwanaume huishi ndani ya mwili wa mwanamke kwa siku 3–5...

↳ Yai la mwanamke linaweza kurutubishwa ndani ya masaa 12–48 tu...

Hii ina maana kwamba... Mbegu iliyoingia leo, inaweza kurutubisha yai kesho au hata kesho kutwa...!


Jinsi ya kukokotoa siku za mwanamke kupata mimba....👇

↳ Kwa wanawake wengi, yai hutolewa (ovulation) siku 12–16 kabla ya kuona hedhi.

Hesabu hivi, Chukua mzunguko wako wote, toa siku 12, halafu toa siku 4 tena. ..

MFANO: Mwanamke mwenye Mzunguko wa siku 21..

21 - 12 = 9
8 - 4 = 5

So, Siku ya 5 hadi ya 9 ni siku za hatari Mwanamke huyu mwenye mzunguruko wa siku 21 atapata mimba....

Tuone kwa Mzunguko wa siku (28) wanawake wengi mzunguko wao ni siku 28...

28-12 = 16
16 - 4 = 12

Siku ya 12 hadi ya 16 Mwanamke mwenye mzunguruko wa siku (28) anaweza kutoa yai...

Na ni muda ambao uwezekano wa kupata mimba ni mkubwa zaidi...

NB: Siku ya ovulation ni fursa kwa wapenzi wanaotafuta mtoto 💑

Kwa wasiokuwa tayari kupata mtoto — hizi ndizo siku za kuchukua tahadhari zaidi...📌

Wewe na mwenza wako mnatumia njia ipi ya uzazi wa mpango..?? Niandikie ujumbe mfupi kwenda WhatsApp namba 0781918586.

Tukutane inbox kwa maswali 😊 pia niandikie kwenda WhatsApp namba 👇
0781918586.

Address

Dodoma, Tanzania
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Godson Afya Page. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram