Triple Sha Health & Consultation

Triple Sha Health & Consultation Building a happy family - How to get the best partner for you and hold hands together ( Uchumba, Mal

MTIZAMO WA AFYA KATIKA TENDO LA NDOAFamilia yenye furaha inasaidia kufanya mazingira bora na mazuri ambayo yatawasaidia ...
07/04/2021

MTIZAMO WA AFYA KATIKA TENDO LA NDOA
Familia yenye furaha inasaidia kufanya mazingira bora na mazuri ambayo yatawasaidia na kuwawezesha watoto wakue na kufanikiwa. Familia ya namna hii imeundwa na kufungwa na vifungo vya upendo na hisia njema kwa wanandoa. Upendo wa kweli katika familia ububujika kutoka katika hali ya wazazi kufurahiana na kuridhikana katika maisha yao ya nyumbani. Katika kupata hali hii ya furaha, ni muhimu kwa wanandoa hao kuwa na hisia zenye afya kabisa katika tendo la ndoa baina yao. Mtizamo wao katika suala hili la tendo la ndoa linatokana na mengi yanayoendelea katika mahusiano yao na mazingira yanayowazunguka. Mahusiano yenye afya na furaha huleta unafuu na kutuepusha na wimbi la msongo na kututua mizigo na misuguano au migongano inayotuelemea kutokana na mbio za kukimbizana na majukumu mbali mbali ya kimaisha katika kutimiza wajibu sehemu zetu za kazi na maeneo mengine yanayotupatia riziki za kila siku. Mahusiano ya aina hii huwajengea heshima na thamani wanandoa , huwaletea maisha mazuri yenye furaha na kuridhikana kwa pamoja.
Ikiwa k**a mume na mke watachukua jukumu kamili na hisia kamili ya ndoa , hakika wanandoa hao watafurahiana na kuelewana kikamilifu. Hakika watajua sababu halisi ya kiasi na kujitawala ambayo hutofautisha mwanadamu na viumbe wengine. Lakini ikiwa k**a wanandoa hao watakosa fikara mathubuti na watakosa kutambua kile kinachowapasa kufanya juu ya ndoa yao , hakika uzoefu wa mapenzi utakuwa k**a pigo kubwa kwao, mathalani kwa wale ambao ni wahoga. Kwakweli matokeo yake huwa ni matokeo yasiyo na furaha , na pengine inaweza pia ikaongeza wimbi kubwa la hofu na uoga.
Lakini mengi hutegemea na jinsi gani marekebisho yanafanywa wakati wa mapumziko ya wanandoa (Honeymoon), kwa sababu hapa ndio wakati sahihi kabisa wa kujenga msingi wa ndoa yenye mafanikio. Ndoa nyingi zinazoshindwa hutokana na kukosa ufahamu wa jukumu lako na kukosa maelezo sahihi na ya msingi katika kujenga ndoa. Baadhi ya wanandoa wachanga walipotoshwa katika maelekezo na mwisho wa siku wanajikuta katika mkondo wa kujuta au kuona wamekosea pindi wanapokumbuka yale mahusiano mengine. Hii itatia doa katika mwenendo na mtazamo mzima wa maisha na kupelekea mkandamizo mkubwa ambao unaweza kupelekea kupoa na kukosa hisia na kutoelewana na mwenza wako. Watu hawa watakuwa na mwenendo wa kinafiki baina yao, na matokeo yake hata ndoa yenyewe itakuwa imepoteza uhalisia wake. Suruhu pekee kwa tatizo hili ni muhimu kabisa kujikubali na kujiamini kikamilifu na kukubaliana na dhana kamili ya maisha mapya.
Ingawa ni kweli kabisa kuna wanandoa wengine wanaishi pamoja wakiwa na fikira na mitizamo tofauti kabisa kuhusu swala la tendo la ndoa, ila hawa katika ujumla wake ni wachache sana katika hali hiyo isiyo ya kawaida. Kwakweli katika hatua hii ndipo hasa ndoa nyingi zinazoshindwa kuendelea huwa zinakwamishwa na kigingi hiki. Madaktari pia wanashauriwa kulikumbuka hili, maana magonjwa mengi makubwa au yanayotesa watu hapa ndipo hasa chimbuko lake.
Maharifa ya kina katika anatomy ya binadamu na fiziolojia itasaidia kutatua baadhi ya haya matatizo yanayotokea kati ya mume na mke. Kila mmoja lazima atambue kwamba tendo la ndoa ni kitu cha msingi na cha kawaida kwa wanandoa katika maisha, k**a vile kupumua, kula au kulala. Katika mazingira sahihi ya tendo hili kusiwepo yoyote wa kusababisha kero kwa mwenzake. Lakini ikumbukwe pia kiasi ni jambo la muhimu, ikiwa k**a kuna yeyote baina ya wenza hawa atahitaji tendo la ndoa kupitiliza viwango vya kawaida kwa mwenza wako vile anavyoweza kustahimili, ikumbukwe inaweza kuwasababishia udhaifu hata ugonjwa katika afya.

MAANA KAMILI YA NDOANdoa imetafsiriwa vizuri k**a ni “ mfumo wa kwanza wa utawala wenye pande mbili uliobuniwa kiupekee ...
22/03/2021

MAANA KAMILI YA NDOA

Ndoa imetafsiriwa vizuri k**a ni “ mfumo wa kwanza wa utawala wenye pande mbili uliobuniwa kiupekee zaidi.” Hii ndio maana nzuri kabisa ya ndoa, kamwe ndoa haikutegemewa iwe na sura yanye maazimio yenye pande moja. Ni kawaida inachukua watu wawili tofauti ambao ndio wanaotengeneza ndoa yenye mafanikio kamil, lakini kwa bahati mbaya mara kadhaa ndoa imekuwa ikitawaliwa na mtu mmoja tu, kwa kupuuzia au ubinafsi ambao mwisho wake unaharibu mantiki halisi ya ndoa.

Katika mahusiano yote ya wanadamu ndoa ndio imekuwa na umuhimu zaidi ya vyote. Ni kimoja tu chapaswa kutangulizwa nacho hicho ni mahusiano yenye umoja katika Mungu. Kwa sababu hiyo sio vyema mtu akashawishika kuingia katika mahusiano ya ndoa kiholela au kijuu juu tu. Kwani kuna vitu vingi ndani yake ambavyo utapaswa kukutana navyo ambavyo ukivijua namna ya kuenenda navyo vitakupa furaha na k**a hukuvijua namna ya kuenenda navyo vinaweza kukuachia maumivu na kutoelewana. Furaha halisi ya mahusiano haijengwi tu kutokana na wapenzi wawili kuendana, lakini furaha halisi hujengwa pia kutokana na wawili hao jinsi gani wanahusiana na kushik**ana pamoja na kupeana umakini na upendo pasipo kuchoka. Kwa maneno mengine wawili hao lazima wapatane katika maisha yao yote ya mapenzi. Pia wawili hao ni kwamba wanatakiwa wawe katika afya njema itayowawezesha wao kupata watoto wenye afya njema, lakini kitu cha muhimu kabisa ni kwamba wawili hao wanapaswa kutengeneza anga lenye furaha na upendo na nia njema katika nyumba.

Ndoa iliyofanikiwa ni ndoa ambayo inaundwa na watu wawili tofauti kabisa katika malezi na makuzi pamoja na fikala na wawili hao wanaunganika pamoja maisha yao na kuwa kitu kimoja kinachokwenda kwa ufanisi na mafanikio makubwa kwani kwa muungano wao wataweza kufanya vitu vikubwa na vya pekee kwa mafanikio makubwa tofauti kabisa ambavyo kwa mtu mmoja k**a angevifanya mwenyewe.

Ndoa ni tukio kubwa sana kwa wale ambao ni wachanga katika fahamu na mioyo. Kuna vitu vingi sana vya kufanya, kuna maeneo mengi sana ambayo utapaswa kuyaona na kuna furaha nyingi sana ambazo mtazipitia na kuzifanya kwa pamoja. Pengine kubwa kabisa kuliko vyote ni furaha ya kufanya tendo la ndoa kwa uhuru kabisa. Hivyo kikubwa kinachojenga nyumba na furaha ni mahusiano yenye kuridhishana na kutoshelezana na kutoshelezwa. Kwa upande ungine hakuna kitu kinachosababisha matatizo mkubwa k**a kushindwa kutambua kwamba hili ni jukumu la kawaida kabisa tangu mwanadamu amekuwepo, kwa hakika hii ni sehemu ya pekee na ya msingi kabisa katika ndoa nzima. K**a hautaona busara ya hili eneo ni wazi kabisa bado hauko tayari kuingia katika ndoa halisi.

Tendo la ndoa kwa wanyama wadogo na jamii nyingine za viumbe wadogo limekuwa na kusudi moja tu la kutunza kizazi chao kwa njia ya kuzaana, kwa gharama yoyote. Kuna jamii Fulani ya viumbe kitoto kinapofikia hatua tu ya kuweza kula basi wazazi hawana tena jukumu la kukiangalia hicho kitoto chao. Katika hatua hiyo mahusiano ya hiyo familia ndio hapo yanakuwa yamefikia mwisho wake na wazazi hawamtambui tena huyo mototo wao. Katika jamii nyingine za viumbe baba kamwe hamuoni mtoto wake lakini pia kuna jamii nyingine za viumbe hata mama anakuwa hayupo pindi watoto wake wanapoangulia kutoka katika mayai.

Hii iko tofauti kabisa katika familia ya mwanadamu, mtoto mdogo aliyezaliwa anakuwa taratibu taratibu akipitia hatua mbalimbali mpaka aje afikie hatua na umri wa kujitegemea. Hii inafaida kubwa kwani hutuwezesha wanafamilia wote kushik**ana kwa pamoja kwa muda wa miaka mingi wakati watoto wakiendelea kukuwa. Lakini wakati ungine huu ushirika wa pamoja unaweza kuwa shida na kuleta matatizo makubwa kabisa hasa pale kunapokuwepo na hali ya mpasuko mkubwa wa kutoelewana nyumbani. Hii huwa ni pigo kubwa sana kwa watoto pindi ubinafsi unapotawala sehemu moja yaani mzazi mmoja au wanapopatwa na ubinafsi huo wazazi wote wawili wakati kila mmoja akiangaika kutimiza tamaa zake kinyume na mwenzake katika vita hiyo maumivu na matatizo makubwa yote huishia kuwapata watoto.

Kuna wengine wanaamini kwamba maisha yanapaswa kuendelea kwa mujibu wa sheria za mwituni kwamba mwenye nguvu mpishe. Kwamba hisia za kibinadamu sio muhimu sana kuzingatiwa, ila ijulikane wazi kwamba dhana hii sio sahihi kabisa. Ikumbukwe mtu aliumbwa kwa mfano na kwa sura ya Mungu na akawekwa katibu bustani nzuri kabisa aishi pawe nyumbani kwake, wala hakuwekwa sehemu ya ovyo, jangwani, au sehemu pasipo na sheria na taratibu au nyikani au mwituni ambako angeishi kwa sheria ya mwenye nguvu mpishe. Japo ni sahihi mwituni kuna maisha pia ila ikumbukwe wazi kwamba huko hakuna furaha ya kweli.

Amani na furaha ya kweli nyumbani hutokana na utii na kuheshimiana katika taratibu zetu nyumbani pasipo kuoneana wala kudharauliana.

BOSI NI NANI KATIKA NYUMBA YAKO?(SEHEMU YA 1)Bosi ni nani katika familia yako?  Mara nyingi hili ni swali lenye mvuto sa...
25/02/2021

BOSI NI NANI KATIKA NYUMBA YAKO?(SEHEMU YA 1)
Bosi ni nani katika familia yako? Mara nyingi hili ni swali lenye mvuto sana. Jibu linategemea vile tunavyotafsiri neno bosi. Kamusi hutupatia maana kadha wa kadha k**a vile bosi ni msimamizi, muongozaji(Kiongozi), mtendaji, meneja na mengineyo. Hii inaonesha kwamba kumbe katika biashara yoyote lazima kuwepo na mtu mmoja ambaye ndiye anayefanya maamuzi ya mwisho, hii ni sahihi hata katika familia na nyumba zetu. Lazima kuwepo na mtu mmoja ambaye ndiye atachukua jukumu zima la kufanya maamuzi ya mwisho katika ustawi wa familia. Pasipo hili hakutakuwa na chochote ambacho kitakamilishwa katika sura inayotakiwa. Kuwa kichwa au kiongozi wa familia haina maana kwamba wewe ndiye mwenye haki ya kuwa jeuri na katili pasipo kujali hisia za wengine.

SERIKALI YA KIFAMILIA
Serikali ya kifamilia ni ya muhimu sana wakati wote. Lakini ni k**a vile katika serikali nyinginezo zote kumbuka wakati wote kutakuwa na tofauti ya mawazo na fikra, hivyo ndivyo itakavyokuwa katika nyumba au familia. Inasemwa kwamba sio vizuri kwa chama kimoja kukaa madarakani wakati wote, pia sio vizuri katika familia au nyumba mtu mmoja ndiye awe anatoa miongozo yote na kupanga mipango yote pekeyake. Mawazo tofauti ni bora zaidi kwa wahusika wote. Tofauti ya mawazo inasaidia sana, japo mara chache inaweza kupelekea kutokea mtafaluku na mvutano kidogo. Haya yote yanaweza kushughurikiwa kikamilifu ikiwa kwamba kila mmoja ana utayari wa kusikiliza na kuona mawazo ya mwenzake . Hii ndio siri kubwa ya serikali bora ya kifamilia.
Vile tunavyosikiliza kwa wengine, tunaweza kuingia kwenye mtego wa kujaribiwa kuhitimisha kwamba ndoa ni safari ndefu, mahaba ya furaha ambayo yanaguswa na mawingu machache angani. Hata hivyo haya yote si kitu. Kimsingi kuna kuwepo na tofauti ambazo lazima zitafutiwe suruhu. Wengi wetu hatuoneshi kuzingatia kwa sehemu au kikamilifu, hatimaye tunaamua kuchukua na kushika njia zetu wenyewe. K**a baadhi ya mashairi yasemavyo:

“ Ninaona mawazo mawili tu—
Wazo la kwanza ambalo sio sahihi na lile wazo langu”

Wakati wote tumekuwa watu wa kuhangaika kuonesha kwamba mawazo yetu ni sahihi zaidi, na sio kutambua kwamba watu wengine wako sahihi.
Haya matakwa ya kuamua kushika njia zetu wenyewe wakati Fulani hujitokeza kutokana na hofu iliyofichika kwamba mwisho wa siku nitaishiwa kuzalauriwa. Zaidi ya kitu chochote ulimwenguni tunaogopa sana kuzalauriwa. Hii yaweza kuwa sawa utotoni . Tunaona baadhi ya watoto huishi na kutenda vibaya katika makundi yao, hakuna sababu ingine isipokuwa hamu yake ni kwamba aweze kutambulika ama kuonekana. Mtoto yuko tayari kuadhibiwa ila haja yake itayomridhisha richa ya adhabu yoyote atayopatiwa ni kwamba aweze kutambulika na kupewa umakini ule alikuwa anautaka toka kwa wale wanaomzunguka. Anapofanikiwa katika hili basi hiyo siku nzima ataishi vizuri mpaka siku nyingine tena atapoingiwa na mawazo yakutaka kutambulika na kukubalika zaidi.
Hii ndio sababu kubwa inayopelekea kujitokeze baadhi ya hali ambazo hazifurahishi majumbani kwetu. Ikumbukwe kwamba hata wazo dogo la wazazi nyumbani siku zote litaweza kutatua hata matatizo makubwa. Hata hivyo mzazi hapaswi kuiangusha au kutoitendea haki nafasi yake ya utawala na maamuzi kwasababu tu anataka kumpendea mtoto, hii haita msaidia mtoto zaidi ya kumuongezea hofu na kutojiamini kutakojifichi ndani yake na kuendelea kumtisha siku zote. Kumbuka kwamba tabia mbaya ina mwito mkubwa na mvuto zaidi kuliko tabia njema, hivyo ni muhimu sana kujua ni kwanini mtoto anafanya hivyo hii ni hatua nzuri ya kuweza kuendelea mbele kumsaidia mtoto ili aweze kujengeka vyema katika fikra sahihi na yeye aweze kujiamini.
Hili pia linapelekea kuibua swali ni nani bosi katika familia au nyumba yako? Je ni nani anayetoa amri zote nyumbani? Je ni nani anayebeba majukumu yote nyumbani?

Tutaendelea na hii makala ndani ya siku tatu zijazo.

KUZUIA MSONGO WA MAWAZOTatizo kubwa la msongo lililoshamili leo linatokana na kutelekezwa katika kipindi cha utoto pale ...
22/02/2021

KUZUIA MSONGO WA MAWAZO
Tatizo kubwa la msongo lililoshamili leo linatokana na kutelekezwa katika kipindi cha utoto pale ulipohitaji malezi na joto la upendo la kutosha toka kwa wazazi au walezi na bahati mbaya likakosekana. Hili janga kwa sehemu kubwa limesababishwa na kutalakiana wanandoa au wazazi. Kutoa au kutaka talaka limekuwa ni jambo la kawaida sana sehemu nyingi duniani. Ila hili ni janga pindi kunapohusisha watoto wa wazazi hao wanaopeana taraka. Kwa ukweli sio wazazi wanaohumia pindi nyumba inapofunjika bali wanaohumia zaidi ni watoto. K**a watu wengi wangelitambua hili wangefikiri kwa makini kabla tofauti zao hazijafika hatua ya kutorudi nyuma.
Nini maana ya nyumba yenye furaha? Ni sehemu ambayo kila mwanafamilia anahisi anapendwa na anahitajika. Mahali hapo ni sehemu ambayo mtoto wakati wote anahakikishiwa kukubalika na wale wampendao. Hari hii itamjengea mtoto hisia sahihi za usalama na upendo. Katika mazingira k**a haya humpatia mtoto kujifunza thamani halisi ya maisha. Katika mazingira haya daima yatamsahaurisha mtoto dhahama na mitafaluku yote yaliyoko duniani.

Huyo mwanao anahitaji wazazi ambao atawapenda na kuwaamini. Anahitaji kuhisi hivyo hata k**a kutatokea shida au tatizo la kiwango gani, wazazi lazima waoneshe upendo na kumthamini, ingiwa sio mara zote wazazi hukubaliana na mtazamo wa mtoto. Maana ni muhimu kumfanya mtoto afurahie na kuona nyumbani ndio sehemu yake ya pekee inayompa furaha na amani. K**a katika umri mdogo mtoto atakuwa katika mazingira ambayo kwake hakuna kufanyiwa ukatili, ubabe, maonezi na kupingwa kwa ukali katika kila wazo analotoa au kufikiri, kina na upana wa uaminifu wake utazidi kuongezeka jinsi vile anavyokuwa na kuongezeka umri. Pia wakati huo huo hata upendo kwa wale awapendao utaongezeka pia.
Mtoto aliyejariwa kuishi katika mazingira haya ya upendo mara nyingi hata wimbi kubwa la matatizo na migongano ya kutoelewana pindi linapofuma hata kumzingira mara nyingi yeye atasimama imara pasipokuyumbishwa. Bado atakuwa na hakika ya watu wake wa karibu, shida na matatizo ambayo huwaangusha watu wengi kwake hayataweza kupata nafasi ya kumdondosha. Je ni kwanini? Ni kwa sababu ya hisia kubwa ya usalama na uaminifu iliyojengwakatika utu wake hasa katika kipindi cha muhimu alipokuwa katika umri mdogo. Japo maisha yake yajayo hayajulikani, lakini hataogopa , kwani akili yake imejengwa barabara na wazani wake ambao kwa pamoja wanashirikiana na wakimtumaini Mungu pia.
Kumbuka hili: wazazi wenye furaha ndio wajengao nyumba/familia yenye furaha. Nyumba yenye furaha ndio huzalisha watoto wenye furaha. Watoto wenye furaha ndio chanzo cha jamii iliyo na furaha. Jamii zilizo na furaha ndizo hujenga dunia iliyo na furaha.

KUTENGENEZA NYUMBA YENYE FURAHAJe kuna neno zuri Zaidi ya neon nyumbani katika lugha yoyote? Je kuna sehemu yoyote iliyo...
19/01/2021

KUTENGENEZA NYUMBA YENYE FURAHA
Je kuna neno zuri Zaidi ya neon nyumbani katika lugha yoyote? Je kuna sehemu yoyote iliyonzuri na ya kupendeza na kuridhisha moyo wa mtu Zaidi ya nyumbani? Mahali popote tuendapo, mawazo yetu daima hubaki yameegemea sehemu moja ambayo hiyo tutaweza kuita kwetu. Hatak**a mawazo yetu na ndoto zetu zimekuwako mahali hapo kwa unyenyekevu na kwa dhati kabisa. Aihitaji kwamba pawe ni mahali penye jumba kubwa la kifahari lililojengwa vizuri na kunakshiwa kwa ufundi na umalidadi mkubwa unaopelekea kuwepo mvuto na muonekano mzuri unaopendeza macho ya kila mtu. Japo hii ni ya muhimu k**a nafasi na mazingira yanakuruhusu kufanikisha hayo, ila haya yote sio ya msingi katika kuleta na kudumisha furaha ya kweli ya mtu. Ila ni k**a mashairi yanavyosema:

”Ni mahali pazuri mno
Hakuna mahali pazuri k**a nyumbani.”

Aina ya nyumbani hapa ni mahali panapotukinga na kutuhifadhi salama zidi ya dhoruba zote za maisha. Hakika mahali hapa ni sehemu moja ambayo familia itafurahia hari ya hewa ya Amani na furaha pamoja na pumziko zuri la moyo. Hapa nyumbani ndipo mahali hasa panapotupa maana ya kina ya kila tunachokifanya, kila tunachokizungumza au pia kila tunachokifikiri. Pia k**a mahali hapo pamebarikiwa kuweko watoto nao watakuwa wakikua vijana wenye furaha na upendo, kwakweli katika dunia hakuna mahali palipo na furaha na upendo wa kweli k**a mahali hapa.

Kujenga nyumba yenye furaha sio kitu rahisi. K**a nyumba itakuwa yenye mafanikio, inahitaji mipango na mikakati mikubwa naya dhati ambapo kila mwanafamilia atahusishwa. Wala hakuna swali ni dhairi kwamba nyumba zetu zilizo nyingi ni kweli ni nzuri na zimejengwa kisasa na zinafutia mno kwa macho lakini baadhi ya hizo nyumba zinakosa furaha ya kweli. Ila tatizo sio nyumba. Ni kweli nyumba inaweza jengwa na kunakshiwa vizuri kwa marembo ya thamani na yaliyopangiliwa vizuri katika kuta zake, paa lake, madirisha yake na milango yake ila hayo yote hayakuhakikishii furaha ya kweli katika hiyo nyumba. Kwa kweli watu wanaoishi ndani ya nyumba hiyo ndio wamuhimu kuliko hata marembo na nakshi zote pamoja na hiyo nyumba yenyewe, kuna wakati mwingine katika jamii zetu kuna watu wanatoka katika familia zilizo na majumba mazuri lakini wamekuwa ni watu wasiokuwa na furaha hata kidogo wala Amani katika maisha yao tofauti na vile tunavyowatamania na kuwaona.


Kila kitu kinategemea mitazamo ya wale wanaoishi katika nyumba. K**a kila mwanafamilia atakuwa na hari na muonekano wa furaha katika maisha yao, hakika hapo kutakuwa na hari ya hewa inayonurulishwa na joto la furaha na upendo unaoshamiri katika kila chumba cha mwanafamilia. Ila k**a baadhi ya wanafamilia wamekuwa watu wenye huzuni na manun’guniko katika mioyo yao, hasira
na chuki itashamiri na kuonekana katika kila wanapozungumza na kile wanachokitenda. Furaha ya kweli haiko katika wingi wa mali za dunia ambazo mtu anazimiliki, bali hupatikana katika moyo ulioridhika na wenye Amani ya kweli. Watu wengine hukosa furaha hata k**a watamiliki mali na utajiri wa namna gani bali wengine hufurahia maisha katika furaha kamili japo wanamiliki utajiri kidogo sana.

Address

P. O. Box 1279
Mbeya
0000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Triple Sha Health & Consultation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram