01/03/2026
NIMEKOMBOLEWA NA KUTUMWA KUTANGAZA HABARI NJEMA ZA WOKOVU KWA WATU WOTE.
Chukua Muda wako Leo soma kitabu cha Marko sura ya 5 msitari wa 1-20.
Utapata habari njema ya Mtu aliyekuwa anaishi makaburini baada ya kuponywa na Yesu, aliomba kuambatana na Yesu lakini Yesu alimwambia Aende nyumbani kwao kwa watu wa kwao kuhubiri yale ambayo ametendewa na Yesu.
Kimsingi alifanya hivyo akihubiri katika miji kumi (Dekapoli inamaanisha Miji kumi).
Kuna mengi ya khjjifnlzal katika habari njema hiyo.
Mimi na wewe ambaye umemjua Yesu wa Nazareti, tumeitwa ili tuwaite wengine kwa Yesu.
Swali je, Tangu umemjua Yesu Mpaka leo umewaleta wangapi kwa Yesu?