Neighbor's Pharmacy

Neighbor's Pharmacy NEIGHBOR'S pharmacy Ni wauzaji Wa Dawa za Binadamu na vifaa tiba.
ipo Shinyanga mjini mkabala na Benki ya NMB manonga house.
(1)

Karbuni sana Wateja wetu. Feel free to contact us any time any hour

06/11/2025

Ndugu zangu Watanzania,

Kwa moyo wa huzuni na majonzi makubwa, natoa pole za dhati kwa familia, ndugu, na marafiki wa wale wote waliopoteza maisha, kujeruhiwa, au kuathiriwa kwa namna yoyote kufuatia vurugu na ghasia zilizojitokeza tarehe 29 Oktoba 2025. Tukio hili limeacha alama ya maumivu katika mioyo ya wengi, hasa pale tunaposhuhudia vijana—nguvu kazi na matumaini ya taifa letu—wakiwa miongoni mwa waliopoteza maisha.

Ni wakati wa taifa letu kutafakari kwa kina juu ya thamani ya amani, umoja, na utu. Vurugu hazijawahi kuwa suluhisho; bali mazungumzo, busara, na huruma ndizo nguzo zinazojenga nchi imara. Wito wangu kwa Watanzania wote, hasa vijana, ni kuendelea kudumisha utulivu, kuheshimiana, na kutafuta njia za amani katika kutatua tofauti zetu.

Tuwaombee waliopoteza maisha wapumzike kwa amani, na tuendelee kuwaombea waliopoteza wapendwa wao wapate faraja na nguvu mpya.
Mungu aibariki Tanzania.
Mungu atulinde sote.


Mwalimu, Mwandishi na Mpenda Amani.

05/11/2025

Tuikumbukeni sauti ya mwalimu — sauti tuliyoizoea kama taa ya hekima na daraja la umoja.

Tuienzi, tuiige, na tuiweke mbele kama mfano wa uongozi wenye busara, uthabiti na moyo wa kuunganisha watu bila kujali kabila, dini, wala tamaduni.

Tusiruhusu matamanio binafsi kuyapofusha maono ya utu.

Utu uwe dira yetu; maadili, nguzo yetu; upendo wetu, na urithi wetu.

Tuipende Tanzania, tuilinde na tusiiruhusu igawanyike kwa sababu ya madaraka.
Hofu ya Mungu na hekima ya moyo vituongoze katika kila hatua ya ujenzi wa taifa letu.

28/10/2025
28/10/2025

Every Child Matters — Every Action Counts.
Inclusiveness with accountability creates lasting change.

26/10/2025

✍️Utambuzi wa mapema wa mahitaji maalumu ya watoto ni nguzo ya mafanikio katika ujifunzaji wao.
Kadiri mtoto anavyotambuliwa mapema, ndivyo walimu, wazazi na jamii wanavyoweza kuandaa mazingira rafiki, salama na yanayojali tofauti zake.

Mtoto mwenye mahitaji maalumu hahitaji huruma — anahitaji uelewa, msaada sahihi na fursa ya kuonesha uwezo wake.
Tuchukue hatua leo kutambua, kuelewa na kusaidia kila mtoto kwa wakati,
ili elimu iwe kweli jumuishi na yenye kuleta matumaini kwa wote.
HakiElimu Tanzania Education Network/ Mtandao Wa Elimu Tanzania Early Childhood Education and Development

23/10/2025

Elimu jumuishi ni daraja la usawa wa kielimu baina ya watoto wote bila kujali tofauti zao.
Kila mtoto anakuwa na ushiriki sawa katika shughuli za kielimu kwa kuwekewa mazingira wezeshi na rafiki ya ujifunzaji.

23/10/2025

Uwepo wa mazingira rafiki na salama ya ujifunzaji wa mtoto kuanzia nyumbani mpaka shuleni, huongeza ufanisi zaidi katika ujifunzaji wa mtoto na kumpa uwanda mpana wa kuonyesha uwezo wake katika ujifunzaji na hata ubunifu.

22/10/2025

🤔Je? Sera yetu ya Elimu inatafsirika kwa vitendo kukidhi matarajio ya dira ya maendeleo ya taifa ?

14/10/2025

Ukombozi wa kweli hauji kwa silaha, bali kwa elimu yenye utu na fikra huru.

14/10/2025

Elimu sambamba na hekima ya maisha

Address

Mitimirefu Street, Uhuru Road-Near NMB Bank
Shinyanga
P.O.BOX39

Telephone

+255765460577

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neighbor's Pharmacy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Neighbor's Pharmacy:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram