26/01/2026
“Mimba yangu ya mwisho hii… sitakuja kuzaa tena.”
Maneno haya husikika kwa wanawake wengi waliopitia shida nzito za mimba — presha ya mimba, kutokwa damu, upasuaji mgumu, kupoteza mimba au uchungu wa muda mrefu.
Ni hisia za kweli. Lakini pia ni muhimu kujua:
👉🏽 Si kila hofu ni mwisho wa safari ya uzazi
👉🏽 Changamoto nyingi za mimba zinaeleweka kitabibu na zinaweza kudhibitiwa kwa ufuatiliaji sahihi
👉🏽 Uamuzi wa kuzaa au kutozaa unahitaji taarifa sahihi, si hofu pekee
Mapendekezo ya kiafya:
✔️ Fanya tathmini ya afya kabla ya mimba (preconception check)
✔️ Zungumza na mtaalamu kuhusu historia yako ya mimba
✔️ Dhibiti magonjwa sugu mapema (presha, kisukari, upungufu wa damu)
✔️ Pata elimu sahihi kabla ya kufanya uamuzi mkubwa
📌 Uzazi salama unaanza na elimu + ufuatiliaji + maamuzi yenye taarifa.
📍 Tunapatikana Zanzibar na mikoa yote ya Tanzania
📞 0787677932
📲