Lubonji Wa Lubonji

Lubonji Wa Lubonji L.W.L MUSIC & INTERNATIONAL NEWS

JB MPIANA ATOA ONYO: HAHUSIKI NA TAMASHA LA LA CIGALEJB MPIANA DÉMENT TOUTE IMPLICATION DANS LE CONCERT ANNONCÉ À LA CIG...
22/02/2026

JB MPIANA ATOA ONYO: HAHUSIKI NA TAMASHA LA LA CIGALE
JB MPIANA DÉMENT TOUTE IMPLICATION DANS LE CONCERT ANNONCÉ À LA CIGALE

Katika hali ya kuweka mambo wazi kwa umma, ni muhimu kufahamisha kwamba JB Mpiana hahusiki kabisa na tamasha linalodaiwa kufanyika Jijini Paris kwenye Ukumbi wa (La Cigale) siku ya Jumamosi iliopita tarehe 21 Februari 2026.
Hakuna ushirikiano, ushiriki, wala mpango wowote wa kisanii aliowahi kuthibitisha kuhusu tukio hilo, ambalo tangazo lake limesambaa bila msingi wowote kasema "Roger Ngandu" Msemaji wa Group Wenge BCBG.

Akitambua mapenzi makubwa anayopata kutoka kwa wapenzi wa muziki hasa kwa Mashabiki wake, JB Mpiana anawaomba wote kuwa waangalifu sana dhidi ya taarifa zisizothibitishwa zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii na vyanzo visivyo rasmi.

Anakumbusha kwamba taarifa zote rasmi kuhusu Show zake, ziara zake aidha miradi yake ya Kisanii hutolewa tu kupitia njia zake halali na timu yake ya usimamizi.

Katika mazingira ya habari ambapo uvumi unasambaa kwa kasi kuliko ukweli, Msanii anawahimiza mashabiki kuwa makini sana, kuthibitisha vyanzo vya taarifa, na kutegemea tu matangazo yaliyo rasmi.
Ujumbe huu unalenga kuwalinda Wapenzi wa muziki dhidi ya mkanganyiko na kurejesha ukweli kwa heshima na umakini unaostahili.

JB MPIANA MET EN GARDE : IL N’EST AUCUNEMENT ASSOCIÉ AU CONCERT ANNONCÉ À LA CIGALE
JB MPIANA DÉMENT TOUTE IMPLICATION DANS LE CONCERT ANNONCÉ À LA CIGALE
Dans un souci de transparence et afin d’éclairer l’opinion publique, il convient de préciser que JB Mpiana n’a absolument aucun lien avec le concert prétendument programmé à Paris, dans la salle de La Cigale, le samedi 21 février 2026.
Aucune collaboration, aucun engagement artistique, ni même la moindre intention de participation n’ont été confirmés par l’artiste au sujet de cet événement dont l’annonce circule sans fondement.
C’est ce qu’a rappelé avec fermeté Roger Ngandu, porte-parole du groupe Wenge BCBG.

Conscient de l’affection profonde que lui portent les mélomanes — et plus particulièrement ses fidèles admirateurs — JB Mpiana appelle chacun à la plus grande prudence face aux informations non vérifiées qui prolifèrent sur les réseaux sociaux et dans divers circuits informels.

Il rappelle que toute communication officielle relative à ses spectacles, à ses tournées ou à ses projets artistiques n’émane que de ses canaux légitimes et de son équipe de management dûment mandatée.

Dans un environnement médiatique où la rumeur circule plus rapidement que la vérité, l’artiste exhorte le public à demeurer vigilant, à vérifier systématiquement les sources et à ne se fier qu’aux annonces authentifiées.
Ce message vise à protéger les mélomanes de toute confusion et à rétablir la vérité avec la dignité, la rigueur et la clarté qui s’imposent.

BABA L.W.L

FALLY IPUPA AMFUFUA KIHESHIMA MWANAMUZIKI MKONGWE FRANCO LUAMBOFRANCO LUAMBO COURONNÉ À TITRE POSTHUME PAR FALLY IPUPA 1...
22/02/2026

FALLY IPUPA AMFUFUA KIHESHIMA MWANAMUZIKI MKONGWE FRANCO LUAMBO
FRANCO LUAMBO COURONNÉ À TITRE POSTHUME PAR FALLY IPUPA

1. Mwezi Agosti 2024, Jiji la Kinshasa ilishuhudia tukio lenye uzito wa kiishara: Fally Ipupa, Gwiji wa Muziki wa kisasa Inchini Congo, alimkabidhi kwa heshima kubwa "Franco Luambo Makiadi" tuzo ya dhahabu baada ya kifo chake.
Tuzo hiyo ilipokelewa na mwanawe, "Yves Emongo Luambo", ikifungua daraja kati ya vizazi na kuthibitisha mchango wa wale waliojenga urithi wa muziki wa Taifa.

2. Kufwatia kitendo hiki, "Fally Ipupa" alionyesha shukrani ya dhati kwa watangulizi wake mashuhuri, huku akishiriki mafanikio ya uboreshaji wake wa wimbo maarufu «Mario», alioupa jina jipya «Lady» katika albamu yake Formule 7 ya mwaka 2022.
Hatua hii ilikuwa jitihada ya kuzirudisha kazi za msingi katika kumbukumbu ya kizazi cha sasa.

3. Kibao «Mario» kilipotoka mwaka 1985, 'Franco Luambo Makiadi" alikuwa tayari amebadilisha kabisa hadhi ya Muziki wa Zaire kwa takriban miaka ishirini.
Akiwa Mrithi wa ubunifu wa kazi kutoka Group la (African Jazz) ya "Joseph Kabasele Grand Kalle" na (African Fiesta National) ya "Tabu Ley Rochereau" kadhalika (African Fiesta Sukisa) ya Dokta Nico Kasanda" hivyo kuanzisha mtindo mpya uliobebwa na kauli mbiu ya Group (Tout-Puissant OK Jazz) : «Unaingia OK, unatoka KO». Sebene, lenye mitiririko ya gitaa yenye nguvu, likawa uti wa mgongo wa rumba iliyotengenezwa upya.

4. "Franco Luambo Makiadi" alikuwa pia kiongozi wa Group mwenye maono mapana sana, akiongoza Group lake lililoweza kutekeleza majukumu kadhaa kwa wakati mmoja.
Wanamuziki wengi mashuhuri k**a "Vicky Longomba" na "Sam Mangwana" walipitia katika Group hili, wakichangia utajiri na utofauti wa muziki wake.

5. Mwaka 1980, "Madilu System" alijiunga (TP OK JAZZ" na taratibu akawa mmoja wa nguzo zake, hasa kupitia mafanikio ya wimbo «Non», utunzi wa dakika kumi na tisa.
Humo alikutana na Magwiji wa gitaa k**a "Papa Noël" na "Dizzy Mandjeku", Majina makubwa katika Muziki wa Congo.

6. Niwakati akiwa pamoja na "Franco Luambo makiadi" ndipo "Madilu System" aliimba Wimbo ambao ulitokea kuwa Tube «Mario», Wimbo namba 1ulio ibeba Album ya jina hilo, na uliotawala upande mzima wa Santuru (Disc A) na kuchukua dakika kumi na tatu.
Tokea pale Wimbo (Mario) ulipowekwa Sokoni, ulikuja juu kileleni na kuzipiku nyimbo zote zilizokua sokoni kipindi kile kadhalika "Madilu System" akatokea kuwa Mwimbaji bora hadi kupelekea nyota ya baadhi wakongwe kwenye Group kufifia.

7. Wimbo (Mario) uliaanza kwa sauti ya gitaa la mi-solo likishikiliwa na "Franco Luambo Makidi" Mwenyewe, kisha likafwatiwa na Gitaa rhythm la "Gégé Mangaya".
Huku "Nado Kakoma" akiwa kwenye Ngoma,, congas (zilizopigwa na "Dessoin Bosuma", "Decca Mpudi" Kwenye Bass Gita, vikiingiliana vizuri pindi tuu Rhytm Gitaa la "Mangaya" linaanza kupiga mkondo wake.
"Franco ndie anayetoa mistari ya mwanzo ya wimbo, kisha ufuatiwe na kiitikio kinachoimbwa na Madilu System.
Solo Gitaa likicharazwa na "Papa Noel Nedule".

8. Wimbo huu unasimulia, kwa ucheshi mkali na kejeli ya kuvutia, hadithi ya kijana anayelelewa na mwanamke, yaani Kijana kabebwa kimapenzi na Mwana mama mwenye umri mkubwa kumzidi. Maneno yake, yenye uhalisia mkali, yanaonyesha tabia, ujanja na masaibu ya gi**lo asiye kuwa na aibu ya kulelewa na Mwanamke, ambaye amekuwa mfano maarufu katika utamaduni wa Congo.

9. Zaidi ya simulizi, "Franco Luambo Makiadi" analeta pia ujumbe wa maadili, unaolingana na msimamo wa utawala wa Mobutu uliotaka kuzuia kupotoka kwa vijana waliokosa mwelekeo.
(Mario), Ni Kijana msomi asie na shughuli, Mtoto wa kijiweni, anageuka kuwa ishara ya ndoto za kijamii zisizo na msingi na kukataa kufanya juhudi.

10 .Umaarufu mkubwa wa wimbo huu ulimfanya "Franco Luambo Makiadi" aendeleze simulizi lake : toleo lingine lilifuata haraka, Mwaka 1987 pale alipotoa Wimbo (La Réponse de Mario ) yaani (Jibu la Mario).
Baada ya "Grand Maitre Franco Luambo makiadi" kufariki dunia mwaka 1989, matoleo mengi ya marudio ya Wimbo (Mario) yaliendelea kusambaa, yakidumisha hadithi hii.

11. Athari za (Mario) zilivuka mipaka ya Kongo.
Uliimbwa upya nchini Côte d’Ivoire, Angola, na kundi la Africando, pamoja na Ray Lema, na ukawa wimbo wa bara zima.
Ushawishi wake ni mkubwa kiasi kwamba katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jina «Mario» sasa linamaanisha mwanaume anayelelewa na mwanamke.

Version Française

FALLY IPUPA RÉHABILITE AVEC SOLENNITÉ LA MÉMOIRE DU MAESTRO FRANCO LUAMBO
FRANCO LUAMBO COURONNÉ À TITRE POSTHUME PAR FALLY IPUPA
1. En août 2024, la ville de Kinshasa fut le théâtre d’un événement d’une portée hautement symbolique : Fally Ipupa, figure majeure de la musique congolaise contemporaine, remit avec une solennité remarquable un disque d’or posthume à l’illustre Franco Luambo Makiadi.
La distinction fut reçue par son fils, Yves Emongo Luambo, consacrant ainsi un pont mémoriel entre les générations et réaffirmant la dette culturelle envers ceux qui ont façonné l’héritage musical de la Nation.

2. À travers ce geste empreint de respect, Fally Ipupa exprimait une gratitude profonde envers ses prestigieux prédécesseurs, tout en partageant le succès de sa réinterprétation du classique «Mario», rebaptisé «Lady» dans son album Formule 7 paru en 2022.
Cette initiative s’inscrivait dans une volonté claire de réinscrire les œuvres fondatrices dans la conscience culturelle du public contemporain.

3. Lorsque le titre «Mario» parut en 1985, Franco Luambo Makiadi avait déjà révolutionné le paysage musical zaïrois depuis près de deux décennies.
Héritier des innovations de l’African Jazz de Joseph Kabasele «Grand Kallé», de l’African Fiesta National de Tabu Ley Rochereau, ainsi que de l’African Fiesta Sukisa de Docteur Nico Kasanda, il imposa une esthétique nouvelle, portée par la devise percutante de son Tout-Puissant OK Jazz : «On entre OK, on sort KO».
Le sébène, avec ses envolées de guitare vigoureuses, devint l’ossature d’une rumba magistralement renouvelée.

4. Franco Luambo Makiadi fut également un chef d’orchestre visionnaire, dirigeant une formation capable de répondre simultanément à plusieurs engagements.
Des artistes de renom tels que Vicky Longomba ou Sam Mangwana y firent leurs armes, contribuant à l’extraordinaire richesse et diversité du répertoire du groupe.

5. En 1980, Madilu System rejoignit le Tout-Puissant OK Jazz et s’y imposa progressivement, notamment grâce au succès retentissant du morceau «Non», une composition fleuve de dix-neuf minutes.
Il y côtoya des Maîtres de la guitare tels que Papa Noël et Dizzy Mandjeku, figures incontournables de la musique congolaise.

6. C’est aux côtés de Franco Luambo Makiadi que Madilu System interpréta le titre qui deviendrait un véritable tube : «Mario».
Pièce maîtresse de l’album éponyme, le morceau occupait à lui seul l’intégralité de la face A du 33 tours, avec une durée de treize minutes.
Dès sa mise sur le marché, «Mario» s’imposa au sommet, éclipsant les autres titres en circulation et propulsant Madilu au rang de voix dominante du groupe, reléguant certains anciens membres au second plan.

7. Le morceau «Mario» s’ouvre sur les notes incisives de la guitare mi-solo, exécutées par Franco lui-même, suivies du jeu rythmique de Gégé Mangaya.
Nado Kakoma assurait les percussions, tandis que les congas étaient tenues par Dessoin Bosuma ; Decca Mpudi soutenait l’ensemble à la basse, créant une harmonie parfaite dès l’entrée du rythme de Mangaya.
Franco lançait les premières lignes du chant, immédiatement relayées par le refrain interprété par Madilu System.
La guitare solo, quant à elle, était magistralement assurée par Papa Noël Nedule.

8. Le morceau raconte, avec une ironie mordante et un humour savoureux, l’histoire d’un jeune homme entretenu par une femme plus âgée.
Les paroles, d’un réalisme saisissant, décrivent les manœuvres, les caprices et les mésaventures d’un gi**lo décomplexé, devenu une figure emblématique de l’imaginaire populaire congolais.

9. Au-delà de la narration, Franco Luambo Makiadi y insuffle une dimension morale, en parfaite résonance avec les préoccupations du régime de Mobutu, soucieux d’encadrer une jeunesse parfois en perte de repères.
Mario, étudiant diplômé mais oisif, devient ainsi le symbole des illusions sociales et du refus de l’effort.

10. Le succès phénoménal de Mario» incita Franco à prolonger la saga : une première variante fut rapidement publiée, suivie en 1987 de «La Réponse de Mario».
Après la disparition du Grand Maître en 1989, de nombreuses versions et réinterprétations continuèrent de circuler, perpétuant la légende.

11. L’influence de «Mario» dépassa largement les frontières du Congo.
Le morceau fut repris en Côte d’Ivoire, en Angola, par le collectif Africando ainsi que par Ray Lema, devenant un classique continental.
Son impact culturel est tel qu’en République démocratique du Congo, le prénom « Mario » désigne désormais, dans le langage courant, un homme entretenu par une femme.

BABA L.W.L

JB MPIANA SHOW YAKE NYINGINE YAFUTWA JIJINI PARIS Wakati tamasha la JB Mpiana kwenye ukumbi wa La Cigale ilitakiwa kufan...
21/02/2026

JB MPIANA
SHOW YAKE NYINGINE YAFUTWA JIJINI PARIS

Wakati tamasha la JB Mpiana kwenye ukumbi wa La Cigale ilitakiwa kufanyika leo tarehe 21 Februari 2026, Msanii huyo anaendelea kukaa kimya kana kwamba mambo hayamhusu.

Huku AEG ikitangaza kuanza kuuza tiketi tokea tarehe 5 Desemba 2025, hakuna taarifa yoyote rasmi kutoka kwake.

Matangazo matatu, ukimya mara tatu, na kufutwa mara tatu…

Je, huu ni mwanzo wa mvutano mpya kati yake na AEG/Mediacom?
Hivi sasa, anapaswa kujitokeza na kutoa kauli wazi, kwani hadhi yake ya kisanii na uaminifu wake kwa umma viko hatarini.

Version Française

Alors que le concert de JB Mpiana annoncé à La Cigale pour ce Samedi 21 février 2026 approche, L’Artiste persiste dans un silence énigmatique.

Pendant ce temps, AEG mettra en vente les billets dès le 5 décembre 2025, sans qu’aucune prise de parole officielle ne vienne éclairer le public.

Trois annonces successives,
Trois absences de communication,
Trois reports…
Faut‑il y voir les prémices d’un nouveau bras de fer avec AEG/Mediacom ?
À ce stade, une clarification s’impose : son autorité artistique comme sa crédibilité publique en dépendent.

Baba L.W.L

FERRE GOLA (Mwaka 1996) Akiwa na Group Wenge BCBG 4X4 FERRE GOLA Année 1996 avec Wenge Musica BCBG 4X4
21/02/2026

FERRE GOLA (Mwaka 1996) Akiwa na Group Wenge BCBG 4X4
FERRE GOLA Année 1996 avec Wenge Musica BCBG 4X4

"KOFFI OLOMIDE" NIKIFA MWILI WANGU UCHOMWEMwanamuziki mashuhuri na hodari Inchini Congo, Koffi Olomide, aliwaacha mashab...
20/02/2026

"KOFFI OLOMIDE" NIKIFA MWILI WANGU UCHOMWE

Mwanamuziki mashuhuri na hodari Inchini Congo, Koffi Olomide, aliwaacha mashabiki wake wakiwa na mshangao mkubwa alipotoa hotuba ya moja kwa moja kupitia TikTok jumapili iliyopita.
Kwa uwazi na utulivu wa kipekee, alieleza maoni yake kuhusu namna anavyotaka kuheshimiwa baada ya maisha yake kufikia tamati.

Mwandishi wa habari alipomuuliza angependa kuenziwa vipi baada ya kufariki, gwiji huyo wa rumba alitoa jibu lililojaa fikra za kina na unyenyekevu.
Alisema hatamani mazishi ya kawaida wala kaburi la kudumu, bali angependa mwili wake uchomwe moto na majivu yake yamiminwe majini ya mto Congo.

Akiendelea kufafanua, alisisitiza kuwa kumbukumbu yake isitafutwe kwenye kaburi, bali katika ishara ya kudumu na yenye thamani, k**a ilivyofanyika kwa marehemu Tabu Ley Rochereau na King Kester Emeneya.

Kwa mtazamo wake, kuipa barabara kuu jina lake kwa mfano kubadilisha jina Barabara kuu ya Jiji la Kinshasa "Boulevard du 30 Juin" na kuiita Boulevard Koffi Olomide au Boulevard Mopao kungekuwa njia bora, ya heshima na ya kudumu ya kuendeleza urithi wake katika fikra za mashabiki wake.

Version Française :

Le Musicien congolais "Koffi Olomide" a déconcerté plus d’un admirateur lors d’une intervention en direct diffusée sur TikTok dimanche dernier.

Avec une lucidité presque désarmante, il y a exposé la nature de ses dernières volontés, évoquant sans détour la manière dont il souhaite que son corps soit traité après sa disparition.

Invité par une journaliste à préciser la forme d’hommage qu’il jugerait appropriée une fois sa vie achevée, le maître incontesté de la rumba congolaise a livré une réponse d’une sobriété radicale. Il a déclaré ne souhaiter ni cérémonies funéraires ni sépulture, mais plutôt la crémation de sa dépouille, suivie de la dispersion de ses cendres dans les eaux du fleuve.

Poursuivant son propos, il a souligné qu’il préférait que sa mémoire ne soit pas attachée à un tombeau, mais à un geste symbolique et durable, à l’image des hommages rendus à "Tabu Ley Rochereau" ou à "King Kester Emeneya".

Selon lui, attribuer son Nom à une grande artère par exemple rebaptiser le boulevard du 30 Juin en «Boulevard Koffi Olomide» ou «Boulevard Mopao» constituerait une manière plus noble, plus pérenne et plus fidèle de préserver son souvenir dans la conscience de ses admirateurs.

BABA L.W.L

KOFF OLOMIDE MIAKA 26 BAADA YA SHOW YA BERCY JIJINI PARIS1. Tarehe 19 Februari 2026 inaadhimisha miaka ishirini na sita ...
19/02/2026

KOFF OLOMIDE MIAKA 26 BAADA YA SHOW YA BERCY JIJINI PARIS

1. Tarehe 19 Februari 2026 inaadhimisha miaka ishirini na sita tokea tukio ambalo limebaki kuwa mojawapo ya matukio muhimu zaidi katika historia ya Muziki wa Afrika.
Siku hiyo ya mwaka 2000, Msanii mmoja kutoka Congo alifanya jambo ambalo halijawahi kufanywa na Mwafrika yeyote kabla yake, na hivyo kubadilisha kabisa upeo wa Muziki wa bara hili.

2. Mnamo tarehe hiyo, Koffi Olomide ambae kwa Jina halisi hufaamika k**a "Antoine Agbepa Mumba" alikua Msanii wa kwanza wa Kiafrika kutumbuiza k**a Nyota Kuu na kuujaza ukumbi mzima wa (Palais Omnisports de Paris-Bercy), ambao kwa leo hii unajulikana k**a (Accor Arena).
Ukumbi huu mkubwa zaidi Jijini Paris ulijaa kwa zaidi ya Watu 18,000 kutoka pembe zote za Ulaya.

3. Diaspora ya Wakongo, ikiwa imeungana kwa hisia za fahari na mshik**ano, ilifurika Paris kwa wingi kumtia moyo Msanii aliyekuwa akiwakilisha ubora wa Muziki wa Afrika.
Tamasha hilo, lililopewa jina la Bercy 2000, lilifanikiwa kwa kiwango cha juu licha ya kutokuwa na kampeni kubwa ya matangazo.

4. Onyesho lilianza majira ya saa saba usiku na kuendelea hadi alfajiri, karibia Saa moja na nusu asubuhi.
Kwa zaidi ya saa sita, "Koffi Olomide" na Group lake la (Quartier Latin International) Walitoa burudani ya kiwango cha juu, iliyojumuisha uimbaji wa hali ya juu, uchezaji ulioratibiwa kwa ustadi na ubunifu wa Kisanii.

5. Kituo cha TV cha MCM Africa kilirekodi Show nzima moja kwa moja, huku Vituo vingine vya TV vikiwemo : France 2, M6 na Canal+ navyo vilikuwepo kulifuatilia Show.
Uwepo wa vyombo hivi vya habari ulithibitisha jinsi muziki wa Afrika ulivyokuwa ukipata nafasi kubwa katika majukwaa ya kimataifa.

6. Show hiyo liliwakaribisha Wageni waalikwa mashuhuri k**a : Roga Roga, Pepe Felly Manuaku, Stomy Bugsy, Passi na Group la Bisso Na Bisso, Coumba Gawlo, Nayanka Bell, Meiway na wengine wengi.
Mchanganyiko huu wa Wasanii uliongeza upeo wa panafrika na ulimwengu katika tukio hilo.

7. Jukwaani, Quartier Latin International liliangaza kwa nguvu zote. Mbali na "Koffi Olomide", kulikuwepo waimbaji k**a :
Fally Ipupa,
Jipson Butokondolo,
Mamale Tupac,
Lola Muana,
Eric Tutsi,
Savanet Depitcho,
Moustapha Nkori,
Jordan Kusa
na JF Ifonge.
Ma Rapa (Atalaku) kwa Uchangamshi wa jukwaa tutawapata :
CNN pamoja na Océan Zibankulu.

8. Kwa Upande wa ala za muziki ulihusisha wakongwe k**a :
Gitaa :
Felly Tyson,
Riddens Makoso
na Deba O’Nei.
Binda Bass na Clovis Silawuka kwenye besi;
Champion Djikapela Esthétique kwenye Drums;
Ondoma Motema kwenye kinanda;
na Nseka Kudifelela Pasekose kwenye percussions.
Ustadi wao uliipa Show uzito wa kipekee.

9. Bila kuwaacha nyuma Wanenguaji :
Bibi Sucre,
Claudine AC Milan,
Chouchou Mbayo,
Blandine Korando
na Solange Ekutshu hawa pia waliongeza mvuto kwenye Show, wakileta urembo, nguvu na mwendo uliokamilisha muziki wa Quartier Latin International.
Walifanya tamasha hili kuwa tukio la Sanaa kamili.

10. Miaka ishirini na sita baadae, Bercy 2000 bado linabaki kuwa tukio la kihistoria, msingi wa mafanikio ya Muziki wa Afrika katika majukwaa ya Dunia.
Kwa kuadhimisha kumbukizi hii, tunatambua si tu ushindi wa Msanii mmoja, bali mwanzo wa enzi mpya kwa Wasanii wa Afrika.
Tamasha hili linabaki kuwa alama ya uthubutu, ubunifu na fahari ya bara zima.

Version Française

KOFFI OLOMIDE — 26 ANS APRÈS LE CONCERT DE BERCY À PARIS
1. Le 19 février 2026 marque le vingt-sixième anniversaire d’un événement demeuré l’un des plus marquants de l’histoire de la musique africaine. Ce jour-là, en l’an 2000, un artiste venu du Congo accomplissait un exploit inédit pour tout musicien africain, redéfinissant ainsi l’horizon artistique du continent.

2. En effet, à cette date, Koffi Olomide connu à l’état civil sous le nom de «Antoine Agbepa Mumba» devint le premier Artiste Africain à se produire en tête d’affiche et à remplir entièrement le (Palais Omnisports de Paris-Bercy), aujourd’hui appelé (Accor Arena).
Cette salle, la plus vaste de Paris, accueillit plus de 18 000 spectateurs venus de toutes les régions d’Europe.

3. La diaspora congolaise, animée d’un profond sentiment de fierté et de solidarité, afflua massivement vers Paris pour soutenir l’artiste qui incarnait alors l’excellence musicale africaine.
Le concert, baptisé Bercy 2000, connut un succès retentissant malgré l’absence d’une véritable campagne promotionnelle.

4. Le spectacle débuta aux environs de vingt-trois heures et se poursuivit jusqu’à l’aube, vers une heure trente du matin.
Pendant plus de six heures, «Koffi Olomide» et son groupe (Quartier Latin International) offrirent une prestation d’une qualité exceptionnelle, alliant virtuosité vocale, chorégraphies minutieusement orchestrées et créativité artistique.

5. La chaîne MCM Africa enregistra l’intégralité du concert en direct, tandis que d’autres chaînes de télévision France 2, M6 et Canal+ étaient également présentes pour couvrir l’événement.
La mobilisation de ces médias confirmait l’ampleur croissante de la place occupée par la musique africaine sur les grandes scènes internationales.

6. Le spectacle accueillit également des invités prestigieux tels que : Roga Roga, Pepe Felly Manuaku, Stomy Bugsy, Passi et le groupe Bisso Na Bisso, Coumba Gawlo, Nayanka Bell, Meiway, ainsi que de nombreux autres artistes.
Cette diversité de talents conféra à l’événement une dimension résolument panafricaine et universelle.

7. Sur scène, le Quartier Latin International déploya toute sa puissance artistique.
Aux côtés de «Koffi Olomide» se produisaient des chanteurs tels que :
Fally Ipupa,
Jipson Butokondolo,
Mamale Tupac,
Lola Muana,
Eric Tutsi,
Savanet Depitcho,
Moustapha Nkori,
Jordan Kusa
et JF Ifonge.
Les rappeurs (Atalaku) chargés de l’animation scénique étaient : CNN et Océan Zibankulu.

8. La section instrumentale réunissait des musiciens chevronnés :
Guitares : Felly Tyson, Riddens Makoso et Deba O’Neil ;
Basse : Binda Bass et Clovis Silawuka ;
Batterie : Champion Djikapela Esthétique ;
Clavier : Ondoma Motema ;
Percussions : Nseka Kudifelela Pasekose.
Leur maîtrise technique conféra au spectacle une profondeur musicale remarquable.

9. Les danseuses :
Bibi Sucre,
Claudine AC Milan,
Chouchou Mbayo,
Blandine Korando et Solange Ekutshu, apportèrent une dimension visuelle essentielle, insufflant grâce, énergie et dynamisme à la prestation du Quartier Latin International.
Leur présence scénique contribua à faire de ce concert une œuvre artistique totale.

10. Vingt-six ans plus t**d, Bercy 2000 demeure un événement historique, un jalon fondateur dans l’ascension de la musique africaine sur les scènes du monde.
En célébrant cet anniversaire, l’on reconnaît non seulement la victoire d’un artiste, mais aussi l’avènement d’une nouvelle ère pour les musiciens africains. Ce concert reste une véritable icône de l’audace, de la créativité et de la fierté d’un continent tout entier.
Sandra Kazadi lisasi ya s**a

BABA L.W.L

JB MPIANA ALBUM TH (Toujours Humble) : Album Jengo Ambamo "JB Mpiana" Anaipa Rumba Hadhi ya Sanaa ilio Kuu !TH (Toujours...
19/02/2026

JB MPIANA ALBUM TH (Toujours Humble) :
Album Jengo Ambamo "JB Mpiana" Anaipa Rumba Hadhi ya Sanaa ilio Kuu !
TH (Toujours Humble) : l’album‑monument où "JB Jb mpiana" érige la rumba en art majeur

Kuna kazi za muziki ambazo hazitosheki kuwa tu albamu katika safari ya Msanii, bali zinajidhihirisha k**a misingi ya ubunifu, tamko la falsafa ya Kisanii, na alama za kihistoria.

TH (Toujours Humble) ni mojawapo ya kazi hizo adimu, Iliyotoka Juni 2000, ikiwa ni Album ya pili ya solo ya JB Mpiana na ya tatu aliyotengeneza kwa pamoja na Group lake (Wenge BCBG)
Nii kazi pana yenye sura mbili, ikiwa na nyimbo kumi katika CD ya Kwanza na sita katika CD ya Pili, jumla ya nyimbo kumi na sita.
Ni kazi ambayo inaonyesha upeo wa ukomavu wa Msanii huyu.

Kazi Kamili, Mchanganyiko wa Mitindo na Hisia Tofauti
TH ni Album yenye sura nyingi, maabara ya ubunifu ambamo "JB Mpiana" anachanganya kwa ustadi wa hali ya juu:

Rumba ya Kongo iliyojaa hadhi na urithi,

Salsa yenye joto la Karibea,

Rap yenye msisimko wa mijini,

Mutuashi Ngoma ya asili ya Kasai,

Soukous na ndombolo zenye nguvu ya kuchezeka,

na hata mguso wa Soul unaoleta ukimya wa hisia.

Mchanganyiko huu si wa kubahatisha laa hashaa, Ni ushahidi wa dhamira ya Msanii kuvuka mipaka ya Muziki, kuunganisha tamaduni, na kuipanua Rumba bila kuipoteza roho yake.

Ushindi wa Kihistoria na Umaarufu Mkubwa
Mapokezi ya TH yalikuwa makubwa kiasi cha kuifanya Album hii kuwa tukio la Muziki barani Afrika. Ilinyakua tuzo zote kuu za soko la Muziki Inchini Congo :

Album Bora,

Wimbo Bora (48H00 GECOCO)

Uandishi Bora,

na "JB Mpiana" mwenyewe kutunukiwa juzo k**a Mwimbaji Bora na Msanii Bora wa Mwaka.

Zaidi ya nakala 100,000 ziliuzwa, na mafanikio haya yakampa "JB Mpiana" Tuzo la diski ya dhahabu kwa mara ya pili, yakithibitisha nafasi yake k**a nguzo ya muziki wa Congo.

Uandishi wa Kipekee : "JB Mpiana" K**a Msanii Kamili
Jambo la kipekee ni kwamba nyimbo zote zimeandikwa na "JB Mpiana mwenyewe" yaani ni Solo Album yake.
Hii inatoa mwendelezo wa kipekee katika album nzima.
Mada zinazoguswa ni nyingi : mapenzi, elimu, changamoto za kijamii, unyenyekevu lakini zote zimewasilishwa kwa :

Ushairi uliofinywa vizuri,

Busara ya watu,

Tafakuri ya ndani,

na Lugha yenye hadhi na umaridadi.

Kila wimbo ni k**a hadithi fupi, taswira ya maisha iliyopakwa rangi za muziki.

Muundo wa Muziki Uliobebwa na “Malaika Wapendwa”
Kando ya "JB Mpiana", tunakuta kundi la Wasanii mahiri, maarufu ambao mchango wao umeipa albamu hii uzito na uzuri wa kipekee.

Waimbaji :
Alain Mpela Afandé

Chay Ngenge

Jules Kibens

Rio Kazadi

Tutu Callugi

Titina Alcapone Mbwinga

Atalaku (Animateurs)
Tutu Callugi

Gentamicyne

Wapiga gitaa
Ficarré Mwamba (mi-solo)

Sunda Bass (Bass)

Alba Accompagnero (Rhytm)

Bukina Fasso Mbokaliya (solo)

Kinanda
Théo Kiavuanga Bidens

Drums :
Titina Alcapone Mbwinga

Seguion Mignon Maniata

Wanenguaji : Ma “Bébés Chéries” :
Monica Celeste

Nono Diamant

Françoise Marcation

Group hili ni k**a mahak**a ya kifalme ya muziki, kila mmoja akitoa rangi na sauti inayokamilisha jengo la ubunifu.

Orodha ya Nyimbo
CD 1:
TH (Toujours Humble)

Walay Danico

Éducation

Sultan de Bruneil Kaskinto

Dis-moi Amour

Rose verte

Grâce à toi Germain

Jeanpy Pipina

48 Heures Gecoco

Bye Bye Julie

CD 2 :
Mohamed Kaniansy

Aminata Sylla

Kinshasa

Bye Bye Julie (toleo la disco)

Lauréat’s 2000

Acappella

Kila wimbo una utu wake, lakini wote wanashikana katika pumzi moja ya ubunifu: pumzi ya Msanii aliye katika kilele cha uwezo wake.

Falsafa ya Unyenyekevu na Ukuu
Jina la album, (TH Toujours Humble), linafupisha roho ya kazi nzima. "JB Mpiana" anaonyesha msimamo wa Msanii anayejua ukubwa wake, lakini anayechagua unyenyekevu k**a taji la hekima.
Hapa unyenyekevu si udhaifu, bali ni hadhi, ni msimamo, ni falsafa ya kuishi na kuumba.

Hitimisho
TH (Toujours Humble) si album tuu; ni ulimwengu wa Muziki, ni kilele cha ubunifu, ni wakati wa neema katika historia ya Muziki wa Kongo.
"JB Mpiana" anajidhihirisha k**a mjenzi wa hisia, mtaalamu wa rumba, Msanii anayejua kuunganisha urithi na ubunifu, hisia na fikra, ustadi na unyenyekevu.

Ni kazi inayosikilizwa, kufikiriwa, na kurudiwa,kazi ya kudumu.

Version Française :
TH (Toujours Humble) : l’album‑monument où "JB Jb mpiana officiel érige la rumba en art majeur
Il est des œuvres qui ne se contentent pas d’occuper une place dans la discographie d’un artiste, mais qui s’imposent comme des actes fondateurs, des manifestes esthétiques, des jalons historiques. TH (Toujours Humble) appartient à cette catégorie rare.
Sorti en juin 2000, ce deuxième album solo de "JB Mpiana" et troisième réalisé avec son orchestre Wenge BCBG se présente comme une fresque musicale d’une ambition souveraine, un diptyque de seize titres répartis en deux volumes, où l’artiste déploie une maîtrise totale de son art.

Une œuvre totale, à la croisée des genres et des sensibilités
TH est un album polymorphe, un véritable laboratoire sonore où JB Mpiana orchestre une rencontre magistrale entre :

la Rumba congolaise dans toute sa noblesse,

la Salsa et ses volutes caribéennes,

le Rap et son énergie urbaine,

le Mutuashi enraciné dans les traditions kasaïennes,

le Soukous et le ndombolo dans leur effervescence dansante,

et même des touches de Soul, subtilement distillées.

Cette hybridation n’est jamais gratuite : elle témoigne d’une volonté de transcender les frontières musicales, de faire dialoguer les héritages, d’ouvrir la rumba à de nouveaux horizons sans jamais trahir son essence.

Un triomphe artistique et populaire
L’accueil réservé à TH fut à la hauteur de son ambition.
L’album connut un succès retentissant, raflant tous les grands prix du marché du disque :

Meilleur album,

Meilleure chanson (48H00 GECOCO)

Meilleure composition,

et "JB Mpiana" sacré meilleur chanteur et meilleur artiste de l’année.

Avec plus de 100 000 exemplaires vendus, TH offre à "JB Mpiana" son deuxième disque d’or, consacrant définitivement son statut de figure majeure de la musique congolaise contemporaine.

Une écriture d’une cohérence rare : "JB Mpiana" en auteur total
Fait remarquable : toutes les chansons de l’album sont écrites et interprétées par JB Mpiana lui-même. Cette unité d’écriture confère à TH une cohérence interne exceptionnelle. L’album aborde une pluralité de thèmes l’amour, l’éducation, les réalités sociales, l’humilité mais toujours avec une plume qui allie :

la finesse poétique,

la sagesse populaire,

la profondeur introspective,

et une élégance littéraire qui distingue "JB Mpiana" dans le paysage musical.

Chaque titre semble être une miniature narrative, un fragment de vie sublimé par la musique.

Une architecture musicale portée par les “Anges Adorables”
Autour de JB Mpiana gravite une constellation de talents, les célèbres Anges Adorables, dont la virtuosité contribue à la majesté de l’album.

Les chanteurs
Alain Mpela Afandé

Chay Ngenge

Jules Kibens

Rio Kazadi

Tutu Callugi

Titina Alcapone Mbwinga

Les animateurs
Tutu Callugi

Gentamicyne

Les guitaristes
Ficarré Mwamba (mi-solo)

Sunda Bass (basse)

Alba Accompagnero (accompagnement)

Bukina Fasso (solo)

Synthétiseur
Théo Kiavuanga Bidens

Percussions et batterie
Titina Alcapone Mbwinga

Seguion Mignon Maniata

Les danseuses — les “Bébés Chéries”
Monica Celeste

Nono Diamant

Françoise Marcation

Cette équipe forme une véritable cour artistique, un ensemble où chaque musicien apporte une nuance, une couleur, une respiration, contribuant à l’édifice sonore avec une précision quasi chorégraphique.

Les titres : un panorama riche et varié
Volume 1
TH (Toujours Humble)

Walay Danico

Éducation

Sultan de Bruneil Kaskinto

Dis-moi Amour

Rose verte

Grâce à toi Germain

Jeanpy Pipina

48 Heures Gecoco

Bye Bye Julie

Volume 2
Mohamed Kaniansy

Aminata Sylla

Kinshasa

Bye Bye Julie (version disco)

Lauréat’s 2000

Acappella

Chaque morceau possède sa propre identité, mais tous participent d’un même souffle, d’une même vision artistique : celle d’un JB Mpiana au sommet de son inspiration, conjuguant virtuosité vocale, sens mélodique et profondeur thématique.

Une esthétique de l’humilité et de la grandeur
Le titre même de l’album, Toujours Humble, résume la philosophie qui le traverse. JB Mpiana y affirme une posture d’artiste conscient de sa stature, mais refusant l’arrogance. L’humilité devient ici une forme de noblesse, un principe directeur, une manière de se tenir face au monde et face à son art.

En conclusion
TH (Toujours Humble) n’est pas seulement un album : c’est une œuvre‑monde, un sommet esthétique, un moment de grâce dans l’histoire de la musique congolaise. JB Mpiana y apparaît comme un architecte du sensible, un esthète de la rumba, un créateur capable d’unir tradition et modernité, émotion et réflexion, virtuosité et simplicité.

C’est un album qui se savoure, se médite, se revisite un classique intemporel

BABA L.W.L

Adresse

Avenue D'ORADOUR SUR GLANE
Bonneuil-sur-Marne
94380

Téléphone

33668312952

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Lubonji Wa Lubonji publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter La Pratique

Envoyer un message à Lubonji Wa Lubonji:

Partager

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram