22/02/2026
FALLY IPUPA AMFUFUA KIHESHIMA MWANAMUZIKI MKONGWE FRANCO LUAMBO
FRANCO LUAMBO COURONNÉ À TITRE POSTHUME PAR FALLY IPUPA
1. Mwezi Agosti 2024, Jiji la Kinshasa ilishuhudia tukio lenye uzito wa kiishara: Fally Ipupa, Gwiji wa Muziki wa kisasa Inchini Congo, alimkabidhi kwa heshima kubwa "Franco Luambo Makiadi" tuzo ya dhahabu baada ya kifo chake.
Tuzo hiyo ilipokelewa na mwanawe, "Yves Emongo Luambo", ikifungua daraja kati ya vizazi na kuthibitisha mchango wa wale waliojenga urithi wa muziki wa Taifa.
2. Kufwatia kitendo hiki, "Fally Ipupa" alionyesha shukrani ya dhati kwa watangulizi wake mashuhuri, huku akishiriki mafanikio ya uboreshaji wake wa wimbo maarufu «Mario», alioupa jina jipya «Lady» katika albamu yake Formule 7 ya mwaka 2022.
Hatua hii ilikuwa jitihada ya kuzirudisha kazi za msingi katika kumbukumbu ya kizazi cha sasa.
3. Kibao «Mario» kilipotoka mwaka 1985, 'Franco Luambo Makiadi" alikuwa tayari amebadilisha kabisa hadhi ya Muziki wa Zaire kwa takriban miaka ishirini.
Akiwa Mrithi wa ubunifu wa kazi kutoka Group la (African Jazz) ya "Joseph Kabasele Grand Kalle" na (African Fiesta National) ya "Tabu Ley Rochereau" kadhalika (African Fiesta Sukisa) ya Dokta Nico Kasanda" hivyo kuanzisha mtindo mpya uliobebwa na kauli mbiu ya Group (Tout-Puissant OK Jazz) : «Unaingia OK, unatoka KO». Sebene, lenye mitiririko ya gitaa yenye nguvu, likawa uti wa mgongo wa rumba iliyotengenezwa upya.
4. "Franco Luambo Makiadi" alikuwa pia kiongozi wa Group mwenye maono mapana sana, akiongoza Group lake lililoweza kutekeleza majukumu kadhaa kwa wakati mmoja.
Wanamuziki wengi mashuhuri k**a "Vicky Longomba" na "Sam Mangwana" walipitia katika Group hili, wakichangia utajiri na utofauti wa muziki wake.
5. Mwaka 1980, "Madilu System" alijiunga (TP OK JAZZ" na taratibu akawa mmoja wa nguzo zake, hasa kupitia mafanikio ya wimbo «Non», utunzi wa dakika kumi na tisa.
Humo alikutana na Magwiji wa gitaa k**a "Papa Noël" na "Dizzy Mandjeku", Majina makubwa katika Muziki wa Congo.
6. Niwakati akiwa pamoja na "Franco Luambo makiadi" ndipo "Madilu System" aliimba Wimbo ambao ulitokea kuwa Tube «Mario», Wimbo namba 1ulio ibeba Album ya jina hilo, na uliotawala upande mzima wa Santuru (Disc A) na kuchukua dakika kumi na tatu.
Tokea pale Wimbo (Mario) ulipowekwa Sokoni, ulikuja juu kileleni na kuzipiku nyimbo zote zilizokua sokoni kipindi kile kadhalika "Madilu System" akatokea kuwa Mwimbaji bora hadi kupelekea nyota ya baadhi wakongwe kwenye Group kufifia.
7. Wimbo (Mario) uliaanza kwa sauti ya gitaa la mi-solo likishikiliwa na "Franco Luambo Makidi" Mwenyewe, kisha likafwatiwa na Gitaa rhythm la "Gégé Mangaya".
Huku "Nado Kakoma" akiwa kwenye Ngoma,, congas (zilizopigwa na "Dessoin Bosuma", "Decca Mpudi" Kwenye Bass Gita, vikiingiliana vizuri pindi tuu Rhytm Gitaa la "Mangaya" linaanza kupiga mkondo wake.
"Franco ndie anayetoa mistari ya mwanzo ya wimbo, kisha ufuatiwe na kiitikio kinachoimbwa na Madilu System.
Solo Gitaa likicharazwa na "Papa Noel Nedule".
8. Wimbo huu unasimulia, kwa ucheshi mkali na kejeli ya kuvutia, hadithi ya kijana anayelelewa na mwanamke, yaani Kijana kabebwa kimapenzi na Mwana mama mwenye umri mkubwa kumzidi. Maneno yake, yenye uhalisia mkali, yanaonyesha tabia, ujanja na masaibu ya gi**lo asiye kuwa na aibu ya kulelewa na Mwanamke, ambaye amekuwa mfano maarufu katika utamaduni wa Congo.
9. Zaidi ya simulizi, "Franco Luambo Makiadi" analeta pia ujumbe wa maadili, unaolingana na msimamo wa utawala wa Mobutu uliotaka kuzuia kupotoka kwa vijana waliokosa mwelekeo.
(Mario), Ni Kijana msomi asie na shughuli, Mtoto wa kijiweni, anageuka kuwa ishara ya ndoto za kijamii zisizo na msingi na kukataa kufanya juhudi.
10 .Umaarufu mkubwa wa wimbo huu ulimfanya "Franco Luambo Makiadi" aendeleze simulizi lake : toleo lingine lilifuata haraka, Mwaka 1987 pale alipotoa Wimbo (La Réponse de Mario ) yaani (Jibu la Mario).
Baada ya "Grand Maitre Franco Luambo makiadi" kufariki dunia mwaka 1989, matoleo mengi ya marudio ya Wimbo (Mario) yaliendelea kusambaa, yakidumisha hadithi hii.
11. Athari za (Mario) zilivuka mipaka ya Kongo.
Uliimbwa upya nchini Côte d’Ivoire, Angola, na kundi la Africando, pamoja na Ray Lema, na ukawa wimbo wa bara zima.
Ushawishi wake ni mkubwa kiasi kwamba katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jina «Mario» sasa linamaanisha mwanaume anayelelewa na mwanamke.
Version Française
FALLY IPUPA RÉHABILITE AVEC SOLENNITÉ LA MÉMOIRE DU MAESTRO FRANCO LUAMBO
FRANCO LUAMBO COURONNÉ À TITRE POSTHUME PAR FALLY IPUPA
1. En août 2024, la ville de Kinshasa fut le théâtre d’un événement d’une portée hautement symbolique : Fally Ipupa, figure majeure de la musique congolaise contemporaine, remit avec une solennité remarquable un disque d’or posthume à l’illustre Franco Luambo Makiadi.
La distinction fut reçue par son fils, Yves Emongo Luambo, consacrant ainsi un pont mémoriel entre les générations et réaffirmant la dette culturelle envers ceux qui ont façonné l’héritage musical de la Nation.
2. À travers ce geste empreint de respect, Fally Ipupa exprimait une gratitude profonde envers ses prestigieux prédécesseurs, tout en partageant le succès de sa réinterprétation du classique «Mario», rebaptisé «Lady» dans son album Formule 7 paru en 2022.
Cette initiative s’inscrivait dans une volonté claire de réinscrire les œuvres fondatrices dans la conscience culturelle du public contemporain.
3. Lorsque le titre «Mario» parut en 1985, Franco Luambo Makiadi avait déjà révolutionné le paysage musical zaïrois depuis près de deux décennies.
Héritier des innovations de l’African Jazz de Joseph Kabasele «Grand Kallé», de l’African Fiesta National de Tabu Ley Rochereau, ainsi que de l’African Fiesta Sukisa de Docteur Nico Kasanda, il imposa une esthétique nouvelle, portée par la devise percutante de son Tout-Puissant OK Jazz : «On entre OK, on sort KO».
Le sébène, avec ses envolées de guitare vigoureuses, devint l’ossature d’une rumba magistralement renouvelée.
4. Franco Luambo Makiadi fut également un chef d’orchestre visionnaire, dirigeant une formation capable de répondre simultanément à plusieurs engagements.
Des artistes de renom tels que Vicky Longomba ou Sam Mangwana y firent leurs armes, contribuant à l’extraordinaire richesse et diversité du répertoire du groupe.
5. En 1980, Madilu System rejoignit le Tout-Puissant OK Jazz et s’y imposa progressivement, notamment grâce au succès retentissant du morceau «Non», une composition fleuve de dix-neuf minutes.
Il y côtoya des Maîtres de la guitare tels que Papa Noël et Dizzy Mandjeku, figures incontournables de la musique congolaise.
6. C’est aux côtés de Franco Luambo Makiadi que Madilu System interpréta le titre qui deviendrait un véritable tube : «Mario».
Pièce maîtresse de l’album éponyme, le morceau occupait à lui seul l’intégralité de la face A du 33 tours, avec une durée de treize minutes.
Dès sa mise sur le marché, «Mario» s’imposa au sommet, éclipsant les autres titres en circulation et propulsant Madilu au rang de voix dominante du groupe, reléguant certains anciens membres au second plan.
7. Le morceau «Mario» s’ouvre sur les notes incisives de la guitare mi-solo, exécutées par Franco lui-même, suivies du jeu rythmique de Gégé Mangaya.
Nado Kakoma assurait les percussions, tandis que les congas étaient tenues par Dessoin Bosuma ; Decca Mpudi soutenait l’ensemble à la basse, créant une harmonie parfaite dès l’entrée du rythme de Mangaya.
Franco lançait les premières lignes du chant, immédiatement relayées par le refrain interprété par Madilu System.
La guitare solo, quant à elle, était magistralement assurée par Papa Noël Nedule.
8. Le morceau raconte, avec une ironie mordante et un humour savoureux, l’histoire d’un jeune homme entretenu par une femme plus âgée.
Les paroles, d’un réalisme saisissant, décrivent les manœuvres, les caprices et les mésaventures d’un gi**lo décomplexé, devenu une figure emblématique de l’imaginaire populaire congolais.
9. Au-delà de la narration, Franco Luambo Makiadi y insuffle une dimension morale, en parfaite résonance avec les préoccupations du régime de Mobutu, soucieux d’encadrer une jeunesse parfois en perte de repères.
Mario, étudiant diplômé mais oisif, devient ainsi le symbole des illusions sociales et du refus de l’effort.
10. Le succès phénoménal de Mario» incita Franco à prolonger la saga : une première variante fut rapidement publiée, suivie en 1987 de «La Réponse de Mario».
Après la disparition du Grand Maître en 1989, de nombreuses versions et réinterprétations continuèrent de circuler, perpétuant la légende.
11. L’influence de «Mario» dépassa largement les frontières du Congo.
Le morceau fut repris en Côte d’Ivoire, en Angola, par le collectif Africando ainsi que par Ray Lema, devenant un classique continental.
Son impact culturel est tel qu’en République démocratique du Congo, le prénom « Mario » désigne désormais, dans le langage courant, un homme entretenu par une femme.
BABA L.W.L