Daktari Mwaka

Daktari Mwaka A Qualified Doctor,Starseed,life coach,an astrologer �

Mercury Retrograde itaanza   9th Nov _29th Nov, Je Maana ya Mercury  Retrograde ni Nini Maana ya Mercury RetrogradeKiast...
07/11/2025

Mercury Retrograde itaanza 9th Nov _29th Nov, Je Maana ya
Mercury Retrograde ni Nini

Maana ya Mercury Retrograde

Kiastronomia, Mercury retrograde ni kipindi ambapo sayari Mercury inaonekana kana kwamba inarudi nyuma angani inapozunguka jua (ingawa kwa kweli haigeuki, ni mwonekano wa macho kutokana na tofauti ya kasi kati ya Dunia na Mercury).

Kiastrolojia na kiroho, huu ni wakati ambao mitetemo ya mawasiliano, akili, teknolojia, na usafiri — ambayo yote inadhibitiwa na Mercury huvurugika au kugeuka ndani (internal reflection).

Athari Zake Kiroho

Mercury ni sayari ya akili, mawasiliano, mantiki, na uelewa wa habari. Wakati ipo retrograde, nguvu zake hugeuka kutoka nje kwenda ndani. Hivyo, huleta athari zifuatazo kiroho:

1. 🧠 Kujichunguza na tafakari ya ndani

Ni wakati wa kujua ulipojikwaa, kufikiri upya maamuzi, na kusafisha akili.

Mizimu au nguvu zako za ndani hukusukuma kuangalia upya njia zako si kupambana, bali kuelewa.

2. 💬 Kuvurugika kwa mawasiliano

Watu huanza kuelewana vibaya, meseji kupotea, au maneno kugonga vibaya.

Kiroho, hii inakufundisha kutulia kabla ya kujibu, na kusikiliza zaidi kuliko kusema.
3. 🪞 Kurudi kwa mambo ya zamani

Wapenzi wa zamani, marafiki wa zamani, au hisia ambazo hukuzimaliza huweza kurudi.

Si lazima warudi ili mkutane tena kimwili bali kurudi kukufundisha kile hukumaliza ndani yako.

4. Kuchelewa au kuvurugika kwa mipango

Kiroho, huu ni muda wa mapumziko kuachilia kasi na kuruhusu maisha yajipange upya.

Universe hukusukuma kupumzika, kurekebisha, na kusafisha njia kabla ya hatua kubwa.

5. 🌫️ Uwazi wa kiroho

Watu wenye mtazamo wa kiroho wa juu huweza kuhisi ndoto nyingi, deja-vu, au ishara kutoka kwa malaika na mizimu.

Ni wakati wa kufanya detox ya akili, kuandika ndoto, na kusikiliza mwongozo wa ndani.

🕯️ Mambo ya Kufanya Wakati wa Mercury Retrograde

Usianzishe mambo mapya subiri baada ya retrograde.

Kamilisha mambo ya zamani.

Tafakari, andika, samehe, safisha nishati zako.

Omba mwongozo wa kiroho kabla ya kufanya maamuzi makubwa.

Fanya grounding (kutembea ardhini, kupumua kwa makini, meditation).

🌙 Kauli ya Kiroho

“Wakati Mercury inarudi nyuma, dunia inataka wewe urudi ndani. Tafakari, sikiliza, na acha mizizi yako ikue tena kabla ya kurudi mbele.”

*AINA 7 ZA UELEWA KUHUSU PESA (Money Intelligence)*Kama unataka kuwa tajiri wa kweli, si lazima uwe na pesa nyingi kwanz...
06/11/2025

*AINA 7 ZA UELEWA KUHUSU PESA (Money Intelligence)*

Kama unataka kuwa tajiri wa kweli, si lazima uwe na pesa nyingi kwanza unahitaji *akili sahihi kuhusu pesa*. Hizi ni *aina 7 za uelewa wa pesa* ambazo kila mtu anapaswa kuzijua:

1.*Akili ya Kifedha (Financial Intelligence)*
Uwezo wa kuelewa namna pesa inavyofanya kazi mapato, matumizi, akiba, uwekezaji, madeni nk. Hii ni msingi wa uhuru wa kifedha.

2.*Akili ya Uwekezaji (Investment Intelligence)*
Uwezo wa kutambua fursa za kuwekeza pesa zako na kupata faida bila kufanya kazi muda wote. Hapa ndipo pesa huanza kukufanyia kazi.

3.*Akili ya Kibiashara (Business Intelligence)*
Kufahamu jinsi ya kuanzisha, kuendesha na kukuza biashara kutambua mahitaji ya wateja, soko, na kushindana.

4.*Akili ya Mahusiano ya Kifedha (Relationship Intelligence with Money)* Uhusiano wako binafsi na pesa: Je, una hofu nayo? Unaithamini? Unaitumia kwa hasira? Hii huamua maamuzi yako ya kifedha kila siku.

5.*Akili ya Elimu ya Kifedha (Financial Literacy)*
Kujua kusoma taarifa za kifedha, kuandaa bajeti, kuepuka madeni mabaya na kuelewa mzunguko wa pesa katika maisha ya kila siku.

6.*Akili ya Ubadilishaji (Income Generation Intelligence)*
Uwezo wa kubuni njia mpya za kipato: biashara ndogo, kazi za ziada, ujasiriamali wa kidigitali nk. Si lazima uwekewe mshahara mmoja tu!

7.*Akili ya Ulinzi wa Pesa (Money Protection Intelligence)*
Kujua namna ya kulinda kile unachokipata: Bima, mikataba, kuzuia wizi, kuepuka matapeli wa kifedha na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

Kama ukikosa maarifa haya, pesa zitakupita tu hata uzipate kiasi gani.

Anza kujifunza, anza kujiuliza: “Ni aina gani ya akili ya kifedha ninayohitaji kukuza leo?”


Good morning

UTANGULIZIWatu wengi huona kuamka mapema ni kama tabia ya watu tu wenye nidhamu au mafanikio tu. Lakini kwa macho ya kir...
05/11/2025

UTANGULIZI

Watu wengi huona kuamka mapema ni kama tabia ya watu tu wenye nidhamu au mafanikio tu. Lakini kwa macho ya kiroho, kuamka mapema ni tendo la kisheria la nishati, ni kuungana na mawimbi ya kwanza ya uumbaji kabla dunia haijaanza kuzungumza.

Kabla jua kuchomoza, dunia huwa katika hali ya kimya cha nishati yani hakuna mawimbi ya hasira, presha, au mawazo ya watu milioni kadhaa wanaoamka na kukimbilia mijini/vibaruani
Ni kipindi ambacho nishati ya Muumba (Source Energy) hujipanga upya ili kuingiza mwanga mpya kwa siku inayofuata.

Ndiyo maana katika tamaduni zote za kale, kuamka mapema kulizingatiwa kuwa mlango wa mawasiliano na ulimwengu wa mwanga:

Wahindi walikiita “Brahma Muhurta” yani wakati wa Muumba.

Waislamu waliuita “Tahajjud” yani wakati wa dua zinazojibiwa.

Wamasai, Wachagga, na Wagogo wa zamani walitoka mapema kufanya matambiko au kupiga mluzi wa rohoni kuamsha nguvu ya dunia ndani mwao.

Kuamka mapema, basi, sio ibada ya dini fulani bali ni sheria ya nishati na vibration.
Ni namna ya kumiliki siku kabla dunia haijaanza kukuamulia wewe.

Ebu nijaribu hivi👇


🌅 1. WAKATI WA “FREQUENCY SAFI” (PRE-SUNRISE PERIOD)

Kipindi cha saa 9 usiku hadi saa 12 alfajiri (3:00–6:00 AM) ndicho kinachoitwa Brahma Muhurta.
Hapa anga linakuwa tulivu kabisa. Dunia inakuwa kama kanda tupu (blank CD) ... bado haijaandikwa mawazo ya wanadamu.

Yes natambua kwamba wakati ww unasema huu ni usiku,kuna maeneo ni mchana, sasa hapa ninacho zungumzia ni nisharti ile itakayo kuangazia katika Eneo lako mfano kwa wewe uliye Tanzania ama Africa ya mashariki tunaoshea muda mmoja..

Sasa Mtu anayeamka na kutulia muda huu wa saa9 usiku- Alfajiri anapata yafuatayo;

▪️Ufahamu wa ndani (inner knowing)

▪️Maono ya siku au maisha yake

▪️Utulivu wa kiroho unaoongeza nguvu ya kuvuta matukio mazuri

👉Kwa lugha ya vibration: huu ni wakati wa kuunganisha akili ndogo (mind) na akili kuu ya ulimwengu (Universal Mind).
Unapoamka muda huu, unakuwa unapanda mbegu ya nishati safi kabla jua halijaweka “signature” yake angani.


☀️ 2. BAADA YA JUA KUCHOMOZA

Kuanzia saa 12:30 hadi saa 2:00 asubuhi (6:30–8:00 AM), frequency ya dunia hubadilika.
Hapa jua linaanza kuchochea nguvu za “kutenda,” ubongo unakuwa hai zaidi, na mfumo wa mwili unaanza kutengeneza homoni za utendaji.

Hapa Mtu ambaye tayari amejiunganisha kabla ya jua, sasa anatembea akiwa ameshika frequency ya mwanga yani Anaitawala dunia yake

Lakini ambaye amelala hadi jua linanoga/limechomoza, anaamka akiwa amekutana na nishati iliyokwisha kuchanganywa na mitetemo ya watu wengi..hapa jua ndilo linakutawala

Ndiyo maana msemo wa kiroho unasema:

🗣️ “Kama hukupanda mapema, utakuta wengine wameshaokota nishati.”

Sio kwamba wamekuchukulia kitu, bali wao walijiunganisha na safu ya kwanza ya mwanga yani ile " 👉 pure light code .... kabla haijaguswa na vibration za woga, wasiwasi, hofu,malalamiko,na presha za dunia,yani za watu wengi nchini kwako ama katika mkoa wako,wila yako,kata yako,mtaa/kijijini kwenu


🌄 3. SASA SWALI NI: KWA NINI NI MUHIMU KUAMKA MAPEMA❓

Kuamka mapema si desturi tu, bali ni kanuni ya kimungu inayofungua mlango wa mawasiliano kati ya roho yako na nguvu kuu ya uumbaji.
Faida zake ni hizi:

1. Akili inakuwa wazi , hakuna kelele za mawazo ya dunia, hakuna mizigo ya mawazo ya jana, hivyo ubongo wako uko safi kupokea maono mapya.

2. Mwili unavuta prana safi , hewa ya asubuhi huwa na nishati ya uhai (prana) ambayo bado haijachanganyikana na vibrations za shughuli za binadamu.

3. Roho inapata mwanga wa kwanza (Divine Light Code) , huu ni mwanga safi wa kimungu unaotoka moja kwa moja kutoka kwenye chanzo, kabla ya polarity ya jua kubadilika saa 7 mchana.

4. Unaandika siku yako mwenyewe kabla dunia haijaanza kukuandikia.

Kwa maneno mengine👇
🗣️ Ukiamka kabla ya jua .. wewe ndiye unaongoza nishati.
Ukichelewa ...nishati ndiyo inakuongoza wewe.

4. KUONDOKA NYUMBANI UKIWA TAYARI KIROHO🌬️

Usiondoke tu kwa kukurupuka.
Kabla hujaondoka, amka ndani yako kwanza.
Tulia, pumua kwa makini, kisha sema kimoyomoyo:

🗣️“Leo nimeunda dunia yangu yenye amani, mafanikio na watu wema wanaonitafuta.”

Hapa ndipo wengi wanakosea ... wanaomba rehema au msaada kila siku kana kwamba hawajaundwa kikamilifu.
Lakini kumbuka:
Usiombe rehema za Mungu, bali tengeneza mwelekeo.
Wewe ni sehemu ya Muumba, sio kiumbe kinachoomba kuumbwa upya kila asubuhi.

Hapa ndipo siri ya manifestation ya kweli inapozaliwa.
Dunia hujibu frequency yako, sio maneno yako.

Angalia mfano huu:
Mtu anaamka amechelewa, hajafanya ibada ya kujiumbia dunia yake, halafu kazini kwake anasema “riziki atatoa Mungu.”
Lakini ukweli ni kwamba ... kama huna nguvu yoyote (iwe chanya au hasi), dunia haitakusikiliza.
Unatakiwa kusema kwa ujasiri:

🗣️ “Leo nimepata elfu 20.”
“Leo nimeingiza tayari laki moja katika kazi yangu.”

Kumbuka, wewe ni nishati, wewe ni roho ... ndiyo muumbaji halisi wa dunia yako.
Usitegemee huruma za Mungu kwa sababu Chanzo (Source) hakitumii hisia bali kanuni.
Ndiyo maana wale wanaotegemea huruma, hupokea kiwango kilekile au pungufu.. kisichotosha.

Usiombe pesa ije, usiitafute pesa, kwa sababu pesa pia ina vibration, ina miguu ya kithabiti ... itakukimbia.
👉 Bali ivute pesa kwa nguvu za uumbaji.
Pesa inavutwa na wenye nguvu, sio wenye maneno.
Haitakuonea huruma ... itaitikia tu frequency yako.


☀️ 5. KUHUSU SAA 7 MCHANA ...KILELE CHA FREQUENCY YA JUA

Kuanzia saa 6:45 hadi 8:00 mchana, jua linapita katikati ya anga.
Huu ndio wakati ambao nishati ya jua inafika kileleni, kisha inaanza kushuka polepole.
Waswahili walikuwa na hekima walisema:

“Ni muda wa treni kubadilisha behewa.” 😄

Ndiyo maana Wahindi wengi hupumzika kipindi hicho.
Wengine hurudi nyumbani kwa dakika chache, si kwa kula tu, bali kwa kusawazisha nguvu zao.

Katika baadhi ya maeneo ya India, hufanyika ibada iitwayo “Agni Meditation.”
Watu hukaa kimya, huhema taratibu, na kumshukuru Surya ... nguvu ya jua.
Wakinyosha mikono kuelekea jua, husema:

🗣️ “Surya Namah... “Naisalimu nguvu ya mwanga.” ☀️

Hii sio ibada ya jua, bali ni kutambua mzunguko wa nishati unaotembea kupitia mwanga wa jua.
Wakati huu, ubongo wa binadamu hubadilisha polarity ... upande wa kulia (hisia) na kushoto (mantiki) huanza kusawazika.
Ndiyo maana kufanya meditation, maombi ya shukrani, au kutulia kimya kipindi hiki huleta utulivu, umakini na nguvu mpya.


⏰ NINI MAANA YA “1:00 PM” NA “PM”❓

Kihistoria, “PM” humaanisha Post Meridiem ... baada ya jua kupita katikati ya anga.
Lakini siri ya kiroho ni kwamba
👉PM = Power Moment,
yaani kipindi cha kutuliza nguvu ya mwanga na kuanza mzunguko mpya wa nishati.

Waratibu wa muda waliweka saa 7 kama 1:00 PM kwa mujibu wa Elimu ya Namba (Numerology) ...namba 1 ikimaanisha mwanzo mpya wa kimfumo wa nguvu.
Wasiokuwa na maarifa haya hudhani ni “umasonic,” lakini ukweli ni kwamba ni hekima ya kale ya kozmiki.

Kwa lugha ya mwanga, saa 7 mchana jua huonekana likisema kwa sauti:

🗣️ ☀️“Nimewasha moto wa siku, sasa ni zamu yako kuutuliza na kuuongoza kwa hekima.”

Kwa hiyo huu ni muda bora wa:
▪️ Meditation ya kimya
▪️ Maombi ya shukrani
▪️Kurekebisha mawazo na mwelekeo wa siku
▪️ Kupumua na kuunganisha moyo na jua


🧘🏽‍♂️ MAZOEZI RAHISI YA SAA 7 MCHANA

Kama uko kazini au huwezi kurudi nyumbani, fanya hivi taratibu:

1. Kaa wima, fumba macho.
👉 Hii inasaidia mwili na akili kutulia, ubongo uanze kupokea mwanga.

2. Pumua ndani kwa sekunde 4, shikilia 4, kisha toa 4.
👉 Hii ni njia rahisi ya kusawazisha pumzi na mzunguko wa damu, huku ukirudisha nguvu ndani yako.

3. Fikiria mwanga wa jua unashuka kupitia kichwa hadi kifua.
👉 Huo ni mwanga wa uzima unaosafisha mawazo, huzuni na uchovu.

4. Sema kimoyomoyo:

🗣️ “Ninaungana na Chanzo cha mwanga, na ninasawazisha nguvu za leo.”
👉 Maneno haya yanaamsha kiungo cha roho yako na jua (Surya Connection).

5. Tabasamu taratibu na endelea na shughuli zako.
👉 Tabasamu ni alama ya kuruhusu mwanga ukae ndani yako.

⏳Ukweli ndugu yangu , Dakika tano tu za utulivu huu zinatosha kabisa kufufua nishati ya mwanga ndani yako na kuondoa uchovu wa mchana.


🌇 JIONI .... KIPINDI CHA TAFSIRI NA SHUKRANI

Baada ya jua kushuka, nishati ya dunia hubadilika kuwa tulivu.
Huu ni muda bora wa:

👉 Kujitafakari ...pima siku yako, angalia ulivyotumia nishati yako.

👉Kuandika mafanikio ya siku.. hata jambo dogo ni ushindi wa mwanga.

👉 Kufanya shukrani na kujiandaa kwa kesho ... shukrani hufunga mlango wa leo kwa amani na kufungua kesho kwa baraka mpya.

Kama uliianza siku kwa mwanga, na ukaimaliza kwa shukrani,
umekuwa mtu wa mzunguko kamili wa nuru , roho yako huingia usingizini ikiwa imetulia, tayari kuumba kesho yenye vibration ya mafanikio mapya


HITIMISHO

Jua sio tu chanzo cha mwanga ... ni kifaa cha kisheria cha ulimwengu, kinachosambaza mawimbi ya uhai na kuamsha roho za viumbe wote.

Kuamka kabla ya jua ni kuungana na nguvu ya uumbaji,
Kupumzika saa 7 mchana ni kuheshimu mzunguko wa uhai,
Kufunga siku kwa tafakari ni kuweka alama ya shukrani kwenye mwanga wa kesho.

Mafanikio ya kweli hayaji tu kwa kuomba dunia ikutendee..bali...
yanakuja pale unapounda dunia yako kwa frequency sahihi.

Kwa hivyo,

🗣️ Usisubiri dunia ikupe nguvu,
amka mapema, shika mwanga, na iandike dunia yako kwa vibration ya roho yako.

Nikwamba, Somo hili linaweza kutumika kama mwongozo wa “SIRI ZA JUA NA NGUVU YA KUAMKA MAPEMA” .. kwa wote wanaotaka kuishi kwa mwanga, uelewa, na mafanikio ya ndani na nje.

litaendelea.............

Mwezi Mkubwa (Supermoon) unakaribia.Jiandaeni. kuanzia Kesho tarehe 5/11, Mwezi Mkubwa utawasili  utakuwa mwezi wa duara...
04/11/2025

Mwezi Mkubwa (Supermoon) unakaribia.

Jiandaeni.

kuanzia Kesho tarehe 5/11, Mwezi Mkubwa utawasili utakuwa mwezi wa duara mkubwa na wenye mwanga zaidi wa mwaka kwa sababu utakuwa karibu zaidi na dunia, ukiwa mkubwa kwa hadi asilimia 14% na mkali kwa hadi asilimia 30% zaidi ya mwezi wa kawaida. Tayari tunaanza kuhisi nguvu zake zikijikusanya. Baadhi watauita “Beaver Moon.”

Mwezi huu utaleta mvutano kati ya kutaka kushikilia usalama na kukubali mabadiliko, hasa kwa kuwa utakuwa na uhusiano wa mvutano na sayari za Jupiter na Pluto hali itakayowasukuma watu katika matamanio ya kupitiliza, kutaka kujumuika na kufurahia maisha, lakini pia inaweza kusababisha mabadiliko makubwa katika mahusiano mengine ya muda mfupi, na mengine yakibadilisha kabisa uhusiano hadi yasirekebishike tena.

Siku chache zijazo zitakuwa na mchanganyiko wa utulivu na msisimko.
Wakati nguvu ya “faraja” inapogongana na nguvu ya “mabadiliko,” kunazuka mvutano nyumbani, kazini, au hata kwenye makundi ya kijamii. Watu wanaweza kujikuta wakijitumbukiza katika matendo ya kupitiliza ili kujifariji kama kutumia pesa hovyo, kula au kunywa kupita kiasi, au kutafuta starehe za haraka kisha baadaye kujikuta wakiwa wamechoka au wamevurugwa kihisia.

Hivyo basi, huu ni wakati wa kujizuia na kujitawala kihisia.
Usifanye jambo lolote wiki hii ambalo utalijutia kesho.
Kaa mtulivu au ondoka kwa amani.

Nguvu za mamlaka na udhibiti zitaanzag kuonekana wazi iwe ni kwa ushindani kati ya marafiki, migongano ya nguvu katika uhusiano, au malalamiko yaliyofichwa ambayo sasa yako tayari kulipuka kwa kisingizio kidogo tu. Kile kinachoanza kama mazungumzo ya kirafiki kinaweza haraka kubadilika kuwa jaribio la mipaka, hasa wakati vivuli vilivyofichwa vya kihisia vinapoibuka ghafla.

Kwa hiyo, kuwa mwangalifu usiahidi kupita uwezo wako, usitumie pesa hovyo, wala usilazimishe watu wakidhi mahitaji yako ya kihisia.
Epuka jaribu la kutaka kudhibiti matokeo au kutumia mvuto wako kuficha ukweli mgumu.

Kihisia na kisaikolojia, miezi mikubwa kama hii huamsha hisia kwa kiwango kikubwa wengi watasumbuliwa na kukosa usingizi na ndoto zenye nguvu.
Lakini upande chanya ni kwamba mwanga huu wa mwezi unaweza kufungua ubunifu wa ajabu, nguvu za kiroho, na uwezo wa kiintuisho (intuition). Hata hivyo, ni ukweli kwamba kwa wengi, hii itakuwa wiki yenye nguvu nzito sana.

Kumbuka, ulimwengu mzima kwa sasa unapitia mabadiliko makubwa, hata katika miili ya watu kimwili.
Kwa wale wanaopitia changamoto za kiakili au kihisia, tafuta msaada usiwe peke yako.
Na kwa wote wanaohisi nishati ni nzito sana wiki hii kumbuka, kuna mwanga mwishoni mwa handaki.
Hii ni kipindi kifupi tu.
Kivumilie. Kwa upendo.

Aliyeonywa mapema, amejiandaa.

Dr.Mwaka✍🏻

Mtazamo wa Akili (Mindset) Ni Msingi wa Maisha YakoMtazamo wako wa kiakili unafanya kazi kama *kichujio* huathiri kila u...
27/10/2025

Mtazamo wa Akili (Mindset) Ni Msingi wa Maisha Yako

Mtazamo wako wa kiakili unafanya kazi kama *kichujio* huathiri kila unachokiona, unachokipitia, unachokihisi, na hata maamuzi unayofanya. Sayansi kupitia dhana ya *neuroplasticity* imethibitisha kuwa *ubongo una uwezo wa kubadilika*, kujenga njia mpya za kufikiri kulingana na mawazo na tabia unazochagua kuziendeleza.

Hii ina maana kuwa *haujafungwa na fikra au mazoea ya zamani.* Unaweza kuamua leo kubadili namna unavyofikiri, ukapinga imani zinazokurudisha nyuma, na ukafungua milango ya uwezekano mpya. Kwa kufanya hivyo, unajipa nguvu ya kuvuka vizuizi vya ndani na kuumba maisha yenye utimilifu zaidi.

*Hatua ya kwanza ni hii:* *Tambua kuwa tayari una hiyo nguvu ndani yako.*
Usisubiri mazingira yabadilike badilisha mtazamo wako, na maisha yako yataanza kubadilika pia.

27/10/2025

JE KUTAHIRIWA NI LAZIMA KIROHO

NUKUU YA LEOSi kila anayekuchekea ni rafiki, na si kila anayekukosoa anakuchukia... Maisha ni somo, akili ni kalamu, cha...
26/10/2025

NUKUU YA LEO

Si kila anayekuchekea ni rafiki, na si kila anayekukosoa anakuchukia... Maisha ni somo, akili ni kalamu, chagua wapi pa kuandika.

Happy Sun day

USIACHE KUSOMA ITAKUSAIDIA SANA 👇👇Inauma sana kuachana!! Ila inauma zaidi kama uliweka na malengo yako hapo — ila inauma...
25/10/2025

USIACHE KUSOMA ITAKUSAIDIA SANA 👇👇

Inauma sana kuachana!! Ila inauma zaidi kama uliweka na malengo yako hapo — ila inauma zaidi kupoteza muda wako for nothing!! Mbaya zaidi kama ulianza kuwatonya wazazi nina mtu halafu AKAKUACHA.

Ila acha nikwambie kitu, muda mwingine MUNGU ana waondoa watu wasio sahihi kwenye maisha yetu sababu AMEONA na KUSIKIA ambayo sisi hatuna uwezo wa kuona wala kusikia. Unaweza kumlilia mtu ambaye ulipaswa ushukuru kwa kukuacha SALAMA.

Wote waliotuacha hawakuwa wetu. Maumivu ni lazima ila yataisha. Sema ashante MUNGU kwa hii pia, maana una makusudio yako. Halafu MOVE ON — mbona jana iliisha bila uwepo wake, leo pia itaisha hivyo hivyo. Siku mpya itakuja nayo itapita, then maisha yataendelea kama hakuna kilichotokea.

Learn to move in silenceMipango haipigiwi kelele. Shock them with results, not words.
23/10/2025

Learn to move in silence
Mipango haipigiwi kelele.
Shock them with results, not words.

Cheating back does not do anything to your spouse!! You are the one exposing yourself while trying to cheat back You are...
14/10/2025

Cheating back does not do anything to your spouse!!

You are the one exposing yourself while trying to cheat back
You are the one dirtying your spirit
You are the one hurting your conscience
You are the one tricking yourself into believing that you are playing a return match

There's nothing like “cheating back”

You have two options when your spouse cheats on you

Either you forgive or you walk away!

You might end up getting into a deeper mess while trying to cheat back

If cheating is your deal breaker, make it known from the very first day you agreed to date

People who ended up cheating back never got back from that journey

You will end up h8ing your spouse, you will start finding them not attractive anymore, you will end up going deeper into other people

Being cheated on hurts but cheating back? That hurts even more
Don't forget to react on the post, share to who needs it, and Follow this Page lets grow together❤️🤍

Sometimes the person who loves you the most doesn’t know how to show it… and the one who shows it best doesn’t really me...
14/10/2025

Sometimes the person who loves you the most doesn’t know how to show it… and the one who shows it best doesn’t really mean it.

Have you ever experienced this before? ❤️‍🔥

Drop a ❤️ if you’ve been there. Be honest.

Address

Mombasa

Telephone

+254743889082

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Daktari Mwaka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Daktari Mwaka:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram