Tahta shajara sunna Clinic &Jinni Research Centre

Tahta shajara sunna Clinic &Jinni Research Centre Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tahta shajara sunna Clinic &Jinni Research Centre, Medical and health, Imara daima, Nairobi Industrial Area.
(1)

TUNAFANYA VISOMO VYA RUQYA KWA WALE WANA MATATIZO YA MAJINI WABAYA MWILINI NA TUNATOA UCHAWI AU SIHR MWILINI NA HASAD NA KIJICHO KWA KUFANYA VISOMO VYA KISHERIA NA PIA TUNAUZA MADAWA YA KISUNNA

Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatuEwe ndugu yangu katika imani jiepushe sana na ushirikina.Na wale ambao tayari wa...
03/07/2025

Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu
Ewe ndugu yangu katika imani jiepushe sana na ushirikina.
Na wale ambao tayari wameingia katika dhambi hii watubie kwa mwenyezi Mungu kabla ya kufikiwa na siku yao ya umauti

Ushirikiana ni miongoni mwa madhambi makubwa sana na ambayo mwenyezi Mungu anayachukia sana.

05/04/2025
MFAHAMU JINNI HALHAL NA MADHARA YAKE.Huyu ni jinni ambaye humbebea upanga wa kivita iblis laana ya mwenyezi Mungu iwe pa...
01/04/2025

MFAHAMU JINNI HALHAL NA MADHARA YAKE.
Huyu ni jinni ambaye humbebea upanga wa kivita iblis laana ya mwenyezi Mungu iwe pamoja naye na ndiye husababisha umwagikaji wa damu duniani.
Wakati anapojitokeza huwa ni k**a moshi mwingi.

01/04/2025

MFAHAMU JINNI AJULIKANAYE K**A ZUHAL NA MADHARA YAKE.
Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na kwa wale ndugu zetu ambao sio waislamu amani ya mwenyezi Mungu iwe pamoja nanyi.
Ni wakati mwingine tunahitaji kuelezea kuhusu jinni huyu hatari ajulikanaye kwa jina la Zuhal.
Ifahamike kwamba Zuhal pia ni jina la sayari ijulikanayo k**a Saturn ambayo inakuwaga ni jumamosi siku yake.
Majini hawa walikuwa wanaabudiwa na kabila la banu jurhum kabla ya uislamu kufika katika mji wa Makka na kabla ya kuja kwake Nabii Muhammad saww.
Zuhal ni jinni wa kiume anayejulikana k**a Nakruh au Kaywan ambaye baadaye aliabudiwa na chaldean au wachalidei na akajulikana kwa jinna la Kaywannu na pia kwa waebrania walikuwa wanamwabudu na kumuita Kiyyun.
Hawa mabedui walikuwa wanamtumikia jinni huyu walikuwa wanaamini kwamba ni jinni wa kilimo au mazao ya mashambani kwa hivyo alikuwa anahusishwa sana na mafanikio.
Jinni Zuhal ambayo nilitangulia kusema kwamba ni sayari hutawaliwa kwa ukaribu zaidi na mfame Maymunna au Maymun ambaye pia ana jinsia ya kike.Yaani ana jinsia zote mbili jini huyu na jina lake alikuwa anajulikana k**a Abu Nuha ijapokuwa nilikuwa nimeelezea kuhusu maimuna katika darasa za hapo nyuma in sha Allah
Jinni huyu ni miongoni mwa majini ambao hutawala chini ya dunia wakiwa pamoja na jinni marikh au kwa Jina lingine ni Al Muharriq na pia ikiwa ni moja miongoni mwa sayari ambayo siku yake ni Jumanne.
Jinni Huyu wa Zuhal ni miongoni mwa majini wenye mtihani mkubwa sana wakati wanapotumwa kuingia kwa mwili wa binadamu kwasababu wachawi hutumwa kwa wakati maalum.
Ifahamike kwamba jinni huyu huwa hakai ndani ya mwili mda wote na hapo ndipo inapokuwaga vugumu sana kwa matabibu ambao hawajui aina za majini na jinsi ya kuwatoa huwa wanapata mtihani kwa viumbe hawa na pia ni miongoni mwa majini wenye nguvu kubwa sana.
Ifahamike kwamba jinni huyu ni mfalme kwa hiyo hata kafara yake ni kubwa ambayo hupewa ili akubali kufanya kazi na hapo ndipo anakuwa mgumu sana kutoka mwilini na madhara yake ni makubwa sana.
Tiba yake ni kutumia mafusho ambayo hutumiwa kwa kila sayari kisha yachanganywe pamoja na halafu afanyiwe kisomo cha Ruqya mfululizo kwa mda wa siku 45 hadi 90 mgonjwa atapona kwa uwezo wa mwenyezi Mungu mtukufu.
Na pia kutahitajika dawa za kula na kunywa na kujipaka mwili mzima kwa muda huo.
Mgonjwa azidishe ibada zaidi na kusoma Quran tukufu na haswa swala za usiku yaani tahajjud.
Kudumisha usafi ni muhimu zaidi kwa mtu ambaye anafanyiwa tiba ya jinni huyu na kujiepusha na kuskiliza mambo ya upuuzi.
***IFAHAMIKE KWAMBA JINNI HUYU HUSABABISHA MARADHI YA KIFAFA***
Kwa matibabu zaidi au ushauri au maoni au mapendekezo wasiliana nami Suleyman Maina wakati wowote kwa namba zifuatazo za WhatsApp/Imo/Telegram.

☎️+254799659791 ☎️+254100987379 ☎️+254773434443

21/03/2025

Big shout out to my new rising fans! Asia Julius

WAFAHAMU MAJINI MBALIMBALI MADHARA YAKE.Kwasasa nahitaji kuelezea kuhusu huyu jinni ajulikanaye k**a Yusuf bin wasif au ...
21/03/2025

WAFAHAMU MAJINI MBALIMBALI MADHARA YAKE.

Kwasasa nahitaji kuelezea kuhusu huyu jinni ajulikanaye k**a Yusuf bin wasif au Yusuf bin yasif.
Huyu ndiye mtume wa mwisho wa kijinni aliyekuwa ametumwa na jinni kwa majini waasi mkuu Azazeel
Tunaambiwa kwamba wakati jinni huyu alikuwa ametumwa kuna mitume wengine wawili walikuwa wameuwawa na hao majini waasi na huyu akawa amejeruhiwa vibaya zaidi na wakati alipopeleka taarifa kwa jinni mkuu huyu ambaye ni azazeel afanya vita vilivyokuwa vikubwa sana na majini na ifahamike kwamba vita vya kwanza vilikuwa vimepiganwa na malaika kipindi hicho iblis au huyo Azazeel akiwa mtoto mdogo sana.
Hii ni kabla ya kuumbwa baba yetu Adam as.
Kwa wale wanaosumbuliwa na majini wabaya mwilini au hasad au sihr tunafanya visomo vya Ruqya kwa uwezo wa mwenyezi Mungu na kutibu maradhi yote hayo.
Na pia tunauza madawa ya kisunna ya kutibu matatizo hayo yote na mengine mengi kwa uwezo wa mwenyezi.
Kwa matibabu zaidi au ushauri au maoni au mapendekezo wasiliana nami Suleyman Maina kwa namba zifuatazo.
Tunapatikana WhatsApp/Imo/Telegram wakati wowote.
☎️+254100987379 ☎️+254799659791 ☎️+254773434443

YAFAHAMU MAJINA YA MAJINI NA MADHARA YAKE.Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na kwa wale ...
21/03/2025

YAFAHAMU MAJINA YA MAJINI NA MADHARA YAKE.
Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na kwa wale ndugu zetu ambao sio waislamu amani ya mwenyezi Mungu iwe pamoja nanyi.
Kwasasa nahitaji kuelezea kuhusu jinni huyu aitwaye Katahur.
Jinnul Katahur ndiye jinni aliyekuwa ametumwa kumpeleleza nabii suleyman as.
Mfalme wa kijinni huyo ambaye alikuwa amemtuma jinni Katahur ndiye aliyempa mtihani nabii suleyman as kwa mda akiwa amejifananisha na nabii suleyman as baada ya kumuibia pete yake hadi kufikia kukosa ufalme kwa fulani.
Habari hizi kwa upana nitazielezea hatua kwa hatua in sha Allah.
Kwa wale wanaosumbuliwa na majini wabaya mwilini au hasad au sihr au matatizo mengine mengi tunayatoa kwa kufanya visomo vya Ruqya kwa uwezo wa mwenyezi Mungu.
Na pia tunauza madawa ya kisunna ya kutoa matatizo hayo na mengine mengi kwa uwezo wa mwenyezi Mungu.
Kwa matibabu zaidi au ushauri au maoni au mapendekezo wasiliana nami Suleyman Maina kwa namba zifuatazo za
Imo/WhatsApp/Telegram wakati wowote tunapatikana.
☎️+254799659791 ☎️+254100987379 ☎️+254773434443.

AINA ZA MAJINI NA MADHARA YAKE.Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na kwa wale ndugu zetu ...
21/03/2025

AINA ZA MAJINI NA MADHARA YAKE.
Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na kwa wale ndugu zetu ambao sio waislamu amani ya mwenyezi Mungu iwe pamoja nanyi.
Leo nitaelezea kwa ufupi kuhusu jinni aitwaye Bubu.
Jinni huyu huingia kwa watoto wadogo nyakati za jioni na mtoto wako dalili zake hijidhihirisha mara moja na ndo maana mtume saww ametuwekea nidhamu kuhusu watoto wetu nyakati za magharibi kwamba ikifika jioni watoto wawe ndani ya nyumba na milango na madirisha yawe yamefungwa.
Nidhamu hii tuliyowekewa lengo lake ni kuwalinda watoto wetu dhidi ya hawa majini wakorofi ambao wakati wanaingia mwilini baadhi ya dalili zake ni mtoto kutapika na kulia sana na pia macho kubadilika pia mtoto anakataa kunyonya au kula chakula
Mtoto pia mwili wake unakuwa na joto na anaanza kushtuka shtuka na kukosa usingizi au hata kupoteza fahamu na tabia hizo anakuwa nazo usiku tu lakini mchana yuko sawa.
Ukiona dalili baadhi ya hizi afanyiwe kisomo cha Ruqya kabla ya kumpeleka hospitali.
Unaweza pia ukatumia mafuta ya habat sawda kumpaka mwili mzima
Muogeshe kwa maji ya zamzam k**a unayo au umuogeshe kwa maji ya Ruqya (maji ya tahlil)
Ukiwa huna vitu vyote hivyo basi chukua kitunguu thawm utwange na kisha msugue mwili mzima mara 2 kwa siku in sha Allah atapona.
Kwa wale wanaosumbuliwa na majini wabaya mwilini au hasad au sihr tunafanya visomo vya Ruqya na kutoa matatizo hayo kwa uwezo wa mwenyezi Mungu.
Na pia tunauza madawa ya kisunna ya kutoa matatizo hayo na mengine mengi na k**a uko mbali pia tunatuma mzigo na utafikiwa popote ulipo kwasababu sisi ni waaminifu.
Kwa matibabu zaidi au ushauri au maoni au mapendekezo wasiliana nami Suleyman Maina kwa namba zifuatazo.

Tena tunapatikana wakati wowote in sha Allah
☎️+254799659791 ☎️+254100987379 ☎️+254773434443

KWANINI MAJINI WENGI SIKU HIZI HAWATOKI?Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na pia kwa wal...
20/02/2025

KWANINI MAJINI WENGI SIKU HIZI HAWATOKI?
Asalam Alaykum warahmatullahi wabarakatu ndugu zangu katika imani na pia kwa wale ndugu zetu wasiokuwa waislamu Amani ya mwenyezi Mungu iwe juu yenu.
Baada ya mapumziko ya mda mrefu sana ndo tumerudi rasmi na tunaanza na mada hii hapa.
Kwanini majini wengi hawatoki mwilini hata baada ya mtu kufanyiwa kisomo cha Ruqya?
Kuna mambo kadhaa ambayo husababisha majini kukosa kutoka mwilini au wanatoka na kurudi mwilini kwasababu zifuatazo.
_✍️Sababu ya kwanza inatokana na mgonjwa kukosa kukubali kwamba yeye ni mgonjwa hivyo basi anakosa kushirikiana na tabibu wakati anapofanyiwa tiba.kwa mfano watu wengi sana ambao nimekutana nao hukosa kufuata masharti ya tabibu.
✍️ Watu wengi wanaofanyiwa kisomo cha Ruqya wanakosa kuiamini Quran tukufu na hivyo kuw na shaka na tiba.
✍️Kukaa sana na janaba baada ya kufanya tendo la ndoa pia ni sababu kubwa sana ambayo husababisha majini kurudi mwilini baada ya kutoka.
✍️ Kupenda sana tabia chafu ya uzinifu
✍️Kukaa mda mrefu bila kuwa na udhu
✍️Kuacha kusali au unaswali wakati unaotaka
✍️ Kusikiliza mambo ambayo hayana maana yeyote yaani ya kipuuzi k**a vile nyimbo,usengenyaji na kuongea uongo,kudhulumu watu haki zao na mambo mengine mfano wake.
✍️Kukosa kutoa sadaka, ifahamike kwamba mtume saww ametwambia kwamba sadaka ni kinga
,,✍️ Kukosa kusoma dua k**a vile tumeamrishwa na mtume saww kila pahala tunapokwenda na chochote tunachofanya.Siku hizi tumeacha mfumo wa kidini na tunataka kufuata umagharibi na hatuoni tena haja ya kufuata Quran tukufu na sunna za mtume saww.Mambo yetu ya kidini yamebaki mdomoni tu na sio katika vitendo.
✍️Kuchanganya tiba ya kisheria na shirki lazima kutakuwa na tatizo kubwa sana kwa mgonjwa.
Kwa wale ambao wanahitaji kufanyiwa visomo vya Ruqya ya kisheria au wanayo maswali au maoni wawasiliane nasi kwa namba zifuatazo.
☎️+254799659791 ☎️+254100987379 ☎️+254773434443

04/08/2024

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Sharamo Hadija, Carabow Ali

Address

Imara Daima
Nairobi Industrial Area

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tahta shajara sunna Clinic &Jinni Research Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Tahta shajara sunna Clinic &Jinni Research Centre:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram