Yunusu AFYA Clinic

Yunusu AFYA Clinic Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Yunusu AFYA Clinic, Medical and health, Kaloleni, Arusha.

YUNUSU AFYA CLINIC
Tunatoa huduma mbalimbali za kiafya kama vile:
•P.I.D
• HORMONE IMBALANCE
•UVIMBE KWENYE KIZAZI
•U.T.I & FANGASI SUGU
•BAWASILI
•MAGONJWA YA MIFUPA NA VIUNGO

*HEPATITIS *Ni maambukizi yanayotokea kwenye *INI*,kutokana na sababu mbalimbali.Sababu kubwa inayotajwa ni .*VIRAL INFE...
29/08/2022

*HEPATITIS *

Ni maambukizi yanayotokea kwenye *INI*,kutokana na sababu mbalimbali.

Sababu kubwa inayotajwa ni .*VIRAL INFECTIONS *
Lakin kuna baadhi ya visababishi mbalimbali vinavyoweza kupelekea ugonjwa huu.
•unywaji wa pombe kupitiliza
•matumizi makubwa ya madawa,mfano kwa wagonjwa wa sukari,presha,pumu,mifupa nk
•matatizo mengine ya kiafya
•uvitaji wa sigara.
•matumizi mengine ya vinywaji vyenye na kemikali.

*KUNA AINA ZA HEPATITIS*
—————————————-
• *hepatitis A:* hii hutokea kupitia matumizi ya maji ambayo si salama
———————————————
•*hepatitis B:* hii huambukizwa kupitia kugusana kwa mwili na mwili,damu,jasho,nk.
——————————————-
•*hepatitis C:* hutokea pia kwa kugusana na mtu mwenye maambukizi
——————————————
•*hepatitis D:* huambukizwa kupitia damu ya mtu mwenye maambukizi.
—————————————-
•*hepatitis E:* huambukizwa kupitia chakula na maji.

•*ALCOHOLIC HEPATITIS * hii inatokea baada ya pombe kuathiri ini na kuvimba

Pia baadhi ya tafiti mbalimbali zinasema
AUTO IMMUNO pia ni moja ya sababu zinazopelekea ugonjwa huu.
Na watu wapatao 800,000 hufariki kila mwaka kutokana na ugonjwa huu.

*DALILI AU VIASHIRIA VYA UGONJWA HUU *
Watu wengi wanaoshi na maambukizi ya ugonjwa huu huwa hawaoneshi dalili mapema hasa hepatitis B,C mpaka tatizo liwe kubwa zaidi.
Miongoni mwa dalili ni k**a ifuatavyo :
•uchovu wais mwili
•mkojo kuwa rangi ya dark
•kupungua uzito
•maumivu ya tumbo
•kukosa hamu ya kula
•macho kuwa ya njano na ngozi (jaundice)nk.

*UGONJWA HUU UNAWEZA KUPELEKEA MADHARA MAKUBWA YAFUATAYO.*
•chronic liver disease
•cirrhosis
•liver cancer
•Portal hypertension
•fluid in the abdominal cavity
•kidney failure
•death

UGONJWA HUU UNAWEZA KUZUILIKA KWA KUCHOMA CHANJO .

Pia tunatoa suppliments nzuri kwa ajili ya kukinga na kupambana na ugonjwa huu mpaka kutibika vizur kabisa.
NB:kila moja anashauriwa kutumia suppliments hizi ili kulinda ini kupitia mfumo wa maisha ambayo kila moja hawezi kuepuka.

*By dr.yunus *
*0655203943*

FAHAMU LEO KUHUSU UGOJWA WA MIFUPA UITWAO OSTEOPOROSIS NA TIBA YAKE NINI MAANA YA UGOJWA HUU? Ni ugojwa unaompata mtu ba...
27/08/2022

FAHAMU LEO KUHUSU UGOJWA WA MIFUPA UITWAO OSTEOPOROSIS NA TIBA YAKE

NINI MAANA YA UGOJWA HUU?
Ni ugojwa unaompata mtu baada ya mifupa kupungua uzito ,ikiwa Ni pamoja na kupoteza madini muhimu Mfano; Calcium


SABABU ZA UGOJWA HUU
★Kupungua kwa madini ya calcium mwilini
★Historia ya kifamilia
★Matumizi mabaya ya madawa ya kupunguza maumivu
★Uzito mkubwa kupitiliza
★matumizi ya pombe/(vilevi)

NANI YUPO KWENYE HATARI?
_Mwanamke mwenye umri mkubwa (40+
_Mwanamke aliyetolewa kizazi
_Mwanamke ambao hawapati hedhi.kuanzia 6months
_Wanaume wanao fanya kazi ngumu;Kama vile kubeba vyuma (body builders)
_Watu wanaofanya riadha muda mrefu

DALILI ZA KUPATA UGONJWA WA OSTEOPOROSIS
•Maumivu ya mwili wakati wa baridi
•Maumivu ya mifupa
•Kupungua kwa uzito
•Kusaga kwa meno
•Maumivu makali ya mgongo na kiuno.

MARHARA
»»Kuvunjika kwa urahisi
»»Kusagika kwa pingili za mgongo.
»»Kupishana kwa pingili za mgongo.
»»Matatizi ya mfumo wa fahamu.
»»Magojwa ya kusahau.

NB;Kwanini watu wengi wanatimia dawa nyingi za kutuliza maumivu bila kupata matokeo?
• jibu ni kwamba matumizi makubwa ya aina hizi za dawa zinapelekea kudhoofisha mifupa ,kwa hiyo unaongezea tatizo lila kujua.

Kwa MAWASILIANO ZAIDI TUPIGIE SIMU:0655203943
Dr.yunus
https://wa.me/message/Q774FNF2XIBAA1

*VIDONDA VYA TUMBO *Vidonda vya tumbo husababishwa na nini?Mara nyingi vidonda vya tumbo huwatesa watu wengi sana bila k...
13/08/2022

*VIDONDA VYA TUMBO *

Vidonda vya tumbo husababishwa na nini?

Mara nyingi vidonda vya tumbo huwatesa watu wengi sana bila kujua sababu za msingi.

Asilimia kubwa ya vidonda vya tumbo hutokea baada ya kuzalishwa kwa acid nyingi na kuanza kuunguza kuta za o esophagus,sehemu za utumbo mkubwa au utumbo mdogo,
Pia sababu zingine ni kuwepo Kwa maambukizi ya bakteria jamii ya H.pylor ambao hushambulisha tissue lain za kwenye kuta za tumbo,

Watu wanaotumia dawa za kupunguza maumivu muda mrefu pia wapo kwenye hatari ya kuugua ugonjwa huu.

DaLili za ugonjwa huu
Ni kutokea kwa maumivu yanayo ambatana na kuwaka moto eneo la katikati ya tumbo au juu ya tumbo

Maumivu ya kuja na kupotea hasa baada ya kumeza dawa za maumivu au vyakula vyenye Acid

Kupata kiungulia
Kupata kichefuchefu au kutapika.

Matibabu ya ugonjwa huu yapo pia yakizingatia na elimu ya lishe.

*Tibanzuri ipo*

By dr yunus.

*LEO TUJIFUNZE KUHUSU KINGA YA MWILI.*Unaweza ukawa unajiuliza je kinga ya mwili ni nini?Majibu: kinga ya mwili ni mtand...
04/08/2022

*LEO TUJIFUNZE KUHUSU KINGA YA MWILI.*

Unaweza ukawa unajiuliza je kinga ya mwili ni nini?

Majibu: kinga ya mwili ni mtandao/muunganiko mkubwa wa organs,seli nyeupe za damu (WBC),proitins (antibodies) na kemikali (homorne),Ambazo zinafanya kazi kwa pamoja kuzuia na kupambana na bacteria,virus,parasites,na fungi,ili zisiweze kuleta magonjwa kwenye mwili.

Kuna baadhi ya Aina za kinga ya mwili.
•innate immunity-hii ni kinga ambayo mtu anazaliwa nayo.
•adaptive immunity-hii inazalishwa kwenye ini
•passive immunity-hii inatokana na vyanzo mbalimbali kwenye mwili.

*VYANZO VINAVYO TAJWA KUPELEKEA KINGA YA MWILI KUSHUKA.*
• uvutaji wa sigara
•unywaji wa pombe
•ulaji mbovu (industry food,vinywaji,nk
•matumizi ya dawa muda mrefu/na mionzi
•maambukizi ya bacteria,virus mara kwa mara,
•umri
•kutofanya mazoezi nk

*DALILI ZIPI ZINAKUONESHA WEWE KINGA YAKO IMESHUKA?*
•kuhisi barid mara kwa mara
•kuchelewa kupona kidonda
•uchovu mara kwa mara
•kusumbua kwa tumbo (kutopata choo vizur ,mingurumo,gesi,viungulia nk)
•shida kwenye ngozi(miwasho,vipele nk)
•magonjwa ya kinga ya mwili
•maambukizi ya mara kwa mara mfano mafua,kikohozi,UTI,fangasi nk.

*MADHARA YA KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI *

• homa zisizoisha
•mwili kunyongonyea
•kukosa raha
•msongo wa mawazo
•viungo kushindwa kufanya kazi yake vzr,mfano kushindwa kukamilisha tendo la ndoa nk
•kifo.

*NINI UFANYE ILI KUPANDISHA KINGA YA MWILI?*

•fanya mazoezi
•tumia suppliments zinazopandisha kinga kwa haraka
•kula vizuri/kulala vzr
•epuka matumizi ya pombe/sigara
•epuka ulaji mbovu.

*
*TUNAZO SUPPLIMENTS NZURI KWA AJILI YA KINGA YA MWILI KWA HARAKA,INAFAIDA YA KUKINGA NA KUTIBU MAGONJWA YOTE MWILINI (UYOGA MWEKUNDU).*

By Dr.yunus
0655203943.

Fahamu leo kuhusu ugonjwa wa mifupa uitwao:OSTEOPOROSIS.Ugonjwa huu unatokea kwa mtu pale ambapo mifupa inapungua uzito ...
30/07/2022

Fahamu leo kuhusu ugonjwa wa mifupa uitwao:OSTEOPOROSIS.

Ugonjwa huu unatokea kwa mtu pale ambapo mifupa inapungua uzito (density) na kuwa dhaifu.

SABABU ZA KUTOKEA UGONJWA HUU.

zipo sababu nyingi zinazotajwa lakin kuna sababu Ambazo zinaongoza k**a vile
• kuishiwa madini muhimu k**a vile calcium.
•Ajali
•historia ya familia
•ulevi
•ulaji mbovu
•matumizi ya steroid drugs
•uzito mkubwa

KUNDI LA WATU WALIOPO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU

•Wanawake
Mwanamke anakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa hasa ambaye amefikia umri wa kukoma hedhi ,kipindi hiki kiwango cha homorne ya OESTROGEN hushika sana,ambaye husaidia pia katika Afya ya mifupa hivyo kupelekea mifupa kudhoofika.

•wanaume
Sababu kubwa ya moja kwa moja ya mwanaume kupata ugonjwa huu haijulikan (unknown)
Baadhi ya tafiti zinaonesha kuwa wanaume ambao wana changamoto ya homoni ya kiume (testosterone) ikiwa chini pia yupo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu.
Homoni hii ndio inamfanya mwanaume aweze kuitwa baba na inazalishwa katika testical na kiwango kidogo kinazalishwa katika tezi dume.
Lakini kuna makundi ya watu wengine ambao wapo kwenye hatari
•wanawake waliofanyiwa upasuaji wa kutolewa kizazi.
•wanawake ambao wanakaa kuanzia miezi 6 bila kuona hedhi
•wanawake ambao wanawahi kukoma hedhi kabda ya 45 yrs

UGONJWA HUU UNAWEZA KUPELEKEA PIA CHANGAMOTO ZA MAUNGIO.(osteoarthritis)

Huu ni ugonjwa ambao unahusisha kulika kwa gengedu kwenye maungio na kuisha kwa uteute na kupelekea mifupa kusagana.

UGONJWA HUU UMEGAWANYIKA KATIKA SEHEMU 2.
1.primary osteoarthritis.
2.secondary osteoarthritis,

Ugonjwa huu husababisha maumivu makali sana ya mifupa na viungo.
Idadi kubwa sana ya watu wanaendelea kumeza dawa za maumivu bila kujua ni moja ya sababu za kuchochea ugonjwa huu.

Leo hii nimekuletea tiba kamili kwa wewe Ambaye unasumbuka na ugonjwa au ndugu jamaa na rafiki.
Pia wewe ambaye umri umeenda huna budi kutumia huduma yetu.

By DR.YUNUS
0655203943.

0655203943.Kwa mtu yoyote mwenye umri wa 35yrs na kuendelea anahitaji kurepair DNA 🧬 zake ili kulinda kupata magonjwa ya...
14/05/2022

0655203943.

Kwa mtu yoyote mwenye umri wa 35yrs na kuendelea anahitaji kurepair DNA 🧬 zake ili kulinda kupata magonjwa yatokanayo na umri, k**a vile,magonjwa ya moyo,presha,sukari,tezi dume,magonjwa ya akili,saratani,magonjwa ya mifupa nk,NMN ni bidhaa ambayo una repair DNA kwa kiwango cha hali ya juu sana faida nyingine ni ant aging,insulin sensitivity kwa watu wenye na kisukari. Wenye shida za macho,ngozi nk,inapatikana kwa ofa ya 190000/=

SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER) 0655203943Ø Ni saratani inayoongoza kwa wanaumeØ Tezi la uzazi la kiume (Prostat...
12/05/2022

SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER)

0655203943

Ø Ni saratani inayoongoza kwa wanaume
Ø Tezi la uzazi la kiume (Prostate)- ni moja ya tezi la uzazi, lilopo chini ya kibofu cha mkojo, mbele ya utumbo.
Ø Inauzunguka mpira unaootoa mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume.
Ø Inatengeneza majimaji meupe yanayotengeneza asilimia kubwa ya shahawa (haitengenezi shahawa)


NINI DALILI ZA SARATANI YA TEZI DUME:

Ø Saratani ya tezi dume inapooanza huwa hakuna dalili na wengi hufa kabla hawajajijua kuwa wana ugonjwa
Ø Huanza k**a uvimbe
Ø ‘D’ tatu-
Ø Dash-kukimbia chooni mara unapojisikia haja
Ø Delay-Ufikapo chooni mkojo unachelewa kutoka
Ø Inavyoendelea kukua inabinya mishipa ya kutolea mkojo na kusababisha kukojoa kwa tabu
Ø Dribble-Hata ukitoka ni kwa kuchuruzika
UGUNDUZI

Ø Ngazi za awali haina dalili
Ø Upimaji wa tezi hufanyika kwa kidole kuingizwa kwenye haja kubwa, kuangalia uvimbe (ngumu)-k**a ndogo sana daktari hawezi kuigusa
Ø Upimaji wa damu-Prostate Specific Antigen (PSA)-inapima protini inayotengenezwa na seli za tezi
TIBA

Ø Upasuaji (surgery)
Ø Mionzi (Radiotherapy)
Ø Protoni (proton therapy)
Ø Vichocheo (Hormonal therapy)
Ø Tiba ya kemikali (chemotherapy)
Ø Tiba ya ubaridi (cryotherapy)
KINGA

Ø Tafiti bado zinaendelea kuona k**a vitu vifuatavyo vina uhusiano na saratani ya tezi dume
Ø Vyakula vyenye mafuta kiasi
Ø Vyakula vyenye soya
Ø Vyakula vyenye “lycopene”-inapatikana kwenye nyanya, tikiti maji, na matunda mengine

HERNIATED DISK /SLIPPED DISC (PINGIRI ZA UTI WA MGONGO KUPISHANA) ▶Ni maumivu yanayotokea baada ya ringi ya nje ya uti w...
09/05/2022

HERNIATED DISK /SLIPPED DISC (PINGIRI ZA UTI WA MGONGO KUPISHANA)
▶Ni maumivu yanayotokea baada ya ringi ya nje ya uti wa mgongo kuwa dhaifu na kuruhusu Ringi ya ndani kutoka nje .Hutokea kwenye lumber 5 na sacrum 1 hii hupelekea maumivu makali sana .
◾Uti Wa mgongo umegawanyika katika sehemu tano
1.cervical vertebrae INA pingiri 7 hii ndio Shingo
2.Thoracic vertebrae hii INA pingiri 12
3.Lumber vertebrae hii INA pingiri 5
4.sacrum vertebrae hii Ina pingiri 3
▶Disc zikipishana MTU husikia maumivu makali na ganzi kwasababu Neva za kwenye pingiri hubanwa MTU hupata ganzi miguuni sababu scia sciatic Neva hubanwa,na ganzi mgongoni na mwili pinched Neva hubanwa .Ganzi ya muda mrefu hupelekea kuparalaizi mwili

▶DALILI ZA PINGIRI ZA UTI WA MGONGO KUPISHANA
1.Maumimu kwenye kiuno yasiyoisha
2.Ganzi mwili mzima
3.maumivu ukusimama au kukaa muda mrefu
4.maumivu ukitembea
5.kukaza kwa kiuno
6.udhaifu Wa misuli na kukaza kwa misuli Mara kwa Mara
7.Kukosa balance ya kusimama
8.kukosa hisia za tendo la ndoa .
9.Kupoteza kumbukumbu
10.kupata shida kutembea vizuri
11.miguu kuwaka moto chini ya unyayo.

FAIDA ZA UYOGA MWEKUNDU KIAFYAKazi zake kwa mtumiaji• Inaongeza kinga ya mwili hivyo muhimu kwa wote wanaougua mara kwa ...
15/03/2022

FAIDA ZA UYOGA MWEKUNDU KIAFYA

Kazi zake kwa mtumiaji
• Inaongeza kinga ya mwili hivyo muhimu kwa wote wanaougua mara kwa mara.
• Inapandisha CD4 mwilini, hivyo ni muhimu kwa kusaidia wenye HIV/AIDS
• Inazuia matatizo ya moyo k**a kutanuka kwa moyo
• Inazuia uzalishwaji wa seli za kansa
• Inapunguza madhara ya mionzi (chemotherapy)
• Inasaidia kuboresha mapafu na mfumo wa upumuaji.
• Inaongeza hamu ya kula
• Inaboresha mzunguuko wa damu katika mishipa mikubwa,hivyo kusaidia watu wenye presha
• Inaponya mishipa ya fahamu. na kuboresha seli za ubongo
• Huondoa mizio (allergy) aina zote.
• Inalinda na kusaidia figo na kufanya ifanye kazi vizuri. • Ni imara kushindana na virusi, fungus, bacteria na wadudu wengine mwilini
• Inasaidia kuondoa sukari,inafanya damu iloganda iyeyuke na inaondoa sumu mwilini.
• Ni rahisi kuyeyuka kwa 100% hivyo kuleta matokeo ya haraka sana

0766786266
0655203943

ZIFAHAMU AINA ZA MAAMBUKIZI YA BAKTERIA KWENYE VIA VYA UZAZI.Maambukizi kwenye via vya uzazi yanajulikana kitaalamu k**a...
21/02/2022

ZIFAHAMU AINA ZA MAAMBUKIZI YA BAKTERIA KWENYE VIA VYA UZAZI.

Maambukizi kwenye via vya uzazi yanajulikana kitaalamu k**a pelvic inflammatory disease.(P.I.D),tatizo hili limekuwa tamko la kawaida sana kutamkika katika jamii ya leo,na limekuwa la kawaida sana mtu kuishi nalo,bila kutambua madhara makubwa yatampata hapa mbeleni.

SABABU ZA KUPATA MAAMBUKIZI HAYA.

Zipo sababu nyingi sana ambazo zinapelekea kupata maambukizi katika via vya uzazi lakini sababu kubwa ni aina ya bakteria waitwao NEISSERIA GONORRHEA,CHLAMYDIA Pia kuna sababu zingine ambazo huwa zinapelekea tatizo hili.
•wakati wa kujifungua
•matumizi ya uzazi wa mpango kiholela
•kutoa mimba au mimba kutoka
•kuwa na wapenzi wengi na kutochukua tahadhar
•kujiingizia vidole ukeni
•kuweka vitu vyenye kemikali ukeni
•kutotibu vizur uti na fangasi
•matumizi makubwa ya antibiotics kiholela .

DALILI ZINAZO ASHIRIA KUWA UNA MAAMBUKIZI.

•kutokwa na uchafu mzito ukeni ,rangi ya cream,njano au kijani.
•maumivu ya tumbo na vichomi chini ya kitovu
•kukosa hisia za tendo la ndoa
•majmivu makali wakati wa tendo la ndoa
•maumivu ya nyonga,kiuno na mgongo
•uchovu wa mwili na kichefuchefu
•maumivu makali wakati wa hedhi.

MADHARA MAKUMBWA K**A HUJATIBU AU KUCHELEWA KUTIBU TATIZO HILI.

•kushindwa kushika ujauzito
•mimba kutoka
•saratani ya shingo ya kizazi
•mirija kuziba
•mvurugiko wa homoni
•kutokea kwa majimaji kwenye mayai (ovarian cyst).

SULUHISHO LA TATIZO HILI

Ili uweze kupata tiba sahihi ya hili tatizo au unaona dalili za hili tatizo tuwasiliane au fika ofisin kwetu mtaa wa kaloleni,uweze kupata suluhisho la kudumu.

0655203943.
0766786266.

*JE WEWE NI MWANAMKE AMBAYE UMEKARIBIA UMRI WA KUKOMA HEDHI,AU TAYAR UMEKOMA HEDHI (menopause)*. Tafiti zinaonesha akina...
17/02/2022

*JE WEWE NI MWANAMKE AMBAYE UMEKARIBIA UMRI WA KUKOMA HEDHI,AU TAYAR UMEKOMA HEDHI (menopause)*. Tafiti zinaonesha akina mama ambao wapo kwenye umri wa kukoma hedhi au tayar wameshakoma hedhi wapo kwenye hatar ya kupata maradhi yafuatayo.*MAGONJWA YA MOYO*_hii hali inatokea kwa wanawake wengi ambao umri wao umeenda kwa kuwa na madadiliko ya homoni hasa homon ya OESTROGEN kushuka.*MAGONJWA YA MIFUPA (osteoporosis)* mwanamke ambaye yupo kwenye kipindi cha kukoma hedhi madini mengi mwilin hupungua kwa kiwango kikubwa sana hasa CALCIUM,AMINO ACIDS ambapo hupelekea mifupa kuwa mepesi na kuanza kuuma.*MATATIZO YA MKOJO * mwanamke amaweza kupata tatizo la kushindwa kuzuia mkojo kutokana na kipindi hiki cha kukoma hedhi sababu misuli ya mfumo mzima hukosa nguvu na kulegea kutokana na upotevu wa madini muhimu. *MAAMBUKIZI YA VIMELEA MBALIMBALI UKENI.* hii hutokea pale ambapo Sehemu za uke zinakuwa kavu sana kutokana na kushuka kwa homon

Nawasaidia wanawake hawa wenye hii changamoto

0655203943.

Address

Kaloleni
Arusha

Opening Hours

Monday 07:00 - 20:00
Tuesday 07:00 - 20:00
Wednesday 07:00 - 20:00
Thursday 07:00 - 20:00
Friday 07:00 - 20:00
Saturday 07:00 - 20:00

Telephone

+255655203943

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Yunusu AFYA Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram