Mwezeshaji Tiba Lishe

Mwezeshaji Tiba Lishe Chakula Tiba Clinic

Insulin resistance ni neno la kitabibu liki maanisha  kuwa ni kitendo kinachotokea pale chembe chembe hai (Cells) za Mis...
16/01/2025

Insulin resistance ni neno la kitabibu liki maanisha kuwa ni kitendo kinachotokea pale chembe chembe hai (Cells) za Misuli (muscle) Mafuta na Ini kushindwa kupokea sukari kwa msaada wa Hormone ya Insulin.

Cells za Misuli, Mafuta (Adipose tissue), na Ini hupokea na kuhifadhi kiwango cha Sukari kinacho zidi kwenye mzunguko wa damu.

Kazi kubwa ya Hormone hii iitwayo Insulin ni kuhakikisha kiwango Cha (glucose) sukari kwenye mzunguko wa damu kinabaki katika Kiwango sahihi, na chenye afya.

Hivyo Insulin resistance inapotokea huchochea kuongeza kwa mlundikano wa sukari (glucose) kwenye mzunguko wa damu, hivyo na kupelekea kuongeza nafasi kubwa ya kuwa hatari kuugua ugonjwa wa Kisukari.

Hali hii huchochewa na Unene uliokithiri (Obesity) , Magonjwa ya Moyo, Wanawake Wenye Changamoto ya Vimbe kwenye Mayai, Watu wenye viwango kikubwa cha mafuta kwenye Ini na baadhi ya matumizi ya dawa, mfano , ARVS , Prednisone.

Kwa tafiti za kina za kisayansi zinaonyesha insulin resistance husababishwa na kiwango cha mafuta Tumboni,
Kuto kuushughulisha mwili (sedentary lifestyle).

Ukiwa unapitia changamoto hii , Tezi inayo tengeneza Hormone hii huongeza kiwango cha uzalishaji ili kuweza kukabiliana na ongezeko la glucose kwenye mzunguko wa damu.

Kitendo hiki kikifanyika kwa muda mrefu hupelekea cell kupoteza uwezo wa kuzalisha Insulin ya kutosha hivyo hupelekea kuongezeka kwa glucose.

Hivyo mtu anaefikia hatua hii hupata dalili hizi
*Kupoteza uzito usioelezeka
*Uchovu uliokithiri
*Kiu iliyo kithiri
*Kukojoa mara kwa mara.
*Njaa iliyo kithiri
*Uono hafifu.

Jinsi ya kuzuia hali hii isikutokee ni
Mazoezi ,( mazoezi hurahisisha misuli kupokea kirahisi glucose)
Kuepuka mtindo wa hovyo wa Ulaji chakula

Kwa maelezo ya kina wasiliana nasi kwa namba
0783905545
0712808001.

Moja ya sababu ya Ugumba kwa mwanaume ni lishe  ambayo hupelekea mbegu za kiume kupoteza ubora wake.Ndizi mbivu moja ya ...
24/10/2024

Moja ya sababu ya Ugumba kwa mwanaume ni lishe ambayo hupelekea mbegu za kiume kupoteza ubora wake.

Ndizi mbivu moja ya tunda lenye uwezo mkubwa wa kuboresha Mbegu za kiume.
Tunda hili lina Virutubisho (micronutrients) vya kutosha kwa ajili ya kuongeza Uzao.

Tunda hili ni chanzo kizuri cha vitamini A, B1, C ambavyo huchochea nguvu za mwili na kuweka uwiano sawa wa homoni ya msongo (,Stress hormone)

Pia ni chanzo kizuri cha kirutubisho kiitwacho tryptophan ambayo ni chanzo kizuri cha protini ambayo huitajika kwa kutengeneza kemikali ya kujisikia vizuri wakati wote ( serotonin enzymes)

Ndizi pia ni chanzo cha madini ya Potassium ambayo hutumika kwa afya ya moyo na uzalishaji wa mbegu za kiume kwa kuchochea uzalishaji wa homoni Kiongozi ya Kiume (Testosterone hormone) hivyo kuboresha mihemko Asili.

Pia ndizi imebeba (Bromelain nutrient) kirutubisho ambacho huchochea mtiririko mzuri wa damu hivyo huimarisha ulijari wa asili.

Magnesium na manganese ni madini tuyapatayo tunapo kula Tunda hili, kazi kubwa ya madini ni kuboresha ufanisi wa tezi Dume kutengeneza kiwango bora cha msanii (Semen).

Moja kati ya sababu ya  kutokuzalishwa kwa mbegu za kiume kwa uchache au kutozalishwa kabisa na pengine Kusinyaa kwa  Ke...
17/10/2024

Moja kati ya sababu ya kutokuzalishwa kwa mbegu za kiume kwa uchache au kutozalishwa kabisa na pengine Kusinyaa kwa Kende huchochewa na matumizi ya dawa za kutanua Misuli (Body Builder), kuongeza mbio (Athletic).

Dawa hizi hutambulika k**a ANABOLIC ANDROGEN STEROIDS, hutengenezwa Maabara kwa mfanano na hormone za Kiume.

Dawa hizi hutumiwa na Madaktari Kuponya changamoto ya Uhanisi, ambao huchangiwa na Kiwango Kidogo cha hormone ya Kiume (Testosterone).

Kuzalishwa kwa wakati sahihi wa homoni hizi kiongozi hujidhihirisha kwa dalili zifuatazo kipindi cha Barehe (puberty) mfano Kuota nywele, Sauti Nzito, kuongezeka kwa misuli , Ngozi Mororo, Kukomaa kwa mbegu za kiume na Mihemko ya Tendo.

Wanariadha, Wapenda muonekano wa misuli mikubwa, na wale waendao gym kwa mazoea wapo hatarini kupata changamoto ya Uzazi kwa sababu ni rahisi kushawishika Kutumia dawa hizi.

Matumizi ya dawa hizi kwa ajili ya kuongeza Misuli na uimara wa mwili, huusaulisha ubongo kuendelea kutoa maelekezo kwenye Kende kutengeneza hormone kiongozi ya Asili, hivyo kupelekea kutotengenezwa tena Mbegu za kiume na Kende kusinyaa.

Changamoto ya Ugumba inayo sababishwa na Matumizi ya Dawa hizi hutibika, wasiliana nasi kwa namba 0712808001.

Varicocele ni Kati ya sababu kubwa inayo changia Ugumba kwa Wanaume. Mara nyingi huanza ghafula katika hali ya Umri mkub...
13/10/2024

Varicocele ni Kati ya sababu kubwa inayo changia Ugumba kwa Wanaume.
Mara nyingi huanza ghafula katika hali ya Umri mkubwa.
VARICOCELE ni neno la Kitabibu likielezea changamoto ya kutanuka kwa mishipa ya damu aina ya Vein zinazo chukua damu kutoka kwenye Kende.

Changamoto hii husababishwa na udhaifu valve za kwenye mishipa hiyo kushindwa kufanya kazi sawasawa na kupelekea damu kushindwa kurudi kwenye Moyo na kurundikana kwenye mishipa hiyo.

Valve hizi zinazopatikana kwenye mishipa hii inayorudisha damu (Vein) kazi yake ni kuhakikisha damu inatembea kwa mtiririko sahihi.

Kipindi valve zinaposhindwa majukumu yake damu huvutwa na kujikusanya kwenye mishipa ya Korodani (Testicular Vein) na kusababisha hii hali inayoitwa Varicocele (kutanuka kwa mishipa).

Hali hii pia hujionyesha kwa kutanuka kwa mishipa hiyo pindi pale Mwanaume anapopitia changamoto ya Uzazi,
na kuamua kufanya vipimo kwa ajili ya kutafuta Chanzo cha kushindwa kusababisha Mimba kwa mwanamke mwenye uwezo wa kushika mimba
Hali hii mara nyingi huanza kipindi cha barehe (puberty) na kuongezeka kidogo kidogo.

Pia ni moja ya sababu ya Korodani Kusinyaa , Maumivu au Kutokujisikia vizuri na kupungua kwa kiwango cha homoni Kiongozi ya Kiume (Testosterone).
Na mara nyingi Korodani ya kulia huathiri zaidi ukilinganisha na ya kushoto.

Kwa sababu hizi matibabu hutegemea na hizo dalili anazopitia Mlengwa.

Baadhi ya Wanaume wenye changamoto hii huzalisha kiwango Kidogo cha mbegu za kiume na pengine zisizalishwe kabisa.

Kwa kawaida Korodani (Te**is) hufanya kazi ya kuzalisha mbegu Bora za kiume kukiwa na kiwango cha chini ya nyuzi joto tatu (3) cha joto la kawaida la mwili wa Mwanadamu.

Hivyo changamoto hii ya Varicocele huongeza Kiwango cha joto kwenye Korodani na kupelekea kupoteza uwezo wa kuzalisha mbegu za kiume na homoni Kiongozi ya Kiume (Testosterone).

Afya mbaya ya Tezi Dume ni Moja ya changamoto inayoweza kumfanya Mwanaume kushindwa kusababisha Mimba. Tezi Dume ni kiun...
05/10/2024

Afya mbaya ya Tezi Dume ni Moja ya changamoto inayoweza kumfanya Mwanaume kushindwa kusababisha Mimba.

Tezi Dume ni kiungo kinachopatikana chini ya kibofu cha mkojo, Msuli huu huzunguka Njia ya mkojo na inakadiriwa kuwa na Ukubwa k**a Punje ya Njegere kabla ya barehe (puberty),
na baada ya hapo huongezeka kidogo na kufananishwa na Punje ya Almond.

Moja ya kazi yake kubwa kwenye Uzazi ni kutengeneza Manii (Semen) kwa kiwango cha asilimia ishirini kati ya asilimia mia moja.

Majimaji haya yamebeba virutubisho muhimu ambavyo huongeza ufanisi wa mbegu za kiume (s***m) kufanya kazi kwa usahihi,
Mfano ni enzymes , Zinc na kemikali zingine muhimu za kuboresha Mbegu za kiume.

Misuli ya Tezi Dume pia huusika na kusukuma majimaji haya (Semen) kutoka nje kupitia njia ya mkojo (urethra).

Endapo Tezi dume ikishambuliwa na bacteria hupelekea kupoteza ufanisi mzuri wa kazi zake,
hivyo huchochea Mbegu za kiume kupoteza Umbo halisia na uwezo wa kukimbia.

Pia sababu nyingine inayoweza kuchochea Ugumba ni Tezi Dume kuongezeka Ukubwa , na mara nyingi changamoto hii huanzia umri wa miaka arobaini na Tano na mwanzoni mwa Umri wa miaka Hamsini,
Kitabibu changamoto hii huitwa BPH na tafiti za kisayansi zinaonyesha Chanzo chake bado hakifahamiki.

Suhisho ni kubadili Mtindo wa maisha na kuongeza afya ya Tezi Dume
Kwa Ushauri wasiliana nasi kwa
# 0712808001.

Moja ya hatari inayoweza kupelekea mwanaume kushindwa kumtungisha mimba mwanamke mwenye uwezo wa kushika mimba ni Stress...
05/10/2024

Moja ya hatari inayoweza kupelekea mwanaume kushindwa kumtungisha mimba mwanamke mwenye uwezo wa kushika mimba ni Stress.

Stress huja kutokana na uhitaji sambamba na misukumo tunayo Kutana nayo kila siku kwenye maisha ya kawaida,
Mfano, Magonjwa Sugu, Magomvi baina yetu yasiyo pata ufumbuzi, Kufanya jambo juu ya uwezo wetu na mengine mengi.

Pale unapopitia changamoto za muda mrefu mwili wako hutengeneza kiwango kikubwa cha sumu mwilini (Oxidation) , kiasi kwamba mwili wako utashindwa kuondoa sumu , kwa sababu hakuta kuwa na uwiano sawa wa kuondoa sumu mwilini (Antioxidant).

Stress za Muda mrefu huchochea kushuka kwa kiwango cha hormone kiongozi ya Kiume (Testosterone hormone),
hivyo uzalishaji na ubora wa mbegu za kiume hupungua, na pengine kutotengenezwa kabisa.
Pia kitendo hiki hupelekea kupoteza hamu ya tendo la ndoa kabisa.

Suluhisho ni kubadili Mitazamo na Mtindo wa Maisha,
Maana mbali na Uzazi, pia unaweza kupata changamoto Lukuki za afya mfano,
Kukaza kwa misuli,
Kuzeeka haraka,
Kushuka kwa kinga za mwili,
Magonjwa ya mishipa ya damu ya Moyo, Kisukari,
Shambulio la Moyo.
Tupigie kwa Ushauri;
0712808001

Tafiti nyingi za kitabibu juu ya afya ya Uzazi kwa mwanaume huzingatiwa zaidi  ubora wa  hormone Kiongozi ya Kiume ambay...
04/10/2024

Tafiti nyingi za kitabibu juu ya afya ya Uzazi kwa mwanaume huzingatiwa zaidi ubora wa hormone Kiongozi ya Kiume ambayo hufahamika kwa jina la Testosterone hormone.

Moja ya changamoto ya kiafya ambayo huchochea mtiririko mbaya wa hormone hoi (Testosterone hormone) ni Unene uliokithiri.

Uwepo wa misuli mieupe kwa wingi mwilini (white adipose tissue) kwa watu wanene (Obesity) ,
huchochea mabadiliko ya hormone hii (Testosterone hormone) na kuongezeka kwa Estrogen hormone,
Hormone hii ya Estrogen ni kati ya hormone Kiongozi kwa jinsia ya K**e.

Kazi kubwa ya Testosterone hormone ni kuchochea uzalishaji na upevushaji wa Mbegu za Kiume zilizo na sifa za kuwezesha Uzao.

Hivyo kuwepo kwa kiwango kikubwa cha hormone ya k**e (Estrogen) kwa Mwanaume ambayo huchangiwa na Unene uliokithiri huchangia Ugumba.

Kubadilisha mtindo wa Ulaji wa vyakula na Mazoezi, kupunguza Unene hivyo huongeza ubora wa hormone kiongozi ya Kiume na Ugumba kuwa Historia.

Kwa Ushauri wasiliana nasi
0712808001.

Tafiti za kisayansi juu ya Tiba Kinga  zinasema Mwanaume mwenye utaratibu wa kula kiwango cha juu cha Matunda, Mboga zen...
27/09/2024

Tafiti za kisayansi juu ya Tiba Kinga zinasema Mwanaume mwenye utaratibu wa kula kiwango cha juu cha Matunda, Mboga zenye asili ya kijani kibichi, sambamba na mboga za jamii ya kunde, mfano;
Maharagwe, kunde , choroko , Soy, Mbaazi na kwa uchache ulaji wa nyama , Samaki na bidhaa za maziwa, Hawasumbuki kwenye Uzazi.

Kwa sababu Mtindo huu wa Maisha huongeza Ujazo wa Mbegu za Kiume (S***m Concetration) na Uwezo mkubwa wa Kukimbia ( S***m Motility), Ukilinganisha na Mwanaume ambaye anatumia kwa kiwango Kidogo wa vyakula hivyo.

Azoos***mia ni neno la Kitabibu linalo elezea kutokuwepo kwa Mbegu za kiume (S***m) kwenye Manii (Semen) kipindi cha kum...
27/09/2024

Azoos***mia ni neno la Kitabibu linalo elezea kutokuwepo kwa Mbegu za kiume (S***m) kwenye Manii (Semen) kipindi cha kumwaga mbegu (ej*****te).

Na hali hii hutambulika pindi pale Mwanaume anaposhindwa kumpatia Mimba mwanamke mwenye uwezo wa kushika mimba, ambayo humpelekea kwenda hospitali kufanya kipimo.

Kati ya kila Wanaume 200 mmoja kati yao hukutwa na hali hii, na ndio sababu ya muhimu ya Utasa kwa Wanaume.

Sababu zinazopelekea hali hii imewekwa katika makundi mawili;

&: Kundi la kwanza ni wale wenye shida kwenye kiwanda cha kutengenezea Manii hutambulika k**a kende.
Eneo hili la kende (testicles) zinaweza kutengeneza Mbegu kidogo, kiasi kwamba hata wakipima sio rahisi kuziona au zisitengenezwe kabisa.

Sababu kubwa huchangiwa na;
Infection (Mumps)
Tatizo kwenye vinasaba
Kende kushindwa kushuka
Matibabu ya Saratani

&: Kundi la pili ni pale njia ya kusafirishia mbegu kuziba.
Hapa Mbegu za Kiume zinazalishwa k**a kawaida lakini hushindwa kusafiri kutoka nje kutokana na kuziba kabisa kwa mirija ya kusafirishia.
Sababu kubwa huchangiwa na;
Magonjwa ya Zinaa UTI na TB,
Upasuaji uliopita
Tatizo kwenye vinasaba
Muda mwingine changamoto hii sababu hazipo wazi (Hazijulikani).

Moja ya changamoto inayo changia mbegu za kiume kupoteza ubora wake na kupelekea mwanaume kushindwa kumtungisha mimba mw...
23/09/2024

Moja ya changamoto inayo changia mbegu za kiume kupoteza ubora wake na kupelekea mwanaume kushindwa kumtungisha mimba mwanamke ni kiwango cha Joto kuongeza kwenye Korodani.
Korodani ndio kiwanda cha kutengeneza Mbegu za Kiume.

Na ndio maana Korodani zipo mbali na viungo vingine vya ndani vya mwili,
mbali na uwepo wake nje , imeumbwa na mnyororo wa mishipa ya damu yenye uwezo wa kumudu kupoza joto litokanalo na mazingira.

Uwepo wa Msuri uitwao Crimaster huwezesha pia Pumbu zako (Sc***um) kusinyaa nyakati za baridi na pia kulegea (kuning'inia) nyakati za joto hatua hizo ni za kulilinganisha joto,
ili mbegu zako ziendelee kuwa bora na uwezo wa kutungisha Mimba.

Mbegu za kiume hua na tabia ya kufa pindi zinapo Kutana na joto kali.
Kuwepo kwenye mazingira ya joto kali kwa Muda mrefu husababisha kuzalisha umbo lisilo faa kwa mbegu za kiume.

(Higher fever) Homa huchangia tatizo hili, pia shughuli k**a vile za jikoni haswa kupika, Kuchoma, bodaboda, baiskeli na kuvaa nguo ndani zinazo bana mwili huchangia ongezeko la joto mwilini.

Suluhisho;
Pumzika,
Vaa nguo zisizo bana,
Zingatia vipindi vya joto kwa kutafuta njia ya kupoza mwili.

NECROZOOSPEMIA; Ni neno la Kitabibu linalo simama au kuelezea uwepo wa Mbegu za kiume (s***m) zilizo kufa kwenye Manii (...
22/09/2024

NECROZOOSPEMIA; Ni neno la Kitabibu linalo simama au kuelezea uwepo wa Mbegu za kiume (s***m) zilizo kufa kwenye Manii (Semen).

Ni moja Tatizo kubwa linalo sababisha Mwanaume kushindwa kutungisha mimba mwanamke mwenye uwezo wa kushika mimba.

Sababu kubwa zinazopelekea Wanaume wengi kupata Tatizo hili ni;
-Msongo wa mawazo
-Matumizi ya Pombe kupita kiasi.
-Matumizi ya Dawa
-Lishe mbaya
-Matibabu ya Saratani
-Kukaa Muda mrefu bila kufanya mapenzi.

Jinsi ya kukabiliana na Tatizo ni mara nyingi ni kubadilisha Mitindo wa Maisha.

Ini Liver ni Kiungo muhimu sana  mwilini ambacho hufanya Kazi zaidi ya Mia Tano muhimu. Ambazo ni kuchuja kemikali na ta...
26/12/2023

Ini Liver ni Kiungo muhimu sana mwilini ambacho hufanya Kazi zaidi ya Mia Tano muhimu. Ambazo ni kuchuja kemikali na takataka kutoka kwenye damu,, kuchunga Kiwango cha sukari kwenye mzunguko wa damu, hutengeneza virutubisho muhimu.

Hapa Leo kwenye Chapisho hili tutawaeleza KAZI muhimu zaidi za kiungo hiki muhimu.

Uzalishaji wa Albumin,
Hii ni aina ya Protini maalumu kwa ajili ya kuchunga maji yasipotee kwenye mzunguko wa damu kwa kuvuja na kubaki kwenye Misuli.
Pia inahusika na kubeba Vitamin, Dawa , enzymes, Hormones na kupeleka sehemu yeyote ya mwili.

Huzalisha Nyongo; ambayo ni muhimu kwa mmeng'enyo na ufyonzaji wa chakula aina ya mafuta kwenye utumbo mwembamba.

Huchuja Damu; mishipa ya damu inayotoka kwenye mfuko wa chakula na UTUMBO hupita kwenye Ini kwa ajili ya kuchuja sumu na kemikali zingine zinazo hatarisha afya.

Huzalisha viambata; ambavyo huusika na kuufutilia mgambo wenye Afya wa damu

Huchunga Protini; uzalishaji wa protini hutegemea Amino acid hivyo Ini huakikisha Amino acid inabaki katika mazingira ya afya.

Hutukinga na Maambuki; mbali na kitendo hicho cha Ini, pia huondoa bacteria kutoka kwenye mzunguko wa damu na kuficha damu safi.

Huifadhi madini na vitamin; Mfano A,D,E,K na B12 bila kusahau madini ya Chuma na Copper kwa matumizi pale Mwili unapohitaji.

Inachakata Glucose; Ini huondoa sukari iliyozidi kwenye damu na kuihifadhi kwa mtindo wa Glycogen na endapo ikiitajika hubadilishwa kutoka Glycogen kuwa Glucose kwa matumizi ya Cell's.

NB:
Hivyo Ini linapo jeruhiwa au kuvimba utendaji wa kazi wake pia hupoteza mwelekeo, hapo ndio hujitokeza changamoto nyingi za kiafya.

JINSI YA KUTUNZA INI;
Epuka Matumizi holela ya Dawa; Mfano Panadol, kutumia dawa hizi huchangia kujeruhi Cells za Ini na kusabisha madhara ya Muda mrefu.

Epuka Kunywa pombe kupita kiasi, pombe huchochea uzalishaji wa chemikali za ni kwa wingi hivyo ni rahisi kulijeruhi.

Shiriki Mazoezi, huongeza ufanisi wa Organ mwilini pamoja na Ini.

Matumizi ya chakula Tiba vilivyo beba nutrient maalum kwa afya ya Ini.
Kula vyakula maalum kwa Afya ya Ini, Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi hupelekea Ini kushindwa kufanya kazi na kuwa na Mafuta mengi.

Fanya Ngono salama, tumia kinga kujikinga na Magonjwa ya ngono haswa Homa ya Ini C

Pata chanzo dhidi ya homa ya ni A and B . Pia tiba sahihi ya malaria

WATU WALIO HATARINI KUPATA CHANGAMOTO YA INI
Wenye Unene uliokithiri
Wagonjwa wa Kisukari
Wenye Umri Mkubwa,
Metabolic Syndrome
Matumizi ya dawa, panadol, co***ne
Walevi
Homa ya Ini B and C

NB
Usipo zingatia Tiba ya Ini hukupelekea kupata saratani kusinyaa kwa Ini

Kwa Ushauri na Tiba
Tupigie kwa #
0712808001
0783905545

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwezeshaji Tiba Lishe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram