b2care_pharmacy

b2care_pharmacy Tunatoa elimu juu ya lishe ya watoto, umri kuanzia 0-5.Tuko mbezi luis brbr ya kwenda goba 0767980751

Haya mwenye ushauri, changamoto tucoment apo chini.Pia k**a ni ishu binafsi unaweza kutu DM, whatsapp, sms    #076798075...
15/03/2024

Haya mwenye ushauri, changamoto tucoment apo chini.
Pia k**a ni ishu binafsi unaweza kutu DM, whatsapp, sms

#0767980751 # Tupigie mda wowote kwa ishu binafsi

Habari za wakati huu wanafamilia wa b2care.🌺Vitamin ni moja ya kirutubisho muhimu sana kwa watoto.🌺Virutubisho hivi huwa...
12/03/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa b2care.

🌺Vitamin ni moja ya kirutubisho muhimu sana kwa watoto.

🌺Virutubisho hivi huwa havitengenezwi mwilini bali vinapatikana kwenye vyakula mbalimbali.

🌺Vyakula hivyo ni jamii ya wanyama navyo ni :-
-Maini
-Kuku
-Mayai
-Samaki wa ziwani na baharini
-Maziwa ya ng’ombe na vinavyotokana na maziwa.
-Nyama nyekundu
-Mayai nk

🌺Vitamin B12 husidia kuboresha afya ya moyo.
🌺Hushiriki katika kutengeneza seli hai nyekundu za damu.
🌺Husaidia kuboresha afya ya ubongo wa mtoto.
🌺Husaidia kuboresha mfumo wa neva na mfumo wa kinga mwilini.
🌺Hutengeneza ngozi,nywele na kucha zenye afya.
🌺Husaidia mtoto kupata nguvu mwilini.

Hivyo kutokana na faida tajwa hapo juu tujitahidi kuwapa watoto wetu vyakula hivyo tajwa hapo juu.

Asanteni kwa kuwa pamoja nasi🤝.

Habari za wakati huu wana familia wa b2care.🍁Mwili wa mtoto unahitaji nishati kufanya kazi zake zote muhimu za kimwili m...
07/03/2024

Habari za wakati huu wana familia wa b2care.

🍁Mwili wa mtoto unahitaji nishati kufanya kazi zake zote muhimu za kimwili mfano mapigo ya moyo, mmeng’enyo wa chakula, kupumua na harakati nyengine ambazo zinahitaji nishati ambayo inasambazwa na mwili kwa namna ya kalori.

🍁Vyakula vyenye kalori nyingi ndio chachu ya kuongezeka kwa uzito kwa mtoto.

🍁Katika machaguzi ya vyakula vyenye kalori nyingi inabidi pia viwe na virutubisho ndani yake ili kuweza kupata uzito pamoja na afya njema itakayomuwezesha mtoto pia kupambana na magonjwa mbalimbali.

🍁Mzazi/mlezi nimekurahisishia hapa chini kukuoredheshea vyakula vyenye kalori nyingi na virutubisho ndani yake.

🍁Navyo ni:-
🌺Nafaka zisizokobolewa mfano dona
🌺Mayai
🌺Maziwa fresh, mtindi,cheese.
🌺Nyama ya ng’ombe, mbuzi
🌺Samaki
🌺Maharage, dengu
🌺Peanut butter , siagi ya amond au korosho
🌺Viazi lishe
🌺Parachichi

Hivyo mzazi/mlezi jitahidi sana katika kumpatia mtoto wako vyakula vyenye kalori ya kutosha kutokana na faida tajwa hapo juu.

Asanteni kwa kuwa pamoja nasi🤝.
Like na mtag mwenzio aje apate elimu hii.


Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Wazazi na walezi wengi huwa wanapata wakati mgumu kujua ni Milo mingapi anat...
04/03/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Wazazi na walezi wengi huwa wanapata wakati mgumu kujua ni Milo mingapi anatakiwa apewe mtoto wake.

🌷Idadi ya Milo ndio itamsaidia mtoto kuongezeka uzito pia.

🌷Kuanzia umri wa miezi 6 ambapo mtoto ndio anaanza kupewa chakula, anatakiwa apewe mara Moja kwa siku na anapewa kwa Idadi ya vijiko 2-3.
Idadi ya Milo na vijiko vitaongezeka kadri siku zinavyosonga mbele.

🌷Miezi 7-8 anatakiwa apate Milo mikuu 2 kwa siku na asusa 1. Na apewe kiasi Cha nusu kikombe

🌷9-12 anatakiwa apate Milo mikuu mitatu kwa siku n asusa 1-2 kwa siku na kiasi cha chakula ni robo tatu ya kikombe.

🌷13-24- Hadi miaka 5 anatakiwa apate Milo mikuu 3-4 kwa siku pamoja na asusa 2 na apewe kiasi cha chakula cha kikombe kimoja Hadi na zaidi.

Asanteni kwa kuwa pamoja nasi.

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Tuendelee na somo letu la kujifunza smoothie mbalimbali zenye faida kwa afya...
29/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Tuendelee na somo letu la kujifunza smoothie mbalimbali zenye faida kwa afya ya mtoto.

🌷Leo tuone smoothie itakayomsaidia mtoto wako kuongezeka damu.

MAHITAJI
💫Papai
💫Tende
💫Spinach
💫Maji/maziwa

🌷Toa mbegu za tende na za papai

🌺Changanya mahitaji yako, saga hadi vichanganyike na tayari kumpa mtoto.

Asanteni

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Wazazi wengi wanakua na shauku sana ya kuwalisha watoto  pindi watoto wao wa...
28/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Wazazi wengi wanakua na shauku sana ya kuwalisha watoto pindi watoto wao wanapofikisha miezi 6.

🌷Hii hupelekea wengine kufanya makosa kwenye ulishaji huo wa mtoto anaenza kula.

🌷Leo tuone mambo muhimu ya kuzingatia pindi unapotaka kumuanzishia mtoto chakula cha ziada.

💫Mzazi/mlezi hakikisha mtoto anaendelea kupata maziwa ya mama/ maziwa ya kopo k**a kawaida, usimpunguzie hata.

💫Mtoto aanzishiwe na kupewa maji safi na salama kipindi hiko ameanza kula vyakula vingine, hii itamsaidia mtoto mmeng'enyo wake wa chakula uwe rahisi.

💫Hakikisha mtoto anapata vyakula vyenye virutubisho muhimu na vyenye kuboresha afya yake kipindi chote hiko cha kula vyakula vya ziada. Hii itamsaidia mtoto kubaki na afya yake nzuri.

💫Katika uandaaji wa chakula cha mtoto, mzazi/mlezi epuka kumuongezea chumvi na sukari kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha afya ya mtoto. Vyakula vyenyewe vina ladha itakayomfaa mtoto bila kuongezea chumvi Wala sukari.

💫Watoto wengi wanaanza kusumbua kipindi hiki wanapoanzishiwa chakula,hivyo mzazi/mlezi jitahidi kuwa mbunifu wa kubadilisha vyakula vya mtoto mara kwa mara ili asikinai chakula kimoja.

💫Anza kwa kumpa kidogo kidogo wiki ya kwanza, anza kumpa vijiko 2-3 vya chakula na utakua unamuongezea kiasi kadri siku zinavyoenda.

Asanteni😊

Habari za wakati huu wanafamilia wa b2care.Je mtoto wako anapenda matunda?🍁Ili mtoto apende matunda inabidi umjengee maz...
22/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa b2care.

Je mtoto wako anapenda matunda?

🍁Ili mtoto apende matunda inabidi umjengee mazingira mazuri kuanzia aina ya matunda na mazingira ya ulishaji.

🍁Zingatia usafi wa matunda na mazingira.

🍁Pindi tuu anapofikisha miezi 6 mzoeshe matunda hasa yale yalotajwa kwa kuanzia (post ilopita).

🍁Anza kwa kumtengenezea k**a smoothie na kadri anavyoendelea kukua mpe vipande ale mwenyewe.

🍁Atakapoanza kuokoteza mwenyewe mpe katika chombo chenye rangi au picha za kuvutia.

🍁Kula pamoja nae ili apate hamasa.

🍁Mchanganyie matunda aliyozoea pamoja na yale ambao hajaanza kula ili apate kuyazoea pia.

🍁Natumaini njia hizi zitakusaidia.


Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Tuendelee na somo letu la kujifunza smoothie mbalimbali zenye faida kwa afya...
14/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Tuendelee na somo letu la kujifunza smoothie mbalimbali zenye faida kwa afya ya mtoto.

🌷Leo tuone smoothie itakayomsaidia mtoto wako kuwa na ngozi yenye afya na kuvutia.

🌷Smoothie hii pia itawasaidia hata wale watoto wenye changamoto za ngozi zao kuwa kavu.

MAHITAJI
💫Tikiti
💫Apple
💫Chungwa
💫Karoti

🌷Changanya mahitaji yako kasoro chungwa, saga hadi vichanganyike halafu kamulia na chunga na tayari kumpa mtoto.

Asanteni

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Kama tujuavyo smoothie zina faida mbalimbali katika ukuaji wa afya ya mtoto....
09/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Kama tujuavyo smoothie zina faida mbalimbali katika ukuaji wa afya ya mtoto.

🌷Leo tuone smoothie itakayomsaidia mtoto kukua kiakili.

🌷Smoothie hii utahitaji:-

💫Maziwa (fresh/mtindi)
💫Tende
💫Walnut
💫Korosho
💫Tende

🌷Saga vyote kwa pamoja kutokana na kiasi utakachohitaji kwa mtoto wako na tayari kwa kuliwa.

🌷Smoothie hii sio tuu kuwa inaimarisha akili ya mtoto Bali pia itamsaidia kuepukana na tatizo la kufunga choo.

NB:- Mtoto chini ya mwaka mchanganyie na maziwa ya mtindi na mtoto juu ya mwaka unaweza kumchanganyia na maziwa fresh.

Asanteni kwa kuwa pamoja nasi.

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Kama tunavyojua umuhimu wa maji kwa mwili wa mtoto.🌷Maji husaidia kupoza kwa...
05/02/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Kama tunavyojua umuhimu wa maji kwa mwili wa mtoto.

🌷Maji husaidia kupoza kwa joto la mwili, humuepusha mtoto na maradhi mbalimbali.

🌷Je mtoto wako anasumbua kunywa maji? Karibu mbinu zifuatazo ili kumsaidia mtoto wako kunywa maji ya kutosha:-

💫Muwekee maji yake katika chupa nzuri ya kuvutia hasa ukipata yenye picha ya katuni anayoipenda.

💫Yaeke maji karibu na sehemu yake anayocheza na anayoweza kuyafikia kwa urahisi ili aweze kuyachukua na kunywa akiyahitaji.

💫Jifunze kunywa maji pamoja nae, hii itamshawishi kunywa maji.

💫Muongezee na ladha za matunda anayopenda kwenye chupa yake ya maji.

💫Muwekee kiasi kidogo Cha maji kwenye chupa yake ili akimaliza umuongezee tena, usijaze chupa kwa mara Moja.

Asanteni kwa kuwa pamoja nasi.

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.🌷Kama tujuavyo maziwa ya mama yanafaida kubwa sana kwa mtoto ikiwepo kumpatia...
31/01/2024

Habari za wakati huu wanafamilia wa B2CARE.

🌷Kama tujuavyo maziwa ya mama yanafaida kubwa sana kwa mtoto ikiwepo kumpatia Kinga ya maradhi mbalimbali.

🌷Ili mtoto apate maziwa ya mama ya kutosha inabidi mama awe anapata vyakula muhimu vya kuongeza maziwa hayo.

🌷Kama inavyosistizwa inabidi mtoto apate maziwa ya mama pekee kwa miezi 6 yote ya mwanzo na hata atakapoanza kula vyakula vya ziada inampasa mtoto apatiwe maziwa ya mama Hadi miaka 2.

🌷Kumekua na changamoto ya wamama wengi kulalamika kuwa hawana maziwa ya kutosha.

🌷Leo tuone namna ya kutatua changamoto hii kwa wamama ili wapate maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto.

🌷Inabidi mama azingatie mlo kamili pamoja na vyakula vifuatavyo avipate kwa wingi:-

⭐Mbegu za maboga
⭐Mbegu za uwatu
⭐Flax seed
⭐Oatmeal (shayiri)
⭐Supu ya pweza
⭐Mboga ya kale
⭐Majani ya uwatu
⭐Jamii za maziwa
⭐Spinach
⭐Maji ya kutosha

🌷Chakuongezea ni kuwa mama apate mda wa kutosha kupumzika na aache stress (msongo wa mawazo).

🌷Asanteni kwa kuwa pamoja nasi.

Haya mwenye ushauri, changamoto tucoment apo chini.Pia k**a ni ishu binafsi unaweza kutu DM, whatsapp, sms or call  #076...
26/01/2024

Haya mwenye ushauri, changamoto tucoment apo chini.
Pia k**a ni ishu binafsi unaweza kutu DM, whatsapp, sms or call #0767980751 #

Address

Mbezi Luis
Dar Es Salaam
0000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when b2care_pharmacy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram