03/01/2023
USIPUUZIE HII:
Huenda katika pitapita zako umekwisha wahi kuona watu wakiongelea faida za kula karanga mbichi. Lakini wengi tumekuwa tukichukulia kwa mazoea au masihara pasipokujua faida zake kiundani na uhusiano wake kisayansi na miili yetu. Karanga mbichi ni moja ya chakula muhimu sana kwa miili yetu, huenda wengi wetu tunajua tuu kuwa zinatumika sana na wanaume katika kuboresha huduma ya unyumba, kwanza hebu niweke sawa hapa ili uweze kujua kuwa inakuwaje karanga mbichi zikatumika katika kuongeza uwezo wa mwanaume. Endapo wewe ni mwanaume na kwa namna moja ama nyingine umekuwa ukishindwa kurudia tendo baada ya mzunguko wa kwanza basi naomba hapa usome kwa umakini. Mbegu za mwanaume hutengenezwa na vitu vitu 6 yaani maji, sukari, vitamin C, zinc, protein na prostaglandins. Sasa kazi kubwa ya Zinc kwenye mbegu ni kuzikomaza kusudi ziwe tayari kwa kutoka na kurutubisha. Karanga na korosho ni vyakula vyenye zinc kwa kiasi kikubwa sana hivyo kula karanga mbichi au korosho kunapelekea mwanaume kukomaza mbegu nyingi zaidi ndiyo maana mtu anaweza akala karanga leo, kufikia kesho akajikuta anahamu sana ya kushiriki tendo, kwasababu mbegu nyingi zinakuwa zimekomazwa na zinc iliyopatikana baada ya kula karanga. Siyo kwa wanaume tuu bali hata kwa wanawake karanga ni kitu muhimu sana, hasa wanawake wenye ujauzito kuanzia wiki 4 mpaka 6 wanashauriwa sana kutumia karanga mbichi kwasababu karanga zina kirutubisho kinachoitwa 'folate' ambacho ni muhimu sana kwaajili ya kukuza ubongo na uti wa mgongo kwa mtoto aliyepo tumboni.
Pamoja na faida hizo lakini pia karanga hutajwa kuwa na faida na matokeo bora zaidi kwa wale wanaotaka kupungua uzito kwa njia ya diet kwasababu karanga hupunguza kwa kiasi kikubwa appetite ya kula hivyo kumfanya mtu kuhisi ameshiba kwa muda mrefu na hatimaye mwili kupungua.
Hali kadhalika kwa wale wenye matatizo ya kukosa choo, au kupata choo kigumu basi ulaji wa karanga hufanya mtu aweze kupata choo kwa ukawaida.