10/03/2026
Madhara ya Kisukari:
MACHO KUTOKUONA
Kisukari kisipodhibitiwa kinaweza kuharibu mishipa midogo ya damu kwenye macho, hali inayojulikana k**a retinopathy ya kisukari.
Sukari nyingi kwenye damu husababisha mishipa hiyo kudhoofika au kuvuja damu, na polepole kuharibu uwezo wa kuona.
Mwanzoni mtu anaweza kuona ukungu, kuona k**a kuna vivuli au nukta ndogo ndogo kwenye macho, au kushindwa kuona vizuri hasa usiku. Watu wengi hupuuza dalili hizi, lakini kadri muda unavyopita hali inaweza kuwa mbaya zaidi.
Bila matibabu au udhibiti wa kisukari, uharibifu huu unaweza kusababisha kupungua kwa uwezo wa kuona au hata upofu kabisa.
Ndiyo maana ni muhimu kudhibiti sukari mwilini na kupima macho mara kwa mara, ili kuzuia madhara makubwa yanayoweza kusababishwa na kisukari.
ποΈWasiliana nasi kwa namba 0713 622 699 kwa Ushauri na Matibabu