17/10/2025
💥 TEZI DUME 💥
❗️Unaelewa nini ukiambiwa kuwa unatatizo la Tezi Dume⁉️
❗️Unaelewa nini ukiambiwa unayo Saratani ya Tezi Dume⁉️
📌Tezi dume sio ugonjwa…Ni kiungo muhimu sana kwa mwanaume.
✍️Kazi yake kubwa ni👇👇👇
✅️Kuzalisha maji yanayounda shahawa, yanayolinda na kusaidia mbegu za kiume kusafiri ili kutungisha mimba...
⚠️Lakini mitindo mibovu ya maisha tunayoishi leo—Ukiachana kabisa na swala la kurithi...
🍁 CHANZO 🍁
1. Kukua kwa tezi dume (BPH – Benign Prostate Hyperplasia)..
✍️Kukua kwa tezi dume, haihusishi, saratani wala maambukizi...
2. Maambukizi ya bacteria (Prostatitis)..
✍️Huambatana na maumivu makali na huathiri uwezo wa uzazi.
3. Saratani ya Tezi Dume (Prostate Cancer),
✍️Hii ndio hatari zaidi husababisha vifo vingi vya wanaume duniani.....
🔥Tuone dalili kuu zinazojitokeza kwa wanaume wenye matatizo ya tezi dume🔥
♦️Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku (Nocturia)...
♦️Mkojo kutoka kwa shida au kuchelewa kuanza kutoka (Hesitancy)...
♦️Mtiririko dhaifu wa mkojo (Weak urine stream)..
♦️Hisia ya kutomaliza mkojo kwenye kibofu (Incomplete bladder emptying)...
♦️Maumivu au kuchoma wakati wa kukojoa (Dysuria)..
♦️Damu kwenye mkojo (Hematuria) au damu kwenye shahawa (Haematospermia)...
♦️Maumivu ya nyonga, chini ya mgongo au sehemu za siri endapo ni saratani....
❗️🤪Kuwa na dalili hizo sio kigezo, UCHUNGUZI WA TEZI DUME —Ni muhimu mno..(Diagnostic Workup)
💧Digital Rectal Exam (DRE), Daktari huingiza kidole kwenye njia ya haja kubwa kuchunguza ukubwa, umbo na uimara wa tezi dume...
💧Prostate Specific Antigen (PSA), Kipimo cha damu kupima kiwango cha protini inayoongezeka endapo kuna saratani au maambukizi...
💧Ultrasound ya tezi dume (Prostate Ultrasound / Transrectal Ultrasound – TRUS), Hutoa picha sahihi kuona ukubwa, umbo na uwepo wa uvimbe.
💧Urinalysis & Urine culture, Kuchunguza kama kuna maambukizi kwenye njia ya mkojo..
💧Biopsy (ikiwa inahitajika), Kuchukua kipande kidogo cha tezi dume kwa ajili ya uchunguzi wa saratani