31/03/2026
TAASISI YA JAI YASHIRIKI HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA NA WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA.
Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wameshiriki hafla fupi ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Jamiiyaatul Akhlaaqul Islaam Wilaya ya Ilala (JAI) ikiwa ni kusherekea kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na Suna ya funga ya siku sita baada ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana kwa ukaribu na hospitali hiyo katika kuwahudumia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kulipa gharama za matibabu.
Ameongeza kuwa Taasisi ya JAI imekuwa mstari wa mbele kutoa msaada kwa makundi ya watu wasiojiweza ikiwemo huduma za kiroho, kulipia gharama za matibabu, chakula cha mchana, nauli pamoja na kuchangia damu.
“Naipongeza sana taasisi ya JAI, imekuwa ikitoa msaada kwa watu wote bila kubagua kabila wala dini, uwepo wao hospitaini hapa inaleta hofu ya Mungu baina yetu na kuleta hamasa kwa taasisi zingine kutamani kujitoa kwa jamii k**a ambavyo JAI wanafanya”amesema Dkt. Kiwelu.
Awali akisoma risala katika hafla hiyo, Bi. Fatuma Saidi amesema taasisi ya JAI imetimiza miaka 13 ya mahusiano baina yake na hospitali ya Amana ambapo hadi sasa taasisi hiyo imetumia zaidi ya TZS, 400MIL. kugharamia matiababu kwa wagonjwa takribani 800 ambao hawana uwezo wanaohudumiwa hospitalini hapo.