Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

MENEJIMENTI YA HOSPITALI YA AMANA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA NMB KUJADILI NAMNA YA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYAMenejimenti ya...
09/03/2026

MENEJIMENTI YA HOSPITALI YA AMANA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA NMB KUJADILI NAMNA YA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA

Menejimenti ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa leo Machi 09, 2026 imekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Benki ya NMB ili kujadiliana namna bora ya kushirikiana katika kuboresha miundo mbinu ya kutolea huduma za afya hospitalini hapo.

Mazungumzo hayo yameangazia zaidi umuhimu wakushirikikiana na benki hiyo katika kuboresha miundo mbinu ikiwemo ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa maalum, ukarabati wa majengo chakavu, miundo mbinu maalum ya kuhifadhia maji ya safi na maji taka ili kusadia kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi wengi zaidi.

Akizungumza na ujumbe huo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kwamba uhusiano huo utasaidia kupunguza mzigo wa gharama kwa hospitali kwa kuwa imekuwa ikitumia gharama kubwa katika kufanya ukarabati wa miundo mbinu ambayo imechakaa kwa kiasi kikubwa.

“Hospitali yetu imejengwa tangu mwaka 1950 na majengo mengi yalijengwa kwa muundo wa kizamani na hivyo marekebisho yake yanahitaji gharama kubwa na sisi k**a hospitali hatuwezi kumudu gharama hizo” amesema Dkt. Kiwelu.

WATUMISHI WANAWAKE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANIWatumishi wanawake ...
08/03/2026

WATUMISHI WANAWAKE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Watumishi wanawake Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wameungana na wanawake wenzao Duniani kusherekea Siku ya Kitaifa ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa imefanyika katika viwanja vya Barafu –Mburahati, mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila

Maadhimisho hayo hufanyika Machi 08 kila mwaka ambao Kauli mbiu ya mwaka huu: “Haki na Ustawi kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kufika Dira 2050”

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Chalamila amesema wanawake ni jeshi kubwa katika taifa hili na ninguzo muhimu katika kujenga na kuimarisha Uchumi wa nchi hivyo wanapaswa kutambua nafasi zao kwakuwa wao ndio wanaotegemewa zaidi katika kuonesha njia.

Pamoja na hayo amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuhamasisha usawa wa kijinsia na kulinda haki na usawa wa wanawake na wasichana, na kujiimarisha kiuchumi ili kuepukana na mikopo isiyo na tija.

Heri ya siku ya wanawake Duniani
08/03/2026

Heri ya siku ya wanawake Duniani

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI ZENUFA YATOA ZAWADI HOSPITALI YA AMANAKampuni ya Zenufa Laboratories imetembelea  Hosp...
07/03/2026

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI ZENUFA YATOA ZAWADI HOSPITALI YA AMANA

Kampuni ya Zenufa Laboratories imetembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana na kutoa zawadi kwa lengo la kuwafariji wagonjwa na kuchangia upatikanaji wa baadhi ya mahitaji muhimu kwa wagonjwa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa Machi 08 kila mwaka.

Akipokea zawadi hizo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amewashukuru wadau hao na kusema zawadi hizo zitawapa faraja wagonjwa pamaja na kuboresha mahusiano baina Yao.

“Tunaishukuru sana kampuni ya Zenufa kwa ushirikiano mzuri walionao baina ya hospitali ya Amana naomba ushirikiano huu uendelee kuimarika zaidi ili sote kwa pamoja tuwe sehemu ya kuleta faraja kwa Jamii” Amesema Dkt. Kiwelu

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, muwakilishi wa kampuni ya Zenufa Bi Anna Marupe Amesema kampuni hiyo imeona umuhimu wa kushiriki katika shughuli za kijamii zinazolenga kusaidia jamii, hususani katika sekta ya afya.

“Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani tumeona ni vyema kuja kuwaunga mkono kwa mnazozitoa za kuhudumia wananchi” Amesema Bi. Marupe

Sambamba na hayo kampuni hiyo imepanda miti ya kivuli katika maeneo ya hospitali ikiwa ni kuunga mkono kampeni ya utunzaji mazingira hospitalini hapo.





MTANDAO WA WANAWAKE JESHI LA POLISI MKOA WA KIPOLISI ILALA WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPITALI YA AMANAKatika kuelekea M...
06/03/2026

MTANDAO WA WANAWAKE JESHI LA POLISI MKOA WA KIPOLISI ILALA WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPITALI YA AMANA

Katika kuelekea Maadhimisho ya Kilele cha siku ya wanawake Duniani Mtandao wa Wanawake Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana na kutoa Zawadi kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Kamishna Msaidiazi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi na Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ilala SASP. Hasina Taufiq alisema askari wanawake wamejitolea kwa hali na mali hadi kufanikisha malengo ya kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii na pia msaada huo utakuwa faraja kwao.

“Tumekusudia kuwatembelea wagonjwa hawa ili kuwashika mkono na kuwafariji kwani tunajua baadhi yao wana hali ya chini na baadhi wametelekezwa na ndugu zao hivyo ujio wetu ni kuwafariji na kuwashika mkono kwakuwa hata sisi ni wagonjwa watarajiwa.” Amesema SASP. Teofiq

Akipokea msaada huo Afisa Uhusiano Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana amewashukuru wanawake hao kwa kuwafariji wagonjwa na kutoa wito kwa wadau wengine kujitolea kuja kuwafariji wagonjwa kadri watakavyojaliwa.

Zawadi zilizotolewa ni Pamoja na Sabuni za kufulia, Dawa za Meno, Taulo za K**e, Maji ya kunywa, Kanga, Vitenge pamoja na Taulo za Watoto.

.tanzania

05/03/2026

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI; ASKARI POLISI WANAWAKE KIKOSI CHA BOHARI DAR ES SALAAM WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPITALI YA AMANA

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI; ASKARI POLISI WANAWAKE KIKOSI CHA BOHARI DAR ES SALAAM WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSP...
05/03/2026

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI; ASKARI POLISI WANAWAKE KIKOSI CHA BOHARI DAR ES SALAAM WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPITALI YA AMANA

Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, inayoadhimishwa kote ulimwenguni kila ifikapo Machi 08, Askari Polisi Wanawake kutoka kikosi cha Polisi Bohari Mkoa wa Dar es Salaam wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa lengo la kutaoa zawadi na kuwafariji wagonjwa waliolazwa katika wodi ya wanawake na watoto.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi hizo Kiongozi wa Wanawake Polisi Kikosi cha Bohari Mkoa wa Dar es Salaam ASP.Cesilia Mauka amesema lengo la ziara hiyo ni kuwafariji wagonjwa, kuonesha mshik**anom na upendo hususani kwa wanawake na Watoto waliolazwa hospitalini hapo.

“Zikiwa zimebaki siku chache kuadhimisha siku ya Wanawake tumeona tuje kujumuika na wanawawe wenzetu waliolazwa hospitalini hapa, tunashukuru wametupokea vizuri na wameonesha moyo shukurani kwa kile tulichowapatia”amesema ASP. Mauka

Wanawake hao wametoa Zawadi mbalimbali ikiwemo, Vitenge, Kanga na taulo za Watoto.
tanzania

JESHI LA MAGEREZA MKOA WA DAR ES SALAAM KUENDELEZA USHIRIKIANO NA HOSPITALI YA AMANA.Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoa w...
04/03/2026

JESHI LA MAGEREZA MKOA WA DAR ES SALAAM KUENDELEZA USHIRIKIANO NA HOSPITALI YA AMANA.

Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 04 Machi, 2026 wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa lengo la kudumisha na kuimarisha mahusiano baina ya taasisi hizo mbili.

Akizungumza na jeshi hilo Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amelipongeza jeshi hilo kwa kuona umuhimu wa kutembelea hospitali hiyo na kusema kuwa mahusiano baina yao yataendelea kuboreshwa zaidi ili kuhakikisha kuwa wafungwa na maabusu wote watakaoletwa hospitalini hapo wanapatiwa huduma bora wanazostahili.

"Hospitali ya Amana tumekuwa tukishirikiana kwa ukaribu na jeshi la magereza na kila wanapokuja hospitanini hapa tunahakikisha kuwa wanahudumiwa kwa wakati bila usumbufu wowote tumekuwa tukiwapa kipaumbele katika kila eneo la kutolea huduma"amesema Dkt. Kiweru

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam Sacp. Rashidi Mangara amesema jeshi la magereza kazi yake kuu ni kuhakikisha inatoa uhifadhi salama kwa wafungwa na mahabusu wote na usalama huo unaenda sambamba na kuwa na afya bora ndio maana wameona kuna umuhimu wa kutembelea hospitali hiyo ili kuwapongeza kwa huduma bora wanazozitoa kwa wafungwa wote na maahabusu wanaofikishwa hospitalini hapo.

"Amana sio hospitali tu bali ni hospitali ambayo watumishi wake wanatoa huduma kwa weledi na kujitoa kwa hali ya juu bila kuchoka wala kubagua wagonjwanjwa" amesema sacp. Mangara.

Jeshi hilo limetembelea maeneo mbalimbali ya kutolea huduma ikiwemo, Jengo la wagonjwa maalum, jengo la wagonjwa wa nje, jengo la kuchuja damu kwa wagonjwa wenye figo, Idara ya Magonjwa ya dharura na Ajali pamoja na jengo la uchangiaji damu.

less

Kuelekea siku ya wanawake Duniani   ni wa Thamani
04/03/2026

Kuelekea siku ya wanawake Duniani
ni wa Thamani

Kuelekea siku ya wanawake Duniani  ni wa Thamani
03/03/2026

Kuelekea siku ya wanawake Duniani
ni wa Thamani

Siku ya Usikivu Duniani
03/03/2026

Siku ya Usikivu Duniani

HOSPITALI YA AMANA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA  TZS. 40MIL KWA AJILI YA MAMA NA MTOTOHospita...
02/03/2026

HOSPITALI YA AMANA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA TZS. 40MIL KWA AJILI YA MAMA NA MTOTO

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Amana imepoke Msaada wa vifaa tiba vya kisasa kutoka mradi wa Breathing for Babies (BFB) kwa kushirikiana na MUHAS pamoja na GOAL 03 wenye lengo la kusaidia kuboresha huduma za afya kwa watoto.

Akipokea msaa huo kiongozi muuguzi mwandamizi hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Bi. Mary Machemba amesema msaada huo utasaidia kupunguza changamoto ya hewa tiba kwa watoto wachanga wanaozaliwa wakiwa na matatizo ya kupumua.

"Vifaa hivi muhimu vimekuja wakati muafaka ambapo serikali ya awamu ya sita umedhamilia kupunguza vifo nchini" amesema Bi. Machemba

Aidha, sambamba na hilo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuaziamini huduma zinazotolewa na hospitalini hapo kwa kuwa serikali imewekeza miundombinu ya kisasa na i awatoa huduma bingwa na bobezi.

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram