30/04/2026
*AMANA YANG’ARA KITAIFA, YASHIKA NAFASI YA TATU TUZO ZA USAFI NA MAZINGIRA*
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea kung’ara kitaifa baada ya kushika nafasi ya tatu kati ya hospitali 28 za mikoa katika tuzo za usafi na mazingira zilizotolewa na Wizara ya Afya katika maazimisho ya kilele cha Wiki ya Afya Kitaifa yaliyofanyika tarehe 29 Aprili, 2026
Tuzo hiyo imetolewa katika kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani ambapo mgeni rasmi alikiwa Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye alizipongeza taasisi za afya kwa kuendelea kuimarisha viwango vya usafi na mazingira katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
Akipokea tuzo hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu, amesema kuwa ushindi huo unatokana na ushirikiano wa watumishi pamoja na juhudi za makusudi za kuhakikisha mazingira ya hospitali hiyo yanakuwa safi na salama kwa watu wote wanaokuja kupata huduma za afya.
Aidha, ameongeza kuwa tuzo hiyo itakuwa chahu kwa watumishi wa hospitali hiyo kuendelea kuboresha usafi ili kufikia viwango vya juu zaidi na kuwa hospitali ya mfano nchini katika utoaji wa huduma bora na utunzaji wa mazingira ya kutolea huduma.