09/03/2026
MENEJIMENTI YA HOSPITALI YA AMANA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA NMB KUJADILI NAMNA YA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA
Menejimenti ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa leo Machi 09, 2026 imekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Benki ya NMB ili kujadiliana namna bora ya kushirikiana katika kuboresha miundo mbinu ya kutolea huduma za afya hospitalini hapo.
Mazungumzo hayo yameangazia zaidi umuhimu wakushirikikiana na benki hiyo katika kuboresha miundo mbinu ikiwemo ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa maalum, ukarabati wa majengo chakavu, miundo mbinu maalum ya kuhifadhia maji ya safi na maji taka ili kusadia kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi wengi zaidi.
Akizungumza na ujumbe huo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kwamba uhusiano huo utasaidia kupunguza mzigo wa gharama kwa hospitali kwa kuwa imekuwa ikitumia gharama kubwa katika kufanya ukarabati wa miundo mbinu ambayo imechakaa kwa kiasi kikubwa.
“Hospitali yetu imejengwa tangu mwaka 1950 na majengo mengi yalijengwa kwa muundo wa kizamani na hivyo marekebisho yake yanahitaji gharama kubwa na sisi k**a hospitali hatuwezi kumudu gharama hizo” amesema Dkt. Kiwelu.