Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

Wasiliana nasi
02/05/2026

Wasiliana nasi

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSIWafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wameung...
01/05/2026

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI

Wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wameungana na wafanyakazi wengine duniani katika kusherehekea Siku ya Wafanyakazi duniani ambayo kimkoa imeadhimishwa katika uwanja wa Mnazi Mmoja Dar es Salaam.

Akizungumza na wafanyakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam mkuu wa mkoa huo, Mh. Albert Chalamila amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii na weledi wa hali ya juu ili kuleta matokeo chanya kwa jamii.

Mh. Chalamila ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hasan imeendelea kufanya maboresho mbalimbali ikiwemo maslahi ya wafanyakazi.

"Kazi zenye Staha ni Nguzo imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050"

Heri ya siku ya wafanyakazi Duniani
01/05/2026

Heri ya siku ya wafanyakazi Duniani

*WATUMISHI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA YA AMANA WATAKIWA  KUDUMISHA UZALENDO*Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa A...
30/04/2026

*WATUMISHI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA YA AMANA WATAKIWA KUDUMISHA UZALENDO*

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wametakiwa kuwa wazalendo, kufanya kazi k**a timu na kudumisha ushirikiano ili kuzidi kuongeza ufanisi na tija katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi wanaofika kupata huduma hospitalini hapo.

Wito huo umetolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu katika kikao cha watumishi ambapo amesema kuwa uzalendo ndio silaha katika utoaji wa huduma bora.

“Huduma bora inaanza na uzalendo na hapa tuna madaktari, wauguzi, wahudumu, watu wa utawala kila mmoja ana jukumu lake, tufanye kazi kwa uzalendo maana hii Hospitali yetu hata k**a ina rasilimali nzuri kiasi gani k**a hatutakuwa wazalendo basi hatutaweza kutoa huduma bora. Amesema Dkt.Kiwelu

Dkt. Kiwelu ameongeza kuwa ni jukumu la kila mtumishi kuwahudumia wagonjwa kwa usawa kwa sababu tunategemea kila anaekuja kupata huduma ni mgonjwa na anatarajia kupata huduma zinazokidhi matarajio yake hivyo unatakiwa kumuhudumia na kumpokea vizuri.

Pamoja na hayo amewataka watumishi hao kudumisha upendo na ushirikiano baina yao ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi.

*AMANA YANG’ARA KITAIFA, YASHIKA NAFASI YA TATU TUZO ZA USAFI NA MAZINGIRA*Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea k...
30/04/2026

*AMANA YANG’ARA KITAIFA, YASHIKA NAFASI YA TATU TUZO ZA USAFI NA MAZINGIRA*

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea kung’ara kitaifa baada ya kushika nafasi ya tatu kati ya hospitali 28 za mikoa katika tuzo za usafi na mazingira zilizotolewa na Wizara ya Afya katika maazimisho ya kilele cha Wiki ya Afya Kitaifa yaliyofanyika tarehe 29 Aprili, 2026

Tuzo hiyo imetolewa katika kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani ambapo mgeni rasmi alikiwa Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye alizipongeza taasisi za afya kwa kuendelea kuimarisha viwango vya usafi na mazingira katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Akipokea tuzo hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu, amesema kuwa ushindi huo unatokana na ushirikiano wa watumishi pamoja na juhudi za makusudi za kuhakikisha mazingira ya hospitali hiyo yanakuwa safi na salama kwa watu wote wanaokuja kupata huduma za afya.

Aidha, ameongeza kuwa tuzo hiyo itakuwa chahu kwa watumishi wa hospitali hiyo kuendelea kuboresha usafi ili kufikia viwango vya juu zaidi na kuwa hospitali ya mfano nchini katika utoaji wa huduma bora na utunzaji wa mazingira ya kutolea huduma.

*AMANA YANG’ARA KITAIFA, YASHIKA NAFASI YA TATU TUZO ZA USAFI NA MAZINGIRA*Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea k...
30/04/2026

*AMANA YANG’ARA KITAIFA, YASHIKA NAFASI YA TATU TUZO ZA USAFI NA MAZINGIRA*

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea kung’ara kitaifa baada ya kushika nafasi ya tatu kati ya hospitali 28 za mikoa katika tuzo za usafi na mazingira zilizotolewa na Wizara ya Afya katika maazimisho ya kilele cha Wiki ya Afya Kitaifa yaliyofanyika tarehe 29 Aprili, 2026

Tuzo hiyo imetolewa katika kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani ambapo mgeni rasmi alikiwa Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye alizipongeza taasisi za afya kwa kuendelea kuimarisha viwango vya usafi na mazingira katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Akipokea tuzo hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu, amesema kuwa ushindi huo unatokana na ushirikiano wa watumishi pamoja na juhudi za makusudi za kuhakikisha mazingira ya hospitali hiyo yanakuwa safi na salama kwa watu wote wanaokuja kupata huduma za afya.

Aidha, ameongeza kuwa tuzo hiyo itakuwa chahu kwa watumishi wa hospitali hiyo kuendelea kuboresha usafi ili kufikia viwango vya juu zaidi na kuwa hospitali ya mfano nchini katika utoaji wa huduma bora na utunzaji wa mazingira ya kutolea huduma.

Hongera Mfanyakazi Bora Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa mwaka 2026
28/04/2026

Hongera Mfanyakazi Bora Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa mwaka 2026

Amana Day bado siku 25 tu
27/04/2026

Amana Day bado siku 25 tu

Heri ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
26/04/2026

Heri ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Simu ya Malaria Duniani
25/04/2026

Simu ya Malaria Duniani

Amana Day
25/04/2026

Amana Day

24/04/2026

*JUMUIYA YA WAFANYA BIASHARA WA SOKO LA KARIAKOO WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA*

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share