Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

Maadhimisho mema ya kumbukumbu ya Karume
07/04/2026

Maadhimisho mema ya kumbukumbu ya Karume

Heri ya pasaka
05/04/2026

Heri ya pasaka

Heri ya ijumaa kuu
03/04/2026

Heri ya ijumaa kuu

MRADI WA BREATHING FOR BABY KUENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NCHINIMganga Mkuu wa Halmas...
01/04/2026

MRADI WA BREATHING FOR BABY KUENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NCHINI

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Dkt. Jonas Lulandala ameupongeza Mradi wa Breathing for Baby (BfB) kwa kusaidia kuboresha miundo mbinu ya kutolea huduma za Watoto wachanga na kupunguza vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati.

Dkt. Lulandala ametoa pongezi hizo leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wakati wa hafla fupi ya kufanya tathmini ya Mradi wa Brething for Baby na kusherekea mafanikio ya mradi huo ambao umekuwa na mafanikio makubwa katika kusaidia kupunguza vifo vya kina mama waliojifungua na Watoto waliozaliwa kabla ya wakati.

“Naipongeza sana Serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia wadau na wawekezaji katika sekta ya afya kwani kupitia mradi huu hospitali zetu zimepatiwa mashine za kisasa zenye uwezo maalum wa kufanya utambuzi wa mapema wa matatizo ya kiafya kwa watoto wenye shida ya kupumua na kuimarisha mfumo mzima wa huduma za watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya wakati”amesema Dkt. Lulandala

Awali akizungumza katika hafla hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema mradi huo umekuwa na mafanikio makubwa katika hospitali hiyo ambapo kwa miezi mitatu mfululuzo hakuna mtoto yoyote aliyepoteza maisha kwa kushindwa kupumua kwakuwa hospitali hiyo imepatiwa msaada wa mashine za kisasa zenye uwezo wa kumsaidia mtoto mchanga mwenye changamoto ya kushindwa kupumua.

TAASISI YA JAI YAAHIDI KUTOA MSAADA WA MACHINE ZA KUCHUJA DAMU HOSPITALI YA AMANATaasisi isiyo ya kiserikali ya Jamiiyaa...
01/04/2026

TAASISI YA JAI YAAHIDI KUTOA MSAADA WA MACHINE ZA KUCHUJA DAMU HOSPITALI YA AMANA

Taasisi isiyo ya kiserikali ya Jamiiyaatul Akhlaaqul Islaam imeahidi kununua mashine za kuchuja damu ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto ya figo na kuboresha huduma za matibabu ya kuchuja damu kwa wagonjwa wanaohudumiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana.

Kauli hiyo imetolewa leo na Amiri Mkuu wa Taasisi ya JAI Ilala Sheikh Abdul Wakati katika hafla fupi ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na taasisi hiyo ikiwa ni kusherekea kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na Suna ya funga ya siku sita baada ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Sheikh. Wakati amesema kuwa gharama za kuchuja damu kwa wagonjwa wenye changamoto za figo ni ghali hivyo taasisi hiyo itanunua mashine za kuchuja damu ili kusaidia kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa hao.

“Nafahamu wagonjwa wengi wenye changamoto ya figo hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu hivyo sisi k**a taasisi tutanunua mashine za kuchuja damu na kuziweka hapa Amana ili kuwasaidia watanzania ambao hawana uwezo”amesema Sheikh. Wakati.

Taasisi ya JAI imekuwa ikishirikiana na Hospitali ya Amana tangu mwaka 2013 ambapo imekuwa ikiwasaidia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kulipa gharama za matibabu pamoja na kuwapatia chakula.

TAASISI YA JAI YASHIRIKI HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA NA WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA. Watumishi wa Hospitali ya Rufaa...
31/03/2026

TAASISI YA JAI YASHIRIKI HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA NA WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA.

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wameshiriki hafla fupi ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Jamiiyaatul Akhlaaqul Islaam Wilaya ya Ilala (JAI) ikiwa ni kusherekea kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na Suna ya funga ya siku sita baada ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana kwa ukaribu na hospitali hiyo katika kuwahudumia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kulipa gharama za matibabu.

Ameongeza kuwa Taasisi ya JAI imekuwa mstari wa mbele kutoa msaada kwa makundi ya watu wasiojiweza ikiwemo huduma za kiroho, kulipia gharama za matibabu, chakula cha mchana, nauli pamoja na kuchangia damu.

“Naipongeza sana taasisi ya JAI, imekuwa ikitoa msaada kwa watu wote bila kubagua kabila wala dini, uwepo wao hospitaini hapa inaleta hofu ya Mungu baina yetu na kuleta hamasa kwa taasisi zingine kutamani kujitoa kwa jamii k**a ambavyo JAI wanafanya”amesema Dkt. Kiwelu.

Awali akisoma risala katika hafla hiyo, Bi. Fatuma Saidi amesema taasisi ya JAI imetimiza miaka 13 ya mahusiano baina yake na hospitali ya Amana ambapo hadi sasa taasisi hiyo imetumia zaidi ya TZS, 400MIL. kugharamia matiababu kwa wagonjwa takribani 800 ambao hawana uwezo wanaohudumiwa hospitalini hapo.

Siku ya kifua kikuu Duniani
24/03/2026

Siku ya kifua kikuu Duniani

Eid Mubarak
20/03/2026

Eid Mubarak

Siku ya kimataifa ya Afya ya Kinywa na Meno
20/03/2026

Siku ya kimataifa ya Afya ya Kinywa na Meno

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KUENDELEA KUBORESHA MASLAHI YA WATUMISHI NA KUBORESHA MIUNDO MBINU YA KUTOLEA HUDUMAUon...
19/03/2026

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KUENDELEA KUBORESHA MASLAHI YA WATUMISHI NA KUBORESHA MIUNDO MBINU YA KUTOLEA HUDUMA

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana umesema kuwa utahakikisha unaendelea kuboresha maslahi ya watumishi pamoja na kuboresha miundombinu ya kutolea huduma ili kukidhi matarajio yao na kila mtumishi aweze kufanya kazi kwa utulivu bila kikwazo chochote.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Japo Lukali amesema uongozi wa hospitali umekuwa ukitatua changamoto mbalimbali za watumishi kadri zinavyojitokeza ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakuwa bora zaidi.

" Vikao vya baraza la wafanyakazi, vinatuleta pamoja ili kujadili changamoto zetu, pia kupitia vikao hivi tunajadili namna ya kuboresha zaidi huduma za afya pamoja na kuondoa wasiwasi kuhusu maslahi yetu," amesema Dkt. Lukali

Katika Baraza hilo mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo kufanya tathmini ya mpango wa mwaka wa 2026/2027 na kupitisha mpango huo pamoja na kupokea taarifa ya ya miradi ya maendeleo ya kimkakati.


19/03/2026
Tunatafuta ndugu zake
18/03/2026

Tunatafuta ndugu zake

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram