Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

10/02/2026

@

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI KATIKA HAFLA YA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA ANAYESHUGHULIKIA MAS...
09/02/2026

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI KATIKA HAFLA YA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA ANAYESHUGHULIKIA MASUALA YA DAWA NA VIFAA TIBA

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa Amana wameshiriki katika hafla fupi ya kumpokea na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Bw. Emmanuel Tayari mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo.

Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 9 Februari, 2026 katika katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) jijini Dar Es Salaam.

Leo tarehe 4 Februari, 2026, Tanzania inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, siku mu...
04/02/2026

Leo tarehe 4 Februari, 2026, Tanzania inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, siku muhimu ya kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu ugonjwa wa saratani, kuhimiza kinga, uchunguzi wa mapema na upatikanaji wa matibabu kwa wote.

Maadhimisho haya yanawakumbusha wananchi kuwa saratani inaweza kuzuilika, kutibika endapo itagundulika mapema, na kwamba kila mmoja ana wajibu wa kuchukua hatua ikiwemo kubadili mtindo wa maisha.

WATAALAM KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA MNAZI MMOJA ZANZIBAR NA WADAU KUTOKA  CHUO KIKUU CHA NORWAY (Hauklanda) WATEMBELEA...
02/02/2026

WATAALAM KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA MNAZI MMOJA ZANZIBAR NA WADAU KUTOKA CHUO KIKUU CHA NORWAY (Hauklanda) WATEMBELEA AMANA KUJIFUNZA NAMNA MFUMO WA eHMS UNAVYOFANYA KAZI

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imepokea wataalam kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar pamoja na wadau kutoka Chuo Kikuu cha Norway (Haukelanda) waliokuja kujifunza kwa vitendo namna mfumo wa kielektroniki wa kutolea huduma za Afya (eHMS) unavyofanya kazi.

Wataalam hao wamtembelea maeneo mbalimbali ya kutolea huduma na kuona namna jinsi mfumo huo unavyosaidia kuhifadhi taarifa za wagonjwa kwa usahihi, kurahisisha utoaji wa huduma na kuongeza uwazi katika utendaji kazi wa hospitali kuanzia mgonjwa anaposajiliwa kwenda kwa daktari hadi hatua ya mwisho ya kuchukua dawa.

Katika ziara hiyo, wataalam hao wameweza walibadilishana uzoefu na watumishi wa hospitali ya Amana kuhusu changamoto na mafanikio katika matumizi ya teknolojia hususani katika kutoa huduma za afya.

Ziara hiyo imefungua milango ya ushirikiano na kuboresha mahusino baina ya Hospitali ya Amana pamoja na taasisi za afya ndani na nje ya nchi.

DKT. KIWELU: KWA SASA HUDUMA ZINAZOTELEWA  HOPSITALI YA AMANA NI BORA ZAIDI YA ZILE ZINAZOTOLEWA HOSPITALI BINAFSIMganga...
02/02/2026

DKT. KIWELU: KWA SASA HUDUMA ZINAZOTELEWA HOPSITALI YA AMANA NI BORA ZAIDI YA ZILE ZINAZOTOLEWA HOSPITALI BINAFSI

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kuwa uwekezaji uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika hospitali hiyo umesaidia katika kuboresha utoaji wa huduma na kwa sasa wananchi hawana haja ya Kwenda kutibiwa katika hospitali binafsi kwakuwa huduma hizo zinapatikana katika hospitali za serikali kwa kiwango chenye ubora wa hali ya juu.

Dkt. Kiwelu ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wazazi CCM Wilaya ya Ilala walipotembelea hospitali hiyo kuangalia hali ya utoaji huduma na kupanda iti ya kivuli hospitalini hapo ikiwa ni maadhimisho ya miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi.

Ameeleza kuwa Hospitali ya Amana inaongeza mwendo kwa kutoa huduma zenye viwango wa kimataifa na inatumia mifumo ya kiteknolojia katika kutoa huduma ambapo kwa sasa mgonjwa haitaji kukaa kwenye foleni muda mrefu kwakuwa huduma zote zinatolewa kwa njia ya kielectoni kuanzia mgonjwa anaposajiliwa hadi hatua ya mwisho anapokwenda kuchukua dawa.

“Hospitali ya Amana tunajivunia kwa kutoa huduma zenye ubora na ili kuthibitisha hayo mwishoni mwa mwaka jana hospitali yetu iliibuka kinara kwa kuwa hospitali ya kwanza inayoongoza kwa kutoa huduma bora kati ya hospitali 23 za rufaa za mikoa nchini”amesema Dkt. Kiwelu.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa Hopsitali ya Amana imeendelea kuboresha huduma ya Mama na Mtoto na kufanikiwa kupunguza vifo vya Watoto wachanga na wazazi wanaojifungua ambapo kwa mara ya kwanza kwa imeweka rikodi ya kutokuwa na kifo chochote cha mama na mtoto kwa kipindi cha miezi sita.

*WAJUMBE WA BARAZA LA WAZAZI CCM WAIPA KONGOLE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA*Wajumbe wa ...
01/02/2026

*WAJUMBE WA BARAZA LA WAZAZI CCM WAIPA KONGOLE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA*

Wajumbe wa Baraza la Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala wameipongeza Hospitali ya Rufaa Mkoa Amana kwa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za afya na kuunga mkono Juhudi za Rais wa Jamuhuri ya Muugano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suhulu Hassan za kuboresha huduma za afya nchini.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Bwn. Haji Kilimo alipotembelea hospitali hiyo kuangalia hali ya utoaji huduma Pamoja na kupanda Miti ya kivuli ikiwa ni maadhimishoya ya miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi.

Bw. Haji amesema kuwa miongoni mwa majukumu ya Chama cha Mapinduzi ni kuhakikisha kuwa inaisimamia Ilani ya Chama katika kutekeleza majukumu yake ya kuboresha huduma za afya kwa wote.

“Sisi k**a wajumbe wa Chama cha Mpinduzi tuna majukumu makuu matatu ambayo ni Kuhimiza, Kusimamia na Kuishauri serikali katika kutekeleza majukumu yake na ikiwemo kuboresha huduma za afya kwa wananchi ili kujenga taifa imara lenye uhakika wa afya na matibabu.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa gharama za matibabu ni ghali duniani kote na kwakutambua hilo serikali ya Awamu ya Sita imeanzisha mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma za afya bila kikwazo chochote hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiunga na Bima ya Afya kwa wote.

Wajumbe hao wametembelea maeneo mbalimbali ya kutolea huduma ikiwemo Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali, Wodi ya Watu Mashuhuri, Wodi ya Wazazi ,Idara ya Radiolojia Pamoja na Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD).

.tanzania

Karibuni sana hospital ya rufaa ya Mkoa Amana
31/01/2026

Karibuni sana hospital ya rufaa ya Mkoa Amana

WATUMISHI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUFANYA TAFITI ZITAKAZOSAIDIA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYAWatumishi w...
29/01/2026

WATUMISHI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUFANYA TAFITI ZITAKAZOSAIDIA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wametakiwa kufanya tafiti zenye kuleta tija kwaajili ya maendeleo ya taifa zitakazotatua changamoto na kuleta suluhisho kwenye magonjwa mbalimbali.

Wito huo umetolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu wakati akifungua mafunzo ya siku nne yanayoendeshwa na Taasisi ya Taifa ya Tafiti za Magonjwa ya Binadamu (NIMR yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wa hospiatli hiyo juu ya namna ya takwimu zinazopatikana hospitalini hapo kufanya tafiti za afya.

Dkt. Kiwelu amesema kuwa Amana inaona wagonjwa wengi kwa siku hivyo ni rahisi kupata takwimu muhimu zinazohitajika katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayoikumba jamii.

“Serikali inayoongozwa na Rais Samia inaamini katika tafiti za kisayansi na inaamini pia kuwa hakuna maendeleo bila utafiti na hivyo ili kupata mafanikio ni lazima tafiti zifanyike na zije na matokeo Chanya” amesema Dkt. Kiwelu

Dkt. Kiwelu ameongeza kuwa ili Tanzania ipate maendeleo katika sekta ya afya inatupasa tuwe na ugunduzi wetu wenyewe na sisi k**a Amana tumejizatiti kuongeza nguvu katika hilo.

28/01/2026


KOICA KUJENGA JENGO LA GHOROFA NNE LA HUDUMA YA MAMA NA MTOTO HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANAUongozi wa Hospitali ya Ru...
27/01/2026

KOICA KUJENGA JENGO LA GHOROFA NNE LA HUDUMA YA MAMA NA MTOTO HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana umekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Shirika la Korea International Coorparation Agency (KOICA) ambapo wamejadili namna wanavyoweza kushikiana katika kuboresha huduma ya mama na mtoto kwa kuboresha miundombinu ya kutolea huduma hizo.

Akizungumza mara baada ya kukutana na Ujumbe huo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu amesema kuwa Shirika hilo limeahidi kujenga jengo la Ghorofa nne ambalo litakuwa maalum kwaajili ya kuwahudumia kinamama waliojifungua na Watoto Wachanga wanaohitaji uangalizi maalum.

Ameeleza kuwa jengo hilo litakuwa na mashine za kisasa Pamoja na vifaa tiba vya kisasa vyenye uwezo wa hali ya juu katika kutoa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi kwa wananchi.

“Jengo hili likikamilika litaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya hususani katika kuboresha huduma ya mama na mtoto na kupunguza vifo vya Watoto wachanga hivyo ni matumaini yetu kuwa Amana itaenda kuwa mfano katika kutoa huduma bora kwa wananchi.”amesema Dkt. Kiwelu.

Dkt. Kiwelu ameongeza kuwa ujenzi wa jengo hilo litaenda sambamba na utoaji wa magari mawili ya kubebea Wagonjwa wa Dharura pamoja na kuendesha mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo watoa huduma Idara ya Mama na Mtoto
https://www.instagram.com/p/DUBQoHRiKUz/?igsh=MW4xZHIxbDJ5ZDhvYw==

Heri ya siku ya kuzaliwa
27/01/2026

Heri ya siku ya kuzaliwa

SHILINGI BILIONI NNE KUGHARAMIA MATIBABU YA UPASUAJI WA MABUSHA NCHINI Serikali ya Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Sul...
26/01/2026

SHILINGI BILIONI NNE KUGHARAMIA MATIBABU YA UPASUAJI WA MABUSHA NCHINI

Serikali ya Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni Nne (4) kwa ajili ya matibabu ya upasuaji wa Mabusha nchini ambapo wananchi wanapata huduma hiyo bila malipo.

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amesema hayo leo Januari 25, 2026 alipofanya ziara kwenye kambi ya upasuaji Mabusha katika Kituo cha Afya Kilakala, Temeke Jijini Dar es Salaam zoezi linaloendelea kwa wiki tatu sasa.

"Serikali imegharamia zaidi ya Shilingi Bilioni Nne katika huduma hii ambapo Upasuaji huu unafanyika kwa kitaalamu, mgonjwa anapewa dawa za usingizi tu sehemu ambayo anafanyiwa upasuaji na ufahamu wake unakuwa upo k**a kawaida na," amesema

Aidha, Dkt. Magembe amesema kuwa tangu kuanza kwa kambi za upasuaji wa mabusha katika Mkoa wa Dar es Salaam, zaidi ya watu 1,300 wamejitokeza kupatiwa huduma. Kati yao, watu 668 walithibitika kuwa na mabusha, na watu 457 wamefanyiwa upasuaji, huku lengo likiwa kuwafikia watu 500 katika vituo vya afya vya Kilakala na Kinondoni.

"Ili kujikinga na magonjwa haya ni muhimu kuzingatia usafi wa mazingira ikiwemo kufukia madimbwi ya maji, kufyeka nyasi katika maeneo yanayotuzunguka ili kuzuia mazalia ya Mbu," amesema

Pia, Dkt. Magembe ametumia fursa hiyo kuwaasa wananchi juu ya umuhimu wa Mfuko wa Bima ya Afya kwa wote kufuatia utekelezaji wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100.

Kwa upande wake Mganga Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Mohammed Mang'una amewataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo kwa kuwa zinatolewa bila malipo ambapo Takwimu zinaonesha kuwa wanaojitokeza zaidi ni wenye umri zaidi ya miaka 45.

Kambi hiyo inafanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo pia itaendelea katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Morogoro pamoja na Mbeya.

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram