03/12/2025
NEST 360 YAKABIDHI MSAADA WA WODI WATOTO WACHANGA WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NA WENYE UZITO PUNGUFU YENYE THAMANI YA TAKRIBANI TZS.582 MIL KWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA
Mpango wa NEST360 ambao unatekelezwa Tanzania na Taasisi ya Afya Ifakara umekabidhi msaada wa wodi maalum ya kuhudumia watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu (njiti) kwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita ya kuboresha huduma ya mama na mtoto na kupunguza idadi ya vifo vya Watoto wachanga wanaozaliwa na kabla ya wakati.
Wodi hiyo yenye vifaa vya kisasa itajumuisha wodi ya watoto wachanga, Kitengo cha Kangaroo kwa kina Mama (Kangaroo Mother Care), na chumba maalum cha Kinababa (Kangaroo Father Care).
Akizungumza wakati wa kuzindua Wodi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe.Albert Chalamila ameipongeza Taasisi ya Afya Ifakara kupitia mpango wa NEST 360 kwa kujitolea kushirikiana na Hospitali ya Amana kuboreshja huduma za Watoto wachanga na kuhakikisha kila mtoto anayezaliwa kabla ya wakati anapata nafasi ya kuishi.
“Vifo vya watoto wachanga ni changamoto kubwa inayotukabili, Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani, WHO za 2023 zinaonesha kuwa kila mwaka, watoto wachanga 50,000 wanapoteza maisha, ambayo ni sawa na mtoto mmoja kwa kila dakika 10 na asilimia 80 ya vifo hivi vinazuilika hivyo hatuna budi kuunganisha nguvu kwa pamoja ili tuweze kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya watoto hawa, amesema Mhe. Chalamila
Awali akikabidhi jengo hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya Ifakara Dkt. Ally Olotu amesema NEST 360 itaendelea kushirikiana na Hospitali ya Amana kwa kusaidi kuboresha miundo mbinu ya huduma ili kupunguza msongamano, kuongeza ufanisi, na kuinua viwango vya ubora wa huduma zinazotolewa katika wodi ya kinamama, watoto wachanga na vitengo vingine vyenye huduma za aina hiyo.
Pia ameongeza kuwa pamoja na kujenga wodi hiyo NEST 360 wameweza kuweka vifaa maalum vya kisasa ikiwemo mashine (CPAP) vifaa vya tiba ya mwanga (phototherapy), na vichujio vya hewa ya oksijeni ili kuwezesha matumizi bora ya vifaa hivyo wametoa mafuzo kwa wataalam 45 ikiwemo wataalam wa afya, wahandisi na mafundi wa vifa