Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

13/12/2025

Mapokezi ya wodi mpya ya neonet

Heri ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara
09/12/2025

Heri ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara

04/12/2025

MPANGO WA NEST 360 KUSAIDIA KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NA UZITO PUNGUFU HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea kuongoza nchini katika kutoa huduma bora za mama na mtoto na kupunguza idadi ya vifo vya Watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu( njiti).

Kauli hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu wakati akipokea msaada wa wodi ya Watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu (njiti) iliyojengwa na Taasisi ya Afya Ifakara kupitia mpango wa NEST 360.

Dkt. Kiwelu ameeleza kuwa Hospitali ya Amana imeweka rekodi ya kuwa hospitali ndogo yenye watumishi wachache, vitanda vichache na wagonjwa wengi ila imefanikiwa kupunguza idadi ya vifo vya watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu hadi kufikia asilimia 9.

“ Tunaishukuru NEST 360, imekuwa ikishirikiana bega kwa bega na hospitali yetu katika kuboresha huduma za watoto wachanga, wamekuwa wakitupatia msaada wa vifaa tiba, dawa pamoja na kuwajengea uwezo wataalam wetu juu ya namna bora ya kuwahudumia wanaozaliwa kabla ya wakati ili kuhakikisha kila pumzi ya mtoto anayezaliwa na changamoto anakuwa salama” amesema Dkt. Kiwelu
Ameongeza kuwa Hospitali ya Amana imekuwa miongoni mwa vituo vya huduma bora kwa watoto wachanga nchini Tanzania yenye teknolojia bunifu, matumizi ya takwimu katika kupanga na kuboresha huduma, pamoja na kuimarisha uwezo wa watumishi kupitia mafunzo na ufuatiliaji endelevu.

MPANGO WA NEST 360 KUSAIDIA KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NA UZITO PUNGUFU HOSPITALI YA RUFAA YA...
03/12/2025

MPANGO WA NEST 360 KUSAIDIA KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NA UZITO PUNGUFU HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeendelea kuongoza nchini katika kutoa huduma bora za mama na mtoto na kupunguza idadi ya vifo vya Watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu( njiti).

Kauli hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu wakati akipokea msaada wa wodi ya Watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu (njiti) iliyojengwa na Taasisi ya Afya Ifakara kupitia mpango wa NEST 360.

Dkt. Kiwelu ameeleza kuwa Hospitali ya Amana imeweka rekodi ya kuwa hospitali ndogo yenye watumishi wachache, vitanda vichache na wagonjwa wengi ila imefanikiwa kupunguza idadi ya vifo vya watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu hadi kufikia asilimia 9.

“ Tunaishukuru NEST 360, imekuwa ikishirikiana bega kwa bega na hospitali yetu katika kuboresha huduma za watoto wachanga, wamekuwa wakitupatia msaada wa vifaa tiba, dawa pamoja na kuwajengea uwezo wataalam wetu juu ya namna bora ya kuwahudumia wanaozaliwa kabla ya wakati ili kuhakikisha kila pumzi ya mtoto anayezaliwa na changamoto anakuwa salama” amesema Dkt. Kiwelu
Ameongeza kuwa Hospitali ya Amana imekuwa miongoni mwa vituo vya huduma bora kwa watoto wachanga nchini Tanzania yenye teknolojia bunifu, matumizi ya takwimu katika kupanga na kuboresha huduma, pamoja na kuimarisha uwezo wa watumishi kupitia mafunzo na ufuatiliaji endelevu.

03/12/2025

NEST 360 YAKABIDHI MSAADA WA WODI WATOTO WACHANGA WALIOZALIWA KABLA YA WAKATI NA WENYE UZITO PUNGUFU YENYE THAMANI YA TAKRIBANI TZS.582 MIL KWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA
Mpango wa NEST360 ambao unatekelezwa Tanzania na Taasisi ya Afya Ifakara umekabidhi msaada wa wodi maalum ya kuhudumia watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati na uzito pungufu (njiti) kwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita ya kuboresha huduma ya mama na mtoto na kupunguza idadi ya vifo vya Watoto wachanga wanaozaliwa na kabla ya wakati.

Wodi hiyo yenye vifaa vya kisasa itajumuisha wodi ya watoto wachanga, Kitengo cha Kangaroo kwa kina Mama (Kangaroo Mother Care), na chumba maalum cha Kinababa (Kangaroo Father Care).

Akizungumza wakati wa kuzindua Wodi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe.Albert Chalamila ameipongeza Taasisi ya Afya Ifakara kupitia mpango wa NEST 360 kwa kujitolea kushirikiana na Hospitali ya Amana kuboreshja huduma za Watoto wachanga na kuhakikisha kila mtoto anayezaliwa kabla ya wakati anapata nafasi ya kuishi.

“Vifo vya watoto wachanga ni changamoto kubwa inayotukabili, Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani, WHO za 2023 zinaonesha kuwa kila mwaka, watoto wachanga 50,000 wanapoteza maisha, ambayo ni sawa na mtoto mmoja kwa kila dakika 10 na asilimia 80 ya vifo hivi vinazuilika hivyo hatuna budi kuunganisha nguvu kwa pamoja ili tuweze kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya watoto hawa, amesema Mhe. Chalamila

Awali akikabidhi jengo hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya Ifakara Dkt. Ally Olotu amesema NEST 360 itaendelea kushirikiana na Hospitali ya Amana kwa kusaidi kuboresha miundo mbinu ya huduma ili kupunguza msongamano, kuongeza ufanisi, na kuinua viwango vya ubora wa huduma zinazotolewa katika wodi ya kinamama, watoto wachanga na vitengo vingine vyenye huduma za aina hiyo.

Pia ameongeza kuwa pamoja na kujenga wodi hiyo NEST 360 wameweza kuweka vifaa maalum vya kisasa ikiwemo mashine (CPAP) vifaa vya tiba ya mwanga (phototherapy), na vichujio vya hewa ya oksijeni ili kuwezesha matumizi bora ya vifaa hivyo wametoa mafuzo kwa wataalam 45 ikiwemo wataalam wa afya, wahandisi na mafundi wa vifa

Uzinduzi wa jengo la watoto waliozaliwa na uzito pungufu
02/12/2025

Uzinduzi wa jengo la watoto waliozaliwa na uzito pungufu

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imepokea msaada wa bima ya afya ya miaka mitano kutoka Assemble Insurance Company kwa n...
02/12/2025

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imepokea msaada wa bima ya afya ya miaka mitano kutoka Assemble Insurance Company kwa niaba ya Perpetua Amana, mtoto aliyezaliwa akiwa na uzito pungufu na akiwa na ulemavu wa mikono. Hatua hii imeleta faraja kubwa kwa hospitali na kwa walezi wa mtoto huyo ambaye bado yupo chini ya uangalizi maalum.

Akizungumza katika tukio hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Amana Dkt. Bryceson Kiwelu aimeipongeza kampuni hiyo kwa mchango wao muhimu katika kuboresha huduma za afya kwa watoto wanaokabiliwa na changamoto za usito pungufu.

“Nawashukuru Assemble Insurance kwa moyo wao wa kipekee na kwa kuonesha kwamba jamii bado ina watu wenye huruma na upendo kwa watoto wanaohitaji zaidi,” alisema Dkt. Kiwelu

Aidha, Mkurugenzi wa Assemble Insurance Bi. Tabia ndiye aliyekabidhi rasmi bima hiyo kwa uongozi wa hospitali, akibainisha kuwa jukumu la kampuni yao ni kushirikiana na jamii katika kuhakikisha watoto wenye uhitaji wanapata huduma bora na endelevu.

Hatua hii imeonesha ushirikiano mzuri kati ya sekta binafsi na taasisi za afya, huku hospitali ya Amana ikiendelea kusimama mstari wa mbele katika kuwahudumia watoto walio katika mazingira hatarishi.

Imarisha mwitikio, Tokomeza UKIMWI
01/12/2025

Imarisha mwitikio, Tokomeza UKIMWI

30/11/2025

Tupo viwanja vya Mnazi mmoja

WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM WAENDELEA KUMIMINIKA KATIKA KAMBI YA UCHUNGUZI NA MATIBABU BILA MALIPO INAYOTOLEWA NA HO...
29/11/2025

WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM WAENDELEA KUMIMINIKA KATIKA KAMBI YA UCHUNGUZI NA MATIBABU BILA MALIPO INAYOTOLEWA NA HOSPITALI YA AMANA , GSM FOUNDATION

Mamia ya wananchi wa Jiji la Dar es salaam na meneo ya jirani wameendelea kujiitokeza kwa wingi katika kambi ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa na ubingwa bobezi bure inayotolewa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa kushirikiana na GSM Foundation ikiwa ni siku ya pili ya utoaji wa huduma hizo katika Viwanja Mnazi Mmoja.

Katika kambi hiyo wananchi wamenufaika na huduma mbalimbali ikiwemo huduma za uchunguzi na matibabu ya macho, afya ya kinywa na meno, magonjwa ya kina mama na afya ya uzazi, magonjwa ya ngozi, magonjwa , sukari , matumizi sahihi ya dawa, elimu juu ya magonjwa yasiyoambukiza, huduma za magonjwa ya Watoto pamoja na Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo.

Kambi hiyo imeanza tarehe 28 hadi 30 Novemba 2025 ambapo itaenda sambamba na utoaji wa bima za afya bila malipo kwa Wanawake, Wazee na Watoto wasio na uwezo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo  ameipongeza Taasisi ya GSM Foundation na  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana ...
28/11/2025

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameipongeza Taasisi ya GSM Foundation na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa kuendesha kambi ya huduma za uchunguzi na matibabu ya ubingwa bobezi bila malipo pamoja utoaji wa bima za Afya kwa watu 300 ikiwa ni Wanawake, Watoto na Wazee wasio na uwezo.

*Dkt.*(Mhe) Mpogolo ametoa pongezi hizo alipotembelea kambi hiyo kwa lengo la kuangalia hali ya utoaji huduma na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kunufaika na huduma hizo ambazo zimesogezwa karibu yao ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya Awamu ya Sita ya *inayohamasisha* Bima ya Afya kwa Wote na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.

Dkt.(Mhe) Mpogolo amebainisha kuwa huduma zinazotolewa na wataalam katika kambi hiyo ni za ubingwa bobezi ambapo ni nadra sana kupata huduma hizo bure,(pasipo malipo) hivyo ni wajibu wa kila Mwananchi wa maeneo hayo kuchangamkia fursa hiyo mapema na kuepuka kufuata huduma ambazo zitawanufaisha watu wa rika zote.

"Nawapongeza GSM Foundation na Hospitali ya Amana kwa kutuletea huduma hizi za kibingwa na ubingwa bobezi, kambi hii imekuwa na upekee kwani kila mwananchi ambaye atafanyiwa uchunguzi na kubainika kuwa na changamoto atapatiwa rufaa ya kwenda kupata huduma zaidi na kulipiwa gharama za matibabu na Taasisi ya GSM Foundation.amesema Mhe.Mpogolo

Aidha, baadhi ya wananchi waliopata matibabu katika kambi hiyo wamesema wamepata huduma kwa muda mfupi bila gharama zozote na kutoa *witoa* wito kwa wananchi wengine kujitokeza zaidi.

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram