Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

Hudhuria kliniki ya Macho kuanzia jumatatu hadi ijumaa saa 2:00 - 8:00 mchana
09/11/2025

Hudhuria kliniki ya Macho kuanzia jumatatu hadi ijumaa saa 2:00 - 8:00 mchana

08/11/2025
MADAKTARI TARAJALI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUJITUMA NA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAOMadaktari tara...
07/11/2025

MADAKTARI TARAJALI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUJITUMA NA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAO

Madaktari tarajali Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wametakiwa kujituma na kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, na Maadili ya taaluma yao ili kutimiza azma ya hospitali hiyo ya kutoa huduma bora nchini.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Jumanne Mafele wakati akifungua mafunzo ya elekezi kwa madaktari tarajali 36 ambapo ameeleza kuwa hospitali ya Amana ni miongoni mwa hospitali za rufaa zinazoongoza kwa kutoa huduma bora hivyo ujio wa madaktari hao utaenda kuwa chahu katika kuendelea kuboresha huduma utoaji wa huduma za afya hospitalini hapo.

" Kuwa daktari si kazi tu ni wito wa moyo na uaminifu mkubwa, nawasihi mkafanye kazi kwa uaminifu, mtunze siri za wagonjwa na mkawahudumie wateja kwa upendo ”amesema Dkt. Mafele

Pamoja na hayo amewahimiza madaktari hao kutumia fursa hiyo k**a daraja la kujifunza kutoka kwa wataalamu waliobobea, huku akisisitiza umuhimu wa kushirikiana na timu nzima ya afya kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi.

Follow us on social media platforms
07/11/2025

Follow us on social media platforms

06/11/2025

  kupiga kura
28/10/2025

kupiga kura

MGANGA MKUU WA SERIKALI AIPA KONGOLE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KWA HUDUMA BORA ZA AFYAMganga Mkuu wa Serikali Dkt...
24/10/2025

MGANGA MKUU WA SERIKALI AIPA KONGOLE HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KWA HUDUMA BORA ZA AFYA

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amefanya ziara ya siku moja Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa lengo la kujionea hali halisi ya utoaji wa huduma za afya pamoja na kuzungumza na watumishi wa hospitali hiyo.

Dkt. Magembe amesema kuwa ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali katika kuimarisha mifumo ya afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazokidhi viwango na kwa wakati.

Aidha ameupongeza uongozi wa hospitali hiyo na kuwataka wataalam kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kufanya hivyo ni kuunga mkono juhudi za kuboresha huduma za afya zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Nimeona moyo wa kujituma miongoni mwa watumishi, na hii ni alama ya uzalendo na weledi, nawasihi muendelee kuzingatia maadili ya kazi, uwajibikaji na mshik**ano miongoni mwenu ili kufanikisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi” amesema Dkt. Magembe

Kwa Upande wake Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu, alitumia fursa hiyo kuwasilisha mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha hivi karibuni ambapo ameeleza kuwa hospitali imefanikiwa kuboresha mifumo wa TEHAMA, kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu, na kuimarisha huduma za dharura.

Katika ziara hiyo Dkt. Magembe ametembelea baadhi ya maeneo ya kutolea huduma ikiwemo Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali, Radiolojia, pamoja na jengo la wagonjwa wa nje (OPD) ambapo amepata nafasi ya kuzungumza na wananchi na kusikiliza maoni yao juu ya huduma wanazopatiwa hospitalini hapo.

Karibu sana hospital ya Rufaa ya Mkoa Amana
24/10/2025

Karibu sana hospital ya Rufaa ya Mkoa Amana

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KUUNGANISHA NGUVU NA DORIS MOLLE FOUNDATION NA SWAHILI FASHION KUBORESHA MALEZI YA WATO...
21/10/2025

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA KUUNGANISHA NGUVU NA DORIS MOLLE FOUNDATION NA SWAHILI FASHION KUBORESHA MALEZI YA WATOTO NJITI

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana umekutana na uongozi wa Taasisi ya Doris Molle Foundation pamoja na wawakilishi wa jukwaa la Swahili Fashion kwa lengo la kujadili namna watakavyoweza kushirikiana katika kuboresha huduma za Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) kwa kuanzisha mradi wa kuwashonea mavazi watoto njiti pamoja na wazazi wanaojifungua watoto hao.

Akizungumza katika kikao hicho Daktari Bingwa wa Watoto Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Grace Mhando amesema hospitali hiyo imekuwa ikijitahidi kuboresha mazingira ya malezi kwa watoto njiti ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto za kiafya na kimazingira tangu siku ya kwanza ya kuzaliwa.

“Tumefurahi sana kwa ujio wenu tunaamini kuwa ushirikiano huu utaleta mabadiliko makubwa, tunawaahidi kuwapa ushirikianao kwakuwa nia yetu ni kuleta faraja, afya bora, na matumaini kwa watoto wanaozaliwa kabla ya wakati” amesema Dkt.Grace

Kwa Upande wa Swahili Fashion wameahidi kuonyesha namna ambavyo wabunifu wamitindo wanavyoweza kuchangia katika sekta ya afya kwa kutengeneza mavazi ambayo yanafaa katumika katika kuwahudumia Watoto njiti na wazazi wao katika kipindi chote cha malezi.

Itambue
21/10/2025

Itambue

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram