Let's Talk..Mental health App

Let's Talk..Mental health App Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Let's Talk..Mental health App, Mental Health Service, Dar es Salaam.

💚 Let’sTalk – Mental Health
🧠 Tunasaidia kufungua mazungumzo ya afya ya akili
🤝 Jukwaa la support, therapy & community
✨ Pakua app yetu & anza safari yako ya uponyaji, Anxiety,Depression, na mengine yanayo husu afya ya akili

“Kuna kipindi mtu anaonekana yuko vizuri, anacheka, anapost, anaonekana yuko strong… lakini moyoni anapigana na vita amb...
05/12/2025

“Kuna kipindi mtu anaonekana yuko vizuri, anacheka, anapost, anaonekana yuko strong… lakini moyoni anapigana na vita ambazo hajawahi kumwambia mtu yeyote.
K**a leo umepitia hapa, nakutumia nguvu hutakiwi kupigana peke yako.”

➡️ “Ulipofika mwisho wa nguvu zako mara ya mwisho, ni kitu gani kilikusaidia kusimama tena?

02/12/2025

“Asubuhi njema 🌞
Leo jaribu kuwa mwema kwako mwenyewe.
Sikiliza mwili wako, heshimu hisia zako, na chukua hatua ndogo za kujijenga.
Hakuna safari ndogo inayopuuzwa kila hatua ina maana.”

30/11/2025

“Leo nataka nikukumbushe kitu kimoja muhimu…
Kuchoka siyo udhaifu. Kukata tamaa kidogo siyo kushindwa.
Ni ubinadamu.”

Kuna siku akili inachoka, moyo unalemaa, na nguvu zinapungua bila sababu hata moja.
Na hilo halikufanyi wewe kuwa dhaifu— linakufanya kuwa binadamu.

Kumbuka:

✨ Una ruhusa kupumzika
✨ Una ruhusa kutulia bila kufanya chochote
✨ Una ruhusa kuhisi unavyohisi
✨ Una thamani hata siku ambazo hujisikii vizuri

Afya ya akili siyo tu kutabasamu — ni kujisamehe, kujitunza na kujikubali hata wakati mambo ni mazito.

👉 Comment “NIPO” k**a leo unachagua kujitunza kwanza.
👉 Share ili ujumbe huu umfikie mtu anayepitia siku ngumu.

30/11/2025

“Asubuhi njema 🌤️💛

Leo chukua sekunde 30 tu ujikumbushe hili:
Hata k**a hujiskii vizuri leo, bado wewe ni muhimu. Bado una thamani. Bado unastahili upendo na utulivu.

K**a unahitaji kusikia hili:
Usiogope kuanza siku polepole. Sio mashindano.
Kila hatua — hata ndogo — ni maendeleo.

✨ Leo andika kitu kimoja tu unachoshukuru au unachotarajia kukifanya kwa ajili ya nafsi yako.

Ujumbe wa leo: “Ninatosha. Nitajali nafsi yangu.”

Niacheni kwenye comment 👉 kitu kimoja unachotaka iwe baraka yako.

29/11/2025

“Sio kila mtu anayekaa kimya anahitaji ushauri; wengine wanahitaji tu mtu aseme, ‘Nipo hapa k**a utahitaji chochote.’

Mara nyingi tunavaa tabasamu lisilo letu, tunasema ‘Nipo sawa’ ilhali mioyoni tunapiga kelele.
Lakini ukweli ni kwamba:
Unachopitia ni halali. Hisia zako ni halisi. Maumivu yako hayakufanyi kuwa dhaifu.
Na kutafuta msaada si kushindwa… ni ujasiri.”

K**a unaona hii imekugusa hata kidogo, weka emoji moja tu yenye hisia yako ya sasa
Huenda ikamsaidia mtu mwingine kujua kuwa si yeye peke yake anayepitia magumu

“Asubuhi njema! 🌅Kumbuka: Kila siku mpya ina nafasi mpya.Usijilaumu kwa yaliyopita jifunze, simama, songa mbele.Leo chag...
23/11/2025

“Asubuhi njema! 🌅
Kumbuka: Kila siku mpya ina nafasi mpya.
Usijilaumu kwa yaliyopita jifunze, simama, songa mbele.
Leo chagua kuwa mwanga hata k**a jana kulikuwa na giza.”

Swali kwa followers:
👉 Leo unaanza siku yako na nguvu gani moja ya kiakili?
(Comment moja tu inaweza kumsaidia mtu mwingine 😊)

Kuna siku moyo unakuwa mzito kuliko hata maneno ya kuelezea.Unatembea, unacheka, unaongea na watu… lakini ndani kuna vit...
22/11/2025

Kuna siku moyo unakuwa mzito kuliko hata maneno ya kuelezea.
Unatembea, unacheka, unaongea na watu… lakini ndani kuna vita ambayo huoni mtu yeyote anayeijua.

Leo nataka kukuuliza bila kificho:
👉 Ni kitu gani kimekuwa kikikutesa kimya kimya?
👉 Ni jambo gani ungependa kusema bila kuhofia kuhukumiwa?

Wacha hii iwe sehemu salama ya kufunguka.
Comment neno 1 linaloelezea hisia zako leo….

Kuna wakati moyo unahitaji tu mtu wa kumuuliza, ’uko sawa kweli?’Lakini wengi wetu tumekuwa mabingwa wa kujifanya tuko p...
22/11/2025

Kuna wakati moyo unahitaji tu mtu wa kumuuliza, ’uko sawa kweli?’
Lakini wengi wetu tumekuwa mabingwa wa kujifanya tuko poa hata k**a ndani tunavunjika vipande vipande.

Leo nataka nikuulize wewe unayesoma hii post…
👉 Unaendelea kupambana kweli, au unaumia kimya kimya?
👉 Ni kitu gani kinakukukosesha amani siku hizi?

Acha tujikumbushe:
Hakuna nguvu k**a kukubali kuwa hujambo. Na hakuna aibu katika kutafuta msaada.
Tuambiane ukweli leo—moyo wako una machungu gani ambayo haujasema kwa mtu yeyote?” ❤️🖤*
“Comment kwa neno moja linaloelezea jinsi unavyojisikia leo…👇

19/11/2025

Kuna wakati maisha huwa yanatubana mpaka tunajisahau.
Tunawaza kila mtu, tunasaidia kila mtu… halafu tunabaki tumechoka sisi wenyewe.
Lakini ukweli ni mmoja: hakuna atakayekuja kukujenga k**a hutaanza kujijenga mwenyewe.

Leo jiulize swali moja tu:
Ni kitu gani kimoja ninachoweza kuanza leo kitakachonipeleka kwenye maisha ninayotamani?
Huenda kikawa ni kujiwekea mipaka, kuacha tabia inayokurudisha nyuma, kusamehe, au kuanza kitu ulichokua unaahirisha kwa muda mrefu.

Hatua ndogo leo inaweza kubadilisha miaka yako ijayo.
Usiogope kuanza, ogopa kubaki pale

14/11/2025

“Wakati mwingine hatujisikii vizuri lakini bado tunaendelea kutabasamu…
Si kwa sababu mambo ni rahisi, ila kwa sababu tumekuwa mabingwa wa kujisimamia kimya kimya.
Lakini ukweli ni huu: unaruhusiwa kuchoka. Unaruhusiwa kupumzika.
Unaruhusiwa kusimama na kusema ‘Leo siwezi, lakini nitaendelea kesho.’

Afya ya akili haimaanishi kuwa na nguvu kila siku
Inamaanisha kujipa ruhusa ya kuwa binadamu: kuhisi, kutulia, kurekebisha, kisha kuendelea polepole.
Leo mpe moyo wako nafasi ya kuwa mkweli bila kujilazimisha.”** 💛

👉 Ni kitu gani ungefanya leo k**a ungejipa ruhusa ya kupumzika kidogo?

14/11/2025

🌤️ Asubuhi Njema wapendwaaaa……
Leo jikumbushe hiki kitu kimoja: Unastahili amani, hata k**a ulimpa kila mtu sababu za kukuharibia siku.
Chagua kuilinda akili yako leo. 💛

🧠 Watu wengi huvaa tabasamu kuficha huzuni zao.Wanaweza kucheka, kuzungumza kawaida, lakini ndani wanapambana na mawazo ...
13/11/2025

🧠 Watu wengi huvaa tabasamu kuficha huzuni zao.
Wanaweza kucheka, kuzungumza kawaida, lakini ndani wanapambana na mawazo mazito, msongo wa mawazo au maumivu ambayo hawawezi kuelezea.

Kabla hujamhukumu mtu au kudhani ana maisha mazuri sana kumbuka: kila mtu ana kitu anachopigana nacho kimya kimya.

👉 Uliza rafiki yako leo, “uko sawa kweli?”
Huenda swali hilo dogo likawa mwanzo wa uponyaji wake ❤️

Address

Dar Es Salaam
000000

Telephone

+255747240062

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Let's Talk..Mental health App posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram