Let's Talk..Mental health App

Let's Talk..Mental health App Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Let's Talk..Mental health App, Medical and health, Dar es Salaam.

💚 Let’sTalk – Mental Health
🧠 Tunasaidia kufungua mazungumzo ya afya ya akili
🤝 Jukwaa la support, therapy & community
✨ Pakua app yetu & anza safari yako ya uponyaji, Anxiety,Depression, na mengine yanayo husu afya ya akili

🧠🧠 Athari za Unyanyapaa kwa Watu Wenye Changamoto za kisaikolojiaKila siku, watu wengi wanapambana kimya kimya na changa...
08/11/2025

🧠🧠 Athari za Unyanyapaa kwa Watu Wenye Changamoto za kisaikolojia

Kila siku, watu wengi wanapambana kimya kimya na changamoto za kisaikolojia msongo wa mawazo, hofu, unyogovu, au majeraha ya kiakili kutokana na matukio mazito. Lakini badala ya kupata msaada na kueleweka, wengi wao hukutana na kitu kingine kinachoumiza zaidi: unyanyapaa.

Unyanyapaa ni pale jamii inapomhukumu mtu kwa sababu ya hali yake ya kisaikolojia. Ni pale anapoitwa majina k**a mwehu, kichaa, au dhaifu. Ni pale watu wanapomgeuka, kumsema kwa siri, au kumpuuza kana kwamba hana thamani tena.

Wengine wanapofikiri kuwa matatizo ya akili ni laana, uchawi, au adhabu kutoka kwa Mungu, wanazidi kumuumiza zaidi yule anayeteseka.
Na matokeo yake?
Mtu huyo anaamua kunyamaza, kujificha, na kubeba mzigo wa maumivu peke yake.

💔 Madhara ya Unyanyapaa

Unyanyapaa si maneno tu ni sumu ya kimya inayoua matumaini taratibu.
Watu wanaonyanyapaliwa mara nyingi hupoteza imani kwa wengine, wanajiona hawafai, na hawastahili upendo wala msaada.
Wengine huanza kujitenga na jamii, hukosa usingizi, hupoteza hamu ya kufanya kazi, au hata kufikiria kujidhuru.

Tafiti nyingi zinaonesha kuwa woga wa kuhukumiwa ndio chanzo kinachowazuia watu wengi kutafuta usaidizi wa kisaikolojia.
Hii inamaanisha, tunaponyamaza au tukinyanyapaa tunakuwa sehemu ya tatizo, si suluhisho.

🌿 Badala ya Kuhukumu, Tuamue Kuelewa

Ni wakati sasa jamii ibadilike.
Badala ya kusema “amechanganyikiwa,” tuanze kusema “anapitia kipindi kigumu, anahitaji msaada.”
Badala ya kusema “ana matatizo ya akili,” tuanze kusema “anapambana na changamoto za kisaikolojia.”

Mabadiliko haya ya maneno yanaweza kuokoa maisha, maana yanaashiria heshima, utu, na huruma.

Kila mmoja wetu anaweza kuwa sehemu ya uponyaji:
• Sikiliza bila kuhukumu.
• Toa bega la faraja.
• Elimisha wengine kuhusu afya ya akili.
• Weka mfano kwa kuzungumza wazi kuhusu hisia zako.

💚 Kumbuka
• Mtu mwenye changamoto za kisaikolojia si mwehu, ni binadamu k**a wewe.
• Kila mtu anaweza kupitia matatizo ya kisaikolojia hata wale wanaoonekana wenye nguvu zaidi.
• Kuomba msaada si udhaifu, bali ni ishara ya ujasiri.

Tukivunja ukuta wa unyanyapaa, tunafungua njia ya upendo, kuelewa, na tiba ya kweli.
Afya ya akili ni haki ya kila mtu na uponyaji huanza pale tunapoamua kuona, kusikia, na kuelewa.

Tuache unyanyapaa. Tuelimishane. Tusaidiane.
Kwa pamoja, tunaweza kujenga jamii inayoponya si inayoumia kimya kimya. 💚

💚 Kujua Wapi pa Kupata Msaada wa KisaikolojiaWatu wengi wanapopitia changamoto za kisaikolojia k**a msongo wa mawazo, hu...
07/11/2025

💚 Kujua Wapi pa Kupata Msaada wa Kisaikolojia

Watu wengi wanapopitia changamoto za kisaikolojia k**a msongo wa mawazo, huzuni, au hofu, huwa wananyamaza kimya wakiamini kwamba “haitasaidia kusema.” Wengine huogopa kuhukumiwa, au hawajui pa kuanzia kutafuta msaada. Lakini ukweli ni kwamba, kuna msaada na msaada huo upo karibu zaidi ya unavyofikiri.

Kwanza, ni muhimu kutambua kuwa kuzungumza kuhusu matatizo yako ya kiakili si udhaifu, bali ni ishara ya ujasiri. Unapochagua kufungua moyo wako na kuomba msaada, unachukua hatua ya kwanza kuelekea katika uponyaji na utulivu wa ndani.

🔹 1. Hospitali na vituo vya afya
Karibu kila hospitali au kituo kikubwa cha afya kina mtaalamu wa saikolojia au mshauri wa afya ya akili. Unaweza kuomba kuonana na mshauri (counselor) au mwanasaikolojia (psychologist). Hawapo kwa ajili ya kukuhukumu, bali kukusaidia kuelewa kinachoendelea na namna ya kukabiliana nacho.

🔹 2. Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs)
Kuna mashirika mengi yanayotoa huduma za ushauri nasaha, hasa kwa watu wanaopitia huzuni, msongo wa mawazo, au changamoto za kifamilia. Baadhi yao hutoa huduma hizi bure au kwa gharama ndogo.

🔹 3. Viongozi wa kiroho
Ikiwa wewe ni mtu wa imani, unaweza pia kuzungumza na mchungaji, sheikh, au kiongozi mwingine wa kiroho unayemuamini. Mara nyingi wanatoa faraja na ushauri wa kiroho unaoweza kusaidia nafsi yako kupumzika.

🔹 4. Marafiki na familia
Usidharau nguvu ya mtu anayekusikiliza kwa makini. Kuongea na rafiki au ndugu anayekuelewa kunaweza kukupunguzia mzigo mkubwa moyoni.

🔹 5. Programu za kidijitali k**a Let’sTalk
Kupitia app k**a Let’sTalk, unaweza kupata elimu kuhusu afya ya akili, kujifunza mbinu za kujituliza, na hata kuzungumza bila kuhukumiwa. Ni jukwaa salama la kujieleza na kujifunza. Nb: app hiyo ya letsTalk ndo ipo mbioni kutoka

✨ Kumbuka: Hakuna haja ya kubeba kila kitu peke yako. Kuomba msaada haimaanishi umeshindwa, bali unachagua kujitunza. Afya ya akili ni muhimu k**a afya ya mwili na wewe unastahili kuwa na amani. 💚

🧠 Mada: Kukubali Hisia ZakoWatu wengi huamini kuwa kuwa na huzuni, hasira, au hofu ni udhaifu lakini ukweli ni kwamba ku...
23/10/2025

🧠 Mada: Kukubali Hisia Zako

Watu wengi huamini kuwa kuwa na huzuni, hasira, au hofu ni udhaifu lakini ukweli ni kwamba kukubali hisia zako ni hatua ya kwanza ya uponyaji wa akili.

Ukijaribu kuzikandamiza hisia, zinajificha kwa muda lakini hubaki ndani zikikuumiza taratibu.
Badala yake, ziheshimu, zielewe, halafu zitumie k**a mwanga wa kuelekea utulivu.

Kumbuka: Hisia zako si adui zako, ni ujumbe kutoka ndani yako…❤️🦋
hisia zako ya akili

21/10/2025

🧠 JINSI YA KUJUA UMEELEMESHA AKILI YAKO KUPITA KIASI

Mara nyingine tunachoka si kwa sababu ya kazi nyingi, bali kwa sababu akili imebeba mzigo mzito wa kufikiri, kuhofia, na kujilaumu.
Dalili kwamba akili yako imeelemewa ni pamoja na:
✨ Kukosa usingizi au kulala kupita kiasi
✨ Kukosa hamu ya kula au kula kupita kiasi
✨ Kujiona huna nguvu wala motisha
✨ Kukasirika kirahisi au kujitenga na watu
✨ Kufikiri sana kuhusu mambo yasiyobadilika

K**a unahisi hivi pumzika.
Usiogope kupunguza kasi, kukaa kimya, au kutafuta msaada.
Kujali akili yako ni hatua ya kwanza ya kupona

💬 Ujumbe wa Asubuhi (Motisha)🌞 “Kila siku mpya ni nafasi nyingine ya kujipenda zaidi, kujitunza zaidi, na kuamini kuwa u...
19/10/2025

💬 Ujumbe wa Asubuhi (Motisha)

🌞 “Kila siku mpya ni nafasi nyingine ya kujipenda zaidi, kujitunza zaidi, na kuamini kuwa una uwezo wa kubadilisha maisha yako.” 💪🕊️


Karibu inbox kwa msaada zaidi

🧠 Kujisamehe Ni Sehemu ya Kupona KisaikolojiaWatu wengi hubeba lawama kwa makosa ya zamani, jambo linalosababisha maumiv...
18/10/2025

🧠 Kujisamehe Ni Sehemu ya Kupona Kisaikolojia

Watu wengi hubeba lawama kwa makosa ya zamani, jambo linalosababisha maumivu ya ndani na msongo wa mawazo. Kujisamehe hakumaanishi kusahau, bali ni kukubali kwamba wewe ni binadamu unayejifunza.

Kujisamehe kunakuondolea mzigo wa hisia hasi k**a hatia, hasira, na aibu. Kadri unavyojifunza kujisamehe, ndivyo unavyopata amani ya akili na nguvu mpya ya kuendelea mbele.

🌿 Jaribu leo: Andika jambo moja ambalo bado unajilaumu nalo, kisha jiambie kwa upole, “Nilifanya nilichoweza kwa wakati ule. Leo najisamehe na naendelea mbele.”

🧠 MCHANA WA LEO: SCHIZOPHRENIA NI NINI?Schizophrenia ni mojawapo ya magonjwa makubwa ya afya ya akili ambayo huathiri ji...
17/10/2025

🧠 MCHANA WA LEO: SCHIZOPHRENIA NI NINI?

Schizophrenia ni mojawapo ya magonjwa makubwa ya afya ya akili ambayo huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kutenda.
Mtu mwenye hali hii anaweza kupoteza uhalisia, yaani hawezi kutofautisha kati ya vitu halisi na vya kufikirika.

Dalili zake kuu ni:

1️⃣ Kusikia au kuona vitu ambavyo havipo (mfano sauti au picha za kufikirika).
2️⃣ Kuwa na imani zisizo sahihi — k**a kuamini kuna mtu anataka kumdhuru bila ushahidi.
3️⃣ Kutokuwa na mpangilio wa mawazo au maneno, mtu anaweza kuzungumza mambo yasiyoeleweka.
4️⃣ Mabadiliko ya hisia na tabia, k**a kujitenga, kutoonyesha hisia, au kupoteza hamu ya mambo aliyoyapenda awali.

Mambo yanayoweza kuchangia:
• Urithi wa kifamilia (genetics)
• Matatizo wakati wa ukuaji wa ubongo
• Matumizi ya dawa za kulevya
• Matukio makubwa ya msongo au trauma

Jambo la Muhimu:

Schizophrenia inaweza kudhibitiwa!
Kwa tiba sahihi k**a vile dawa, ushauri nasaha, na msaada wa familia, mtu anaweza kuishi maisha ya kawaida na yenye furaha. 💚

🩵 Tujifunze kuelewa, si kuhukumu.
Watu wenye schizophrenia wanahitaji msaada, si unyanyapaa.

16/10/2025

🧠 Elimu ya Afya ya Akili: Kujitambua Kisaikolojia

Kujitambua ni hatua ya kwanza kuelekea afya bora ya akili.
Ni uwezo wa kuelewa hisia zako, nguvu zako, udhaifu wako, na namna unavyoitikia mazingira yanayokuzunguka.

✨ Watu wanaojitambua vizuri:
• Hujua lini wanahitaji kupumzika au kuzungumza na mtu.
• Hujua jinsi ya kudhibiti hasira, huzuni, au msongo wa mawazo.
• Hufanya maamuzi kwa utulivu na busara.

🪞Jaribu leo:
Tenga dakika 10 ukiwa kimya, jiulize: “Ninajisikiaje kweli ndani yangu?”
Jibu lako linaweza kuwa mwanzo wa kujitambua😌

🌸 Chapisho la Leo:Kichwa: “Kuna Nuru Hata Baada ya Giza”Wakati mwingine maisha yanakuwa magumu hadi unaona hakuna njia y...
16/10/2025

🌸 Chapisho la Leo:

Kichwa: “Kuna Nuru Hata Baada ya Giza”

Wakati mwingine maisha yanakuwa magumu hadi unaona hakuna njia ya kutoka.
Lakini kumbuka: hata usiku mrefu zaidi una mwisho, na alfajiri inakuja. 🌅

Usikate tamaa pumua✊🏻pumzika 🤜🏻zungumza na mtu unayemwamini.

Una thamani. Wewe ni zaidi ya maumivu unayopitia sasa. 💚


inbox kwa msaada zaidi

Kila mtu amekulia katika mazingira tofauti ambapo mazingira hayo yana mchango mkubwa sana kwenye kumfanya yeye kuwa huyu...
19/08/2025

Kila mtu amekulia katika mazingira tofauti ambapo mazingira hayo yana mchango mkubwa sana kwenye kumfanya yeye kuwa huyu wa sasaivi 🙇‍♀️.

Mchango huo unaweza kuonekana kwenye tabia, hisia pamoja na vitu unavoviamini ambavyo vinaweza kuwa ni hasi au chanya🥲

Karibu tuzungumze kuhusu hilo kwa pamoja ili tuweze kujua maisha yetu ya nyuma yanamchango gani kwenye maisha yetu ya sasa kiujumla.🤗

Usisite kutuma message or comment .
Kuomba msaada siyo udhaifu , udhaifu ni kukaa kimya

Let’s face this together🫂( childhood trauma)

🥰🥰🥰learn to know yourself 🥰🥰take time
02/07/2025

🥰🥰🥰learn to know yourself 🥰🥰take time

26/06/2025

*Tuongee kuhusu Uponyaji (Healing)*

*Uponyaji ni nini ?*
Uponyaji ni mchakato wa kuendelea mbele baada ya kupitia jambo au tukio lililokuumiza. Maana yake unaweza kulizungumzia jambo hilo bila kujihisi maumivu makali k**a mwanzo.

Katika maisha, watu hupitia mambo mbalimbali yanayowaumiza—yawe ni kutoka kwenye familia, mahusiano ya kimapenzi au jamii. Ni sawa kabisa kuhisi kuumizwa au kuvunjika moyo kwa sababu wewe ni binadamu. Lakini si sawa kuendelea kubaki kwenye hali hiyo kwa muda wote 😔. Unahitaji kujiponya na kuendelea mbele.

*Kumbuka: Uponyaji ni mchakato, si tukio moja la haraka. Unahitaji muda na juhudi. Watu wengi wanateseka kwenye familia zao kwa sababu hawajapona majeraha ya zamani—na sasa wanawaumiza wengine bila kujua. Katika mahusiano pia, watu wanaingia na majeraha yao na wanawaumiza wenzao ambao hawakuwasababishia maumivu hayo.💔

*Kuingia kwenye uhusiano bila kupona ni sawa na kumuumiza mtu mwingine kihisia, kiakili, na hata kimwili. Acha kujiua na kuwaua wengine kiakili 😓
Kuanzia leo acha kuumiza wengine kwa majeraha yako—pona kwanza kabla ya kuanzisha urafiki, mahusiano ya kimapenzi au ya kifamilia.💪

Mambo ya Kufanya Kwenye Safari ya Uponyaji:

- *Jijali na Jipende:
Anza kwa kujipenda wewe mwenyewe kabla ya kumpenda mtu mwingine. Jitunze, toka kwenda sehemu safi za kukupumzisha akili na moyo😊.

- *Zungumza:
Zungumza na mtu unayemwamini. K**a huna, andika kwenye daftari (journal) mambo unayotaka kubadilisha, mipango yako, mambo mazuri ya siku yako, na hata hisia zako🤗.

- *Fanya Mazoezi:
Ikiwezekana, fanya mazoezi. Yatakusaidia kuelekeza mawazo yako kwenye wewe mwenyewe na kukuimarisha kimwili na kiakili.

- *Tambua Mazuri Kuhusu Wewe:
Jiangalie, tambua mambo mazuri kuhusu wewe na uyape kipaumbele. Pia, fanyia kazi udhaifu wako ili uendelee kuwa bora zaidi.🤗

- *Samehe Bila Hukumu:
Samehe wote waliokuumiza, lakini haina maana lazima urudi kwenye yale mazingira au watu waliokuumiza. Msamaha ni kwa ajili yako—unakupa amani ya moyo na utulivu wa nafsi🚶‍♀️.

*Kwa hiyo, samehe, jiponye na songa mbele.
Una thamani kubwa kuliko unavyofikiria—jipe muda, utapona. 💖.
Tujali afya zetu za kiakili kwa kujiponya ,afya ya akili ni Mali 🧠.

Address

Dar Es Salaam
000000

Telephone

+255747240062

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Let's Talk..Mental health App posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram