Medical Stores Department (MSD)

Medical Stores Department (MSD) MSD is annually audited by CAG and has fully-fledged competent internal audit Unit that oversees internal controls effectiveness.

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by the public health services as the Ministry of Health may from time to time approve. Board of Trustees is the highest decision-making body that governs and set the directions of MSD on behalf of the Minister for Health, The Board composed of nine(9) members appointed every three years. The Chairman appointed by the President of the United Republic of Tanzania, eight (8) members are appointed by the Minister responsible for health.The Board is comprising of a multidisciplinary team including eminent public servants, scientists, practicing medical doctors, lawyers, accountants, professors and renowned economists. To implement its responsibilities the Board operates through three committees namely; Audit and Risk Management Committee that provides the management with accurate information on the effectiveness of risk management and internal controls including regulatory compliance by the Department; Technical Services Committee that handles all matters related to quality of medicines and medical supplies together with management expired medicines. Finance and Administration Committee tha is mandated in handling all matters related to MSD Financial Management, Human Resources Management and Administrative functions of the Department. The Board delegates the day to day management of the department operations to Director General who is appointed by the President of the United Republic of Tanzania. The administrative functions and operations of Department are carried by and through the Executive Management Team (EMT).The EMT is constituted by the Director General, Director of Human Resources and Administration, Director of Finance and Planning, Director of Logistics, Director of Procurement, Director of Information and Communication Technology, Director of Customer Service and Zonal Operations as well as Chief Legal Counsel. The departnment operates through eight zonal stores in Dar-es-salaam, Mwanza, Iringa,Moshi,Mbeya,Tabora, Dodoma and Mtwara suppoted by two Sales Points in Tanga and Muleba.

Mashindano ya SHIMMUTA yaliyokuwa yanafanyika mkoani Morogoro yamemalizika leo, ambapo mtumishi wa MSD, Heavenlight, ame...
06/12/2025

Mashindano ya SHIMMUTA yaliyokuwa yanafanyika mkoani Morogoro yamemalizika leo, ambapo mtumishi wa MSD, Heavenlight, ameibuka kinara kwa kutwaa medali mbili za dhahabu katika mbio za riadha kwa wanawake.

Heavenlight aling’ara kwenye fainali za mbio za mita 100 kwa kushika nafasi ya kwanza, na pia akachukua nafasi ya pili katika mbio za mita 200.

Mashindano ya SHIMMUTA yaliyokuwa yanafanyika mkoani Morogoro yamemalizika leo, ambapo mtumishi wa MSD, Heavenlight, ame...
06/12/2025

Mashindano ya SHIMMUTA yaliyokuwa yanafanyika mkoani Morogoro yamemalizika leo, ambapo mtumishi wa MSD, Heavenlight, ameibuka kinara kwa kutwaa medali mbili za dhahabu katika mbio za riadha kwa wanawake.

Heavenlight aling’ara kwenye fainali za mbio za mita 100 kwa kushika nafasi ya kwanza, na pia akachukua nafasi ya pili katika mbio za mita 200.

06/12/2025

Hakika MSD imebeba dhamana kubwa ya kuhakikisha watanzania wanapata dawa zenye ubora na viwango vinavyokubalika.

Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi, anaeleza kwa kina kuhusu dhana hii.

04/12/2025

MSD tumeshiriki kikamilifu kwenye maadhimisho ya kikanda ya Afrika ya wiki ya kimataifa ya kudhibiti usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.
Msikilize Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa MSD, Bi. Etty Kusiluka akitanabaisha yaliyojiri.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Tanzania imedhamiria kuhakikisha in...
03/12/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Tanzania imedhamiria kuhakikisha inalinda afya za wananchi na maisha yao kiujumla ikiwa ni pamoja na mazingira kwa kuwekeza kwenye tafiti za kisayansi na kuhimiza matumizi sahihi ya dawa k**a inavyoelekezwa na wataalam.

Dkt. Mchimbi ameyasema hayo leo wakati akifungua maadhimisho ya kikanda ya Afrika ya wiki ya kimataifa ya kudhibiti usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, yanayoendelea kufanyika jijini Dar es salaam. Amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa kwenye sekta ya afya, Tanzania ina dhamira ya kuongeza juhudi za kukabiliana na usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa kupitia mipango mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji ili kuwa sera na afua zinazozingatia ushahidi.

Awali, Makamu wa Rais alitembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ya wadau wa afya ikiwemo banda la Bohari ya Dawa (MSD) na kupata maelezo ya namna ambavyo MSD inahakikisha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya haukatiki ili kuwezesha wananchi kupata dawa zenye viwango vilivyothibitishwa wakati wote.

Meneja Mawasaliano na Uhusiano, Bi. Etty Kusiluka alimueleza kiongozi huyo kuwa serikali imeendelea kutoa fedha za bajeti za kununulia dawa kwa wakati, k**a ilivyopangwa kwenye bajeti ya serikali. Ameeleza kuwa hadi sasa, tayari serikali imetoa asilimia 42 ya bajeti iliyopangwa mwaka huu wa fedha.

Kwa upande mwingine Meneja Uhusiano ameleza kuwa MSD imeweza kununua na kusambaza vifaa vya kisasa ikiwa ni pamoja na viti vya kinywa na meno 693, na mashine zake za mionzi 538, na kumuonyesha baadhi ya vifaa vilivyokuwepo bandani hapo,ikiwemo vya kinywa na meno.

Vilevile, Dkt. Nchimbi alipata wasaa wa kuona baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na MSD, mathalani glavu na barakoa.

Bohari ya Dawa (MSD) imeshiriki maadhimisho ya wiki ya kukabiliana na usugu wa dawa na matumizi holela ya dawa kwa binad...
03/12/2025

Bohari ya Dawa (MSD) imeshiriki maadhimisho ya wiki ya kukabiliana na usugu wa dawa na matumizi holela ya dawa kwa binadamu, mifugo na kilimo yaliyoanza leo jijini Dar es salaam.

Mbali na kushiriki mkutano wenye majadiliano mbalimbali kuhusu kukabiliana na usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA), MSD imeonyesha bidhaa zake na kuelezea majukumu yake kwa wadau walioshiriki maadhimisho hayo.

Akizungumza kwenye shughuli hiyo, Mganga Mkuu wa serikali (CMO) Dkt. Grace Magembe ameeleza kuwa tafiti zinaonyesha kuwa yapo matumizi holela ya dawa za binadamu, mifugo na mazao ambayo yanaweza kusababisha madhara makubwa.

Hata hivyo, amewashauri baadhi ya watu wanaokatisha dozi wanazoandikiwa na madaktari waache mara moja kwani tabia hiyo inaongeza usugu wa vimelea vya maradhi.

02/12/2025

Katika kipindi cha miaka mitatu, MSD imekuwa chachu ya mageuzi makubwa kwenye huduma za radiolojia nchini, kutoka kuongeza upatikanaji wa vifaatiba vya kisasa hadi kuboresha teknolojia za uchunguzi.

Safari hii ya maboresho inaendelea, ili kuwezesha huduma bora za afya kwa Watanzania. Msikilize Mradiolojia ambaye ni mtaalamu wa Uhakiki Ubora kutoka MSD, Bw. Grayson Mwakalindile akifafanua zaidi.



01/12/2025
Matuki mbalimbali katika Picha, Wakati wa Mkutano Mkuu wa TARA 2025.
01/12/2025

Matuki mbalimbali katika Picha, Wakati wa Mkutano Mkuu wa TARA 2025.

30/11/2025


29/11/2025

*MSD YASHIRIKI WARSHA NA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA TARA 2025*Novemba, 13-15 2025 Dodoma.Bohari ya Dawa (MSD) imeshiriki k...
29/11/2025

*MSD YASHIRIKI WARSHA NA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA TARA 2025*

Novemba, 13-15 2025
Dodoma.

Bohari ya Dawa (MSD) imeshiriki kikamilifu katika Warsha ya Kitaalamu na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Radiolojia Tanzania (TARA), uliofanyika jijini Dodoma kuanzia tarehe 13 hadi 15 Novemba 2025.

Ushiriki huu unaonyesha dhamira ya MSD kuendelea kuimarisha mnyororo wa upatikanaji wa vifaa tiba na bidhaa za afya nchini, hususan katika eneo la radiolojia ambalo ni nguzo muhimu katika utambuzi na utibabu wa magonjwa.

Kando ya mkutano huo, MSD imeshiriki maonyesho maalum yaliyoandaliwa na chama hicho, ambapo imepata fursa ya kuonesha bidhaa na vifaa mbalimbali vya radiolojia vinavyopatikana kupitia mfumo wake wa ununuzi.

Bidhaa hizo ni pamoja na:
Vifaa vya uchunguzi ikihusisha Digital X-ray (DR), Ultrasound machines za teknolojia ya kisasa zinazorahisisha utambuzi wa mapema wa magonjwa, CT-scan consumables- filamu za kidigitali (Digital Imaging Plates) na vifaa vingine saidizi vya radiolojia.

Kupitia ushiriki huu, MSD imeendelea kuimarisha uhusiano wake na wataalamu wa radiolojia, hospitali, pamoja na wadau wa sekta ya afya, huku ikiendelea kujidhatiti katika kuhakikisha vifaa vya kisasa, vyenye ubora na teknolojia ya hali ya juu, vinapatikana nchini ili kukuza utoaji wa huduma bora za uchunguzi wa magonjwa.

Address

Off, Nyerere Road, Keko Mwanga
Dar Es Salaam
9081

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Medical Stores Department (MSD) posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram