24/07/2025
MAISHA NA AFYA
Lishe kwa mgonjwa wa Kisukari.
Basics.
Na Dr. Chris Cyrilo:
Tuanze na kuzingatia kanuni hizi!
1. Tuache kabisa matumizi ya sukari na vinywaji vya sukari (soda nk).
Chai tutakunywa ya tangawizi, mdalasini, iliki, mchaichai, karafuu nk.
2. Tupunguze vyakula vya wanga k**a Ugali, Wali, Ndizi, Viazi nk.
📌Ugali au wali tutakula ukubwa wa ngumi. Kunja ngumi, huo ukubwa unaouona ndio ukubwa wa ugali au wali au viazi nk tunapaswa kula.
K**a unafanya kazi nzito unaweza kuongeza ngumi ya pili.
3. Chakula cha hapo juu si cha kushiba kwa wengi. Kwahiyo tutaongeza mbogamboga na matunda (hasa yasio na sukari nyingi - Parachichi, Tango, Apple (Tofaa), Papai, Pera, Tikiti (pamoja na utamu lkn haliongezi sana sukari).
Matunda k**a Nanasi, Ndizi zilizoiva sana, chungwa, embe ni matunda ya kula kidogo.
Maandalizi/mapishi ya mboga nayo ni kitu cha msingi. Mara nyingi mafuta tunayotumia ni mengi au hayafai kiafya kwa hiyo tunakuwa hatujaepuka kitu. Kile ulichokiacha kwenye ugali/wali unakiingiza kupitia mafuta. Unashangaa unakula kidogo lkn mwili unaongezeka, kumbe ni mafuta unayotumia kwenye mboga/nyama ma vitoeo vingine.
Mbogamboga inabidi ziwe nusu ya mlo wako wote wa mchana au jioni/usiku.
Note; Mbogamboga sio majani pekee. Ni pamoja na nyanya, karoti, hoho, maboga, nyanya chungu, bilinganya, vitunguu nk. Hivi sio viungo, ni vyakula. Tumejisahau na kuvifanya viungo kwahiyo tunakula kidogo sana. Hivi ndio tunapaswa kushiba.
4. Tule zaidi nafaka nzima kuliko zilizosagwa. Badala ya ugali, tule zaidi kande, mahindi ya kuchemsha, mtama, uwele, mchele wa brown.
Vyakula jamii ya kunde (kunde, maharage, njegere, mbaazi) vinaweza kuliwa na mboga za majani badala ya wali na ugali.
5. Maji ya kutosha, angalau glasi 8 kwa siku/lita 2 kwa siku.
6. Punguza vyakula vya kukaanga, vyenye chumvi na sukari nyingi. Zidisha vyakula vya kuchemsha/kupwaza.
7. Mazoezi, angalau kutembea kwa dakika 30 - 45 kwa siku au hatua 10,000 (k**a mita 500 kwa siku). Ukiweza zaidi ni vizuri.
MFANO WA RATIBA YA LISHE KWA MTU MWENYE KISUKARI
ASUBUHI
Vinywaji;
Ujiwa Dona usio na sukari,
Uji wa Ulezi usio na sukari,
Chai ya mchaichai, iliki, mdalasini (bila sukari)
Maziwa bila sukari.
Vitoweo;
Yai la kuchemsha 1,2 (mayai hayana shida labda uogope kuvuruga tumbo 😂)
Kiazi kitamu (ukubwa wa ngumi)
Ndizi za kuchemsha (ukubwa wa ngumi)
Punguza vyakula vya ngano kwasbb ya ngano yenyewe na mafuta (vyote viwili vinaongeza uzito wa mwili na kuathiri afya).
Nyongeza!
Maharage, Mbaazi, Kunde, Njegele
Hivi unaweza kuchemsha au kupika kwa n**i.
Karanga au Korosho kwa ajili ya kutafuna.
NB. Pamoja na kuwa vyakula hivi ni salama, EPUKA KULA SANA.
MCHANA
Vyakula kikuu;
Ugali wa dona, wali wa brown (brown rice), Ndizi za kuchemsha, magimbi, Viazi, Ugali wa Ulezi, Mtama, Muhogo
📌ZINGATIA - Hivi tunakula ukubwa wa ngumi yako.
Makande ya n**i, mahindi ya kuchemsha, kunde za n**i, maharage ya n**i, vinaweza kuwa vyakula vikuu mbadala wa ugali na wali. Hivi unaweza kula zaidi ya ngumi yako.
Mboga;
Mboga za majani - zozote.
Kumbuka Nyanya, bilinganya, hoho, karoti, vitunguu, nyanya chungu...ni mboga pia. Usijipunje.
Mboga ziwe nusu ya chakula chako chote.
Kumbuka kupunguza sana mafuta, au usitumie kabisa mafuta. Punguza chumvi, Ongeza viungo kwa ajili ya ladha nzuri.
Mboga Protini!
Nyama - chemsha, ongeza viungo kwa ajili ya ladha.
Samaki au Dagaa - chemsha, ongeza viungo kwa ajili ya ladha. Nyama, samaki na dagaa vinaweza kupikwa pamoja na mboga.
JIONI
Unaweza kuchagua moja ya mifano hiyo ya asubuhi au mchana.
Nyongeza;
- Supu ya mbogamboga
- Mtori wa viazi au ndizi na nyama
- Maboga
- Mapapai mabichi (Yaweza kupikwa na n**i)
- Mboga ya Mayai
- Kande za Nyama (Mahindi na Nyama)
Vyakula vizuri ni vingi sana.
Cha msingi ni kuzingatia maandalizi!
Epuka mafuta mengi.
Epuka Sukari.
Epuka kuivisha sana.
Punguza chumvi, ongeza viungo.
Pombe (kwa mgonjwa wa kisukari nakushauri uache. Ile kisataarabu imekaa kimtegomtego!
Sigara acha!
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.