29/01/2026
VIDEO
Kijana, raia wa Kenya akiwa vitani kupigania maslahi ya Urusi katika eneo la Donesky, mashariki mwa Ukraine. Eneo hilo kwa sasa linakaliwa na Urusi baada ya uvamizi wa Februari 2022.
Warusi, baada ya kuona vita dhidi ya Ukraine inakuwa ngumu kutokana na misaada ya kijeshi kutoka Ulaya na Marekani, waligundua vita hii itakuwa ndefu na kwahiyo walichukua hatua kadhaa;
Moja, walianza kutafuta silaha za gharama nafuu katika mataifa rafiki, hasa Iran na Korea Kaskazini. Kwahiyo, badala ya kutumia makombora ya mamilioni ya dola wakageukia drones kutoka Iran zinazogharimu dola 20,000 tu kwa kila moja.
Pili, walianza kukarabati silaha zao za zamani enzi za Sovieti ili kufidia mahitaji ya muda mrefu.
Tatu, waliitisha upya, kwa nguvu zaidi wito wa vijana kujiunga na jeshi ili kuongeza idadi ya wapiganaji.
Nne, Walianza kutumia mamluki wa kijeshi. Mfamo wa mamluki hawa ni Wagner Group. Mamluki wengi walitoka katika nchi za kiarabu za Mashariki ya Kati na Afrika.
Somo! Matukio ya dunia ya sasa yameanza kutupa ishara kwamba mataifa makubwa yanapotaka mambo yao hayaangalii sheria za kimataifa. Lakini raia wa mataifa madogo nao wamekuwa mashabiki na wafuasi wa mataifa makubwa. Hili ni kumbusho kwa mataifa madogo. Pengine kuna raia wengi wa Urusi na/au Marekani waliozaliwa Tanzania/Kenya na wanaoishi TZ, Kenya nk.
Mfano halisi ni huyu kijana wa k**enya aliyaemua kufa au kuua kwa ajili ya Urusi. Wapo watanzania pia wanaopigana huko Urusi (na kwenye vikosi vya kijeshi vya mataifa mengine ya Ulaya na Marekani).
Hii ni Wake-up call kwa mataifa madogo. Kwamba kadiri siku zinavyoenda, mipaka ya ardhi inapoteza umuhimu wake. Dunia inaendelea kukumbatiwa pamoja. Siasa zinakuwa za kidunia zaidi kuliko kitaifa. Raia wa nchi moja wanaweza kuamua kufa kwa ajili ya nchi nyingine. Vijana wanapata mbinu za kijeshi na uzoefu kutoka kwenye vita kubwa, wakati viongozi wao wa kijeshi katika nchi zao wanapata vitambi.
Ole wao serikali za mataifa madogo zinazochochea mivunjiko ya amani ndani ya nchi zao wenyewe na kufanya kila jitihada za kuwafanya vijana wasiwe wazalendo; wizi, ufisadi, dhuluma, uzembe, utekaji, mauaji na matusi kwa vijana.
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo