Dr. Christopher Cyrilo

Dr. Christopher Cyrilo Medical Doctor| Health Literacy expert | Social Activist | Writer
(1)

Yes! Ni upumbavu.
02/02/2026

Yes! Ni upumbavu.

Una mdada wa kazi, ni msichana wa miaka 18 au zaidi), maana yake ana mahitaji yake ya kiutu uzima! Sio?Je! Unampa muda w...
01/02/2026

Una mdada wa kazi, ni msichana wa miaka 18 au zaidi), maana yake ana mahitaji yake ya kiutu uzima! Sio?

Je! Unampa muda wa kutoka kwenda ku-refresh mwili na akili au unamfungia ndani k**a mfungwa?
Unahakikisha anapata elimu na ushauri juu ya masuala ya mahusiano, maradhi ya zinaa, ujauzito nk? Au yeye ni wa kupika, kutunza nyumba na watoto ila mambo mengine ya kibinadamu hayamuhusu?

Halafu akipewa mimba na vijana huko nje, unamfukuza. Kumbe ulikuwa na nafasi ya kumsaidia kiakili.
Akilala na kijana wako wa kiume?
Akianza kumtega Baba wa familia?

Umewahi kufikiria kwamba mfanyakazi wako wa k**e k**a ni mtu mzima atahitaji muda wake wa mambo binafsi? Tena ikibidi umwambie akipata boy friend amlete amtambulishe kwako. Ni salama! Ni utu uzima.
Sasa endelea kuamini huyo ni mtoto wa miaka 14, mnyime uhuru, mdhibiti ndani ya geti, subiri surprise.

Pombe kistaarabu!
Sigara acha.
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.

Na Naitwa Dr.A.C. Namuombea msaada huyu binti Neema (22) mzaliwa wa Bukoba lakini mkazi wa Shinyanga kwa sasa.Historia y...
01/02/2026

Na
Naitwa Dr.A.C. Namuombea msaada huyu binti Neema (22) mzaliwa wa Bukoba lakini mkazi wa Shinyanga kwa sasa.

Historia yake ni ndefu kidogo. Ni yatima aliyelelewa na baba mdogo huko Ifakara Morogoro. Mwaka 2022 mlezi wake alifariki, hivyo akalazimika kurudi Bukoba kwa bibi yake.

Akiwa Bukoba alikutana na kijana mmoja ambaye alimpa ujauzito akajifungua 2024. Baadae alianza kupata maumivu na uvimbe kwenye taya. Mzazi mwenzie alimuaga anaenda Shinyanga kutafuta kazi ili aweze kumhudumia yeye na mtoto.

Uvimbe ulizidi kuongezeka hivyo akalazimika kumfuata mwenzie Shinyanga. Kijana alipoona hali ya uvimbe alimkimbia na hadi leo hajulikani alipo. Baada ya muda alifukuzwa walipokuwa wakiishi kwa kushindwa kulipa kodi. Akaanza kuhangaika mtaani akiwa na mtoto wa miezi 18 na uvimbe ukizidi kukua.

Muuguzi mmoja alimsaidia kumleta hospitalini. Vipimo ilionesha ana saratani ijulikanayo k**a “Ameloblastoma” yani seli za “ameloblasts" kukua na kuharibu mfupa wa taya na kusababisha sura ya uso kubadilika.

Akifanyiwa upasuaji anaweza kupona kwa sababu ni saratani isiyosambaa. Tumempa rufaa ya kwenda Bugando, lakini hana uwezo wa kumudu gharama. Maisha yake ni magumu na tumekuwa tukimsaidia yeye na mwanae kuanzia malazi, chakula na matibabu.

Anahitaji upasuaji wa kuondoa uvimbe na sehemu ya taya iliyoathirika (Wide local excision). Kisha kurejesha muonekano (aesthetics) na kazi ya taya (function). Kwa cash gharama inaweza kuwa kubwa lakini akipata bima ya NHIF kifurushi cha juu cha Tanzanite (TZS 2,712,000/=) kinaweza ku-cover sehemu kubwa ya matibabu, zikabakia gharama ndogondogo.

:
Maisha ya Neema hayajawa rahisi tangu utotoni. Kufiwa na wazazi na kuachwa yatima, kulelewa na baba mdogo naye akafariki, kurudi kwa bibi Bukoba, kupewa ujauzito, kuugua saratani, kukimbiwa na mwenzie kutokana na ugonjwa. Yote hiyo ni mitihani ya maisha. Hana ndugu wa kumlilia. Sisi ndio ndugu zake.

Tumchangie angalau 5M ili apate matibabu na kiasi kingine kimsaidie kujiuguza. Tuma sadaka yako kupitia M-PESA #0752581983, Tigopesa #0719744954, CRDB #0150633516500, NMB #24110012109 Gifted Hearts Foundation. RudishaTabasamu LetLoveLead.

29/01/2026

VIDEO
Kijana, raia wa Kenya akiwa vitani kupigania maslahi ya Urusi katika eneo la Donesky, mashariki mwa Ukraine. Eneo hilo kwa sasa linakaliwa na Urusi baada ya uvamizi wa Februari 2022.

Warusi, baada ya kuona vita dhidi ya Ukraine inakuwa ngumu kutokana na misaada ya kijeshi kutoka Ulaya na Marekani, waligundua vita hii itakuwa ndefu na kwahiyo walichukua hatua kadhaa;
Moja, walianza kutafuta silaha za gharama nafuu katika mataifa rafiki, hasa Iran na Korea Kaskazini. Kwahiyo, badala ya kutumia makombora ya mamilioni ya dola wakageukia drones kutoka Iran zinazogharimu dola 20,000 tu kwa kila moja.

Pili, walianza kukarabati silaha zao za zamani enzi za Sovieti ili kufidia mahitaji ya muda mrefu.

Tatu, waliitisha upya, kwa nguvu zaidi wito wa vijana kujiunga na jeshi ili kuongeza idadi ya wapiganaji.

Nne, Walianza kutumia mamluki wa kijeshi. Mfamo wa mamluki hawa ni Wagner Group. Mamluki wengi walitoka katika nchi za kiarabu za Mashariki ya Kati na Afrika.

Somo! Matukio ya dunia ya sasa yameanza kutupa ishara kwamba mataifa makubwa yanapotaka mambo yao hayaangalii sheria za kimataifa. Lakini raia wa mataifa madogo nao wamekuwa mashabiki na wafuasi wa mataifa makubwa. Hili ni kumbusho kwa mataifa madogo. Pengine kuna raia wengi wa Urusi na/au Marekani waliozaliwa Tanzania/Kenya na wanaoishi TZ, Kenya nk.
Mfano halisi ni huyu kijana wa k**enya aliyaemua kufa au kuua kwa ajili ya Urusi. Wapo watanzania pia wanaopigana huko Urusi (na kwenye vikosi vya kijeshi vya mataifa mengine ya Ulaya na Marekani).

Hii ni Wake-up call kwa mataifa madogo. Kwamba kadiri siku zinavyoenda, mipaka ya ardhi inapoteza umuhimu wake. Dunia inaendelea kukumbatiwa pamoja. Siasa zinakuwa za kidunia zaidi kuliko kitaifa. Raia wa nchi moja wanaweza kuamua kufa kwa ajili ya nchi nyingine. Vijana wanapata mbinu za kijeshi na uzoefu kutoka kwenye vita kubwa, wakati viongozi wao wa kijeshi katika nchi zao wanapata vitambi.

Ole wao serikali za mataifa madogo zinazochochea mivunjiko ya amani ndani ya nchi zao wenyewe na kufanya kila jitihada za kuwafanya vijana wasiwe wazalendo; wizi, ufisadi, dhuluma, uzembe, utekaji, mauaji na matusi kwa vijana.

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo

Nauliza!
27/01/2026

Nauliza!

Tuishi humu
26/01/2026

Tuishi humu

26/01/2026

NAUNGANA NA UONGOZI WA CHADEMA; MWIGULU HASTAHILI HESHIMA.

Mmoja wa wanasayansi bora wa eneo la fizikia, mvumbuzi wa Theory of Relativity na kanuni ya E = MC² ambaye pia ni mwanafalsafa, Albert Einstein alipata kusema;
Dunia haitaharibiwa na watenda maovu, bali dunia itaharibiwa na wale wasiochukua hatua dhidi ya uovu.

Nautafakari ujumbe huu nikitazama tukio hili la kumpa heshima Mwigulu Nchemba kwenye msiba wa mwasisi wa CHADEMA. Mwigulu ni mmoja wa waasisi wa mipango ya kuiua CHADEMA kwa njia za kikatili. Yeye mwenyewe kwa kauli zake akiwa Mwenezi wa CCM alitangaza kuiua CHADEMA. Lakini kauli zake hazikuwa za kisiasa tu, zilikuwa kauli zilizojengwa kwa chuki dhidi ya CHADEMA. Huyu ni mtu ambaye, akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, viongozi wa CHADEMA walikiona cha Mtema kuni.

Akiwa Waziri wa Mambo ya ndani Tundu Lissu alipigwa risasi hadharani, na hakuna uchunguzi wowote uliofanyika. Alphonse Mawazo alichinjwa kule Geita, hakuna uchunguzi uliofanyika. Ben Saa Nane alitekwa na kupotezwa, hakuna uchunguzi uliofanyika. Na yeye k**a Waziri wa Mambo ya Ndani hakuwahi kutoa kauli yoyote ya kuonasha uwajibikaji, hata ya kuzuga tu. Hakuwahi. Sanasana alizuia watu wasikusanyike kumuombea tundu Lissu. Alifika mbali na kuzuia hata watu kuvaa fulana za kumuombea Tundu Lissu.
Ni wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, matukio ya kuteka na kupoteza wakosoaji wa CCM yalipamba moto.

Ingawa siwezi kumuhusisha moja kwa moja Mwigulu Nchemba na matukio hayo, lkn kwa nafasi yake k**a Waziri wa Mambo ya ndani, yeye mwenyewe hakuwahi kufanya jambo la kuonesha hausiki na matukio hayo. Na zaidi kauli zake, za huko nyuma na hata sasa zinaonesha aina ya mtu aliyepo ndani ya mwili wa Mwigulu Nchemba.

Swali; Je! Mwigulu Nchemba alistahili kupewa heshima kwenyw Msiba wa mwasisi wa CHADEMA?

Kwa matendo yake, kwa kauli zake anazotoa huko barabarani, huyu hakupaswa kupewa hata nafasi ya kuongea tu.
Naungana na Heche na viongozi wengine kukataa kusimama na kumpa heshima Mwigulu Nchemba. Hastahili!

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo

Serikali haramu!
25/01/2026

Serikali haramu!

Now this! 😴
22/01/2026

Now this! 😴

Uzazi wa Mpango! Ni njia gani unayopendelea kutumia kupanga uzazi? Wanawake wengi wanatoa malalamiko yanayotokana na mat...
21/01/2026

Uzazi wa Mpango!
Ni njia gani unayopendelea kutumia kupanga uzazi?

Wanawake wengi wanatoa malalamiko yanayotokana na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango. Malalamiko ni mengi. Ingawa wataalamu tunasema kuna maudhi madogo madogo yatokanayo na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango, lakini kwa idadi fulani ya wanawake inaonekana maudhi hayo si madogo.

Je! Umewahi kutumia njia yoyote ya uzazi wa mpango?
Una uzoefu gani juu ya maudhi yanayotokana na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango?
Umeongezekwpa uzito kupita kiasi (umenenepeana)?
Uke unakuwa mkavu sana?
Unapata mzunguko wa hedhi bila mpangilio? Maumivu huwa makali na damu huwa nyingi au kidogo kuliko kawaida?
Kichwa kuuma mara kwa mara?
Unajisikia kuchokachoka?
Umeacha kutumia uzazi wa mpango (sindano vidonge) na sasa unataka ujauzito lakini hupati?
Unadhani changamoto hizi kubwa zinatokana na ubora mdogo wa dawa zinazotumika? Au hata katika nchi zilizoendelea changamoto hizi zipo?
Ni uzoefu wako binafsi, au umesikia, umeshuhudia?

Unadhani ni zipi njia sahihi za uzazi wa mpango ambazo mtu anaweza kutumia bila maudhi au kwa maudhi yanayovumilika?

Niambie!
Dr. Chris Cyrilo.
Nawasilisha!


Umefanya mazoezi leo? Au wewe ndio huyu mtu hapa? Vifo vya ghafla vinaongezeka kila siku kwa sababu ya ongezeko la marad...
20/01/2026

Umefanya mazoezi leo? Au wewe ndio huyu mtu hapa?
Vifo vya ghafla vinaongezeka kila siku kwa sababu ya ongezeko la maradhi yasioambukiza.

Kuna maradhi makuu mane yanayochangia idadi kubwa ya vifo duniani;
1. Maradhi ya mfumo wa mzunguko wa damu (maradhi ya moyo na mirija ya damu).
2. Maradhi ya Kansa
3. Maradhi ya Kisukari
4. Maradhi sugu ya mfumo wa upumuaji.

Vilevile kuna sababu kuu nne ambazo huchangia zaidi maradhi haya;
1. Vyakula/Mlo usiozingatia afya
2. Maisha bila mazoezi
3. Uvutaji wa Tumbaku
4. Matumizi mabaya ya Pombe.

Ukitazama sababu hizo nne utaona kila sababu moja inaweza kusababisha maradhi mawili au matatu pale juu. Zaidi ya vifo Milioni 40, ambavyo ni zaidi ya asilimia 70 ya vifo vyote kila mwaka, hutokana na maradhi yasioambukiza.

Miongoni mwa maradhi 10 yanayosababisha vifo vingi zaidi duniani, maradhi 7 ni maradhi yasioambukiza.
Lakini sababu kuu ni hizo zilizotajwa hapo juu ambazo zinaepukika.
1. Kuzingatia Milo wenye afya,
2. Kufanya mazoezi,
3. Kuacha kabisa matumizi ya Tumbaku
4. Kuacha au kunywa pombe kistaarabu.

Kipi unachoshindwa, kipi unachoshindwa kabisa? Kipi unajaribu, kipi unakiweza, kipi umefanikiwa kukiepuka?

Tambua pia mlo wenye afya ni suala linalohitaji ufahamu, zingatia ushauri wa mtaalamu anayetambulika, aliyethibitishwa.
Kwa upande wa mazoezi nako kuna changamoto, tunafanya mazoezi kuepuka maradhi kadhaa ikiwemo maradhi ya moyo, lakini wakati huohuo mazoezi yanaweza kusababisha hatari ikiwa mtu ana maradhi ya moyo bila kujitambua. Kumbe pamoja na yote ni muhimu kupima afya zetu mara kwa mara.

Nawasilisha
Dr. Chris Cyrilo.

Je! Mzee Butiku anaipenda Tanzania, lakini hawapendi Watanzania? Ukiwa na uwezo wa kusoma katikati ya mistari, juu ya ki...
20/01/2026

Je! Mzee Butiku anaipenda Tanzania, lakini hawapendi Watanzania?

Ukiwa na uwezo wa kusoma katikati ya mistari, juu ya kichwa cha habari na chini ya mstari wa mwisho wa habari, utaelewa ninapohoji endapo Mzee Butiku anaipenda Tanzania wakati hawapendi Watanzania!

Ni mmoja wa wazee wa Taifa, ameishi Ikulu, amekua Katibu wa Rais Nyerere kwa miaka mingi. Anaijua nchi, anaijua mifumo, na amekuwa mtetezi mzuri wa nchi na mifumo.

Kwenye kauli zake neno Watanzania halikosi, kuonesha namna anavyowafikiria Watanzania. Lkn kauli zake nyingine zinakufanya ujiulize kuhusu nia yake hasa ya kuwataja Watanzania.

Alisema nini baada ya hotuba ya Kapteni Tesha?
Alitoka na kupinga vikali jeshi kuingilia siasa. Lakini hakuwahi kutoka na kukemea Jeshi linapohusishwa na siasa kwa faida ya CCM.

Wanaokumbuka wakati wa mchakato wa Katiba Mpya, Mzee huyu alikuwa akimtetea sana Rais Kikwete hata baada ya Serikali ya Kikwete kuonekana inaharibu mchakato wa Katiba Mpya kwa makusudi. Yeye hakutaka kabisa Rais Kikwete aguswe. .

Mzee Warioba alibaki peke yake kusimamia maoni ya wananchi hadi akina Makonda wakamvamia na kumpiga. Baadae Makonda akapewa Ukuu wa Wilaya.

Mzee Butiku alikuwa na namna yake tofauti; watu wakikosoa mienendo ya serikali anawaunga mkono, lakini Rais akiguswa tu, anaanza kumtetea Rais.
Na hili limejitokeza pia awamu hii baada ya mauaji ya halaiki ya Oktoba 2025. Mzee Butiku ametoa hotuba yake na kuongea mengi, lakini kubwa ni pale anapotaka kumpamba Samia Suluhu. Anamuita Rais wetu, eti bado anafikiria yaliotokea. Anataka tuamini Samia Sulihu hahusiki na mauaji ya Watanzania.

Ewe Mzee Butiku!
HAIWEZEKANI kumuepusha Samia Suluhu na mauaji yale. HAIWEZEKANI.

Kwa kauli zake mwenyewe, kabla na baada ya mauaji, Samia Suluhu anahusika kwa namna moja au nyingine na mauaji ya maelfu ya Watanzania. Jaribio la Mzee Butiku za kutaka kumtoa Samia Suluhu kwenye uhusika wa mauaji, LIMESHINDWA.

Je! Inawezekana vipi kuipenda Tanzania, bila kuwapenda Watanzania? Kupinga matukio ya uhalifu yanayofanywa na dola dhidi ya Watanzania, na papo hapo kuwatetea kutetea viongozi wakuu wa hiyo dola kuna maana gani?

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha!

Address

Zip Code 00083
Dar Es Salaam

Telephone

+255713933736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Christopher Cyrilo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr. Christopher Cyrilo:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category