Dr. Christopher Cyrilo

Dr. Christopher Cyrilo Medical Doctor| Health Literacy expert | Social Activist | Writer
(1)

Shughuli nyingi za uchumi zinasimama kwa sababu kuna watu wamekataliwa ila wanalazimisha!
09/12/2025

Shughuli nyingi za uchumi zinasimama kwa sababu kuna watu wamekataliwa ila wanalazimisha!

Kwa mtu mwenye akili, Katiba yetu mbovu inatosha kumweka madarakani, sio lazima kuteka na kuua raia. Kwa mtu mwenye akil...
08/12/2025

Kwa mtu mwenye akili, Katiba yetu mbovu inatosha kumweka madarakani, sio lazima kuteka na kuua raia. Kwa mtu mwenye akili.

08/12/2025
Dini ya kweli ni UPENDO, UKWELI na HAKI. Bila kuzingatia hayo mambo matatu hakuna dini ni imani za kishetani.
08/12/2025

Dini ya kweli ni UPENDO, UKWELI na HAKI.
Bila kuzingatia hayo mambo matatu hakuna dini ni imani za kishetani.

Tunaongozwa na watu washamba na malimbukeni wa mali na madaraka.
05/12/2025

Tunaongozwa na watu washamba na malimbukeni wa mali na madaraka.

Kwa mujibu wa muongozo wa CIA uliopewa jina la 'CIA art of assassination' au sanaa ya mauaji ya kupanga ya CIA, mwanadam...
04/12/2025

Kwa mujibu wa muongozo wa CIA uliopewa jina la 'CIA art of assassination' au sanaa ya mauaji ya kupanga ya CIA, mwanadamu mwenye akili timamu anaweza kushawishiwa na kutumwa kutekeleza mauaji ya kupanga kwa sababu kuu tatu tu;

1. Dini
2. Siasa
3. Kisasi
Sababu hizi zinaweza kutumika pia katika kuchochea migogoro kwa pande hasimu, au kuchonganisha pande mbili zinazohasimiana.

Na endapo sababu hizi zitachanganywa pamoja, matokeo huwa hatari zaidi. Vyombo vya intelijensia vinapotaka kusajili wauaji, hutafuta wauaji kwa kutazama mambo hayo matatu. Mnaofuatilia mgogoro wa mashariki ya kati bila shaka mnafahamu sababu kuu ni mchanganyiko wa hayo mambo matatu chuki za kidini, kisiasa na visasi.

Tanzania ya leo ina watu wengi wenye roho za visasi kutokana na matukio ya kisiasa waliotendewa wao na/au ndugu, jamaa na marafiki zao. Sasa naona taratibu tunaanza kuingiza na dini. Haya mambo matatu; Siasa, Dini na Visasi yakikolea hakuna Mungu ataweza kufanya lolote - kwa sababu hali ikifikia hapo, kila mtu anabaki na Mungu wake.
Mungu atusaidie.

Shetani limeshika hatamu!
Shetani halishibi damu!

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.
--------------------------
Kitabu ni ISTILAHI ZA UHALIFU NA USALAMA kinapatikana popote Tanzania.
Kisomwe na watu wema.
0713933736

Kukiri kosa ni ushahidi wa moja kwa moja.
03/12/2025

Kukiri kosa ni ushahidi wa moja kwa moja.

Shetani tokaaa!
02/12/2025

Shetani tokaaa!

01/12/2025

ASKARI WALILAZIMISHA WATU WALIO HAI WAPELEKWE MOCHWARI!!

Anachokisema Father Kitima kimenikimbusha enzi nikiwa nafanya Intern Temeke Hospital, nikiwa zamu usiku, polisi walileta mtu amepigwa sana, amekatwa na vitu vyenye ncha kali kichwani na maeneo mengine. Alikuwa anavuja damu sana.

Nilitumia muda mrefu kumpa huduma yule jamaa, kumshona majeraha yote na kumtafutia damu ya kumuongezea.

Polisi mmoja akawa amekasirika anasema, 'Dokta mbona unamsaidia huyu kibaka k**a vile ni mtu mwema'.
Nikamwambia kwangu mimi ni mgonjwa, ukibaka wake ni huko sio hospitali. Yule askari akatulia.
Baada ya masaa machache yule jamaa alizinduka tukaanza kuongea, askari wakataka kumchukua waondoke naye, nikawaambia huyu analazwa kwa hali yake siwezi kumruhusu.
Lakini asubuhi nilipoondoka wakamchukua!

Kwa ufupi tumewapa wanyama silaha na sare za polisi tukawaita 'jeshi la polisi'.

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.

"Vijana wa Chama"
01/12/2025

"Vijana wa Chama"

Nauliza!
28/11/2025

Nauliza!

Yaani hata rafiki zako wa Burundi watakukataa...
28/11/2025

Yaani hata rafiki zako wa Burundi watakukataa...

Address

Zip Code 00083
Dar Es Salaam

Telephone

+255713933736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Christopher Cyrilo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr. Christopher Cyrilo:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category