Afya Maridhawa Tanzania

Afya Maridhawa Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afya Maridhawa Tanzania, Medical and health, Magomeni, Dar es Salaam.

_*Alikuwa na Tatizo la P.I.D Toka mwezi wa 3, Alitumia Dawa mbali Mbali Bila mafanikio.*_Akapewa namba Yetu na Rafiki ya...
17/10/2025

_*Alikuwa na Tatizo la P.I.D Toka mwezi wa 3, Alitumia Dawa mbali Mbali Bila mafanikio.*_

Akapewa namba Yetu na Rafiki yake, ambaye Mwka Jana tulimtinu Tatizo Kam Hilo. Tukaanza Dawa ya STD CARE. Kwa ajili ya kumaliza kabisa P.I.D SUGU

Amefanikiwa Kupiga Hatua za Mafanikio.

Hautoki n Uchafu Tena, Hn Maumivu katika tendo Wala Kiuno, nyonga n Tumbo Havimuumu.

Anamalizia Dawa ili kumaliza Tatizo na mizizi yake.

_*Kisa Hiki kinanifanya nione Nguvu Kubwa ya Shuhuda Halisi, zinazowafanya Marafiki kupeana namba. Shuhuda za Hivi zinanibariki Zaidi*🤓🤗_

DR LUTAMBI
0711556377

🌟 _*Mtoto Kucheza Tumboni Mambo 9 Ya Muhimu Kuyajua*_ 🌟____________________________🤰 Hali ya mtoto kucheza tumboni kwa m...
23/09/2025

🌟 _*Mtoto Kucheza Tumboni Mambo 9 Ya Muhimu Kuyajua*_ 🌟
____________________________

🤰 Hali ya mtoto kucheza tumboni kwa mjamzito (Quickening) ni hali ya mama mjamzito kuanza kuhisi mtoto akicheza tumboni kwa mara ya kwanza kabisa katika kipindi cha ujazito.
Huonekana kama miale midogo ✨, mapigo ❤️, au mpapaso hafifu.
Kwa kawaida hutokea kati ya wiki ya 16–20 📅, ingawa baadhi ya wanawake huweza kuhisi mapema au kuchelewa kidogo.

💞 Kuhisi harakati hizi huleta faraja kwa mama kuwa mtoto wake anaendelea kukua vizuri na pia huimarisha uhusiano wa kihisia kati ya mama na mtoto 👶.

🔹 _*1. Mtoto kucheza tumboni (Quickening) Utahisi vipi?*_ 🤔

Wanawake huelezea kama:
• 🦋 Kuruka kama kipepeo
• ✨ Mipapaso midogo
• 🎈 Maputo yanavyopasuka
• 🔄 Mizunguko midogo midogo tumboni au kujiviringisha
• ⚡ Mishtuko midogo ya misuli tumboni

Mwanzoni huweza kuchanganyikana na gesi 💨, lakini kadri wiki zinavyosonga, mama hutambua bayana harakati za mtoto wake.

🔹 _*2. Mtoto kucheza tumboni (Quickening) huanza lini?*_ ⏰

• Mtoto huanza kusogea kuanzia wiki ya 12, lakini mama hajahisi mapema.
• Kwa mimba ya kwanza 👩, kawaida huhisiwa wiki ya 18–20.
• Kwa waliowahi kupata mimba, huweza kuhisiwa mapema zaidi wiki ya 16–18.

Mambo yanayoathiri muda huu:
• Ikiwa ni mimba ya kwanza au sio 👩‍👦
• Mahali kondo la nyuma lilipojishikiza (placenta) 🌱
• Tabia ya mtoto (mtulivu au mchangamfu) 😊

🔹 _*3. Utahisi harakati Upande gani wa tumbo?*_ 🫄

Kwa kawaida chini ya kitovu ➡️ karibu na mfupa wa yonga au kinena.
Kadri mimba inavyokua, harakati huhama juu zaidi.

🔹 _*4. Ni mara ngapi unatakiwa kuhisi?*_ 🔢

• Wiki ya 20–24 mama huhisi mara kwa mara.
• Wiki ya 28+ 🤱, anatakiwa kuhisi angalau michezo 10 ndani ya masaa 2.

⚠️ Ukihisi chache au hakuna kabisa siku nzima, mjulishe daktari 🩺.

🔹 _*5. Kucheza hubadilika kuwa mateke (kicks) lini?*_ 🦶👊

Kipindi cha tatu cha ujauzito (Trimester 3) mtoto huanza kupiga miguu, ngumi, kujiviringisha na hata kucheua (hiccups).
Mama anaweza kuona mkao wa mtoto wake.
👉 Kupiga hesabu za miguu husaidia kufuatilia hali yake.

🔹 _*6. Kwa nini mtoto hujongea tumboni?*_ 🤱

Harakati husaidia ukuaji wa mifupa 🦴, misuli 💪 na viungo vya mtoto.
Kukosa harakati kabisa kunaweza kuashiria tatizo kwenye kondo la nyuma au maji ya uzazi 🌊.
⚠️ Ukiona hivyo, mjulishe daktari.

🔹 _*7. Je, mtoto kucheza kunaweza kutoweka kisha kurudi?*_ 🔄

Ndiyo ✅. Watoto hulala 😴 na kuamka ⏰.
Kwa hiyo ni kawaida kuhisi harakati zikapotea kidogo kisha kurudi.
Kadri zinavyokua nguvu, huwa thabiti zaidi.

🔹 _*8. Njia za kumchochea mtoto kucheza*_: 🎶🍹

• Kunywa kitu chenye utamu (juisi/matunda) 🍊🥭
• Kula chakula kizuri unachopenda 🍲
• Kutembea kidogo 🚶‍♀️
• Baba kumpapasa/shika tumbo 🤲
• Kusikiliza muziki mzuri 🎧
• Mama kuzungumza na mtoto 💬
• Kukaa kimya na kutulia 🧘‍♀️

🔹 _*9. Wakati gani wa kumpigia daktari*_: 📞🩺

• Baada ya wiki 28, hujahisi michezo 10 ndani ya masaa 2.
• Ikiwa harakati ghafla zimepungua au zimesimama kwa siku kadhaa 🚨.

❓_*Je, mtoto kucheza kunaleta maumivu?*_
❌ Hapana.
👉 Harakati hazipaswi kuleta maumivu.
⚠️ Ukihisi mikakamao au maumivu makali, mjulishe daktari.

_*Hitimisho*_
Kuhisi harakati za kwanza za mtoto tumboni ni hatua ya kusisimua zaidi 🤗.
Kwa kawaida hutokea wiki ya 16–20, lakini kila mimba ni tofauti.
Ikiwa una wasiwasi kuhusu harakati za mtoto wako, wasiliana na mtoa huduma wako wa afya 🩺 kwa uhakika.

Pata Msaada wa Dakitari WhatsApp.
0711556377

*Tatizo la Chango la Uzazi (Endometriosis): Sababu ya Maumivu Makali ya Hedhi kwa Wanawake Wengi**Je, umewahi kuumwa san...
18/09/2025

*Tatizo la Chango la Uzazi (Endometriosis): Sababu ya Maumivu Makali ya Hedhi kwa Wanawake Wengi*

*Je, umewahi kuumwa sana wakati wa hedhi kiasi cha kushindwa kufanya shughuli zako za kawaida? Unaweza kuwa unakabiliwa na changamoto ya kiafya inayoitwa *Endometriosis* au kwa lugha rahisi, *Chango la Uzazi*.*

*Endometriosis ni nini?*

Endometriosis ni hali ambapo tishu zinazofanana na zile za ndani ya mfuko wa kizazi (*endometrium*) hukua nje ya mfuko huo – mara nyingi kwenye ovari, mirija ya uzazi au hata kwenye viungo vya karibu kama kibofu na utumbo.

Tishu hizi zinapokua zimeotea mahali pasipostahili, huendelea kubadilika kila mwezi kama hedhi ya kawaida, lakini kwa kuwa damu zake kutokea Hazina pa kutokea, huleta maumivu makali, uvimbe na kuleta kovu (scar tissue) ndani ya tumbo la uzazi.

*Dalili za Endometriosis (Chango la Uzazi)*

✅ Maumivu makali sana wakati wa hedhi
✅ Maumivu ya tumbo chini ya kitovu kabla ya hedhi au baada ya hedhi
✅ Maumivu wakati wa tendo la ndoa
✅ Kutokwa na damu isiyo ya kawaida
✅ Ugumu wa kushika mimba (Ugumba).
✅ Kukojoa au kwenda haja kubwa kwa maumivu wakati wa hedhi

*Sababu Zinazoweza Kuchangia*

- Kurithi kutoka kwa mama au dada aliye na hali kama hiyo
- Mzunguko wa hedhi ulio mfupi sana
- Kutokwa na damu nyingi au hedhi ya siku nyingi
- Kuvuja damu ya hedhi nyuma badala ya kutoka nje (retrograde menstruation)
- Mfumo wa kinga kushindwa kuondoa tishu chafu zilizopo nje ya mfuko wa uzazi.

*Madhara Makubwa ya Endometriosis*

- Kukosa ujauzito au ugumba
- Kuvimba kwa viungo vya uzazi
- Maumivu ya kudumu ya nyonga na tumbo
- Msongo wa mawazo (depression) kwa sababu ya maumivu ya mara kwa mara.

*Je, Chango la Uzazi Hutibika?*

*Ndiyo!* Ingawa tiba ya hospitali mara nyingi ni kupunguza maumivu au upasuaji, *tiba asili* imethibitika kusaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa kabisa changamoto ya chango la uzazi.

Dawa za asili huondoa mzizi wa tatizo kwa:

✅ Kusafisha kizazi na mirija ya uzazi
✅ Kusaidia kurejesha mzunguko wa hedhi kuwa wa kawaida
✅ Kuondoa uvimbe na tishu zisizotakiwa
✅ Kurekebisha homoni za uzazi
✅ Kuondoa maumivu kabisa na kusaidia mwanamke kushika mimba

*Je Unahitaji Msaada w Tatizo Hili?*
Usiendelee kuteseka na maumivu ya kila mwezi. Endometriosis *inatibika kabisa* kwa kutumia *tiba asili salama na yenye ufanisi mkubwa.*

📞 *Tuma neno* *"CHANGO"* *kwenda WhatsApp*
*0711 556 377 – Dr Lutambi*
*Tiba salama. Matokeo ya uhakika. Hali hii itabaki kuwa historia!*

*✅ Sababu Kuu Zinazokwamisha Ushikaji wa Mimba — Ambazo Wanawake Wengi Hawazijui:*1. *Maambukizi Yasiyotibika Vizuri (PI...
18/09/2025

*✅ Sababu Kuu Zinazokwamisha Ushikaji wa Mimba — Ambazo Wanawake Wengi Hawazijui:*

1. *Maambukizi Yasiyotibika Vizuri (PID)*
- Maambukizi kwenye kizazi au mirija ya uzazi (Pelvic Inflammatory Disease) yanaweza kuziba mirija au kuharibu mfumo wa uzazi bila dalili za haraka.

2. *Mzunguko wa Hedhi Usioeleweka*
- Mzunguko ukibadilika-badilika huathiri siku za ovulation, hivyo ni vigumu kujua lini mimba inaweza kutungwa.

3. *Matatizo ya Homoni (Hormonal Imbalance)*
- Homoni zikiwa hazipo kwenye kiwango sahihi, mayai hushindwa kupevuka au kupasuka kwa wakati sahihi.

4. *Fibroids (Vimbe Kwenye Kizazi)*
- Huzuia mimba kutunga kwa kuathiri nafasi ya yai kujipandikiza au kuathiri mirija.

5. *Cysts (Vimbe za Maji kwenye Mayai)*
- Huzuia mayai kupevuka au kuachiliwa kabisa.

6. *Uchafu au Sumu Kwenye Mfuko wa Kizazi*
- Hutokea baada ya matumizi ya vidonge kwa muda mrefu, mimba kuharibika mara kwa mara, au maambukizi yasiyotibika.

7. *Uzito Kupita Kiasi au Kupungua Kupita Kiasi*
- BMI isiyo sawa huathiri uzalishaji wa homoni na ovulation.

8. *Msongo wa Mawazo (Stress)*
- Huathiri moja kwa moja mfumo wa homoni na uzazi bila kujua.

9. *Matumizi Mabaya ya Dawa za Uzazi wa Mpango*
- Husababisha kizazi kutokuwa tayari kwa mimba kwa miezi kadhaa baada ya kuacha.

10. *Ubora Mdogo wa Mbegu za Mume*
- Mimba haitatungwa kama mbegu ni chache, dhaifu au hazina kasi ya kutosha.

*Ushauri:*
Ushikaji wa mimba siyo tu suala la "kujaribu mara nyingi" bali kuelewa afya ya mfumo wako wa uzazi.

Ukiwa na changamoto, tafuta vipimo na ushauri wa kitaalamu mapema.
📞 *Mawasiliano kwa msaada zaidi:* *0711 556 377 - Dr Lutambi*

15/09/2025

I got over 20 reactions on one of my posts last week! Thanks everyone for your support! 🎉

_*VYAKULA 7 VINAVYOONGOZA KUHARIBU NGUVU ZA KIUME.*____________________________kuna *vyakula vya kisasa* vinavyoharibu a...
15/09/2025

_*VYAKULA 7 VINAVYOONGOZA KUHARIBU NGUVU ZA KIUME.*_
___________________________

kuna *vyakula vya kisasa* vinavyoharibu au kupunguza nguvu za kiume, hasa kwa kuvuruga homoni, kuathiri mzunguko wa damu au kusababisha uzito kupita kiasi. Hapa chini ni baadhi ya *vyakula vya kuepuka*:

*Vyakula vinavyoharibu nguvu za kiume:*

*1) Vyakula vyenye mafuta mengi (trans fats & saturated fats):*
- Chipsi, maandazi, vyakula vya kukaanga sana
- Fast food (burger, fried chicken)
- Hupunguza mzunguko wa damu na kuathiri mishipa ya uume

*2) Sukari nyingi:*
- Soda, keki, pipi, juisi zisizo asilia
- Sukari nyingi huongeza insulin na kupunguza testosterone

*3) Vyakula vya kusindikwa (processed foods):*
- Sausages, nyama ya makopo, biskuti
- Vina kemikali zinazopunguza uzalishaji wa homoni za kiume

*4) Pombe kupita kiasi:*
- Huzuia uzalishaji wa testosterone na kupunguza hamu ya tendo la ndoa

*5) Soya nyingi (hasa kwa wanaume):*
- Ina phytoestrogens, kemikali zinazofanana na homoni ya kike (estrogen), huathiri homoni za kiume

*6) Kafeini nyingi (kahawa kupita kiasi):*
- Inaweza kusababisha msongo na kushusha nguvu za mwili

*7) Soda za energy drinks (Red Bull, etc):*
- Hutoa nguvu ya muda mfupi lakini hushusha nguvu kwa muda mrefu.

Je Ungependa nikupe Pendekezo la Vyakula Bora Zaidi Ambavyo Unaweza kutumia Wewe Binafsi Ili kuwa Fit Zaidi.
Tuma Ujumbe _*VYAKULA BORA VYA MWANAUME*_ (BURE) Kwenda WhatsApp 0711556377

_*MAMBO 7 MUHIMU KUYAJUA KUHUSU TATIZO LA UGUMBA*_______________________________Ugumba ni Ile Hali ya Kushindwa kushika ...
15/09/2025

_*MAMBO 7 MUHIMU KUYAJUA KUHUSU TATIZO LA UGUMBA*_
______________________________
Ugumba ni Ile Hali ya Kushindwa kushika Ujauzito Richa ya Kushiriki tendo katika Siku za Hatari. Hii hali ni pale Wanandoa Wanapokaa kwenye ndoa Kwa Miezi 12 (Mwaka 1) au zaidi Bila Ujauzito.

_*Yafuatayo Ni Mambo 7 Unayopaswa kuyajua Kuhusu Ugumba Ambyo Yatabadilisha Mtazamo wako Kabisa. Haya Twende Pamoja.*_

_*[1]. Ugumba si tatizo la wanawake pekee Yao*_
______________________
Mara nyingi wanawake hudhaniwa kuwa wao pekee ndo chanzo cha ugumba, lakini siyo kweli.

Takriban asilimia 30-40 ya visa vya ugumba husababishwa na wanaume, asilimia nyingine ni wanawake, na zingine kutokana na sababu zisizojulikana au mchanganyiko wa sababu.

*[2].Sababu za ugumba ni nyingi*
______________________
Ugumba unaweza kusababishwa na matatizo Mengi kama vile:
▫️ Matatizo ya ovulation (kutotoa yai),
▫️Mirija ya uzazi iliyoziba,
▫️Ugonjwa wa P.I.D,
▫️Uvimbe kwenye kizazi (fibroids),
▫️ Hitilafu ya homoni (Hormonal Imbalance),
▫️Hali ya kiafya zama magonjwa kama kisukari au magonjwa ya tezi za thyroid,
▫️Pamoja na mtindo wa maisha kama uzito uliopitiliza au kuwa mwembamba kupita kiasi.

*[3]. Umri una athari kubwa kwenye uzazi*
______________________
Uwezo wa kushika mimba hupungua kadri mwanamke anavyozeeka, hasa baada ya miaka 35.

Kwa wanaume pia ubora wa shahawa hupungua taratibu na kuathiri uwezo wa kumpa mimba Mwanamke.

*[4].Dalili za ugumba si rahisi kuzitambua mara moja*
______________________
Ugumba mara nyingi hauna dalili wazi, isipokuwa pale ambapo mtu anajaribu kupata mtoto bila mafanikio kwa mwaka mzima (au miezi 6 kwa wenye zaidi ya miaka 35). Huyo Anaonekana ni mgumba.

*[5].Matibabu ya ugumba yapo na yanategemea chanzo Chake*
______________________
Kuna matibabu ya dawa, upasuaji, na teknolojia ya kisasa kama IVF, IUI n.k.
▫️Pia tiba mbadala Pamoja na lishe bora,
▫️Mitindo sahihi ya maisha, na dawa asilia husaidia kwa baadhi ya watu.

*[6].Mtindo wa maisha una mchango mkubwa Kufanya Tatizo Litokee*
______________________
Mmbo kama Msongo wa mawazo, kutopata usingizi wa kutosha, matumizi ya pombe, sigara na madawa ya kulevya, au ulaji duni vinaweza kuathiri uwezo wa kuzaa kwa Pande zote mbili Kwa wanaume na wanawake.

*[7].Ugumba unaweza kuzuilika au kudhibitiwa mapema*
______________________
Mambo Muhimu yanayoweza Kudhibiti Kutokea kwa Ugumba.
▫️Kufanya vipimo vya afya ya uzazi mapema,
▫️kudhibiti magonjwa sugu,
▫️kula lishe bora,
▫️kufanya mazoezi, na
▫️kuepuka mimba za utotoni au,
▫️kuharibika mimba mara kwa mara kunaweza kusaidia kuepuka na ugumba.

Je Ungependa Kupata Mwongozo Zaidi Kuhusu Vipimo unavyopaswa Kufanya na Jinsi Gani Unaweza Kushika Mimba Kwa Haraka Zaidi. Wasiliana Nami _*INBOX 📥 KWA KUBOFYA LINK HAPA*_ 👉👉👉https://wa.me/message/342RRPB6UFETA1

*DR LUTAMBI*
0711556377
0745889503

*Ugumu wa Kushika Mimba Unaotokana na Mvurugiko wa Homoni*Homoni ndizo zinazoongoza mzunguko wa hedhi na uwezo wa mwanam...
15/09/2025

*Ugumu wa Kushika Mimba Unaotokana na Mvurugiko wa Homoni*

Homoni ndizo zinazoongoza mzunguko wa hedhi na uwezo wa mwanamke kushika mimba.

Zinapovurugika, mwili hupoteza mpangilio wa kawaida, na kusababisha ugumu wa kupata ujauzito.

*Jinsi Mvurugiko wa Homoni Unavyoathiri Uzazi*

1. Ovulation kuharibika – mayai hayaachiwi (hayiwi na ovulation), hivyo hakuna yai la kurutubishwa.

2. Mzunguko wa hedhi kuvurugika – hedhi kuwa fupi sana, ndefu sana au kutopatikana kabisa.

3. Ubora wa yai kushuka – homoni zikiwa hazipo sawa, mayai yanayokomaa hayawi imara kwa urutubishaji.

4. Uterine lining isiyo imara – homoni zinapokuwa chache au nyingi, ukuta wa mfuko wa uzazi hauwi tayari kupokea mimba.

5. Shida ya homoni ya projesteroni – ambayo ni muhimu sana katika kudumisha ujauzito wa mwanzo.

*Dalili Zinazoashiria Kuna Mvurugiko wa Homoni*

Hedhi isiyo na mpangilio (huchelewa, huja mara mbili, au haiji kabisa).

Maumivu makali au kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi.

Chunusi nyingi au mafuta kupita kiasi usoni.

Kuongezeka au kupungua ghafla uzito bila sababu.

Unywele mwingi usiokuwa wa kawaida (hasa usoni, kifuani).

Mabadiliko ya hisia (mood swings, msongo, hasira).

*Sababu Kuu za Mvurugiko wa Homoni*

PCOS (Polycystic Ovary Syndrome)

Uzito kupita kiasi au kupungua sana

Msongo wa mawazo (stress)

Matatizo ya tezi (thyroid disorders)

Matumizi ya baadhi ya dawa

Kuzeeka kwa mayai (ovarian aging)

*Ushauri kwa Mwanamke*
Kuangalia uzito na kudumisha lishe bora.

Kupunguza msongo wa mawazo.

Kufanya mazoezi mara kwa mara.

Kupima homoni na ushauri wa kitaalamu mapema (FSH, LH, Prolactin, Thyroid, n.k.).

Matibabu ya homoni au tiba asilia hutolewa kulingana na chanzo.

👉 Hivyo, mvurugiko wa homoni ni sababu kubwa ya ugumba (infertility) kwa wanawake, lakini unaweza kutibika iwapo utagunduliwa mapema na kupata ushauri wa kitaalamu.

🫀 _*Sababu Kuu za Shinikizo la Juu la Damu (Hypertension) na Jinsi ya Kujikinga*_____________________________*1. Sababu ...
01/09/2025

🫀 _*Sababu Kuu za Shinikizo la Juu la Damu (Hypertension) na Jinsi ya Kujikinga*_
___________________________
_*1. Sababu Kuu Zinazochangia Hypertension*_
Kuna mambo mbalimbali yanayoweza kuongeza hatari ya kupata shinikizo la juu la damu, ikiwemo:

🔸 *Urithi (Genetics):* Ikiwa kuna historia katika familia, uwezekano huongezeka Zaidi.

🔸 *Kuwa na Umri mkubwa*: Kadri mtu anavyozeeka, mishipa ya damu hupoteza unyumbufu na kusababisha presha kupanda.

🔸 *Unene/uzito mkubwa:* Uzito huongeza kazi ya moyo na kubana mishipa ya damu.

🔸 *Lishe isiyo bora:* Ulaji wa chumvi nyingi, vyakula vya mafuta na sukari nyingi huongeza hatari mara Dufu Zaidi.

🔸 *Kutofanya mazoezi:* Ukosefu wa shughuli za mwili hupunguza uimara wa moyo na mishipa ya damu.

🔸 *Uvutaji wa sigara na pombe:* Huathiri mishipa ya damu na kuongeza shinikizo.

🔸 *Msongo wa mawazo (Stress)*: Unachochea homoni zinazoinua shinikizo la damu kupanda juu Zaidi.

🔸 *Uwepo wa Magonjwa mengine:* Magonjwa kama Kisukari, magonjwa ya figo, na matatizo ya homoni Pia Huchochea presha kupanda.

_*2. Namna ya Kujikinga na Kudhibiti Presha*_

_Habari njema ni kwamba hypertension inaweza kuzuilika au kudhibitiwa kwa hatua sahihi za kila siku:_

✅ Punguza chumvi kwenye chakula (tumia chini ya kijiko 1 kwa siku).

✅ Kula mboga na matunda kwa wingi pamoja na nafaka zisizokobolewa.

✅ Fanya mazoezi angalau dakika 30 kila siku (kutembea, kuogelea, kuruka kamba, nk).

✅ Dhibiti uzito kwa kula kwa mpangilio na kudumisha uwiano wa mwili.

✅ Epuka pombe na sigara kabisa.

✅ Punguza msongo wa mawazo kwa mapumziko, ibada, na mbinu za kupumzika.

✅ Pima presha mara kwa mara hata kama hujisikii vibaya.

✅ Tumia dawa kwa usahihi endapo umeandikiwa na daktari – Usitumie Bila Ushauri, Wala usiache bila ushauri.

Hypertension Ukiwa ni ugonjwa wa muda mrefu unaoweza kusababisha madhara makubwa, lakini kwa mtindo bora wa maisha na ufuatiliaji wa kiafya, unaweza kuishi maisha marefu na yenye afya.

📌 *Ushauri:* Anza leo kupima shinikizo lako la damu, fanya mabadiliko kwenye lishe na mtindo wa maisha, na uelimisha familia yako kuhusu ugonjwa huu unaoua kimya “kimya”.

Pata Msaada wa Kidakitari Kwa Kupiga Simu au Whatsapp 0711556377

🫀 _*Ugonjwa wa Shinikizo la Juu la Damu (Hypertension)*______________________________*1. Shinikizo la Juu Ni Ugonjwa gan...
01/09/2025

🫀 _*Ugonjwa wa Shinikizo la Juu la Damu (Hypertension)*_
____________________________

_*1. Shinikizo la Juu Ni Ugonjwa gani?*_

Shinikizo la juu la damu (Hypertension) ni hali ambapo nguvu ya damu inayosukumwa kwenye mishipa ya damu inakuwa kubwa zaidi kuliko kawaida, na Hali hiyo inaendelea kwa muda mrefu.

Hali hii huongeza kazi ya moyo na kuathiri mishipa ya damu, jambo linaloweza kusababisha madhara makubwa kiafya kama vile kiharusi (Stroke), mshtuko wa moyo (Heart Attack), kushindwa kwa figo (Kidney Failure ) na hata kifo cha ghafla.

Kwa kawaida, mtu husemekana ana presha ya juu endapo vipimo vinaonyesha wastani zaidi ya:

▫️Systolic Ikiwa Zaidi ya: ≥ 140 mmHg

▫️Diastolic Ikiwa Zaidi ya: ≥ 90 mmHg

_*2. Tatizo Hili Linabainikaje?*_

Hypertension ni ugonjwa unaoua kimya Kimya(silent killer) kwa sababu mara nyingi Huwa haina dalili za wazi z Moja kw mona.

Njia kuu ya kubaini ni kwa kupima shinikizo la damu mara kwa mara.

_*Njia Hizi zitakusaidia kubaini Tatizo*_:
✅ Kupimwa na kifaa cha “BP machine” (sphygmomanometer).
✅ Kufanya Vipimo vya mara kwa mara hospitalini au nyumbani.
✅ Uchunguzi wa kiafya kwa mtu aliye na dalili au mwenye historia ya familia yake kuwa na hypertension.

_*Dalili zinazoweza kujitokeza (kwa baadhi ya watu):*_
▫️Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara.
▫️Kizunguzungu.
▫️Kuona ukungu au madoa machoni.
▫️Mapigo ya moyo kwenda kasi.
▫️Uchovu usioelezeka.

_*Zingatia Kuwa:*_ Shinikizo la juu la damu ni ugonjwa hatari lakini unaweza kudhibitiwa kwa njia rahisi Zikiwemo:

▫️Kupima mara kwa mara.
▫️Kufuata ushauri wa daktari.
▫️Kufanya mabadiliko ya mtindo wa maisha (lishe bora, mazoezi, kuepuka uvutaji na pombe).

📌 *Kumbuka*: Hypertension haichagui umri – kila mtu yupo kwenye hatari, hivyo pima shinikizo lako la damu mara kwa mara hata kama hujisikii vibaya.

Pata Msaada na Ushauri Zaidi wa Kidakitari 0711556377 DR LUTAMBI Dar es salaam, Tanzania

*Yajue Matatizo 6 ya Mbegu za Kiume yanayoweza Kuwafanya Wanaume kushindwa Kutungisha mimba.*___________________________...
27/08/2025

*Yajue Matatizo 6 ya Mbegu za Kiume yanayoweza Kuwafanya Wanaume kushindwa Kutungisha mimba.*
___________________________
Haya hapa ni matatizo 6 ya mbegu za kiume yanayoweza kumfanya mwanaume ashindwe kutungisha mimba:

1. *Oligospermia* – Idadi ndogo ya mbegu za kiume kuliko kawaida (chini ya milioni 15/ml). Hii hupunguza nafasi ya mbegu kufika kwa yai.

2. *Azoospermia* – Kutokuwa na mbegu kabisa kwenye shahawa. Hali hii huondoa kabisa uwezekano wa kumpa mwanamke mimba bila msaada wa tiba maalum.

3. *Asthenozoospermia* – Mbegu za kiume kutokuwa na kasi au nguvu ya kutosha kusafiri hadi kufikia yai la mwanamke.

4. *Teratozoospermia* – Umbile la mbegu kuwa na kasoro (mfano: kichwa au mkia kuwa na sura isiyo ya kawaida), jambo linalozuia kupenya yai.

5. *Kuwahi kufika kileleni sana (PE)* – Hii huzuia shahawa kufika kwa wakati mzuri wa kutungisha mimba.

6. *Maambukizi kwenye mfumo wa uzazi* – Maambukizi kwenye korodani au njia ya mbegu yanaweza kuathiri uzalishaji au usafirishaji wa mbegu.

Ukiwa na Shida Yoyote Kati Ya Hizo Usijikatie Tamaa Tupo Kwa Ajili ya kukusaidia, uweze kutungisha mimba kama kawaida.
Tuma ujumbe Whatsapp 0711556377

Address

Magomeni
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Maridhawa Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram