Bupe Books, Counselling & Training Services

Bupe Books, Counselling & Training Services Discussions of pyschosocial issues on physical, emotional, cognitive, social and spiritual issues especially relationships on personal and Interpersonal.

10/09/2022

OPEN DISCUSSION 12
1.Ni kweli kwamba ukiwa mke uliyeolewa, maombi yako kwa Mungu yanasikiwa kuliko wanawake wengine?
2. Je kuna wanawake ambao hawajaolewa, wengine wachepukaji nao maombi yao yanasikiwa na Mungu?
3.Je mwanamke mchepuko anaweza fanikiwa kifedha au kwenye maeneo mengine?Je mafanikio yake yanayoka kwa Mungu ama kwa shetani?
4.Je ni lazima mchepuko akutwe na mabaya???Mnaita Karma?

Mihemko pole pole.....
Jadili hoja na ushahidi na maandiko!

Ministering in one of the colleges in Arusha!
10/05/2019

Ministering in one of the colleges in Arusha!

03/12/2018

There are men who rather than marrying a girl who has a child, they better marry the one who had aborted many times!

Get your copy in exchange with money!
12/06/2018

Get your copy in exchange with money!

17/06/2017

Epuka kupima upendo wa mwenzi wako kwa mambo ya kufanyiana kwenye mitandao ya kijamii. Ni bora awe mwenza mwema nyumbani, hata akiwa passive mtandaoni, kuliko akawa active mtandaoni, akachemka nyumbani. Mitandao ya kijamii ni zaidi ya mahusiano yenu! Akiweza vyote, then ya pili itakuwa ni added advantage, siyo basic.
Kufurahi ni Kuchagua!

23/02/2017

Mume kutoa affection kwa mke ni lazima.
Tuendelee na mada yetu ya mume kutoa affection kwa mke. Kwa posts za huko nyuma, imeshajadiliwa kuwa affection ni nini na inakuwaje. Ni ukweli ulio wazi, kuwa mume ameamua kuoa, basi affection ni lazima ni wajibu wake wa msingi k**a ilivyo kwenye kutoa mahitaji na tendo la ndoa. Ila ni ukweli usiopingika kuwa kuna wanaume wengi wamefanikiwa katika meeengi na wakafeli kwenye hili, wakiwemo waliokoka, watumishi na majina yao makubwa makubwa kabisa, na maafisa na vyeo vyao vikubwa vikubwa kabisa.
Kwa post iliyopita ilijadiliwa baadhi ya sababu zinazowafanya wanaume walio wengi kufeli kwenye affection.Je mke ufanyaje?
1. Ni busara, na hekima na muhimu kumjua mumeo. Ni vizuri kumjua kuwa kwenye maisha ya kawaida anaweza nini zaidi, anashindwa nini zaidi, anapenda nini zaidi na anachukia nini zaidi, ( Irene Mbowe anasemaga kutoa alama sijui) na kwa uhalisia jizoeshe kuishi na kufurahia yale anayoweza zaidi, na potezea yale asiyoweza.
2. Jifunze kutafsiri lugha yake ya affection. Hili ,linaweza lisiwe zoezi jepesi, maana hata yeye anaweza asiseme au asijue. Ila kila mwanaume anapooa anakuwa na ndoto zake kichwani, kuwa yeye kumpenda mke ni kufanyaje na kumuonyesha anampenda ni kufanyaje. Badala ya kulazimisha afanye k**a wale wa kwenye movie, soma lugha yake. Kuna mwingine anasimulia zaidi nje, kuliko kukwambia wewe, kuna mwingine akiandika message atasema nakupenda, ila kusema na mdomo anapata ganzi, kuna mwingine akihudumia familia ndio anaona amekuwa affectionate, huwezi kulazimisha awe asivyo, au afanye asivyoweza au asivyotaka, kwa muda huo shukuru na uendelee kuridhika.
3. Fanya sehemu yako bila kujalisha yeye anafanya au hafanyi. Huko duniani, kuna wanawake wengi utasikia, asipoleta mboga, namuwekea ugali na chumvi, wazungu wanakwambia ''two wrongs do not make one correct thing". Kosa lako haliwi halali kwasababu wa kwanza kakukosea. Wewe tenda wema, jifunze kwa Paulo aliyemquote Yesu, ''ni heri kutoa kuliko kupokea''.
4. Usipimie thamani yako kwa jinsi mume anavyokutendea. Hutakaa uwe na furaha, na Kibo na Mawenzi utavisikia kwa watalii. Amini kuwa thamani yako haiongezeki kwa jinsi watu wanavyokutendea, bali inabaki vile unavyoitengeneza wewe kwa msaada wa Mungu. Ukitupa elf kumi chini na kuikanyaga, thamani yake inabaki kuwa elf kumi. Hivyo na wewe, upate affection usipate, upate kwa uchache au kwa wingi, unabaki kuwa ni wewe, na furaha haiongezeki au kupungua k**a wewe mwenyewe usipoiruhusu.
Happiness is a choice

23/02/2017

Mume kutoa affection kwa mke ni lazima.
Tuendelee na mada yetu ya mume kutoa affection kwa mke. Kwa posts za huko nyuma, imeshajadiliwa kuwa affection ni nini na inakuwaje. Ni ukweli ulio wazi, kuwa mume ameamua kuoa, basi affection ni lazima ni wajibu wake wa msingi k**a ilivyo kwenye kutoa mahitaji na tendo la ndoa. Ila ni ukweli usiopingika kuwa kuna wanaume wengi wamefanikiwa katika meeengi na wakafeli kwenye hili, wakiwemo waliokoka, watumishi na majina yao makubwa makubwa kabisa, na maafisa na vyeo vyao vikubwa vikubwa kabisa.
Kwa post iliyopita ilijadiliwa baadhi ya sababu zinazowafanya wanaume walio wengi kufeli kwenye affection.Je mke ufanyaje?
1. Ni busara, na hekima na muhimu kumjua mumeo. Ni vizuri kumjua kuwa kwenye maisha ya kawaida anaweza nini zaidi, anashindwa nini zaidi, anapenda nini zaidi na anachukia nini zaidi, ( Irene Mbowe anasemaga kutoa alama sijui) na kwa uhalisia jizoeshe kuishi na kufurahia yale anayoweza zaidi, na potezea yale asiyoweza.
2. Jifunze kutafsiri lugha yake ya affection. Hili ,linaweza lisiwe zoezi jepesi, maana hata yeye anaweza asiseme au asijue. Ila kila mwanaume anapooa anakuwa na ndoto zake kichwani, kuwa yeye kumpenda mke ni kufanyaje na kumuonyesha anampenda ni kufanyaje. Badala ya kulazimisha afanye k**a wale wa kwenye movie, soma lugha yake. Kuna mwingine anasimulia zaidi nje, kuliko kukwambia wewe, kuna mwingine akiandika message atasema nakupenda, ila kusema na mdomo anapata ganzi, kuna mwingine akihudumia familia ndio anaona amekuwa affectionate, huwezi kulazimisha awe asivyo, au afanye asivyoweza au asivyotaka, kwa muda huo shukuru na uendelee kuridhika.
3. Fanya sehemu yako bila kujalisha yeye anafanya au hafanyi. Huko duniani, kuna wanawake wengi utasikia, asipoleta mboga, namuwekea ugali na chumvi, wazungu wanakwambia ''two wrongs do not make one correct thing". Kosa lako haliwi halali kwasababu wa kwanza kakukosea. Wewe tenda wema, jifunze kwa Paulo aliyemquote Yesu, ''ni heri kutoa kuliko kupokea''.
4. Usipimie thamani yako kwa jinsi mume anavyokutendea. Hutakaa uwe na furaha, na Kibo na Mawenzi utavisikia kwa watalii. Amini kuwa thamani yako haiongezeki kwa jinsi watu wanavyokutendea, bali inabaki vile unavyoitengeneza wewe kwa msaada wa Mungu. Ukitupa elf kumi chini na kuikanyaga, thamani yake inabaki kuwa elf kumi. Hivyo na wewe, upate affection usipate, upate kwa uchache au kwa wingi, unabaki kuwa ni wewe, na furaha haiongezeki au kupungua k**a wewe mwenyewe usipoiruhusu. Mwisho.
Happiness is a choice

04/01/2017

MAHUSIANO YENYE AFYA YATAHUSISHA MTU FULL 1
Ukitaka kwa namna yoyote kuishi mahusiano yenye afya, hakikisha unahusisha wewe mzima mzima! Mwanadamu ameumbwa na mwili, akili na roho. Na kila kimoja kina umuhimu sawa na kingine, hivyo kupuuza kimojawapo, au kuzidisha kimojawapo utapata changamoto za mahusiano. Hakikisha you are a balanced being! Hakikisha kila sehemu ya wewe inakaa sawa na kukaba nafasi yake, vyema!

31/10/2016

Life is all about choices!What you choose, is what you become!

Address

Mbezi Msigani Tanesco
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bupe Books, Counselling & Training Services posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram