MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

06/12/2025

Je unafahamu kwa nini hufanyika oparesheni za marejeo ya nyonga na magoti?

Shilekirwa Makira, Daktari Bingwa Mbobezi wa upasuaji wa nyonga na magoti kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila anaeleza kwa undani zaidi.

06/12/2025

MUHIMBILI -MLOGANZILA YAWAFANYIA UPASUAJI WA NYONGA NA MAGOTI WAGONJWA 350.

MUHIMBILI -MLOGANZILA YAWAFANYIA UPASUAJI WA NYONGA NA MAGOTI WAGONJWA 350.Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila ndan...
06/12/2025

MUHIMBILI -MLOGANZILA YAWAFANYIA UPASUAJI WA NYONGA NA MAGOTI WAGONJWA 350.

Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila ndani ya kipindi cha miaka miwili imefanikiwa kuwafanyia upasuaji wagonjwa 350 wenye changamoto ya nyonga na magoti.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji MNH, Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Pasuaji MNH Mloganzila Dkt. Godlove Mfuko amesema Serikali ya Awamu ya Sita imefanya uwekezaji mkubwa
katika sekta ya afya ikiwemo manunuzi ya vifaa tiba, kusomesha wataalam hivyo ni wajibu wetu k**a wataalam kufanya kila linalowezekana kuanzisha huduma mpya ambazo zitawafanya watu wa ndani na nje ya nchi kuja kupata huduma hivyo kukuza utalii
tiba.

Ameongeza kuwa kutokana na ongezeko la wagonjwa wenye changamoto ya nyonga na magoti hospitali hiyo inaona wagonjwa wa kliniki wastani wa 100-150 kwa wiki na kwa hivi sasa idara hiyo inauwezo wa kuwafanyia upasuaji wagonjwa 10-15 kwa siku.

Kwa upande Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Mifupa aliyobobea katika Upasuaji wa Nyonga na Magoti Shilekirwa Makira, amesema kwa sasa Kuna Madaktari Bingwa na Bingwa Bobezi wenye uzoefu wa kutosha katika upasuaji wa nyonga na magoti na kufanya idara hiyo kuwa kitovu cha umahiri wa huduma za upasuaji wa nyonga na magoti ndani na nje ya nchi.

05/12/2025

Je! Unafahamu visababishi vya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa?

Ungana na Biton Kigunga, Mfamasia kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila kwa ufafanuzi zaidi.

WAFANYAKAZI MUHIMBILI -MLOGANZILA WASHAURIWA KUTAMBUA UMUHIMU WA KUJIUNGA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI.Wafanyakazi wa Hospit...
05/12/2025

WAFANYAKAZI MUHIMBILI -MLOGANZILA WASHAURIWA KUTAMBUA UMUHIMU WA KUJIUNGA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI.

Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila wameshauriwa kutambua umuhimu wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi kulingana na taaluma au kada zao ili vyama hivyo kuwa daraja zuri baina ya mwajiri na mwajiriwa ambapo itarahisisha mawasiliano na kuongeza utendaji mzuri wa kazi.

Akizungumza katika kikao cha mwaka cha Chama cha Madaktari na Wafamasia, Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali watu na Utawala, Bw. Abdallah Kiwanga ametaja faida mbalimbali za kuwa mwanachama wa chama cha wafanyakazi kuwa ni pamoja na kulinda usalama kwa mfanyakazi, kupata jukwaa la kusemea kero za mfanyakazi, kuboresha mahusiano, ushirikishwaji katika mambo mbalimbali na kumsaidia mwajiri kutochukua maamuzi akiwa peke yake.

Ameongeza kuwa kila mwanachama wa chama cha wafanyakazi anatakawi kutambua wajibu wake k**a kuzingatia sheria na katiba, kushiriki katika shughuli za chama, kusemea, kutetea na kutangaza chama, kuhamisha wafanyakazi kutoa michango na kuhamasisha wafanyakazi kujiunga na chama.

Kikao hicho kimeambatana na uchaguzi ili kupata viongozi wapya wa muhula ujao ili kuendelea kutimiza majukumu ya chama chao.

04/12/2025

*Katika kuendelea kuboresha huduma ya mama na mtoto, Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila imeanzisha mafunzo maalum kwa wataalam wa afya kuhusu afya ya akili kwa mama mjamzito wakati na baada ya kujifungua.*

Kwa undani wa hili, ungana na Deodatus Fintien, Mkunga Mbobezi kutoka Muhimbili -Mloganzila.

03/12/2025

“Nilipata changamoto ya shinikizo la damu wakati wa ujauzito , nilifikishwa hospitalini hapa nikapatiwa huduma kwa wakati, ninawashukuru wataalam wote wa afya kwa huduma nzuri”

Bi Doreen Nicholous
Shuhuda wa huduma Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila.

   MITANDAO YETU YA KIJAMII ILI KUPATA TAARIFA MBALI MBALI KUHUSU HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA #
03/12/2025

MITANDAO YETU YA KIJAMII ILI KUPATA TAARIFA MBALI MBALI KUHUSU HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA #

02/12/2025

“Njooni Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila mpate mafunzo mbalimbali ikiwemo afya ya akili kwa mama kipindi akiwa mjamzito”.

Evodia Mlawa,Muuguzi mnufaika wa mafunzo kutoka Hospitali ya Tosa Maganga Iringa.

01/12/2025

Je unafahamu mambo ya muhimu ya kuzingatia kwa mwenza mwenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi anayeishi na mwenza asiye na maambukizi ili asipate maambukizi?

Ungana na Happiness Mollel, Afisa Muuguzi kwa undani zaidi.

MUHIMBILI -MLOGANZILA YAANZA  KAMBI MAALUM YA UPANDIKIZAJI NYONGA NA MAGOTI Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila ime...
01/12/2025

MUHIMBILI -MLOGANZILA YAANZA KAMBI MAALUM YA UPANDIKIZAJI NYONGA NA MAGOTI

Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila imeanza kambi maalum ya upandikizaji wa nyonga na magoti kwa wagonjwa wenye changamoto ya maradhi ya nyonga na magoti ambapo kambi hiyo inafanyika kwa kushirikiana na Daktari Bingwa Mbobezi wa upandikizaji wa nyonga na magoti Prof. Mamoun Gadir kutoka Hospitali ya Queen Elizabeth ya nchini Uingereza.

Kambi hiyo itafanyika kwa siku tano kuanzia Desemba 1 hadi 5, 2025, hivyo watakaonufaika na kambi hiyo ni wagonjwa wa nyonga na magoti yaliyosagika yenye maumivu makali, na wale ambao baada ya kupandikizwa awamu zilizopita na nyonga hizo kusagika tena.

Matibabu hayo ni mwendelezo wa kutekeleza mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kuwa huduma za kibingwa na kibobezi zinapatikana hapa nchini ili kuwapunguzia usumbufu wananchi wa kutafuta matibabu hayo nje ya nchi. @

29/11/2025

Je unayafahamu magonjwa ya mwendo wa ghafla usiodhibitika?

Ungana na Kigocha Okeng’o Daktari Bingwa wa Ubongo, Uti wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu kwa undani zaidi.

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram