MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

28/10/2025

“Kutokana na uboreshaji wa miundombinu ya kutolea huduma, Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imefanikiwa kuanzisha huduma ya watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi ambapo zaidi ya watoto 450 wamehudumiwa na kufanyiwa upasuaji.

Dkt Godlove Mfuko
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Upasuaji
MNH-Mloganzila

28/10/2025

WAZIRI GWAJIMA APONGEZA UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA MUHIMBILI-MLOGANZILA.Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wanawake ...
28/10/2025

WAZIRI GWAJIMA APONGEZA UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA MUHIMBILI-MLOGANZILA.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Mh. Dkt. Dorothy Gwajima ametembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa lengo la kuwajulia hali wagonjwa ambapo pia amepata fursa ya kuzungumza na uongozi wa hospitali hiyo na kupongeza juhudi kubwa zinazofanywa na menejimenti katika kuhakikisha hospitali inaendelea kutoa huduma bora za ubingwa bobezi za afya kwa wananchi.

Dkt. Gwajima amesema ubora wa huduma zinazotolewa na hospitali hiyo unatokana na uwekezaji mkubwa wa vifaa tiba, wataalam na miundombinu wezeshi uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

28/10/2025

“Namshukuru sana rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan na serikali yake ya awamu ya sita kwa kugharamikia huduma zote za matibabu za mwanangu. Kwa sasa mwanangu ni mzima na ataendelea na masomo yake”.

Emilia Nduguru
Shuhuda wa huduma
Mkazi wa songea.

27/10/2025

“Huduma za ICU kwa watoto wachanga zimeendelea kuboreshwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, hivyo tunaweza kuhudumia watoto wachanga 60 mahututi kwa wakati mmoja”

24/10/2025

“Upatikanaji wa dawa haukuwa na changamoto kwa upande wangu, dawa zote zilizohitajika mtoto alipewa kwa wakati na watoa huduma walikuwa na mimi bega kwa bega”

Bi.Yuditha Kidava
Shuhuda wa huduma
Mkazi wa Morogoro.

23/10/2025

Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila imefanikiwa kuanzisha na kuboresha huduma mbalimbali za Ubingwa na Ubingwa Bobezi sambamba na kufanya ukarabati wa miundo mbinu ya kutolea huduma.

Haya yote yamefanyika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi thabiti wa Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

SEKTA YA AFYA #

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram