MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

KAMBI MAALUM YA KUTENGENEZA NA KUREKEBISHA MISHIPA YA KUCHUJA DAMU, YAANZA RASMI MUHIMBILI MLOGANZILA.Hospitali ya Taifa...
15/02/2026

KAMBI MAALUM YA KUTENGENEZA NA KUREKEBISHA MISHIPA YA KUCHUJA DAMU, YAANZA RASMI MUHIMBILI MLOGANZILA.

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeanza kambi maalum ya kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu (Arterio-Venous Fistula Creation) kwa wagonjwa wenye changamoto za figo, kambi hiyo inafanywa na wataalam wa Muhimbili -Mloganzila kwa kushirikiana na jopo la wataalam kutoka Korea Kusini inatarajia kuhitimishwa tarehe 18 Februari 2026 ambazo takribani wagonjwa 50 watanufaika na huduma hiyo.

31 WAJITOKEZA KUCHANGIA DAMU MUHIMBILI–MLOGANZILAKatika  kuadhimisha ya Siku ya Wapendanao Duniani, Hospitali ya Taifa M...
14/02/2026

31 WAJITOKEZA KUCHANGIA DAMU MUHIMBILI–MLOGANZILA

Katika kuadhimisha ya Siku ya Wapendanao Duniani, Hospitali ya Taifa Muhimbili – Mloganzila imeendesha zoezi la uchangiaji damu kwa wafanyakazi wa Shule ya Msingi Hanester iliyopo Kibamba, Dar es Salaam na kufanikiwa kukusanya chupa 31 za damu.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mkuu wa Kitengo cha Damu Salama MNH–Mloganzila, Bw. Wilson Hape, amesema hospitali ina uhitaji wa wastani wa chupa 60 za damu kwa siku ili kukidhi mahitaji ya wagonjwa ambao wanahitaji huduma hiyo, wakiwemo wanaofanyiwa upasuaji, wagonjwa wa saratani, kina mama wanaojifungua pamoja na wagonjwa wa dharura.

“Upatikanaji wa damu bado ni mdogo kulinganisha na mahitaji yaliyopo, hivyo tunahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi ili kusaidia kuokoa maisha ya wagonjwa,” amesema Bw. Hape.

Aidha amesema kwa niaba ya Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila anawashukuru na kuwapongeza wale ambao wamejitokeza kuchangia damu siku hii ya leo kwani wameonesha upendo na kujali wagonjwa.

Baadhi ya wafanyakazi kutoka Shule ya Hanester iliyopo kibamba wilaya ya Ubungo ambao leo wamejitokeza kuchangia damu ka...
14/02/2026

Baadhi ya wafanyakazi kutoka Shule ya Hanester iliyopo kibamba wilaya ya Ubungo ambao leo wamejitokeza kuchangia damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila.

Baadhi ya wafanyakazi kutoka Shule ya Hanester iliyopo kibamba wilaya ya Ubungo ambao leo wamejitokeza kuchangia damu ka...
14/02/2026

Baadhi ya wafanyakazi kutoka Shule ya Hanester iliyopo kibamba wilaya ya Ubungo ambao leo wamejitokeza kuchangia damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila.

MUHIMBILI YAIMARISHA  HUDUMA ZA KIBINGWA NA KIBINGWA BOBEZI; KAMBI MAALUM ZA UPASUAJI NA TIBA ZA MAUMIVU KUFANYIKA.Hospi...
13/02/2026

MUHIMBILI YAIMARISHA HUDUMA ZA KIBINGWA NA KIBINGWA BOBEZI; KAMBI MAALUM ZA UPASUAJI NA TIBA ZA MAUMIVU KUFANYIKA.

Hospitali ya Taifa Muhimbili–Mloganzila imetangaza kuanza kwa kambi maalum za huduma za kibingwa na kibingwa bobezi zitakazofanyika Februari 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kusogeza huduma za matibabu ya hali ya juu karibu na wananchi na kupunguza rufaa za nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Siku 100 za Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Delilah Kimambo amesema, kambi hizo zinajumuisha huduma ya AVF Fistula kwa wagonjwa wa figo wanaohitaji usafishaji damu (dialysis) itakayofanyika tarehe 14–18 Februari 2026 kwa ushirikiano na wataalam kutoka Korea Kusini.

Aidha, kuanzia tarehe 16–20 Februari 2026 hospitali itatoa huduma ya Advanced Image Guided Percutaneous Pain Management kwa wagonjwa wenye maumivu sugu, kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kuongoza matibabu kwa picha ili kuhakikisha usahihi na ufanisi mkubwa.

Sambamba na kambi hizo, hospitali inaendelea kutoa huduma za kibingwa bobezi ikiwemo upasuaji wa matundu madogo (Interventional Radiology), upandikizaji wa nyonga na magoti kwa zaidi ya wagonjwa 305, pamoja na kuondoa mawe kwenye figo bila kufungua mwili.

Wananchi wamehimizwa kujitokeza mapema kwa uchunguzi na usajili ili kunufaika na huduma hizi za kisasa zinazotolewa hapa nchini.

13/02/2026

Shuhuda wa huduma Bi. Magdalena Nyoni, aeleza uduma bora za afya alizopatiwa mtoto wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila.

13/02/2026

12/02/2026

“Mwanangu alikuwa na hali mbaya sana, lakini alipata matibabu bila kujali hali yangu ya uchumi na sasa hivi anaendelea kupata matibabu ya dialysis nashukuru sana juhudi za wataalam wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, afya ya mwanangu inaendelea kuimarika”.
Bi. Jessica Peter,
Shuhuda wa huduma.

12/02/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeandaa kambi maalum
ya kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu (Arterio-Venous Fistula Creation) kwa wagonjwa wenye
changamoto za figo, itakayofanyika kuanzia Februari 14 hadi 18, 2026, kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma bora na salama za kuchuja damu.

11/02/2026

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA: MUHIMBILI YAWAFIKIA WATU ZAIDI YA 3000 HUDUMA ZA AFYA ZA KIBINGWA BOBEZI.

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA: MUHIMBILI YAWAFIKIA WATU ZAIDI YA 3000 HUDUMA ZA AFYA ZA KIBINGWA BOBEZI.Katika kipindi hiki cha...
11/02/2026

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA: MUHIMBILI YAWAFIKIA WATU ZAIDI YA 3000 HUDUMA ZA AFYA ZA KIBINGWA BOBEZI.

Katika kipindi hiki cha siku 100, Hospitali ya Taifa Muhimbili (Upanga & Mloganzila) imefanikiwa kuwasogezea huduma za kibingwa bobezi wananchi zaidi ya 3000 k**a lilivyo lengo la serikali kuwanufaisha wananchi na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya afya na kuhakikisha huduma za ubingwa bobezi zinamfikia kila mwananchi.

Akizungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji MNH Dkt. Delilah Kimambo ameelezea jinsi Hospitali ya Muhimbili kampasi zote mbili Upanga na Mloganzila zinavyoshirikiana na wadau wa maendeleo kuendelea kupanua wigo wa huduma kwa kuwasogezea wananchi huduma karibu na kuboresha miundombinu ya utoaji huduma.

“Katika kipindi hiki hospitali imetekeleza huduma za kibingwa na kibingwa bobezi k**a upandikizaji uroto,figo, nyonga na magoti huku ikiwa katika maandalizi ya mwisho ya kuanza upandikizaji wa Ini”. Amesema Dkt. Kimambo.

Aidha ameongeza kuwa hospitali hiyo inatekeleza kwa ufanisi agizo la kutozuia miili hospitalini kwasababu ya madeni na kufafanua utaratibu maalum unaotumika sasa unamruhusu mfiwa kuchukua mwili wa mpendwa wake hata akiwa hajak**ailisha gaharama ambazo zilitumika wakati wa matibabu yake.

Kwa upande mwingine Dkt. Kimambo amewataka wananchi kuchangammkia suala la bima ya afya kwa wote kwani itasaidia na kurahisisha huduma na kuwafanya kupata huduma kwa wakati na kuondoa usumbufu wa kudaiwa madeni wakati wapendwa waon wanapopoteza maisha.

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram