15/02/2026
KAMBI MAALUM YA KUTENGENEZA NA KUREKEBISHA MISHIPA YA KUCHUJA DAMU, YAANZA RASMI MUHIMBILI MLOGANZILA.
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeanza kambi maalum ya kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu (Arterio-Venous Fistula Creation) kwa wagonjwa wenye changamoto za figo, kambi hiyo inafanywa na wataalam wa Muhimbili -Mloganzila kwa kushirikiana na jopo la wataalam kutoka Korea Kusini inatarajia kuhitimishwa tarehe 18 Februari 2026 ambazo takribani wagonjwa 50 watanufaika na huduma hiyo.