MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

16/03/2026
WATUMISHI MNH–MLOGANZILA WAHIMIZWA KUENDELEA KUFANYA TAFITI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYAWatumishi wa Hospitali ya Taifa Muhi...
16/03/2026

WATUMISHI MNH–MLOGANZILA WAHIMIZWA KUENDELEA KUFANYA TAFITI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA

Watumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila wamehimizwa kujikita katika kufanya tafiti mbalimbali za kitaalam zitakazosaidia kuboresha huduma za afya pamoja na kuchangia maboresho ya sera za afya nchini.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu na Utawala Bw. Abdalah Kiwanga wakati akifunga mafunzo ya tafiti kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, ambapo watumishi 34 kutoka kada mbalimbali wamepata fursa ya kushiriki mafunzo hayo .

Bw. Kiwanga ameeleza kuwa MNH Mloganzila haitoi huduma za matibabu ya kibingwa na kibingwa bobezi pekee bali pia ni kituo muhimu cha tafiti kinachochangia maboresho ya sera na mifumo ya utoaji huduma za afya nchini, kwani tafiti zinazofanywa na wataalam hao zina mchango mkubwa katika kufikia malengo ya sekta ya afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Tiba Shirikishi ambaye pia ni Mwenyekiti wa k**ati ya tafiti MNH–Mloganzila, Dkt. Lulu Sakafu ameeleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uwezo wa wataalam wa afya katika kufanya tafiti zitakazosaidia kuboresha huduma za matibabu pamoja na kuchangia katika maboresho ya sera za afya nchini.

WATUMISHI MNH–MLOGANZILA WAHIMIZWA KUFANYA TAFITI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYAWatumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mlog...
16/03/2026

WATUMISHI MNH–MLOGANZILA WAHIMIZWA KUFANYA TAFITI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA

Watumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila wamehimizwa kujikita katika kufanya tafiti mbalimbali za kitaalamu zitakazosaidia kuboresha huduma za afya pamoja na kuchangia maboresho ya sera za afya nchini. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu na Utawala Bw. Abdallah Kiwanga wakati akifunga mafunzo ya tafiti yaliyofanyika katika MNH Mloganzila, ambapo watumishi 34 walipata fursa ya kushiriki mafunzo hayo.

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu na Utawala Bw. Abdallah Kiwanga ameeleza kuwa hospitali hiyo haitoi huduma za matibabu ya kibingwa na kibingwa bobezi pekee, bali pia ni kituo muhimu cha tafiti kinachochangia maboresho ya sera na mifumo ya utoaji huduma za afya nchini. Amesema tafiti zinazofanywa na wataalamu wa hospitali hiyo zina mchango mkubwa katika kufikia malengo ya sekta ya afya na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Tiba Shirikishi na Mwenyekiti wa Kamati ya Tafiti MNH–Mloganzila, Dkt. Lulu Sakafu amesema kukamilika kwa mafunzo hayo ni hatua muhimu katika kuimarisha utamaduni wa utafiti hospitalini hapo. Amesema mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uwezo wa wataalamu wa afya katika kufanya tafiti zitakazosaidia kuboresha huduma za matibabu pamoja na kuchangia katika maboresho ya sera za afya nchini.

14/03/2026

Ugonjwa wa shinikizo la macho au Glaucoma ni kundi la magonjwa ya macho yanayoshambulia mshipa wa fahamu unaopeleka mawasiliano ya kuona kwenye Ubongo.

Ungana na Dkt. Yusta Mtogo, Daktari Bingwa wa Macho kutoka MNH-MLOGANZILA kwa ufafanuzi zaidi.

12/03/2026

“Uthubutu,uwajibikaji na moyo wa kujituma katika utekelezaji wa majukumu ni nyenzo muhimu kwa ajili ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja”.

Bi.Merry Amri, Mwanzilishi wa Kampuni ya Mariedo.

12/03/2026

“Tulichokifanya ni kuangalia kitu gani cha muhimu kwa watumishi, tuliona kuna gap kwenye swala la saikolojia na matumizi au uhifadhi wa fedha hivyo tukatafuta watu husika ili kutoa elimu stahiki”.

Dkt. Julieth Magandi, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

12/03/2026

“Tumekuja bila kitu lakini hatukutegemea k**a tutaondoka na elimu kubwa ambayo hatujalipia na yenye umuhimu mkubwa k**a tukiitumia”.

Bi. Luiza Ullaya ,Afisa Ustawi wa Jamii Muhimbili-Mloganzila.

*MNH-Mloganzila: Watumishi wanawake wahimizwa uthubutu na uwajibikaji kazini.*Watumishi wanawake wa Hospitali ya Taifa M...
11/03/2026

*MNH-Mloganzila: Watumishi wanawake wahimizwa uthubutu na uwajibikaji kazini.*

Watumishi wanawake wa Hospitali ya Taifa Muhimbili – Mloganzila wamehimizwa kuendelea kuonesha uthubutu, uwajibikaji na moyo wa kujituma katika utekelezaji wa majukumu yao ya kuwahudumia wagonjwa.

Akizungumza katika hafla maalum ya watumishi wa MNH Mloganzila, Mwanzilishi wa Kampuni ya Mariedo, Bi. Merry Amri, amewataka watumishi hao kuendelea kuwa na moyo wa kujituma na kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kijamii na kitaaluma, huku akisisitiza kuwa kujitoa kunachangia mafanikio binafsi na ya taasisi kwa ujumla.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili – Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi, amewapongeza watumishi kwa juhudi, nidhamu na moyo wa kujituma wanaouonesha katika kuwahudumia wananchi.

Katika hafla hiyo mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo saikolojia na usimamizi wa fedha.

Hafla ya Watumishi Wanawake Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila yaendelea, ambapo pamoja na mambo mengine watapata f...
11/03/2026

Hafla ya Watumishi Wanawake Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila yaendelea, ambapo pamoja na mambo mengine watapata fursa ya kupata elimu juu ya usimamizi wa masuala ya fedha na saikolojia.

09/03/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imehitimisha mafunzo ya muda mfupi(short course) ya Fiziotherapia kwa watu wanaohitaji uangalizi wa karibu (Physiotherapy in critical care).

Kutana na mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo Bw. Ambwene Mwakyagi, Mfizioterapia kutoka Hospitali ya Rufaa mkoa Temeke.

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram