04/10/2021
𝕁𝕀ℕ𝕊𝕀 𝕐𝔸 𝕂𝕌ℙ𝕌ℕ𝔾𝕌ℤ𝔸 𝕌ℤ𝕀𝕋𝕆 𝕂𝕀𝕌𝕊𝔸ℍ𝕀ℍ𝕀 ( 𝕄𝕒𝕞𝕓𝕠 𝕪𝕒 𝕜𝕦𝕫𝕚𝕟𝕘𝕒𝕥𝕚𝕒 )
SEHEMU YA 1
Ni vema kupunguza uzito taratibu kadiri siku zinavyoenda . Iko hivi unapopunguza uzito wako haraka sana utapoteza misuli (Nina maanaisha ubora , na wingi wa misuli), mifupa itapoteza ubora na utapoteza maji mengi pia badala ya mafuta ( The Academy of Nutrition and Dietetics )
🌏Fikiria kupunguza nusu kilo hadi kilo 1 kwa kila wiki , na usikimbilie kupunguza uzito kwa bidhaa au suppliments au vyakula ambavyo vina kupunguza kilo nyingi kwa haraka . Mwili wako unahitaji utaratibu , kila kitu kwenye mwili wako kinataka utaratibu , mwili unapopungua taratibu unabadili mifumo yake ya kihuduma kulingana na mahitaji ya mwili kwa wakati husika
🌏Nakushauri ukiamua kuanza zoezi hili , uwe na usimamizi wa daktari ili kuhakikisha unapungua katika utaratibu mzuri , na hukosi virutubisho muhimu kwa afya yako.
Sishauri kabisa na wala sio utaratibu mzuri kusema uache kula wanga , hapana , swala la msingi hapa ni kupunguza ratio (Kiasi) unachotumia na upate kiasi salama na kisichozidi mahitaji , mazoezi ufanye pia
🌳WEKA LENGO /MALENGO
Ule msemo kwamba ule tu chakula kingi na utafanya mazoezi , haisaidii kabisa wewe kupunguza uzito . Fanya utaratibu huu ufuatao endapo utataka upate kiwango cha kawaida cha calories kwa siku :
🍎Punguza mlo wako ( Ratio/kiasi)
Kwanza fikiria ni kiasi gani cha chakula huwa unakula katika mlo mmoja ( Ni calories ngapi unakula ) , kisha punguza kidogo . Mfano huwa unakula sahani nzima ya chakula , sasa waweza amua kwamba kuanzia sasa utakua unakula robo tatu ya sahani . Kisha kadiri siku zinavyoenda utazidi kupunguza , ila uhakikishe hautapunguza chini ya kiwango cha kawaida na cha chini sana mfano robo sahani.
Sasa hapo unakazia na maji ya kutosha ili ujihisi umeshiba
Kwa mlo wowote utakao kula hakikisha sahani yako inahusisha vyakula aina ya wanga ( Naweza ita nafaka) , protein , mbogamboga na matunda ili upate virutubisho vyote muhimu kwa afya yako
Inaendelea......