03/12/2025
WA MWENYEKITI NA MAKAMU MWENYEKITI HALMASHAURI YA KALAMBO WAKAMILIKA
Leo tarehe 03 Novemba 2025 Mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani wilayani ya Kalambo umefanyika agenda zikiwa ni
1. Uapisho wa Waheshimiwa Madiwani
2. Uchaguzi wa Mwenyeki na Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri
3. Kuunda kamati za kudumu za Halmshauri
4. Kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za Halmshauri kwa kipindi cha kuanzia Julai hadi Novemba 2025
5. Kupitisha vikao vya Halmshauri.
Madiwani wote wameweza kuapishwa na ndipo Uchaguzi wa kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ukafanyika
Ambapo Mh: Leopard John Mbita Diwani wa kata ya Kasanga maarufu kwa jina Kanyerere ameibuka mshindi kwenye nafasi ya Mwenyekiti Halmshauri kwa kura 32 sawa na 100% za madiwani wote.
Aidha Mh: Kassim Lupia Simchimba Diwani wa kata ya Mnamba Maarufu kwa jina la Diwani Mgeni ameibuka mshindi kwenye nafasi ya Makamu Mwenyekiti kwa kura 32 sawa 100% za madiwani wote.
Katika kushukuru Mh: Mbita amewashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa kumwamini,kumchagua na kumtengenezea Historia kubwa katika ukoo wake ambayo haiya wahi kutokea
Ameahidi kufanya kazi kwa ushirikiano weledi na kujishusha akitambua kwamba yeye sio kiongozi ni mtumishi ameahidi kutumika kwa maslahi ya umma.
Mh: Kassim pia amewashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa kumchagua yeye Diwani mgeni na kwamba yeye kwake ni muujiza nikama ndoto lakini anashangaa imekuwa kweli, ameahidi kushirikiana na Mwenyekiti, Mbunge,Madiwani, Mkurugenzi na wakuu wa Idara kupeleka mbele Kalambo.
Katika kutoa nasaa Mh: Edephons Joachim Canoni Mbunge wa jimbo la Kalambo amewakaka Madiwani kuondokana na makundi migogoro na chuki
Wadumishe mshikamano upendo kujaliana na kuthaminiana hayo yaki fanyika Maendeleo yata kuwepo lakini kukiwa na migogoro hakuwezi kuwepo maendeleo
Ameahidi kutoa ushirikiano kwa wote bila kubagua wala kutengeneza matabaka, watafanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wote na wakuu wa idara
Ameomba kila mtu akafanye kazi na kutimiza ahadi alizo ahidi huku akitambua maboss wa kila Diwani na yeye Mbunge ni wananchi hivyo ofisi yake itakuwa wazi kwajili ya kusikia kero na changamoto na kuzitafutia ufumbuzi.
Mh: Lazaro Komba Mkuu wa Wilaya ya Kalambo amewaomba Waheshimiwa Madiwani viongozi wa dini, viongozi wa kimila na taasisi mbalimbali kuhamasisha amani
Kwani amani ikitoweka hakutakuwa na maendeleo hata shughuli za kila siku za wananchi zita simama
Pia amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Kalambo kuwepo kwa amani na utulivu na kuahidi kuendelea kulinda amani na utulivu ili Kalambo iweze kuendelea kupata maendeleo.
Na Ndg: Shafi Mpenda Mkurugenzi Mtendaji Halimashauri ya Kalambo amewaasa Madiwani kufanya kazi kwa kushirikiana
Na kuweza kuwasilisha kero na changamoto za wananchi ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi sio kubaki na kero mfukoni
Amewatalifu pia kuwa ameandaa ziara anasubiri kibali cha mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo Waheshimiwa madiwani wata tembelea baadhi ya wilaya ili kujifunza
Jinsi wilaya nyingine wanavyo tafuta fedha wanavyo buni Miradi, kusimamia na kutatua kero na changamoto za wananchi, ili kuongeza msukumo kwa Madiwani utakao saidia wilaya ya Kalambo kusonga mbele.
By Musa Mzopola βοΈ