03/02/2026
Kiungo wa Kimataifa wa Ivory Coast na Klabu ya Al Wasl FC ya Saudi Arabia, Jean N'guessan .jean21_officiel ameonesha nyumba aliyomjengea Mama yake mzazi huko kwao nchini Ivory Coast k**a zawadi kutokana na mafanikio aliyoyapata kupitia soka.
Kwenye post alizotuma kwenye akaunti yake ya Instagram ameonesha na picha za maisha yao kabla hajafanikiwa.
Jean ameandika hivi baada ya kupost
Ilikuwa ni ndoto yangu siku moja kuifuta machozi yako, kukuona ukiwa na furaha haina thamani yoyote kwangu, kwa sababu yote uliyokuwa unayafanya kwa ajili yangu kwa siri ni deni ambalo sitaweza kulilipa
kamwe.
Asante kwa kuniamini, nakupenda sana MAMA ��