09/03/2026
Ripoti za ujasusi za Urusi zinaeleza kuwa Israel imepata hasara kubwa sana ndani ya masaa 72, baada ya mashambulizi ya kulipa kisasi yaliyofanywa na Iran, mashambulizi hayo ya Iran yamesababisha madhara kwenye kituo cha Nyuklia cha Israel (Dimona Nuclear reactor) kituo hicho cha Nuclear kimepoteza kabisa uwezo wake wa kufanya kazi.
Lakini pia sambamba na hasara hiyo list ya watu muhimu waliouwawa wa Israel ni k**a ifuatavyo wameuwawa wanasayansi 11 ambao walikua ni wakuu na wataalam wa Nuclear, Majenerali 6 wakuu wa Israel, Maafisa 198 wa jeshi la anga wakiwemo marubani wakuu, wanajeshi 462 wameuwawa kwenye Operation za ardhini na mashambulizi kwenye kambi za kijeshi, na Maajent 32 wa Mossad wameuwawa katika operation za siri zilizofeli.
Jumla ya vifo vya wanajeshi na maafisa wa ngazi za juu vinazidi 700, lakini Netanyahu bado hajazungumza madhara yaliyotokea katika kituo cha Nyuklia ( Dimona Nuclear reactor) lakini imeripotiwa kuwa mikutano ya dharura ya baraza la vita la Israel inaendelea.
Jeshi la Iran IRGC limesherehekea hadharani ushindi huo kwa kusema "Ni ushindi kutoa kwa Mwenyezi Mungu".