Ayoub Butandu

Ayoub Butandu Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Ayoub Butandu, Family Therapist, Dar es Salaam.

👨‍👩‍👧‍👦Mtaalamu wa Familia na Mahusiano
✍️Natoa mwongozo wa kitaalamu kwa familia zinazotafuta amani, upendo na furaha ya kweli.
🌿 Elimu | Ushauri | Mabadiliko ya maisha ya kifamilia
📌 "Familia yenye Amani na Furaha Huishi Maisha Bora."

Familia Yako ina Furaha? | Is Your Family Happy?Furaha ndiyo imebeba maana halisi ya maisha. Kila mtu anahitaji kufurahi...
22/09/2025

Familia Yako ina Furaha? | Is Your Family Happy?

Furaha ndiyo imebeba maana halisi ya maisha. Kila mtu anahitaji kufurahi maishani. Hata k**a mtu anaweza kuwa na maisha mazuri kiasi gani akikosa furaha tu basi huwa haoni uthamani wa maisha yake tena. Ndiyo maana wakati mwingine watu licha ya kuwa na mali, utajiri au vyeo vikubwa wanaamua kujinyonga😭😭😭. Ni baada ya kuona hayo yote waliyonayo hayawapatii furaha maishani mwao.

Furaha ndio kitu pekee ambacho hakipaswi kukosa kwenye familia bila kujali ina hali gani! Furaha kwenye familia si zawadi bali ni hitaji la lazima. Je, wewe unaipatiaje furaha familia yako? Tupe mbinu wenzio😊😊😊.



Nyumbani ni Nyumbani | East or West Home is the BestKila mtu ana nyumbani! Hata asiye na nyumba ana nyumbani. Nyumbani k...
04/09/2025

Nyumbani ni Nyumbani | East or West Home is the Best

Kila mtu ana nyumbani! Hata asiye na nyumba ana nyumbani. Nyumbani kwako ni pale unapoishi kwa sasa, bila kujali umejenga ama umepanga. Umejiegesha kwa rafiki yako ama upo kwa mjomba au shangazi.

Kila siku watu wanadamka majogoo na kwenda kusaka riziki lakini lazima warudi nyumbani kupumzisha miili yao baada ya shughuli zao. Nyumbani kunapaswa kuwa sehemu ya pumziko, mtu ambako anasahau shida zake zote na sio sehemu ya makelele na zogo chungu nzima. Ndiyo maana hata mwana mpotevu maji yalipozidi unga aliamua kurudi home. Bila shaka hata sisi tuliotoka kijijini kuja kusaka maisha mjini, mambo yanapokuwa hayaeleweki tunapoamua kurudi zetu kwetu tunajifunza kwake 😂

Anyway tuacha na hayo, mzee wangu alikuwa anarudi nyumbani k**a kawaida ya waja wote dunia nzima. Lakini isivyo bahati kapotea njia, yupo NJIAPANDA anaomba msaada. Tafadhali naomba unisaidie kumwelekeza mzee wangu njia ya kumfikisha nyumbani asilale porini.




MAISHA NI WATU NA KUISHI NI KUHUSIANA NA KUCHANGAMANA NA WATU HAOLicha ya kitabu cha "A Man of the People" kuchapishwa m...
08/05/2024

MAISHA NI WATU NA KUISHI NI KUHUSIANA NA KUCHANGAMANA NA WATU HAO

Licha ya kitabu cha "A Man of the People" kuchapishwa miaka mingi iliyopita kila kukicha kinazidi kujipatia umaarufu na kupendwa zaidi kwa sababu ya umahiri wa gwiji Chinua Achebe katika kueleza mambo yasiyopitwa na wakati.

Naomba nitoe mfano mmoja kutoka kwenye kitabu hicho kilichochapishwa na kampuni ya Heinemann mwaka 1966. Katika kitabu hicho kuna mhusika aitwaye Odili ambaye baada ya kuhitimu chuo alirudi kwao na kuanza kufundisha shule. Baadaye Odili anakutana na mheshimiwa mmoja aitwaye Chifu Nanga ambaye ni mbunge na waziri na kabla ya kuwa mbunge alikuwa mwalimu kwenye shule hiyohiyo Odili anayofundisha.

Baada ya wasomi hawa wawili wanaofahamiana na kutoka sehemu moja kukutana, Chifu Nanga anamsihi Odili akawe katibu ofisini kwake maana katibu wake ni wa kabila jingine. Mhe. Nanga anahitimisha kauli yake kwa kusema, "Nowadays, it doesn't matter what you know but who you know". Basi, k**a hali ilikuwa hivyo miaka ya 66 kitabu hiki kilipochapishwa je itakuwaje leo miaka zaidi ya 50 baadaye? Bila shaka itakuwa ni mbaya zaidi ya mara mia.

Kwanini nimeanza na mfano huu ama kueleza kuhusu kitabu hiki? Katika jamii yetu ya sasa kuna watu hawana habari na watu. Wao wanajidai kuwa wako bize na mambo yao wenyewe na wanajua kujifungia kwelikweli. Hata siku moja huwezi kuwaambia kuchangamana na watu wengine kwenye maeneo yanayokutanisha watu k**a michezo, sherehe mbalimbali n.k. Wakati mwingine hata wanapokuwa katika mikusanyiko ya watu wanabaki kuwa wao k**a wao hata huwezi kuwaambia kuchangamana ama kusemeshana na wenzao. Watu wa hivi hata akikukuta umekaa ama upo sehemu ambayo naye amekuja si ajabu hata akakuvungia hata kukusalimu tu.

K**a wewe ni mmoja wa watu wa aina hii napenda leo nikujulishe kuwa maisha ni watu na kuishi ni kuchangamana nao. Kwa kadiri unavyojifungia mwenyewe ndivyo unavyojikwamisha mwenyewe. Labda tu nikwambie kwamba unavyojifungia ndivyo unafungia michongo unayohitaji ili utoboe maisha.

Kwa taarifa yako unahitaji watu ili ufanikiwe. Katika dunia ya leo kila kitu unachohitaji kipo kwa watu na ili ukipate itategemea jinsi unavyohusiana na watu hao. Kazi ama fedha ama mwenza unayemhitaji leo ili ubutue maisha yupo kwa watu hao unaowachukulia poa. Siku hizi watu wengi wanasota kitaa kwa kukosa kazi na wengine wameshahaso kila kona kupata ajira imekuwa ngumu kwao wakati mwingine anapata kazi ya heshima na mshahara mnono bila hata ku-apply kwa sababu anajuana na mwajiri k**a Odili na Chifu Nanga.

Kuna mtu baada ya kuhitimu chuo amekaa mtaani miaka ya kutosha mpaka anazeekea nyumbani kwa kukosa "connection" wakati mwingine anamaliza mtihani leo kesho anaenda kuanza kazi. It's doesn't matter what you know but who you know - hivi ndivyo dunia inakwenda siku hizi ndugu yangu.

Mpendwa k**a kweli unataka kufanikiwa katika ndoto yako unahitaji watu kuliko kitu kingine chochote kile unachofikiria wewe. K**a bado upo chuo unasoma labda digrii ya kwanza na una ndoto za kusoma Master's na kuendelea nikukumbushe kuwa unahitaji kuwa na mtu atakaye-recommend application/scholarship yako.

K**a huna ndoto za kuendelea kuongeza kisomo na unafikiri wewe ukimaliza chuo utazama moja kwa moja kufanya kazi na kula mshahara. Basi ngoja nikukumbushe tu kuwa ndugu yangu unahitaji referee wa kuweka kwenye CV yako ili upate hiyo kazi unayoitaka. Soko la ajira siku hizi limechangamka mno, hata k**a una sifa zote ama hata za ziada anazohitaji mwajiri k**a huna referee wa kukunenea mema ajira hiyo uliyostahili utaikosa hivihivi huku ukiitazama kwa macho yako mawili (wakati mwingine na miwani juu).

Lakini huenda huwazi kuendelea na masomo ama kufanya kazi. Labda wewe unafikiria kufanya biashara na kupiga hela. Mwenzangu huku nako si salama. Ili ufanikiwe katika biashara yako unahitaji mtu atakayekupa machimbo/masoko ya bidhaa zako. Unahitaji mtu wa kukuletea wateja. Biashara yako itahitaji mtu atakayekusaidia katika masuala ya usajili, (hapa Bongo bila kuwa na mtu leseni ya biashara utaipata umepata taabu sana ama la ukubali kuzunguka mbuyu) kulipa ritani za TRA na k**a utahitaji mikopo ili kuipanua zaidi, utahitaji mtaalamu wa masuala ya fedha wa kukusaidia katika eneo hilo.

Aidha, k**a hufikirii kufanya lolote kati ya hayo niliyoyataja hapo juu lakini ungali kijana basi utahitaji watu kwa ajili ya send off/harusi yako. Hii ndiyo sehemu yenye utata sana hasa kwa vijana wengi - linapofika jambo lake ndiyo anakutafuta ili tu umchangie apate mume ama mke kwa sapoti ya jasho lako wakati hakuwa na muda nawe. Kwani wewe haijawahi kutokea unawasha data kwenye simu yako mara paaaap unajikuta kwenye group la michango ya sherehe ama harusi ya mtu ambaye hajawahi kukutafuta japo hata kwa kukutumia sms moja kwa zaidi ya miaka 5? Kwa sababu maji yanakuwa yamemfika shingoni ndio anakumbuka kulazimisha undugu hata kwa watu ambao hatukuwa na muda nao.

Kila mtu kwenye jamii anahitaji watu. Hawa watu sio lazima wawe ndugu, wala watu unaotoka nao sehemu moja huko kijijini. Si lazima wawe wa umri, elimu ama jinsi yako. Bali hawa ni watu wako wa nguvu, watu waliotayari kulichukulia jambo lako k**a jambo lao wenyewe. Ni watu ambao ukianguka wapo tayari kukuinua na ukiteleza watajitoa kukudaka ili k**a utaumia au kuanguka basi potelea mbali muumie ama kuanguka wote. Waingereza wana msemo wao usemao, "You will never walk alone" k**a wewe unafikiri unaweza kwenda peke yako basi endelea kujifungia nimekaa palee, mwisho wa siku tutaona. Ukitoboa kwa mtindo huo basi nasi tutafuata nyendo zako.

Ndugu yangu maisha ni watu. Husiana na watu, changamana na watu ishi na watu hayo ndiyo maisha. Kumjua mtu jina lake haitoshi katika zama za leo bali tafuta kila namna ya kutengeneza naye undugu. Nakuhakikishia k**a sio kesho basi keshokutwa huyo mtu atakufaa. Katika maisha ya sasa ni vema mtu kuwa na watu anaojuana nao katika nyanja zote za maisha. Tengeneza undugu na watu wa afya (madaktari, wauguzi n.k), tengeneza uhusiano mwema na watu wa ulinzi na usalama (wanajeshi, polisi, mgambo n.k), tengeneza ukaribu na watu wa masuala ya utawala (wanasiasa, mameneja, wakurugenzi n.k) tengeneza familia na watu wa rohoni kulingana na imani yako (wachungaji, manabii, wainjilisti, mapadri, masheshe, waganga wa kienyeji n.k) hao ndio watakaokuufaa kwa wakati usiotarajia.

Kwa leo naomba niishie hapa. Naamini umepata kitu cha kujifunza... Si mbaya ukiweka comment yako hapo chini ama kushea kwa wenzako ujumbe huu ili nao wapate cha kujifunza pia. Maisha ni watu na unavyowatumia andiko hili ndivyo unaiishi dhana hii.

Wasalaam;

Ayoub Butandu

ayoubbutandu@gmail.com

Sio Dhambi Kusema Hauwezi Siku za hivi karibuni nilipeleka laptop yangu kwa fundi baada ya kupata hitilafu fulani. Mara ...
30/04/2024

Sio Dhambi Kusema Hauwezi

Siku za hivi karibuni nilipeleka laptop yangu kwa fundi baada ya kupata hitilafu fulani. Mara baada ya fundi kuifungua aliniambia kuwa amebanwa na kazi za wateja wengine kwa hiyo niiache atakwenda kuitengenezea nyumbani hivyo niifuate kesho yake mchana. Nami kwa kuwa nilikuwa na haja ya kuona laptop yangu ikipona sikuona shida kuiacha wakati fundi mwenyewe alikuwa na ofisi yake jirani yetu tu.

Cha ajabu ni kuwa baada ya kuiacha, huo ndio ulikuwa mwisho wa kuiona kompyuta yangu. Kesho yake nilipoifuata zilianza "danadana". Kwanza aliniambia kifaa chenye shida hana hivyo bado anakitafuta niifuate kesho yake. Kesho ikazaa kesho na kesho na kesho na kesho. Baada ya kumaliza k**a mwezi mzima nafuatilia kompyuta yangu mwisho nilighafilika kwa ahadi zake ambazo zilikuwa zimeshanichosha mno.

Basi nilimfuata kwa lengo moja tu la kutaka kompyuta yangu k**a ilivyo, nilipomkuta ofisini nilimwambia leo sitoki bila kunipa laptop yangu. Baada ya kunisihi nirudi kesho sikutaka hata kusikia, hivyo mwisho alinifungia kompyuta yangu na kunirudishia. Niliondoka moja kwa moja kwenda kwa fundi mwingine, alipoitazama kila kifaa cha ndani alikuwa ameshakwangua mpaka HDD.

Nilimfuata na kumweleza kuwa ingawa amenirudishia huku akidai kuwa kila kitu kilichokuwemo kwenye laptop kakirudisha basi ajue nimeshajua kila kitu cha maana ndani kachukua tena kwa bahati mbaya kwa kuniwekea vibovu. Niliwaza sana jinsi ya kumfanya huyu fundi mwisho nikajishauri kuwa hasara roho tu hivi vingine k**a uzima upo vinatafutwa na kupatikana. Niliondoka zangu kwa machungu!

Watu kibao wamepata visanga k**a hivi kwa mafundi. Unapeleka simu au redio ama TV badala fundi akuambie hilo tatizo hawezi na kukuambia upeleke kwingine anachukua kitu chako halafu anaanza kukuzungusha weee! Utafuatilia mpaka uamue kumwachia k**a una roho nyepesi k**a mimi.

Ndugu zangu tujifunze kwa hospitali. Anapokuja mgonjwa mwenye tatizo ambalo hospitali fulani haiwezi kulitibu anapewa rufaa ya kwenda hospitali nyingine yenye uwezo wa kushughulikia tatizo lake. Hii huipa sifa hospitali iliyotoa rufaa kwa mgonjwa na wakati mwingine akiwa na shida anaweza kurudi pale hospitalini kuliko fundi ambaye anakuzungusha wee. Huyu ukimalizana naye huna hamu ya kurudi kwake hata wakati mwingine unapoweza kuwa una shida ambayo unafikiri ipo ndani ya uwezo wake.

TUBADILIKE! Tukitaka kufanikiwa tuwe wakweli, sio dhambi kusema huwezi na kumwonesha mhitaji anayeweza kutatua shida yake. Hii itakupa kuaminiwa na kuwa na sifa njema hata kwa watu wengine. Mimi fundi aliyeniharibia laptop, akaniibia vifaa na kunipiga zile danadana siwezi kurudi kwake wala kurecommend mtu mwingine kwake.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255764284549

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ayoub Butandu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ayoub Butandu:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram