Evangelist, Teacher, Pastor. Lion A Mangole

Evangelist, Teacher, Pastor. Lion A Mangole how to visit in our Church? we are in Yombo vituka next to Malawi Hospital. Dar es salaam mob. +255 755528965. email. gmahanaimu@yahoo.com. P.O.Box. 17512

33. JE! TANZANIA KUNA WATAFITI/WANASAYANSI KWELI?. (SOMA MAKALA HII MWANZO HADI MWISHO TAFADHALI).  NUKUU KUTOKA KITABU ...
28/04/2024

33. JE! TANZANIA KUNA WATAFITI/WANASAYANSI KWELI?.
(SOMA MAKALA HII MWANZO HADI MWISHO TAFADHALI). NUKUU KUTOKA KITABU CHA KUWA NA UWEZO MKUBWA KIAKILI 2018. Kuna mambo yamekuwa sababu ya mimi kujiuliza maswali haya. Ili kujiridhisha na hata kujua au kupata jawabu na kisha kutoa ushauri wangu kwa mustkabali wa taifa langu Tanzania.
Moja ya sababu zilizonifanya nijiulize maswali haya ni.

1. Daraja la Jagwani/ Kituo au ofisi kuu ya mabasi yaendayo
kasi UDART Jangwani.

Hii imetokana na baada ya mvua nyingi kutokea mwaka 2018 za masika, daraja lilifunikwa na maji, na ukizingatia barabara husika ni mpya kabisa na imejengwa kwa gharama kubwa. Na isitoshe ofisi za mwendokasi kufurika maji hata kupelekea ofisi hizo kufungwa kwa muda ili kupisha maji yatoke.

Maswali ya kujiuliza.
Utafiti gani uliofanyika hata ukaona ujenzi wa barabara k**a ile ndio inafaa kwa eneo lile? Ni mtafiti gani aliyeona kuwa ofisi ya mwendo kasi ikijengwa pale jangwani na kwa mtindo ule hakutakuwa na madhara? Hivi huwezi kukubaliana nami kuwa, hata wewe ambaye haujasoma au si mtaalam wa mambo ya ujenzi utabaini kuwa haikupaswa kujengwa daraja k**a lile pale jangwani? Au haikupaswa kujengwa ofisi za UDART Kwa aina k**a ile? Aidha ilipaswa kuwa juu zaidi kutoka usawa wa ardhi ya kawaida?

Kutokana na asili ya eneo la jangwani na kukaribiana na bahari ya hindi kutoka darajani wastani wa kilomita moja kasoro makutano ya mto msimbazi na bahari ya hindi (Sarenda brige). Historia ya mto msimbazi, na uwingi wa maji yanayosafirishwa na mto huo. Inaaminika kuwa karibu maji yote ya jiji la Da es salaam yanasafirishwa kupitia mto huo. Mto Msimbazi umetokea nje ya jiji la Dar es salaam meneo ya Pugu, ukaingia Gongolamboto, ukapitia Vingunguti, Kisha Buguruni, na maeneo ya Buguruni chini maeneo Kigogo kuna makutano ya mito kadhaa ya jiji la Dar es salaam inakutana kwa pamoja na kuunda mto mmoja mkubwa maeneo ya Jangwani huitwa Jagwani, lakini Jangwani ni makutano ya mito yote, na mto huo sana unaelekea kufika maeneo ya makutano ya bahari ya Hindi (Sarenda brige).

Kwa wastani mto huu umepita katika Wilaya ya Ilala yote, ikiwa na maana karibu maji yote ya Wilaya ya Ilala na ikijumuishwa na maji yatokayo katika majengo ya katikati ya jiji hasa Kariakoo yote yanaingia katika mto huo.

Pia asilimia ya mito mingi ya Wilaya ya Kiondoni iliyopita maeneo ya Kigogo, Magomeni, Mkwajuni nk, yote inaingia katika Mto wa Msimbazi. Hii bila ya kujumuisha tani za taka ngumu au shehena za taka ngumu zinazoingia katika mito hii.

Tabia ya makutano ya bahari na mito.
Kwa kawaida maji yanayoingia bahari yanaingia taratibu ili kuchanganyika na maji ya bahari, pia wakati fulani bahari inakuwa kupwa na kujaa. Kwa hiyo ikiwa ndio wakati wa kujaa na mvutano wa mawimbi makubwa, bila ya shaka maji ya mto yataingia lakini kasi yake haitakuwa kubwa k**a wakati bahari imekuwa kupwa (Maji yamepungua). Bila shaka uwezekano wa kuwepo mafuriko ni mkubwa sana, katika eneo hili la Jangwani kipindi ambacho maji mengi ya mvua za masika yakitaka kuingia kwa wingi na kwa wakati mmoja.

2. Barabara ya mwengo kasi Kariakoo mtaa wa/barabara ya
Msimbazi,
Maeneo ya mataa Uhuru na Msimbazi, na karibu na kituo cha DDC. Kituo cha mwendokasi DDC Kariakoo, Kabla ya kujengwa barabara mpya ya mwendokasi, palikuwa na utiririshaji majitaka kutoka katika mifereji ya barabara kwa miaka mingi. Lakini cha kusikitisha, hata baada ya kujengwa barabara mpya na ya kisasa zaidi na mifereji kujengwa upya, lakini bado tatizo la mifereji ya maji taka inaenedelea kububujisha au kutiririsha maji taka ndani ya barabara hadi kuleta tishio la kiafya kwa wakaazi wake. (Hii ni hadi kufikia mwaka 2018)

Swali la kujiuliza.
Ni utafiti gani uliofanyika na kujiridhisha kuwa, iwapo barabara ikijengwa kwa aina k**a ile na mifereji k**a ile utaondoa tatizo la utiririsha wa maji taka barabarani k**a hapo kwanza? Kwa nini wakandarasi wetu na wataalamu wetu, kwa mfano wataalamu wa mazingira wasiwe na majibu sahihi ya matatizo ya mazingira yetu? Au kazi yao ni nini k**a sio kuchunguza

nini kinahitajika katika mazingira yetu ili kuondoa tatizo? Leo tunapoona matatizo k**a haya yakijirudia huwa tunapata shaka na wataalamu wetu, au tunajaribu kuhisi k**a hatuna wataalamu au watafiti?

3. Madaraja mapya kusombwa na maji au maji kuacha daraja na kupasua sehemu nyingine.(Hii ni kwa mjibu wa utafiti wangu hadi kufikia mwaka 2018.)
Ndugu msomaji, kuna mambo huwa yanatia aibu kubwa taaluma za watu, au pia yanaitia aibu nchi yetu kwa kiasi kikubwa. Hivi unajiuliza iwapo daraja likisombwa na maji au maji kuacha kupitia darajani na kuvunja sehemu nyingine na kutoroka, je utafiti ulifanyika kikamilifu?

Ni wazi kabisa iwapo madaraja yakikatika au maji kupasua sehemu nyingine na kumomonyoa udongo na kuikata barabara, hii inaonyesha wazi wajenzi hawakuchunguza eneo hilo vya kutosha. Au hatuna tafiti zinazo saidia kujua tabia za asili za maeneo yanayotaka kujengwa madaraja au mifereji. Mjenzi anatakiwa awe na majibu ya matatizo kabla hayaja tokea. Ikiwa na maana aione hatari ya eneo husika analofikiria kulijenga na kujenga kulinga na mahitaji ya eneo. Nadhani kipimo cha mkandarasi mzuri ni pale majanga k**a haya yakitokea na kisha kazi yake ikibaki salama huyo ndio mjenzi bora. K**a umejenga kwa udanganyifu mvua zikija kazi yako itapimwa na kuonekana ni kazi mbovu.

4. Ujenzi wa shule.
Kwa mujibu uchunguzi wangu hadi kufikia mwaka 2018. Kumekuwa na idadi kubwa ya wanafunzi haswa kwa shule za serikali hata kufikia madarasa hayatoshi kuchukua idadi kubwa k**a hiyo. Na majengo kila kukicha yanajengwa na hata maeneo ya kujenga yanakosekana.

Ujenzi wa nyumba za chini.
Kosa kubwa linalofanyika ni ujenzi ya nyumba za chini ambazo si ghorofa. Kwa kawaida nyumba za paa (Ambazo sio ghorofa) Zinachukua Idadi ndogo ya watu na pia zinatumia eneo kubwa la ardhi. Katika kitabu changu kiitwacho UCHUMI HURU USIOKUWA NA MAJUTO, Nimeandika umuhimu wa matumizi bora ya ardhi.

Na katika mada hiyo, nimeelezea umuhimu wa kutumia eneo dogo la ardhi kwa manufaa makubwa. Ukubwa wa ardhi wenye urefu wa mita 20x20. Unaweza kujenga nyumba zaidi ya moja kuwenda juu, ikiwa na maana unaweza kujenga nyumba moja ya ghorofa yenye ghorafa 5 au 10, au 20. Sawa na nyumba moja kwa 5 au moja kwa 10 au moja kwa 20. Ambapo k**a nyumba tano za chini zingechukua eneo la ukubwa wa mita 100 sasa unatumia mita 20 kwa nyumba tano na zaidi katika eneo moja tu.

Swali langu la msingi ni.
Tumekosa wataalamu waliogundua kuwa serika inatumia vibaya ardhi na kuingia gharama za kujenga kila kukicha na kuishauri serika kwa sasa waanze kujenga nyumba za juu?

5. Wamachinga.
Sijaelewa k**a ni utafiti gani umefanyika na kubaini kuwa kuwa na umachinga holela itasaidia kitu fulani katika taifa letu? Nani aliyefanya utafiti ili kujua kuwa kuna faida kadhaa na madhara kadhaa?

6. Tatizo ni idadi ya watumishi au udhaifu wa watumishi?
Kwa nini serikali zetu za Africa huona kuwa jibu la utendaji
bora ni kuwa na watumishi wengi au Wizara nyingi?

Hali ya kuwa utitiri wa watumishi hao wanafanya kazi chini ya kiwango? Gharama za uendeshaji serikali zinakuwa kubwa kutokana na kuwa na serikali yenye watumishi wengi. Kwa nchi za Afrika hazinabudi kupunguza idadi ya watumishi wake, na kuzingatia usimamizi mzuri wa watumishi wachache watakao kuwanao ili wafanye kazi kwa ufanisi mkubwa, na huku wakiwalipa malipo mazuri.

NUKUU KUTOKA KITABU CHA KUWA NA UWEZO MKUBWA KIAKILI 2018.
BEI YA KITABU NI TSH 20,000 MAWASILIANO 0717528272 / 0788170367 /0755528965

ROHO INA NAFASI GANI KATIKA AKILI ZA BINADAMU? SOMA MAKALA YOTE TAFADHALI. (Nukuu kutoka katika kitabu cha, Kuwa na uwez...
27/04/2024

ROHO INA NAFASI GANI KATIKA AKILI ZA BINADAMU? SOMA MAKALA YOTE TAFADHALI.

(Nukuu kutoka katika kitabu cha, Kuwa na uwezo mkubwa Kiakili).

Kwa kweli katika mambo ya kusoma na kuchunguza kuhusu uumbaji wa Mungu, kuna mengi ya kujifunza. Kwani hata ukimtafakari tu binadamu jinsi alivyoumbwa huwezi kummaliza kwa mara moja, nadhani itachukua muda mwingi sana kujua jinsi alivyoumbwa na jinsi anavyofanya. Kuhusu roho. Roho ni sehemu moja inayoweza kutawala maamuzi ya mwili iwapo hiyo roho ikishinda vita vya mwili. Mwili una akili zake ambazo ni tofauti na roho. Haya ni kwa mujibu wa maandiko matakatifu.

Wagalatia 5:16.17. Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

Andiko la hapo juu linasema, mwili na roho zimepingana au zinatofautiana maamuzi. Ikiwa na maana kuna matakwa ya roho na matakwa ya mwili.

Katika andiko la Wagalatia 5:16.17 Inataja habari ya kuongozwa na Roho, Ikiwa na maana kuongozwa na Roho wa Mungu. Lakini chakuzingatia hapo ni kwamba Roho au roho, zote zinatabia ya kuongoza. Ikiwa na maana hata roho ya binadamu ina sifa ya kuongoza maamuzi ya mwili, au huulazimisha mwili kufanya ambacho roho ya binadamu imekusudia. Kwa kifanya.

Mara nyingi roho ndio inayotegeneza aina ya mtu. Roho ndio ina picha halisi ya kiumbe kuwa ni cha aina gani. Ili kupata aina ya kitu tunahitaji aina ya roho. Na ili kupata aina ya mtu au watu, tunahitaji aina ya roho. Roho ndio inayotengeneza tofauti ya hiki na hiki. Roho ndio inayotengeneza aina ya vizazi (Kabila)

Mithali 30:11.14. Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao. Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao. Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka k**a nini! Na kope zao zimeinuka sana. Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni k**a visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.

Hapo imetaja aina ya vizazi (Binadamu) na tabia zao, sisi binadamu k**a unavyoona mbenu za vitu mbalimbali ambazo hata k**a ni mmea wa aina moja lakini utatofautiana na mwingine kwa kitu fulani au sifa fulani nasi vivyo hivyo. Yesu aliongea kuhusu tabia za kizazi (Roho za kurithi kutoka kwa mababa na mama).

Mathayo 12:34. Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.

Kwa hiyo inaonyesha wazi kuwa kuna tabia nyingine zinatokana na roho za familia au kabila. Yesu amesema tena kuhusu roho za kurithi,

Mathayo 12:39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

Yesu alikitaja kizazi kibaya cha zinaa kinatafuta ishara, Ikiwa na maana ni uzao wenye roho ya uovu, hao hutenda si kwa sababu walifundishwa bali wanatenda kwa sababu ndani yao kuna roho inayowaongoza kutenda uovu hata k**a hawataki. Kuna matendo ndani ya mtu wakati fulani sio maamuzi yake bali ni roho aliyozaliwa nayo ndio inaamua nini afanye au asifanye au awe na tabia gani.

Akili kubadilishwa kwa kuvamiwa na pepo wachafu(roho chafu, shetani).

Kuna ukweli mkubwa kuwa mtu anaweza kubadilishwa akili zake mara tu mtu huyo akivamiwa na mapepo (Majini). Sayansi ya kiroho inathitisha kuwa, pepo anapomuingia mtu, na sehemu muhimu anayoikimbilia ni kwenye akili za mtu.

2 Wakorinto 4:3.4. Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.

Andiko hili linasema kuwa mungu (Shetani) wa dunia hii hupofusha watu fikira zao. Ikiwa na maana mtu akiingiwa na roho chafu, ile roho chafu itapofusha fikira au akili za mtu, ili akili zake huyo mtu zisifanye kazi k**a inavyohitajika, badala yake akili za kipepo zianze kufanya kazi kwa kuchukua nafasi ya akili halisi ya binadamu mwenyewe. Yaani akili ya roho chafu ndio inakuwa tabia na muonekano wa yule mtu.

Uthibitisho wa jinsi roho chafu (Mapepo) zinavyobadilisha akili za mtu.

Luka 8:27.35 Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini. Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese. Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule. Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo, akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo. Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia. Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsi- hi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa. Pepo wakamtoka mtu yule wakawaingia nguruwe, nalo kundi lilitelemka gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa maji. Wachungaji walipoona lililotokea walikimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka kwenda kuliona lililotokea, wakamwendea Yesu, wakamwona mtu yule aliyetokwa na pepo ameketi miguuni pa Yesu, amevaa nguo, ana akili zake; wakaogopa.

Kwa mijibu wa andiko la hapo juu, tumeona mtu ambaye alikuwa amechanganyikiwa akili, alikuwa kichaa na alikuwa mtu hatari sana mwenye tabia za ajabu sana, alikuwa uchi alikuwa na nguvu mno. Lakini kwa mujibu wa maandiko, hali hiyo imesababishwa na mapepo yaliyokuwa ndani ya huyo mtu (Sio tu kuwa ndani ya mtu, bali yalikuwa kwenye akili zake kichwani mwake).

Ni wazi kuna matendo au tabia ndani ya binadamu sio za kawaida, bali ni za kipepo. Wakati fulani mtu akili zake zinaweza kuwa sio za kawaida au anakuwa na matendo ya ajabu, lakini hiyo inatupasa kujua kuwa sio akili za kawaida za huyo mtu.

Kuna ukweli mwingi sana kuhusu pepo wabaya kuingilia mfumo wa akili za binadamu na kuutumia k**a atakavyo na muhusika asijue k**a afanyacho sio yeye.

Labda katika mambo ya mitandao kuna watu wajanja wanaweza au wanautaalamu wa kuingilia akaunti ya mtu katika mtandao maarufu kwa Kingereza ni (Hackers), tafsiri yake kwa kingereza ni a person who uses computers to gain unauthorized access to data.)

Aanapoingilia akaunti ya mtu mwingine anaitumia k**a yeye ndiye mwenye akaunti, na mara kadhaa wanaweza kuposti vitu vya ajabu ajabu hata watu wakashangaa baadae ndipo mwenye akaunti atagundua kuna mtu mwingine anaitumia akaunti yake bila ya kujua amefanyaje hadi akaiingilia akaunti hiyo.

Katika ulimwengu wa roho pia kuna uingiliaji wa kihalifu ambao pepo wabaya hufanya kwa ajili ya upotosha watu na kuwavuruga. Nadhani mwanzilishi wa wahalifu wa kimtandao (Hackers) atakuwa ni shetani. Maana shetani yeye ndiye aliye kuwa (Hacker) wa kwanza kwa kuingilia uhusiano wa binadamu na Mungu na kuuharibu. Leo haya k**a marudio ya matendo ambayo shetani aliyafanya na anaendelea kuyafanya.

Katika sayansi hii ya kiroho, shetani anaweza akazini kupitia mtu kwakutumia akili za mtu, anaweza akaiba, anaweza akaua, anaweza akawa kiburi kupitia mtu, anaweza akawa mkatili sana kupitia mtu, anaweza akawa shoga, anaweza akawa mbakaji, anaweza akawa mchawi, anaweza akawa mtumiaji pesa vibaya hata bila ya kuzihurumia, anaweza akawa mlevi mbwa, (Shetani) yeye anakuwa nyuma ya hayo matukio lakini haonekani yeye bali ataonekana yule binadamu anayetumiwa na shetani hata bila ya yeye kujua.

Huduma ya shetani ni uwalimu wa uongo.
Kazi kubwa ya shetani ni kuwa mwalimu mdanganyifu, tangu Edeni alifanya huduma ya kufundisha uongo.

Mwanzo 3:1.7. Hivyo shetani kazi yake nikuwafanya watu wajifunze mambo ya kuwapotosha, au kuwapoteza au kupoteza hata malengo yao mazuri kupitia udanganyifu wa shetani. Kazi ya shetani ni kumshawishi mtu aamue mambo yatakayompoteza.

Roho za kurithi na uhusiano wake kiakili.
Mtu anapozaliwa katika familia fulani yenye roho fulani, mara nyingi yule mtoto atachukua hali (Akili) ya ile roho ya familia. Ikiwa na maana kuwa, ni kitu cha kuzaliwa nacho sio cha kujifunza.

Anaweza akazaliwa na ujuzi, au ujinga, au utambuzi, au hekima, au ukatiri, au roho mbaya, au uongo, au wizi, au uzinzi, au umalaya wa kuzaliwa.

Kuna matendo ya kujifunza na matendo yaliyoumbika ndani ya mtu tangu kuzaliwa kwake. Mtu atazaliwa na kile kinachofanana na familia yake.

Ndio maana kwa mfano mtu akiwa malaya au mzinzi lakini ule uzinzi sio wa kuiga bali ni wa familia, kuacha kwake ni vigumu sana, na anaweza akazini k**a mbwa au akafanya umalaya k**a hajipendi. Hiyo ni wazi huyo sio malaya wa kufundishwa bali ni malaya wa kuzaliwa nao.

Kwa hiyo basi, kuna ukweli mkubwa kuhusu roho za kurithi kutawala akili za kizazi kitakachozaliwa.

Roho ya taifa/nchi (Spirit of nation), mji, kijiji, eneo, mtaa.
Kila taifa lina roho yake inayotenda kazi, na kila mji una roho yake inayotenda kazi, na kila kijiji au eneo au mtaa lazima kuna roho yake inayotenda kazi katika eneo hilo, na ndio inayoamua watu wawe na mtazamo gani au akili gani.

Huwezi ukawa na akili kupita akili ya taifa lako, au mji wako au kijiji chako au mtaa wako. Na iwapo utajaribu kuwa na akili zaidi ya akili ya mahali husika hilo eneo litakuangamiza au utaishi kwa shida sana.

Na ndio maana kuna umuhimu sana wa kiongozi wa juu awe na roho na akili sahihi, ili nchi iwe na akili kubwa. Niliwahi kwenda taifa fulani, nikagundua kuwa hilo taifa lina roho ya uzinzi sana, nilishawahi kwenda mahali fulani nikagundua hilo eneo kuna roho ya ulevi. Ikiwa na maana k**a utaishi eneo hilo (K**a huna nguvu ya Mungu au neema ya Mungu) nguvu ya ulevi au uzinzi au ujinga itakuvuta uwe sawa na lile eneo.

Jinsi ya kutoka.

1. Njia ya kutoka ni kuzaliwa mara ya pili (Kuokoka), kwa kumuamini Yesu kristo k**a Bwana na mwokozi wa maisha yako, yeye ana uwezo wa kuwafanya wale waliomuamini kuwa watoto wa Mungu.

Yohana 1:12.13 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, kwa Mungu.

Yohana 3:3.7 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.

Biblia inapotaja umuhimu wa kuzaliwa upya(mara ya pili) bila shaka, ina maanisha imetambua kuwa bila ya mtu kubadili aina ya uzaliwa, au kizazi, au roho ya familia ni vigumu kumpende- za Mungu. Au imebaini kuwa asili ya kuzaliwa ni tatizo kubwa katika mtazamo wa binadamu. Bila shaka mtu hawezi kujitoa alipokwama kabla ya kujitoa kwenye tope la kale(asili)

2. Kujifunza kuhusu ukweli huu kuhusu roho zinavyoweza kumiliki akili, na kuweka mpango mkakati wa kuzikataa, na kutafuta mabadiliko.

3. Maombi. Wakati fulani ni vigumu kujitoa katika nguvu za roho za asili yoyote, iwe kuzaliwa, ukoo, au kabila, au taifa pasipo maombi ya kuvunja hizo roho za asili.

4. Maombi kwa ajili ya kuivunja roho ya taifa. 2. Nyakati 7:14
2 Timoseo 2:2.

Kuagiza kitabu au manunuzi ya jumla na rejareja wasiliana nasi kwa 0717528272 /0788170367 / 0755528965.

Roho ya uasi. Kuna mithali inasema “Mvumilivu, hula mbivu” Tumeona jinsi Ruthu alivyokuwa mvumilivu, na hatimaye akavuna...
12/04/2024

Roho ya uasi. Kuna mithali inasema “Mvumilivu, hula mbivu” Tumeona jinsi Ruthu alivyokuwa mvumilivu, na hatimaye akavuna matunda ya uvumilivu wake.

Unapovumili unaweza kuona k**a unapoteza muda, lakini ule uvumilivu hautakutupa mkono, lazima utakuletea matunda yake. Unaweza kushik**ana na mtumishi wa Mungu, lakini huduma ikawa ngumu na ya mapito makubwa, kiasi kwamba haisongi mbele imeganda na mwisho wa yote unaweza kukata tamaa ukidhani Mchungaji hana maono ndio maana mmebaki hapo kwa muda mrefu, kumbe ni kipimo chako cha uvumilivu mbele za Mungu.

Roho ya uasi. Hakuna kitu kibaya k**a roho ya uasi, watu wengi hawana roho ya kuambatana, isipokuwa wana roho ya uasi. Roho ya uasi maana yake ni mtu ambaye hawezi kutunza uaminifu wake kwa kiongozi wake au mtu wake wa karibu. Kuna watu wana asili ya kukosa uaminifu, ni watu ukiwa nao elewa wakati wowote watakuacha. Wewe mtu wa Mungu usiwe mtu uliyekosa uaminifu, na udumu katika uaminifu kwa kiongozi wake na huduma na Bwana atakubariki.

UKIFIKA KATIKA SANDUKU LA KURA!!!!Ukifika katika sanduku la kura, hebu usichague kwa ushabiki wa kisiasa, kwamba mgombea...
13/03/2024

UKIFIKA KATIKA SANDUKU LA KURA!!!!

Ukifika katika sanduku la kura, hebu usichague kwa ushabiki wa kisiasa, kwamba mgombea wa chama chako unajua wazi hana sifa wala uwezo wa kuwa kiongozi, lakini kwa sababu tu ni wa chama chako unamchagua, hilo sio sahihi, chagua sifa na uwezo na maendeleo sio chama.

Tunapochagua kwa upepo wa chama, au uhasama wa vyama, mara zote tutachagua viongozi wasiokuwa na sifa. Kumbuka sisi sote ni Watanzania, hata awe chama chako au sio chama chako, sote tupo nchi moja, na huyo kiongozi atafanya maendeleo sio ya chama chake tu bali atafanya maendeleo ya nchi nzima kwa ujumla wake na maendeleo ya wanachi wote. Uchaguzi wa kuchagua rangi za chama sio uchaguzi wenye tija kwa taifa, bali ni uchaguzi wa upepo wa kisiasa. lIKE PAGE YANGU PLZ Lion A. Mangole

07/03/2024

Bwana awabariki nyote wapendwa.

05/02/2024

Wanaume wanaoumia ni wale wanawadharau wanawake. Wanawaona ni simpo, sio kivile!

22/02/2023

JIPATIE VITABU VYA

LION A MANGOLE, ORODHA NI K**A IFUATAVYO.

1. KUWA NA UWEZO MKUBWA KIAKILI. 20,000
2. Sumu ya Ukuaji wa Kanisa. Chenye masomo ya kuujenga ushirika. 10,000
3. Huduma ya Mchungaji, chenye mwongozo wa ibada maalumu k**a maziko, ubatizo, ndoa, kubariki watoto nk. 10,000
4. Vita katika Madhabahu. 10,000
5. Wajibu wa Mama Mchungaji na Wake wa viongozi wa Kanisa. 5000
6. Ufunguo wa kuzungumza na Waislamu, kina aya 323 za Quran pamoja na majibu ya maswali tata. 10,000
7. Kinga na dawa ya mapenzi kinachofundisha
uchumba hadi ndoa. 5000
8 . Uchumi huru usiokuwa na majuto. Kinachofundisha
uchumi na ujasiriamali. 10,000
9 Kuchinja ni haki ya nani?. 2000
10 Omba k**a Tai Maombi ya upenyo, Kina aina kumi za maombi. 4000
11. Ufunguo wa kuzungumza na Waislamu Toleo maalumu namba 1. 5000
12. Chochote kinaweza kuwa k**a dhahabu. 3000
13. Nguvu ya Agano. 3000
14. Jifunze ukweli kuhusu mavazi. 3000
15. Biashara isiyododa. 3000
16. Kanuni bora za kufanya maombezi (kitabu cha kiongozi &muumini ). 5000
17. Kuwatunza Wazee na Vikongwe. 5000
18 Wamachinga. 5000
19. Sababu 11 za kumuombea Mchungaji wako 4000
20. Maombi ya kuushinda uchawi. 10,000
21. Kuwa Tajiri kwa Mbinu rahisi. 4000
22. Historia Halisi ya Maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w). 10,000
23. Huduma ya Uinjilisti (Kozi ya Kwanza I ). 5000
24. Vita katika Malango ya Familia. 5000
25. Mafisi katika Kanisa. 5000
26. Huduma ya Uinjilisti (Kozi ya II-III). 10,000
27. Kitabu cha, Masomo ya kuukulia Wokovu. 5000.

28. Nyimbo zinazokelewa k**a sadaka kwa Mungu Sh 10,000

Hutajutia kusoma vitabu vya mwandishi Lion Mangole. Kwa sasa kwa hapa Tanzania, ni miongoni mwa vitabu vinavyosomwa zaidi. Aidha, Unaweza kuvipata Mikoa ya Mbeya, Mwanza, Morogoro, Arusha, Dar es salaam na pia tunatuma kwa njia ya magari na kwa posta. Mawasiliano no 0718528272/0755528965/0788170367

06/10/2022
USIACHE KUTAZAMA SOMO HILI YOUTUBE. KISHA SHEA KWA UWAPENDAO, PIA NIKUOMBE K**A HUJA SUBSCRIBE CHANEL YANGU PLZ SUBSRIBE...
13/09/2022

USIACHE KUTAZAMA SOMO HILI YOUTUBE. KISHA SHEA KWA UWAPENDAO, PIA NIKUOMBE K**A HUJA SUBSCRIBE CHANEL YANGU PLZ SUBSRIBE, LIKE, BOFYA ALAMA YA KENGELE.

MAOMBI YA KUUSHINDA UCHAWI - PRAYER TO OVERCOME WITCHCRAFT -Je! Uchawi upo kweli? - Does magic really exist? Waefeso 6:12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si ...

Jiulize. Kwanini video hii hadi sasa ina viewers 5.3 K? ikiwa na maana watu 5300 wameitazama? Tafadhali, ukiingia kwenye...
06/09/2022

Jiulize. Kwanini video hii hadi sasa ina viewers 5.3 K? ikiwa na maana watu 5300 wameitazama? Tafadhali, ukiingia kwenye youtube chanel yangu, subscribe na kisha like na bofya alama ya kengele ili uendelee kupata huduma zangu.

MAHUBIRI. MAOMBI YA KUVUNJA LAANA, MIKOSI NA NUKSI. EFESO 6:10.12 YOHANA, 8:36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli. EFESO 4:27 wala msimpe Ib...

Tazama somo hili kwenye chanel yangu youtube. Pia nakuomba u SUBSRIBE, na like na kubofya alama ya kengele ili kupata ta...
22/08/2022

Tazama somo hili kwenye chanel yangu youtube. Pia nakuomba u SUBSRIBE, na like na kubofya alama ya kengele ili kupata taarifa na mafundisho mara mwa mara. Asante.

Somo la maandiko ya maisha, ni somo ambalo Mchungaji Lion Mangole amedindisha ili ufahamu kwamba, maisha yako hayapo kwa bahari mbaya, bali yapo katika mfumo...

11/08/2022

Somo hili limefundishwa na Mchungaji Lion Mangole, k**a utahitajji CD za mafundisho ya ndoa uwasiliane nasi, pia k**a unahitaji ushauri au maombi au utahitaj...

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255755528965

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Evangelist, Teacher, Pastor. Lion A Mangole posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Evangelist, Teacher, Pastor. Lion A Mangole:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram