Siri Za Ndoa

Siri Za Ndoa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Siri Za Ndoa, Marriage Therapist, lumumba, Dar es Salaam.

|| Jukwaa la mafunzo na ushauri kuhusu siri za Ndoa na Mahusiano | kuangalia changamoto za ndoa na kuzipatia njia ya kukabiliana nazo | huku ukipewa fursa ya kuiboresha ndoa yako ||

🌸 WANAUME, KUWENI NGUZO ZA NYUMBA ZENU 🌸Mwanamke hathamini maneno matamu pekee, bali anahitaji pia:πŸ’ Bega la kutegemea k...
30/09/2025

🌸 WANAUME, KUWENI NGUZO ZA NYUMBA ZENU 🌸

Mwanamke hathamini maneno matamu pekee, bali anahitaji pia:
πŸ’ Bega la kutegemea katika nyakati za dhiki na majaribu,
πŸ’ Mgongo thabiti wa kumsapoti katika siku za udhaifu,
πŸ’ Na mwandani wa kweli atakayeambatana naye katika safari ndefu ya maisha.

πŸ•ŠοΈ Maneno ya upole humtia nguvu,
🌹 Heshima humuinua juu ya hofu na mashaka,
πŸ’« Na moyo wa kumkumbatia humletea amani ya ndani.

πŸ‘©β€πŸ¦± Kuweni kwao nguzo…
Kwa sababu mioyo yao ikipata utulivu:
πŸ’ž Nyumba hububujika mwanga wa mapenzi,
πŸ’ž Hewa hujaa harufu ya utulivu,
πŸ’ž Na maisha hugeuka kuwa furaha isiyo na kikomo.

https://chat.whatsapp.com/EQbA7JXvDfrF5xjwP1azB5?mode=ems_copy_t

✨ Mwanzo wa Baraka, Mwangaza wa Ndoto βœ¨β˜€οΈ Asubuhi daima huangaza zaidi tunapoielekeza mioyo yetu kwenye uzuri wa maisha....
14/09/2025

✨ Mwanzo wa Baraka, Mwangaza wa Ndoto ✨

β˜€οΈ Asubuhi daima huangaza zaidi tunapoielekeza mioyo yetu kwenye uzuri wa maisha.

Ndoto kuu na malengo makubwa hutupa nguvu ya kusonga mbele kwa matumaini na furaha ya kweli. 🌿🌸

Asubuhi njema kwako β€”iwe ni mwanzo wa baraka, mwangaza wa matumaini na utimilifu wa ndoto zako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu insha'Allah.🌸

WAZAZI WETU WALIKUWA WAKWELI – Tuwashukuru na Tuwaheshimu────────────────────────────Kuna wakati katika maisha yetu, has...
15/08/2025

WAZAZI WETU WALIKUWA WAKWELI – Tuwashukuru na Tuwaheshimu
────────────────────────────

Kuna wakati katika maisha yetu, hasa tulipokuwa watoto au vijana, tulidhani kwamba wazazi wetu walikuwa wakitoa visingizio. Tulipowasikia wakisema:

β€œMwanangu, sina pesa… bado sijapata mshahara wa mwezi huu.”

πŸ€¦πŸΎβ€β™‚οΈ Tuliishia kwa huzuni, au pengine tukajihisi kutelekezwa kabisa. Lakini leo, tukiwa tumeingia kwenye majukumu ya maisha, tunaelewa vizuri kwamba walikuwa wakituambia ukweli wa moyo wao.

Msanii maarufu duniani, Idris Elba, aliwahi kusema:
β€œWe all owe our parents an apology for not believing them when they said they don’t have money even on payday.”

Akimaanisha kwamba: ‡️
β€œSote tunapaswa kuwaomba radhi wazazi wetu kwa kutowaamini walipotuambia hawana pesa, hata siku ya mshahara.”

πŸ‘‰πŸΎ Kauli hii si maneno matupu β€” ni sauti ya ukweli inayotufikia moja kwa moja kwenye dhamiri. Wazazi wetu walikuwa askari wa mstari wa mbele katika mapambano ya maisha, wakipigana ili waweze kutupatia makazi, chakula, elimu, na hata furaha ndogo tulizoona k**a za kawaida sana.

πŸ‘¨πŸΏβ€πŸΌ Walikuwa wanajinyima ili sisi tupate. Walikuwa wanavumilia njaa ili Sisi tule. Walikuwa wanavaa nguo zilizochakaa ili sisi tuvae vizuri shuleni. Lakini sisi tulichokiona ni kauli ya kuepuka majukumu tu.

πŸ“ Leo hii, baada ya kupitia gharama za maisha, bili zisizopungua, na majukumu yasiyoisha, tunagundua kwamba hakuna mzazi aliyekuwa akidanganya. Bali wazazi walikuwa wanasema ukweli, ukweli ambao wakati ule sisi tuliuona k**a uongo.

πŸ•— Hii leo, tuchukue muda kuwatambua k**a mashujaa wetu wa kweli. Tuwaombe radhi, tuwashukuru, na zaidi ya yote, tuwape heshima wanayostahili.

🌹 Kwa sababu nyuma ya kila β€œsina pesa” kulikuwa na moyo uliojaa mapenzi, kujitolea, na kujitoa sadaka kwa ajili yetu.

πŸ’¬ Kumbuka: Shukrani isiyosemwa ni deni lisilolipwa.

πŸ€²πŸΎπŸ™πŸ» Usisahau kusambaza ujumbe huu Kwa marafiki zako ili na wao waweze kukumbuka Swala hili na waweze kuwashukuru wazazi wao.

Follow Baaqir Media na ‡️
https://whatsapp.com/channel/0029Vb8HuEw9mrGcbCt1ts27

11/07/2025

Habari za muda rafiki zangu

Hivi karibuni tutaendelea na maswala yote yanayohusu ndoa na Siri zake pamoja na maisha ya mahusiano

Hivyo kuwa karibu na ukurasa huu ili usipitwe

11/07/2025

Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyetuneemesha kwa neema ya uhai mpya, Na kutuamsha katika siku nyingine tukufu katika uumbaji Wake.

EWE MOLA WETU!
🀲🏻 Tunakuomba utupe amani, utulivu na ulinzi katika nchi zetu,

Utujalie usalama na ulinzi katika dini zetu na afya njema katika miili yetu,

πŸ™πŸΎ Uwasamehe wazazi wetu { baba zetu na mama zetu } kwa rehema Zako zisizo na mipaka,

Na uzitie baraka riziki zetu,
Na tunakuomba utujalie Afya kamili katika miili yetu, ili tuweze kukutumikia kwa ikhlasi.

🌸 Asubuhi njema yenye baraka na nuru ya Mola wetu.

09/07/2025

πŸ’” Kila Siku ni Ashura, Kila Ardhi ni Karbala...

{Kila siku ni fursa ya kusimama dhidi ya dhulma, na kila mahali panastahiki kuwa uwanja wa haki.}

Katika siku hizi Tukufu na zenye huzuni kubwa kwa Waislamu wa madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s), tunakumbuka kwa majonzi makubwa tukio la kuuawa shahidi mjukuu wa Mtume (s.a.a.w), Imam Hussein bin Ali (a.s), katika ardhi ya Karbala.

πŸŒ‘ Katika siku hizi Tukufu na za huzuni, ambapo hata mbingu hulia kwa huzuni Kwa ajili ya Imamu Hussein (a.s), BAAQIR MEDIA inatoa salamu za rambirambi kwa Imam wa Zama (a.f) na kwa waumini wote duniani, kwa mnasaba wa nyakati zenye kuumiza za mwezi huu wa Muharram.

πŸ•ŠοΈ Tumuenzi Imam Hussein (a.s) kwa kushik**ana na haki, kulinda misingi ya Uislamu na kupambana na dhulma, na kuendeleza ujumbe wake wa islah na ucha Mungu.

πŸ“Ώ Ewe Mola wetu! tunakuomba utufanye kuwa miongoni mwa wafuasi waaminifu wa njia ya Imamu Hussein (a.s).

Kwa heshima na majonzi, Baaqir Media – Uislamu karibu yako

28/05/2024

🟒 Unaweza kumgeuza mkeo kuwa shujaa wa hadithi za mapenzi.

❀️ Katika hali nyingi, mtu ambaye huchukua hatua ya tendo la ndoa ni mwanaume, na wakati mwingine wanawake hawaonyeshi tamaa zao za tendo la ndoa na hushiriki penzi katika uhusiano huo kwa kusita ( kukosa hamu) na wakati mwingine kwa kulazimishwa.

πŸ’• Lakini ukweli ni kwamba wanawake wengi hawana hasira, na kwa kuwa karibu na mmewe mwenye kumchochea, wanawake hugeuka kutoka viumbe waoga na wanaochukia tendo la ndoa na kuwa mashujaa wa hadithi za upendo.

✍️ Na wewe mwanaume ndio unapaswa kumbadilisha mkeo kuwa shujaa..



Follow πŸ†” Siri Za Ndoa πŸ‘«πŸ’« kwa mambo mengi zaidi

Siku zote Ikiwa hutaki kuwa mgonjwa, ni bora ukaelezea hisia zako!❀️ Kushindwa kueleza hisia, pamoja na kusababisha mata...
27/05/2024

Siku zote Ikiwa hutaki kuwa mgonjwa, ni bora ukaelezea hisia zako!

❀️ Kushindwa kueleza hisia, pamoja na kusababisha matatizo ya kisaikolojia, huongeza uwezekano wa kuteseka na matatizo ya kimwili na magonjwa k**a vile saratani.

✍️ kuwa muwazi tu kwa yule unayempenda ili kuepusha madhara na magonjwa yasiyotakiwa



Follow πŸ†” Siri Za Ndoa πŸ‘«πŸ’«

Chumba cha kulala ambacho kimejaa picha za marehemu, wazazi, babu na bibu, mara nyingi hukumbusha zaidi kumbukumbu za za...
26/05/2024

Chumba cha kulala ambacho kimejaa picha za marehemu, wazazi, babu na bibu, mara nyingi hukumbusha zaidi kumbukumbu za zamani na husababisha mfadhaiko.

✍️ Katika mfadhaiko na kushuka hali ya kujiamini, motisha ya mapenzi huwa ya chini sana!

Follow πŸ†” Siri Za Ndoa πŸ‘«πŸ’«

Address

Lumumba
Dar Es Salaam

Telephone

+255747001440

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Siri Za Ndoa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram