National Institute For Medical Research

National Institute For Medical Research The National Institute for Medical Research (NIMR) is a government research institution under the Ministry for Health established in 1979.

NIMR has the dual mandate to conduct and regulate health research on Tanzania Mainland. The National Institute for Medical Research (NIMR) is the largest public health research institution in Tanzania. It was established by the Parliament Act No. 23 of 1979 as a parastatal organization under the Ministry of Health. The establishment of NIMR was in recognition by the government of the need to generate scientific information required in the development of better methods and techniques of enhancing disease management, prevention and control in the country.

๐“๐ก๐ž ๐œ๐จ๐ฎ๐ง๐ญ๐๐จ๐ฐ๐ง ๐ข๐ฌ ๐จ๐ง! โฐ Seize the opportunity to showcase your research and help shape the future of health in Tanzania.๐Ÿ“Œ...
05/03/2026

๐“๐ก๐ž ๐œ๐จ๐ฎ๐ง๐ญ๐๐จ๐ฐ๐ง ๐ข๐ฌ ๐จ๐ง! โฐ

Seize the opportunity to showcase your research and help shape the future of health in Tanzania.
๐Ÿ“Œ Apply now and be part of advancing evidence-based health solutions in Tanzania!

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ธ๐—ฒ๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐—ž๐˜‚๐—ผ๐—ป๐˜†๐—ฒ๐˜€๐—ต๐—ฎ ๐— ๐˜„๐—ฒ๐—น๐—ฒ๐—ธ๐—ฒ๐—ผ ๐— ๐—ฝ๐˜†๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—ž๐˜‚๐—ท๐—ฒ๐—ป๐—ด๐—ฎ ๐—จ๐˜€๐˜๐—ฎ๐—ต๐—ถ๐—บ๐—ถ๐—น๐—ถ๐˜ƒ๐˜‚ ๐——๐—ต๐—ถ๐—ฑ๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ด๐—ผ๐—ป๐—ท๐˜„๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—น๐—ถ๐—ฝ๐˜‚๐—ธ๐—ผ ๐—ฌ๐—ฎ๐—ป๐—ฎ๐˜†๐—ผ๐˜€๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฏ๐—ถ๐˜€...
01/03/2026

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ธ๐—ฒ๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐—ž๐˜‚๐—ผ๐—ป๐˜†๐—ฒ๐˜€๐—ต๐—ฎ ๐— ๐˜„๐—ฒ๐—น๐—ฒ๐—ธ๐—ฒ๐—ผ ๐— ๐—ฝ๐˜†๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—ž๐˜‚๐—ท๐—ฒ๐—ป๐—ด๐—ฎ ๐—จ๐˜€๐˜๐—ฎ๐—ต๐—ถ๐—บ๐—ถ๐—น๐—ถ๐˜ƒ๐˜‚ ๐——๐—ต๐—ถ๐—ฑ๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ด๐—ผ๐—ป๐—ท๐˜„๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—น๐—ถ๐—ฝ๐˜‚๐—ธ๐—ผ ๐—ฌ๐—ฎ๐—ป๐—ฎ๐˜†๐—ผ๐˜€๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฏ๐—ถ๐˜€๐—ต๐˜„๐—ฎ ๐—ป๐—ฎ ๐—ช๐—ฎ๐—ฑ๐˜‚๐—ฑ๐˜‚ ๐——๐—ต๐˜‚๐—ฟ๐—ถ๐—ณ๐˜‚

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti kuhusu magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu pamoja na usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu, hatua inayolenga kuimarisha ustahimilivu wa taifa katika kukabiliana na vitisho vya magonjwa hayo.
Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Mkurugenzi wa Kuratibu na Kukuza Tafiti, Dkt. Nyanda Elias Ntinginya, amesema Tanzania inahitaji kuimarisha mifumo yake ya ufuatiliaji na maandalizi ili kukabiliana kwa ufanisi na ongezeko la vitisho vya magonjwa yanayoenezwa na mbu.
Amesisitiza kuwa tafiti za kisayansi zinapaswa kuwa msingi wa maamuzi ya kisera, hasa katika kipindi hiki ambacho mabadiliko ya mazingira, ukuaji wa miji na ongezeko la mwingiliano wa watu vinaongeza hatari ya milipuko ya magonjwa k**a dengue na magonjwa mengine ya virusi yanayoenezwa na mbu.
Kwa upande wake, Mtafiti Kiongozi wa Mradi wa RAFT, Dkt. Alphaxard Manjurano, amesema lengo la mkutano huo lilikuwa kuwasilisha matokeo muhimu kuhusu usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu na vitisho vya magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu, pamoja na kuyajadili kwa kina na wadau wakuu wa udhibiti wa wadudu dhurifu nchini.
Akiwasilisha matokeo ya tathmini ya kitaifa ya utayari wa mfumo wa afya kukabiliana na vitisho vya mbu, Dkt. Manjurano alibainisha kuwa licha ya kuwepo kwa vituo 34 vya ufuatiliaji wa malaria (sentinel sites), bado kuna haja ya kuanzisha programu mahsusi ya kitaifa ya ufuatiliaji wa kawaida wa mbu wanaoeneza magonjwa.
โ€œKwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2024, ufuatiliaji wa mbu wa kuanzia hatua za mabuu hadi mbu waliokomaa haujawahi kufanyika kwa mfumo wa kitaifa. Hii inaonesha umuhimu wa kuimarisha mfumo wa utambuzi wa mapema wa hatari za milipuko ya magonjwa ya yanayoenezwa na wadudu,โ€ alisisitiza Dkt. Manjurano.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya kupitia Programu ya Taifa ya Udhibiti wa Malaria, Bw. Winfred Mwafongo, amesema matokeo hayo yatasaidia kuboresha sera na miongozo ya kukabiliana na malaria na magonjwa mengine yanayoenezwa na wadudu.
Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Jovin Kitau, ameipongeza NIMR kwa kufanya utafiti huo, akisema utachangia kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu na kuongeza usalama wa afya ya umma.
Aidha, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, Dkt. William Kisinza, amesema katika majadiliano ya kikao hicho wadau wamependekeza kuimarishwa kwa programu maalumu inayosimamia masuala ya wadudu dhurifu ili kuongeza ufanisi wa udhibiti wa magonjwa yanayoenezwa na wadudu.
Kwa upande wake, Bi. Jackeline Martin, Mtafiti kutoka NIMR aliyefanya utafiti kuhusu ufanisi wa viuatilifu vilivyopo kwenye vyandarua, amesema matokeo yanaonesha ongezeko la usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu hivyo, jambo linaloonesha umuhimu wa kuendelea kuboresha mikakati ya udhibiti ili kuhakikisha vyandarua vinaendelea kuwa na ufanisi.
Mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Protea, jijini Dar es Salaam, uliwakutanisha wadau mbalimbali wa udhibiti wa wadudu dhurifu kutoka Wizara ya Afya, NIMR, Shirika la Afya Duniani (WHO), Taasisi ya Afya ya Ifakara, pamoja na wadau wengine wa sekta ya afya.
.

28/02/2026

NIMR yazindua utafiti wa utoaji dawa ya kichocho kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5

๐—ญ๐—œ๐—”๐—ฅ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐— ๐—ž๐—จ๐—ฅ๐—จ๐—š๐—˜๐—ก๐—ญ๐—œ ๐— ๐—ž๐—จ๐—จ ๐—ช๐—” ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ž๐—œ๐—ง๐—จ๐—ข ๐—–๐—›๐—” ๐—ง๐—”๐—ก๐—š๐—” ๐—ฌ๐—”๐—œ๐— ๐—”๐—ฅ๐—œ๐—ฆ๐—›๐—” ๐— ๐—ช๐—˜๐—Ÿ๐—˜๐—ž๐—˜๐—ข ๐—ช๐—” ๐—ง๐—”๐—™๐—œ๐—ง๐—œ ๐—ญ๐—œ๐—ก๐—”๐—ญ๐—ข๐—Ÿ๐—˜๐—ก๐—š๐—” ๐— ๐—”๐—›๐—œ๐—ง๐—”๐—๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ง๐—”๐—œ๐—™๐—”Mkurugenzi M...
26/02/2026

๐—ญ๐—œ๐—”๐—ฅ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐— ๐—ž๐—จ๐—ฅ๐—จ๐—š๐—˜๐—ก๐—ญ๐—œ ๐— ๐—ž๐—จ๐—จ ๐—ช๐—” ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ž๐—œ๐—ง๐—จ๐—ข ๐—–๐—›๐—” ๐—ง๐—”๐—ก๐—š๐—” ๐—ฌ๐—”๐—œ๐— ๐—”๐—ฅ๐—œ๐—ฆ๐—›๐—” ๐— ๐—ช๐—˜๐—Ÿ๐—˜๐—ž๐—˜๐—ข ๐—ช๐—” ๐—ง๐—”๐—™๐—œ๐—ง๐—œ ๐—ญ๐—œ๐—ก๐—”๐—ญ๐—ข๐—Ÿ๐—˜๐—ก๐—š๐—” ๐— ๐—”๐—›๐—œ๐—ง๐—”๐—๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ง๐—”๐—œ๐—™๐—”

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Profesa Said Aboud, tarehe 24 Februari 2026, ametembelea Kituo cha Utafiti cha NIMR Tanga katika ziara ya kikazi iliyolenga kuimarisha mwelekeo wa tafiti na mashirikiano ya kitaasisi.
Kituo cha NIMR Tanga ni miongoni mwa vituo vinara vya tafiti za majaribio ya kitabibu (clinical trials) na tafiti za magonjwa ya binadamu, kikijikita katika kushughulikia magonjwa ya kuambukiza pamoja na vipaumbele vingine vya afya ya umma. Tafiti zinazoendelea katika kituo hicho zinahusisha malaria, maambukizi mapya ya virusi vinavyoenezwa na wadudu dhurifu (arboviral infections), ugonjwa wa Mpox, usugu wa vimelea dhidi ya dawa (AMR), pamoja na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs) k**a vile Usubi, Matende na Mabusha, pamoja na kifafa. Aidha, kituo kinafanya tafiti bunifu zinazoangazia uhusiano kati ya mabadiliko ya tabianchi na afya ya binadamu.
Katika ziara hiyo, Profesa Aboud alipata fursa ya kujionea miradi inayoendelea na kuzungumza na watafiti pamoja na watumishi wa kituo hicho. Alitoa maelekezo na ushauri wa kitaalamu utakaosaidia kuimarisha mikakati ya utekelezaji wa tafiti kwa kuendana kikamilifu na mpango mkakati wa taasisi pamoja na vipaumbele vya afya vya taifa.
Akizungumza na watumishi, Profesa Aboud alisisitiza umuhimu wa tafiti kujikita katika mahitaji halisi ya jamii. โ€œTafiti lazima zijikite moja kwa moja katika kutoa shahidi za kisayansi ili kushughulikia mahitaji na vipaumbele vya ndani, hususan magonjwa yasiyoambukiza yanayoongezeka kwa kasi na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini,โ€ alisisitiza.
Aidha, alihimiza kuimarishwa kwa mashirikiano kati ya vituo vya NIMR, wadau wa ndani na wa kimataifa pamoja na jamii, ili kuimarisha mifumo ya afya na kuongeza tija za tafiti. Aliwataka watafiti kutumia mitandao, ubia na mshirikiano mpana ili kukabiliana na mabadiliko na changamoto katika mazingira ya tafiti yanayobadilika kwa kasi.
Profesa Aboud pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, sheria, taratibu, kanuni na miongozo ya Serikali akibainisha kuwa uadilifu, uwajibikaji na weledi ni msingi wa mafanikio ya pamoja na ubora endelevu wa taasisi.
Kwa upande wao, Meneja wa Kituo cha NIMR Tanga alimshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa ziara hiyo akieleza kuwa imetoa hamasa mpya kwa watumishi wakiwemo watafiti kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kujituma na ubunifu zaidi. Alisema ujio wa kiongozi huyo umedhihirisha dhamira ya Menejimenti ya NIMR ya kusikiliza, kuimarisha na kuunga mkono kazi zinazofanywa katika vituo vya utafiti nchini, huku wakiahidi kuendeleza tafiti zenye ubora wa hali ya juu zitakazochangia ushahidi wa kisayansi katika kuboresha sera na huduma za afya kwa manufaa ya jamii.

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ ๐—˜๐—”๐—›๐—ฅ๐—– ๐—Ÿ๐—ฎ๐˜‚๐—ป๐—ฐ๐—ต ๐—Ÿ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ๐—บ๐—ฎ๐—ฟ๐—ธ ๐—ก๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ฎ๐—น ๐—ช๐—ผ๐—ฟ๐—ธ๐˜€๐—ต๐—ผ๐—ฝ ๐—ผ๐—ป ๐—˜๐˜ƒ๐—ถ๐—ฑ๐—ฒ๐—ป๐—ฐ๐—ฒ-๐—•๐—ฎ๐˜€๐—ฒ๐—ฑ ๐—›๐—ฒ๐—ฎ๐—น๐˜๐—ต๐—ฐ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฒThe National Institute for Medical Research...
21/02/2026

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ ๐—˜๐—”๐—›๐—ฅ๐—– ๐—Ÿ๐—ฎ๐˜‚๐—ป๐—ฐ๐—ต ๐—Ÿ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ๐—บ๐—ฎ๐—ฟ๐—ธ ๐—ก๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ฎ๐—น ๐—ช๐—ผ๐—ฟ๐—ธ๐˜€๐—ต๐—ผ๐—ฝ ๐—ผ๐—ป ๐—˜๐˜ƒ๐—ถ๐—ฑ๐—ฒ๐—ป๐—ฐ๐—ฒ-๐—•๐—ฎ๐˜€๐—ฒ๐—ฑ ๐—›๐—ฒ๐—ฎ๐—น๐˜๐—ต๐—ฐ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฒ

The National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the East African Health Research Commission (EAHRC), have launched the 1st National Workshops on Ethics and Clinical Research to strengthen Tanzaniaโ€™s capacity to generate ethical, high-quality research evidence that is critical for improving healthcare outcomes.
The workshop equips health professionals with essential knowledge and practical skills in ethics and clinical research while highlighting regional support mechanisms that are available through EAHRC to promote research excellence.
Speaking at the opening ceremony, NIMR Director General, Prof. Said S. Aboud, emphasized the central role of research in improving public health outcomes across East Africa and urged participants to utilise existing health data to generate meaningful evidence actively.
โ€œWe already have a wealth of data in our health facilities. What we must do is to transform the available health data into research evidence. Turning data into actionable knowledge is key to advancing evidence-based healthcare,โ€ he said.
The Director of Research Coordination and Promotion, Dr. Nyanda Ntinginya, oversaw the conduct of this landmark national workshop.
The East African Health Research Commission serves as a regional advisory body supporting knowledge generation, technological advancement, and harmonized research practices across East Africa.
The five-day intensive training, held from 17thโ€“21st February 2026 at the Golden Tulip Hotel, in Dar es Salaam brought together health professionals from across Tanzania Mainland and Zanzibar including clinicians, epidemiologists, researchers, academicians, and other experts from Government and private institutions such as research organizations, universities, hospitals, and NGOs. NIMR has formal MoUs with many of these institutions fostering structured collaborations that support capacity building, mentorship and promotion of health research particularly among early career scientists. The workshop thus aimed to strengthen research capacity and promote ethical evidence-based healthcare across the region.

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜‡๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐˜‚๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ผ๐—ฎ๐—ท๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐——๐—ฎ๐˜„๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—ž๐—ถ๐—ฐ๐—ต๐—ผ๐—ฐ๐—ต๐—ผ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐—ช๐—ฎ๐˜๐—ผ๐˜๐—ผ ๐‚๐ก๐ข๐ง๐ข ๐ฒ๐š ๐Œ๐ข๐š๐ค๐š ๐Œ๐ข๐ญ๐š๐ง๐จ ๐—ž๐˜‚๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ฎ ๐— ๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฆ๐—ง๐—˜๐—ฃ๐—ฃ๐—ฆTaasisi ya T...
19/02/2026

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜‡๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐˜‚๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—จ๐˜๐—ผ๐—ฎ๐—ท๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐——๐—ฎ๐˜„๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—ž๐—ถ๐—ฐ๐—ต๐—ผ๐—ฐ๐—ต๐—ผ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐—ช๐—ฎ๐˜๐—ผ๐˜๐—ผ ๐‚๐ก๐ข๐ง๐ข ๐ฒ๐š ๐Œ๐ข๐š๐ค๐š ๐Œ๐ข๐ญ๐š๐ง๐จ ๐—ž๐˜‚๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ฎ ๐— ๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฆ๐—ง๐—˜๐—ฃ๐—ฃ๐—ฆ

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa STEPPS (Strengthening Health System Capacity for Access and Delivery of Paediatric Praziquantel for Schistosomiasis in Tanzania) tarehe 18 Februari 2026 imezindua rasmi Utafiti wa utoaji wa dawa ya kichocho aina ya paediatric praziquantel kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, hatua inayopanua wigo wa matibabu kwa kundi ambalo kwa muda mrefu halikujumuishwa katika kampeni za utoaji dawa kwa pamoja. Uzinduzi huo umefanyika jijini Mwanza wakati wa Warsha ya Wadau ya kuanza kwa utoaji wa dawa hiyo chini ya Mradi wa STEPPS.
Akizindua rasmi utafti huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, amesema hatua hiyo ni ya kihistoria kwa Tanzania, hasa baada ya nchi kuwa ya kwanza katika ukanda huu na huenda duniani kusajili dawa ya paediatric praziquantel. Ameongeza kuwa matokeo ya mwisho ya utekelezaji wa mradi huo yataisaidia Serikali kuiingiza dawa hiyo katika mwongozo rasmi wa utoaji wa huduma za afya nchini. Ameeleza kuwa ushahidi wa kisayansi uliokusanywa kwa zaidi ya muongo mmoja umeonesha kuwa watoto chini ya miaka mitano wanaoishi katika maeneo yenye maambukizi makubwa ya kichocho wanaweza pia kuambukizwa, hali iliyosukuma juhudi za kutafuta mfumo maalumu wa dawa kwa kundi hilo la watoto chini ya miaka mitano. Aidha, amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada za kupambana na ugonjwa huo kupitia utoaji wa elimu kwa jamii, utekelezaji wa afua za kinga na tiba pamoja na kuboresha usimamizi wa maji katika maeneo yenye maambukizi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema uzinduzi huo ni matokeo ya safari ndefu ya utafiti, ubunifu na ushirikiano wa kimataifa ulioanza mwaka 2020 kupitia Mradi wa STEPPS. Amefafanua kuwa katika hatua ya utekelezaji, mifumo miwili jumuishi ya utoaji dawaโ€”Test and Treat na Mass Drug Administration (MDA)โ€”ilijaribiwa ili kubaini njia bora yenye ufanisi, gharama nafuu na inayokubalika zaidi kwa jamii kabla ya upanuzi wa kitaifa.
Naye Mtafiti Kiongozi wa mradi huo, Dkt. Paul Erasto Kazyoba, amesema tafiti zimeonesha kuwa watoto chini ya umri wa miaka mitano pia wana maambukizi ya kichocho, ilhali awali afua za dawa zililenga zaidi watoto wa umri wa kwenda shule kuanzia miaka sita. Ameongeza kuwa dawa hiyo imefanyiwa majaribio na imeonesha usalama na ufanisi kwa watoto wadogo, ikiwa na maboresho makubwa ikilinganishwa na dawa ya awali, ikiwemo kupunguza usumbufu uliokuwa ukijitokeza kwa baadhi ya watumiaji. Amesisitiza kuwa mradi huo umejengwa juu ya ushirikiano kati ya NIMR, Wizara ya Afya na washirika wa maendeleo wakiwemo UNDP, WHO/TDR na PATH, kwa ufadhili wa GHIT Fund ya Japan pamoja na END FUND.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa UNDP na Naibu Mwakilishi Mkazi wa Tanzania, Bw. John Rutere, amesema taasisi hiyo imeona umuhimu wa kushirikiana na NIMR, Serikali na wadau wengine katika kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata dawa stahiki ya kutibu kichocho, akibainisha kuwa ushirikiano huo utaendelea si tu katika kudhibiti kichocho bali pia katika kushughulikia changamoto nyingine za afya ya jamii. Naye Bi. Grace Bahati, mkazi wa Kijiji cha Ishayahisho, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, ameishukuru NIMR kwa mradi huo wa utafiti akisema utasaidia kubaini maambukizi ya kichocho mapema na kuwapatia watoto dawa, hatua itakayochangia kulinda afya ya jamii.
Warsha hiyo imewakutanisha wadau kutoka ndani na nje ya nchi kujadili mikakati ya kuongeza upatikanaji wa dawa hiyo nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, sambamba na kuimarisha mifumo ya afya kwa ajili ya kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ifikapo mwaka 2030. Warsha hiyo ilitanguliwa na ziara ya kutembelea maeneo ambayo utafiti unafanyika, ikiwamo Hospitali ya Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, ambapo wadau walijionea zoezi la utambuzi wa ugonjwa na ugawaji wa dawa likiendelea.

๐‚๐š๐ง ๐ฒ๐จ๐ฎ๐ซ ๐‘๐ž๐ฌ๐ž๐š๐ซ๐œ๐ก ๐ข๐ง๐Ÿ๐ฅ๐ฎ๐ž๐ง๐œ๐ž ๐๐จ๐ฅ๐ข๐œ๐ฒ ๐š๐ง๐ ๐๐ซ๐ข๐ฏ๐ž ๐ซ๐ž๐š๐ฅ ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐ž ๐ข๐ง ๐ญ๐ก๐ž ๐‡๐ž๐š๐ฅ๐ญ๐ก ๐’๐ž๐œ๐ญ๐จ๐ซ?Researchers in Tanzania with ongoing or co...
16/02/2026

๐‚๐š๐ง ๐ฒ๐จ๐ฎ๐ซ ๐‘๐ž๐ฌ๐ž๐š๐ซ๐œ๐ก ๐ข๐ง๐Ÿ๐ฅ๐ฎ๐ž๐ง๐œ๐ž ๐๐จ๐ฅ๐ข๐œ๐ฒ ๐š๐ง๐ ๐๐ซ๐ข๐ฏ๐ž ๐ซ๐ž๐š๐ฅ ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐ž ๐ข๐ง ๐ญ๐ก๐ž ๐‡๐ž๐š๐ฅ๐ญ๐ก ๐’๐ž๐œ๐ญ๐จ๐ซ?
Researchers in Tanzania with ongoing or completed studies on Cancer and Neglected Tropical Diseases (NTDs) are invited to submit abstracts for a Virtual Policy Brief Write-shop organized by the National Institute for Medical Research (NIMR).
Selected participants will receive structured virtual training to develop high-quality policy briefs, which will be published in the Tanzania Journal of Health Research (TJHR) and presented at a national policy dialogue.
๐Ÿ—“ Submission Deadline: 28 March 2026
๐Ÿ”— More info: nimr.or.tz/policy-brief-workshop
๐Ÿ“ž Contact: +255 758 777 704 | +255 719 563 662
๐€๐œ๐ญ ๐ง๐จ๐ฐ! ๐๐ฎ๐ญ ๐ฒ๐จ๐ฎ๐ซ ๐ซ๐ž๐ฌ๐ž๐š๐ซ๐œ๐ก ๐จ๐ง ๐ญ๐ก๐ž ๐ฉ๐จ๐ฅ๐ข๐œ๐ฒ ๐ฆ๐š๐ฉ ๐š๐ง๐ ๐ฆ๐š๐ค๐ž ๐š ๐๐ข๐Ÿ๐Ÿ๐ž๐ซ๐ž๐ง๐œ๐ž.

๐‹๐š๐ฎ๐ง๐œ๐ก๐ข๐ง๐  ๐๐„๐ƒ๐ˆ๐€๐“๐‘๐ˆ๐‚ ๐๐‘๐€๐™๐ˆ๐๐”๐€๐๐“๐„๐‹ ๐ƒ๐ž๐ฅ๐ข๐ฏ๐ž๐ซ๐ฒ ๐ข๐ง ๐“๐š๐ง๐ณ๐š๐ง๐ข๐š!On 18th February 2026, Tanzania takes a bold step in protecting ch...
16/02/2026

๐‹๐š๐ฎ๐ง๐œ๐ก๐ข๐ง๐  ๐๐„๐ƒ๐ˆ๐€๐“๐‘๐ˆ๐‚ ๐๐‘๐€๐™๐ˆ๐๐”๐€๐๐“๐„๐‹ ๐ƒ๐ž๐ฅ๐ข๐ฏ๐ž๐ซ๐ฒ ๐ข๐ง ๐“๐š๐ง๐ณ๐š๐ง๐ข๐š!
On 18th February 2026, Tanzania takes a bold step in protecting childrenโ€™s health. The National Institute for Medical Research (NIMR), with global partners like WHO, UNICEF, Merck, PATH, and more, is rolling out paediatric praziquantel to fight schistosomiasis.
This milestone marks a critical move toward safer, healthier futures for children across Tanzania and East Africa.
๐Ÿ“ Malaika Beach Resort, Mwanza, Tanzania
๐Ÿ’ก Stay tuned for updates on this game-changing initiative!

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ป๐—ฎ ๐—›๐—ผ๐˜€๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ฎ๐—น๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ง๐—ฎ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—”๐—ณ๐˜†๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—”๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ถ ๐— ๐—ถ๐—ฟ๐—ฒ๐—บ๐—ฏ๐—ฒ ๐—ญ๐—ฎ๐˜€๐—ฎ๐—ถ๐—ป๐—ถ ๐—›๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—ฏ๐—ฎ๐—น๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ผ ๐—ž๐˜‚๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ฟ๐—ถ๐—ธ๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ธ๐—ฎ ๐—ง๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐—ก๐—ฐ๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ถTaasisi...
13/02/2026

๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ป๐—ฎ ๐—›๐—ผ๐˜€๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ฎ๐—น๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ง๐—ฎ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—”๐—ณ๐˜†๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—”๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ถ ๐— ๐—ถ๐—ฟ๐—ฒ๐—บ๐—ฏ๐—ฒ ๐—ญ๐—ฎ๐˜€๐—ฎ๐—ถ๐—ป๐—ถ ๐—›๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—ฏ๐—ฎ๐—น๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ผ ๐—ž๐˜‚๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ฟ๐—ถ๐—ธ๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ธ๐—ฎ ๐—ง๐—ฎ๐—ณ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐—ก๐—ฐ๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ถ

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe (MNMH) leo tarehe 13/02/2026 zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) inayolenga kuimarisha mashirikiano katika tafiti, mafunzo na matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa huduma bora za afya ya akili nchini.
Kupitia ushirikiano huu, taasisi hizo zitaongeza uwezo wa wataalamu wa afya ya akili kupitia mafunzo na tafiti shirikishi zitakazotoa ushahidi wa kisayansi kwa lengo la kuboresha sera, miongozo na utoaji wa huduma kwa kutumia teknolojia za kisasa ili kuongeza ufanisi na ubora kwa wananchi. Ushirikiano huo pia utahusisha utekelezaji wa pamoja wa miradi ya utafiti, kuandika machapisho ya kitaaluma, kuandaa vijarida sera na ushawishi katika kuboresha huduma kwa wananchi.
Makubaliano haya yanakusudia kupanua wigo wa tafiti katika eneo la afya ya akili, kuunganisha utaalamu, matumizi ya rasilimali watu wenye ubobezi na uzoefu wa taasisi hizo, na kuhakikisha matokeo ya tafiti yanawafikia wananchi na kuleta mabadiliko chanya katika maisha yao.
Hafla ya utiaji saini imefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya NIMR jijini Dodoma na kuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, akiwa na Meneja wa Kituo cha NIMR Dodoma, Dk. Basiliana Emidi. Kwa upande wa MNMH, ujumbe uliongozwa na Dk. Innocent R. Mwombeki aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji, akiongozana na Veronica Haule na Anewa Saweni.
.

13/02/2026
๐๐ˆ๐Œ๐‘ ๐˜๐š๐ฐ๐š๐ง๐จ๐š ๐–๐š๐ญ๐ฎ๐ฆ๐ข๐ฌ๐ก๐ข ๐ฐ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐š ๐‡๐จ๐ฌ๐ฉ๐ข๐ญ๐š๐ฅ๐ข ๐ฒ๐š ๐‘๐ฎ๐Ÿ๐š๐š ๐ฒ๐š ๐Œ๐ค๐จ๐š ๐€๐ฆ๐š๐ง๐š ๐Š๐ฎ๐š๐ง๐๐ข๐ค๐š ๐Œ๐š๐š๐ง๐๐ข๐ค๐จ ๐ฒ๐š ๐”๐ญ๐š๐Ÿ๐ข๐ญ๐ข ๐Š๐ฎ๐›๐จ๐ซ๐ž๐ฌ๐ก๐š ๐‡๐ฎ๐๐ฎ๐ฆ๐š ๐ณ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐šTaa...
12/02/2026

๐๐ˆ๐Œ๐‘ ๐˜๐š๐ฐ๐š๐ง๐จ๐š ๐–๐š๐ญ๐ฎ๐ฆ๐ข๐ฌ๐ก๐ข ๐ฐ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐š ๐‡๐จ๐ฌ๐ฉ๐ข๐ญ๐š๐ฅ๐ข ๐ฒ๐š ๐‘๐ฎ๐Ÿ๐š๐š ๐ฒ๐š ๐Œ๐ค๐จ๐š ๐€๐ฆ๐š๐ง๐š ๐Š๐ฎ๐š๐ง๐๐ข๐ค๐š ๐Œ๐š๐š๐ง๐๐ข๐ค๐จ ๐ฒ๐š ๐”๐ญ๐š๐Ÿ๐ข๐ญ๐ข ๐Š๐ฎ๐›๐จ๐ซ๐ž๐ฌ๐ก๐š ๐‡๐ฎ๐๐ฎ๐ฆ๐š ๐ณ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐š

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa maandiko ya utafiti (Proposal Development), hatua inayolenga kuboresha huduma za afya kwa jamii kupitia tafiti zenye ubora na ushahidi wa kisayansi.
Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 26 hadi 29 Januari 2026 katika hospitali hiyo yakilenga kuwawezesha watoa huduma wa afya kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi zinazoweza kupata ufadhili na kuleta matokeo chanya katika sekta ya afya.
Kupitia mafunzo hayo ya vitendo, washiriki walipata ujuzi wa kuandaa maandiko ya kisayansi yenye viwango, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kitaaluma, kuelewa na kuzingatia maadili ya utafiti pamoja na kutumia takwimu sahihi katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili wananchi.
Akifungua mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Bryceson Loti Kiweru, alisema utafiti ni nyenzo muhimu isiyoweza kuepukika katika sekta ya afya.
โ€œSwala zima la utafiti haliepukiki katika sekta ya afya na inahitajika ushirikiano na taasisi zinazofanya utafiti ili kuboresha huduma za afya nchini,โ€ alisema Dkt. Kiweru.
Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Tafiti kutoka kituo cha NIMR Muhimbili, Dkt. Ester Mbutolwe, alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi ya takwimu katika kuibua suluhisho la changamoto za afya.
โ€œKila mtu akijengewa uwezo vizuri anaweza kutoa mchango wake katika kuboresha afya za wananchi. Takwimu sahihi ni msingi wa utafiti wenye matokeo ya kuaminika. Ushirikiano kati ya NIMR na hospitali za rufaa za mkoa ni muhimu,โ€ alisisitiza Dkt. Mbutolwe.
Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za NIMR za kuimarisha tafiti za afya nchini kwa kuwajengea uwezo wataalamu walioko kwenye vituo vya kutolea huduma, ili tafiti zinazofanyika ziweze kutoa majibu ya changamoto halisi za jamii na kuboresha ubora wa huduma za afya nchini.

๐—ช๐—ฅ๐—”๐—œ๐—ฅ ๐——๐—ฒ๐—น๐—ฒ๐—ด๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป ๐—ฉ๐—ถ๐˜€๐—ถ๐˜๐˜€ ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅโ€“๐— ๐—ฏ๐—ฒ๐˜†๐—ฎ ๐—–๐—ฒ๐—ป๐˜๐—ฟ๐—ฒ ๐˜๐—ผ ๐—”๐—ฑ๐˜ƒ๐—ฎ๐—ป๐—ฐ๐—ฒ ๐—›๐—œ๐—ฉ ๐—ฅ๐—ฒ๐˜€๐—ฒ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฐ๐—ต ๐—–๐—ผ๐—น๐—น๐—ฎ๐—ฏ๐—ผ๐—ฟ๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ปThe National Institute for Medical Resear...
12/02/2026

๐—ช๐—ฅ๐—”๐—œ๐—ฅ ๐——๐—ฒ๐—น๐—ฒ๐—ด๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป ๐—ฉ๐—ถ๐˜€๐—ถ๐˜๐˜€ ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅโ€“๐— ๐—ฏ๐—ฒ๐˜†๐—ฎ ๐—–๐—ฒ๐—ป๐˜๐—ฟ๐—ฒ ๐˜๐—ผ ๐—”๐—ฑ๐˜ƒ๐—ฎ๐—ป๐—ฐ๐—ฒ ๐—›๐—œ๐—ฉ ๐—ฅ๐—ฒ๐˜€๐—ฒ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฐ๐—ต ๐—–๐—ผ๐—น๐—น๐—ฎ๐—ฏ๐—ผ๐—ฟ๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป

The National Institute for Medical Research โ€“ Mbeya Medical Research Centre (NIMR-MMRC) on 10th February 2026 hosted a high-level delegation from Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR) in a strategic visit aimed at strengthening collaboration in HIV and clinical research. The delegation was led by Commander Colonel (COL) Brianna Perata and accompanied by senior representatives from WRAIR-USA, WRAIR-Tanzania and CDC-Tanzania, as well as officials from the Ministry of Foreign Affairs and East Africa Cooperation and the Regional Commissionerโ€™s Office in Mbeya.
The visit marked a significant milestone in the long-standing partnership between WRAIR and NIMR, particularly under PEPFAR-supported HIV research programs, reinforcing joint efforts to advance scientific innovation and improve public health outcomes.
The WRAIR delegation was officially received and welcomed at NIMR-MMRC by the Director General of NIMR, Prof. Said Aboud. In a notable highlight of the event, NIMR-MMRC was awarded a Medal of Excellence by COL Brianna Perata in recognition of the outstanding contributions to medical research and public health in Tanzania. During his remarks, Prof. Aboud reaffirmed NIMRโ€™s commitment to advancing high-quality, impactful research through strong global partnerships.
During the visit, the delegation received a comprehensive overview of ongoing clinical trials and collaborative research initiatives at the Centre. Presentations were delivered by the Centre Manager, Dr. Bariki Mtafya, and the Director of Research Coordination, Dr. Nyanda Elias Ntinginya, highlighting the Centreโ€™s growing role in HIV and TB research; cohort, epidemiological, vaccines including broad neutralizing antibodies (bNAbs), drugs, therapeutics, biomarkers, diagnostics and preventive therapy.
The delegation toured key research facilities including the HIV Vaccine Trial Clinics, the state-of-the-art main laboratory accredited by the College of American Pathologists (CAP), and the DAIDS/NIH-certified pharmacy, where ongoing clinical research activities were showcased. The technical teams demonstrated the Centreโ€™s operational excellence and research capacity. Prof. Aboud accompanied the Commander and her delegation throughout the tour, underscoring the importance of the collaboration.
The engagement reaffirmed the strong partnership between NIMR-MMRC and WRAIR and emphasized a shared commitment to advancing cutting-edge research to improve health outcomes in Tanzania and beyond.
research /NIH

Address

3 Barack Obama Drive
Dar Es Salaam
P.O.BOX9653

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when National Institute For Medical Research posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to National Institute For Medical Research:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram