26/07/2024
LIJUE, LIISHI ,ACHA ALAMA KATIKA KUSUDI LA KUUMBWA KWAKO: ✍️
Kwa nini hili somo kwako mda huu,
>Ukombozi wa kwanza wa mtu ni kufahamu kipi sahihi zaidi
>Kuna ongezeko la vijana wengi waliojikuta kwenye pressure ya kimaamuzi kwani kila analoliona likifanywa na wengine na yeye anataka kulifanya na baadae halifanikiwi na kukata tamaa (Dying before death) ~Hongera kwa kulifahamu hili mapema 👋
>lawama nyingi zinapelekwa kwa matendo yasiyo ya kimaadili kwa vijana sababu ni moja tu kukosa (kufahamu, uvumilivu, Imani) katika maono
anaye potea ni yule anaye jua anaelekea wapi na ni rahisi kurekebisha makosa yake
Mambo matano (05) yatakayoweza kukufunulia wewe ni nani /Umebeba nini kwa jamii yako hata taifa kiujumla;
1.Angalia vitu unavyo vipenda /kuvutiwa navyo
(Na ukivibadilisha vinakuwa faida kwa jamii na hatimaye vinaweza kukuingizia kipato)
Mfano;
Uimbaji ,uchoraji ,biashara, ufugaji, ubunifu ......
2.Angalia vitu ambavyo unatamani kuona vinabadilika kwenye jamii lakini kwa sababu ya uwezo wako wa sasa huwezi kufanya hivyo
>ila una imani ukipewa muda na maarifa yakutosha kuhusu hilo jambo unaweza kulifanya
Mfano :Uongozi /siasa
3.Vitu ambavyo unapenda kutumia sana muda wako mwingi
>Zingatia vitu hivi lazima viwe na uwezo wa kukuletea faida na jamii inahitaji/itafaidika navyo utakapo amua kuvibadili Mfano, kuimba ...
4.Jambo ambalo ukilifanya furaha yako ni kuona linakuwa na msaada kwa we wenzako kwanza hata k**a hautalipwa kwa muda huo inabaki kuwa furaha
>Baadhi ya watu kuongoza kikundi cha watu ni rahisi na ndio furaha yao
5.Jambo ambalo unahisi ingekuwa ni maamuzi yako bila msukumo kutoka kwa wazazi,familia/marafiki ungelifanya
>Ndoto nyingi zinapotea kutokana na kushinikizwa kutoka nje
unahitaji uhusiano mkubwa baina yako na Mungu ili Ufanye maamuzi sahihi na salama kwa kesho yako
Stay blessed 🙌
YOUTH FOR HERITAGE
TALENT WITHOUT FEAR OF GOD IS LIKE A POISON IN THE SOCIETY