01/07/2024
Licha ya kwamba watu wanaoongoza kwa utajiri duniani wengi wao wametoka kwenye kiwanda cha internet, Bill Gates(Microsoft), Mark Zuckerberg(Facebook - Meta), Larry page na Sergey Brin (Google - Alphabet), Jeff Bezos(Amazon) na wengine wengi. Nasisi Africa tutafika huko.
Hebu tupia jicho kwenye biashara ya Kilimo kwanza.
Chakula lazima kiliwe hata k**a maisha yatakuwa magumu kiasi gani, Hivyo mazao ya chakula k**a nafaka, mahindi, maharagwe na mpunga ndiyo mazao yanayoongoza kwa kuliwa sana kwenye jamii zetu.
Hivyo hili ni eneo ambalo unaweza kuingia kibiashara na ukafanya vizuri.
Unaweza kuingia kwenye kilimo moja kwa moja na ukalima kibiashara, kwa njia ambayo utazalisha kwa kiwango kikubwa na kwa ubora wa kuweza kuuza.
Lakini pia k**a huwezi kulima, kwa kukosa nafasi au usimamizi mzuri,unaweza kununua mazao hayo kwa wingi kwenye msimu wa mavuno, kuyaongeza thamani na kuyauza kwa wahitaji. Mfano kununua mpunga wakati wa mavuno,kuukoboa, kuuhifadhi kwenye vifungashio vizuri na kuuza kwa watumiaji
(Anza na mtaji mdodgo ili upate uzoefu), ni biashara ambayo inaweza kukupeleka kwenye mafanikio makubwa.
NB: Fanya k**a biashara na siyo mazoea, Jifunze kila hatua acha kwanza "ustar" na uweke tamaa pembeni.
Tuko pamoja 🤝 tutafika