Afyaclass

Afyaclass Ushauri|Tiba|Afya
Elimu ya afya kwa lugha rahisi
Call,Sms,Whatsapp+255758286584

Ugonjwa wa chembe ya moyo au kwa kitaalam huitwa angina pectoris ni ugonjwa wa moyo ambao huhusisha maumivu makali ya up...
10/12/2025

Ugonjwa wa chembe ya moyo au kwa kitaalam huitwa angina pectoris ni ugonjwa wa moyo ambao huhusisha maumivu makali ya upande wa kushoto mwa kifua na wakati mwingine maumivu haya husambaa hadi mashavuni,shingoni, mgongoni,mkono wa kushoto N.K

CHANZO CHA UGONJWA WA CHEMBE YA MOYO

Chanzo kikubwa cha ugonjwa wa chembe ya moyo(angina pectoris), ni kutokana na shida kwenye mishipa ya damu ya moyo hali ambayo hupelekea kuwepo kwa kiwango kidogo cha damu kwenye mishipa ndani ya moyo pamoja na ukosefu wa hewa ya oxygen ya kutosha

DALILI ZA UGONJWA WA CHEMBE YA MOYO NI PAMOJA NA;

- Mgonjwa kupata maumivu makali ya upande wa kushoto mwa kifua na wakati mwingine maumivu haya husambaa hadi mashavuni,shingoni, mgongoni,mkono wa kushoto N.K

- Hali ya kushindwa kupumua au kupata shida ya upumuaji.....!!!!

K**a kazi zako Zinahusisha kukaa kwa Muda mrefu,Unashauriwa kupata Muda wa kufanya Mazoezi ya mwili angalau kwa dakika 3...
09/12/2025

K**a kazi zako Zinahusisha kukaa kwa Muda mrefu,Unashauriwa kupata Muda wa kufanya Mazoezi ya mwili angalau kwa dakika 30/Nusu saa kila siku.

Hii itakusaidia sana kujikinga na Athari hizi za kukaa kwa muda mrefu....!!!!

Wakati mwingine kichwa kuuma sana,unaweza kunywa maji ya kutosha tu ukakaa sawa kabsa bila hata kutumia dawa yoyote.K**a...
08/12/2025

Wakati mwingine kichwa kuuma sana,unaweza kunywa maji ya kutosha tu ukakaa sawa kabsa bila hata kutumia dawa yoyote.

K**a unapata hali hii ya kuumwa na kichwa mara kwa mara,Zingatia pia unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakaa Sawa...!!!

Tonsillitis ni tatizo ambalo huhusisha kuvimba kwa tonses. Tatizo la Kuvimba kwa Tonses husababishwa na maambukizi ya Vi...
06/12/2025

Tonsillitis ni tatizo ambalo huhusisha kuvimba kwa tonses. Tatizo la Kuvimba kwa Tonses husababishwa na maambukizi ya Vimelea vya magonjwa k**a vile bacteria au Virusi.

Na jamii ya bacteria inayohusika Zaidi ni pamoja na Streptococcus pyogenes au group A streptococcus, Pia jamii zingine za Streptococcus pamoja na bacteria wengine huweza kusababisha tatizo la tonses kuvimba.

Na Dalili kubwa za Tatizo hili la Tonses ni pamoja na:

- Eneo la Tonses kubadilika rangi na kuwa jekundu

- Kuvimba eneo la tonses

- Kupata shida ya kumeza kitu

- Au kupata maumivu wakati wa kumeza kitu

- Homa

- Kuhisi hali ya Vidonda kooni,Sore throat

- Tezi za shingoni maarufu k**a Lymph nodes kuongezeka ukubwa,kuuma n.k

- Sauti kukwaruza

- Kupata maumivu ya Shingo

- Shingo kukak**aa

- Kupata maumivu ya Kichwa n.k

NB: K**a unasumbuliwa na tatizo hili,Usile Vitu vya baridi sana k**a Ice cream,Soda za baridi,Juice za baridi,maji ya baridi sana au Kula Pilipili.

Njia hizi zitakusaidia kupata Usingizi mzuri;1.Punguza Matumizi ya mwanga wa Blue au vitu venywe mwanga mkali wakati wa ...
04/12/2025

Njia hizi zitakusaidia kupata Usingizi mzuri;
1.Punguza Matumizi ya mwanga wa Blue au vitu venywe mwanga mkali wakati wa siku,k**a vile kwenye Taa au simu,Computer,TV n.k.. Tafiti zinaonyesha kwamba mwanga wa Blue hupunguza uzalishaji wa Homoni au kichocheo aina Ya Melatonin ambacho ndyo huhusika na kuleta Usingizi.

2.Kaa kwenye Mwanga wa Kutosha wakati wa Mchana, Hii husaidia mwili wako kuweza kutofautisha wakati wa usiku ni upi na wakati wa Mchana ni upi,hivo kukusaidia wewe kupata usingizi mzuri wakati wa usku.

3.Matumizi ya Vinywaji vyenye Caffeine hasa wakati wa Usiku huuchangamsha mwili wako na kukusababishia kukosa Usingizi kabsa wakati wa Usku. Hivo epuka matumizi haya ya Vinywaji vyenye Caffeine wakati wa Usku.

4.Punguza tabia ya kulala wakati wa mchana,hii itakusaidia wewe kulala vizuri wakati wa Usku.

5.Inashauriwa kwa asilimia kubwa muda wa kulala na kumka kila siku uzingatiwe sana,hali hii huuzoesha mwili kwamba sasa ni wakati wa usku na ni wakati wangu wa kulala.

6.Epuka matumizi ya pombe au kilevi chochote,kwani hivi huathiri uzalishaji wa kichocheo au homoni hii ya Melatonin ambayo inahusika na Usingizi moja kwa moja.

7.Boresha Mazingira yako ya kulala,Tafiti zinaonyesha watu wengi wanaosumbuliwa na matatizo ya kukosa Usingizi, hulala kwenye vyumba ambao si rafiki mfano,Chumba ambacho kina mwanga sana,chumba chenye Joto sana,Chumba chenye baridi sana,Chumba ambacho kina makelele ya aina yoyote,mfano Redio au watu.

8.Epuka matumizi au ulaji mwingi wa chakula wakati wa usiku,pia Epuka kula vyakula vizito sana wakati wa Usku.

9.Pumzisha akili yako na iburudishe na vitu k**a Mziki laini n.k kabla Ya kulala na epuka kutazama vitu k**a Movies ndefu za kutisha wakati wa usku

10.Hakikisha umeoga kabla ya kwenda kulala Au kuupumzisha mwili wako kitandani.

11.Fanya mazoezi kila siku wakati wa mchana kabla siku yako haijaisha au kabla hujaenda kulala kitandani

12.Epuka kunywa kwa wingi vimiminika,kwani vitakufanya uanze kuamka amka mara kwa mara wakati wa usku,hivo kupelekea kukosa usingizi mzuri.

Sababu za Mtoto Kutokukaza Shingo1. Udhaifu wa misuli (Muscle weakness)Hii ndiyo sababu ya kawaida. Misuli ya shingo ina...
04/12/2025

Sababu za Mtoto Kutokukaza Shingo
1. Udhaifu wa misuli (Muscle weakness)

Hii ndiyo sababu ya kawaida. Misuli ya shingo inakuwa haijaimarika vizuri.

2. Kukaa muda mwingi mgongoni

Mtoto akikaa muda mwingi mgongoni bila kufanyishwa tummy time(kuwekwa eneo la tumboni),kupakatwa na kupata Support ya mikono, anaweza kuchelewa kuimarisha misuli ya shingo.

3. Kuzaliwa kabla ya wakati (prematurity)

Watoto njiti mara nyingi huchelewa milestones k**a kukaza shingo.

4. Kuwa na matatizo yanayosababisha udhaifu wa misuli (Hypotonia)

Hii husababisha mwili kuwa “legelege”. Inaweza kusababishwa na:

matatizo ya mishipa ya fahamu (neurological issues),

genetic syndromes,

matatizo ya ukuaji wa ubongo.n.k.

5. Ugonjwa uliopata wakati wa kuzaliwa

Mfano: upungufu wa oksijeni wakati wa kuzaliwa (birth asphyxia),au kuugua magonjwa mengine,inaweza kuchelewesha hatua za ukuaji kwa Mtoto

6. Ugonjwa wa mifupa ya shingo (Torticollis / neck stiffness)

Mtoto anaweza kushindwa kugeuza au kuikaza shingo vizuri.

7. Maambukizi makali au utapiamlo

Severe infections au lishe duni vinaweza kuchelewesha ukuaji wa misuli.....!!!!!

Kwanini korosho zinatajwa kwa habari ya Afya ya Moyo?Siyo tu kwamba korosho zina kiwango kidogo cha mafuta lakini pia zi...
04/12/2025

Kwanini korosho zinatajwa kwa habari ya Afya ya Moyo?

Siyo tu kwamba korosho zina kiwango kidogo cha mafuta lakini pia zina aina ya mafuta ambayo hutoa kinga kwenye moyo. Aidha, ndani ya korosho, kuna kirutubisho aina ya Oleic Acid ambacho huimarisha afya njema ya moyo na huwafaa hata wagonjwa wa kisukari.......!!!

Sababu za Vidonda Kwenye Ulimi ni pamoja na hizi:(a) MaambukiziMaambukizi ya virusi: K**a vile virusi vya Herpes Simplex...
03/12/2025

Sababu za Vidonda Kwenye Ulimi ni pamoja na hizi:

(a) Maambukizi

Maambukizi ya virusi: K**a vile virusi vya Herpes Simplex

Maambukizi ya bakteria: Hasa kwa wale wanaougua streptococcus au kaswende.

Maambukizi ya fangasi: K**a vile thrush (oral candidiasis) inayosababishwa na fangasi aina ya Candida albicans.

(b) Majeraha ya Kimwili

Kung’ata ulimi kwa bahati mbaya.

Kula kitu chenye ncha kali au chakula kinachowasha sana,chamoto sana.n.k

Matumizi mabaya ya mswaki au meno bandia.

(c) Magonjwa ya Kinga ya Mwili

Magonjwa k**a HIV n.k.

(d) Upungufu wa Virutubisho

Upungufu wa madini chuma au iron, vitamin B12, na folic acid unaweza kusababisha vidonda kwenye ulimi.n.k.

Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuongeza uwezekano wa mtu kupata tatizo la miguu kuwaka moto k**a vile;- Mtu kuwa ...
02/12/2025

Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuongeza uwezekano wa mtu kupata tatizo la miguu kuwaka moto k**a vile;

- Mtu kuwa na ukosefu wa kutosha wa vitamins mwilini k**a vile; Vitamin B n.k

- Kuwa na tatizo la upungufu wa vichocheo vya thyroid shingoni

- Kuwa na maambukizi ya magonjwa mbali mbali yanayoshusha kinga ya mwili

- Kuwa na tatizo la Ugonjwa wa Kisukari

- Mtu Kuwa na matitizo ya Figo

- Mtu kuwa na tatizo la Fangasi wa miguuni

- Kuharibika kwa mfumo wa Nerves maeneo ya miguuni

- Kuwa na tatizo la Saratani pamoja na matumizi ya baadhi ya dawa za kutibu tatizo hili n.k......!!!!!

Chanzo cha Kuwashwa Mwili ni nini?Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kusababisha hali hii ya kuwashwa mwilini na Saba...
01/12/2025

Chanzo cha Kuwashwa Mwili ni nini?
Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kusababisha hali hii ya kuwashwa mwilini na Sababu hizo ni pamoja na;

– Tatizo la ngozi kukauka kupita kawaida(dry skin)

– Magonjwa yanayohusisha ngozi k**a vile;

Ugonjwa wa pumu ya ngozi(eczema)

Fangasi wa kwenye damu au ngozi

Tatizo la Scabies

Pamoja na matatizo mengine ya ngozi k**a vile Psoriasis n.k

– Tatizo la Allergies au mzio juu ya vitu mbali mbali ikiwemo, baadhi ya mafuta ya kupaka au kupikia,vyakula,dawa n.k

– Mashambulizi ya vimelea wengine wa magonjwa k**a vile parasites,MINYOO n.k

– Sumu inayotokana na kung’atwa na wadudu mbali mbali

– Na wakati mwingine hali ya kuwashwa ngozi ya mwili huweza kutokana na magonjwa ya ndani(Internal diseases) k**a vile;Ugonjwa wa Ini(Liver disease), Homa ya Ini,n.k.......

Watu wengi wanaoambukizwa HIV hupata dalili ndani ya wiki 2–6 baada ya kuambukizwa, lakini sio wote hupata “mafua” au da...
29/11/2025

Watu wengi wanaoambukizwa HIV hupata dalili ndani ya wiki 2–6 baada ya kuambukizwa, lakini sio wote hupata “mafua” au dalili zozote.

Hali zinavyoweza kuwa:

1.Wengine hupata dalili k**a za mafua: homa, maumivu ya kichwa, koo kuuma, uchovu, au tezi kuvimba.

2.Wengine hupata dalili tofauti k**a: upele wa ngozi, kuharisha, jasho la usiku, au vidonda mdomoni.

3.Wengine hawapati dalili kabisa kwa miezi au hata miaka......!!!!

Dalili zifuatazo za ugonjwa huu wa ngozi hutokea kwa watu wazima:- vipele ambavyo vina magamba zaidi kuliko vinavyotokea...
28/10/2025

Dalili zifuatazo za ugonjwa huu wa ngozi hutokea kwa watu wazima:

- vipele ambavyo vina magamba zaidi kuliko vinavyotokea kwa watoto

- vipele ambavyo kwa kawaida huonekana kwenye mikunjo ya viwiko au magoti au sehemu ya shingo.

- vipele vinavyofunika sehemu kubwa ya mwili

- ngozi kuwa kavu sana kwenye maeneo yaliyoathirika

- vipele ambavyo huwashwa sana n.k

Je,Una tatizo hilo na hujapata Tiba,Kwa Ushauri zaidi na Tiba tuwasiliane +255758286584.

Address

Dar Es Salaam
00000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afyaclass posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram