02/04/2026
Kujisaidia kinyesi kigumu au choo kigumu (constipation) hutokea pale kinyesi kinapokuwa kigumu wakati kinapita. Hali hii inaweza kuwa ya muda mfupi au ya muda mrefu kulingana na chanzo.
SABABU KUU ZA KINYESI KIGUMU:
1.Kukosa nyuzinyuzi (fiber) kwenye chakula, ukila vyakula ambavyo havina nyuzinyuzi kwa kiwango kikubwa unakuwa kwenye hatari ya kupata tatizo hili.
-Kula vyakula vilivyosindikwa sana (mfano mikate meupe, nk)
-Kutokula matunda na mboga za majani
2.Kunywa maji kidogo
Mwili ukikosa maji, kinyesi hukauka na kuwa kigumu
3.Kutokufanya mazoezi
Kukaa muda mrefu bila kusogea hupunguza mwendo wa utumbo na kuongeza hatari ya tatizo hili.
4.Kujizuia kwenda chooni
Ukizuia haja mara kwa mara, mwili unapoteza hisia ya kawaida ya kwenda,Lakini pia maji hufyozwa zaidi kwenye haja kubwa,hivo kuongeza hatari ya kinyesi kutoka kigumu.
5.Mabadiliko ya maisha mfano;Kusafiri(kubadilisha mazingira), kubadilisha ratiba ya kula,kujisaidia au kulala.
6.Matumizi ya dawa fulani
mfano: iron supplements, nk
7.Kwa wanawake wajawazito, Pia hali hii huwasumbua Sana.
Je,una hali hii na hujapata Ufumbuzi wake,Tumia mawasiliano +255758286584....