Afyaclass

Afyaclass Dr.Ombeni Mkumbwa|Ushauri|Tiba|Afya
Elimu ya afya kwa lugha rahisi
Call,Sms,Whatsapp+255758286584

Je,Unalifahamu hili? Watu Wengi wanajua aina moja ya Bawasiri ambayo kinyama hutokeza Sehemu ya haja kubwa kwa nje(Hii n...
31/01/2026

Je,Unalifahamu hili? Watu Wengi wanajua aina moja ya Bawasiri ambayo kinyama hutokeza Sehemu ya haja kubwa kwa nje(Hii ni Bawasiri ya Nje)

Ipo aina nyingine ya Bawasiri ya Ndani ambayo Si Lazima Uone kinyama kwa nje, Hii unaweza kuhisi maumivu kwa ndani,Unaona damu wakati wa kujisaidia n.k.....

Chanzo cha Maumivu ya Tumbo chini ya Kitovu kwa MwanamkeMaumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa mwanamke yanaweza kusababis...
28/01/2026

Chanzo cha Maumivu ya Tumbo chini ya Kitovu kwa Mwanamke

Maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa mwanamke yanaweza kusababishwa na mambo mbalimbali;

1. Maumivu ya Siku za Hedhi

Maumivu haya yanaweza kuhusiana na siku za hedhi, hasa kabla au wakati wa hedhi kutokana na kukaza kwa mfuko wa uzazi.

2. Maambukizi ya bacteria kwenye via vya uzazi vya Mwanamke(PID) yanaweza kusababisha maumivu chini ya kitovu, na mara nyingi huambatana na uchafu usio wa kawaida ukeni, harufu mbaya au maumivu wakati wa kujamiiana.n.k.

3. Tatizo la Uvimbe kwenye kizazi(Fibroids) au Tatizo la Vivimbe maji(Ovarian cysts)

Ovari cysts pia husababisha maumivu ya upande mmoja au chini ya tumbo kwa Wanawake wengi,

Uvimbe kwenye kizazi ni uvimbe ambao huonekana sana kwa wanawake hasa wenye umri wa miaka 30-40. Ingawa baadhi ya wanawake wanaweza kuwa hawana dalili zozote, wengine wanaweza kupata maumivu ya tumbo, maumivu ya mgongo, maumivu wakati wa tendo la ndoa, au ugumu wa kupata mimba.

4. Maambukizi kwenye njia ya Mkojo(UTI)

Sababu nyingine ni matatizo ya mfumo wa mkojo ikiwemo Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) husababisha maumivu chini ya kitovu, hisia ya kuchoma wakati wa kukojoa, kukojoa mara kwa mara au mkojo wenye harufu kali n.k. Na Wakati mwingine maumivu huongezeka unapobana mkojo.

5. Tatizo la Mimba kutunga nje ya Kizazi(Ectopic pregnancy)

Mimba kutunga nje ya kizazi huweza kuambatana na dalili mbali mbali ikiwemo; maumivu makali ya tumbo (mara nyingi huonekana upande mmoja)

6. Magonjwa ya Zinaa-Sexually Transmitted Infections (STIs)

Maumivu ya Tumbo chini ya Kitovu kwa Mwanamke yanaweza kusababishwa pia na magonjwa ya zinaa k**a vile;kisonono,chlamydia n.k.

7. Tatizo la Mawe kwenye Figo(Kidney Stones)

Tatizo hili pia huweza kusababisha hali ya Maumivu hasa pale Mawe haya Yanaposogea, yanaweza kusababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu.
8. Tatizo la appendicitis au kidole tumbo(Appendix) pia huanza k**a maumivu chini ya kitovu kisha kuhamia upande wa kulia.

Gesi tumboni, kuvimbiwa, au matatizo ya utumbo k**a IBS husababisha maumivu ya chini ya tumbo yanayokuja na kuondoka....

Ukilala Taa Izimwe au Iwashwe?,Ukiwa unataka usingizi mzuri, Fanya hivi:1.ZIMA TAAFahamu Mwanga hasa wa taa kali au simu...
26/01/2026

Ukilala Taa Izimwe au Iwashwe?,Ukiwa unataka usingizi mzuri, Fanya hivi:

1.ZIMA TAA
Fahamu Mwanga hasa wa taa kali au simu hupunguza melatonin – homoni ya usingizi, hali ambayo huweza kukufanya usipate usingizi vizuri

Usingizi unakuwa mzito na bora zaidi gizani, na pia
Hupunguza kuamka usiku bila sababu.

NB: Ukiwa na hofu, watoto, au wagonjwa unaweza kuwasha taa lakini iwe na Mwanga hafifu sana

2.WASHA TAA YENYE MWANGA HAFIFU / DIM LIGHT
Taa hafifu (sio yenye mwanga mkali) inasaidia utulivu, hivo Kwa watoto na wagonjwa ni sawa

ya macho
Kulala na taa kali imewashwa muda mrefu si nzuri kwa macho. Inaweza kuchosha macho na kuvuruga mzunguko wa usingizi

βœ… Ushauri wa kitaalamu
πŸ‘‰ Zima taa kabisa, au
πŸ‘‰ Tumia taa yenye mwanga hafifu sana (dim light) k**a unaona ni lazima kutumia...

Usitumie Kahawa k**a una Presha ya kupandaHushauriwi kutumia kahawa k**a tayari una tatizo la Presha ya kupanda,mbali na...
23/01/2026

Usitumie Kahawa k**a una Presha ya kupanda

Hushauriwi kutumia kahawa k**a tayari una tatizo la Presha ya kupanda,

mbali na kwamba baadhi ya watu hutumia kahawa kwa lengo la kupoteza Usingizi,lakini kahawa pia inaweza kupandisha presha yako ndani ya muda mfupi baada ya kutumia.

Machapisho zaidi ya 34 ya tafiti mbali mbali yanaonyesha kwamba;

200–300 mg za caffeine kutoka kwenye Kahawa sawa na makadirio ya kikombe kimoja na Nusu(1.5) mpaka vikombe viwili(2) vya kahawa,

huweza kuongeza presha kwa kiwango cha 8 mm Hg na 6 mm Hg kweny systolic na diastolic blood pressure,

Na mabadiliko hayo yalionekana ndani ya masaa 3 tu baada ya mtu kutumia Kahawa,

Ongezeko hilo hutokea kwa watu wote,walio na presha ya kawaida(normal bp), walio kwenye hatari ya kupata presha, na ambao tayari wanashida ya presha.

Lakini pia kwa kadri mtu anavyozoea kutumia Kahawa mara kwa mara hutengeneza kitu kinaitwa caffeine tolerance mwilini,

Ndo mana matokeo ya kahawa kwa siku za mwanzo,ni tofauti kadri unavyotumia mara kwa mara, hata kwenye swala la presha ni hivo hivo.....

Zingatia Mambo haya Muhimu sana kwako k**a unatatizo la Kukosa Choo1. Fanya Mabadiliko ya lishe yako,Ongeza vyakula vyen...
22/01/2026

Zingatia Mambo haya Muhimu sana kwako k**a unatatizo la Kukosa Choo

1. Fanya Mabadiliko ya lishe yako,Ongeza vyakula vyenye nyuzinyuzi k**a vile:

Mboga za majani k**a (sukuma, mchicha, kabichi)

Matunda (papai, embe, parachichi, ndizi mbivu)

Nafaka zisizosindikwa (mtama, ulezi, unga wa dona)

Epuka vyakula vya kukaanga sana na vyakula vya mafuta mengi.

2. Kunywa maji ya kutosha

Angalau glasi 6–8 za maji kila siku. Ingawa hii itategemea na vitu vingi ikiwemo umri wako,Uzito wako,hali ya hewa,kazi unayofanya,hali yako ya kiafya n.k.

Pia Maji ya uvuguvugu asubuhi yanaweza kusaidia kusisimua utumbo,Na kukufanya ujisaidie haraka.

3. Fanya Mazoezi ya mwili

Kutembea kwa dakika 30 kila siku husaidia kuamsha utumbo na kuondoa hali hii ya kukosa choo.

4. Kuanzisha ratiba ya kwenda chooni

Jisaidie kila siku muda uleule, hasa baada ya kula.

5. Tiba ya dawa (ikiwa njia asili hazijasaidia)

Pata Dawa za kuondoa tatizo hili,Tumia dawa kwa ushauri wa daktari tu, kwani matumizi mabaya yanaweza kusababisha madhara zaidi.

Wanawake wengi baada ya kujifungua husubiri kwanza waone hedhi ndipo waanze kuchukua tahadhari ya kujikinga na Mimba,Kum...
20/01/2026

Wanawake wengi baada ya kujifungua husubiri kwanza waone hedhi ndipo waanze kuchukua tahadhari ya kujikinga na Mimba,

Kumbuka hedhi ni matokeo ya kutokuwa na urutubishaji wa Yai, endapo yai limerutubishwa huwezi ona hedhi k**a ulivyokuwa unasubiria ndipo uanze kujikinga,

Hii imepelekea wanawake wengi kubeba mimba ambazo hazijapangwa baada ya kujifungua,

Una mimba nyingine na huku bado unanyonyesha,

JIKINGE NA MIMBA AMBAZO ZIPO NJE YA MPANGO.

Choo unachotumia na mazingira yake kwa ujumla huweza kuwa chanzo cha UTI za mara kwa mara:Ikiwa mazingira ya Chooni sio ...
19/01/2026

Choo unachotumia na mazingira yake kwa ujumla huweza kuwa chanzo cha UTI za mara kwa mara:

Ikiwa mazingira ya Chooni sio masafi,Choo unashare na watu wengine(public toilet),Unaweka maji juu ya maji mengine yaliyokaa muda kwa wale wanaotumia vyombo k**a ndoo n.k.

Vitu hivi huweza kuongeza hatari ya wewe kupata UTI za mara kwa mara. Kati ya Mazingira ambayo unatakiwa kuhakikisha USAFI wa hali ya juu ili kujikinga na magonjwa mbali mbali ikiwemo UTI ni CHOO. Hakikisha mazingira haya yanakuwa na usafi wa hali ya juu......

Saratani ya shingo ya kizazi au Mlango wa kizazi(Cervical cancer) ni mojawapo ya aina za saratani zinazoweza kuzuilika n...
16/01/2026

Saratani ya shingo ya kizazi au Mlango wa kizazi(Cervical cancer) ni mojawapo ya aina za saratani zinazoweza kuzuilika na kutibika zaidi, ikigunduliwa mapema.

Kwa mujibu wa Shirika la afya Duniani Wanawake wanapaswa kuchunguzwa saratani ya shingo ya kizazi kila baada ya miaka 5-10 kuanzia umri wa miaka 30.

Uchunguzi unapaswa kupatikana kwa wanawake katika nchi zote, ikifuatiwa na matibabu ya haraka inapohitajika..

Hata k**a Kitovu cha Mtoto kimechelewa kukauka au kukatika usiweke Vitu hivi;-Mavi ya kuku,ng'ombe-Kupaka masizi-Kupaka ...
14/01/2026

Hata k**a Kitovu cha Mtoto kimechelewa kukauka au kukatika usiweke Vitu hivi;

-Mavi ya kuku,ng'ombe
-Kupaka masizi
-Kupaka Dawa ya Meno n.k.

Hivi ni Vitu ambavyo baadhi ya Jamii au Watu hutumia wakiamini kwamba ni Tiba, Epuka vitu hivi huongeza hatari zaidi ya maambukizi ya Vimelea vya magonjwa na kutengeneza tatizo kubwa zaidi kwa Mtoto wako.......

Minyoo husababishwa na nini,Minyoo huingiaje mwiliniMinyoo kwa binadamu hupatikana kutokana na vyanzo mbalimbali, hasa v...
12/01/2026

Minyoo husababishwa na nini,Minyoo huingiaje mwilini

Minyoo kwa binadamu hupatikana kutokana na vyanzo mbalimbali, hasa vinavyohusiana na usafi duni na mazingira.

Kwanini Unasikia Meza dawa za Minyoo Kila baada ya miezi 3, Miezi 6 na kuendelea hata k**a huoni dalili zozote. Hii inatokana na Mazingira mengi tunayoishi yanakuwa na Kiwango kikubwa cha Minyoo hali ambayo hupelekea watu wengi kuipata bila wao kujua.

Katika Makala hii nmekuchambulia baadhi ya vyanzo vikuu vya kupata Minyoo,Soma hapa...

Hivi ndiyo vyanzo vikuu vya minyoo kwa mtu:

1. Kula Chakula kichafu

Kula mboga au matunda yasiyooshwa vizuri

Kula chakula kilichochafuliwa na mayai ya minyoo

Kula nyama au samaki wasioiva vizuri n.k

Vitu hivi huweza kuwa vyanzo vikuu vya wewe kuwa na Shida ya Minyoo

Ushauri: Hakikisha Mazingira ya kuandalia vyakula ikiwemo vyakula vyenyewe vinakuwa Safi

2. Kunywa Maji machafu

Kunywa maji yasiyochemshwa au yasiyotibiwa

Kutumia maji yaliyochafuliwa kupikia au kuosha vyombo

Ushauri: Kunywa maji Safi na Salama,maji yaliyochemshwa,kutibiwa n.k. Pamoja na vyombo vya kuhifadhia maji ya kunywa Viwe Visafi Sana.

3. Usafi binafsi duni

Kutokunawa mikono kabla ya kula au baada ya kutoka chooni huongeza hatari ya kuingiza minyoo kwenye mwili wako

Kucha ndefu zinazohifadhi uchafu na mayai ya minyoo, hii pia ni hatari kwa Watu wengi wanaofuga kucha bila wao kujua.

Ushauri: Hakikisha unanawa mikono kabla ya kula,baada ya kutoka chooni,Usafi wa kucha pia usisahau..

4. Kutembea peku au bila Viatu

Minyoo aina ya hookworm huingia mwilini kupitia ngozi ya mguu

Hutokea zaidi kwenye udongo wenye uchafu wa kinyesi

Ushauri: Usipende kutembea Peku,Vaa Viatu, hata k**a ni Mkulima upo shambani usitembee peku kwenye Udongo hii ni hatari zaidi kushambuliwa na minyoo.

5. Vyoo visivyo salama

Kutumia vyoo vibovu au Vichafu sana hii huweza kuongeza hatari ya wewe kupata minyoo

Uchafu wa Vyoo huweza kuhusisha;

Mazingira yake kwa ujumla

Vyombo vya maji

Maji yenyewe yanayotumika n.k.

Pia kujisaidia eneo la wazi huweza kuongeza hatari ya minyoo kwani Huchafua udongo na maji pia.

Ushauri: Hakikisha vyoo vinakuwa Safi na Salama kwa matumizi muda wote

6. Kula Udongo

Wapo baadhi ya Watu hupenda kula Udongo ikiwemo watoto wadogo na wakina mama wajawazito, hii huweza kuwa chanzo kikubwa cha kupata Minyoo pia.

Ushauri: Acha Tabia ya kula Udongo,Lakini pia Mzuie mtoto wako kula Udongo

Article author: Dr.Ombeni Mkumbwa
Reviewed: Afyaclass, MD's......

Sababu za Tatizo La Kutoa Harufu Mbaya Puani ni Zipi? fahamu hapa chanzo cha shida hii(Baadhi ya Sababu):- Mtu kupatwa n...
10/01/2026

Sababu za Tatizo La Kutoa Harufu Mbaya Puani ni Zipi? fahamu hapa chanzo cha shida hii(Baadhi ya Sababu):

- Mtu kupatwa na mashambulizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa puani k**a vile; fangasi,virusi au Bacteria

- Mtu Kupatwa na tatizo la kuota vinyama puani hali ambayo hujulikana kwa kitaalam k**a Nasal polyps

- Kuanza kutoa harufu puani baada ya kutolewa mpira wa puani ambao ulitumika kwa sababu mbali mbali k**a vile; kwa ajili ya kupata chakula, Hewa n.k

- Kupatwa na tatizo la jino au meno kuharibika na sehemu ya jino kuoza kutokana na mashambulizi ya wadudu k**a Bacteria n.k, hali ambayo husababisha harufu mbaya kutokea puani

- Kuwa na tatizo la figo kwa muda mrefu yaani Chronic kidney diseases, hali ambayo hupelekea kukusanyika kwa kiwango kikubwa cha taka mwili, na kuleta athari hadi puani.

Dalili za Nyama Puani kwa Mtoto– Kutoa Sauti wakati wa kupumua au mtoto kukoroma(Snoring)– Kupata shida ya kupumua(kuvut...
06/01/2026

Dalili za Nyama Puani kwa Mtoto
– Kutoa Sauti wakati wa kupumua au mtoto kukoroma(Snoring)

– Kupata shida ya kupumua(kuvuta hewa na kutoa hewa)

– Mtoto kupumua kwa kutumia mdomo badala ya Pua

– Mtoto kuwa na mafua ambayo hayakatiki, ya mara kwa mara

– Mtoto kuvimba pua au kuwa na shida ya Runny nose

– Kupungua kwa uwezo wa kunusa na kusikia harufu ya vitu mbali mbali(Decreased sense of smell)

Kwa Ushauri Zaidi,Elimu au Tiba tuwasiliane:Call,Sms,Whatsapp +255758286584.

Address

Dr. Ombeni Mkumbwa
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afyaclass posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram