22/01/2026
Zingatia Mambo haya Muhimu sana kwako k**a unatatizo la Kukosa Choo
1. Fanya Mabadiliko ya lishe yako,Ongeza vyakula vyenye nyuzinyuzi k**a vile:
Mboga za majani k**a (sukuma, mchicha, kabichi)
Matunda (papai, embe, parachichi, ndizi mbivu)
Nafaka zisizosindikwa (mtama, ulezi, unga wa dona)
Epuka vyakula vya kukaanga sana na vyakula vya mafuta mengi.
2. Kunywa maji ya kutosha
Angalau glasi 6β8 za maji kila siku. Ingawa hii itategemea na vitu vingi ikiwemo umri wako,Uzito wako,hali ya hewa,kazi unayofanya,hali yako ya kiafya n.k.
Pia Maji ya uvuguvugu asubuhi yanaweza kusaidia kusisimua utumbo,Na kukufanya ujisaidie haraka.
3. Fanya Mazoezi ya mwili
Kutembea kwa dakika 30 kila siku husaidia kuamsha utumbo na kuondoa hali hii ya kukosa choo.
4. Kuanzisha ratiba ya kwenda chooni
Jisaidie kila siku muda uleule, hasa baada ya kula.
5. Tiba ya dawa (ikiwa njia asili hazijasaidia)
Pata Dawa za kuondoa tatizo hili,Tumia dawa kwa ushauri wa daktari tu, kwani matumizi mabaya yanaweza kusababisha madhara zaidi.